Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Rhoda Edward Kunchela (34 total)

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Katika
Mkoa wa Katavi kumekuwa na changamoto kubwa ya miradi ya maji kuendelea
kusuasua kwisha. Je, ni lini sasa Serikali itasema mikakati ya kujenga hii miradi ili
iishe kwa wakati, kwa sababu pesa nyingi zimekuwa zikitumika mfano, kwenye
Kata ya Ugala ambako kuna mradi mpaka sasa ni miezi sita, mradi umesimama.
Sasa, ni lini Serikali itamaliza kujenga hii miundombinu ya umwagiliaji.
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika,
kwanza kabisa Mkoa wa Katavi, eneo la Mpanda linahitaji lita milioni 11 kwa siku,
lakini sasa hivi maji yanayozalishwa ni lita milioni 3.5. Tayari tumeshakamilisha
mradi wa Ikolongo na wananchi wanaendelea kupata huduma; lakini tuna
miradi miwili ambayo tunasaini mwezi huu kwa ajili ya kuleta maji Mji wa
Mpanda. Kwa upande wa eneo la Ugala kwanza lina bwawa moja kubwa
ambalo linaweza kuhudumia ule Mji wa Ugala. Sasa hivi kupitia kwenye
Halmashauri tunayo miradi ambayo inaendelea kuhakikisha kwamba wananchi
wa Ugala wanapata huduma ya maji.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami nataka kuuliza swali la nyongeza kuhusiana na elimu Mkoa wa Katavi. Ukosefu wa Chuo Kikuu cha Kilimo Mkoa wa Katavi umeleta usumbufu kwa wananchi wa Katavi. Serikali ilitenga pesa kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha Kilimo lakini chuo hicho kimeyeyuka. Ni nini mkakati wa Serikali kufuatilia zile pesa zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha Kilimo Mkoa wa Katavi?
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Chuo kikuu kilichokuwa kinategemewa cha Mkoa wa Katavi kilikuwa kinadhamiriwa kujengwa kwa ushirikiano wa Halmashauri ya Mpanda pamoja na wawekezaji ambao walikuwa ameingia nao ubia. Kwanza katika taratibu zilizokuwa zinaendelea kulikuwa na suala la mbia kutaka kupewa dhamana ya Serikali katika kujenga chuo hicho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hilo tuliona kwamba, kama mtu anahitaji kujenga chuo, wakati yeye tunategemea kwamba ni mwekezaji kwa maana kwamba atakuja kuwekeza katika kile chuo, dhamana ya Serikali inaweza ikasababisha mtu kuchukua deni mahali na kukimbia na kazi isiwe imefanyika. Ni vema mwekezaji awe ni mwekezaji wa kweli na awekeze kadri inavyotakiwa. Hata hivyo, kwa fedha zilizotolewa Halmashauri ya Mpanda inafahamu juu ya mambo yake na hivyo kwa kutumia Baraza lao wafuatilie na kuona kwamba fedha zao hazipotei.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Waziri nilitaka kufahamu wakazi wa
Mkoa wa Katavi wamekuwa wakisubiri sana mradi ambao unaendelea kujengwa mradi wa maji wa Ikolongo B, wakazi wa Kata ya Ilembo, Misunkumilo, Kakese pamoja na maeneo mengine mradi huu umepita nyuma ya hizo Kata, lakini wakazi hawa wanakosa maji lakini pia wanatumia maji ambayo ni mchafu ya kutoka kwenye mabwawa pamoja na mito. Sasa naomba unieleze kwamba ni lini mradi huu utakamilika kwa sababu Serikali tayari ilishatenga pesa lakini mradi bado unasuasua? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna baadhi ya sehemu zingine kwamba miradi inasuasua na mnakumbuka kwamba hata Mheshimiwa Rais alivyofika Mkoa wa Lindi aliweza kutoa maelekezo mahususi kwa mkandarasi anaejenga mradi wa maji pale katika Mji wa Lindi na hii ina maana kwamba maana yake ni maeneo mbalimbali kulikuwa na tatizo kubwa hasa baadhi ya wakandarasi wanaoshindwa kutimiza vizuri wajibu wao, wengine wameomba kazi lakini baadae wakienda kule site wanashindwa kutimiza wajibu wao, lakini naomba nikuhakikishie kwamba Serikali hivi sasa inafanya vetting kwa Wakandarasi wote ambao wanashindwa kutimiza wajibu wao, lengo kubwa ni kwamba atakaposhindwa bora atolewe aletwe mkandarasi mwingine aweze kutimiza wajibu wale na Mkandarasi huyu tutaenda ku-assess kazi yake
inaendaje. Lakini hata hivyo ulizungumza ajenda suala zima la kwamba Wananchi wengine ambao wa maeneo yale wanakosa maji, tutafanya mahitaji halisi kuangalia kwa sababu siwezi kuzungumza hapa moja kwa moja kule site
sijaangalia lakini najua suala hilo linamhusu hata ndugu yangu Richard Mbogo, Mbunge wa Nsimbo pale nilivyofika nae ana hoja hiyo hiyo inayolingana ni kwamba tutaangalia kwa kina
tutafanyaje lengo kubwa ni kwamba wananchi wote wa Tanzania kama lengo la Serikali hii kuwatua wakina mama ndoo ya maji liweze kufikia; haliwezi kufikia lazima tupambane wote kwa pamoja, aliyekuwa mzembe tumtoe katika daraja hilo la uzembe awe katika suala zima la sawa sawa wananchi wapate huduma ya maji.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, nataka kuuliza swali kuhusiana na changamoto ya gari katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda. Hospitali hii imepandishwa hadhi kutoka kwenye Wilaya kwenda kwenye Mkoa, lakini
pia gari lililopo pale ni bovu na halikidhi haja ya Watanzania
waliopo katika Mkoa wa Katavi. Je, ni lini Serikali itaongeza
nguvu katika Halmashauri ili gari lingine lipatikane katika
Manispaa ya Mkoa wa Katavi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, kwanza Hospitali ya Mpanda haijapandishwa hadhi na kuwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ila kwa sasa inatumika tu kama Hospitali
ya Rufaa ya Mkoa lakini yenyewe bado ni Hospitali ya Wilaya ya Mpanda. Kwa sasa Mkoa wa Katavi unajenga Hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa, wapo kwenye mchakato huo.
Mheshimiwa Spika, kuhusu gari la wagonjwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda ni kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi kwamba utaratibu ni kwa Halmashauri yenyewe kuweka kipaumbele kwenye kununua gari la wagonjwa kama Halmashauri inaona inalihitaji kwa wakati huo. Sisi kama Serikali Kuu, wajibu wetu siyo kuwapangia vipaumbele Halmashauri zote nchini.
Halmashauri zenyewe zinapaswa ziweke vipaumbele vyao, watumie vyanzo vyao mbalimbali vya fedha na hata ruzuku inayotoka Serikali Kuu wanaweza wakaitumia kwa namna
yoyote ile watakavyoona wao wenyewe kwenye Halmashauri yao ili waweze kununua gari la wagonjwa.
Mheshimwa Spika, kwa hivyo kuhusiana na Mpanda mahsusi kama tutapata fursa ya misaada ya magari, nilikwishamuahidi Mheshimiwa Kakoso lakini pia Mheshimiwa Mhandisi Kamwelwe kwamba tutatoa kipaumbele cha kipekee kwa Mkoa huu mpya wa Katavi kwa sababu nilifanya ziara pale na nikaona kwa kweli miundombinu yake ipo katika hali mbaya. Nilisema kama kutatokea sisi tukapata ambulances pale Wizara ya Afya huu ni katika Mikoa ambayo tutaipa kipaumbele cha kwanza.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nilitaka nimuulize Mheshimiwa Waziri. Imekuwa ni kero kubwa kwa wananchi wa Manispaa ya Mpanda kuendelea kusubiri miradi ambayo haitekelezeki, lakini pia ni wiki sasa maji hayatoki. Sasa ni nini tamko la Serikali ili kuhakikisha wananchi hao wanapata maji lakini pia wasiendelee kulipa bili ambazo hawapati maji?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, Mji wa Mpanda mahitaji ya maji ni lita 10,200,000 kwa siku. Hadi sasa kwa mradi uliopo unatoa maji lita 3,150,000 kwa siku. Sasa hivi kuna miradi miwili ambayo wakati wowote itasainiwa, miradi hiyo ikikamilika basi itaongeza kiwango cha maji hadi kufikia lita 6,000,000. Kwa hiyo, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba utekelezaji unaendelea. Changamoto kama maji hayajapatikana, kwanza tufahamu kwamba maji yaliyopo yanatosheleza kwa asilimia 30 tu. Kwa hiyo, si suala kwamba maji hayapo, hapana, ni kidogo. Serikali inaendelea kujitahidi kuhakikisha kwamba yale mahitaji ya lita 10,200,000 yanafikiwa na tatizo la maji kutokupatikana halitakuwepo tena.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Na mimi nilitaka kumwuliza Mheshimiwa Waziri, ni lini Serikali itakuja kutatua mgogoro wa wananchi katika Kata ya Kakese katika shamba la Benki ya NBC? Shamba hili lilikuwa la uwekezaji lakini mpaka sasa shamba lile lipo limekaa dormant na wananchi hawakuweza kuendelea kulima shamba lile na shamba lile bado lina mgogoro.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri haoni kwamba
ule ni upotevu wa malighafi na wananchi wanashindwa kuendelea kuendeleza lile shamba ili waendelee kujipatia kipato?
