Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Je, Serikali inatumia utaratibu gani wa kuratibu na kutekeleza ahadi za Viongozi Wakuu nchini ili zisionekane ni za uongo?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali, majibu ambayo yanatia moyo na kuonyesha kwamba ni kweli kuna uratibu. Nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa sababu ahadi hizi huwa zinatekelezwa kwenye Wizara za Kisekta. Je, Serikali haioni umuhimu, huko kwenye Wizara za Kisekta kukawekwa mafungu maalumu, yaani kwenye bajeti ikaonekana kwamba fedha hizi zinakwenda kutekeleza ahadi fulani ili Wabunge waweze kufuatilia pale ambapo bajeti hiyo inaweza kutekelezwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kule kwangu barabara ya Nangurukuru – Liwale na Nachingwea – Liwale, ni miongoni mwa ahadi za Uchanguzi wa 2015/2020. Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya utekelezaji wa ahadi hizo?

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee kumpongeza Mheshimiwa Kuchauka kwa kazi, lakini nimwambie kwenye hili la Wizara za Kisekta, ahadi za viongozi ni kipaumbele cha kila sekta wanapowasilisha bajeti.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, wamekuwa wakiendelea kuziweka kila wanavyowasilisha bajeti zao. Sisi Ofisi ya Waziri Mkuu, tunafanya kazi ya kuratibu kuhakikisha kwamba ahadi hizi zimewekwa na kama nilivyosema kwenye dashboard tunaona kila ahadi imefikia hatua gani na asilimia ngapi kwenye utekelezaji, kwenye kila sekta.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, Halmashauri ya Liwale kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI mwaka jana tu tumetoa fedha kwenye yale maafa yaliyotokea ya El Nino na Kimbunga Hidaya, shilingi bilioni 1.3 ili kuweza kuendelea kutengeneza barabara zile. Lakini pia, bajeti yako Mheshimiwa Mbunge Kuchauka imeongezeka kutoka shilingi milioni 839 hadi tunavyoongea leo ni shilingi bilioni 2.4. Nataka nikuhakikishie, ahadi zote za Viongozi wetu Wakuu tunaendelea kuzifanyia kazi. Sisi tunawaomba Watanzania waendelee kutuamini, waendelee kuiamini Serikali ya Awamu ya Sita, kwa sababu ahadi zote ni vipaumbele vya Serikali, ahsante. (Makofi)

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Je, Serikali inatumia utaratibu gani wa kuratibu na kutekeleza ahadi za Viongozi Wakuu nchini ili zisionekane ni za uongo?

Supplementary Question 2

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini ahadi ya Waziri Mkuu ya kujenga Kituo cha Afya katika Kata ya Butimba itatekelezwa?

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba niagize Wizara ya Kisekta iendelee kulifanyia kazi jambo la Mheshimiwa Mbunge ambalo ameulizia kuhusu ujengaji wa kituo hicho cha afya.