Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Lucy Fidelis Owenya (8 total)

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa barabara ya kutoka Sumbawanga kwenda Mpanda takriban kilometa 50 zimeshatengenezwa na magari makubwa ya mahindi zaidi ya tani 60, 70 yanapita kuelekea Mpanda. Nimeshamwomba Waziri wa Ujenzi kupeleka gari ya mizani ili kudhibiti uharibifu wa barabara kabla wakandarasi hawajakabidhi kwa sababu barabara inaanza kuharibika kabla haijakabidhiwa. Je, ni lini Serikali itapeleka gari ya mizani ili kudhibiti barabara hiyo isiendelee kuharibika?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchukua nafasi hii kumhakikishia Mheshimiwa Keissy na wananchi wa Sumbawanga hadi Mpanda kwamba barabara ile kwanza tutaikamilisha kuijenga. Tutakapoona umuhimu wa kuweka mizani kutokana na tathmini ya wataalam tutakaowapeleka kufanya shughuli hiyo tutaweka mizani hiyo.
MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua kwamba barabara hii inasimamiwa na Halmashauri ya Moshi, lakini kwa kuzingatia kwamba ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais Mstaafu na aliyekuwa Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Magufuli, ambaye ni Rais kwa sasa, katika bajeti ya mwaka 2015 waliahidi kutoa shilingi milioni 810 kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami, lakini mpaka sasa hivi wananchi wa Old Moshi na wa Kilimanjaro kwa ujumla wake hawajaona chochote kinachoendelea zaidi ya ahadi ya pesa ambazo ziko kwenye makaratasi tu.
Sasa tunataka kujua, watupe time frame, ni lini barabara hii itaanza na ni lini hii zabuni itapitishwa ili barabara ile iweze kujengwa kwa kiwango cha lami, ukizingatia barabara ile kule Tsuduni kuna vivutio vya utalii, kuna vipepeo, kuna waterfalls na kadhalika? Sasa Mheshimiwa Waziri atueleze ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami una hatua. Tunaanza na upembuzi yakinifu, baada ya hapo tunafuata usanifu wa kina na baadaye ndipo tunaingia kwenye ujenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Fidelis Owenya kwamba barabara hii kutokana na ahadi ambayo Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne aliiitoa tayari imeingizwa katika mchakato. Tumemaliza hatua ya kwanza ya upembuzi yakinifu, sasa hivi tunakaribia kumaliza hatua ya pili ya usanifu wa kina ambapo kilichobakia sasa ni kupata tu taarifa ya mwisho ya msanifu na baada ya hapo barabara hii itaanza kujengwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, isitoshe, kama ambavyo nilivyosema katika jibu langu la nyongeza, Mheshimiwa Owenya barabara hii imeshatengewa fedha kwa mwaka huu wa fedha na bahati nzuri sasa hatua zile za mwanzo ambazo zilikuwa ni za lazima zikamilike kabla ya ujenzi kuanza sasa zinakaribia kukamilika. Nimhakikishie ahadi tutaitekeleza kama ilivyoahidiwa na viongozi wetu wakuu.
MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.
Namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kunipa majibu yenye matumaini.
Mheshimiwa Spika, tatizo la kukatika kwa umeme limeleta madhara makubwa sana kwa wateja. Watu wamekuwa wakiunguliwa nyumba zao wengine vifaa ndani ya nyumba vikiungua kama friji, television na kadhalika. Tatizo
la hitilafu ya kukatikakatika kwa umeme na kuunguza vifaa vya wateja si tatizo la mteja, ni tatizo la TANESCO. Nataka kujua kutoka kwa Mheshimiwa Waziri ni lini sasa TANESCO itaanza kufidia wananchi kwa kuunguliwa na vitu kwa sababu siyo tatizo lao, kama ilivyo kwenye nchi za Ulaya ambako huwa wanafidia wananchi wakati matatizo yakitokea na kupata hitilafu?
Mheshimiwa Spika, swali la pili. Sasa hivi tunakwenda katika Tanzania ya viwanda, na Mheshimiwa Waziri amesema Kilimanjaro tutakuwa na umeme wa uhakika. Nataka nijue na uwahakikishie wananchi wa Kilimanjaro, je, umeme huu utaweza kutosheleza kwa wafanyakazi na wafanyabiashara wa Mkoa wa Kilimanjaro ambao wanataka kuwekeza katika viwanda? Ahsante sana.
WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, kwanza niongee tatizo la kukatikakatika umeme.