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Rhoda Kunchela, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, nitoe ufafanuzi tu kwamba migogoro yote kwa ngazi tofauti siyo kwamba lazima itatuliwe na ngazi ya Wizara. Migogoro mingi na hasa ya kwenye kata na vijiji inatatuliwa na mamlaka zilizoko kule ikiwemo Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, kuna Ofisi ya Kanda ya Ardhi katika maeneo yale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu amesema mgogoro huu uko kwenye ngazi ya Kata, naomba tu Mkuu wa Wilaya wa eneo husika pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri husika waende kwenye Kata yenye mgogoro waweze kutatua mgogoro ule na wananchi waweze kupewa haki yao kama wanastahili kwa sababu amesema lilikuwa linamilikiwa na NBC, lakini siyo kila mgogoro lazima uje Wizarani.
Waheshimiwa Wabunge, nawaomba sana, migogoro mingi wakati mwingine hata tunapokwenda kufanya ziara, unakuta ni mgogoro ambao ungeweza kumalizwa na Mkuu wa Wilaya pale au Mkuu wa Mkoa au Mkurugenzi mwenyewe husika katika eneo lile. Ukienda pale unakuta wewe unakuwa kama mtazamaji, watu wanamaliza wenyewe.
Mheshimiwa Spika, nashauri tu ile ambayo inahitaji Wizara basi ijulikane na ile inayohudumiwa na Mkoa na Wilaya basi nao wachukue nafasi yao kuhakikisha kwamba wanatatua migogoro hii na isiwe ni kikwazo kwa wananachi.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante na nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, Mheshimiwa Rais kabla ya Mei Mosi alitoa kauli akiwa Hai kwamba anaondoa kero ndogo ndogo za ushuru ambazo wanalipishwa watu ambao wanafanya biashara ndogo ndogo, akina mama pamoja na vijana.
Swali langu ni kuwa kauli hii ya Rais ililenga kuondoa
kero ya huu ushuru ndogo ndogo katika Halmashauri ya Hai peke yake au katika masoko yote Tanzania nzima likiwemo Soko la Buzogwe, soko kubwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda, Soko la Mpanda Hoteli na masoko madogo yote yaliyoko katika Mkoa wa Katavi? Kauli hii pia inawalenga watu wa Mkoa wa Katavi?
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, nilitaka kufahamu, kumekuwa na wawekezaji ambao wamekuwa wakienda kuihadaa Serikali kuomba maeneo kwa ajili ya uwekezaji, ikiwepo katika Kata ya Kekese ambako kuna mwekezaji ambaye alichukua eneo zaidi ya eka 1,000 akiwahadaa wananchi kwamba anahitaji kuwapatia ajira. Lakini mpaka sasa shamba lile analitumia kwa manufaa yake binafsi, hakuna ajira zozote alizotengeneza katika hilo shamba lililopo katika Kata ya Kekese, Manispaa ya Mpanda. Nini tamko la Serikali kumuwajibisha mwekezaji huyu kwa sababu anatumia pesa za wananchi na watu wa Katavi, vijana pamoja na akina mama wanahangaika hawaelewi nini cha kufanya?
WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ni kweli suala la ushuru na tozo ndogo ndogo limekuwa kero ya muda mrefu kwa wakulima wa nchi hii na Rais alikwishatoa maelekezo kuanzia wakati wa kampeni na katika mikutano mbalimbali kwamba, Serikali iangalie namna ya kupunguza, kama si kuondoa kabisa shuru tozo na hizi ambazo zinashumbua wananchi na zitaondolewa sio kwahalmashauri moja moja kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Spika, niseme tu kwamba Mheshimiwa avute subira ya siku chache sana zijazo hazizidi 13 atasikia kwa kiwango gani Serikali itafutilia mbali tozo na ushuru mwingi sana ambao unasumbua wananchi mbalimbali. Tunadhamiria kufanya hivyo na tuseme tu kwamba nina hakika kila mtu atafurahi jinsi tutakavyokuwa tumeshughulikia hili tatizo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, na kwa upande wa mashamba ambayo wawekezaji mbalimbali wameyachukua kwa lengo la kuyaendeleza halafu hawayaendelezi uko utaratibu unaofanywa na Wizara yetu ya Kilimo ya Ardhi, mashamba haya yanafuatiliwa na wale wote ambao hawatekelezi masharti yale yaliyo katika mikataba yao. Mashamba haya yako katika hatua mbalimbali, mengine yameshachukuliwa yamefutwa, mengine yanaendelea kufanyiwa utaratibu wa kuyafuta ili yarejeshwe kwa wananchi au mikononi mwa Serikali.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Majibu ya Mheshimiwa Waziri nadhani hayana uhalisia na mazingira ya Manispaa ya Mpanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwezi Machi, 2014 Halmashauri ya Mpanda ilitenga shilingi milioni 200 kwa ajili ya ununuzi wa gari la kukusanya taka, gari la kisasa na siyo haya malori mawili ambayo umeyasema.
Kutokana na ubadhirifu ambao umefanyika kwenye Manispaa hii, Serikali inachukua hatua gani kwa huyu mzabuni aliyetumia fedha hizi na mpaka sasa hajarudisha na baadhi ya hao watendaji ambao wamekula pesa hii, wananchi wa Manispaa ya Mpanda hivi tunavyoongea wanashinda na takataka ndani, wanashindwa kuzitoa na Manispaa imeshindwa kukusanya hizi taka kwa wakati. Serikali inamchukulia hatua gani huyu Ndugu Kisira pamoja na watendaji waliokula pesa hizi katika Manispaa ya Mpanda?(Makofi)
Swali la pili, imekuwa ni tabia ya Serikali kuendelea kuhamasisha wananchi kufanya usafi kwenye maeneo yao, lakini kitu kibaya zaidi ni kwamba wananchi hawa wanalazimishwa kufunga maduka, kila siku ya Jumamosi kuanzia saa 1:00 asubuhi mpaka saa 4:00 aasubuhi na siyo Mkoa wa Katavi peke yake au Manispaa ya Mpanda peke yake ni nchi nzima, ikiwepo na maduka ya Dar es Salaam, Kigoma, Mbeya, Mwanza pamoja na Katavi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa tabia hii ya kuendelea kufunga maduka, je, Serikali hamuoni kwamba mnapoteza uchumi wa wananchi wao kuendelea kufunga maduka na huku wakiendelea kufanya usafi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Rhoda tutende haki, swali lako ulilouliza halafu una ajenda, inawezekana swali lako ungeli-frame vizuri lingepata majibu mazuri sana. Kwa sababu swali lako lilikuwa linajenga suala la ubadhirifu wa fedha zilizotengwa, ungelitengeneza vizuri halafu tungeweza kupata majibu mazuri sana katika hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, nimesema kwamba pale kuna magari ya taka mawili, kama kuna suala la ubadhilifu hiyo ni ajenda nyingine, tunachotakiwa kukifanya ni kwamba hatuvumilii ubadhirifu wa aina yoyote, na kama ubadhirifu huo upo, tutaenda kuufanyia kazi tutaenda kufuatilia nini kilichojiri katika Manispaa ya Mpanda kama fedha zilizitengwa lakini hazikutumika vizuri katika suala hilo.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala zima la ajenda kwamba siku ya Jumamosi wananchi wanafunga maduka, kumbukumbu yangu Waziri Mkuu hapa aliulizwa na Mheshimiwa Ulega, Mbunge wa Mkuranga katika suala ya siku ya Jumamosi utaratibu wa kufanya, lengo kubwa ilikuwa usafi ufanyike lakini usizuie shughuli za wananchi katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, agizo hili limeishatolewa kwamba Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya katika maeneo yao tunapofanya utaratibu wa usafi tuangalie modality nzuri usafi ufanyike, lakini kama kuna mambo mengine ambayo saa nyingine yanahusu shughuli mahsusi zinaweza kufanyika. Hapa Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa maelekezo naomba tufanye rejea ile vizuri tusitoe majibu mawili itakuwa ni sub-standard siyo vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niichukue kwamba hoja yako ya usafi ni ajenda yetu ya Kitaifa, lazima kama Wabunge, lazima kama Viongozi tusimame pamoja katika jambo hili. (Makofi)
