Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Questions from Hon. Miza Bakari Haji (1 total)

MHE. MIZA B. HAJI aliuliza:-
Kumekuwepo na kutoridhishwa kwa wananchi kutokana na barabara zetu kutengenezwa chini ya kiwango hali ambayo inapelekea barabara hizo kufanyiwa matengenezo mara kwa mara.
(a) Je, Serikali inaweza kugundua ni barabara ngapi nchini zilizotengenezwa chini ya kiwango?
(b) Je, ni hatua gani zilizochukuliwa kwa waliosababisha tatizo hilo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Miza Bakari Haji Mbunge wa Viti Maalum, lenye vipengele (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimwa Spika, Serikali inaweza kugundua kama barabara imejengwa chini ya kiwango kwani ukaguzi wa ujenzi wa miradi ya barabara unatekelezwa wakati wote wa ujenzi na hata baada ya mradi kukamilika kabla ya muda wa ukaguzi wa mwisho kupita. Aidha, ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara nne za Mbagala Rangi Tatu - Bendera Tatu, Sekenke - Shelui, Kyamyorwa - Buzirayombo na Nangurukuru – Mbwemkulu ulipokamilika yalijitokeza matatizo mbalimbali kabla ya muda uliotarajiwa yalijitokana na mapungufu kwenye ubora kama mashimo madogo madogo katika maeneo kadhaa ya barabara na kuharibika kwa tabaka mbili za juu.
Mheshimiwa Spika, kwa kawaida ujenzi wa barabara hutekelezwa kwa kuzingatia mikataba kati ya TANROADS na mkandarasi, na kati ya TANROADS na mhandisi msimamizi. Viwango vinavyotakiwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara vimetajwa katika mikataba husika. Endapo kunatokea tatizo lolote kuhusu ubora wa kazi, kwa mfano barabara kujengwa chini ya kiwango, vipengele vya mikataba husika hutumika kabaini nani aliyesababisha mapungufu hayo kati ya mkandarasi, mhandisi msimamizi au mwajiri na hatimaye kuwajibika. Kutokana na mapungufu hayo niliyoyataja juu katika barabara hizo nne, hatua zilichukuliwa kulinganana vipengele vya mikataba husika na makandarasi wa miradi hiyo walirekebisha mapungufu hayo kwa gharama zao wenyewe.
Mheshimiwa Spika, sababu nyingine inayosababisha uharibifu wa barabara ni wingi wa magari makubwa ya mizigo hususan magari makubwa ya mizigo yanayotumia excel zenye tairi moja yaani super single tyre. Hivyo kwa kuwa Sheria ya Uthibiti wa Uzito wa Magari ya Jumuiya ya Afrika Mashariki imeweka kiwango kidogo cha uzito wa tani 8.5 kwenye excel zenye tairi moja (super single), Wizara inafanya utaratibu wa kuona ni jinsi gani itafanya mabadiliko ya Kanuni za Usalama Barabarani za mwaka 2001 ziweze kuona na sheria hiyo kwenye kipengele cha super single.