Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Answers to Primary Questions by Hon. Eng. Ramo Matala Makani (71 total)

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:-

Mheshimiwa Spika, kumekuwepo na uvamizi wa tembo kutoka Hifadhi ya Serengeti na kupelekea vifo na uharibu wa mashamba katika Wilaya ya Serengeti na maeneo jirani:-

(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kunusuru maisha na mali za Watanzania waishio Serengeti?

(b) Je, Serikali ina mpango wa kutathimini upya fidia inayotolewa kwani haiendani na uhalisia wa uharibifu wa mali na upotevu wa maisha ya watu?
NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa spika, kwa kuwa hii ni mara yangu ya kwanza kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu katika jukumu hili nililopewa, napenda nimshukuru Mwenyezi Mungu na kwa kweli namrudishia sifa na utukufu. Lakini pia napenda kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa uteuzi huu na kwa kweli natoa ahadi kwamba sitomwangusha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa naomba nijibu swali la Mheshimiwa Marwa Ryoba Chacha, Mbunge wa Serengeti lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Spika, kutokana na madhara yanayosababishwa na wanyamapori hususani Tembo, Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ili kunusuru maisha na mali za wananchi waishio kando ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Hatua hizo ni pamoja na zifuatazo:-

i. Kuunda timu ya udhibiti wa wanayamapori hatari na waharibifu ambayo inajumuisha watumishi kutoka kikosi dhidi ya ujangili cha Bunda, Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Pori la Akiba Ikorongo, Halmashauri ya Wilaya na Mwekezaji Grumeti Reserves. Lengo ni kuhakikisha kwamba tukio lolote la uvamizi wa tembo linashugulikiwa kwa haraka iwezekanavyo.

ii. Kuweka minara au madungu (observation towers) ambayo hutumiwa na Askari Wanyamapori katika kufuatilia mwenendo wa tembo ili wanapotaka kutoka nje ya maeneo ya hifadhi hatua za kuwadhibiti zichukuliwe mapema, kama ilivyofanyika katika Kijiji cha Rwamchanga mpakani na Pori la Akiba la Ikorongo.

iii. Kutumia teknolojia ya mizinga ya nyuki ambayo huwekwa pembenzoni mwa mashamba na kufanya tembo wanapoingia katika mashamba yenye mizinga kufukuzwa na nyuki.

iv. Kutoa elimu ya uhifadhi kwa jamii ili wananchi waepuke kulima kwenye shoroba za wanyamapori pamoja na umuhimu wa kuandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi.

Mheshimiwa Mwenyeikiti, aidha, Serikali ina mpango unaoendelea wa kutumia ndege zisizokuwa na rubani (UAV) kwa ajili ya kufukuza tembo. Mafunzo kuhusu matumizi ya ndege hizo yanaendelea kutolewa kwa watumishi kwa kushirikiana na Taasisi ya World Animal Protection (WAP).

(b) Mheshimiwa Spika, kulingana na Kifungu cha 71 cha Sheria ya Uhifadhi Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009, Waziri mwenye dhamana ya Maliasili amepewa mamlaka kuandaa kanuni za malipo ya kifuta jasho au machozi kwa wahanga wa wanyamapori hatari. Aidha, Kanuni ya 3 ya Kanuni za malipo ya kifuta jasho au machozi za mwaka 2011, inaainisha kuwa malipo hayo yatafanyika endapo mwananchi atajeruhiwa au kuuawa, ama kuharibiwa mazao au mifugo na wananyamapori. Malipo hayo huzingatia uwezo wa fedha na upatikanaji wa taarifa za kweli kutoka kwa wahanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Wizara itaendelea kurejea kanuni na viwango kadri hali ya maisha inavyobadilika.
MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza:-
Katika Bunge la Kumi aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii aliunda Kamati Ndogo ya kushughulikia mgogoro uliopo kati ya wananchi wa Kata ya Buger na Hifadhi ya Taifa ya Manyara:-
(a) Je, ni nini matokeo ya Kamati Ndogo iliyoundwa?
(b) Je, ni lini wananchi watapewa taarifa ya Kamati Ndogo iliyokuwa inashughulikia mgogoro huo?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii alifanya ziara katika Wilaya ya Karatu tarehe 2 Juni, 2015 na kuteua Tume iliyopewa Hadidu za Rejea kuhusu kutatua mgogoro baina ya wananchi wa Kata ya Buger na Hifadhi ya Taifa ya Manyara.
Tume ilifanya mahojiano na makundi mbalimbali na kupitia taarifa zote zilizotolewa na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) na Taarifa ya awali imeandaliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Taarifa ya Tume imebaini kuwa kwa ujumla chanzo kikubwa cha migogoro baina ya wananchi na Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara ni idadi kubwa ya mifugo na kukosekana eneo la kuchungia katika Kijiji cha Buger. Tume imependekeza hatua za kuchukuliwa ambazo ni pamoja na hizi zifuatazo:-
(a) Kufanya sensa ya mifugo kwa vijiji vilivyopo katika Kata ya Buger ili kubaini idadi ya mifugo iliyopo dhidi ya ukubwa wa ardhi waliyonayo;
(b) Vijiji kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi;
(c) Kutoa elimu ya uhifadhi na Sheria katika vijiji vinavyozunguka hifadhi, hasa Msitu wa Marang;
(d) Kuanzisha Kamati za Mazingira za Vijiji na kuimarisha zilizopo ili kutekeleza vema majukumu yake; na
(e) TANAPA kuweka nguvu katika kuchangia miradi ya maendeleo ya jamii kwenye vijiji vinavyozunguka hifadhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara itaandaa kikao cha wadau ndani ya miezi mitatu ili kuwasilisha mapendekezo ya Kamati na kujadili utekelezaji wake.
MHE. RISALA S. KABONGO aliuliza:-
Hifadhi za Mikoa ya Kusini za Mikoa ya Kusini za Ruaha, Kitulo, Udzungwa, Mikumi na Katavi na maeneo mengine ya kihistoria husifika sana kwa vivutio vyake, lakini kutembelewa na idadi ndogo sana ya watalii na hivyo kuwa na mapato madogo na kuwa tegemezi kwa Hifadhi za Mikoa ya Kaskazini:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa muda mfupi na mrefu wa kuongeza idadi ya wageni katika hifadhi hizo?
(b) Je, Serikali ina mikakati gani ya kuboresha miundombinu ya barabara, malazi na viwanja vya ndege katika hifadhi hizo kwa matumizi ya watalii?
(c) Je, kwa nini Serikali isishirikiane na wawekezaji binafsi ili kuwekeza katika maeneo ya utalii kwenye Hifadhi hizo za Mikoa ya kusini?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Risala Saidi Kabongo, lenye sehemu (a), (b) na (c) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa na Shirika la USAID, ilifanya upembuzi yakinifu na kuandaa mikakati ya kuendeleza na kutangaza utalii kwenye eneo la Kusini mwa Tanzania mwaka 2015. Ili kutekeleza mikakati hiyo, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia itatekeleza mradi utakaojulikana kama Tanzanian Resilient Natural Resources Management for Growth. Mradi huu ambao utatekelezwa kwa miaka sita, umepangwa kuanza kutekelezwa Januari, 2017 na utagharimu takribani Dola za Kimarekani milioni 100.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi zitakazotekelezwa na mradi huo ni pamoja na kuimarisha uhifadhi wa mazingira, kuendeleza utalii na kuwezesha wananchi kunufaika na utalii. Mradi huu utahusisha pamoja na mambo mengine, uimarishaji wa miundombinu ya utalii hasa barabara, viwanja vya ndege na huduma za malazi. Vilevile kutengeneza circuit ya utalii kwa upande wa Kusini ili mgeni aweze kutembea au kutembelea eneo au hifadhi zaidi ya moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, jitihada mbalimbali zimefanywa na zinaendelea kufanywa ili kuboresha shughuli za utalii Kusini na Magharibi mwa Tanzania. Jitihada hizo ni pamoja na kuimarisha barabara toka Tunduma kwenda Mpanda kupitia Sumbawanga kwa kiwango cha lami ambayo itaziwezesha hifadhi za Katavi na Mahale kufikika kwa urahisi.
Mheshimiwa Naibu Spika, halikadhalika, ujenzi wa barabara ya Sumbawanga hadi Kasanga kwa kiwango cha lami ambayo itapanua wigo wa wataalii kutembelea Ziwa Tanganyika pamoja na vivutio vingine nje ya hifadhi kama vile maporomoko ya Kalambo.
Mheshimiwa Naibu Spika, jitihada nyingine ni kuimarisha na kuboresha viwanja vya ndege vya Songwe, Kigoma na Mpanda ambavyo vitasaidia kufikika kwa maeneo ya vivutio yaliyotajwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile ukarabati wa barabara itokayo Kigoma kuelekea Kusini hadi Kaliya, Namwese ambayo itaunganisha Mkoa wa Katavi, hivyo kuwezesha watalii kufika Mahale kwa urahisi zaidi. Shirika la Hifadhi za Taifa litaunganisha Hifadhi ya Mikumi na Pori la Akiba la Selous kwa barabara itakayopitika mwaka mzima ili kuwezesha watalii wengi wanaofika Selous kufika Mikumi, kutembelea maeneo hayo kwa urahisi zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, vivutio vya Utalii Kusini mwa nchi vitaendelea kutangazwa na taasisi zilizo chini ya Wizara na kuimarisha Ofisi ya Kanda ya Iringa Mjini.
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuvutia wawekezaji binafsi kutoa huduma mbalimbali za watalii ikiwemo malazi, ambapo vibali 11 vimetolewa kuwekeza kwenye huduma za malazi katika Hifadhi za Ruaha, Mikumi, Katavi na Mahale. Uwekezaji huo ambao upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji utaongeza jumla ya vitanda 544.
MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:-
Wananchi wa Serengeti wamekuwa wakiathirika sana na wanyamapori hususan tembo ambao huharibu na kula mazao ya wananchi katika mashamba yao na kuikosesha Halmashauri mapato:-
(a) Je, Serikali itarejesha chanzo cha mapato yaani bed fee na sehemu ya gate fee kwa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti?
(b) Makampuni mengi ndani ya hifadhi yanagoma kulipa ushuru wa huduma (service levy) kwa Halmashauri. Je, Serikali inaisaidiaje Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kupata ushuru huu wa huduma?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Marwa Ryoba Chacha, Mbunge wa Serengeti, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ya Utalii Na. 29 ya mwaka 2008 ilifuta Sheria ya Hoteli Sura ya 105 ya mwaka 2006 iliyokuwa inaruhusu tozo za bed fee ambapo Tozo ya Maendeleo ya Utalii ilianzishwa. Tozo ya Kitanda Siku (Bed Night Levy) ambayo ni sehemu ya Tozo ya Maendeleo ya Utalii hukusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa niaba ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Tozo ya Maendeleo ya Utalii hugharimia shughuli za kuendeleza utalii nchini ikiwa ni pamoja na kutangaza vivutio vya utalii, kupanga hoteli kwenye daraja na kugharamia masuala ya kitaaluma yanayohusiana na utalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, Shirika la Hifadhi za Taifa linayo mamlaka kisheria kusimamia kulinda na kuendeleza Hifadhi za Taifa. Aidha, makusanyo ya Gate Fee hufanywa na TANAPA ambapo kupitia vitengo vyake vya ujirani mwema vilivyoko kwenye kila hifadhi, huchangia moja kwa moja kwenye miradi ya maendeleo na huduma za kijamii pamoja na kutoa elimu ya mazingira kwa vijiji vinavyozunguka hifadhi hizo.
Kwa upande Wilaya ya Serengeti, kati ya mwaka wa fedha 2004/2005 mpaka 2014/2015, TANAPA iligharimia miradi 37 ya maendeleo na huduma za kijamii yenye thamani ya jumla ya shilingi 1,521,362,239.71.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu inayo taarifa kwamba kumekuwapo na mabishano ya kisheria baina ya Makampuni yanayotoa huduma kwa watalii na Halmashauri kuhusu uhalali wa makampuni hayo kulipa ushuru wa huduma, yaani Service Levy. Suala hili lipo Mahakama ya Rufaa ya Tanzania, Civil Appeal No. 135 ya mwaka 2015 na kwa sababu hiyo, ni vema likasubiri maamuzi ya Mahakama. (Makofi)
MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza:-
Wananchi wa Bonde la Mwakaleli, Kata za Kandete, Isange na Luteba wanaoishi kando ya Hifadhi ya TANAPA wamekuwa wakinyanyaswa sana na watumishi wa TANAPA kwa kisingizio kwamba wamevamia Hifadhi wakati TANAPA ndio waliovamia makazi ya wananchi kwa kuweka mipaka mipya tofauti na ile ya zamani hali inayofanya baadhi ya shule na taasisi zingine kuonekana kuwa ndani ya Hifadhi ya TANAPA kwa sasa:-
Je, ni lini Serikali itarudisha mipaka ya zamani ili wananchi wasiendelee kuishi kwa wasiwasi, lakini pia waendelee na shughuli za kilimo kama ilivyokuwa zamani?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Atupele Fredy Mwakibete, Mbunge wa Busokelo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Msitu wa Livingstone ulikuwa Msitu wa Hifadhi yaani Forest Reserve ulioanzishwa kwa Tangazo la Serikali Na. 48 la mwaka 1940, kwa lengo la kutunza vyanzo vya maji vya Ziwa Nyasa na baianuwai nyingine muhimu. Wananchi wa Kata za Kandete, Isange na Luteba katika Jimbo la Rungwe Mashariki mnamo mwaka 1945 walianza taratibu kuingia katika msitu huo na kufanya shughuli za kibinadamu ikiwa ni pamoja na makazi, kilimo na ufugaji, kinyume na Tangazo la Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kunusuru vyanzo muhimu vya maji vya Ziwa Nyasa na baianuwai muhimu ndani ya msitu, Serikali iliamua kubadilisha hadhi ya Msitu wa Livingstone kutoka Forest Reserve kuwa Hifadhi ya Taifa Kitulo, iliyotangazwa rasmi katika Gazeti la Serikali Na. 279 la mwaka 2005, baada ya hatua zote muhimu za Kiserikali kukamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya Tangazo hilo la Serikali la mwaka 2005, mnamo mwaka 2007 lilifanyika zoezi la uhakiki na uwekaji wa mawe ya mipaka ya hifadhi zoezi ambalo lilishirikisha wataalam wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na wadau wengine muhimu ikiwa ni pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, Menejimenti ya Hifadhi ya Taifa Kitulo na viongozi wa vijiji husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, zoezi la uhakiki na uwekaji mipaka kwa eneo lote la hifadhi lilikamilika mwaka 2010. Aidha, katika zoezi hilo ilibainika kuwa baadhi ya mashamba, makazi na miundombinu ya taasisi kama vile shule na kanisa, vimo ndani ya mipaka ya hifadhi na hivyo kusababisha migogoro kati ya hifadhi na wananchi, mgogoro ambao unahitaji kupatiwa ufumbuzi wa pamoja baina ya Serikali na wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ufumbuzi wa kudumu wa suala hili unafanyiwa kazi na Shirika la Hifadhi za Taifa, kwa niaba ya Wizara yangu kwa kushirikiana na wataalam wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na uongozi wa Mkoa wa Mbeya na unatarajiwa kukamilika katika kipindi cha mwaka mmoja. Wakati suala hili likisubiri kupatiwa ufumbuzi, wananchi wawe wavumilivu kwa kutofanya shughuli za uharibifu wa mazingira katika maeneo husika.
MHE. HAROON M. PIRMOHAMED aliuliza:-
Katika GN. Na. 28 ya mwaka 2008 inawataka wananchi wanaoishi katika vijiji 21 vilivyopo katika Jimbo la Mbarali, Wilaya ya Mbarali, Mkoani Mbeya wahame ili kupisha Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ingawa wananchi katika vijiji hivyo wameishi katika maeneo hayo tangu enzi za mababu zao:-
Je, ni lini Serikali itafuta GN. Na. 28 ya mwaka 2008 ili wananchi katika vijiji hivyo waweze kuishi bila kubughudhiwa pamoja na kuendelea na shughuli zao za kilimo na ufugaji?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Haroon Mulla Pirmohamed, Mbunge wa Mbarali, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, tangazo la Serikali Na. 28 la mwaka 2008 lilihusu kuhifadhiwa Bonde la Usangu kama sehemu ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha hatua ambayo ulihusisha kutunza vyanzo vya maji kwa ajili ya shughuli za kilimo na kibinadamu, uzalishaji wa umeme na matumizi ya kiikolojia kwa maslahi mapana ya kitaifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wanaoishi katika vijiji 21 vilivyopo katika Jimbo la Mbarali, Wilaya ya Mbarali, Mkoani Mbeya wamewasilisha malalamiko yao Serikalini wakipinga uhalali wa mpaka mpya uliotokana na Tangazo la Serikali nililolitaja na hivyo kuendelea kuwepo ndani ya mpaka. Aidha, baadhi ya wananchi waliotii sheria na kuondoka katika maeneo husika wamelalamikia viwango vya fidia vilivyolipwa katika kipindi cha mwaka 2006 hadi 2008 baada ya taratibu zote za kiserikali ikiwemo kufanya tathmini kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikifanya kila jitihada kutatua mgogoro huo katika ngazi mbalimbali ikiwemo vikao vya ushauri baina ya wadau wakiwemo wananchi katika eneo husika, uongozi wa Wilaya ya Mbarali na Mkoa wa Mbeya, Wizara ya Maliasili na Utalii na Ofisi ya Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iliunda timu ya wataalam na kupitia upya mipaka iliyotangazwa ili kutoa ushauri wa kitaalam juu ya mipaka hiyo na kuwasilisha ripoti kwenye Kamati ya pamoja kati ya Mkoa wa Mbeya na Wizara ya Maliasili na Utalii na kuhakiki malipo ya fidia kwa wananchi waliohama kupisha eneo lililojumuishwa kwenye Hifadhi ya Taifa Ruaha.
Mheshimiwa Naibu Spika, uhakiki huo ulikusudia kuondoa malalamiko ya mapunjo yaliyojitokeza kutoka kwa baadhi ya wananchi, kupitia na kuhakiki maeneo yote ya mpaka ardhini ili kujua maeneo gani yataathiriwa na mpaka mpya na kuona ni kwa namna gani mpaka utaweza kurekebishwa bila kuathiri lengo kuu la kuhifadhi sehemu ya eneo hilo la Bonde la Usangu. Mapedekezo yatakayotokana na kazi hii yatatumika kufanya maamuzi sahihi juu ya mipaka ya eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kusisitiza kuwa eneo la Bonde la Usangu, lililotajwa kwenye GN. Na. 28 ya mwaka 2008 ni eneo linalolindwa kisheria na umuhimu wake bado uko pale pale. Hivyo, badiliko lolote la mipaka ndani yake litahitajika kufanyika kwa kuzingatia taratibu za kisheria kupitia Bunge lako Tukufu.
MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:-
Ili Mtu au Kampuni iweze kufanya biashara ya Mazao ya Misitu anapaswa kusajiliwa:-
(a) Je, ni kwa nini usajili huu hufanywa kila mwaka?
(b) Je, Serikali haioni kwa kufanya hivyo kunaongezea walipa kodi mzigo?
(c) Je, usajili huu hauwezi kufanywa pale tu mtu au Kampuni inapoanza biashara kwa mara ya kwanza na anapoendelea aweze kuhuisha badala ya kusajiliwa upya kila mwaka.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi, lenye sehemu (a), (b) na (c), kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, usajili wa wafanyabiashara wa mazao ya misitu hufanywa kwa mujibu wa Sheria ya Misitu Sura 323, kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002, Kifungu cha tano (5) na Kifungu cha 108 na Kanuni zake za mwaka 2004, Kanuni ya 54 kwa kuzingatia kiasi cha mazao ya misitu cha kuvuna mwaka hadi mwaka, ambacho hutegemea uwezo na ndicho kigezo cha kutambua idadi ya wafanyabiashara wa mazao ya misitu watakaopewa vibali vya kuvuna ili kuepuka kuwa na idadi kubwa ya wateja kuliko uwezo wa msitu kuvunwa katika mwaka husika.
Mheshimiwa Naibu Spika, usajili wa kila mwaka husaidia kutekeleza mipango endelevu ya usimamizi kwa ajili ya kupanga kiwango kinachotakiwa kuvunwa kwa mwaka. Aidha, utaratibu huu hutoa fursa kwa wafanyabiashara wapya kuingia kwenye soko hivyo kuweka mipango mizuri zaidi ya kutambua mahitaji yao kulinganisha na uwezo wa misitu iliyopo. Vile vile kutoa fursa kwa wananchi wengi zaidi kushiriki na kunufaika na uvunaji wa rasilimali za Taifa, mazao ya misitu ikiwa ni sehemu yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa zoezi la usajili huambatana na ada mahsusi, wafanyabiashara waone kuwa hii ni fursa kwao kuchangia pato la Taifa kupitia biashara wanazozifanya, utaratibu ambao unafanana na masharti ya biashara nyingine zinazofanyika hapa nchini.
MEH. RISALA S. KABONGO aliuliza:-
Utekelezaji wa Tangazo rasmi la Serikali la Mwaka 2008 juu ya mpaka mpya wa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha katika Bonde la Usangu umeshindikana, hivyo kufanya upanuzi holela wa maeneo ya kilimo, uvamizi wa mifugo mingi na matumizi holela ya maji katika kilimo, jambo ambalo limesababisha uharibifu wa mazingira, Mto Ruaha Mkuu kuendelea kukauka kila mwaka na kuathiri uzalishaji umeme katika Bwawa la Mtera na Kidatu na shughuli zingine na matumizi ya maji ya Mto Ruaha Mkuu:-
(a) Sababu zipi za msingi zilizosababisha utekelezaji wa Tangazo hilo kushindwa kwa takribani miaka nane sasa?
