Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, Serikali ipo hatua gani kwenye ujenzi wa kipande cha barabara kutoka Katoro hadi Daraja la Nyikonga kwenye Barabara ya Katoro – Ushirombo?

Supplementary Question 1

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali kuhusu barabara ya kutoka Ushirombo – Katoro, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, je, upembuzi yakinifu uliofanyika miaka kadhaa iliyopita bado unafaa kwenye ujenzi wa barabara hiyo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kutoka Geita kwa maana ya Mpomvu – Nyarugusu – Bukoli – Irogi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ahsante, kuhusu kama upembuzi yakinifu na usanifu wa kina utakuwa unafaa au laa, wataalam watakwenda uwandani wakati kipande hiki kitakapotakiwa kuanza kujengwa na kupitia upya ule usanifu na kama kutakuwa na marekebisho basi wataalam watafanya hayo marekebisho yatakayohitajika.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Barabara ya Mtakuja – Nyarugusu – Bukoli – Kakola nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari mkandarasi alishapatikana na kinachosubiriwa sasa hivi ni kwamba mkataba huo upo kwa Mwanasheria Mkuu kwa ajili ya vetting, ahsante.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, Serikali ipo hatua gani kwenye ujenzi wa kipande cha barabara kutoka Katoro hadi Daraja la Nyikonga kwenye Barabara ya Katoro – Ushirombo?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante, barabara inayoanzia Ramadhan – Iyai inayounga Mkoa wa Njombe kupita Jimbo la Njombe, Halmashauri ya Mji wa Njombe – Wanging’ombe, ni lini barabara hii itapata fedha za kutosha ili ikamilishwe?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ahsante, Ramadhan – Iyai kilometa 74 imeshafanyiwa usanifu na kwa sasa tumekuwa tukiijenga kwa awamu na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti ya mwaka tunaouendea wa 2025/2026 tumeitengea fedha ili iweze kuanza kujengwa, ahsante.