Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kujenga miundombinu ya maji katika vijiji vya Kipunda, Minyughe, Ighombwe, Makungu, Mpetu, Magungumka na Mnang’ana?

Supplementary Question 1

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana, sana, sana, ambayo kimsingi yatawatia moyo sana wapiga kura wangu pamoja na wananchi wa Jimbo la Singida Magharibi kutoka kwa Mheshimiwa Waziri, naomba kuuliza swali dogo la nyongeza. Mradi wa Maji wa Kata ya Mtunduru umechukua muda mrefu sana katika kukamilika.

Nilikuwa nataka nijue; je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kutoa agizo kwa Serikali ku-release fedha haraka ili mradi wa maji wa Mtunduru pamoja na vijiji vya Igombwe uweze kukamilika haraka?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza kama yangu Mheshimiwa Kingu. Kiukweli wewe ni Mbunge unayetosha mpaka chenji inabaki. Kubwa ambalo ninataka niseme, sisi Wizara ya Maji tunapokea fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji kupitia Mfuko wa Maji kila mwezi. Ndani ya mwezi huu tutatoa fedha kwa ajili ya mradi wako kuhakikisha tunaukamilisha. Ahsante sana (Makofi)

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kujenga miundombinu ya maji katika vijiji vya Kipunda, Minyughe, Ighombwe, Makungu, Mpetu, Magungumka na Mnang’ana?

Supplementary Question 2

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya swali la nyongeza. Kwa kuwa kuna kero kubwa ya maji katika Kata za Ruaha, Mikumi, Ulaya, Tindiga na Malolo; na Serikali inatambua hilo:-

Je, ni lini Serikali itakwenda kutatua shida ya maji katika Kata hizo? Nashukuru. (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge, lakini sisi kama Wizara ya maji kwa dhati kabisa tunataka kumaliza tatizo la maji Mikumi pamoja na Morogoro. Hakuna sababu hata moja ya wananchi wa Morogoro na Mikumi kulalamikia suala la maji ilhali wana vyanzo vya maji vya kutosha. Kwa hiyo, sisi kama Wizara ya Maji tumejipanga sasa kujenga miundombinu ili wananchi wako wa Mikumi waweze kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upendeleo mkubwa baada ya bajeti nitafika katika Jimbo la Mikumi ili kuhakikisha kwamba tunakwenda kufanya kitu pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kujenga miundombinu ya maji katika vijiji vya Kipunda, Minyughe, Ighombwe, Makungu, Mpetu, Magungumka na Mnang’ana?

Supplementary Question 3

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Changamoto za maji zilizopo katika Jimbo la Kalenga kwa Kata za Lumuli, Masaka, Kiwele, Luhota, Kalenga yenyewe na Magulilwa zimekuwa ni kubwa sana:-

Je, Serikali mna mkakati gani sasa wa kuhakikisha wananchi hawa wanapata huduma za maji safi na salama? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kilio hiki cha wananchi wake, lakini kubwa sisi kama Wizara ya maji, tumepewa maelekezo mahususi kabisa na Mheshimiwa Rais wetu kipenzi Mama Samia Suluhu Hassan; na akaenda mbali kabisa, kwamba tukizingua atatuzingua. Sisi hatupo tayari kuzinguliwa, tutakwenda kuhakikisha kwamba wananchi wako wanapata huduma ya maji. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kujenga miundombinu ya maji katika vijiji vya Kipunda, Minyughe, Ighombwe, Makungu, Mpetu, Magungumka na Mnang’ana?

Supplementary Question 4

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kumwuliza swali Mheshimiwa Waziri kuhusiana na mradi wa maji wa Hanga, Mawa na Msindo ambapo upembuzi yakinifu ulishafanyika na uko Wizarani:-

Je, Serikali inaweza kutueleza ni lini mradi huo au inaweza ikaweka katika bajeti hii mradi huo ukaanza? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeze kaka yangu Mheshimiwa Kawawa kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya katika Jimbo lake la Namtumbo. Wizara yetu ya maji jukumu letu mahsusi ni kuhakikisha wananchi wa Tanzania na Namtumbo wanapata huduma ya maji. Namwomba sana kaka yangu, eneo kama mradi unahitaji kibali na sisi kama Wizara ya Maji tupo tayari kutoa kibali na mradi ule uanze na wananchi wako waweze kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kujenga miundombinu ya maji katika vijiji vya Kipunda, Minyughe, Ighombwe, Makungu, Mpetu, Magungumka na Mnang’ana?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Nami naomba kuuliza swali dogo la nyongeza kuhusiana na ahadi ya Serikali ya kupeleka matawi ya maji katika vijiji vilivyopo pembezoni mwa bomba kubwa la maji safi na salama yaliyotoka katika mto simba Mlimani Kilimanjaro kwenda Longido na vijiji hivyo ni Eliarai hasa Kitongoji cha Himotong, Tingatinga, Ngareiyani na Sinya?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge. Kiukweli historia kubwa ambayo umeiacha Longido ni juu ya ule mradi wa shilingi bilioni 16 ambao tumeutekeleza katika Jimbo lako.