(b) Je, Serikali inachukua hatua gani za haraka ili kunusuru na kusitisha uharibifu mkubwa wa mazingira unaoendelea katika Bonde la Usangu?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Risala Said Kabogo, Mbunge wa Viti Maalumu, lenye Sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifutavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inampongeza Mheshimiwa Risala Kabongo kwa kutambua na kuthamini jitihada za Serikali na kuona umuhimu wa uhifadhi katika Taifa, hususan uhifadhi katika eneo la Hifadhi ya Taifa ya Ruaha katika Bonde la Usangu, ambako shughuli za kilimo, uingizaji, uchungaji na ulishaji mifugo na matumizi ya maji yasiyo endelevu katika kilimo zimesababisha uharibifu mkubwa wa mazingira, unaosababisha pamoja na athari nyingine kukauka kila mwaka kwa Mto Ruaha Mkuu na hatimaye kuathirika shughuli za uzalishaji umeme kutokana na kukosekana kwa kiasi cha maji kinachohitajika katika mabwawa ya Mtera na Kidatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuzingatia umuhimu nilioainisha hapo juu Serikali ilikamilisha taratibu zote husika na kutoa Tangazo la Serikali Namba 28 la mwaka 2008, ambalo msingi wake ni Sheria ya Hifadhi za Taifa, Sura ya 282, hususan Kifungu cha tatu (3) na cha nne (4) cha sheria hiyo ili eneo la Bonde la Usangu lijumuishwe ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa Tangazo la Serikali Namba 28 la mwaka 2008 haujashindikana na badala yake matakwa ya Tangazo hilo yameanza kwa kuhakiki mipaka na kuweka alama za kudumu beacons kwa baadhi ya maeneo yaliyoongezwa. Kutoa elimu na kuhamasisha wananchi waliotakiwa kuhama ili kupisha hifadhi, kufanya tathmini na kulipa fidia ya ardhi na mali zisizohamishika kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi Na. 4 na Na. 5 za mwaka 1999. Aidha, Serikali inaendelea na utekelezaji wa matakwa ya Tangazo la Serikali Namba 28 la mwaka 2008, ambapo baada ya changamoto zilizojitokeza kutatuliwa, wananchi walioko katika eneo husika pamoja na mali zao zinazohamishika wataondoka kupisha shughuli za uhifadhi.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, katika majibu yangu ya swali Namba 53 lililouliza na Mheshimiwa Haroon Mulla Pirmohamed, Mbunge wa Jimbo la Mbarali, katika Kikao cha Sita cha Mkutano wa Tatu wa Bunge la Kumi na Moja kilichofanyika tarehe 27/4/2016, nilisisitiza kuhusu umuhimu wa kuhifadhi eneo la Bonde la Usangu kwa maslahi mapana ya Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika majibu hayo nilieleza kuhusu kuwepo kwa timu ya Wataalam iliyopitia changamoto za utekelezaji wa Tangazo la Serikali, ikiwa ni pamoja na kutafsiri mpaka, kuweka alama na kukamilisha malipo ya fidia kwa mujibu wa sheria katika kipindi cha mwezi mmoja, hatua ambayo itawezesha Serikali kuendelea na hatua muhimu na za haraka ili kudhibiti uharibifu wa mazingira katika Bonde la Usangu.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza:-
Serikali ilitenga eneo la Sayaka Salama Bugatu kuwa hifadhi ya msitu, lakini msitu wenyewe haukui huku wananchi, wafugaji na wakulima wakikosa maeneo ya mifugo yao na kilimo.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwarudishia wananchi maeneo hayo ili waweze kuyatumia kwa kilimo na mifugo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Boniventura Desdery Kiswaga, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, msitu na hifadhi Sayaka ulitangazwa rasmi kuwa Msitu wa Hifadhi chini ya Serikali Kuu kwa Tangazo la Serikali namba 90 la tarehe 19 Juni 1996. Katika siku za nyuma Halmashauri ya Wilaya ya Magu iliomba kubadilishwa kwa matumizi ya msitu huu wenye ukubwa wa hekta 5421, lakini kwa kuzingatia sababu za msingi za kiuhifadhi, Wizara kupitia barua kumbukumbu namba JA/66/298/02/33 ya tarehe 19 Desemba, 2001 ilikataa ombi hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hifadhi ya msitu wa Sayaka ni sehemu muhimu sana inayochuja na kudhibiti taka nyingi kutoka mto Duma unaopita katika hifadhi hii. Uwezo huu wa kudhibiti na kuchuja taka ambazo ni pamoja na tope na viuatilifu vinavyotoka mashambani unatokana na uoto wa asili uliopo ambao unahitaji kuboreshwa zaidi ili uendelee kupunguza athari za tope na viuatilifu katika Ziwa Victoria.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, hatua ya kubadilisha msitu huu na kuwa mashamba eneo la kuchungia mifugo au shughuli nyingine za kibinadamu zisizo za uhifadhi itasababisha kupotea kwa uoto wa asili na kusababisha mmomonyoko mkubwa wa udongo ndani ya hifadhi na hivyo kuruhusu taka nyingi kuingia ziwani jambo ambalo litapunguza uhifadhi wa mazingira ya Ziwa Victoria ambalo ni muhimu kwa Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua umuhimu mkubwa wa msitu wa Sayaka, Serikali haina mpango wa kubadilisha matumizi yake kinyume na malengo ya kuanzishwa kwake, kwani hatua hiyo itasababisha athari kubwa na nyingi za kimazingira na kiuchumi. Aidha, wananchi wanaoishi vijiji vinavyozunguka Msitu wa Hifadhi ya Sayaka ndiyo watakaokuwa waathirika wa kwanza kwa upepo mkali, upungufu wa mvua utakaoathiri mifugo na kilimo na athari nyinginezo kwa siku zijazo.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuanzishwa kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania mnamo mwaka 2011, usimamizi na ulinzi wa misitu huu umeimarishwa na kufanya uoto wa asili kurejea kwa kufanya marejeo ya soroveya, kuimarisha mipaka na kuweka vigingi 65 katika mipaka. Aidha, Kamati za Maliasili za Vijiji Kumi ndani ya Halmashauri ya Magu zimeanzishwa kwa ajili ya kushirikiana na wataalam katika ulinzi wa msitu huu.
MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi kati ya hifadhi ya Mpanga na wananchi wa Wilaya ya Wanging‟ombe?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa William Mgaya Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, uhifadhi katika hifadhi ya Mpanga Kipengele ulianzishwa za Tangazo la Serikali (GN) Na. 483 la tarehe 25 Oktoba, 2002 ambapo eneo lililoidhinishwa lilitangwazwa kuwa pori la akiba kwa maslahi mapana ya Kitaifa. Uhifadhi wa eneo hili unahusisha utunzaji wa rasilimali zinazotoa fursa ya utalii, matumizi ya kiikolojia na vyanzo vya maji kupitia mito ya Mbarali, Mlomboji, Kimani na Ipera ambayo kwa pamoja huchangia maji ya mtoa Ruaha Mkuu, ambao ni muhimu kwa shughuli za kilimo ikiwemo umwagiliaji wa mashamba, mahitaji ya watu na uzalishaji wa umeme katika mabwawa ya Mtera na Kidatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na Wilaya za Makete na Mbarali, poli la akiba Mpanga na Kipengere limepatikana na takribani Vijiji kumi vya Wilaya ya Wanging‟ombe ambapo chanzo cha mgogoro ni wananchi wa Vijiji vinne ambavyo viko ndani ya mpaka wa hifadhi, na vingine vinne nje wa mpaka wa hifadhi kukataa kutambua mipaka iliyowekwa na Tangazo la Serikali na hivyo kugoma kuhama kupisha shughuli za uhifadhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika juhudi za kutafuta suluhu ya mgogoro huu na eneo lote linalozunguka pori hili, Wizara yangu ilifanya vikao vya majadiliano na Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya ya Makete tarehe 20 mpaka 21, Novemba, 2014; Wanging‟ombe tarehe 26 mpaka 27, Novemba 2014 na Wilaya Mbarali tarehe 26 mpaka 27, Februari, 2015 na hatimaye kufanyika kwa tathmini kutambua idadi ya wananchi na mali zao zisizohamishika na uthamini wa kiasi cha fedha kitakachohitajika kuwalipa fidia kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Naibu Spika, kufuatia uthamini uliofanyika mwaka 2007 na 2012 katika Wilaya ya Makete mwaka 2007, wananchi 325 wa Vijiji vya Ikovo, Usalimwani na Kigunga vya Wilaya ya Makete walilipwa fidia ya shilingi 190,067,151. Mwaka 2012 wananchi 161 wa Kijiji cha Ikovo walilalamikia kupunjwa, hivyo uthamini wa ardhi na gharama za kuhama ulifanyika tena ambapo walilipwa jumla ya shilingi 829,841,000.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika tathmini iliyofuata iliyofanyika na kukamilika mwaka 2015 Wilayani Mbarali, wananchi 308 katika Kitongoji cha Machimbo, Kijiji cha Mabadaga wanategemewa kulipwa jumla ya shilingi 717,650,000 katika mwaka wa fedha 2016/17. Tathmini na uthamini kwa Vijiji vya Wilaya ya Wanging‟ombe imepangwa kufanyika kupitia bajeti ya mwaka wa fedha ujao.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuwaomba wananchi kuendelea kuwa watulivu, wavumilivu na kuepukana na shughuli ambazo zinaweza kuleta athari katika maeneo hayo muhimu kwa Taifa letu, kwani Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kutatua changamoto za migogoro ya mipaka kati ya hifadhi na ya wananchi. Vilevile tunahimiza Mkoa, Halmashauri za Wilaya na Waheshimiwa Wabunge washirikiane na Wizara kuhamasisha elimu ya uhifadhi na pia kuwashawishi wananchi kukubali kuhama na kupisha uhifadhi mara baada ya taratibu kukamilika.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB aliuliza:-
Wakulima 1,128 wa msitu wa derema kata ya Amani Muheza wamekuwa wakilalamika kwa muda mrefu kupunjwa fidia ya mimea yao kutoka shilingi 3,315 kw a shina moja:-
(a) Je, ni lini wakulima hapo watalipwa stahiki zao,
(b) Je, kwa nini kwenye malip hayo Serikali sijijumiushe fidia ya ardhi yao?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Balozi Adadi Mohamed Rajab, Mbunge wa Muheza, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa jumla ya wananchi 1,128 waliokuwa wakifanya shughuli za kilimo ndani ya hifadhi ya msitu wa Derema, walihamishwa na kulipwa stahiki zao ili kupisha uhifadhi kati ya mwaka 2001 na mwaka 2009, lakini siyo kweli kuwa wananchi hao walipunjwa fidia ya mazao yao. Ukweli zaidi ni kuwa katika mchakato wa kuhakikisha eneo lote la msitu linahifadhiwa kama ilivyokusudiwa, mazoezi mawili tofauti yalifanyika kwa vipindi tofauti na kwa ufadhili wa taasisi tofauti ambazo ni Shirika la Maendeleo la Nchi ya Ufini, FINNIDA lililofadhili fidia kwa mazao kwenye mpaka na Benki ya Dunia waliofadhili fidia kwa mazao ndani ya hifadhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika zoezi la kwanza lililofanyika mwaka 2001 mpaka 2002 chini ya ufadhili wa FINNIDA kupitia mradi uliojulikana kama East Usambara Conservation and Management Programe, idadi ya wakulima 172 waliokuwa wakifanya shughuli za kilimo upande wa nje wa eneo la msitu walilipwa fidia ya mazao yao. Kwa kuzingatia muda mfupi uliokuwa umebaki hadi mradi kufikia tamati yake, shirika hilo liliwalipa wakulima kiwango cha shilingi 28,000/= kwa kila shina moja la mmea wa Iliki, bila ya masharti au kigezo kingine chochote mahsusi kutumika, lengo likiwa ni kuharakisha uhamishaji wananchi na uwekaji wa mipaka rasmi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha mwaka 2002 hadi 2008 wananchi 1,128 waliokuwa na mazao ndani ya msitu walilipwa stahiki zao zenye jumla ya shilingi 1,633,893,595.85. Malipo hayo yalitokana na ufadhili wa Benki ya Dunia ambayo ilitoa jumla ya shilingi 1,238,653,060.85 na vyanzo vingine mbalimbali ambavyo vililipa jumla ya shilingi 395,240,535/=. Tofauti na zoezi la kwanza ulipaji katika zoezi hili ulizingatia masharti ya Benki ya Dunia, Sheria ya Ardhi 1998 na Sheria ya Ardhi ya Vijiji ya 1999 pamoja na miongozo mingine ya fidia za mazao.
Mheshimiwa Naibu Spika, thamani ya fidia iliwekwa katika viwango tofauti kulingana na sifa za ukomavu wa mazao, umri wa miche, utunzaji wa shamba na idadi ya mazao. Kulingana na vigezo hivyo, viwango vilivyokubalika vilikuwa shilingi 102/=, shilingi 204/=, shilingi 2,040/=, shilingi 3,315/= na shilingi 5,100/= kwa shina. Tathmini kwa mazao ya wananchi yaliyomo ndani ya msitu ilifanyika kwa ushiriki wa karibu wa timu huru za Wakaguzi kutoa Wizara, Taasisi za Umma na Taasisi Binafsi, Mashirika ya Kimataifa na wananchi wenyewe. Aidha, kiwango cha chini kilichofidiwa ni shilingi 3,315/= na kiwango cha juu ni shilingi 22,832,172.32 kwa mkulima mmoja. Nakala ya nyaraka za tathmini na malipo yaliyofanyika zinapatikana katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Muheza na Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu fidia ya ardhi, Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Muheza na Mkoa wa Tanga iliahidi kuwapatia wananchi ardhi mbadala ambapo hadi sasa jumla ya maeneo 408 yenye ukubwa wa hekta tatu kila moja yamekwishapimwa na kwamba zoezi hilo la upimaji linaendela hatua kwa hatua kilingana na upatikanaji wa fedha kwa ajili ya gharama za upimaji. Namshauri Mheshimiwa Mbunge awasiliane na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza ili kufahamu zaidi hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa zoezi la ugawaji wa ardhi na namna linavyoendelea.
MHE. AMINA NASSORO MAKILAGI aliuliza:-
(a) Je, Viwanda vinavyozalisha nguo aina ya khanga vipimio vyake na ubora wake vinafaa kwa matumizi ya wanawake wa Kitanzania?
(b) Je, upande wa khanga kwa kila kiwanda ni mita ngapi?
(c) Je, malighafi gani inayotumiwa kuzalisha khanga kati ya pamba, uzi wa katani, uzi wa nailoni, au uzi wa sufi?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI (K.n.y WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Nassoro Makilagi Mbunge wa Viti Maalum lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, vipimo vya ubora wa khanga zinazozalishwa na viwanda hapa nchini, vinafaa sana kwa matumizi ya wanawake hapa Tanzania. Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia shirika la viwango Tanzania (TBS) limetoa viwango elekezi vya uzalishaji wa khanga kwa kutumia pamoja na nyombo vingine ni 16165 ya 2009. Viwango hivi vimezingatia mahitaji ya watumiaji na matakwa ya wataalamu.
Mheshimiwa Naibu Spika, upande wa khanga kwa kila kipande unatofautiana kutoka kiwanda kimoja hadi kingine.
Aidha, kiwango cha centimeter 165 cha 2009 kinaelekeza upande wa khanga uwe wa kipimo kisichopungua urefu wa centimeter 165 na upana wa centimeter 116. Hata hivyo, kila kiwanda kinachozalisha khanga kinapaswa kuzingatia vipimo hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, khanga husokotwa kwa kutumia malighafi za nyuzi pamoja na pamba. Hata hivyo, katika umaliziaji wa kipande hicho hutengenezwa kwa kutumia asilimia 100 lakini polyester kwa asilimia 100 au mchanganyiko wa pamba pamoja na polyester.
MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:-
Jimbo la Mufindi Kusini linazungukwa na msitu wa Serikali na vijana wanaishi humo hawana ajira.
(a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapa vibali vya kupasua mbao ili kwa kazi hiyo wajiajiri?
(b) Je, Serikali haioni haja ya kuwapa vijana hao mtaji ili waanzishe viwanda vidogo vya mbao?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola, Mbunge wa Mufindi Kusini, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Mufindi Kusini linapakana na msitu wa shamba la miti la Sao Hill ambalo ni miongoni mwa mashamba ya misitu ya kupandwa 18 nchini. Upasuaji wa mbao ni sehemu moja tu ya mchakato mzima wa uvunaji wa mazao ya misitu unaotekelezwa na Wizara yangu kwa mujibu wa mwongozo wa uvunaji endelevu na biashara ya mazao ya misitu yanayovunwa katika mashamba ya miti na misitu ya mikoko kwa mwaka 2014, chini ya Sheria ya Misitu namba 14 ya mwaka 2002 na Sera ya Taifa ya Misitu ya mwaka 1998. Mwongozo huo umeweka vipaumbele mbali mbali katika uvunaji wa mazao ya misitu ikiwemo vikundi vya vijana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kutambua changamoto za kiuchumi na kijamii kwa vijana katika maeneo husika Serikali imekuwa ikishirikiana na umoja wa vikundi vya kijamii Wilayani Mufindi kwa kuwapatia vibali kwa ajili ya kuwezesha kupata mitaji ili kuwekeza katika miradi mingine ya kiuchumi. Kwa miaka mitatu mfululizo 2013/2014 hadi 2015/2016 vijana kupitia umoja huo wamekuwa wakigawiwa mita za ujazo 200 kila mwaka. Fedha inayotokana na vibali hivi huratibiwa na umoja wao, na imewawezesha kuanzisha shughuli mbalimbali ikiwemo kununua mizinga ya ufugaji nyuki, ufugaji wa ng’ombe wa maziwa, ufugaji wa kukuna hata mitaji kwa ajili ya biashara ndogo ndogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha uwezeshaji wa vijana wanaoishi jirani na msitu kwa namna endelevu, shamba la miti Sao Hill hutoa miche ya miti kwa ajili ya kupanda kwenye mashamba wanayomiliki wenyewe ili waweze kuvuna na kuuza mbao na kujipatia mfanikio ya kiuchumi na kijamii ikiwemo upatikanaji wa ajira. Kwa mfano katika mwaka 2015/2016 shamba lilitoa bure miche 600,000 yenye thamani isiyopungua shilingi 120,000,000 kwa ajili ya kuwawezeshavijana hao.
Aidha, ili kuhakikisha kuwa jamii inanufaika na uwepo wa shamba hilo na kuwapunguzia adha ya michango kwa shughuli za maendeleo vijiji vinavyozunguka shamba hilo vinapatiwa vibali vya kuvuna miti kwa ajili ya shughuli za kimaendeleo ikiwemo kutengeneza madawati, kazi ambayo pia hupewa mafundi ambao ni vijana wanaishi katika vijiji vinayozunguka shamba hilo. Kwa mfano, katika kipindi cha mwaka 2011/2012 hadi 2014/2015 jumla ya meta za ujazo 40,000 zilitolewa kwa vijiji vya jirani na kwa mwaka 2013/2014 pekee baadhi ya vijiji vilitumia mgao huo kutengeneza jumla ya madawati 2,469.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu inatoa ushauri kwa vijana kuungana pamoja na kuunda ushirika ambao utawezesha kupata mikopo kutoka taasisi mbalimbali za fedha na hatimaye kujenga uwezo wa kuendesha shughuli zao za kila siku ikiwa ni pamoja na kuwekeza katika viwanda vya mbao yaani saw mills ili waweze kuomba vibali vya uvunaji kajadiliwa kama wateja wengine wenye viwanda.
MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI aliuliza:-
(a) Je, Serikali inasafirisha nje ya nchi mbao na magogo kiasi gani kwa mwaka?
(b) Je, ni nchi gani inaongoza kwa kununua mbao na magogo kutoka Tanzania?
(c) Je, ni fedha za kigeni kiasi gani zimepatikana kutokana na mauzo ya magogo na mbao nje ya nchi kwa kipindi cha mwaka 2010 - 2015?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Immaculate Sware Semesi, lenye sehemu (a), (b) na (c) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kanuni ya 50 ya Kanuni za Sheria ya Misitu Namba 14 ya mwaka 2002, inakataza usafirishaji wa magogo kwenda nje ya nchi. Aidha, Kanuni hiyo hairuhusu uuzaji nchi za nje wa mbao zenye unene unaozidi inchi sita. Kanuni hii na sheria vinaweka zuio ili kutoa fursa ya kukuza viwanda vya ndani ya nchi na ajira kwa Watanzania katika kupasua mbao na utengenezaji wa samani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha mwaka 2010 hadi 2015 jumla ya mita za ujazo 333,404.91 za mbao chini ya inchi sita ziliuzwa na kusafirishwa kwenda nchi za nje.
