Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Nimrod Elirehemah Mkono (1 total)

Butiama linafanana sana na swali lililoulizwa hapo nyuma; nataka kujua, kwanini maji kutoka Mgangu kwenda Butiama hayajafika, sasa ni kipindi kama miaka 20. Itatokea lini maji yafike pale Butiama?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, tayari tunakamilisha usanifu wa mradi wa Mgango Kyabakari na tumeshaomba fedha kutoka Benki ya Maendeleo KFW kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo, mradi huo utakapokuwa umekamilika utapita kwenye vijiji vingi. Mradi huu tunaukarabati; kwasababu ni mradi ambao upo, tunafanya ukarabati kuhakikisha kwamba tunasambaza maji maeneo mengi na tunaongeza chanzo cha upatikanaji wa maji.
Kwa hiyo, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mradi huu tunao tayari kwenye andiko na tukishamaliza usanifu, wakati wowote tunaanza kusambaza maji na tutarudi nyuma zaidi, tutaenda mpaka vijiji vya Byaiku Musoma, tutapitisha maji kule. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge, mradi huu tunao.