Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa fidia ya shilingi 236,000,000 kwa wananchi wanaopisha ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Nyang’hwale?

Supplementary Question 1

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, nianze kuipongeza Serikali kwa kutambua fidia ile ya wananchi 31 ya Kijiji cha Busengwa. Swali la kwanza; je, Serikali haioni haja ya kuanza kuandaa michoro ya gereza hilo ili fidia hiyo itakapolipwa ujenzi uanze?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; je, Serikali haioni kufanya ujenzi huo kwa haraka, ili kuokoa gharama za wananchi kufuata huduma hiyo ya magereza kutoka Nyang’hwale kwenda Geita zaidi ya kilometa 130?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Hussein Nassor Amar, Mbunge wa Nyang’hwale, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kuandaa michoro. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, michoro itaandaliwa haraka iwezekanavyo lengo letu ni tuhakikishe kwamba, gereza hili linajengwa haraka, ili kuhudumia wananchi wa maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kuhusu ujenzi kuanza haraka. Kama nilivyosema, baada ya kukamilisha michoro hatua inayofuata ni tutatenga fedha kwenye Mwaka 2025/2026, baada ya hapo ni kuanza ujenzi mara moja, ili wananchi wasipate tabu ya kutoka Nyang’hwale kwenda Geita ambako ni umbali mrefu. Ahsante sana.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa fidia ya shilingi 236,000,000 kwa wananchi wanaopisha ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Nyang’hwale?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Gereza la Wilaya ya Liwale limejengwa Mwaka 1982, lakini wananchi waliopisha ujenzi wa gereza lile mpaka leo hawajapata fidia. Nini Kauli ya Serikali ya kuwapatia fidia wananchi wale?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba jambo hili nilichukue na niagize Jeshi la Magereza kwenda kufanya tathmini katika eneo hilo, ili wananchi hawa wapate fidia, kama ambavyo walitoa eneo hilo, kwa ajili ya ujenzi wa magereza. Ahsante.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa fidia ya shilingi 236,000,000 kwa wananchi wanaopisha ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Nyang’hwale?

Supplementary Question 3

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Je, ni lini Serikali itatoa majibu kwa wananchi wanaoishi pembezoni mwa Gereza la Keko kwa sababu, Gereza la Keko wanalalamika ni eneo lao, lakini wananchi wanaozunguka hapo wana vithibitisho maalum kabisa kwamba ni eneo lao. Je, ni lini Serikali itaenda kutatua tatizo hili?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kilave, Mbunge wa Temeke, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama kuna mgogoro huo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, tutaenda.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa fidia ya shilingi 236,000,000 kwa wananchi wanaopisha ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Nyang’hwale?

Supplementary Question 4

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Jimbo la Kishapu wamechangia jumla ya shilingi milioni 250, kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Wilaya. Ni lini Serikali itatimiza ahadi iliyoahidi kwa ajili ya kuwachangia ili wakamilishe mradi huo na uweze kufanya kazi? Nakushukuru sana.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, hebu rudia tena swali lako.

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Wilaya ya Kishapu wameshapata eneo, kwa ajili ya ujenzi wa magereza na tayari taratibu zote za fidia zimeshafanyika na Serikali ilishaahidi kwamba, itakwenda kutekeleza ujenzi huo kuanzia Mwaka wa Fedha 2024/2025. Je, ni lini mradi huo utaanza kutekelezwa? Ninashukuru.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Butondo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeshatenga fedha kwenye Mwaka huu wa Fedha 2024/2025. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, as long as tumeshatenga fedha na bado mwaka wa fedha unaendelea, basi tutatekeleza mradi huo kwa ujenzi wa magereza katika jimbo lake. Ahsante.