Aidha, kwa mujibu wa takwimu nchi ya India inaongoza kwa kununua mbao kutoka Tanzania ambapo katika kipindi cha mwaka 2010 hadi 2015 jumla ya meta za ujazo 210,968.07 zilisafirishwa kwenda India, ikifuatiwa na nchi ya China ambayo ilinunua mita za ujazo 68,337.04.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha mwaka 2010 hadi 2015 jumla ya fedha zilizopatikana ni shilingi 269,985,300,000 kutokana na mauzo ya mbao nchi za nje. Aidha, hakuna kiasi cha fedha kilichopatikana kutokana na mauzo ya magogo kwa kuwa biashara ya magogo kwa mujibu wa sheria haikufanyika.
MHE. ESTER A. BULAYA aliuliza:-
Kumekuwepo na matukio ya mara kwa mara ya wananchi wa Vijiji vya Guta, Tairo, Nyamtwali na Njabeu kukamatwa na kuliwa na mamba; hadi swali hili linaandikwa, jumla ya watu watatu wameliwa na wengine kumi wamejeruhiwa.
Je, Serikali inajipangaje ili kuokoa maisha ya wananchi kutokana na hatari kubwa ya mamba hao?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ester Amos Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Vijiji vilivyotajwa na Mheshimiwa Mbunge vinapakana na Ziwa Victoria. Mazingira hayo yanasababisha kuwepo mwingiliano wa shughuli za kibinadamu na makazi ya wanyamapori kama vile mamba na viboko ambayo yanaweza kusababisha matukio ya wananchi kuuawa na kujeruhiwa na wanayama hao.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu imepokea taarifa zilizowasillishwa na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ambazo zinaendelea kuhakikiwa, kwamba katika Kijiji cha Guta jumla ya wananchi wanne waliuawa na wengine tisa walijeruhiwa na mamba katika kipindi cha mwaka 2013 hadi 2015. Katika kipindi hicho, hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na kupokelewa kuhusu matukio katika Vijiji vya Tairo, Nyamtwali na Njabeu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kifungu cha 69 cha Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009, kimempa mamlaka Mkurugenzi wa Wanyamapori kukasimu majukumu ya kushughulikia masuala ya wanyamapori wakali na waharibifu kwa Afisa aliyeidhinishwa. Aidha, Sheria imeainisha utaratibu wa kutoa taarifa za matukio kuanzia kwa Mtendaji wa Kijiji, Maafisa Wanyamapori walio karibu hadi Wizarani kwa hatua zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuokoa maisha ya wananchi kutokana na hatari ya mamba na viboko katika vijiji vilivyotajwa, Wizara yangu kupitia Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori (TAWIRA) kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda itafanya tathmini ya ongezeko la mamba na iwapo itadhihirika kuwa idadi yao ni kubwa kuliko viwango vinavyokubalika, hatua stahiki zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kuweka utaratibu wa kuwavuna wanyama hao. Utaratibu huu utatumika katika maeneo yote yenye uhatarishi wa mamba na viboko. Wizara itaendelea kutoa elimu kuhusu uhifadhi, jinsi ya kujilinda na kujiepusha na wanyamapori wakali na waharibifu wakiwemo mamba pamoja na taratibu za kuwasilisha madai ya malipo ya kifuta jasho na machozi kwa wale watakaoathirika.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na jitihada hizo za Serikali, Wizara inatoa wito kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari katika maeneo hatarishi hususan ambayo yamebainika kuwa na mamba au viboko na kuwasilisha taarifa za matukio haraka kwa Viongozi wa Vijiji husika na Maafisa Wanyamapori walio karibu ili kumbukumbu za matukio na hatua stahiki ziweze kuchukuliwa mapema.
MHE. HASSAN S. KAUNJE aliuliza:-
Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2015 - 2020, imeeleza juu ya uendelezaji wa utalii kwa Ukanda wa Kusini kama Program Maalum:-
Je, ni lini Serikali imepanga kuanza mpango huo maalum?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Seleman Kaunje, Mbunge wa Lindi Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2015 - 2020, Sura ya Pili katika aya ya 29 imeainisha program maalum ya uendelezaji wa utalii nchini ikiwemo katika Ukanda wa Kusini.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Awamu ya Tano yenye dhamana ya kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi imeandaa Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano kuanzia 2016/2017 - 2020/2021 ambao ni sehemu ya pili ya Mpango Elekezi wa miaka 15, (2011/2012 – 2025/2026) na Dira ya Taifa ya Maendeleo, 2025.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, katika mpango huo wa miaka mitano, Serikali imejumuisha hatua ya kufungua fursa za utalii katika Ukanda wa Kusini kama mojawapo ya hatua muhimu kwa maendeleo ya viwanda na ukuzaji wa uchumi. Ili kutekeleza azma hii, Wizara yangu imejipanga kushirikisha sekta binafsi kuwekeza katika miundombinu ya utalii, kuwekeza na kuendeleza maeneo mengine yenye fursa za utalii, kutekeleza mkakati wa Kitaifa wa Utangazaji wa utalii ili kuwavutia watalii wengi zaidi, kutoa mafunzo ya ukufunzi katika Chuo cha Taifa cha Utalii kwa lengo la kuimarisha mafunzo ya Utalii na kutenga maeneo maalum ya utalii, hususan ya fukwe za bahari na maziwa kwa ajili ya hoteli za kitalii kama maeneo muhimu kwa ukuaji wa uchumi na ustawi wa Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi hicho, Serikali itashirikisha sekta binafsi ili iwekeze katika kuboresha miundombinu na vivutio vya utalii katika Ukanda wa Kusini na kuvitangaza hususan maeneo ya utalii wa kihistoria na kitamaduni kama vile mji wa kihistoria wa Mikindani, Kilwa Kivinje, Pori la Akiba Lukwika-Lumesule na Pori la Akiba la Selous upande wa kusini na maeneo mengine katika Ukanda huo. Aidha, ili kukuza utalii wa baharini na katika fukwe za bahari, Serikali imepanga kutenga maeneo maalum ya utalii hususan kwa ajili ya hoteli za kitalii kando ya Bahari ya Hindi Mkoani Lindi na Mtwara.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upana wake, utalii wa Kusini unatarajiwa pia kuboreshwa kupitia program na miradi mbalimbali kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo ikiwa ni pamoja na mradi ujulikanao kama REGROW unaofadhiliwa na Benki ya Dunia kwa gharama ya Dola za Kimarekani zisizopungua milioni 100.
Pori la Akiba la Kagera Nkanda lililopo Wilaya ya Kasulu lilianzishwa kipindi ambacho Wilaya ya Kasulu ilikuwa na wakazi wachache na kwa sasa idadi ya watu katika Wilaya hiyo imekuwa kubwa na kufanya mahitaji ya ardhi kuwa makubwa, pia hivyo kusababisha mgogoro baina ya wakulima na wafugaji na mamlaka za misitu na wanyaa pori.
Je, Serikali imejipanga vipi kumaliza migogoro hii na kuwasaidia wananchi?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Augustine Vuma Holle, Mbunge wa Kasulu Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Kagera Nkanda ni kijiji kilichopakana na Hifadhi ya Msitu wa Makere Kusini na si Pori la Akiba. Msitu huu ulihifadhiwa kwa Tangazo la Serikali Namba 250 la mwaka 1956 na una ukubwa wa hekta 99,682.7. Uhifadhi wa msitu huo unatokana na umuhimu na faida zake kwa Taifa ikiwa ni pamoja na kuwa chanzo kikuu cha maji yanayoingia kwenye Mto Malagarasi, ushoroba wa wanyamapori kati ya Pori la Akiba Moyowosi na Kigosi, sehemu ya eneo la ardhi oevu lenye umuhimu wa kimataifa (The Malagarasi Moyowosi Ramsar Site), Hifadhi ya viumbe na mimea na hivyo kusaidia kupunguza madhara ya mabadiliko ya tabianchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, chanzo cha migogoro na wananchi wanaoishi jirani na hifadhi hii ni mahitaji ya ardhi kwa ajili ya shughuli za kibinadamu hususani kilimo. Swali hili limejibiwa na Serikali mara mbili ndani ya Bunge lako Tukufu, ambapo mara moja lilijibiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii tarehe 26 Juni, 2014 na mara nyingine lilijibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI mnamo tarehe 18 Juni, 2015.
Mheshimiwa Naibu Spika, viongozi mbalimbali akiwemo Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Awamu ya Nne walifanya ziara katika eneo husika na kusikiliza hoja kutoka kwa wananchi, lakini kumbukumbu zinaonesha kuwa hakuna madai yaliyotolewa kuhusiana na uhitaji wa ardhi ya hifadhi kutoka kwa wananchi ispokuwa kwamba baadhi ya wananchi walivamia msitu wamekuwa wakiomba na kuruhusiwa kuvuna mazao waliyoyapanda kabla Serikali haijatekeleza operesheni ya kuwaondoa katika hifadhi ya msitu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu haya, wakati wa zoezi la kushughulikia matatizo ya ardhi kwa nchi nzima ikihusisha Wizara sita, zoezi ambalo litaanza baada ya Bunge la Bajeti, Wizara yangu itazingatia wito uliotolewa Bungeni kupitia jibu la msingi lililotolewa na TAMISEMI mnamo tarehe 18 Juni, 2015 kuhusu mgogoro huu.
MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:-
Kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu wa mipaka kati ya TANAPA na vijiji na vitongoji jirani vinavyowazunguka.Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza mgogoro huu kati ya TANAPA na vitongoji vya Kitame, Razaba, Gama-Makani katika Kata ya Makurunge?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Shukuru Kawambwa, Mbunge wa Bagamoyo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro yote mitatu iliyotajwa na Mheshimiwa Mbunge inahusiana na hifadhi ya Taifa Saadani iliyoanzishwa kisheria kwa Tangazo la Serikali Namba 281 la mwaka 2005.
Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro baina ya Kitongoji cha Kitame, Kijiji cha Makurunge na hifadhi umetokana na malalamiko kwamba wananchi hawakushirikishwa katika zoezi la uwekaji wa mipaka hivyo kusababisha yaliyokuwa maeneo yao kuingizwa ndani ya hifadhi bila ridhaa yao. Hata hivyo, kumbukumbu zinaonyesha kwamba kuwa wananchi walishikikishwa kikamilifu kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu ikiwa ni pamoja na kufanyika kwa mkutano wa kijiji mama cha Makurunge ambacho kitongoji hiki ni sehemu yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro baina ya shamba la Razaba na hifadhi umetokana na utata wa takribani eneo la hekta 3,441 alilopewa mwekezaji Bagamoyo Eco-Energy kwa hati miliki namba 123097 ya terehe 9 Mei, 2013 ili amiliki na kuendesha shughuli za kilimo cha miwa katika eneno ambalo kiuhalisia limo ndani ya hifadhi ya Taifa ya Saadani. Juhudi za kutatua mgogoro huu ziliendelea kufanyika kwa takribani miaka minne kwa kuhusisha ngazi za Vijiji, Wilaya, Mkoa na Wizara zinazohusika na hatimaye kutolewa maelekezo kupitia agizo la Mheshimiwa Waziri Mkuu agizo ambalo lilizingatia athari za mazingira zilizotishia uwepo wa hifadhi ya Saadani iwapo kilimo cha miwa kingeruhusiwa katika eneo linalozungumziwa.
Mgogoro baina ya Gama -Makani na hifadhi unatokana na malalamiko ya wananchi kuwa baadhi ya waliofidiwa wakati wa uanzishwaji wa hifadhi katika eneo hilo hawakuwa wamiliki wazawa wa maeneo hayo. Hata hivyo taarifa zinaonyesha kuwa mchakato wa malipo ya fidia ulifuata taratibu muhimu ikiwemo ushirikishwaji wa karibu wa uongozi wa Wilaya ya Bagamoyo, Serikali za Kata na Serikali za Vijiji husika ambao ulizingatia ilivyohitaji la kuwalipa wananchi waliostahili na si vinginevyo. Pamoja na maelezo haya, Serikali imekwishaunda timu ya pamoja ya wataalam ambayo inaendelea na kazi ya kutafuta suluhisho la migogoro ya ardhi nchini ikishirikisha Wizara mbalimbali kama ilivyoahidiwa wakati wa Bunge la Bajeti lililoahirishwa mwezi Juni, 2016.
MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza:-
Katika eneo la Ndolezi Wilaya ya Mbozi kuna kimondo ambacho ni cha aina yake katika nchi hii na dunia kwa ujumla:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhamasisha watalii wa ndani na nje ya nchi kuja kukiangalia Kimondo hicho ili kuchangia pato la taifa?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii napenda kujibu swali la Mheshimiwa Japhet Ngailonga Hasunga Mbunge wa Vwawa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubalina na Mheshimiwa Mbunge kuwa Kimondo hiki kilichopo Kusini Magharibi mwa Kilima cha Marengi, Kijiji cha Ndolezi Wilaya ya Mbozi, Mkoani Mbeya ni cha kipekee hapa nchini, na kwakweli na duniani kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kulingana na taarifa za kitaalamu kimondo hiki kinaaminika kuwa kati ya vimondo nane vikubwa zaidi duniani kikikadiriwa kuwa na uzito wa tani 12, urefu wa mita 3.3, upana wa mita 1.63 na kimo cha mita 1.22. Sehemu yake kubwa ni chuma ambayo asilimia 90.45 na sehemu iliyobaki inajumuisha nikeli asilimia 8.69, shaba asilmia 0.66, sulphur asilimia 0.01, fosfori asilimia 0.11. Kwa kuzingatia upekee na umuhimu wake, mwaka 1967 kilitangazwa kuwa Urithi wa Taifa kwa tangazo la Serikali Na. 90 la tarehe 1967. Taarifa kuhusinaa na tarehe na mwaka wa kuanguka kwa kimondo hiki bado haijulikani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu imeendelea kutangaza Kimondo cha Mbozi kama moja ya vivutio muhimu na adimu nchini na duniani. Uhamasishaji umefanyika kwa kutumia njia mbalimbali ndani na nje ya nchi, ikiwa ni pamoja na vipindi vya runinga vya zamadamu (Televisheni ya Taifa TBC1) na utalii wa ndani kupitia Kituo cha Channel Ten. Pia machapisho ya Tanzania; The Land of Great Heritage Sites na Tanzania Cultural Heritage Resources ambayo nakala zake pia husambazwa katika maonesho mbalimbali na balozi zetu nje ya nchi. Machapisho mengine ambayo hutolewa kwa Kiswahili ni pamoja na Jarida la Ifahamu Idara ya Mambo ya Kale na Jarida la Maliasili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maelezo na picha za kimondo hiki pia vimewekwa katikatovuti na mitandao mbalimbali duniani. Juhudi hizi pamoja na nyingine zimeendelea kuonesha matunda kwani takwimu zinaonesha kuongezeka kwa idadi ya watalii na mapato. Kwa mfano kati ya mwaka 2012/13 na 2014/2015 watalii waliongezeka kutoka jumla ya 990 hadi 1,681 na mapato kuongezeka kutoka Shilingi 811,000 hadi 2,426,000.
MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:-
Wavunaji na watumishi wa msitu wa Taifa Sao Hill wanapata huduma za kijamii na mahitaji yao katika Jimbo la Mafinga Mjini na kwa kuwa msimu uliopita hakuna kijiji au mtaa hata mmoja uliopata kibali cha kuvuna msitu katika Jimbo hilo:-
(a) Je, Serikali iko tayari kutoa kibali cha kuvuna msitu kwa kila kijiji au mtaa ili fedha zitakazopatikana kutokana na vibali hivyo ziweze kusaidia shuguli za kuboresha huduma za jamii kama vile kuchonga madawati na kumalizia ujenzi wa zahanati?
(b) Je, Serikali iko tayari kutoa vibali vya kuvuna misitu kwa vikundi rasmi vya wajasiliamali ili kuwasaidia kukuza mitaji yao na kujipatia maendeleo ya kiuchumi?
(c) Je, ni kiasi gani cha fedha kimetolewa kama sehemu ya kurejesha hisani kwa jamii kutoka kwa kampuni ya misitu na viwanda vikubwa vya mazao ya misitu vilivyopo kwenye Jimbo la Mafinga na maeneo ya jirani?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini lenye sehemu (a), (b) na (c) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ugawaji wa malighafi kutoka katika mashamba ya miti unaongozwa na Mwongozo wa Uvunaji wa mwaka 2007 uliofanyiwa mapitio mwaka 2015. Aidha, Wizara yangu kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania imekuwa ikipokea na kuyafanyia kazi maombi mengi ya vibali vya uvunaji vyenye uhitaji wa mita za ujazo nyingi kuliko kiwango kinachoruhusiwa ikilinganishwa na uwezo wa mashamba wa kutoa malighafi kwa viwanda vya uchakataji wa mazao ya misitu kwa mwaka. Kwa mfano mwaka 2015/2016, jumla ya maombi 4,986 ambayo yalihitaji mita za ujazo 15,454,214 yalipokelewa na kufanyiwa kazi. Hata hivyo, ni maombi 1,030 pekee yenye jumla ya mita za ujazo 740,800 yaliidhinishwa, ambacho ndicho kiwango cha ukomo kulingana na uwezo wa mashamba katika mwaka huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na uchache wa malighafi, Wizara imekuwa inatoa kipaumbele cha vibali vya uvunaji miti kwa viwanda vyenye mikataba na Serikali, miongoni mwao ni baadhi ya viwanda vya Serikali vilivyobinafsishwa, viwanda vingine vikubwa na vya kati, ikifuatiwa na wavunaji wadogo wadogo, vikundi na taasisi za watu binafsi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara imekuwa ikitoa vibali pia kwa wadau na vijiji vinavyopakana na misitu kwa ajili ya shughuli za maendeleo ikiwa ni pamoja na utengenezaji wa madawati. Kwa mfano, katika shamba la miti la Sao Hill kati ya mwaka 2010/2011 na 2015/2016 vibali vya uvunaji kwa vijiji 183 vyenye thamani ya sh. 2,820,000,000 vilitolewa. Vile vile, shamba la Sao Hill lilihifadhili miradi ya maendeleo yenye thamani ya shilingi milioni 880 ikiwemo utengenezaji wa madawati katika vijiji 23.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na uzoefu wa hivi karibuni Wizara yangu imeona haja ya kupitia upya mwongozo wa uvunaji wa mwaka 2007 kwa namna ambayo itazingatia manufaa kwa jamii jirani na misitu hiyo kama ilani ya CCM inavyoelekeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu haina takwimu zinazohusu kiasi cha fedha zilizorejeshwa kama hisani kwa jamii kutoka kampuni na viwanda vikubwa vya mazao ya misitu vilivyopo kwenye Jimbo la Mafinga Mjini na maeneo ya jirani. Aidha, ushauri unatolewa kwa Mheshimiwa Mbunge awasiliane na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafinga ili aweze kupatiwa takwimu hizo.
MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:-
Je, Serikali ina uhakika gani na usalama wa nchi yetu katika mpaka wa Pori la Akiba la Kimisi na Burigi na Mto Kagera?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Constatine John Kanyasu Mbunge wa Geita Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu inaendelea kuimarisha ulinzi wa rasilimali za wanyamapori zilizopo ndani ya Mapori ya Akiba yakiwemo ya Kimisi na Burigi katika kukidhi malengo ya uhifadhi endelevu kwa maslahi ya Taifa. Hii ni pamoja na kupambana na uvamizi wa mifugo, shughuli za kilimo, uharibifu wa mazingira na ujangili ndani ya hifadhi hizo. Aidha, pamoja na ulinzi wa ndani ya hifadhi, eneo la mpaka wa Mto Kagera na Pori la Akiba la Kimisi na Burigi limeonesha kuwa na changamoto zaidi zikiwemo za uhamiaji haramu na uingizaji wa silaha ambazo zinatumika kwa ujangili na ujambazi hivyo kulifanya eneo hilo la mpakani kuhitaji ulinzi zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu imekuwa ikishirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama ngazi za Wilaya na Mkoa, kuimarisha ulinzi na usalama wa nchi kwa upana wake katika eneo hii mpakani.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu itaendelea kuimarisha doria ndani ya mapori ili kuboresha uhifadhi wa wanyamapori na kuhakikisha usalama katika maeneo hayo. Aidha, wavamizi wa hifadhi kwa shughuli za mifugo wanaweza kutumiwa kuhatarisha usalama wa nchi. Hivyo tunatoa rai kwa wananchi na wadau wengine kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali katika dhana nzima ya ulinzi shirikishi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama itaendelea kuimarisha ushirikiano na nchi jirani kuhakikisha ulinzi na usalama wa mipakani unakuwa madhubuti ili kudhibiti madhara yanayotokana na uvamizi wa mifugo na wahamiaji haramu.
MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:-
Mbuga ya Hifadhi ya Wembere ni mbuga iliyotelekezwa na Serikali na kupoteza sifa za kuendelea kuwa hifadhi na sasa inatumika na wafugaji kulisha mifugo na wakulima kulima alizeti na mpunga kwenye eneo hilo.