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami nataka niulize swali la nyongeza. Kwa wachimbaji wadogowadogo waliopo katika Mkoa wa Katavi hususan katika Machimbo ya Ibindi na Kapanda, vijana hawa wamekuwa na changamoto kubwa nyingi mno ikiwepo gharama kubwa ya kukata leseni za uchimbaji lakini pia gharama kubwa ya dawa za kusafishia dhahabu wanazopata na gharama za umeme pia ziko juu. Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha sasa inawasaidia hawa vijana kupunguziwa gharama hizi ambazo ni kero? Tamko la Serikali linasema nini ili kuwasaidia vijana kupata mikopo ili wajiendeleze kiuchumi na kupata kipato?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, ni kweli kabisa maeneo ya uchimbaji maarufu sana kwa maeneo ya Mpanda ni pamoja na Ibindi, Kapanda pamoja na Dilifu. Hata hivyo, nimtaarifa Mheshimiwa Mbunge kwamba hatua ambazo Serikali imechukua, la kwanza kabisa ni kurasimisha maeneo hayo ambayo nimeyataja kuwa maeneo maalum kwa ajili ya wachimbaji wadogo na wapo wachimbaji wadogo wazuri sana kwenye eneo lako ikiwa ni pamoja na Mheshimiwa Kapufi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kuhusu mkakati ambao tunafanya…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Niseme tu, tumetoa ruzuku mwaka juzi kwa wachimbaji wa Ibindi na Kapanda na bado tunawapatia elimu na uwezeshaji kwa ajili ya uchimbaji mzuri kwa wachimbaji hawa wadogo.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nilitaka nipate ufafanuzi kutoka kwa Mheshimiwa Waziri, kuna ujenzi wa barabara ambao unaendelea ya kutoka Sumbawanga – Stalike – Kigoma. Barabara ile kuna maeneo ambayo tayari ujenzi umeshapita na wananchi wanaoishi pembezoni mwa barabara ya kwenda Kigoma wameshahamishwa na baadhi ya wananchi tayari walishalipwa fidia lakini kuna wengine wamerukwa. Sasa Serikali inatumia utaratibu gani kuendelea kuwabagua kuwalipa baadhi ya wananchi fidia na wengine kuwaruka?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ujenzi wa barabara hii ya kutoka Sumbawanga - Stalike - Kigoma unaendelea na unafahamu kwamba kwa sasa tunajenga vile vipande viwili ambavyo wakandarasi wako kwenye eneo na lingine lile la kutoka Mpanda - Tanganyika unafahamu kwamba tuna fedha lakini napo tunatarajia mkandarasi hivi karibuni atakuwepo site na tunaendelea kutafuta fedha kukamilisha kabisa hadi Kigoma. Nikuombe tu kwa kawaida ulipaji wa fidia ni kutegemea na makadirio yaliyofanywa na valuers waliopita katika maeneo hayo. Mara nyingi inatokea maeneo mengine kuna watu ama wanarukwa na wakati mwingine wanarukwa kwa sababu wakati ule valuation inafanyika pengine yule mtu hakuwepo. Kwa hiyo, nikuombe tu suala hili tutaendelea kulishughulikia na tushirikiane kuhakikisha kwamba wale waliosahaulika na kama kweli wana haki wapate haki yao. Sisi muda wote tunasema mwenye haki ya kulipwa fidia ni lazima alipwe fidia na kwa vyovyote kama kuna watu ambao hawana haki ya kulipwa fidia hatutawalipa fidia.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kumekuwa na upungufu wa vituo vya polisi nchini. Pamoja na changamoto hizo, lakini polisi hao wamekuwa na changamoto za kukosa magari na mafuta kwa ajili ya kulinda wananchi wetu kwenye maeneo yetu. Vilevile hivi karibuni polisi wamekuwa wakilalamika kwamba magari hayana mafuta, kwa hiyo, wanashindwa kufanya doria kuzunguka kwenye maeneo korofi kwa ajili ya kuwalinda wananchi wa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha sasa polisi hao wanapatiwa mafuta, lakini pia kuongezewa magari kwa ajili ya usalama wa Watanzania? Ahsante.
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia jambo la sskari wetu. Niwahakikishie tu Waheshimiwa Wabunge kwamba katika bajeti hii tuliyopitisha, fedha zilizotengwa kwa ajili ya mafuta, doria pamoja na shughuli nyingine imeongezeka tofauti na iliyokuwa inatoka katika Awamu ya Kwanza ya mwaka wa fedha uliopita. Kwa maana hiyo, tutakuwa tumepunguza kwa kiwango kikubwa ukosefu wa mafuta katika shughuli zetu hizo za doria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2016 tulipokea magari 77 kwa ajili ya askari wetu na kati ya mwezi huu mpaka mwezi wa saba tunatarajia kupokea magari mengine zaidi ya 200 na tutayagawa katika maeneo ambayo yana uhitaji mkubwa wa magari kwa ajili ya shughuli za doria ikiwemo Mikoa kama ya Kagera, Kigoma, Katavi pamoja na maeneo mengine ambayo yanahitaji doria na yanahitaji magari yawepo katika maeneo yale ikiwemo kwa ndugu yangu Mheshimiwa Nsanzugwanko na Mheshimiwa Bilago.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata ya Isulamilomo, Jimbo la Nsimbo katika Mkoa wa Katavi kuna mwekezaji yuko pale, hana leseni na kuna vijana zaidi ya 4,000 hawana leseni, lakini mwekezaji huyu sijui anapata nguvu gani ya kuwazuia hawa wachimbaji wadogo wadogo zaidi ya 4,000 kuchimba lakini zaidi wanapigwa na wananyanyaswa kwenye huu mgodi mpya ulioko katika Jimbo la Nsimbo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nini tamko la Serikali sasa ili tujue nani ni halali kuchimba katika mgodi huu?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninamshukuru kwa kutupa taarifa, lakini atusaidie zaidi mwekezaji huyu ni nani, utatusaidia sana Mheshimiwa Mbunge. Hebu tupatie huyo ni nani halafu tukafanyie kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jibu la msingi ni kwamba maeneo yote ambayo wawekezaji wameyashikilia bila kuyafanyia kazi Serikali sasa inayatwaa kwa mujibu wa sheria ili iwagawie wananchi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge tutakaa pamoja tuone kero hiyo tuitatue kwa mujibu wa sheria, ikiwezekana kabisa tutachukua hatua za kisheria. (Makofi)
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kutokana na changamoto za upungufu wa viwanda katika Mkoa wa Katavi, lakini pia kuna tatizo kubwa linawasumbua wakazi wa Manispaa ya Mpanda.
Je, Serikali iko tayari kufuatialia mashine ya kukoboa na kusaga iliyonunuliwa na Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda ambayo pia iligharimu pesa nyingi mno, mpaka sasa wananchi hawaelewi kwamba mashine hii iko wapi? Sehemu ambayo ilitakiwa kujengwa kwa ajili ya kuiweka ile mashine ili ifanye kazi mpaka sasa lile eneo ni gofu. Wananchi hawaelewi, nini mkakati wa Serikali kusaidia na kuokoa fedha hizi ili wananchi wapate ajira katika Manispaa ya Mpanda?
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge ameuliza swali lake ili kuweka msisitizo. Tumeshakubaliana kwamba tutakwenda kwenye Jimbo lako tuweze kuona hilo suala tulishughulikie. Kwa hiyo, hakuna tatizo Katavi na Rukwa, nimeshazungumza, mikoa yote miwili nitakwenda pamoja na ule mwongozo niliowatolea. Kwa hiyo, masuala yenu nitayashughulikia, tutajipanga upya.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kutokana na majibu ya Mheshimiwa Waziri ni kwamba wananchi hawa watabomolewa nyumba zao na Serikali haitalipa fidia na tafsiri yake ni kwamba wananchi hawa wamevunja sheria.