Waheshimiwa Wabunge njia nyingi za umeme nchini ni zile ambazo TANESCO ilianza nazo mwaka 1964. Hata mimi kwetu Musoma Mjini umeme ulikuja mwaka 1967, hata pale kwetu hazijabadilika. Sasa ni uamuzi wetu, tuamue kuwa na uvumilivu tuzime tutengeneze au tuendelee na matatizo uwe unawaka unakatikakatika. Kwa hiyo, nadhani jibu zuri ni kwamba tuvumilie miundombinu ni ya zamani na tunairekebisha, hilo la kwanza.
Mheshimiwa Spika, kuhusu suala ambalo Mheshimiwa Mbunge amesema TANESCO ina taratibu za kutoa fidia ikiwa kama vyombo vimeharibika na kosa ni la umeme, kosa ambalo ni la TANESCO, wana taratibu zao unapeleka madai unajaza fomu wanafanya tathmini, huo utaratibu upo.
Sasa niongelee hili la kukatikakatika kwa ujumla lingine la umeme wa uhakika. Kilimanjaro kama alivyosema
Mheshimiwa Naibu Waziri ni kwamba inawekwa miundombinu mipya halafu Kilimanjaro na Arusha kuna sub
station tutakwenda kuifungua ya KIA ambayo ni mpya, umeme umeongezeka pale tumeweka substation. Lakini
isitoshe ni kwamba tunaongeza umeme wa msongo mkubwa. Hii Waheshimiwa Wabunge na Watanzania
wanaonisikiliza ni kwamba njia za kusafirishia umeme nchini zilikuwa za KV 220, sasa hivi tunaweka 440, ni karibu mara mbili.
Kwa hiyo, njia ya kutoka Iringa, Dodoma kwenda mpaka Shinyanga tayari, ndiyo maana siku hizi umeme
haukatikikatiki kwa sababu tuna umeme mwingine unasafirishwa humu, na uwezo wake unaweza ukachukua
mpaka MW 5000 kutoka Iringa kwenda Shinyanga. Kwa hiyo, inabidi tujaze mle umeme ni kama ambavyo unajaza maji zaidi kwenye bomba, kwa hiyo, umeme mwingi unakuja.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Kaskazini tunajenga transmission line mpaka kutoka Singida kwenda
Namanga ambayo nayo ni ya kilovolts 400; itachukua huo umeme. Juzi nilikuwa naongea na mkandarasi anataka
kujenga transmission line ya kutoka Dar es Salaam kuja Dodoma.
Ndugu zangu wa pembeni mwa Ziwa Tanganyika, tunakamilisha majadiliano ya njia kubwa ya umeme kutoka
Iringa, Sumbawanga, Mpanda, Kigoma na Nyakanazi. Kuna ambayo imeshaanza kujengwa na Balozi anataka akaizindue ya kutoka Makambako kwenda Songea kusudi Songea iwe kwenye Gridi ya Taifa. Kwa hiyo, ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote hii nchi ya viwanda itajengwa na Wizara ya Nishati na Madini, ndiyo yenye uwezo wa kuijenga msiwe na wasiwasi.
MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Nina swali dogo la nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri. Tatizo la ukosefu wa dawa ni tatizo kubwa katika mahospitali mengi nchini, kuanzia Zahanati na Vituo vya Afya. MSD imeshalipwa zaidi ya shilingi bilioni 80. Sasa Mheshimiwa Waziri naomba atueleze ni kwa nini MSD inashindwa kuagiza dawa wakati wana fedha katika akaunti zao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua kwamba sasa hivi tunapeleka fedha nyingi sana. Kama nilivyosema hapa mara kadhaa katika Bunge letu hili, kupitia ule mfuko (basket fund) peke yake, tuna fedha nyingi ambazo tumezipeleka kule na nimekuwa nikihamasisha Halmashauri mbalimbali wafanye procurement.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tumeweka utaratibu kwamba endapo dawa zinakosekana, kuna prime vendors ambao wanapatikana kwa ajili ya kuhakikisha dawa zinapatikana. Kwa hiyo, endapo dawa zimeonekana miongoni mwa dawa zilizoombwa kutoka MSD zimekosekana, basi tumewaelekeza wataalam wetu katika kanda kwamba waweze kutumia prime vendors ambao wamekuwa identified kabisa na Serikali, kuhakikisha kwamba tuna-fast truck katika suala la upatikanaji wa dawa. Lengo kubwa ni kwamba Hospitali zetu, Zahanati zetu na Vituo vya Afya viweze kupata dawa kwa ajili ya wananchi wetu.
MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Katika Jimbo la Hai kuna kivutio cha Bwawa moja ambalo lina maji ya moto linaitwa Chemka. Wageni wamekuwa wakienda kule, lakini wanafika kwa kutumia kama vile njia za panya, lakini Serikali kama Wizara bado hawajakitambua kivutio kile na barabara ya kwenda kule ni mbaya sana. Swali langu, je, Serikali mpo tayari kwenda kukitembelea kituo kile cha maji ya moto na kukifanya official ili Serikali nayo iweze kupata mapato? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kifupi tu anazungumzia juu ya kivutio ambacho kiko kwenye Wilaya ya Hai...