Je, ni kwa nini Serikali isibadilishe matumizi ya mbuga hiyo badala yake ipimwe na kutumika kwa wafugaji na wakulima na kuondoa migogoro inayoendelea kati ya wakulima na wafugaji ambayo wakati mwingine inasababisha mauaji na uharibifu wa mali?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Dalaly Peter Kafumu, Mbunge wa Igunga kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mbuga ya Wembere ipo ndani ya mipaka ya mikoa ya Tabora na Singida. Umuhimu wa eneo hili ni pamoja na kuwa chanzo cha maji yanayokwenda katika maziwa Eyasi na Kitangire. Mbuga hiyo pia ni maarufu kwa aina (species) za mimea na wanyamapori mbalimbali na muhimu kwa mazalia ya ndege mbalimbali wenye sifa za Kitaifa na Kimataifa. Eneo hilo linatambuliwa Kimataifa kama mahsusi kwa kundi muhimu la uhifadhi wa ndege duniani tangu mwaka 2001.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kuwa eneo hilo linakabiliwa na changamoto ya uvamizi kwa shughuli za kilimo na ufugaji kama alivyobainisha Mheshimiwa Mbunge, bado Serikali haijaitelekeza mbuga hiyo na kinyume chake eneo hilo linatumika kwa shughuli za uwindaji wa kitalii ambapo linaliingizia Taifa fedha za kigeni na kutoa ajira kwa wananchi waishio kando ya eneo hilo. Kwa mfano, katika kipindi cha mwaka 2013/2014 hadi 2015/2016 Serikali imepata kiasi cha dola za Kimarekani 142,450 kutokana na shughuli za uwindaji katika vitalu vilivyoko ndani ya eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na umuhimu kiikolojia wa eneo hilo Kitaifa na Kimataifa Wizara yangu itaendeleza majadiliano na Serikali ya Mkoa wa Tabora na Singida ili kuona uwezekano wa kupandisha hadhi eneo hilo ili kuwa na uhifadhi endelevu wa bioanuai zilizopo.
MHE. KISWAGA B. DESTERY (K.n.y. MHE. NJALU D. SILANGA) aliuliza:-
Mheshimiwa Rais kwenye kampeni za uchaguzi aliahidi kupanua mpaka wa Game Reserve iliyoko Maswa:-
Je, ni lini ahadi hiyo itatekelezwa?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Njalu Daudi Silanga, Mbunge wa Itilima, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Pori la Akiba Maswa lilianzishwa kisheria kwa Tangazo la Serikali Namba 270 la mwaka 1962. Pori hilo ni sehemu muhimu ya uhifadhi wa baioanuai katika mfumo wa ikolojia ya Serengeti ambayo inatoa mchango muhimu kwa viumbe mbalimbali wanaopatikana katika maeneo hayo ikiwemo kutunza vyanzo vya maji kwa mahitaji ya binadamu na shughuli za kiuchumi hususan utalii. Kwa muda mrefu tokea kuanzishwa kwa pori hili, wananchi wa vijiji husika wamekuwa wakinufaika na pori hili kwa shughuli mbalimbali za kiuchumi, upatikanaji wa ajira na mgao wa fedha ambapo asilimia 25 ya mapato yatokanayo na shughuli za uwindaji wa kitalii hutolewa kwa Halmashauri ya Wilaya husika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Pori la Akiba la Maswa limefanyiwa marekebisho ya mpaka mara tano katika jitihada za kutatua changamoto ya mahitaji ya ardhi kwa wananchi wanaoishi jirani na pori hili. Hata hivyo, uamuzi wa kumega ardhi ya pori hili kwa kurekebisha mipaka mara kwa mara haujaweza kukidhi haja ya kumaliza tatizo hili kwa namna endelevu.
Mheshimiwa Naibu Spika, chanzo kikuu cha changamoto hii ni ukosefu wa mpango wa matumizi bora ya ardhi ambapo wananchi huendelea na utamaduni wa kumiliki idadi kubwa ya mifugo inayozidi uwezo wa maeneo ya malisho na kilimo cha kuhamahama. Uzoefu umeonyesha kuwa umegaji wa ardhi kwa namna ulivyofanyika siku za nyuma si suluhu endelevu ya tatizo la migogoro kati ya hifadhi na wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu katika swali namba 332 la tarehe 8 Juni, 2016 linalohusu marekebisho ya mipaka ya Hifadhi ya Moyowasi na wananchi, Wizara yangu itaorodhesha maombi haya katika orodha ya maeneo yanayopakana na hifadhi yatakayoshughulikiwa kimkakati na Serikali kwa kushirikisha wadau wote muhimu ikiwa ni pamoja na wananchi, Wizara ya Maliasili na Utalii, Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, TAMISEMI, Maji, Nishati na Madini na Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira kwa nchi nzima.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu inaendelea kusisitiza kwamba utekelezaji wa azma ya Serikali ya kujibu kero za wananchi kuhusu changamoto za mahitaji ya ardhi utazingatia uwepo wa sheria, kanuni na taratibu na pia kuweka mbele maslahi ya Taifa.
MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:-
Sekta ya utalii ina mchango mkubwa katika kuliingizia Taifa fedha za kigeni:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ya barabara, hoteli na airstrips katika Pori la Akiba la Kigosi ili kuweza kuvutia watalii wengi zaidi kutembelea vivutio vilivyopo katika Pori hili zuri la Kigosi na Muyowosi?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba mchango wa sekta ndogo ya utalii katika uchumi wa Taifa na maendeleo ya jamii ni mkubwa sana hususan kwa kuongoza katika kuipatia Serikali fedha nyingi za kigeni na pia kuchangia Pato la Taifa kwa ujumla kwa kiwango cha asilimia 17. Aidha, Wizara yangu inaamini kwamba kwa kuboresha miundombinu, vivutio na utoaji huduma, sekta hii inaweza kuchangia zaidi katika Pato la Taifa na upatikanaji wa fedha za kigeni.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mapori ya Akiba ya Moyowosi na Kigosi yenye jumla ya kilometa za mraba 21,060 yanapakana na Mikoa ya Kigoma, Shinyanga na Geita. Eneo kubwa la mapori hayo ni ardhi oevu ambayo inawezesha upatikanaji wa maji kwa kipindi chote cha mwaka kwa ajili ya ustawi wa wanyamapori. Mapori haya ni moja kati ya maeneo ya mkakati ya Wizara katika kuinua utalii wa Kanda ya Magharibi na Kanda ya Ziwa Magharibi ambapo kwa sasa yanatumika kwa shughuli za utalii wa uwindaji. Aidha, baadhi ya maeneo ndani ya mapori haya yana rasilimali za wanyamapori na uoto wa asili mzuri unaofaa kwa shughuli za utalii wa picha na hivyo kuhitaji uboreshaji wa miundombinu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Ibara ya 3(c) ya Ilani ya CCM 2015 – 2020 inasisitiza juu ya umuhimu wa suala hili na inaelekeza Serikali kuboresha miundombinu ndani ya mapori ya akiba ikiwa ni mojawapo ya mikakati ya kuhakikisha kwamba mazao yatokanayo na maliasili yanaendelea kuchangia katika ukuaji wa uchumi na fursa za ajira katika kuwaongezea wananchi kipato.
MHE. DOTO M. BITEKO aliuliza:-
Maafisa wa Idara ya Misitu walivamia wananchi wa kitongoji cha Idosero kilichosajiliwa kwa GN na kuchoma nyumba 40 za wananchi na kuharibu mazao yao.
Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Idosero kwa hasara kubwa waliyopata?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Doto Mashaka Biteko, Mbunge wa Jimbo la Bukombe kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la Idosero limo ndani ya misitu ya Biharamulo na Kahama yenye jumla ya hekta 134,684 iliyoanzishwa kwa sheria, Sura ya 389, Nyongeza ya 59 ya mwaka 1954 na kufanyiwa marekebisho kwa Tangazo la Serikali namba 311 la mwaka 1959. Misitu hii kwa sasa inasimamiwa na Sheria ya Misitu Sura ya 323 Toleo la mwaka 2002.
Mheshimiwa Naibu Spika, mnamo tarehe 07 Novemba, 2015 Maafisa kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe walifanya operesheni ya kuhamisha wavamizi katika misitu.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakazi wa eneo la Idosero walianza kuingia na kufanya shughuli za kibinadamu ndani ya misitu hii mwaka 1985 na uvamizi uliongezeka hatua kwa hatua na kukithiri baada ya kutolewa kwa Tangazo la Serikali Namba 221 la tarehe 27 Juni, 2015 lililolipa eneo hilo hadhi ya kitongoji kipya katika kijiji cha Nampalahala, bila kubainisha mipaka ya kitongoji hicho. Tamko hilo lilikizana na matangazo ya Serikali yaliyopita au yaliyotangulia na Sheria ya Misitu Sura ya 323 ya mwaka 2002 yanayotambua kuwa eneo hilo ni hifadhi ya misitu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na hali hiyo, Kamati ya Ulinzi na Usalama yaWilaya ya Bukombe ilifanya mkutano na wakazi wa eneo la Idosero tarehe 08 Mei, 2015 na kuwataka waondoke kwa hiari yao ifikapo tarehe 08 Julai, 2015. Wakazi hao walikaidi amri hiyo kwa madai kuwa eneo hilo si hifadhi kwa kuwa Tangazo la Serikali Namba 221 limetambua eneo hilo kuwa ni kitongoji cha makazi. Aidha, mnamo tarehe 09 hadi 20 Juni, 2014 Serikali ilifanya sensa ya kuhesabu watu na kubaini kuwepo kwa kaya 309 zenye jumla ya wakazi 2,777 ndani ya eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutekeleza Sheria ya Misitu Sura ya 323 ya mwaka 2002, watumishi wa TFS au Mamlaka ya Misitu walifanya zoezi la kuwaondoa wavamizi katika eneo hilo ambalo hata hivyo halifanikiwa na wananchi bado wanaendelea kuhamia na kupanua shughuli za kibinadamu katika misitu hiyo na kuendelea kufanya uharibifu wenye athari kubwa za kimazingira.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyokwishaeleza katika majibu ya msingi na nyongeza yaliyopita kwa maeneo yenye changamoto zinazofanana na hii utatuzi wa mgogoro huu utapatikana wakati wa zoezi la pamoja la utatuzi wa matatizo ya ardhi linalotarajiwa kuanza baada ya kukamilika kwa shughuli za Mkutano wa Tatu wa Bunge la Kumi na Moja.
MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE aliuliza:-
Mwezi Septemba, 2015 Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, aliwaahidi wananchi wa Kata za Busonzu, Busagara na Murungu ambao wamepakana na Hifadhi ya Taifa ya Muyowosi kwamba mpaka kati ya wananchi hao na hifadhi hiyo, utarekebishwa ili wananchi wapate eneo kwa ajili ya kilimo.
Je, utekelezaji wa ahadi hiyo utaanza lini?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mhandisi Atashasta Justus Nditiye, Mbunge wa Muhambwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu kupitia uongozi wa Serikali ya Wilaya ya Kibondo inayo taarifa ya maombi kutoka kwa wananchi wa Kata za Busonzu, Busagara na Murungu kuongezewa maeneo kutoka Pori la Akiba la Moyowosi kwa matumizi ya shughuli za kibinadamu, ikiwa ni pamoja na shughuli za kiuchumi na kijamii katika vijiji vya kata hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu itayaorodhesha maombi haya katika orodha ya maeneo yanayopakana na hifadhi, yatakayoshughulikiwa kimkakati na Serikali; kwa kushirikisha wadau wote muhimu, zikiwemo Wizara za Maliasili na Utalii, Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, TAMISEMI, Maji, Nishati na Madini na Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, kwa nchi nzima. Utaratibu huu unaotarajiwa kuanza baada ya Mkutano wa Tatu wa Bunge la Kumi na Moja kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu inaendelea kusisitiza kwamba utekelezaji wa azma ya Serikali ya kujibu kero za wananchi kuhusu changamoto za mahitaji ya ardhi, utazingatia uwepo wa sheria, kanuni na taratibu na pia kuweka mbele maslahi ya Taifa. Aidha Hifadhi ya Pori la Akiba la Moyowosi lilianzishwa kisheria, kwa Tangazo la Serikali namba moja, la mwaka 1981 baada ya kukidhi vigezo vyote, ikiwemo ushirikishwaji wa wananchi katika hatua za Vijiji, Kata, Mkoa hadi Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, umuhimu wa kuhifadhi Pori la Akiba la Moyowosi Kitaifa, unazingatia bioanuwai katika mfumo wa ikolojia ya Moyowosi Malagarasi. Inayotoa mchango mkubwa wa viumbe mbali mbali wanaopatikana katika maeneo hayo, pamoja na utunzaji wa vyanzo vya maji kwa matumizi ya binadamu. Eneo hilli pia ni sehemu ya ardhi ya owevu, yenye hadhi ya kimataifa yaani Ramsar Site.
MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:-
Mbuga ya Akiba ya Uwanda katika Wilaya ya Sumbawanga Vijijini ilitengwa miaka ya nyuma wakati idadi ya watu ikiwa ndogo sana ikilinganishwa na sasa.
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kulipunguza pori hilo ili kunusuru shida inayowapata wananchi wanaozunguka eneo hilo ya kukosa maeneo ya kilimo na ufugaji?
(b) Je, kwa nini wananchi wa maeneo hayo wanapigwa na Askari wa Wanyamapori na kunyang’anywa mali zao, wakati hakuna alama yoyote inayoonyesha mpaka katika mbuga hiyo?
(c) Je, wananchi wa vijiji vinavyozunguka pori hilo wamenufaika na nini zaidi ya vipigo wanavyovipata?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ignas Aloyce Malocha, Mbunge wa Kwela, lenye sehemu (a), (b) na (c) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Pori la Akiba Uwanda lenye ukubwa wa kilometa za mraba 5,000 lilianzishwa mwaka 1959 na kutangazwa upya kwa Sheria ya Uhifadhi Wanyamapori Namba 12 ya mwaka 1974, kwa tangazo la Serikali namba 275 la tarehe 8 Novemba, 1974. Kati ya mwaka 1974 na 2013 pori hilo lilikuwa chini ya usimamizi ya Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ambapo lilikabidhiwa rasmi kwa Wizara ya Maliasili na Utalii tarehe 20 Januari, 2014.
Mheshimiwa Naibu Spika, pori hili linazungukwa na jumla ya vijiji tisa ambapo asilimia kubwa ya wakazi wake wanajihusisha na shughuli za kilimo, uvuvi na ufugaji. Umuhimu wa pori hili umejikita katika uhifadhi wa rasilimali wanyamapori, mimea na mazalia ya samaki katika Ziwa Rukwa ambayo ni mojawapo ya vyanzo vikuu vya kiuchumi kwa wananchi wa eneo hilo. Pamoja na umuhimu huo, Pori la Akiba Uwanda kama yalivyo maeneo mengine ya hifadhi, linakabiliwa na changamoto ya ongezeko la shughuli za kibinadamu.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, eneo kubwa la pori hili ni sehemu ya Ziwa Rukwa, na sehemu iliyobaki yenye eneo la kilometa za mraba 400 ni nchi kavu. Kutokana na umuhimu huo Wizara yangu inaona ni mapema kupunguza ukubwa wa pori hilo kwa sababu uamuzi huo utaathiri sababu na malengo ya kuanzishwa kwake. Hata hivyo, Serikali kwa upana wake itajumuisha eneo hili la Pori la Akiba la Uwanda, kuwa miongoni mwa maeneo yanayotarajiwa kushughulikiwa kimkakati zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu haikubaliani na vitendo vya baadhi ya watumishi wake, wakiwemo Askari Wanyamapori kujichukulia sheria mkononi kwa kuwapiga, kuwanyang’anya mali, kuwatoza faini kinyume cha utaratibu, kuwachomea moto nyumba zao, na kuwanyanyasa kwa namna yoyote ile, kwa kisingizio cha kutekeleza matakwa ya sheria. Wizara yangu inasisiza msimamo wa Serikali wa kuendelea kusimamia utawala wa sheria, na hivyo kujipanga zaidi, ili kuchukua hatua kali dhidi ya watumishi watakaodhibitika kukiuka, kwa mujibu wa sheria, kanuni, na taratibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wanaombwa, kutoa ushirikiano katika kuwabaini watumishi wa aina hii, na pia wachukue hatua stahiki kabla, wakati na baada ya matukio ya aina hiyo ili kuirahisishia Serikali kuchukua hatua sahihi kwa wakati sahihi. Hata hivyo Wizara yangu inasisitiza kuwa wananchi wanaoishi katika maeneo yanayopakana na hifadhi, wazingatie na kutii sheria bila shuruti. Ili hifadhi hizo ziendelee kuleta manufaa kwa taifa wakiwemo wananchi hao kwa tija zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kwamba ni kipindi kifupi tu, takribani miaka miwili na nusu tangu usimamizi wa Pori la Akiba Uwanda, ukabidhiwe kwa Wizara yangu. Tayari tumeanza mkakati wa kuwekeza kwa kuboresha miundombinu na vivutio ili kuhakikisha kwamba pori hilo linarudi kwenye hadhi yake ya awali. Kabla ya kufanyika kwa shughuli za utalii zitakazoiwezesha Serikali kushughulikia ipasavyo changamoto za maendeleo ya wananchi. Azma hii inaendana na mipango ya Serikali ya muda mrefu ya kuboresha shughuli za utalii Ukanda wa Kusini.
MHE. MARIA N. KANGOYE aliuliza:-
Sekta ya Utalii ni Sekta inayotegemewa kuliingiza Taifa mapato kwa sababu ya vivutio vingi tulivyojaliwa Tanzania:-
(a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza ahadi iliyopo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2016 - 2020 katika kuongeza bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii?
(b) Je, ni nini mkakati wa Serikali kukiimarisha Chuo cha Utalii ili kutoa mafunzo ya Hoteli na Utalii katika ngazi ya Stashahada ili kuongeza ubora wa Watumishi wa huduma za ukarimu na utalii?
(c) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweka mazingira bora ya kuwezesha vijana kuanzisha makampuni ya kutembeza watalii katika maeneo mbalimbali ya utalii?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maria Ndilla Kangoye, lenye sehemu (a), (b) na (c) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2016 -2020, katika Ibara ya 29(c) inaainisha azma ya Chama cha Mapinduzi kusimamia Serikali katika utekelezaji wa mikakati ya kukuza utalii nchini kwa kuhakikisha kwamba bajeti ya Sekta ya Utalii inaongezeka ili kuutangaza utalii ndani na nje ya nchi.
Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza mkakati huo, Wizara yangu kupitia Bodi ya Utalii na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania imetenga jumla ya sh. 2,730,188,676/= kwa ajili ya shughuli za utangazaji kwa mwaka wa fedha 2016/2017, hii ikiwa ni ongezeko la asilimia 14.7 ikilinganishwa na mwaka 2015/2016. Serikali itaendelea kuboresha utekelezaji wa ahadi hii kwa kushirikisha pia wadau mbalimbali wa maendeleo na vyanzo vingine kama inavyoainishwa na mpango wa maendeleo wa miaka mitano 2016/2017 – 2020/2021.
Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali katika kukiimarisha Chuo cha Utalii katika Kampasi zake zote tatu za Bustani, iliyoko Dar es Salaam; ya Temeke iliyoko Dar es Salaam pia na ya Arusha. Ni pamoja na kuongeza idadi na umahiri wa wakufunzi, kuboresha upatikanaji wa vifaa mbalimbali vya kufundishia na kuboresha miundombinu ya chuo katika kampasi zote.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mipango ya hivi karibuni Chuo cha Utalii kitaboresha utoaji wa mafunzo katika Tasnia ya Ukarimu (Hospitality) na Utalii (Tourism) katika ngazi ya Shahada.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Chuo cha Utalii kwa kushirikiana na Chuo cha Vancouver Island University cha Canada kupitia Mradi wa ISTEP chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kitaanzisha mafunzo ya uongozi katika ngazi ya Shahada kuanzia mwezi Septemba, 2018.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu uimarishaji wa miundombinu, Wizara yangu imetenga jumla ya shilingi milioni 500 katika mwaka wa fedha 2016/2017 ili kukamilisha ujenzi wa jengo la Utalii (Utalii House) Phase II katika Kampasi ya Bustani ya Chuo cha Utalii, Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mazingira bora ya kuwezesha vijana kuanzisha makampuni ya kutembeza watalii katika maeneo mbalimbali ya utalii; Serikali itaendelea kwa msisitizo zaidi kushirikisha sekta binafsi ili kuwashauri vijana wajiunge katika vikundi na kuwapa elimu ili waanzishe na kushiriki kwa tija zaidi katika biashara hii kwa maslahi yao na kwa maslahi ya Taifa. Serikali pia itapitia masharti yote yaliyopo kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu ili kuona kama kutakuwa na uhitaji wa kuyafanya masharti hayo kuwa rafiki zaidi kwa vijana wenye nia thabiti ya kushiriki katika ujenzi wa uchumi wa Taifa kupitia shughuli za uongozaji watalii.
MHE. HAFIDH ALI TAHIR (K.n.y. MHE. ALI SALIM KHAMIS) aliuliza:-
Kisiwa cha Shungimbili kilichopo Wilaya ya Mafia kinamilikiwa na mwekezaji ambaye amekibadilisha jina na kukiita Thanda, mmiliki wake ni Kampuni ya Utalii ya Zululand ya Afrika Kusini. Aidha, kuna madai kuwa kisiwa hicho kimeuzwa kwa mwekezaji huyo; kwenye kisiwa hicho kuna hoteli yenye hadhi ya dunia na ndicho kisiwa ghali duniani kuishi kwani kwa siku ni USD 10,000 na ili upate chumba ni lazima ufanye booking kwa muda usiopungua siku saba:-
(a) Kama kisiwa hicho kimeuzwa: Je, kimeuzwa shilingi ngapi na hoteli hiyo inalipa kodi kiasi gani kwa Serikali?
(b) Je, Wizara ya Maliasili na Utalii inashirikiana vipi na Wizara ya Utalii Zanzibar hasa ukizingatia Wizara ya Mambo ya Nje ni ya Muungano katika Mikataba ya Kimataifa?
