Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza:- Je, lini ujenzi wa Madaraja ya Bujonde na Ilondo Mwaya - Kyela utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, wakati Serikali inaendelea na upembuzi yakinifu, je, ni mkakati gani unafanywa kwa barabara ambazo zinaunganisha madaraja hayo mawili, kati ya Kajunjumele – Mwaya – Lusungo na Matema?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Daraja la Bujonde pia lina kipande cha barabara cha Ibanda – Itungi Port, je, baada ya kumwondoa mkandarasi nini mkakati wa Serikali kwa sasa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tunavyojenga madaraja ambayo mara nyingi ndiyo kikwazo kikubwa cha kuunganisha eneo na eneo Serikali itazijenga hizo barabara ambazo zinaunganisha haya madaraja.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu baada ya kumwondoa mkandarasi, kwanza nimwagize Meneja wa Mkoa wa Mbeya kwamba kama kuna changamoto zozote ambazo zinaendelea sasa hivi ahakikishe kwamba anaweka utaratibu wa kuzikarabati hizo barabara wakati Serikali inakamilisha taratibu za kuweza kufanya tathmini na kuona namna ya kusimamisha au kusitisha mkataba na mkandarasi ambaye alikuwa amepewa barabara hii kwa kufuata taratibu zote za mkataba, ahsante.