Tuko tayari kwenda kukagua lakini nilitaka kuweka nyongeza...
MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Tatizo la kukatika kwa umeme katika Mji wa Mtwara limefanana kabisa na Moshi Manispaa. Moshi umeme huwa unakatika sana na hata ukirudi, unarudi mdogo sana.
Je, ni lini sasa Serikali itahakikisha Moshi inapata umeme wa uhakika ukizingatia Moshi ni Mji wa viwanda?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge Lucy Owenya wa Viti Maalum swali lake kuhusu kukatika katika kwa umeme kwa maeneo ya Moshi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme wakati mwingine sababu zinazopelekea kukatika kwa umeme ni uchakavu wa miundombinu ya kusafirishia umeme. Kwa kuliona hilo, Serikali kupitia ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, umekuja na mradi wa ujenzi wa njia ya Msongo wa KV 400 unaotoka Singida mpaka Namanga ambao huo pia utatumika kusafirishia umeme ambao utakuwa wa kutosha kufika maeneo ya Moshi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, tuna ujenzi pia wa njia ya msongo wa KV 400 ambao utatoka Kinyerezi – Kibaha – Chalinze – Segera na Moshi. Kwa hiyo, nataka nimthibitishe Mheshimiwa Mbunge kwamba hilo suala limeonekana kwa kuwa mahitaji ya umeme kwa ajili ya viwanda yameongezeka sana Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro, ndiyo maana Serikali inataka kutekeleza hiyo miradi ili umeme unaozalishwa kwa wingi usafirishwe na uweze kutumika. Ahsante.
MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Moshi Vijijini Kata ya Mbokomu, tumekuwa tukizungumza mara nyingi kwamba kuna mti mkubwa sana ambao ni kivutio cha utalii pale; lakini Serikali haijachukua jitihada zozote kwenda kuutangaza mti ule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa napenda kujua Mheshimiwa Waziri ana mkakati gani wa kuhakikisha wanautangaza mti ule uwe ni moja ya kivutio cha utalii katika Mkoa wa Kilimanjaro?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli nilikuwa sina taarifa kama kuna mti mkubwa wa namna hiyo, lakini naamini kabisa kama kuna mti mkubwa wa namna hiyo, basi itakuwa ni kivutio kizuri sana cha utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tutachukua hatua za kuhakikisha kwamba kwanza nautembelea, lakini la pili, tuweze kuutangaza kusudi wananchi waweze kujua kwamba kuna mti mkubwa ambao ni kivutio kizuri sana katika Mkoa wa Kilimanjaro na katika eneo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ambalo naomba niliseme, nchi ya Tanzania ni nchi tajiri sana ambayo ina vivutio vingi sana. Tukiwekeza, tutaweza kuivusha nchi hii na tutaweza kuisogeza mbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tushirikiane Wabunge wote kuhakikisha vivutio vyote tunavitangaza kwa pamoja ikiwemo…
kwenye Instagram na Facebook mlizonazo muweke picha cha utalii. (Makofi)
MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona. Hospitali yetu ya Mawenzi nayo inayo kitengo cha afya ya wagonjwa wa akili na imejenga eneo katika eneo la Longuo; na kitengo hicho kinahudumia Kanda nzima ya Kaskazini. Hata hivyo katika kitengo kile hakuna uzio pia wahudumu hawako wa kutosha. Sasa nataka nijue, je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba wanakarabati eneo lile na kuweka uzio na kuwepo na wahudumu wa kutosha kwa sababu inahudumia Kanda nzima ya Kaskazini?
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Lucy Owenya kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kama nilivyosema katika jibu langu la msingi eneo hili la afya ya akili sasa hivi limeanza kuwekewa msukumo kidunia na sisi kama nchi tumeanza kuliwekea nalo msisitizo. Tunatambua kwamba vitengo vyetu vingi vya afya ya akili vimekuwa na uchakavu na vinahitaji kufanyiwa ukarabati mkubwa, ikiwa ni pamoja na kuongeza wigo wa watumishi. Watumishi katika kada hii ni wachache sana, na ndiyo maana sasa hivi Serikali imewekeza katika mafunzo ya wataalamu wa afya wa akili ili tuweze kwenda sambamba na changamoto na wimbi kubwa ambalo tunaliona katika jamii kwa wahanga wa afya ya akili.

Mheshimiwa Spika, kadri ya uwezo wa kifedha unapopatikana na sisi kama wizara tutaendelea kufanya ukarabati wa kiuo hichi pamoja na vituo vingine vya afya ya akili nchini.