NAIBU WAZIRI WA MALISILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ali Salimu Khamisi, Mbunge wa Mwanakwerekwe, lenye vipengele (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kisiwa cha Shungimbili ni moja ya visiwa vitatu vilivyopo katika Wilaya ya Mafia. Visiwa hivyo vitatu na vingine 12 vinafanya jumla ya visiwa 15 ambavyo ni maeneo tengefu yanayosimamiwa na Taasisi ya Hifadhi za Habari na maeneo tengefu yaliyopo nchini, chini ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
Kimsingi Taasisi hii ilianzishwa kwa Sheria ya Bunge Namba 29 ya mwaka 1994 ambapo miongoni mwa majukumu yake ni kusimamia maeneo yote yaliyotangazwa kuwa hifadhi za habari (Marine Parks) na maeneo tengefu ya bahari (marine reserves).
Mheshimiwa Naibu Spika, Kisiwa cha Shungimbili hakijauzwa na baada yake kimeingizwa katika uwekezaji kupitia Kampuni ya Thanda Tanzania Limited inayojenga Lodge ya kitalii ikiwa ni majawapo ya mipango ya Taasisi ya MPRU ya kuimarisha uwekezaji katika maeneo inayosimamia ili kuongeza mapato ya Serikali na kutekeleza Sera ya Utalii ya mwaka 1999. Aidha, uwekezaji huo umepita taratibu zote za Serikali na utakapokamilika mwekezaji atatekeleza wajibu wake ikiwemo kulipia tozo zote kwa mamlaka zinazohusika kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, ndiyo yenye dhamana ya kuingia mikataba yote ya Kimataifa, yenye maslahi kwa nchi nzima Bara na Visiwani. Hata hivyo, pamoja na kwamba nyongeza ya kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 haijaorodhesha Sekta ya Utalii kama moja ya maeneo ya Muungano, haijazuia Wizara zinazosimamia Sekta ya Utalii kutoka pande hizi mbili kuendelea kushirikiana.
Mheshimiwa Naibu Spika, ushirikiano kati ya pande mbili za Muungano unaozungumziwa unajumuisha maeneo ya utangazaji wa vivutio vya Tanzania Kimataifa kama nchi moja, utayarishaji taarifa na ujenzi wa mifumo imara ya ukusanyaji wa takwimu kupitia Kamati inayojulikana kama The Steering Committee of the Tanzania Tourism Sector Survey na mikutano mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania Bara na Zanzibar na ile ya uwezeshaji utalii (Tourism Facilitation Committee) ya wadau wa utalii. Wizara yangu itaendelea kudumisha na kuuboresha uhusiano huu kwa sababu mtawanyiko wa vivutio vya utalii unagusa Tanzania kama nchi moja.
MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO (K.n.y. MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI) aliuliza:-
Sekta ya maliasili na utalii ni rasilimali inayobeba uchumi wa Tanzania, ikitumika vizuri kwa uendelevu, italeta maendeleo katika jamii na uchumi wa nchi kwa ujumla:-
(a) Je, ni lini Serikali itaanza kuipa kipaumbele sekta ya utalii?
(b) Je, ni lini Serikali itaboresha mazingira ya kazi ya askari wanyamapori?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Immaculate Sware Semesi, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba sekta ya maliasili na utalii inatoa mchango mkubwa na kubeba uchumi wa Tanzania. Kwa mfano, sekta hii imechangia takribani asilimia 25 ya fedha zote za kigeni nchini katika kipindi cha miaka mitatu mfululizo yaani 2012/2013 – 2014/2015 na hivyo kuchangia zaidi ya asilimia 17 ya Pato la Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sekta ya Utalii imechangia pia katika ajira nchini ambapo takribani ajira 500,000 za moja kwa moja ambayo ni takribani asilimia 11 ya ajira zote na ajira takribani 1,000,000 zisizo za moja kwa moja zimetolewa. Aidha, sekta hii imeendelea kuwa kichocheo cha ukuaji wa sekta mbalimbali zikiwemo kilimo, elimu, mawasiliano, burudani usafirishaji na uzalishaji wa huduma mbalimbali kwa watalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutekeleza mipango ya uendelezaji wa sekta ya utalii kama ilivyoainishwa katika Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016/2017 – 2020/2021 na mipango ya kila mwaka wa fedha. Kwa ujumla mipango ya uendelezaji wa sekta inajumuisha utunzaji na uboreshaji wa vivutio vya utalii vilivyopo, uainishaji na uboreshaji wa vituo vipya vya utalii, uboreshaji wa miundombinu ya utalii, uboreshaji wa utoaji wa huduma kwa watalii na kwa umuhimu wa pekee kuongeza mbinu na jitihada za kutangaza utalii wa Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, kwa upande mwingine Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo katika kutekeleza programu na miradi mbalimbali ya maendeleo ya sekta ya utalii. Kwa mfano, kwa kipindi cha mwaka 2017 – 2022, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia itatekeleza mradi wa kuboresha utalii Ukanda wa Kusini mwa Tanzania kwa gharama ya takribani Dola za Kimarekani zisizopungua milioni mia moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua na kuthamini kazi kubwa na ngumu inayofanywa na Askari Wanyamapori wanapotekeleza majukumu yao ya kutoa ulinzi na kusimamia uhifadhi kwa ujumla wa wanyamapori hususani kupambana na ujangili. Aidha, kuanzia mwaka wa Fedha 2016/2017, Serikali imejipanga kuboresha mazingira ya kazi ya Askari Wanyamapori sambamba na watumishi wengine ambapo kwa upande wa Askari Wanyamapori, upatikanaji wa vitendea kazi, uboreshaji wa stahili zao na usimamizi bora zaidi wa utendaji kazi ni miongoni mwa malengo ya Mamlaka ya Wanyamapori (TAWA). Mamlaka hii imeanzishwa tarehe 16 Oktoba, 2015 ili ifanye kazi sambamba na Mamlaka ya Ngorongoro na TANAPA katika kutekeleza lengo kuu la udhibiti wa ujangili nchini.
MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza:-
Mgogoro wa mipaka kati ya Hifadhi ya Serengeti na Vijiji vya Wilaya ya Ngorongoro ni wa muda mrefu na sasa umekuwa sugu na kusababisha kero kwa wananchi wa maeneo hayo:-
Je, ni lini Serikali itaainisha mipaka ya maeneo hayo ili kumaliza mgogoro huu?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Catherine Valentine Magige, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwa muda mrefu sasa kumekuwepo na migogoro ya mipaka baina ya Hifadhi ya Serengeti na baadhi ya vijiji katika Wilaya za Serengeti, Bunda, Ngorongoro, Tarime, Busega, Bariadi na Meatu.
Kwa upande wa Wilaya ya Ngorongoro, Vijiji vinavyohusika ni pamoja na Ololosokwani, Soitsambu, Maaroni, Arashi, Piyaya, Orelian na Magaidulu. Kwa kiasi kikubwa migogoro ya mipaka katika vijiji hivi imechangiwa na kutohakikiwa kwa mipaka ya hifadhi baada ya Tangazo la Serikali Na. 235 la tarehe 21 Juni, 1968, zoezi ambalo lingefuatiwa na uwekaji wa alama za kudumu chini ya usimamizi wa kitaalam wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, migogoro ya mipaka katika Vijiji vya Wilaya za Serengeti, Bunda, Tarime, Busega, Bariadi na Meatu ilipatiwa ufumbuzi baada ya zoezi shirikishi miongoni mwa wadau wa pande za migogoro na wataalam wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, pamoja na jitihada zote zilizofanyika ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa wananchi na viongozi wa vijiji vya Wilaya ya Ngorongoro ambavyo eneo lake kwa ujumla lina umuhimu mkubwa na wa kipekee kiikolojia, wananchi hawa walikataa kutoa ushirikiano na hivyo kukwamisha zoezi hilo. Wizara yangu imeorodhesha mgogoro huu wa mpaka baina ya Hifadhi ya Serengeti na Vijiji vya Wilaya ya Ngorongoro vilivyotajwa hapo juu kwenye orodha ya migogoro yote ya ardhi hususani inayohusu mipaka ya Hifadhi za Taifa na misitu inayopangwa kushughulikiwa kimkakati zaidi zaidi na Serikali hivi karibuni.
MHE. SUSAN L. KIWANGA aliuliza:-
Serikali imetwaa maeneo ya vijiji katika Kata za Idete, Namwala, Mofu, Mbinga, Igima, Mchombe, Mngeta, Kalengakelu, Mlimba, Kamwene, Chita na Utengule kwa madai kwamba ni maeneo ya hifadhi bila kuwashirikisha wananchi, jambo ambalo limefanya wananchi kushindwa kuendeleza shughuli zao za kilimo na ufugaji na hivyo kuendelea kuwa maskini.
Je, Serikali itakuwa tayari kushirikisha wananchi ili kuweka mipaka kati ya maeneo ya kilimo na ufugaji na yale ya Hifadhi ya Taifa ili kuondoa mgogoro wa ardhi uliopo hivi sasa kwa wananchi kukosa maeneo ya kilimo na malisho ya mifugo?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Susan Limbweni Kiwanga, Mbunge wa Mlimba, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu haijawahi kutwaa na haina utaratibu wa kutwaa maeneo ya vijiji na kuyafanya kuwa maeneo ya hifadhi bila ya kuwashirikisha wananchi. Aidha, sehemu ya maeneo ya vijiji vilivyoko ndani ya kata 12 zilizotajwa yamo ndani ya eneo la Hifadhi ya Ramsar ya Bonde la Kilombero iliyotambulika na kuorodheshwa mwaka 2002.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la Ramsar la Bonde la Kilombero ni muendelezo wa hifadhi ulioanza na Pori Tengefu la Kilombero lililoanzishwa kwa Sheria ya Uhifadhi Wanyamapori, Sura ya 302 ya mwaka 1952 kupitia Tangazo la Serikali Namba107. Pori hili lilirithiwa na Sheria ya Uhifadhi Wanyamapori Namba12 ya mwaka 1974 na kuboreshwa na Sheria Namba 459 ya mwaka 1977 baada ya taratibu zote za kisheria kukamilika ikiwemo ushirikishaji wananchi. Aidha, eneo hili ambalo ni chanzo kikubwa cha maji na lenye uwepo wa viumbe adimu duniani lina ukubwa wa kilometa za mraba 7,967.35 sawa na hekta 795,735 sifa ambazo zinalifanya kuwa eneo la tatu kwa ukubwa lenye umuhimu wa Kimataifa nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro ya ardhi liliyopo baina ya wananchi na vijiji katika kata zilizotajwa ambavyo vilianzishwa baada ya kuanzishwa kwa Pori Tengefu la Kilombero imetokana na hatua mbalimbali za ukiukaji wa sheria, kanuni na taratibu. Aidha, katika kutatua migogoro hiyo, Serikali inaendelea kutekeleza yafuatayo:-
(a)Kupitia Mradi wa KILORWEMP unaotekelzwa chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii; kupitia upya mipaka, kuweka alama, kuchora ramani na kutunza kumbukumbu kwa njia za kawaida na kielektroniki.
(b)Kupitia mpango wa upimaji ardhi za vijiji vya Wilaya za Kilombero, Ulanga na Malinyi unaosimamiwa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; kukamilisha upimaji na urasimishaji wa ardhi ambapo mipango ya matumizi bora ya ardhi ya vijiji itaandaliwa na wananchi na watamilikishwa ardhi kisheria.
(c)Kupitia Kamati Maalum ya Kitaifa iliyoundwa kushughulikia migogoro ya rdhi nchini; kufika katika maeneo ya Ramsar na Pori Tengefu la Kilombero na kutekeleza majukumu yake katika kutatua migogoro kwa kuwashirikisha wananchi kama ilivyo kwa utekelezaji wa hatua zingine nilizozitaja hapo juu.
MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:-
Msitu wa Shagayu ndio wenye vyanzo vingi vya mito katika Jimbo la Mlalo, msitu huu uliungua takribani hekari 49 mwaka 2012:-
Je, ni lini Serikali itapanda miti katika eneo lililoungua ili kulinda vyanzo vya maji?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa mwaka 2012 Hifadhi ya Msitu wa Shagayu wenye ukubwa wa hekta 8,296.8 iliungua moto ambapo eneo lililoathirika, karibu na Vijiji vya Sunga, Mtae na Mpanga lina ukubwa wa jumla ya hekta 49 sawa na asilimia 0.6 ya msitu wa Shagayu kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jitihada za kurudisha uoto wa asili katika hali yake ya ustawi kama ilivyokuwa kabla ya kuungua na pengine kuwa bora zaidi, Wizara yangu imefanya yafuatayo:-
(a) Kupanda miti rafiki kwa mazingira kama vile ocotea, mibokoboko, minyasa, markamia na mipodo katika eneo la ukubwa wa hekta 11 kati ya 49 zilizoungua, ambalo liliathirika zaidi.
(b) Kuweka mazingira ya kuruhusu kukua kwa uoto wa asili kwa njia asilia katika eneo la hekta 38, njia ambayo kwa kawaida ndiyo mbinu ya kipaumble kutumika katika uboreshaji wa maeneo ya misitu ya asili yaliyoharibika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge, kuwa hali ya ulinzi katika eneo la hekta 38 zilizoachwa zikue asilia itaendelea kuimarishwa ili kuliwezesha kukua na kurudi katika ubora wake. Aidha, Mheshimiwa Mbunge, anahamasishwa kushirikiana na Serikali na wadau wengine katika kutoa elimu na kuwashawishi wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya uchomaji moto usio rafiki kwa mazingira na hivyo kuepukana na ajali na athari za moto hususan katika misitu.
MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:-
Serikali ilielekeza nguvu zake katika kutangaza vivutio vya utalii na wawekezaji kuja Kanda ya Kusini ili kupunguza msongamano wa utalii Kaskazini mwa Tanzania:-
(a) Je, ni kwa kiasi gani Serikali imeyatangaza maporomoko ya Kalambo ambayo ni ya pili Afrika baada ya yale ya Victoria kuwa kivutio cha utalii?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Hifadhi ya Msitu wa Kalambo pamoja na maporomoko haya yanakuwa chini yake kupitia Shirika lake la TANAPA?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege, Mbunge wa Kalambo, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Msitu wa Kalambo pamoja na maporomoko yake ipo chini ya Wizara yangu na inasimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kwa mujibu wa Sheria ya Misitu Na.14 ya mwaka 2002.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu kupitia Bodi ya Utalii nchini imekuwa ikitangaza utalii katika maeneo ya Kusini na Magharibi mwa Tanzania ikiwemo maporomoko ya Kalambo kupitia Jarida Maalum la kutangaza maeneo ya utalii yenye changamoto ya kimiundombinu lijulikanalo kama Hard Venture Tourism, majarida mengine ya utalii, vipeperushi, tovuti mbalimbali ikiwemo the destination portal chini ya Bodi ya Utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, TANAPA ni shirika la umma chini ya Wizara yangu lililoanzishwa chini ya Sheria ya Hifadhi za Taifa kwa madhumuni mahsusi ya kuendesha na kusimamia matumizi endelevu ya maeneo yote yaliyopitishwa kisheria na Bunge kuwa Hifadhi za Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Hifadhi ya Msitu wa Kalambo, maporomoko ya Kalambo yakiwa ni sehemu yake siyo Hifadhi ya Taifa, hivyo kusimamiwa chini ya Sheria ya Misitu. Kwa sasa Serikali itaendelea kusimamia msitu huu kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania na siyo TANAPA.
MHE. MOSHI S. KAKOSO Aliuliza:-
Vijiji vya Kabage, Kungwi, Sibwesa, Kasekese na Kaseganyama viko kwenye mgogoro mkubwa wa ardhi na WMA.
Je, ni lini Serikali itaingilia kati na kutatua mgogoro huo unaoleta usumbufu mara kwa mara?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Moshi Selemani Kakoso, Mbunge wa Mpanda Vijijini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Kanuni ya Maeneo ya Jumuiya ya Hifadhi za Wanyamapori za mwaka 2012 zinaelekeza wananchi kuanzisha maeneo hayo katika ardhi ya kijiji kwa ridhaa yao wenyewe, kwa faida yao kiuchumi na kijamii, lakini pia kwa faida za uhifadhi.
Mheshimiwa Spika, eneo linalopendekezwa kuwa WMA ya Ubende ilianza na vijiji kumi ambavyo vimeongezeka kufikia vijiji 18. Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda lilitoa baraka za kuanzishwa kwa WMA hiyo katika kikao chake cha tarehe 25 Machi, 2005.
Mheshimiwa Spika, mchakato wa kuanzishwa kwa WMA ya Ubende haukuweza kuendelea katika hatua za mbele baada ya kusajiliwa kwa Chama Wakilishi cha Jumuiya (CBO) mwaka 2006 kwa sababu mbalimbali zikiwemo ukosefu wa fedha, uvamizi wa maeneo yaliyotengwa, mabadiliko ya maeneo ya kiutawala na kutoelewana kwa baadhi ya makundi ya wananchi.
Mheshimiwa Spika, kutokana na umuhimu wa eneo hili husika kiikolojia na kiuhifadhi kwa ujumla, Wizara yangu itaharakisha kutoa ushauri, msaada wa kitaalam na kushirikiana na Halmashauri za Wilaya ya Mpanda, Manispaa ya Mpanda na Wilaya ya Nsimbo ili kufikia malengo mapana ya kuanzishwa kwa WMA ya Ubende. Aidha, Wizara yangu inaamini kwamba kuanzishwa na kuendeshwa kwa tija kwa Jumuiya ya Uhifadhi ya Ubende kutaleta mafanikio siyo tu ya kiuhifadhi lakini pia ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa vijiji husika na Taifa kwa ujumla.
MHE. PROF. NORMAN A. S. KING aliuliza:-
Hifadhi ya Kitulo ni muhimu sana kwa Taifa lakini mpaka sasa TANAPA haijaweka miundombinu ya hoteli na barabara ili kuwezesha watalii wanaokwenda Kitulo wawe na mahali pa kukaa:-
(a) Je, ni lini Serikali itawezesha ujenzi wa hoteli ya kitalii katika Tarafa ya Matamba?
(b) Je, ni lini Serikali itawezesha ujenzi wa barabara ya Chimala – Matamba – Kitulo ili kuinua utalii katika Hifadhi ya Kitulo?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Profesa Norman Adamson Sigalla, Mbunge wa Makete, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Kitulo inasimamiwa kwa kufuata mpango wa jumla (General Management Plan) wa miaka 10 ulioandaliwa mwaka 2008. Mpango huo umetoa fursa ya kujenga lodge ya vitanda 50 ndani ya hifadhi. Kulingana na taratibu za Hifadhi za Taifa, ujenzi wa huduma za malazi ya aina hiyo hufanywa na sekta binafsi. Serikali itaendelea kuweka kipaumbele katika kutangaza fursa za utalii, hivyo kuvutia uwekezaji katika ujenzi wa miundombinu ya hoteli ili kuboresha shughuli za utalii katika eneo la magharibi na kusini mwa Tanzania ikiwemo Hifadhi ya Taifa ya Kitulo.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Barabara ya Chimala – Matanda – Kitulo ni sehemu ya mipango ya Serikali ya kuendeleza na kusimamia miundombinu inayoelekea kwenye maeneo yenye fursa za kiuchumi. Wizara yangu itaendelea kushirikiana na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ili kuweka kipaumbele katika ujenzi wa barabara zinazoelekea kwenye maeneo yenye vivutio vya utalii zikiwemo za Chimala – Matamba – Kitulo ambayo ni muhimu kwa Hifadhi ya Kitulo, lakini vilevile Iringa – Tungamalenga – Ruaha mahsusi na muhimu kwa Hifadhi ya Ruaha na nyinginezo kwa kiwango cha lami ili kuchochea maendeleo ya utalii.
MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA aliuliza:-
Sheria zinatoa ridhaa kwa watu kuwinda ndani ya hifadhi:-
Je, Serikali inachukua hatua gani kutoa ridhaa kwa wananchi waishio maeneo ya hifadhi kupata ruhusa kisheria ili kuweza kuvua samaki ndani ya mabwawa kama ilivyokuwa miaka ya nyuma kwa wanakijiji waishio maeneo ya hifadhi hususan Kata za Mwaseni, Mloka na nyingine?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Omary Mchengerwa, Mbunge wa Rufiji, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 1994 wananchi wa Kata za Mwaseni, Mloka, Ngoroko na Kipungila Wilayani Rufiji waliruhusiwa kuingia ndani ya Pori la Akiba Selous na kuvua samaki. Hata hivyo, baadhi ya wanavijiji walikiuka taratibu zilizokuwa zimewekwa kwa kuingia ndani ya hifadhi bila kujiandikisha na kuvua samaki kinyume cha sheria. Aidha, baadhi yao walibainika kujihusisha na vitendo vya ujangili wa wanyamapori kama vile utoaji wa taarifa za mwenendo wa doria na uwindaji wa wanyamapori, uvuvi haramu wa kutumia sumu, ukataji miti ovyo kwa ajili ya kukaushia samaki na kutengeneza mitumbwi na uharibifu wa mazingira kutokana na uchomaji wa moto ovyo kinyume cha sheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia hali ya usalama katika maeneo ya uhifadhi ya wanyamapori, kwa sasa Wizara yangu itaendelea kutoruhusu uvuvi kufanyika ndani ya Pori la Akiba Selous. Hata hivyo, Wizara yangu inawashauri wananchi wa Kata za Mwaseni, Mloka na nyinginezo zilizo jirani kutumia mabwawa mengineyo yaliyopo nje ya pori yenye fursa kubwa ya kufanya shughuli za uvuvi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baadhi ya mabwawa hayo ni Zumbi katika Vijiji vya Nyaminywili, Kipugira na Kipo, Bwawa la Ruwe karibu na Mkongo, Bwawa la Lugongo katika Kijiji cha Mtanza na Bwawa la Zimbwini katika Mji wa Kibiti.