Mheshimiwa Spika, tarehe 30 Oktoba, 2017 Rais alipokuwa Mwanza, alizuia wananchi wa Mwanza kubomolewa makazi yao. Je, kauli hii ililenga Ukanda wa Mwanza peke yake au ni Tanzania nzima? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, imekuwa ni kawaida kwa Serikali hii ya CCM kuendelea kupeleka huduma za kijamii katika maeneo hayo ambayo wananchi wanabomolewa ikiwepo kata ya Tambukareli, Msasani pamoja na Ilemo, huduma za maji, umeme pamoja na vituo vya kupigia kura lakini leo hii mnakwenda kuwabomolea. Je, ni kwa nini Serikali haina mkakati wa kuhakikisha sasa inazuia huduma hizo katika maeneo hayo kwa sababu hayajapimwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Spika, wakati mwingine ni lazima Waheshimiwa Wabunge tushirikiane na Serikali na tufuatilie taarifa rasmi zinazotolewa na Serikali. Mheshimiwa Rais kauli yake haikumaanisha waliovamia hifadhi ya reli.

Mheshimiwa Spika, wale ambao wamevamia hifadhi nya reli ambapo vipimo vyake vipo kabla ya mwaka 1904 wataondolewa bila kulipwa fidia yoyote na wale ambao reli itawafuata kwenye maeneo yao utaratibu wa fidia unaendelea kupangwa na watalipwa kwa mujibu wa sheria. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili linauliza kuhusu huduma zinazoendelea kupelekwa. Kiukweli ni kwamba sehemu nyingi sana ambazo ni maeneo ya hifadhi ya reli baadhi ya watumishi wasiokuwa waaminifu wameendelea kuwapimia viwanja wananchi. Wale tulikwishaongea na kwamba Wizara ya Ardhi kwa kushirikiana na TAMISEMI watawachukuliwa hatua watumishi wasiokuwa waaminifu lakini bado nina hakika wananchi walikuwa wanajua kwamba wanapimiwa maeneo ambayo si sahihi kwao kwenda kujenga kwa sababu yanaeleweka wazi.
Mheshimiwa Spika, labda nitoe mfano kidogo, maeneo yaliyopita umeme mkubwa wa Gridi ya Taifa yako wazi na wananchi hawaendi kujenga kule, lakini wao hawalalamikiwi isipokuwa sehemu ya reli ambayo ni muhimu sana kwa Taifa letu watu wanaivamia na hawaulizwi. Kwa hiyo, ukweli kwamba huduma zilizopelekwa zitaondolewa uko palepale kwa sababu hata waliojenga mabondeni nao huduma zinaondolewa ili kupisha huduma za kijamii, ahsante.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Tatizo la Iramba Mashariki linafanana kabisa na matatizo ambayo yako katika Mkoa wa Katavi. Uhaba wa Madaktari Bingwa katika Mkoa wa Katavi umekuwa ni changamoto kubwa sana, kwa mfano katika Kata za Mishamo, Chamalendi, Kakese pamoja na Mwamkulu, ni maeneo ambayo wananchi wamekuwa wakisafiri umbali mrefu kufuata huduma za Madaktari na wanapopewa rufaa kwenda katika Mikoa ya Mbeya pamoja na Dar es Salaam inawagharimu gharama kubwa za kuishi pamoja na za madawa. Sasa nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha wanaharakisha tunapata Madaktari Bingwa katika Mkoa wa Katavi?
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, nakiri kwamba tumekuwa na changamoto kidogo katika upatikanaji wa Madaktari Bingwa, lakini hivi karibuni tumepata kibali cha kuajiri wataalam wapya wa afya na Mkoa wa Katavi ni mmoja k atika mikoa ambayo imepata Madaktari hao.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, katika kipindi cha mpito, tumeongeza udahili katika fani za Madaktari Bingwa, lakini vilevile tumekuwa tunaendesha mobile clinics kwa ajili ya kuwapeleka wale wataalam wachache katika mikoa iliyo pembezoni kwa ajili ya kupata huduma hizo.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Tatizo lililopo Mlimba linafanana kabisa na tatizo la ukosefu maji safi na salama lililopo katika Mkoa wa Katavi. Serikali iko tayari kutumia maji ya Mto Mpanda, Mto Manga, Mto Katuma ili wakazi wa Kata ya Mwamkulu, Kakese pamoja na Kasokola wapate maji safi na salama hususani katika suala la kilimo katika Mkoa wa Katavi? Ahsante. (Makofi)
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshatekeleza miradi mingi ya visima katika Mkoa wa Katavi na tayari tumetumia mito iliyopo kupeleka maji katika Mji wa Mpanda na sasa hivi tunaelekea kuwa na asilimia zaidi 70 ya maji safi na salama katika Mji wa Mpanda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari tumeshapokea andiko na tunalifanyia kazi ili tuweze kumaliza tatizo la maji kabisa katika Mkoa wa Katavi kwa kuchukua maji kutoka katika Ziwa Tanganyika. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ya Chama cha Mapinduzi inafanya kazi kunakikisha mikoa yote inapata maji safi na salama. (Makofi)
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, changamoto zilizopo katika Jimbo la Chilonwa linafanana kabisa na changamoto zilizopo katika Wilaya ya Mpanda, Mkoa wa Katavi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi kuna ujenzi ambao unaendelea kutoka katika Mkoa wa Tabora barabara ya Inyonga - Ipole kuelekea Mpanda. Barabara hii inajengwa lakini wakandarasi hawaweki alama za ujenzi kwamba kuna madaraja yanajengwa, kuna mashimo yamechimbwa na jambo hili limekuwa linasababisha ajali nyingi kwa wakazi wa Mpanda, kwa wakazi wa Mkoa wa Katavi.
Nini tamko la Serikali kuhakikisha inatoa maekelezo kwa hawa wakandarasi ili kupunguza ajali za barabarani katika Mkoa wa Katavi?
WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO:
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Mbunge swali lake la ujenzi wa barabara ya kutoka Katavi mpaka Tabora. Ni kweli Serikali tumeanza ujenzi wa barabara hiyo na hatua tunayokwenda nayo sasa ni hatua ya mobilization yaani makandarasi kwa sasa wanakusanya vifaa vya ujenzi katika maeneo hayo, bado kabisa kazi ya ujenzi haijaanza. Mara itakapoanza kazi ya ujenzi tutaweka alama kuhakikisha kwamba watumiaji wote wanaotumia barabara hiyo wako salama.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa takwimu hizi, kutokana na bajeti ya Mheshimiwa Waziri, bado Serikali hii haijajipanga kutatua tatizo la maji nchini. Mkoa wa Katavi una vituo zaidi ya 148 vinahitaji ukarabati na hivi tunavyoongea, wakazi wa Mpanda pamoja na Katavi hawajapata maji karibu wiki mbili zimepita. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha hivi vituo 148 vinafanyiwa ukarabati na wananchi wanapata maji kwa wakati?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani na kuunda Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Mkoa wa Katavi tayari tumeshachimba visima zaidi ya 40 na wananchi wanapata maji. Kwa hiyo, huduma ya maji katika Mkoa wa Katavi imeongezeka. Kwa sasa tumeshasaini mkataba mmoja ili kuleta bomba lingine kutoka Ikorongo kwa ajili ya Mji wa Mpanda na tayari mkandarasi yuko kazini na tunatarajia kusaini mkataba mwingine wa pili ili kuongeza kiwango cha maji kutoka kilichopo sasa hivi cha lita 3,150,000 ili twende zaidi ya lita milioni sita. Kwa hiyo, kwanza ni kwamba maji Katavi tayari yanaendelea kuongezeka.
Mheshimiwa Spika, lakini pili tulipeleka mashine ili kufanya ukarabati wa visima vyote ambavyo vilikuwa havitoi maji kwa maana ya kuvifanyia flushing na zoezi hilo limefanyika na linaendelea kufanyika ili kuhakikisha vile visima ambavyo uwezo wake wa kutoa maji ulikuwa umepungua basi vinaendelea kutoa maji wananchi waendelee kupata huduma. Kwa hiyo, si kweli kwamba Serikali imeshindwa kutoa maji, tayari kiwango kilichokuwepo tumeongeza na tunaendelea na tutafikisha asilimia 85 itakapofika mwaka 2020.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Majibu ya Mheshimiwa Waziri nadhani hayana uhalisia na mazingira ya Manispaa ya Mpanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwezi Machi, 2014 Halmashauri ya Mpanda ilitenga shilingi milioni 200 kwa ajili ya ununuzi wa gari la kukusanya taka, gari la kisasa na siyo haya malori mawili ambayo umeyasema.