Kwa hiyo, eneo lile ambalo limepitwa na bomba kuu vijiji upande wa kulia wa bomba kuu na kushoto, zaidi ya kilometa 12 navyo tutavipatia huduma za maji safi na salama. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kujenga miundombinu ya maji katika vijiji vya Kipunda, Minyughe, Ighombwe, Makungu, Mpetu, Magungumka na Mnang’ana?

Supplementary Question 6

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ina Kata 20 na vijiji 76, lakini bado upatikanaji wa maji ni wa shida sana hasa hasa kwenye vijiji vya Kihangara, Makata, Kikulyungu, Nahoro, Lilombe, Ngorongopa, Mkutano, Mtawatawa, Kimambi na Nanjegeja.

Mheshimiwa Waziri, ni lini vijiji hivi vinaweza kupatiwa maji safi na salama?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ukimwona mtu mzima analia ujue kuna jambo. Mheshimiwa Mbunge wa Liwale amekuwa akilia sana juu ya suala zima la maji katika Jimbo lake. Sisi kama Wizara ya Maji tumewapatia fedha wakala wa Uchimbaji visima DDCA waende katika Jimbo lako la Liwale waende wakachimbe visima ili wananchi wako waweze kupata huduma ya maji safi na salama. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kujenga miundombinu ya maji katika vijiji vya Kipunda, Minyughe, Ighombwe, Makungu, Mpetu, Magungumka na Mnang’ana?

Supplementary Question 7

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana nami kuniona. Changamoto zilizopo katika Jimbo la Singida Magharibi hasa kwenye miundombinu ya maji zinafanana sana na zile zilizoko Arumeru Mashariki, hususani Kata ya Keri ambayo ina taasisi nyingi za Serikali:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuja kukarabati ile miundombinu na kuhakikisha kwamba wananchi wanapata maji safi na salama kwenye kata hiyo pamoja na Embaseni, Maji ya Chai, Kikatiti, Maroroni na Majengo? Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikushukuru. Nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwani amekuwa mfuatiliaji mkubwa hususan wananchi wake wa Arumeru. Tunachotaka ni kujenga commitment katika Wizara yetu ya Maji kupitia bajeti yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, maoni makubwa ya Waheshimiwa Wabunge tumeyazingatia, nataka nikuhakikishie maeneo ambayo ameyaeleza tutayafanyia kazi kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma ya maji safi na salama. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kujenga miundombinu ya maji katika vijiji vya Kipunda, Minyughe, Ighombwe, Makungu, Mpetu, Magungumka na Mnang’ana?

Supplementary Question 8

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Serikali iliahidi kupeleka visima 23 kwenye Halmashauri ya Mji wa Tarime kuweza kupeleka visima hivyo pembezoni mwa kata ambazo zipo nje ya mji tangu mwaka 2018.

Ni lini sasa Serikali itakwenda kuchimba visima hivyo wakati tukisubiria mradi wa Ziwa Victoria?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana dada yangu Mheshimiwa Matiko. Maji hayana mbadala. Maji ni uhai, nasi hatupo tayari kupoteza uhai wa wana Tarime. Kabla ya mwaka huu wa bajeti kwisha tutafanya shughuli hiyo kuhakikisha wananchi wake tunawachimbia visima vya maji. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kujenga miundombinu ya maji katika vijiji vya Kipunda, Minyughe, Ighombwe, Makungu, Mpetu, Magungumka na Mnang’ana?

Supplementary Question 9

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa pamekuwa na malalamiko ya mara kwa mara kwa watumiaji wa maji kubambikizwa bili:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kubadilisha mfumo wa kufunga mita ambao zitakuwa za malipo kwanza kama Luku ya umeme?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge, Mzee wangu, Mzee Hussein. Kiukweli kongwe huvusha, tunakushukuru sana. Kubwa ambalo nataka kusema, kizuri huigwa. Tumeona wenzetu wa TANESCO za kuwa na mita hizi za Luku, nasi kama Wizara ya Maji tuna pre-paid meter ambapo tumeshaanza na tumefunga katika baadhi ya taasisi. Mkakati wetu na maelekezo kwa mamlaka zetu zote za maji ni kuhakikisha tunajielekeza huko katika pre-paid meter ili kuhakikisha kwamba wananchi wanalipa bili halisia bila ya usumbufu wowote. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa kujenga miundombinu ya maji katika vijiji vya Kipunda, Minyughe, Ighombwe, Makungu, Mpetu, Magungumka na Mnang’ana?

Supplementary Question 10

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kufahamu kwa Mheshimiwa Waziri: Ni lini miradi mikubwa ya kutatua changamoto ya maji kwa hatua ya awali iliyopo Jimbo la Ndanda itatekelezwa, zaidi kwenye Kata za Namajani, Mpanyani, Msikisi pamoja na Chiwale? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nampongeza Mheshimiwa Mbunge, kaka yangu Cecil Mwambe, kwa kweli amekuwa mfuatiliaji mkubwa hasa katika Jimbo lake la Ndanda. Ahadi ambayo nampa katika maeneo ya kipaumbele nitakayokwenda mimi mwenyewe baada ya Bajeti, ni katika eneo lake katika Jimbo la Ndanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, kubwa ni kwamba katika Bajeti hii pia tumezingatia ushauri wa Waheshimiwa Wabunge. Ni imani yangu maeneo ambayo ameyataja yatakuwemo ili kuhakikisha tunakwenda kutatua tatizo la maji. Ahsante sana. (Makofi)