Mabwawa hayo na Mto Rufiji vinatoa fursa ya shughuli za uvuvi, hivyo kusaidia kuinua kipato cha wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua mahitaji ya wananchi katika maeneo haya, ya kufanya kazi na kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kijamii, Wizara yangu inaendelea kushauriana na Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji kuhusu namna ya kutekeleza mpango wa kuwajengea mabwawa ya samaki ili pamoja na mabwawa ya asili yaliyopo yawawezeshe kufanya shughuli za uvuvi endelevu.
MHE. HAWA M. CHAKOMA, aliuliza:-
Tarehe 25 Oktoba, 2016 Kituo cha Televisheni cha Mlimani TV kilirusha Kipindi cha Urithi Wetu kilichozungumzia Malikale za Taifa letu na namna ambavyo agizo la Rais wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete la ufunguzi wa nyayo za Laetoli linavyosuasua kutekelezwa kwa kisingizo cha ukosefu wa wataalam.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuajiri wataalam hao?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nyayo za Laetoli zilizogunduliwa na mtafiti Dkt. Mary Leakey mwaka 1978 katika eneo la Laetoli katika Hifadhi ya Ngorongoro ni ushahidi wa pekee duniani usiopingika kwamba binadamu wa umri wa miaka milioni 3.6 iliyopita waliweza kutembea wima kwa miguu miwili katika eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Rais wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mwaka 2007 aliagiza Wizara yangu kufukua nyayo hizo na kuzihifadhi kwa njia ya kisasa itakayoruhusu matumizi ya elimu na utalii kwa Watanzania na wageni na kwamba Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro igharamie kazi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi unakadiriwa kugharimu takribani Dola za Marekani milioni 50 sawa na shilingi za Kitanzania bilioni 105. Fedha hizo zitatumika kuwasomesha wataalam, kuandaa michoro ya ujenzi wa makumbusho, kufukua na kuhifadhi nyayo, kusimamia ujenzi na kuweka mifumo ya uhifadhi. Fedha hizo ni nyingi ukilinganisha na mapato na majukumu ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro. Hivyo Wizara yangu inaendelea na jitihada za kutafuta vyanzo vingine vya fedha ili kugharamia utekelezaji wa mradi huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni dhahiri kwamba hakuna hali ya kusuasua katika katika utekelezaji wa mradi huu muhimu na kwamba baadhi ya kazi zimekwishakamilika na nyingine ziko katika hatua mbalimbali za utekelezaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi zilizokamilika ni pamoja na kuundwa kwa Idara ya Urithi wa Utamaduni, kukamilika kwa michoro ya awali ya jengo la mapokezi, jengo la utafiti na jengo la elimu kwa umma, kuwasilishwa kwa tathmini ya athari kwa mazingira kwa mamlaka husika ikiwa ni pamoja na UNESCO kwa uchambuzi wa kina kwa lengo la kutoa idhini na mafunzo ya shahada ya uzamivu kwa watumishi wawili.
Kazi ambazo zinaendelea kutekelezwa ni pamoja na kukamilisha taratibu za ajira kwa baadhi ya wataalam wanaopatikana nchini na ukusanyaji wa takwimu sahihi kuhusu mazingira rafiki ya nyayo hizo kazi ambayo inafanywa na wataalam kutoka nje ya nchi na inatarajiwa kukamilika mwezi Februari 2017 na kwa maana hiyo, napenda kusema kwamba kazi hii imekwishakamilika kwa sababu tulikuwa tumepanga ikamilike mwezi huu, mwaka 2017.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika maeneo ya Kata mpya ya Bonyokwa Jimboni Segerea kuna msitu
unaoitwa “Msitu wa Nyuki” ambao kwa muda mrefu umekuwa kichaka cha
kujifichia majambazi; na wapo wananchi ndani ya Jimbo hilo waliokumbwa na
tatizo la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi ambao hawana
pa kwenda:-
Je, Serikali haioni kuwa ni busara kurudisha Msitu huu kwa wananchi hao
waliokumbwa na tatizo la bomoabomoa ili waweze kuweka makazi yao eneo
hilo.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Moses Kaluwa, Mbunge wa
Segerea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Kinyerezi wenye ukubwa wa hekta 4.4
ulipimwa mwaka 1997 ukiwa chini ya usimamizi wa Serikali Kuu kwa kushirikiana
na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Msitu huu ambao ndio msitu pekee uliopo
ndani ya Jiji la Dar es Salaam ukiacha misitu ya mikoko, kwa sasa unatumika
kama Ukanda wa Kijani (Green belt), hifadhi ya ardhi kwa ajili ya kuzuia
mmomonyoko wa udongo ambao unatishia kutokea katika maeneo
yanayozunguka msitu na kituo kwa ajili ya mafunzo ya elimu ya misitu na
upandaji miti.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwepo wa msitu huu ndani ya Jiji ni fursa adimu
inayoweza kuendelezwa na kutumika kama sehemu muhimu ya kutembelea
kwa utalii katika Jiji la Dar es Salaam. Serikali ina mpango kabambe wa kufanya
msitu huu kuwa forest park ili kufanya shughuli za utalii wa kiikolojia (eco-tourism)
kwa kuwa katika msitu huo pamoja na sifa nyingine kuna aina za miti zilizo
hatarini kutoweka duniani ukiwemo mpingo. Hivyo, Serikali inahamasisha uhifadhi
shirikishi kwenye rasilimali hiyo kwa manufaa ya wananchi waishio jirani na msitu
huo na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wananchi waliokumbwa na
zoezi la bomoa bomoa katika Kata za Buguruni Mnyamani, Tabata Liwiti,
Vingunguti na Kipawa wanaozunguka bonde la Mto Msimbazi na kukosa makazi,
Wizara yangu inawashauri wachukue hatua sahihi kwa kushirikiana na taasisi na
mamlaka husika za Serikali ili kupata elimu na taratibu za mipango miji
zitakazowezesha upatikanaji wa suluhisho endelevu la changamoto walizonazo
kuhusu makazi bila kuathiri dhana nzima ya uhifadhi endelevu wa misitu.
MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:-
Wakazi wanaoishi katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro wamekatazwa kulima kwenye maeneo wanayoishi kwa mujibu wa sheria hali iliyochangia wakazi wengi katika eneo hilo ambao ni wafugaji kukabiliwa na njaa pamoja na umaskini mkubwa wa kipato:-
Je, ni lini Serikali itarekebisha Sheria ya Mamlaka ya Hifadhi (Ngorongoro Conservation Area Act), 1959 Revised Edition, 2002) ili wananchi wa maeneo haya wapate maeneo kwa ajili ya shughuli zao za kilimo na ufugaji?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Saleh Mollel, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kwa mujibu wa sheria iliyoanzisha Hifadhi ya Ngorongoro, Sheria ya Kuhifadhi Eneo la Ngorongoro ya mwaka 1959 iliyopitiwa mwaka 2002 (The Ngorongoro Conservation Area Act 1959, R.E 2002) wananchi wakaazi katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro hawaruhusiwi kulima bali kufuga peke yake.
Mheshimiwa Spika, kutokana na zuio la kisheria la kulima, wakazi wa eneo la Ngorongoro ambao kwa asili yao ni wafugaji, wamekuwa wakitengewa bajeti ya kununulia mahindi ambapo takribani tani 3,600 hugawiwa bila malipo kila mwaka kwa matumizi ya chakula hususan kwa wale uwezo, mahindi hayo huuzwa kwao kwa bei pungufu ya bei ya soko.
Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na changamoto ya chakula, mnamo mwaka 2007, mamlaka ilianza mchakato wa kupata maeneo ya kilimo nje ya hifadhi kwa kutenga bajeti na kuwezesha mradi wa JEMA. Malengo mawili ya mradi wa JEMA ulioko katika Kata ya Oldonyosambu ni haya yafuatayo:-
(a) Kuwaondoa wahamiaji walioingia ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro ambao hawakuwa wakazi halali kwa kuzingatia kwamba wakazi halali ni wale waliokuwepo pamoja na uzao wao wakati eneo la Hifadhi ya Ngorongoro lilipotangazwa rasmi mwaka 1959.
(b) Kutoa fursa kwa wakazi wenyeji na halali ambao wangependa kufanya shughuli za kilimo na ufugaji nje ya hifadhi.
Mheshimiwa Spika, pamoja na mradi huu kuendelea, tathmini ya awali inaonesha upungufu kwa baadhi ya waliohamishiwa eneo la mradi kuuza maeneo waliyopewa na kurejea kinyemela ndani ya hifadhi. Kutokana na upungufu huo, Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa kushirikiana na uongozi wa Wilaya ya Ngorongoro, inaendelea kuchukua hatua ya kuzuia uuzwaji wa maeneo katika eneo la mradi.
Aidha, kwa kuwa maeneo yaliyopatikana hapo awali hayakuweza kutosheleza mahitaji, Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa kushirikiana na wadau wengine inaendelea kutafuta maeneo mengine yatakayotumika kwa kilimo.
Mheshimiwa Spika, sheria iliyoanzisha eneo la Hifadhi ya Ngorongoro ilianza kutumika zaidi ya miaka 50 iliyopita na Serikali iko kwenye maandalizi ya awali ya kufanya marekebisho yake. Ni muhimu kuzingatia kwamba, katika marekebisho hayo Serikali itaweka msisitizo zaidi katika kuboresha shughuli za uhifadhi wa eneo la Ngorongoro ili libakie katika orodha ya maeneo ya urithi wa dunia.
MHE. MUSUKUMA J. KASHEKU Aliuliza:-
Wakala wa Misitu Tanzania amehamisha vigingi vya mipaka ya misitu vilivyowekwa tangu mwaka 1974 na kuviweka katikati ya vijiji kwa kufuata ramani ya mwaka 1984, vijiji ambavyo vina GN ya Serikali na vinatambuliwa na hata Mheshimiwa Rais amezuia zoezi hilo, lakini hakuna
kilichofanyika hivyo kuwafanya wananchi wa vijiji hivyo kuishi maisha ya mashaka na sintofahamu.
Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya tatizo hilo?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII Alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Musukuma Joseph Kasheku, Mbunge wa Geita, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Msitu wa Hifadhi wa Geita wenye ukubwa wa hekta 47,700 ulisajiliwa kwa ramani namba Jb 146 ya mwaka 1952 na ulitangazwa rasmi kwa Tangazo la Serikali Namba 110. Sehemu kubwa ya msitu huu ipo kwenye miteremko ya milima ya Geita inayozunguka mji wa Geita sehemu ya Magharibi, Kaskazini na Kaskazini Mashariki.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 1984 Serikali ilifanya mapitio ya soroveya ya mipaka ya msitu kwa lengo la kuweka alama kwa kutumia ramani iliyoanzisha msitu huo. Katika mapitio hayo ilibainika kuwa mpaka halisi wa msitu kwa mujibu wa sheria umepita katikati ya vijiji vilivyoanzishwa na kusajiliwa mwaka 1974 wakati wa operation vijiji. Alama za mipaka zikawekwa kufuata mpaka huu halisi na hivyo kusababisha eneo ambalo wananchi walikuwa wameanza kuishi na kufanya shughuli za kibinadamu na baadaye kusajiliwa kuwa vijiji kuangukia ndani ya eneo la msitu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kubaini tatizo hilo Serikali haijafanya operation yoyote ya kuwaondoa wananchi katika maeneo hayo, bali ipo katika mjadala unaotafuta njia za kutatua tatizo hili bila ya kuleta athari hasi na kubwa kwa maisha ya wananchi. Aidha, Mheshimiwa Mbunge anashauriwa kuwa na subira wakati Wizara yangu kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Geita inaendelea kutafuta suluhisho la mkanganyiko uliojitokeza kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizopo.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA Aliuliza:-
Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) ni hifadhi ya kipekee hapa nchini, Afrika na dunia kwa ujumla; hifadhi hii ina vivutio vya kipekee pamoja na kuwa na matumizi mseto (multiple land use) ambapo wanyama na mifugo inachungwa pamoja; kutokana na upekee huo hifadhi hii imetambuliwa
na kuwekwa kwenye maajabu saba ya dunia chini ya Shirika la Uhifadhi Dunia (UNESCO).
Je, Serikali ina mpango gani endelevu wa kuhakikisha hadhi ya hifadhi hii inabaki kwenye ubora wake kwa ajili ya vizazi vya leo na vijavyo na pia kwa uchumi wa Taifa letu?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII Alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Magdalena Hamis Sakaya, Mbunge wa Kaliua, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa eneo la hifadhi la Ngorongoro ni muhimu na lina hadhi ya kipekee inayotokana na wingi na ubora wa vivutio vyake ambavyo vinatambulika Kitaifa na Kimataifa. Vivutio hivyo ni pamoja na matumizi mseto ya eneo, uwepo wa viumbe hai walioko hatarini
kutoweka duniani na umuhimu wa kihistoria uliothibitishwa na tafiti mbalimbali kuwa binadamu wa kwanza aliishi katika eneo hilo takriban miaka milioni 3.6 iliyopita. Aidha, kutokana na sifa hizo Shirika la Umoja wa Mataifa la UNESCO kupitia orodha yake ya maeneo ya urithi wa dunia (World Heritage Sites) imelipatia eneo hilo hadhi ya kimataifa, ambapo tangu mwaka 1979 limekuwa moja ya maeneo ya Urithi wa Dunia
kwa kigezi cha thamani ya maliasili iliyomo (The Integrity for natural value).
Mheshimiwa Spika, pamoja na sifa zilizotajwa hapo juu, kuanzia Februari, 2010 eneo hili limepewa hadhi nyingine kwa kigezo cha eneo la rasilimali mseto za maliasili, malikale na utamaduni yaani the mixed heritage value hivyo basi kwa kutambua upekee huo kwa Taifa, Serikali imejipanga kuhakikisha kuwa eneo hili linabaki katika viwango bora vya uhifadhi kwa kuchukua hatua zifuatazo:-
(a) Kudhibiti ongezeko la idadi ya watu na mifugo ndani ya eneo la hifadhi, zoezi ambalo litaanza rasmi tarehe 12 Aprili, 2017 na kukamilika mwezi Juni, 2017. Aidha, wadau mbalimbali watashirikishwa katika zoezi hili ikiwemo mamlaka za Mkoa na mamlaka ya Wilaya, Taasisi ya Taifa ya Takwimu, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa na TAMISEMI.
(b) Kuendelea kuimarisha ulinzi wa wanyamapori na maeneo yote muhimu kwa shughuli za utalii kama vile crater na kutoruhusu shughuli za kibinadamu katika maeneo hayo.
(c) Kufanya mapitio ya sheria iliyoanzisha Mamlaka ya Hifadhi na kuiboresha ili iendane na hali halisi ya sasa.
Zoezi hili liko katika hatua za awali na linatarajiwa kukamilika katika kipindi cha mwaka wa fedha 2017/2018.
MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA Aliuliza:-
Matatizo ya mipaka kati ya wanakijiji na maeneo ya hifadhi husababisha migogoro kati ya wanakijiji na watumishi wa hifadhi.
Je, Serikali inachukua hatua gani kurejesha mahusiano kati ya watumishi wa hifadhi na wananchi?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII Alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Omary Mchengerwa, Mbunge wa Rufiji, kama kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba matatizo ya mipaka kati ya vijiji na maeneo ya hifadhi mara kadhaa imesababisha migogoro kati ya wananchi na wahifadhi na wakati mwingine hata kusababisha maafa katika baadhi ya maeneo.
Wizara yangu imeendelea kuchukua hatua mballimbali katika kudumisha na kuboresha mahusiono baina ya wananchi na wahifadhi zikiwemo:-
(a) Kuendelea kutoa elimu ya uhifadhi na faida zake na kuwakumbusha wahifadhi juu ya umuhimu wa kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, kanuni na utaratibu.
(b) Kusaidia kuimarisha uwezo wa usimamizi wa maliasili katika ngazi za vijiji na Wilaya ikiwemo kuhamasisha uanzishwaji wa Jumuiya za Hifadhi za Wanyamapori (Wildlife Management Areas – WMAs) na kuimarisha zilizopo.
(c) Kuhakikisha wananchi wanaoishi katika maeneo yanayopatikana na hifadhi wanafaidika na faida zitokanazo na uhifadhi katika maeneo yao kwa mujibu wa kanuni na taratibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu itaendelea kushikiana na wadau mbalimbali katika kutekeleza sera taratibu za uhifadhi shirikishi ili kuboresha uhifadhi na kudumisha mahusiano na mashirikiano kati ya wahifadhi na wananchi.
MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:-
Tanzania ni nchi yenye misitu mingi na Sheria ya Usafirishaji wa Mazao ya Misitu inazuia kusafirisha zaidi ya sentimeta15 au inchi sita.
Je, Serikali imepata hasara kiasi gani kwa kuruhusu usafirishaji wa sentimeta 20 sawa na inchi nane ili kujenga uwezo wa kiushindani na nchi nyingine katika soko?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massarem, Mbunge wa Manyoni Magharibi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 50 cha Kanuni za Sheria ya Misitu kinakataza kusafirisha magogo nje ya nchi. Sheria hiyo pia hairuhusu kuuza nje ya nchi mbao zote zenye unene unaozidi inchi sita, uamuzi ambao azma yake kubwa ni kutoa fursa ya kukuza viwanda ndani ya nchi na kupanua wigo wa ajira kwa vijana nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kwa mujibu wa sheria, Serikali hairuhusu usafirishaji wa mbao zenye unene wa sentimeta 20 sawa na inchi nane ni dhahiri kwamba haiwezi kuwa na takwimu za hasara iliyoipata kwa kuruhusu usafirishaji wa mbao za unene huo.
MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:-
Kati ya mwaka 1954 na 1957 kulifanyika zoezi la upimaji wa maeneo ya Hifadhi za Misitu, Mapori ya Akiba na Hifadhi katika Wilaya ya Sikonge ambapo kulikuwa na wakazi takribani 16,000 na ng’ombe wapatao 2500. Kwa sasa wakazi wameongezeka hadi kufikia takribani 300,000 na ng’ombe wapo takribani 200,000 lakini eneo la kuishi, kulima na malisho ya mifugo na shughuli nyingine za kiuchumi ni lile lile la asilimia 3.7 ya eneo lote la Wilaya huku eneo la Hifadhi likibaki asilimia 96.3 na hali hii inasababisha migogoro kati ya wakulima, wafugaji na warina asali dhidi ya Maafisa Maliasili.
(a) Je, ni lini Serikali itawaongezea wakazi wa Wilaya ya Sikonge eneo la kuisha, kulima na kulishia mifugo kutoka asilimia 3.7 hadi angalau asilimia 25 ya eneo lote la Wilaya?
(b) Je, Serikali haioni kuwa kuongeza eneo la Wilaya hiyo kwa asilimia 25 kutaepusha migogoro iliyopo sasa na hivyo wananchi watatekeleza shughuli zao kwa amani na utulivu huku wakilinda mazingira pamoja na hifadhi?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph George Kakunda, Mbunge wa Sikonge, lenye sehemu (a) na
(b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kulingana na takwimu za Taasisi ya Takwimu ya Taifa (The National Bureau of Statistics) na Sensa ya mwaka 2012, Wilaya ya Sikonge ina ukubwa wa kilometa za mraba 27,873 na idadi ya watu wapatao 179,883. Aidha, maeneo ya hifadhi za misitu na wanyamapori yana ukubwa kilometa za mraba 20,056.94 sawa na asilimia 72 ya eneo lote la Wilaya, hivyo kufanya eneo la makazi na shughuli nyingine za binadamu kuwa sawa na asilimia 28.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hifadhi za misitu na mapori ya akiba katika Wilaya ya Sikonge ni muhimu kwa uhifadhi na maendeleo ya sekta nyingine, ikiwa ni pamoja na kuwa vyanzo vya mto Ugalla, ziwa Sagara, Nyamagoma na ardhi oevu ya Malagarasi - Moyowosi. Kwa mantiki hiyo, kugawa maeneo haya na kuruhusu shughuli za kibinadamu kutahatarisha upatikanaji wa rasilimali za maji kwa ajili ya shughuli za uvuvi, kilimo, ufugaji, matumizi ya nyumbani na mengineyo kwa kiasi kikubwa. Muhimu zaidi ni mchango mkubwa wa misitu hiyo katika hali ya hewa na udhibiti wa mabadiliko hasi ya tabianchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, imethibitika kwamba kilimo cha kuhama hama, ikiwa ni pamoja na utumiaji wa maeneo makubwa ya ardhi; ufugaji wa kuhama hama ukijumuisha uingizaji wa mifugo katika maeneo yaliyohifadhiwa, ni matumizi mabaya ya rasilimali ardhi na yasiyo na tija kwa Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi nitumie nafasi hii kuwakumbusha na kuwaomba wananchi kwa kushirikiana na uongozi wa Halmashauri za Wilaya husika, kuchukua hatua za makusudi kuandaa na kutekeleza mipango ya matumizi bora ya ardhi; hatua ambazo zitasaidia kuondoa changamoto za mahitaji ya ardhi katika Wilaya zote nchini ikiwa ni pamoja na Wilaya ya Sikonge iliyoko Mkoani Tabora.
MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN aliuliza:-
Kumekuwa na ongezeko kubwa sana la uwekezaji katika sekta ya utalii nchini:-
Je, Serikali imejipanga vipi ili kukabiliana na ongezeko hilo?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yussuf Salim Hussein, Mbunge wa Chambani, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba kumekuwa na ongezeko la uwekezaji katika miundombinu na mahitaji mengine yanayochangia ukuaji wa sekta ya utalii nchini; ikiwa ni pamoja na ujenzi wa hoteli za aina na madaraja mbalimbali, uimarishaji wa vyombo vya usafiri kuelekea ndani ya hifadhi na maeneo mengine yeye vivutio na uboreshaji wa vifaa mbalimbali vinavyotumika kuhudumia watalii; mambo ambayo kwa kiwango kikubwa hutekelezwa na sekta binafsi.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Serikali, pamoja na mambo mengine, ujenzi wa barabara na viwanja vya ndege uliokamilika na unaoendelea, ununuzi wa ndege mbili uliokamilika na zingine nne zinazotarajiwa kuja nchini katika siku za karibuni, zote ni jitihada zinazochangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa sekta ya utalii nchini. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, mafanikio haya yamewezesha kuongezeka kwa idadi ya watalii ambapo mwaka 2016 idadi hiyo iliongezeka kutoka jumla ya watalii 1,137,182 wa mwaka 2015 hadi jumla ya watalii 1,284,279 kwa mwaka 2016. Hii ikiwa sawa na ongezeko la asilimia 12.9 na ongezeko linaloendelea kuonekana katika hifadhi moja kwa moja ikiwa ni pamoja na eneo la Hifadhi la Ngorongoro na Hifadhi za Taifa zinazosimamiwa na TANAPA.
Mheshimiwa Spika, ili kufanya ongezeko hilo liwe na tija na endelevu Wizara yangu imejikita katika kusimamia ubora wa huduma na utoaji huduma, kutangaza zaidi vivutio hususan vivutio vipya na kusambaza shughuli za utalii nchi nzima hususan Ukanda wa Kusini (The Southern Circuit) ili kutimiza azma ya Serikali kwa mujibu wa Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano wa Mwaka 2016/2017 – 2020/ 2021 unaoainisha utanuaji wa uwigo wa mazao ya utalii (diversification of tourism products) kama mojawapo ya hatua muhimu za kuchukua (key interventions) katika kukuza utalii nchini.
Mheshimiwa Spika, Wizara yangu inatoa wito wa sekta binafsi kuongeza mbinu, bidii na mitaji kuunga mkono jitihada za Serikali katika kukuza utalii na uchumi wa Taifa kwa ujumla.
MHE. JOSEPH M. MKUNDI alijibu:-
Kisiwa cha Ukerewe kina vivutio vingi vya utalii vinavyoweza kuiingizia nchi yetu pesa nyingi za kigeni vikiwemo mapango ya Handebezyo, Makazi ya Mtemi Rukumbuzya, Jiwe linalocheza la Nyaburebeka huko Ukara na kadhalika.
Je, Serikali ina mpango gani wa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kuimarisha na kujenga mazingira na kuvitumia vivutio hivyo ili kuongeza pato la Taifa na wananchi wa Ukerewe?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Sura ya Nne aya ya 4.2.7 ya Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2016/2017 - 2020/2021) unasisitiza pamoja na mambo mengine upanuzi wa wigo wa vivutio vya utalii na utalii utokanao na vivutio vya urithi wa utamaduni (The heritage tourism)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu kwa kuzihusisha Halmashauri husika inakamilisha orodha ya vivutio vyote vya utalii ikiwa ni pamoja na vivutio vya malikale nchini ili kuweka utaratibu wa kuvisajili, kuviboresha na hatimaye kuvitangaza na kuviuza kwa watalii wa ndani na wa nje. Zoezi hili linatengemea kukamilika mwaka wa 2017/2018. Vivutio vya mapango ya Handebezyo, Makazi ya Mtemi Rukumbuzya na Jiwe linalocheza la Nyaburebeka vilivyoko katika kisiwa cha Ukara katika Halmashauri ya Ukerewe ni miongoni mwa vivutio hivyo.
MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:-
Mkomazi Game Reserve (sasa Hifadhi ya Taifa Mkomazi) ilianzishwa kabla ya Uhuru wakati tukiwa na idadi ndogo ya watu na mifugo.
Je, Serikali haioni kwamba sasa ni wakati muafaka wa kusogeza mipaka ya Hifadhi ya Taifa Mkomazi ili wananchi wa Kata za Visiwani, Mji Mdogo wa Same na Vumari wapate maeneo ya kuishi, kilimo na ufugaji?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Taifa Mkomazi imetokana na kupandishwa hadhi kwa Pori la Akiba la Mkomazi – Umba kupitia Tangazo la Serikali Namba 27 la mwaka 2008. Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi ilirithi mipaka ya lililokuwa Pori la Akiba la Mkomazi – Umba mipaka ambayo ilitambulika kisheria kwa mujibu wa Tangazo la Serikali Namba 275 la mwaka 1974.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi ni sehemu muhimu ya mfumo wa kiikolojia na toshelezi kwa idadi ya wanyamapori waliopo hifadhini kujipatia mahitaji yao ikiwemo malisho, maji na maeneo ya mazalia hivyo kufanya hatua za kupunguzwa kwa eneo kusababisha athari hasi ikiwemo baadhi ya wanyamapori kutoka nje ya hifadhi kwa ajili ya kujitafutia mahitaji yao muhimu na hatimaye kusababaisha kuongezeka kwa migogoro kati ya binadamu na wanyama pori.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Wanyamapori Namba 5 ya mwaka 2009 hairuhusu kufanyika kwa shughuli za kibinadamu ndani ya hifadhi ikiwepo kilimo, ufugaji na uchimbaji madini. Hivyo, kutokana na sababu hizi za msingi za kiuhifadhi, kwa sasa Serikali haioni haja ya kusogeza mipaka ya hifadhi ya Taifa ya Mkomazi, isipokuwa kwamba Serikali itaendelea kupokea kutoka kwa wananchi na wadau wengine maoni yatakayozingatia matakwa ya sheria na taaluma ya uhifadhi. (Makofi)
MHE. ZUBERI M.KUCHAUKA (K.n.y. MHE. VEDASTO E. NGOMBALE) aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuitangaza Wilaya ya Kilwa kuwa ni moja ya maeneo makubwa ya Kiutalii katika Kanda ya Kusini kwa kuzingatia historia yake, maajabu mbalimbali yaliyopo, fukwe, mapango, malikale, mbuga, mabwawa na utamaduni wake?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Vedasto Edger Ngombale, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana na hoja ya Mheshimiwa Mbunge kuwa Wilaya ya Kilwa ni miongoni mwa maeneo yenye fursa za uendelezaji utalii wa kihistoria na kiutamaduni yakiwemo magofu ya malikale yaliyopo eneo la Kilwa Kisiwani na Songo Mnara ambayo ni maeneo yaliyopo kwenye orodha ya urithi wa dunia pamoja na vivutio vingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuitangaza Wilaya ya Kilwa kuwa eneo muhimu la kiutalii Ukanda wa Kusini, Wizara imeandaa jarida la Karibu Kilwa (Kilwa District Heritage Resources); vipeperushi kama Welcome to Kilwa in Tanzania; ambavyo vinaonyesha picha na maelezo ya vivutio vya utalii vilivyopo Wilayani Kilwa na kuanzisha Kituo cha Taarifa za Kiutalii (Tourist Information Centre).
Mheshimiwa Naibu Spika, Jarida na vipeperushi hivi vinatolewa kwa wageni wanaotembelea Kilwa pamoja na kutumika kutangaza utalii wa Kilwa katika maonesho ya ndani, hususan maonyesho ya Saba Saba; Nane Nane na Maonyesho ya nje ya nchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Wizara kupitia Bodi ya Utalii na kwa kushirikiana na taasisi ya nchini Ufaransa imeweza kuandaa filamu maalumu ambayo inaitangaza Kilwa. Filamu hiyo ilizinduliwa rasmi mwaka 2016 na imetafsiriwa kwa lugha tatu za Kimataifa ambazo ni Kiswahili, Kiingereza na Kifaransa. Filamu hiyo inapatikana kupitia mtandao, kwenye tovuti ya Bodi ya Utalii na kwenye wavuti ya YouTube.
MHE. RITTA E. KABATI aliuliza:-
Zao la mbao linachangia pato la Taifa katika nchi yetu na zao hili linazalishwa kwa wingi katika Wilaya ya Mufindi katika Mkoa wa Iringa:- Je, zao hili linaingiza fedha kiasi gani kwa mwaka.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ritta Enespher Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba mbao ni miongoni mwa mazao yanayochangia pato la Taifa na pia kutoa ajira kwa wananchi. Zao hili linazalishwa kwa wingi katika Wilaya ya Mufindi kutoka katika shamba la miti la Serikali la Sao Hill. Aidha, kiasi cha fedha kinachopatikana kwa mwaka hutegemea kiasi cha meta za ujazo kilichopangwa kuvunwa ambacho nacho kutegemeana na kiasi kinachoruhusiwa kitaalam kuvunwa kwa mwaka kulingana na mpango wa uvunaji wa kila shamba (annual allowable cut).
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na mdororo wa uchumi mwanzoni mwa miaka ya 1980, Serikali ilibinafsisha viwanda vyake vikiwemo viwanda vya bidhaa za misitu. Serikali ilibakia na jukumu la kuhifadhi misitu pamoja na kukuza miti katika mashamba yake. Hivyo, Serikali huuza miti iliyosimama kwa wawekezaji binafsi ambao huvuna na kuchakata magogo kwa ajili ya mbao, karatasi, nguzo na mazao mengine; shughuli za uchakataji zinabaki kuwa jukumu la sekta binafsi. Kwa kuwa Serikali haihusiki moja kwa moja na uchakataji, takwimu halisi zilizopo wizarani ni za ujazo wa miti inayouzwa kwa wadau mbalimbali na kiasi cha fedha kilichopatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka 2015/2016, jumla ya meta za ujazo wa miti zipatazo 767,946.46 zilivunwa kutoka kwenye mashamba ya Serikali na kuiingizia Serikali jumla ya Sh.58,312,894,416.20. Aidha, kwa mwaka 2016/2017, mashamba ya Serikali yalivunwa na kuuza miti yenye meta za ujazo 754,931 kwa viwanda vya kuzalisha mbao na kuipatia Serikali fedha zipatazo Sh.55,102,043,000.00 ikiwa ni mrabaha na tozo, ushuru wa Halmashauri za Wilaya (CESS) na kodi ya ongezeko la thamani (VAT).
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa misitu ya asili, mapato yanayotokana na zao la mbao, ni wastani wa shilingi bilioni 18.3 kwa mwaka.
MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN (K.n.y. MHE. RAISA ABDALLAH MUSSA) aliuliza:-
Kutokana na umuhimu wa misitu hapa nchini na kwa kuzingatia kuwa theluthi moja ya ardhi ya Tanzania ni misitu; na kwa kuwa, Serikali ina Chuo kimoja tu cha Misitu cha Olmotonyi ambacho sasa kinakaribia kufikisha karne moja tangu kianzishwe:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha vyuo vingine vitakavyotoa taaluma zaidi ya misitu kwa Watanzania?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Raisa Abdallah Mussa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania Bara ina eneo la takribani hekta milioni 48 za misitu sawa na 55% ya eneo lote la nchi kavu lipatalo hekta milioni 88.1. Kwa mujibu wa viwango vinavyoratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, inakadiriwa kuwa Afisa Misitu mmoja husimamia wastani wa hekta 5,000 za misitu hivyo, kwa ukubwa wa eneo la misitu katika nchi yetu kiasi cha wataalam wa misitu 9,600 wenye jukumu la kusimamia misitu moja kwa moja ukiondoa watawala na watumishi wa viwandani na kadhalika wanahitajika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina vyuo vitatu vinavyotoa taaluma ya misitu. Vyuo hivyo ni pamoja na Chuo Kikuu cha Sokoine kilichoko Morogoro ambacho kinatoa Shahada ya Kwanza, Shahada ya Uzamili na Shahada ya Uzamivu katika Fani ya Misitu; Chuo cha Viwanda vya Misitu kilichopo Moshi, ambacho kinatoa Astashahada ya Teknolojia ya Viwanda vya Misitu na Astashahada ya Teknolojia ya Viwanda vya Misitu na Chuo cha Misitu kilichopo Olmotonyi, ambacho kinazungumziwa na Mheshimiwa Mbunge muuliza swali, nacho kinatoa mafunzo ya Astashahada na Stashahada ya Misitu.
Mheshimiwa Naibu Spika, bila kujali vyuo walivyosoma, taaluma mahsusi ya misitu na ngazi za shahada walizohitimu, katika kipindi cha miaka 10 vyuo nilivyovitaja hapo juu vimeweza kuzalisha jumla ya wataalam 3,500 ambao wameingia kwenye soko la ajira. Kufikia mwaka 2020, Serikali inao mpango wa kuongeza udahili, mara mbili ya viwango vya sasa, katika vyuo vilivyopo kwa kutekeleza, pamoja na mambo mengine, uboreshaji miundombinu ya kufundishia, kuongeza ubora na idadi ya wakufunzi na vifaa vya kufundishia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, mipango ya Serikali inaonesha uwezekano mkubwa wa kufikiwa kwa malengo ya kupatikana kwa wataalam wa kutosha kwa idadi na uweledi, kwa sasa Serikali haioni umuhimu wa kuongeza vyuo vingine kwa madhumuni hayo.
MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:-
Mkoa wa Katavi ni miongoni mwa mikoa ambayo ina vivutio vingi vya utalii kama vile Mbuga ya Katavi yenye wanyama wengi, kivutio cha pekee cha twiga weupe ambao hawapatikani mahali pengine popote duniani:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kukitangaza kivutio hiki pekee cha utalii?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Katavi ni miongoni mwa mikoa yenye vivutio vingi vya utalii, vikiwemo Mbuga ya Wanyama ya Katavi, Mti wa Mzimu wa Katavi pamoja na vivutio vingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu kupitia Bodi ya Utalii Tanzania na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania, imekuwa ikitangaza vivutio vya utalii vya Katavi kwa ujumla wake kupitia mitandao na tovuti mbalimbali za kijamii. Aidha, Majarida ya Utalii ya TANAPA na TTB yanayotolewa kwa lugha za Kiswahili, Kingereza, Kidachi, Kichina, Kifaransa na Kirusi ni sehemu ya njia zitumikazo katika kutangaza utalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, baadhi ya Majarida hayo ni Selling Tanzania na Explore Tanzania yatolewayo na TTB na TANAPA Today na Hifadhi za Taifa Tanzania au Tanzania National Parks yanayotolewa na TANAPA. Aidha, TANAPA hutangaza pia utalii kupitia kipindi maalum kiitwacho Hifadhi za Jamii za Taifa kilichorushwa na Kituo cha Luninga cha Taifa (TBC). Kipindi hiki hurushwa kila wiki na kupitia kipindi hiki vivutio vinavyopatikana Hifadhi ya Taifa ya Katavi, kikiwemo kivutio pekee cha twiga weupe hutangazwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kukamilika kwa ukarabati mkubwa wa Uwanja wa Ndege wa Mpanda kulikofuatiwa na ujio wa Ndege za Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) kutasaidia sana kuongezeka kwa idadi ya watalii ambao watatembelea maeneo mbalimbali Mkoani Rukwa, ikiwemo Hifadhi ya Katavi. TTB na ATCL wanakamilisha matayarisho ya kuanzisha safari maalum za siku za mwisho za juma na siku za sikukuu kwa lengo la kuhamasisha na kuwawezesha Watanzania wengi zaidi kutembelea vivutio vya utalii vilivyoko Katavi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu kupitia Bodi ya Utalii, Shirika la Hifadhi za Taifa la TANAPA na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro itaendelea kuboresha mbinu zilizopo na kubuni mbinu mpya, ili kuimarisha utangazaji wa vivutio vya utalii na hatimaye kuvutia watalii wengi zaidi katika sekta ya utalii nchini.
MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa Pori Tengefu la Loliondo uliodumu zaidi ya miaka 25?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALI: alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Catherine Valentine Magige, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, mwezi Desemba, 2016 Mheshimiwa Waziri Mkuu alipofanya ziara katika Wilaya ya Ngorongoro pamoja na mambo mengine, alitoa maelekezo ya jinsi ya kupata ufumbuzi wa mgogoro wa matumizi ya ardhi katika Pori Tengefu Loliondo ambao unahusisha wananchi, wawekezaji na wahifadhi. Katika utekelezaji wa agizo hilo, Kamati Maalum Shirikishi inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha iliundwa ili kupata mapendekezo ya namna ya kutatua mgogoro huo. Kamati hiyo maalum ilifanya kazi yake kwa njia mbalimbali zikiwemo kufanya vikao na wadau mbalimbali, kutembelea eneo lenye mgogoro ili kujua hali halisi na kuandaa taarifa yenye mapendekezo ya jinsi ya kutatua mgogoro husika. Mapendekezo ya Kamati hiyo yamewasilishwa kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa hatua zaidi.
MHE. MBARAKA K. DAU (K.n.y- MHE. HAWA M. CHAKOMA) aliuliza:-
Kisiwa cha Mafia kina vivutio vingi vya utalii kama viumbe wanaoishi kwenye maji, mikoko na kadhalika lakini vivutio hivyo havijatangazwa vya kutosha:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa kutangaza utalii wa Kisiwa cha Mafia?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Chakoma Mchafu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kwa muda mrefu sasa Wizara kupitia Bodi ya Utalii, Shirika la Hifadhi za Taifa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imekuwa ikielekeza juhudi zaidi katika kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania kupitia tovuti, mitandao ya kijamii, Ofisi za Ubalozi, kuteua Mabalozi wa hiari kwa ajili ya kuitangaza Tanzania, kutumia Watanzania waishio nchi za nje yaani (diaspora), kuendesha mafunzo ya utalii kwa njia ya mtandao kwa mawakala wa utalii na kuandaa majarida, vipeperushi, CDs na DVDs.
Mheshimiwa Spika, aidha, jitihada zaidi zimewekwa katika matangazo kupitia redio, magazeti, runinga, mabango kwenye maeneo ya mipaka na vituo vya mabasi, kudhamini matukio mbalimbali ya ndani na nje ya nchi, kuwa na wawakilishi wa kutangaza utalii kwenye masoko ya utalii pamoja na kutumia watu mashuhuri.
Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kuboresha utangazaji wa vivutio vya utalii Wizara imeanzisha mkakati wa kutangaza kwa pamoja kati ya Bodi ya Utalii na Taasisi nyingine ikishirikisha Sekta Binafsi. Mkakati huo umeonekana kuwa na tija na unasaidia kutangaza vivutio vya utalii nchini ikiwemo Kisiwa cha Mafia na hivyo kuitangaza Tanzania kwa ujumla na kwa gharama nafuu.
Mheshimiwa Spika, kuhusu kutangaza Kisiwa cha Mafia pamoja na matangazo yaliyoainishwa hapo juu, Bodi ya Utalii iliingia mkataba na kampuni ya kutengeneza filamu nchini ijulikanayo kama Aerial Tanzania kutengeneza filamu maalum ya Kisiwa cha Mafia ambayo ilizinduliwa mwezi Machi, 2017. Filamu hii itachangia kuongezeka kwa idadi ya watalii wanaotembelea Kisiwa cha Mafia sambamba na kuongezeka kwa shughuli mbalimbali za utalii katika kisiwa hicho.
Mheshimiwa Spika, utangazaji wa vivutio vya utalii Kisiwani Mafia unaojumuisha viumbe vinavyoishi majini kama Papa Potwe na aina nyingine za samaki adimu wa aina mbalimbali ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa maendeleo wa Taifa wa miaka mitano, ule wa mwaka wa 2016/2017 - 2020/2021 unaosisitiza juu ya utangazaji wa vivutio na uibuaji wa vivutio vipya vya utalii katika maeneo mbalimbali nchini.
MHE. JOSEPH R. SELASINI aliuliza:-
Kumekuwa na usumbufu na uharibifu unaosababishwa na ongezeko la nyani ambao wanavamia mashamba ya wananchi na kula mazao kama mahindi, ndizi na sasa wanaingia katika majumba ya watu na kubeba chakula katika Kata za Ushiiri, Mrao – Keryo, Kirua – Kei, Katangera – Mrere, Kirongo – Samanga na Olele.
(a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapunguza au kuwahamisha nyani kwenye maeneo hayo?
(b) Je, kuna utaratibu gani wa kuwafidia wananchi hasara waliyoipata kutokana na uharibifu wa nyani hao?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Roman Selasini, Mbunge wa Rombo, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maliasili na Utalii inatambua uwepo wa tatizo la wanyamapori wasumbufu na waharibifu ambao wanaharibu mazao katika kata zilizotajwa ambazo zinapakana na Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro. Wizara kupitia Taasisi yake ya TAWIRI imepanga kuendesha zoezi la utafiti wa wanyamapori aina ya nyani, ngedere na kima katika kipindi cha mwezi Oktoba hadi Disemba 2017 ili kubaini idadi na mienendo yao na kuwianisha na shughuli za kilimo zinazofanyiwa na wananchi katika maeneo ya vijiji vya kata zilizotajwa. Kwa sasa Wizara imeandaa utaratibu wa kushirikisha jamii husika katika kulinda mazao yao kwa kutumia mbinu mbalimbali za kitaalam na za kijadi, hatua ambayo itatekelezwa kuanzia mwezi Oktoba 2017 kwa Wizara kuwashauri wananchi kuanzisha vikundi, kuendesha mafunzo na kuwapatia silaha za jadi.
