Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Mradi wa Maji wa Kintinku- Lusilile katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue nafasi hii kuishukuru sana Serikali, lakini nimshukuru Waziri kwa majibu mazuri na kwa juhudi ambazo wanaendelea kuzifanya kuhakikisha kwamba huu mradi unakamilika.

Mheshimiwa Spika, nina maswali madogo mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa tayari vijiji vitatu vimeanza kupata maji, ni nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba zile Jumuiya za Watumia Maji zinakuwa jumuiya endelevu zenye uongozi imara hususani kuweka mafundi katika ngazi ya kata ili waweze kusaidia?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kuna maeneo ambayo Wizara imechimba visima mara tatu wamekosa maji, kwa mfano; Kijiji cha Mpapa, Igwamadete na hata Mazuchii. Nini mpango wa Serikali kuja na njia mbadala kunusuru vijiji hivi? Ahsante sana.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

MHE. NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Dkt. Pius Chaya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nipende kupokea pongezi zake, lakini ni kwa sababu ya mashirikiano aliyonayo Mheshimiwa Mbunge na tuendelee kushirikiana lengo ni kuona tunapeleka maji kwa wananchi wetu.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na jumuiya kuwa na mafundi ngazi ya kata tayari hili ni agizo limeshatolewa na Mheshimiwa Waziri na maeneo mengi yameshafanya. Hivyo nipende kutoa agizo kwa watendaji waliopo katika jimbo lako kama hawajafanya hivyo wanapaswa kufanya hivyo haraka iwezekanavyo kuwa na fundi ngazi ya kata.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na njia mbadala; sisi kama Wizara maeneo yote ambayo yana changamoto ya maji ardhini, tunaendelea kuona chanzo kilicho karibu kiweze kuleta maji safi na salama. Mheshimiwa Mbunge hili tuendelee kushirikiana kama ambavyo tumekuwa tukishirikiana, lengo hivi vijiji ambavyo maeneo haya maji ardhini ni shida, basi nao tuweze kuwapelekea kupitia njia nyingine.