Kutokana na ubadhirifu ambao umefanyika kwenye Manispaa hii, Serikali inachukua hatua gani kwa huyu mzabuni aliyetumia fedha hizi na mpaka sasa hajarudisha na baadhi ya hao watendaji ambao wamekula pesa hii, wananchi wa Manispaa ya Mpanda hivi tunavyoongea wanashinda na takataka ndani, wanashindwa kuzitoa na Manispaa imeshindwa kukusanya hizi taka kwa wakati. Serikali inamchukulia hatua gani huyu Ndugu Kisira pamoja na watendaji waliokula pesa hizi katika Manispaa ya Mpanda? (Makofi)
Swali la pili, imekuwa ni tabia ya Serikali kuendelea kuhamasisha wananchi kufanya usafi kwenye maeneo yao, lakini kitu kibaya zaidi ni kwamba wananchi hawa wanalazimishwa kufunga maduka, kila siku ya Jumamosi kuanzia saa 1:00 asubuhi mpaka saa 4:00 aasubuhi na siyo Mkoa wa Katavi peke yake au Manispaa ya Mpanda peke yake ni nchi nzima, ikiwepo na maduka ya Dar es Salaam, Kigoma, Mbeya, Mwanza pamoja na Katavi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa tabia hii ya kuendelea kufunga maduka, je, Serikali hamuoni kwamba mnapoteza uchumi wa wananchi wao kuendelea kufunga maduka na huku wakiendelea kufanya usafi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Rhoda tutende haki, swali lako ulilouliza halafu una ajenda, inawezekana swali lako ungeli-frame vizuri lingepata majibu mazuri sana. Kwa sababu swali lako lilikuwa linajenga suala la ubadhirifu wa fedha zilizotengwa, ungelitengeneza vizuri halafu tungeweza kupata majibu mazuri sana katika hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, nimesema kwamba pale kuna magari ya taka mawili, kama kuna suala la ubadhilifu hiyo ni ajenda nyingine, tunachotakiwa kukifanya ni kwamba hatuvumilii ubadhirifu wa aina yoyote, na kama ubadhirifu huo upo, tutaenda kuufanyia kazi tutaenda kufuatilia nini kilichojiri katika Manispaa ya Mpanda kama fedha zilizitengwa lakini hazikutumika vizuri katika suala hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala zima la ajenda kwamba siku ya Jumamosi wananchi wanafunga maduka, kumbukumbu yangu Waziri Mkuu hapa aliulizwa na Mheshimiwa Ulega, Mbunge wa Mkuranga katika suala ya siku ya Jumamosi utaratibu wa kufanya, lengo kubwa ilikuwa usafi ufanyike lakini usizuie shughuli za wananchi katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, agizo hili limeishatolewa kwamba Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya katika maeneo yao tunapofanya utaratibu wa usafi tuangalie modality nzuri usafi ufanyike, lakini kama kuna mambo mengine ambayo saa nyingine yanahusu shughuli mahsusi zinaweza kufanyika. Hapa Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa maelekezo naomba tufanye rejea ile vizuri tusitoe majibu mawili itakuwa ni sub-standard siyo vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niichukue kwamba hoja yako ya usafi ni ajenda yetu ya Kitaifa, lazima kama Wabunge, lazima kama Viongozi tusimame pamoja katika jambo hili. (Makofi)
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mkoa wa Katavi bado una changamoto ya kupata maji safi na salama, lakini kibaya zaidi katika Jimbo la Katavi ambalo ni Jimbo la Mheshimiwa Waziri, katika maeneo ya Songambele, Kamsisi na Ilunde hakuna maji kabisa. Sasa Mheshimiwa Waziri ni lini utapeleka maji kwa sababu wananchi hawa umewatelekeza kwa muda mrefu? (Kicheko)
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Spika, nijibu tu swali kwa ufupi kwa Mheshimiwa Rhoda Kunchela kwa sababu amechokoza jimbo langu.
Mheshimiwa Spika, Kamsisi wana visima vitatu tayari na wanapata maji. Songambele wana visima vinne na tayari wanapata maji, Ilunde tayari wana visima vitano na tayari wanapata maji, ndiyo tunaongeza vingine, kwa hiyo tayari jimbo langu linatendewa haki. (Makofi)
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa majibu haya inaonesha kabisa dhahiri kwamba Mheshimiwa Waziri amedanganywa na uhalisia wa wananchi wa Jimbo la Mpanda Vijijini, kutokana na swali hili kwa sababu imekuwa ni mara ya tatu nauliza swali hili, lakini pia Serikali imeshindwa kutatua migogoro pamoja na mauaji yanayoendelea katika kata hizi, Kata ya Kapalamsenga, Ikola, Isengule, Iteteme pamoja na Kalema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vijiji hivi wananchi wamekuwa wanateswa na askari wa Wanyamapori na mwaka jana wamekufa zaidi ya vijana wawili kwa kupigwa risasi na askari wa wanyamapori. Ni nini tamko la Serikali kutokana na vifo na manyanyaso yanayoendelea katika Jimbo hili la Mpanda Vijijini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika majibu haya ndiyo maana nikasema kwamba Mheshimiwa Waziri, amedanganywa. Hakuna ushirikishwaji wowote kati ya Vijiji, Vitongoji pamoja na wananchi. Ni kwa nini Serikali inatumia nguvu wakati wananchi wanatakiwa wapewe elimu, washirikishwe kuliko kulazimishwa kupeleka hizo GN kwenye maeneo ambayo vijiji hawajapewa ramani husika kujua na kutambua mipaka yao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme tu kwamba siyo azma ya Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wake wanateswa, hiyo haturuhusu. Haturuhusu kabisa, lakini pale ambapo wananchi wale ambao wanaenda kuingia katika maeneo ya hifadhi bila kufuata taratibu, hatua za kisheria lazima zichukuliwe. Kuchukuliwa siyo kuwatesa wala kuwapiga, lazima wanakamatwa wanapelekwa katika mikondo ya sheria na hapo wanashitakiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kwenye maeneo ya Mheshimiwa kuna tatizo la namna hiyo, basi nitaomba tuwasiliane baadae ili unipe baadhi ya watu ambao wamepata matatizo hayo, kusudi tuweze kuwachukulia hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wote tunafahamu tunapoenda katika mipango ya matumizi bora ya ardhi hasa katika vijiji lazima mipango iwe shirikishi kwa sababu wanaotakiwa kupanga ni wananchi wenyewe wote wanahusika, sasa akiniambia kwamba wananchi hawakushirikishwa kwa kweli nashindwa kuelewa. Huo mpango lazima upitishwe na mkutano wa Kijiji. Sasa ulipitishwaje kama wananchi hawakushirikishwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama kuna changamoto hizo, basi nitakapokwenda katika hilo eneo basi tukae wote kama Serikali pamoja na wananchi tuone kama kweli hawakushirikishwa au kuna tatizo lingine la mahitaji ya ardhi. (Makofi)
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa majibu haya inaonesha kabisa dhahiri kwamba Mheshimiwa Waziri amedanganywa na uhalisia wa wananchi wa Jimbo la Mpanda Vijijini, kutokana na swali hili kwa sababu imekuwa ni mara ya tatu nauliza swali hili, lakini pia Serikali imeshindwa kutatua migogoro pamoja na mauaji yanayoendelea katika kata hizi, Kata ya Kapalamsenga, Ikola, Isengule, Iteteme pamoja na Kalema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vijiji hivi wananchi wamekuwa wanateswa na askari wa Wanyamapori na mwaka jana wamekufa zaidi ya vijana wawili kwa kupigwa risasi na askari wa wanyamapori. Ni nini tamko la Serikali kutokana na vifo na manyanyaso yanayoendelea katika Jimbo hili la Mpanda Vijijini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika majibu haya ndiyo maana nikasema kwamba Mheshimiwa Waziri, amedanganywa. Hakuna ushirikishwaji wowote kati ya Vijiji, Vitongoji pamoja na wananchi. Ni kwa nini Serikali inatumia nguvu wakati wananchi wanatakiwa wapewe elimu, washirikishwe kuliko kulazimishwa kupeleka hizo GN kwenye maeneo ambayo vijiji hawajapewa ramani husika kujua na kutambua mipaka yao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme tu kwamba siyo azma ya Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wake wanateswa, hiyo haturuhusu. Haturuhusu kabisa, lakini pale ambapo wananchi wale ambao wanaenda kuingia katika maeneo ya hifadhi bila kufuata taratibu, hatua za kisheria lazima zichukuliwe. Kuchukuliwa siyo kuwatesa wala kuwapiga, lazima wanakamatwa wanapelekwa katika mikondo ya sheria na hapo wanashitakiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kwenye maeneo ya Mheshimiwa kuna tatizo la namna hiyo, basi nitaomba tuwasiliane baadae ili unipe baadhi ya watu ambao wamepata matatizo hayo, kusudi tuweze kuwachukulia hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wote tunafahamu tunapoenda katika mipango ya matumizi bora ya ardhi hasa katika vijiji lazima mipango iwe shirikishi kwa sababu wanaotakiwa kupanga ni wananchi wenyewe wote wanahusika, sasa akiniambia kwamba wananchi hawakushirikishwa kwa kweli nashindwa kuelewa. Huo mpango lazima upitishwe na mkutano wa Kijiji. Sasa ulipitishwaje kama wananchi hawakushirikishwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama kuna changamoto hizo, basi nitakapokwenda katika hilo eneo basi tukae wote kama Serikali pamoja na wananchi tuone kama kweli hawakushirikishwa au kuna tatizo lingine la mahitaji ya ardhi. (Makofi)
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa majibu haya inaonesha kabisa dhahiri kwamba Mheshimiwa Waziri amedanganywa na uhalisia wa wananchi wa Jimbo la Mpanda Vijijini, kutokana na swali hili kwa sababu imekuwa ni mara ya tatu nauliza swali hili, lakini pia Serikali imeshindwa kutatua migogoro pamoja na mauaji yanayoendelea katika kata hizi, Kata ya Kapalamsenga, Ikola, Isengule, Iteteme pamoja na Kalema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vijiji hivi wananchi wamekuwa wanateswa na askari wa Wanyamapori na mwaka jana wamekufa zaidi ya vijana wawili kwa kupigwa risasi na askari wa wanyamapori. Ni nini tamko la Serikali kutokana na vifo na manyanyaso yanayoendelea katika Jimbo hili la Mpanda Vijijini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika majibu haya ndiyo maana nikasema kwamba Mheshimiwa Waziri, amedanganywa. Hakuna ushirikishwaji wowote kati ya Vijiji, Vitongoji pamoja na wananchi. Ni kwa nini Serikali inatumia nguvu wakati wananchi wanatakiwa wapewe elimu, washirikishwe kuliko kulazimishwa kupeleka hizo GN kwenye maeneo ambayo vijiji hawajapewa ramani husika kujua na kutambua mipaka yao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme tu kwamba siyo azma ya Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wake wanateswa, hiyo haturuhusu. Haturuhusu kabisa, lakini pale ambapo wananchi wale ambao wanaenda kuingia katika maeneo ya hifadhi bila kufuata taratibu, hatua za kisheria lazima zichukuliwe. Kuchukuliwa siyo kuwatesa wala kuwapiga, lazima wanakamatwa wanapelekwa katika mikondo ya sheria na hapo wanashitakiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kwenye maeneo ya Mheshimiwa kuna tatizo la namna hiyo, basi nitaomba tuwasiliane baadae ili unipe baadhi ya watu ambao wamepata matatizo hayo, kusudi tuweze kuwachukulia hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wote tunafahamu tunapoenda katika mipango ya matumizi bora ya ardhi hasa katika vijiji lazima mipango iwe shirikishi kwa sababu wanaotakiwa kupanga ni wananchi wenyewe wote wanahusika, sasa akiniambia kwamba wananchi hawakushirikishwa kwa kweli nashindwa kuelewa. Huo mpango lazima upitishwe na mkutano wa Kijiji. Sasa ulipitishwaje kama wananchi hawakushirikishwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama kuna changamoto hizo, basi nitakapokwenda katika hilo eneo basi tukae wote kama Serikali pamoja na wananchi tuone kama kweli hawakushirikishwa au kuna tatizo lingine la mahitaji ya ardhi. (Makofi)
MHE. RHODA E. KUMCHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Nataka niulize swali moja la nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri. Manispaa ya Mpanda imekuwa na changamoto kubwa ya upatikanaji wa maji safi na salama na kutokana na ongezeko kwamba kwa sasa hivi ni Manispaa kumekuwa na changamoto hiyo na Idara ya Maji wamekuwa hawatoi taarifa kwamba ni lini watakata maji au ni lini maji yanaweza kuwa yanapatikana kwa wingi. Sasa nini tamko la Serikali kuhakikisha kwamba wakazi wa Manispaa ya Mpanda wanapata maji kwa wingi na yanawatosheleza wakazi hao?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, nikushukuru na pia nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa swali nzuri. Kikubwa sisi kama Wizara ya Maji jukumu letu ni kuhakikisha wananchi wanapata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza. Nimepokea changamoto hiyo na namhakikishia Mheshimiwa Mbunge nitalifuatilia ili tuweze kuhakikisha watanzania wale wa Mpanda wanapata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na Serikali kuendelea kutenga maeneo ya kibiashara kwa ajili ya wajasiriamali wadogo, lakini bado kumekuwa na changamoto kubwa kwa wajasiriamali hawa wadogo hususani katika Manispaa ya Mpanda Mjini kwamba wamepelekwa kwenye maeneo ambayo miundombinu ya kibiashara pamoja masoko imekuwa na changamoto kubwa. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wajasiriamali hawa katika Manispaa ya Mpanda Mjini? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, kuanzia mwaka juzi Serikali imetoa maelekezo kila Halmashari, Wilaya na mkoa kutenga maeneo maalum kwa ajili ya uwekezaji. Uwekezaji ni kuanzia uwekezaji mdogo, wa kati na mkubwa hususani maeneo ya viwanda, viwanda vidogo, viwanda vya kati na vikubwa na yawepo maeneo maalum kwa ajili ya biashara katika kila mji na kila Halmashauri. Kwa hiyo, hayo ni maelekezo ambayo yanakwenda kuboresha maeneo yetu ya Miji, Halmashauri na minada.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, napenda nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hayo maelekezo ya Serikali yatakapokamilika kutekelezwa vizuri, miundombinu ni sehemu ya mahitaji kwenye maeneo hayo mapya. Kwa hiyo, tunazidi kusisitiza kila halmashauri inapotenga eneo jipya lazima liambatane na miundombinu inayohitajika, ikiwemo umeme, maji na vyoo. Kwa hiyo, masuala yote ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyazungumza, kama ni Mpanda basi tutafuatilia tuhakikishe kwamba hiyo miundombinu inayokosekana inakuwepo. Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Waziri ambayo kimsingi hayajaonesha kutatua migogoro ya ardhi katika Taifa hili, swali la kwanza; migogoro hii imekuwa ni mingi katika mikoa, hususan Mikoa ya Dar es Salaam, Katavi, Mwanza na maeneo mengine. Cha kushangaza, majibu haya ya Serikali yanasema kwamba wametenga shilingi bilioni nne. Lengo hapa ni kutatua, kwamba wanapokuwa wanawaondoa wananchi kwenye maeneo yao, kwa sababu Serikali ndiyo inakuwa imefanya uzembe kuwashirikisha wananchi moja kwa moja kuwaondoa katika maeneo yao lakini pia katika suala la kuwalipa fidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kata ambazo zimeathirika katika Manispaa ya Mpanda ni Kata ya Misunkumilo ambayo iliondolewa na Jeshi, Kata ya Shanwe ambayo ilipisha ujenzi wa barabara lakini pia Kata ya Uwanja wa Ndege ambayo kulikuwa na ujenzi wa Chuo cha Kilimo. Sasa wananchi hawa wanapata shida na hawaelewi hatma yao ya kulipwa fidia zao. Sasa Serikali imepanga nini ii kulipa wananchi hao?

swali la pili ni suala la upimaji shirikishi. Serikali imekuwa ikitoa vifaa kama alivyosema Mheshimiwa Waziri, lakini hakuna ushirikishwaji wa moja kwa moja kwa wananchi kwa maana ya kwamba wanapima maeneo yao lakini kwa wananchi ambao wanakuwa hawana pesa ya kulipia viwanja, angalau basi Serikali ione namna ya kuweza kuchukua; kwa mfano, kama mwananchi ana viwanja vitatu au vine, basi anapimiwa eneo lake na anapewa hatimiliki ili baadaye aweze kulipa hiyo fedha au achukuliwe baadhi ya viwanja ili kukamilisha mchakato wa ulipaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nataka nimfahamishe Mheshimiwa Rhoda kwamba Serikali imeshachukua hatua za dhati kuhakikisha ya kwamba migogoro yote ya ardhi iliyoko kati ya wananchi na Taasisi mbalimbali ikiwemo Jeshi na wengineo inafikia ukomo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais ameunda Tume ambayo ina Mawaziri wanane, ambao wamepitia maeneo karibu ya mikoa yote na kuweza kupitia maeneo yenye migogoro ili waweze kumshauri Mheshimiwa Rais nini kifanyike katika maeneo hasa ambayo yamekuwa na migogoro mingi. Kwa hiyo, kama kuna eneo lake ambalo pia lina mgogoro na Wanajeshi, nadhani hilo linachukuliwa hatua na baada ya muda siyo mrefu, basi Serikali itatoa maelekezo nini kifanyike katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile katika suala la kusema kwamba unamwachia mwananchi eneo lake, nadhani Halmashauri nyingi; nimepita katika mikoa zaidi ya 18 na nikatoa maelekezo na nilikuta wengine wameshaanza kufanya kazi yao vizuri. Mfano mzuri ni Halmashauri ya Kalambo ambao walikuta kwamba tayari wana makubaliano na wananchi, wanamwachia asilimia 60 na wao wanachukua 40; na ile asilimia wanammilikisha yote.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo lililopo kwa wananchi wetu, hata ungempa yote, hawezi kuilipia yote. Tumewaelekeza ya kwamba lazima ifanyike kama walivyokubaliana na ukishaipima ile ardhi inakuwa imeshaongezewa thamani. Kwa hiyo, hata kama atauza, yeye mwenyewe hawezi kumiliki, tayari umeshaongeza thamani na iko katika mpango ambao ni wa kimipango miji, kwa hiyo, haiwezi tena kuwa na ujenzi holela.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naomba tu Halmashauri zisimamie mambo haya kwa sababu ziko Halmashauri nyingi ambazo zinafanya wakiwemo Chemba na wengineo ambako tumepita.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nasisitiza Mheshimiwa Mbunge afuatilie kwenye Halmashairi yake ambayo ni Mamlaka ya Upangaji. Alichosema kwamba Serikali imetoa shilingi milioni nne, siyo shilingi milioni nne, ni shilingi 6,400,000,000/= ambazo zimekwenda kwenye hizo Halmashauri nilizotaja. Tuna imani wakizitumia vizuri wakapanga miji yao, suala la ujenzi holela halitakuwepo.
MHE. RHODA E. KUMCHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na changamoto za kukosa huduma za kibenki katika Mkoa wa Katavi, Wilaya ya Mlele pamoja na Wilaya ya Tanganyika ni moja ya Wilaya ambazo zinakosa huduma za kibenki na ukizingatia asilimia 80 ya wakulima walioko kule wanafanya biashara kubwa na wana pesa nyingi wanasafirisha kwa njia ya magari. Sasa usalama wa fedha zao kutoka katika Wilaya hizi wanatembea zaidi ya kilometa 60 mpaka katika Wilaya ya Mpanda.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha tunapata matawi ya kibenki ili wakulima hawa waweze kusafirisha fedha zao katika mazingira yaliyo salama? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali moja la Mheshimiwa Rhoda Kunchela, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, inashangaza kidogo kusema wananchi bado wanasafirisha pesa kwa magari wakati Serikali imefungua na imeongeza mawanda mapana kabisa ya huduma za kibenki hapa nchini. Hakuna eneo lolote utakapofika hapa nchini ukakosa huduma za kifedha za mawakala wa benki zetu mbalimbali na huduma za simu banking katika maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, ndio maana Tanzania inaongoza kwa Afrika kwa huduma za fedha jumuishi. Kwa hiyo, niwaombe sana wananchi wetu Wilaya ya Mlele, Wilaya ya Katavi waweze kuzitumia fursa hizi zilizopo baada ya Serikali yao kuweka mazingira mazuri ya kufanya biashara nchini. Mawakala wengi wa huduma za fedha wapo kwenye maeneo yote nchini na sasa kila mwananchi ana simu yake, tumeweza kusajili simu kwa hiyo sasa hivi ni rahisi sana kufanya transactions.

Sasa hivi unapofanya transaction niwaambie wananchi wa Tanzania huna wasiwasi wa kutuma pesa yako kwa simu kwa sababu mfumo umeunganishwa na Benki Kuu ya Tanzania, kwa hiyo, unajua kabisa kabla hujatuma kuliko kukaa na kuanza kufikiri fedha yangu imepotelea njiani, sasa unaulizwa kabisa unamtumia fulani bin fulani, una uhakika kwa hiyo hakuna wasiwasi wowote. Niwaombe Watanzania watumie fursa hii ya huduma za fedha jumuishi kwa maendeleo yao na maendeleo ya Taifa letu.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya kutoka Tabora – Ipole – Koga – Inyonga kuelekea mpaka Mkoa wa Katavi kwa kipindi hiki cha mvua, barabara hii ni mbaya na haipitiki. Na wiki moja iliyopita daraja la Koga lilifungwa kwa hiyo ikasababisha wananchi wa Mkoa wa Katavi wakaanza kuzunguka kutoka Mpanda kuelekea Kigoma na kwenda mikoa mingine.

Je, Serikali hii ya Awamu ya Tano inajipangaje kuhakikisha inakamilisha ujenzi wa barabara hii wenye kilometa 359 ili wananchi hawa wa Mkoa wa Katavi waepukane na usumbufu na gharama ambazo wanazipata. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba ni muda mrefu fursa ya kutengeneza barabara ya lami kutokea Tabora kwenda Mpanda haikuwepo. Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba zipo kandarasi kubwa pale zinaendelea, mradi wa kilometa 103,
kilometa 105 na kilometa 108 unafahamu na kwamba makandarasi waliopo hapo wana uwezo mkubwa hata kasi ya utengenezaji wa barabara upo mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu ushoroba ule kwa maana ya ukanda ule tunautazama kwa macho mawili ndio maana tumeweza kuweka fedha nyingi. Nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa msukumo mkubwa, ujenzi unaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto za mvua hatuwezi kuzikwepa, Mheshimiwa Mbunge atakubaliana na mimi kwamba kwenye Mto Koga, ule mto ni mkubwa sana na tunapopata mvua nyingi, miaka mingi iliyopita tumekuwa na shida hiyo na hata hivyo tulikuwa tumetoa maelekezo kwa makandarasi kwamba wanavyoanza kufanya ujenzi waanze kushughulikia sehemu ambazo zina changamoto, ni kitu ambacho kinaendelea kufanyika lakini kwa sababu ya nature ya mvua kuwa nyingi, tulilazimika kuifunga ile barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge mkakati mkubwa wa kuunganisha Mkoa wa Katavi na mikoa mingine unafanyika kwa Serikali ya Awamu ya Tano unafahamu kwamba ipo barabara ile ukitoka Mpanda kwenda kule Malagarasi ujenzi unaendelea na unafahamu tumeshaunganisha vizuri na Rukwa na unafahamu upo mpango wa kujenga barabara kutoka maeneo ya Stalike kwenda Kizi kule unafahamu.

Kwa hiyo, niseme katika Mkoa wa Katavi miradi mikubwa sana ipo kuhakikisha kwamba mkoa huu unaunganishwa na mikoa mingine kama ilivyofanyika kwenye mikoa mingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge wakati huu wa mvua tuvumiliane na tuendelee kumuomba Mungu atupe mvua zenye heri ili adha kubwa ambayo wananchi wanaipata tuweze kuondokana nayo, ahsante sana. (Makofi)
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante halmashauri zimekuwa zikichukua hatua kali sana kwa hawa wafanyabishara wa mkaa hususani katika mikoa ya pembezoni.

Sasa nataka nifahamu mkakati wa Serikali pamoja na juhudi ambazo mnazifanya za kuhakikisha tunatunza mazingira na ukizingatia uuzaji wa gesi bado ni gharama kwa mwananchi ambaye hana kipato kikubwa. Serikali mna mkakati wa gani wa kuhakikisha haya matumizi ya gesi kwa bei ya chini yanaenda sambamba na kupunguza gharama za manunuzi ya mkaa? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa kuleta gesi wananchi watumie umeshanza. Napongeza Wizara ya Nishati Pardot Project imeshaanza na imeshaanza kuonesha gharama ni za chini na hivi karibuni Wizara ya Nishati itaanza mkakati kuhakikisha gesi tunapitisha katika nyumba zote Dar es Salaam na tukitoka Dar es Salaam tunakwenda mikoa mingine Iringa kwa Msigwa kule. (Makofi)
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na changamoto za kuelekea Serikali ya viwanda, Mkoa wa Katavi kuna wafugaji wa kutosha, yaani kuna wafugaji wengi katika Jimbo la Mpanda Vijijini, ukienda Jimbo la Kavuu, Inyonga pamoja na Nsibho.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini Serikali kupitia Sera ya Serikali ya Viwanda mtafungua kiwanda cha nyama kitakachowezesha kupata mazao ya mifugo kwa maana ya maziwa, ngozi, pamoja na nyama ili wafugaji wa Mkoa wa Katavi wanufaike na Sera hii ya Awamu ya Tano?
NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mikoa ya Rukwa na Katavi, tunacho kiwanda kizuri sana cha Safi ambacho kimesimama kwa muda mrefu kufanya kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Kunchela kwamba mchakato ndani ya Serikali unaendelea kung’amua matatizo yote na kuyasuluhisha yaliyokipata kiwanda hiki na kusababisha kutokufanya shughuli zake. Naomba niwahakikishie wana-Katavi na wana-Rukwa wote, baada ya kupatikana kwa utengamano, kiwanda kile kitaendelea kufanya kazi na matokeo yake wafugaji wa Rukwa na Katavi watapeleka mifugo yao pale kwa ajili ya uchakataji na hatimaye kuongeza thamani ya mazao yao.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante pamoja na changamoto za kulipa fidia wananchi katika Taifa hili lakini Mkoa wa Katavi katika barabara ya kutoka Sumbawanga kuelekea Kigoma wakazi wa Kata ya Mpanda hoteli Misukumilo pamoja na Ilembo pamoja na Milala walirukwa katika masuala ya fidia mpaka sasa ni mwaka wa nne hawajalipwa pesa hizo. Je, ni kwanini Serikali mnawazungusha kuwalipa watu hawa ambao walitumia gharama kubwa kujenga nyumba zao?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwa ujumla hii Serikali hii inawajali sana wananchi wake na hakuna sababu ya kutokumlipa mwananchi haki yake. Kwa hiyo, naomba tu nilichukuwe hili kama ni suala mahususi ili nilifuatilie nione nini kilitokea kwa sababu ni nia ya Serikali kuwahudumia vema wananchi na kuwalipa haki zao kwa hiyo, tutalifuatilia suala hili.
MHE. RHODA E: KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mkoa wa Katavi bado una changamoto kubwa ya miradi ya umwagiliaji kuchukua muda mrefu na bila sababu ya msingi. Mradi wa mamba katika Jimbo la Kavuu ni miongoni mwa miradi, ambao imechukua muda mrefu na kuleta usumbufu mkubwa sana kwa wananchi wa jimbo la kavuu. Serikali inasema nini kuhusiana na mradi huu?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA): Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rhoda Kunchela kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli miradi hii mingi ya umwagiliaji imechukua muda mrefu kumaliziwa. Kama nilivyozungumza hapo awali, ni kwamba changamoto kubwa ilikuwa ni kwamba miradi hii haikuleta gharama halisi wakati wa ujenzi wake. Kama tunavyofahamu wakati ule kulikuwa na miradi tuliyokuwa tunaitekeleza kwa ngazi mbili. Kuna miradi ambayo ilikuwa inatekelezwa kwenye ngazi ya wilaya ambao ni ya DIDF miradi ambayo ilikuwa inatekelezwa ngazi ya taifa. Miradi yote ambayo ilikuwa chini ya thamani ya milioni 500 ilikuwa ni ngazi ya wilaya na miradi ambayo ilikuwa ni zaidi ya milioni 500 tunatekeleza ngazi ya taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kuna baadhi ya halmashauri, mojawapo ikiwa yakwako, ilileta mradi huo chini ya thamani ya mradi ili kwamba wapate kigezo hela hizo ziende kwenye wilaya yako wakatekeleza wao ilhali mradi ulikuwa unahitaji fedha nyingi. Sasa baada ya mapungufu hayo tumesema kwamba tunaunda kikosi kazi ili kupitia kujua gharama halisi ya kiasi gani kinachohitajika; na baada ya gharama hizo ndio tutaanza ujenzi wa mradi huo.
MHE. RHODA E. KUMCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Changamoto ya ukosefu wa maji katika Manispaa ya Mpanda pia nayo ni tatizo kubwa. Kata ya Mwamkulu, Kasokola, Kakese pamoja na Makanyagio ni Kata ambazo zina uhaba wa maji na upungufu wa maji. Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari kuhakikisha miradi ya maji pamoja na visima vilivyopo katika maeneo hayo vinatoa maji yenye uhakika ambayo yatawatosheleza wakazi wa Kata hizo?
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Waziri alishafika Mpanda na tumeunda timu maalum kwa ajili ya kutatua tatizo la maji. Kwa hiyo, ipo kazi inayofanyika katika eneo la Mpanda katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nina maswali mawili ya nyongeza, wachimbaji wadogo wadogo katika taifa hili wamekuwa ndiyo wagunduzi wa kwanza wa maeneo ya machimbo, hususan katika mikoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kutokana na ukiritimba unaoendelea kwa baadhi ya matajiri, especially katika Mkoa wa Katavi, wamekuwa wanapora maeneo ya wananchi baada ya kugundua kwamba kuna madini, wanawapora lakini wanakwenda kufanya mazingira ya rushwa kwenye ofisi za madini wanahakikisha wanapata leseni za uchimbaji na huku wakiwaacha wachimbaji hawa wakiendelea kutapatapa na kukosa maeneo ya kuweza kuchimba.

Nini sasa Serikali ifanye ili kuhakikisha inatatua janga hili ambalo linaleta umaskini mkubwa kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, mkononi hapa nina malalamiko ya wachimbaji wadogowadogo ambao wameajiriwa sasa kwenye haya machimbo, wamekuwa wanasainishwa mikataba ambayo ni feki, wananyanyaswa na wanapokuwa wanadai mafao yao au wanadai mishahara yao wamekuwa wakifukuzwa na kupigwa, wengine na kufunguliwa mashitaka. Migodi hiyo iko katika Kata za Idindi, Isulamilomo, Magula, Kasakalawe pamoja na Society ambako ni katika Kata ya Magama.

Niambie Mheshimiwa Waziri ni lini utakuja sasa kuwasikiliza wachimbaji hao wadogo na kero na unyanyasaji ambao wanafanyiwa katika migodi hii ambayo nimeitaja?
NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimhakikishie, katika swali la pili kwamba niko tayari kuja Katavi, kuja kutembelea na kusikiliza kero za wachimbaji wadogo na tumekuwa tukifanya hivyo na nilikwenda Katavi, lakini vilevile niko tayari kwenda tena kama kweli kuna specific issue ambayo ninaweza kwenda kusikiliza na kuweza kuitatua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile, labda nimweleza tu Mheshimiwa Mbunge, kwamba kama kuna matatizo ya waajiriwa, kwa sababu kwenye wachimbaji wadogo kuna waliojiajiri na walioajiriwa, kama kuna matatizo ya walioajiriwa na migodi, tunaomba hizo taarifa mtuletee. Yetote aliyeajiri na ananyanyasa wafanyakazi, sisi kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo inashughulika na masuala ya ajira ambao wanashikilia Sheria ya Kazi, tuko nao kushirikiana nao kuhakikisha kwamba tunatatua kero za wafanyakazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika swali lake la msingi Mheshimiwa Mbunge ameuliza katika masuala ya ushirika, ni kweli. Kuna vikundi vya ushirika, acha ushirika wa mazao, ushirika wa madini, tumewapa watu leseni mbalimbali kuchimba kwa ushirika, lakini unakuta wale wafanyakazi wanaochimba au wanachama wa vikundi vile, wananyanyaswa na viongozi wa vikundi hivyo. Tunaomba kutoa wito na tunatoa onyo, kwa wale ambao ni viongozi wa vikundi, wanawanyanyasa wenzao, waache mtindo huo mara moja kwa sabahu sasa hivi tunawashughulikia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na hatusiti kuwanyang’anya leseni vikundi ambavyo havifanyo mikutano ya mwaka, havitoi taarifa ya mapato na matumizi, tuko tayari kuvifuta na kuwapa watu wengine kuchimba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini, vilevile, katika alipozungumza Mheshimiwa Mbunge kwamba, wachimbaji wadogo ndiyo wagunduzi wakubwa wa machimbo. Nikubaliane na yeye, kuna baadhi ya maeneo wachimbaji wadogo kweli unakuta ndiyo wamevumbua wachimbaji na wamekuwa wakinyanyasika, sasa hivi mtindo huu tumeukomesha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile kuna maeneo mengine watafiti wanakuwa wanagundua, wanapofanya kazi zao wa utafiti, wachimbaji wadogo wanavamia maeneo yale, kwa sababu wanaona kwamba kuna hali na dalili ya uchimbaji. Kwa hiyo, kunakuwa ni maeneo ambayo unaweza kukuta wachimbaj wadogo wametangulia au watafiti wametangulia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Wizara ya Madini kwa kushirikiana na Tume ya Madini, tunayaangalia hayo na tunatatua kero mbalimbali zinazotokana na migogoro hiyo.