Mheshimiwa Spika, kuhusu kufidia hasara, kwa sasa Serikali haina utaratibu wa kufidia mazao yaliyoharibiwa au kuliwa na wanyamapori na badala yake Kanuni za Dangerous Animals Damage Consolation za mwaka 2011 chini ya Sheria ya Wanyamapori ya mwaka 2009 zinaelekeza ulipaji wa kifuta jasho. Hata hivyo, katika kanuni hizo, jamii ya nyani siyo miongoni mwa wanyama wanaotambulika kisheria katika ulipaji wa kifuta jasho. (Makofi)
MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA aliuliza:-
Msitu wa Hifadhi ya Taifa Minziro una vivutio vingi vya utalii.
(a) Je, ni watalii wangapi wametembelea msitu huo ndani ya kipindi cha miaka 20 hadi sasa?
(b) Je, wananchi wanaoishi karibu na msitu huo wananufaikaje?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Balozi Dkt. Diodorus Buberwa Kamala, Mbunge wa Nkenge, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kabla ya mwaka 2015, Msitu wa Hifadhi wa Minziro haukuwa miongoni mwa maeneo yaliyohifadhiwa na kusimamiwa kwa ajili ya shughuli za utalii. Hata hivyo, kwa sasa hifadhi hiyo ipo katika hatua za awali za maandalizi ya mpango endelevu wa kuendesha utalii wa ikolojia katika msitu huo.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2015 Serikali ilianzisha mradi wa kuboresha uhifadhi wa bionuwai katika hifadhi 12 za misitu ya mazingira asilia zilizopo nchini. Hifadhi hizo zikiwa ni pamoja na Mlima Rungwe kule Mbeya, Udzungwa na Kilombero zinazopakana na Iringa na Morogoro, Uluguru na Mkingu zinazopakana na Morogoro, Amani, Nilo na Magamba zilizopo ndani ya Mkoa wa Tanga, Chome kule Kilimanjaro, Rondo – Lindi na Mlima Hanang Mkoa wa Manyara, chini ya mradi unaofadhiliwa na Mfuko wa Mazingira na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP). Aidha, kutokana na kuwepo kwa mipango ya awali ya kuanzisha utalii wa ikolojia katika hifadhi hiyo, katika kipindi cha mwaka 2014 hadi 2015 jumla ya watalii 11 walitembelea hifadhi hiyo ambapo tisa ni raia wa kigeni na wawili ni Watanzania.
Mheshimiwa Spika, wananchi wanaoishi jirani na Msitu wa Minziro kwa kutunza, kuhifadhi na kulinda msitu huu kwa sasa wananufaika kwa kupata vyanzo bora vya maji, hali ya hewa iliyo bora na ardhi yenye rutuba na sifa nyinginezo muhimu kwa kilimo na maisha ya wananchi kwa ujumla. Aidha, katika siku zijazo baada ya kukamilika kwa mpango unaoandaliwa na Wakala wa Huduma za Misitu, wananchi hao watanufaika kwa kupata gawio la asilimia 26 ya mapato yatakayotokana na utalii wa ikolojia ambao hufanyika kwa njia shirikishi na wananchi katika kusimamia hifadhi na kuendesha utalii huo.
MHE. DKT. HADJI H. MPONDA (K.n.y. MHE. GOODLUCK A. MLINGA) aliuliza:-
Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano aliahidi kuwapatia wananchi wa Kata za Lupiro, Iragua, Milola na Minepa eneo la ardhi oevu ya Bonde la Mto Kilombero kwa ajili ya makazi na kilimo pindi tu atakapoingia madarakani. Je, utekelezaji wa ahadi hiyo imefikia wapi?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Goodluck Asaph Mlinga, Mbunge wa Jimbo la Ulanga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliahidi kumaliza matatizo ya ardhi katika maeneo mbalimbali nchini yakiwemo maeneo ya kata nne zilizotajwa ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi, Ibara ya 22(e). Hata hivyo, utaratibu wa kushughulikia ahadi hiyo katika kata hizo haukutajwa kuwa ni kwa kumega sehemu ya ardhi oevu katika Bonde la Mto Kilombero. Napenda kutumia fursa hii kumfahamisha Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari kazi ya kushughulikia tatizo hili la ukosefu wa ardhi kwa wananchi wa kata hizo limeanza kupitia Mradi wa KILORWEMP, Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA) na kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Serikali ya Mkoa wa Morogoro pamoja na Wilaya za Malinyi, Kilombero na Ulanga.
Mheshimiwa Spika, kazi hii inafanyika kwa umakini mkubwa ili kuepuka kukiuka misingi na dhana nzima ya uhifadhi, kwanza kwa kuzingatia vigezo na umuhimu wa ardhi oevu na pili kwa kuhakiki mipaka halali ya vijiji yaani village approved survey plans. Aidha, kupitia Land Tenure Support Program unaotekelezwa chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, mipango ya matumizi bora ya ardhi ya vijiji inaandaliwa hadi hatua ya kutoa hati miliki za kimila kwa vijiji vyote vinavyozunguka Bonde la Mto Kilombero.
Mheshimiwa Spika, suala hili pia linafanyiwa kazi sambamba na maombi ya wananchi kupitia wawakilishi wao wakiwemo Waheshimiwa Wabunge na Madiwani ambayo yamekuwa yakipelekwa katika ngazi mbalimbali likiwemo Bunge lako Tukufu. Kazi hii ni shirikishi, wananchi wa kata na vijiji katika Wilaya husika wanashirikishwa kikamilifu hadi kufikia maridhiano ya pamoja. Kwa mfano, katika Kijiji cha Igawa, Kata ya Igawa, Wilaya ya Malinyi, baada ya kufikia maridhiano na kwa kuzingatia vigezo vya pande zote, eneo la kijiji liliongezeka kutoka kilometa za mraba 39.8 hadi 86.97 ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 118.5. Eneo la Kijiji cha Sofi Majiji liliongezeka kutoka kilometa za mraba 93.9 hadi ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 16.1. Kuongezeka au kupungua kwa eneo kunatokana na vigezo vilivyowekwa ingawa hadi sasa hakuna kijiji kilichopoteza eneo.
MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatengeneza miundombinu ya maji katika Hifadhi ya Mkomazi ili kuzuia wanyamapori kuzurura kwenye makazi ya wananchi wakitafuta maji na kuharibu mazao yao?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Same Mashariki, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi inapatikana katika nyanda kame na hivyo kukabiliwa na uhaba wa maji kwa ajili ya matumizi ya wanyamapori. Wizara imefanya juhudi za kuchimba mabwawa kwa ajili ya kuhifadhi maji ambapo hadi sasa kuna jumla ya mabwawa tisa ambayo ni Mabata, Kuranze, Zange, Ndindira, Nobanda, Ngurunga, Mbula, Kavateta na Maore. Hata hivyo, kutokana na mabadiliko ya tabianchi ni mabwawa matatu tu yanahifadhi maji mwaka mzima.
Mheshimiwa Spika, kutokana na changamoto hiyo ya upungufu wa maji, Serikali inaendelea kuchimba mabwawa sita ili kukidhi mahitaji ambapo bwawa moja lilikamilika katika mwaka wa fedha wa 2016/2017 na mengine matano yatachimbwa katika mwaka huu wa fedha 2017/2018.
Aidha, katika mwaka 2017/2018 kisima kirefu kimoja kitachimbwa kwa ajili ya kusukuma maji na kujaza mabwawa yanayokauka ili kukidhi mahitaji ya maji wakati wa kiangazi kikali na wakati huo huo doria za kudhibiti wanyamapori wasitoke nje ya hifadhi zinaendelea kuimarishwa.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza:-
Kati ya mwezi Juni – Desemba, 2015 wananchi wapatao sita walishambuliwa na kuuawa na wanyamapori na Shirika la Hifadhi Tanzania (TANAPA) halikushiriki mazishi ya watu hawa, wala hakuna fidia yoyote waliyopata ndugu wa marehemu, hali inayoonesha mahusiano mabaya kati ya jamii na Mamlaka ya Hifadhi, zaidi ya hayo wanyama kama tembo, wamesababisha hasara kubwa sana kwa kuharibu mazao katika Tarafa ya Daudi, Kata za Marangwa, Daudi, Bargish na Gehandu.
• Je, ni lini Serikali itawalipa fidia ndugu wa hao watu sita waliouawa na wanyama wakali katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu?
• Je, ni lini Serikali kupitia TANAPA italipa fidia kwa wale wote walioharibiwa mazao shambani mwaka 2014/ 2015?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaya, Mbunge wa Mbulu Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali hailipi fidia kwa madhara yanayosababishwa na wanyamapori hatari au waharibifu, badala yake inatoa kifuta jasho au kifuta machozi, kwa mujibu wa kifungu cha 68(1) cha Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009. Aidha, kifungu cha (3) cha Kanuni za Malipo ya Kifuta Jasho na Kifuta Machozi za mwaka 2001 kinaainisha masharti na viwango vya malipo ya kifuta jasho na kifuta machozi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu imepokea madai ya wananchi watano waliouawa, wanne walijeruhiwa na 31 walioharibiwa mazao yao katika eneo ambalo Mheshimiwa Mbunge analizungumzia. Madai hayo yamefanyiwa kazi kwa mujibu wa kanuni na yatalipwa mara fedha zitakapopatikana.
MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:-
Mkomazi Game Reserve (sasa Hifadhi ya Taifa Mkomazi) ilianzishwa kabla ya Uhuru wakati tukiwa na idadi ndogo ya watu na mifugo.
Je, Serikali haioni kwamba sasa ni wakati muafaka wa kusogeza mipaka ya Hifadhi ya Taifa Mkomazi ili wananchi wa Kata za Visiwani, Mji Mdogo wa Same na Vumari wapate maeneo ya kuishi, kilimo na ufugaji?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Taifa Mkomazi imetokana na kupandishwa hadhi kwa Pori la Akiba la Mkomazi – Umba kupitia Tangazo la Serikali Namba 27 la mwaka 2008. Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi ilirithi mipaka ya lililokuwa Pori la Akiba la Mkomazi – Umba mipaka ambayo ilitambulika kisheria kwa mujibu wa Tangazo la Serikali Namba 275 la mwaka 1974.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi ni sehemu muhimu ya mfumo wa kiikolojia na toshelezi kwa idadi ya wanyamapori waliopo hifadhini kujipatia mahitaji yao ikiwemo malisho, maji na maeneo ya mazalia hivyo kufanya hatua za kupunguzwa kwa eneo kusababisha athari hasi ikiwemo baadhi ya wanyamapori kutoka nje ya hifadhi kwa ajili ya kujitafutia mahitaji yao muhimu na hatimaye kusababaisha kuongezeka kwa migogoro kati ya binadamu na wanyama pori.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Wanyamapori Namba 5 ya mwaka 2009 hairuhusu kufanyika kwa shughuli za kibinadamu ndani ya hifadhi ikiwepo kilimo, ufugaji na uchimbaji madini. Hivyo, kutokana na sababu hizi za msingi za kiuhifadhi, kwa sasa Serikali haioni haja ya kusogeza mipaka ya hifadhi ya Taifa ya Mkomazi, isipokuwa kwamba Serikali itaendelea kupokea kutoka kwa wananchi na wadau wengine maoni yatakayozingatia matakwa ya sheria na taaluma ya uhifadhi. (Makofi)
MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI aliuliza:-
Kwa kuwa Serikali kupitia Idara ya Misitu ina jukumu la kutathmini rasilimali zake ikiwemo miti:-
• Je, Wizara inatekeleza kwa kiwango gani katika kufanya tathmini za idara zake kuangalia athari za magonjwa ya miti?
• Je, nchi inazo ekari ngapi za mioto ya asili na iliyopandwa?
• Je, hadi sasa ni ekari ngapi za miti zimekatwa kwa ajili ya mbao na mkaa?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Immaculate Sware Semesi, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a), (b) na (c), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sheria ya Misitu Namba 14 ya Mwaka 2002, shughuli zote za utafiti za kitaalam kuhusiana na magonjwa ya miti na athari zake hutekelezwa na Taasisi ya Utafiti wa Misitu (TAFORI) chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Taasisi hii hufanya utafiti wa utambuzi wa aina ya magonjwa, ukubwa wa matatizo na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukua kutegemeana na uzito wa matokeo ya utafiti husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa ya Tathmini ya Rasilimali Misitu (NAFORMA) iliyotolewa mwaka 2015 inaonesha kuwa nchi yetu ina misitu yenye hekta milioni 48.1 ambapo misitu ya asili ni hekta 47.528, sawa na asilimia 98.8 na misitu ya kupandwa ni hekta 572,000, sawa na asilimia tu.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kasi ya uharibifu wa misitu ni kubwa sana bila kujali aina ya uharibifu wa misitu ambapo kiasi cha ekari 372,000 za misitu huangamizwa kila mwaka nchini. Aidha, takwimu zinaonesha kwamba ili kurejesha hali ya misitu nchini katika viwango vyake vya kawaida, kiasi cha jumla ya ekari 185,000, sawa na jumla ya miti milioni 230 kinahitajika kupandwa kila mwaka kwa kipindi cha miaka 17.
MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:-
Sehemu kubwa ya Misitu ya Hifadhi ndani ya Wilaya ya Same ni Msitu wa Shengena ambao ni chanzo cha Mito mikubwa ya Nakombo, Hingilili, Yongoma na Saseni ambayo maji yake yanatumiwa na wakazi wa Majimbo ya Same Mashariki, Mlalo na Korogwe Vijijini:-
• Je, ni lini Serikali itaanzisha doria kulinda Msitu wa Shengena kuzuia uharibifu unaoendelea ikiwemo uchomaji moto ambao pia unaathiri maisha ya watu?
• Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha utaratibu wa uvunaji wa miti iliyokomaa katika Msitu wa Shengena na kuweka mkakati wa kuotesha miti mingine ili msitu uwe endelevu?
• Je, Serikali inasema nini juu ya athari za kimazingira zinazotokana na uchimbaji wa madini ya Bauxite unaoendelea katika Msitu wa Shengena?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Same Mashariki, lenye sehemu (a), (b) na (c), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kupitia Wakala wa Huduma za Misitu kwa kushirikiana na Mamlaka ya Serikali ya Wilaya ya Same imekuwa ikitekeleza shughuli za doria na operations za mara kwa mara katika hifadhi za misitu ambapo wahalifu wanaopatikana na hatia ikiwa ni pamoja na uchomaji moto huchukuliwa hatua za kisheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, kwa kuwa uharibifu wa misitu unahusisha baadhi ya wananchi wasiozingatia Sheria, Serikali inakamilisha mpango wa usimamizi shirikishi na wananchi wa vijiji vyote 23 alivyovitaja vinavyopakana na hifadhi ya Chome ushiriki ambao utaboresha ulinzi wa hifadhi.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, uhifadhi wa misitu ya mazingira asilia pamoja na mambo mengine unazingatia kutokuvuna miti hata baada ya kukomaa na pia kuacha miti ya asili iendelee kuota yenyewe badala ya kupanda miti mingine ili kulinda hifadhi na kuendeleza mfumo wa kiikolojia na bioanuwai zilizopo ndani ya hifadhi. Aidha, hatua hii inalenga kutunza, kuhifadhi na kuendeleza mfumo wa ikolojia ikiwa ni pamoja na vyombo vya maji na viumbe hai waliopo.
(c) Mheshimiwa Mwenyekiti, uchimbaji wa madini katika maeneo ya hifadhi husimamiwa na sheria zikiwemo Sheria za Madini ya mwaka 2010, Sheria ya Misitu namba 14 ya mwaka 2002 na Sheria ya Usimamizi wa Mazingira (NEMA) ya mwaka 2004.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa hakuna taarifa rasmi zinazohusu uchimbaji wa madini ya Bauxite katika Hifadhi ya Msitu wa Shengena. Aidha, iwapo mtu yoyote binafsi au taasisi itahitaji kufanya shughuli za uchimbaji madini ndani ya hifadhi hiyo, atatakiwa kufuata taratibu za kisheria zitakazozingatia masuala yote muhimu ikiwemo kufanyika kwa tathmini ya athari ya mazingira kabla ya kuanza kwa uchimbaji huo.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA (K.n.y. MHE. VEDASTO E. NGOMBALE) aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuitangaza Wilaya ya Kilwa kuwa ni moja ya maeneo makubwa ya Kiutalii katika Kanda ya Kusini kwa kuzingatia historia yake, maajabu mbalimbali yaliyopo, fukwe, mapango, malikale, mbuga, mabwawa na utamaduni wake?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Vedasto Edger Ngombale, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana na hoja ya Mheshimiwa Mbunge kuwa Wilaya ya Kilwa ni miongoni mwa maeneo yenye fursa za uendelezaji utalii wa kihistoria na kiutamaduni yakiwemo magofu ya malikale yaliyopo eneo la Kilwa Kisiwani na Songo Mnara ambayo ni maeneo yaliyopo kwenye orodha ya urithi wa dunia pamoja na vivutio vingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuitangaza Wilaya ya Kilwa kuwa eneo muhimu la kiutalii Ukanda wa Kusini, Wizara imeandaa jarida la Karibu Kilwa (Kilwa District Heritage Resources); vipeperushi kama Welcome to Kilwa in Tanzania; ambavyo vinaonyesha picha na maelezo ya vivutio vya utalii vilivyopo Wilayani Kilwa na kuanzisha Kituo cha Taarifa za Kiutalii (Tourist Information Centre).
Mheshimiwa Naibu Spika, Jarida na vipeperushi hivi vinatolewa kwa wageni wanaotembelea Kilwa pamoja na kutumika kutangaza utalii wa Kilwa katika maonesho ya
ndani, hususan maonyesho ya Saba Saba; Nane Nane na Maonyesho ya nje ya nchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Wizara kupitia Bodi ya Utalii na kwa kushirikiana na taasisi ya nchini Ufaransa imeweza kuandaa filamu maalumu ambayo inaitangaza Kilwa. Filamu hiyo ilizinduliwa rasmi mwaka 2016 na imetafsiriwa kwa lugha tatu za Kimataifa ambazo ni Kiswahili, Kiingereza na Kifaransa. Filamu hiyo inapatikana kupitia mtandao, kwenye tovuti ya Bodi ya Utalii na kwenye wavuti ya YouTube.
MHE. HAMIDU H. BOBALI aliuliza:-
Kumekuwa na Maswali yaliyokosa majibu stahiki kila mara kuhusu suala la mabaki ya mjusi (Dinosaur) yaliyopo Ujerumani, kila linapoulizwa au kuchangiwa hapa Bungeni:-
(a) Je, ni nini kauli ya mwisho ya Serikali kuhusu faida ambayo wananchi wa Mkoa wa Lindi na Tanzania kwa ujumla watanufaika kutokana na mabaki hayo?
(b) Je, kwa nini Serikali isishauriane na Serikali ya Ujerumani kuboresha barabara na huduma za maji katika Kijiji cha Manyangara katika Kitongoji cha Namapwiya, ambapo mabaki ya mjusi huyo yalichukuliwa?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamidu Hassan Bobali, Mbunge wa Mchinga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, maswali kuhusu mijusi mikubwa (Dinosaria) iliyochimbuliwa katika Kilima cha Tendaguru, Mkoani Lindi, nchini Tanzania kati ya mwaka 1909 hadi mwaka 1913 na kupelekwa katika Makumbusho ya Elimu Viumbe ya Berlin, nchini Ujerumani, yamejibiwa kwa miaka mingi na wakati tofauti Bungeni ambapo Serikali imekuwa ikitoa ufafanuzi uliokidhi haja katika mazingira yaliyokuwepo wakati maswali hayo yanajibiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika siku za hivi karibuni Wizara yangu imefuatilia suala hili kwa umakini mkubwa kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kujiridhisha kama ifuatavyo:-
(a) Wazo la kuwarudisha dinosaria nchini halina tija kutokana na changamoto za kiteknolojia na gharama, ikilinganishwa na faida za kuchukua hatua hiyo.
(b) Tanzania iendelee kusisitiza kupata manufaa kutokana na uwepo wa dinosaria wake huko Berlin, Ujerumani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kufuatia majadiliano bya kina yaliyohusisha pia wataalam waliobobea katika masuala ya malikale kutoka pande zote mbili, imekubalika kama ifuatavyo:-
i. Serikali ya Ujerumani itendesha shughuli za utafiti zaidi huko Tendaguru na katika maeneo jirani, ili kuwezesha uchimbuaji wa mabaki ya dinosaurian wengine yanayoaminika kuwepo katika maeneo hayo.
ii. Serikali ya Ujerumani itawezesha kuanzishwa kwa kituo cha makumbusho, ili shughuli za utalii zifanyike katika eneo hilo na kuvutia watalii kutoka nchini na nje ya nchi.
iii. Serikali ya Ujerumani itafadhili zoezi la uimarishaji idara inayohusika na malikale katika Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam na kuwezesha upatikanaji wa watalaam wa kutosha wa fani husika, ili kuendeleza utalii wa malikale nchini. Hivyo, uboreshaji wa barabara na miradi ya maji anaouzungumzia Mheshimiwa Mbunge utakuwa sehemu ya mafanikio ya shughuli za utalii katika eneo linalozungumziwa.