Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Ikungi – Mang'onyi – Londoni hadi Kilimatinde?

Supplementary Question 1

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake, lakini ninayo maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; barabara hii inakatisha katikati ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi pamoja na hospitali ya wilaya, tayari tumejengewa kilometa mbili ambazo hazijafika kwenye ofisi hizo. Je, ni nini mpango wa muda mfupi wa Serikali kuhakikisha kwamba, Ofisi za Serikali na Hospitali ya Wilaya inafikiwa barabara ya lami? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; nataka tu kueleza kwamba, barabara hii ni barabara ya kiuchumi inakatisha kwenye Kata ya Mang’onyi ambayo imebeba Mgodi mkubwa wa Madini wa Shanta Gold Mine na kwa sababu, mgodi huu tayari umeanza kumimina dhahabu, kwa mwaka unatoa ounce 30,000 ambazo ni sawasawa na dola bilioni 60 au Shilingi za Kitanzania bilioni 150, maana yake ni mapato mengi ya Serikali. Kwa sababu, mgodi unahitaji pia barabara hii, je, ni nini mpango wa Serikali kwa kushirikiana na mwekezaji huyu ili kuhakikisha Barabara hii ya kutoka Ikungi mpaka Mangonye ambayo ni kilometa 50 tu iweze kuwekwa lami na kumsaidia mwekezaji aweze kuwa na mazingira mazuri? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kwamba, barabara hii inafanyiwa usanifu, lakini tunatambua kwamba, barabara hii ndio inapita kwenye Ofisi ya Halmashauri, Mkuu wa Wilaya na Hospitali ya Wilaya. Tayari tumeanza na pia, tayari tumepata maombi ya Meneja wa Mkoa kutaka kuendelea kujenga kwa awamu hadi kufika katika hospitali ya wilaya. Kwa hiyo, hilo tutaendelea nalo wakati tunaendelea na usanifu kuhakikisha kwamba, tunafika hapo. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante. La pili, tayari?

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, la pili bado.

NAIBU SPIKA: Haya, jibu la pili.

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili, hata wawekezaji wenyewe wamekuja Ofisi ya Mkoa na Wizarani pia, kuomba barabara hii iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Ushauri wake kama alivyosema, tutaendelea kushauriana kama tulivyofanya Barrick ambao wameamua kusaidia kujenga kama CSR. Kwa hiyo, taratibu zinafanyika kuona namna ambavyo tunaweza kusaidiana na Serikali na Shanta Mine kuweza kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)
NAIBU SPIKA: Ahsante. La pili, tayari?

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, la pili bado.

NAIBU SPIKA: Haya, jibu la pili.

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili, hata wawekezaji wenyewe wamekuja Ofisi ya Mkoa na Wizarani pia, kuomba barabara hii iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Ushauri wake kama alivyosema, tutaendelea kushauriana kama tulivyofanya Barrick ambao wameamua kusaidia kujenga kama CSR. Kwa hiyo, taratibu zinafanyika kuona namna ambavyo tunaweza kusaidiana na Serikali na Shanta Mine kuweza kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Ikungi – Mang'onyi – Londoni hadi Kilimatinde?

Supplementary Question 2

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kupata nafasi. Tumepata barabara ya kutoka Tarime Mjini mpaka pale Mugumu, Serengeti, hasa maeneo ya Nyamongo, lakini barabara imesimama ujenzi wake kwa muda mrefu sasa kwa sababu, yule mkandarasi anadai shilingi bilioni 6.8 mpaka leo. Je, ni lini mkandarasi huyu atalipwa fedha ili ujenzi ukamilike kwa wakati na watu wetu waendelee kupata huduma? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, taarifa nilizonazo, nitaongea na Mheshimiwa Mbunge ni kwamba, tuna lot mbili, lot ya kwanza ni Mugabiri kwenda Serengeti na kipande kile ambacho ni cha pili, nilichoambiwa ni kwamba, yupo kwenye mobilization na anaendelea kuandaa camp kwa ajili ya kujenga. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi tumekuwa na changamoto kubwa, barabara nyingi zimesimama kwa sababu ya hali ya hewa ambayo inazuia wakandarasi kuendelea na kazi za ujenzi wa barabara, lakini nitaomba nionane na Mheshimiwa Mbunge, tuone kama kuna changamoto nyingine zaidi ya hii. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Ikungi – Mang'onyi – Londoni hadi Kilimatinde?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Nyanguge – Airport yenye urefu wa kilometa 46, Serikali ilipanga kuijenga kwa kilometa 10 na tayari mkandarasi alipatikana. Je, ni lini mkandarasi huyu atakabidhiwa site ili aanze kazi? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tumetangaza na Mkandarasi amepatikana, lakini kutokana na ukubwa wa barabara imehamishiwa, badala ya kusimamiwa na mkoa sasa itasimamiwa na TANROADS, Makao Makuu. Kwa hiyo, ni suala linalosubiri kumkabidhi mkandarasi hiyo site ili aanze kazi ya ujenzi. Ahsante. (Makofi)

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Ikungi – Mang'onyi – Londoni hadi Kilimatinde?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali ya nyongeza. Barabara ya kutoka Bariadi – Itilima – Kisesa - Meatu mpaka Sibiti – Singida iko kwenye ilani. Je, ni lini itajengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja ni Barabara ya Mkoa ambayo tunavyoongea sasa hivi ipo kwenye utaratibu wa usanifu wa kina. Ikikamilika, Serikali itatafuta fedha ya kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Ikungi – Mang'onyi – Londoni hadi Kilimatinde?

Supplementary Question 5

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza. Barabara inayotokea Tegeta kupita Mabwepande mpaka Mbezi imekuwa ni kero, haipitiki na kumekuwa na msongamano mkubwa katika Barabara ya Bagamoyo. Je, ni lini Serikali itaijenga barabara hii ili kuondoa adha kwa wananchi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Hii barabara ni kati ya barabara ambazo zipo kwenye mpango mkubwa wa kupunguza foleni katika Mkoa wa Dar es Salaam. Tunavyoongea sasa hivi ni kwamba, kuanzia Bunju B – Mabwepande hadi Station ya Magufuli ipo kwenye usanifu. Tunategemea mwaka ujao wa fedha tutaanza kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Ikungi – Mang'onyi – Londoni hadi Kilimatinde?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itaijenga kwa kiwango cha lami barabara ya mchepuo inayotoka Tumaini kwa kuwa kumekuwa na ongezeko kubwa la magari makubwa yanayopita katikati ya mji na kusababisha hatari kwa wafanyabiashara pamoja na watumiaji wengine wa barabara? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naamini Barabara ya Mchepuo kutoka Tumaini ni ile inayokwenda Station Kuu pale Ipogolo chini, kilometa saba. Barabara hiyo ilikuwa haipo, ndiyo tunaendelea kuifungua na baada ya kuifungua, kwa umuhimu wake na eneo ilipo baada ya kuifungua kinachofuata ni kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)