Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Esther Nicholus Matiko
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ESTHER N. MATIKO K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isiagize CAG akague URA SACCOS ya Jeshi la Polisi?
Supplementary Question 1
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, pamoja na majibu ya Serikali lakini bado kumekuwa na malalamiko kuhusiana na hizi SACCOSS ambazo kwenye Idara ya Polisi, lakini na Idara nyingine ambazo zipo ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Sasa Serikali mnachukua hatua gani kuhakikisha kwamba mnatekeleza yale madhaifu ambayo mnakuta yametokana na ukaguzi wa CAG? (Makofi)
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu la msingi SACCOSS hii haikaguliwi na CAG, inakaguliwa kwa mujibu wa sheria namba sita inayosimamiwa na kusajiliwa kwa mujibu wa Sheria ya Ushirika na. 6 ya mwaka 2013 na kama nilivyosema URA SACCOSS hii ni SACCOSS bora hapa nchini kama nilivyosema imepata tuzo toka mwaka 2021/2024 kwa hiyo ni SACCOSS ambayo haina malengo yoyote ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani na Jeshi la Polisi, ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved