Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Magdalena Hamis Sakaya (63 total)

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpango wa mwelekeo wa bajeti uliowasilishwa na Waziri wa Fedha na Uchumi alisema Serikali inataka Tanzania kuwa nchi ya viwanda, kuelekea uchumi wa kati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwenye hotuba hii imesema itawavutia wawekezaji waje kujenga viwanda hapa nchini, kwa mwendo wa kusubiri wawekezaji waje wajenge viwanda hatuwezi kwenda na kufikia malengo ya Taifa tuliojiwekea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muda wa miaka 10 sasa kila hotuba ya Viwanda na Biashara inaeleza kuwaita wawekezaji wa kujenga viwanda, ni kwa kiasi gani tumefanikiwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeeleza Mkoa wa Tabora kunajengwa kiwanda cha Tumbaku ili kutoa ajira kwa vijana na ku-process tumbaku ambapo asilimia 60 ya tumbaku inalimwa Tabora. Tuelezwe ni mipango gani ya awali iliyofanywa ili kufanikisha azima hii ya Serikali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo Makaa ya Mawe kwa wingi sana kule Namtumbo-Songea. Kuna Malori zaidi ya 80 hadi 100 yanabeba makaa yale kila siku na kupeleka Kenya na kwingineko. Serikali itueleze, makaa hayo yanapelekwa huko kwa utaratibu gani, tunanufaikaje na makaa hayo ili kutuongezea nishati na kuokoa misitu yetu inayoteketea kwa uchomaji wa mkaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tabora tuna misitu na mbao zenye thamani kubwa. Mbao zile zinasafirishwa kwenda nje na Mikoa mingine kutengeneza Furniture (Samani). Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha tunapata kiwanda cha mbao Mkoa wa Tabora ili vijana wa Tabora wapate ajira na mbao ya Tabora iweze kuwa na thamani zaidi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu imekuwa ni dampo la bidhaa ambazo hazina viwango kwa kila kitu, vifaa vya umeme, nguo, viatu, vifaa vya ujenzi na kadhalika. Kwa nini Serikali imeshindwa kuweka sheria za bidhaa hapa nchini? TBS wameshindwa kabisa kudhibiti bidhaa duni hapa nchini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mpango gani wa kuhakikisha bidhaa feki, duni na dhaifu haziingii hapa nchini? Sheria ya Uwekezaji inamtaka mtu anayekuja hapa nchini kuwekeza anatakiwa kuwa na mtaji wa kuwekeza na kutoa ajira kwa wazawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itueleze, Wachina na Wahindi wanaozagaa Kariakoo na maeneo mengine wakiuza maua, karanga, mitumba na kadhalika wanaruhusiwa na nani? Serikali imeruhusu ajira za wananchi wake zichukuliwe na watu wa nje ambao wanaitwa wawekezaji, tunakwenda wapi? Ni lini Serikali itahakikisha biashara ndogondogo zote hapa nchini zinafanywa na wazawa na hivyo kuwaondoa Wachina wote waliopo Soko la Kariakoo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda vilivyobinafsishwa wawekezaji wamebadilisha matumizi na kufanya magodauni, vingine havijalipiwa fedha ya kununuliwa na vingine vimeng‟olewa mashine zote zilizokuwepo. Serikali inasema nini kuhusu viwanda hivi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ihakikishe mazao yote yanachakatwa ndani ya nchi na hivyo kuongeza thamani tofauti na sasa ambapo mazao mengi yanasafirishwa ghafi na hivyo kukosesha mapato mengi Taifa na kupoteza ajira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itaacha kuagiza samani za maofisini kutoka China na hivyo kununua samani ndani ya nchi kutokana na mbao ya Tanzania. Hii ni aibu kubwa!
Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge ni chombo cha uwakilishi. Ndani ya Bunge hili kila Mtanzania anawakilishwa kwa Mbunge waliyemchagua wao wenyewe. Wananchi wana haki Kikatiba kuona live nini wawakilishi wao wanakifanya na nini kinaendelea ndani ya chombo hiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu zote zilizotolewa na Mheshimiwa Waziri kuhusu kuzuia matangazo ya Bunge Live hazina mashiko hata moja.
Mheshimiwa Waziri akiwa Mwanza alipohojiwa sababu hasa alisema Bunge la Kumi 2010 – 2015 lilifanya maamuzi hayo jambo ambalo ni uongo wa mchana kweupe. Sisi tuliokuwepo wakati huo hatukuwahi kujadili suala hilo wala kutoa maamuzi ya kipuuzi kama hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali leo ieleze Watanzania sababu hasa ya kuzuia matangazo ya Bunge live kwa Watanzania. Kitendo cha TBC kurudia matangazo ya Bunge usiku kuanzia saa 4.30 usiku baada ya kuchuja na kuondoa wasiyotaka yaonekane wakati ambapo watu wamechoka na kazi za kutafuta kipato mchana kutwa na wanatakiwa kupumzika ili wapate nguvu ya kufanya kazi siku inayofuata, ni manyanyaso kwa Watanzania, ni matumizi mabaya ya kodi zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vipaji vya michezo hujengwa kuanzia primary school, secondary school ndipo tunaweza kupata wanamichezo wazuri wenye weledi na wanaoweza kujiajiri kwenye michezo na kuleta heshima kwa Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha za michezo zinazotolewa kwa shule zetu kwa watoto wetu huko shuleni ni kidogo sana; hakuna vifaa vya michezo, hawapati mazoezi ya kutosha na walimu wa michezo hawawezeshwi. Serikali imejipanga vipi kuhakikisha michezo shuleni inawezeshwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, watoto wanacheza wakiwa shuleni na hata wakiwa majumbani kwao. Viwanja vya michezo kwenye mitaa mingi maeneo mbalimbali hapa nchini yamevamiwa na kujengwa nyumba na shughuli nyingine. Watoto wanacheza barabarani na kila leo wanagongwa na magari, pikipiki na vyombo vingine vya usafiri. Serikali ina mpango gani mahususi kuhalalisha inafanya uhakiki wa viwanja vya watoto wetu vilivyoporwa, kuvamiwa ilimradi kutumiwa na watoto kwa malengo ya michezo na kukuza vipaji vya watoto wetu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilipiga marufuku kuwatumia watoto wadogo kwenye maigizo na kutengeneza mikanda ya sanaa za maigizo. Tumeendelea kuona watoto wadogo wakitumika kwenye maigizo na hivyo kuathiriwa kisaikolojia na kushindwa kufikia ndoto zao. Watoto wenye ndogo za kuwa madaktari wanapoingizwa kwenye maigizo wakati akili zao hazijaweza kuamka, automatically tunawahamisha mwelekeo wa ndoto zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ieleze Bunge, kwa nini watoto bado wanaendelea kushirikishwa kwenye maigizo? Umri wa mtoto unajulikana ni miaka 18 kushuka chini.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia kidogo kwenye hotuba iliyoko mbele yetu na kwa sababu ya muda nienda straight kwenye hoja zangu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu tumekuwa tunatumia fedha nyingi sana kwa ajili ya kujenga miundombinu ya barabara, nyingine za nchi na nyingi pia za jasho la walipa kodi. Kwa bahati mbaya sana barabara hizi zimekuwa zikichukua muda mfupi sana kwa sababu kwanza viwango vya ujenzi ni dhaifu, utunzaji wake ni dhaifu lakini pia tunatumia makandarasi ambao baadhi yao hawana viwango vya kuweza kujenga barabara kwa uhakika. Badala ya kutengeneza barabara angalau tumalize miaka kumi ili tuhame kutoka eneo moja twende eneo lingine tunarudi mle mle huku maeneo mengine hayana barabara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Wabunge wanazungumzia juu ya kubandua barabara za lami kujenga nyingine wakati mikoa mingine wako kwenye udongo. Miaka 54 ya uhuru tunabandua lami na kurudisha lami pale pale wakati wengine wako kwenye udongo hawajui ni lini watapata barabara za lami. Kwa hiyo, tatizo kubwa ni kwamba hatusimamii vizuri barabara zetu. Ifike mahali tuwe na standards za ujenzi wa barabara nchi nzima. Tuamue kwamba mkandarasi ambaye anashindwa kukidhi vigezo vya matengenezo tunayoyataka asipate kandarasi. Kwa sababu ya kubeba wakandarasi mtu anaharibu huku anapelekwa kule, matokeo yake tunaingiza hasara kubwa kwa Taifa hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ukienda kwenye barabara nyingi, niseme kabisa barabara zilizotengenzewa ndani ya miaka kumi ya uongozi wa Awamu ya Nne zote ziko kwenye hali mbaya. Nyingi zina mashimo mengi, nyingi zina migongo, nyingi zinaanza kuchimbika kuanzia pembeni, Awamu ya Nne barabara zote zimeharibika. Pamoja na kuwa anasifika kwamba alitengeneza barabara nyingi lakini kaziangalieni, nimefanya utafiti barabara nyingi za uongozi wa Kikwete ziko kwenye hali mbaya kwa sababu usimamizi ulikuwa mbovu. Hatuwezi kuwa na barabara za lami za kutosha kama tunashindwa kuweka standards kwa ajili ya barabara zetu za lami. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine, tumekuwa tunatoa fedha kidogo kidogo kwenye ujenzi wa barabara matokeo yake tunaweka vyombo vya ujenzi barabarani kwa muda mrefu na tunalipa wakandarasi waelekezi kwa muda mrefu, tunapoza fedha nyingi sana za walipa kodi kwa kitu ambacho hakitakiwi. Tunapotengeneza barabara miaka minne, mitano haijakamilika lakini vyombo vinalipiwa, mkandarasi mwelekezi analipwa, how much are we wasting? Ni pesa nyingi sana tunapoteza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuwe na utaratibu, tunapopanga kutengeneza barabara tuitengee muda, ndani ya mwaka mmoja, miwili ikamilike ili tuokoe fedha na faini tunazolipa kwa ajili ya kuweka vyombo barabarani wakati huo hatutoi fedha kwa ajili ya kutengeneza barabara zile. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la reli. Suala hili ni uchumi wa Taifa. Ni jambo la ajabu kwa nchi inayotegemea kilimo kwa zaidi ya asilimia 80, leo tuna reli kwanza sio za standards, zinabomoka kila siku, lakini kwa kiwango kidogo, ni aibu mpaka leo. Sambamba na kwenda kwenye uchumi wa viwanda, sambamba na kwenda kwenye uchumi wa kati, suala la reli halikwepeki. Kwa hiyo, katika mawazo yote ya Serikali ili tuweze kwenda pamoja lazima suala la reli lipewe kipaumbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kwanza nilianza kuumizwa na Waziri wa Fedha. Kwanza alikuja na mpango wa kwanza kwamba lazima tutengeneze reli ya kati kwa standard gauge, tulipokwenda Dar es Salaam kwenye semina anasema kwamba tunatafuta wabia na nchi ambazo tuna-share matumizi ya reli hiyo, hatuwezi kutegemea watu wa nchi nyingine, pengine kwao reli si priority lakini ndani ya nchi yetu reli ni priority. Kwa hiyo, ni lazima tujipange sisi wenyewe kuhakikisha kwamba tunajenga reli zetu? Leo tunategemea Burundi, Burundi kwake pengine reli si priority, au Rwanda, it is not their priority, au Kenya, sisi kama sisi tunafanyaje?
Kwa hiyo, suala la reli ya kati na matawi yake ina-cover karibu mikoa 15 ya nchi hii. Wengi wamezungumza kwa msisitizo tunaomba wakati wa ku-wind up kesho tuambiwe tarehe ya kuanza na kumaliza kujengwa reli ya kati na kwa standard gauge, halikwepeki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la upungufu wa mabehewa. Kuna shida kubwa ya upungufu wa mabehewa ya abiria. Reli yote hii ya kati mabehewa ni machache sana matokeo yake imeleta matatizo makubwa. Leo Wabunge walikuwa wanazungumzia suala la bei kwenda juu pamoja na kuwepo kwa walanguzi, shida kubwa ni mabehewa machache. Leo ndani ya Wilaya ya Kaliua kwenye stop station ya Kaliua kwa siku moja, kwanza treni ni siku mbili tu kwa wiki, lakini hiyo siku mbili eti siku kumi, can you imagine? Watu kumi kwenye kituo kwa wiki mara mbili! Reli iko kwenye wilaya yao, wengi hali ya uchumi ni mbaya, hawana uwezo wa kutumia 50,000, 60,000 kwa basi angalau reli ndicho chombo chao wanaambiwa siti kumi. Matokeo yake watu ambao si wasafiri na wanakwenda na vitambulisho wananunua wanakwenda kuziuza mitaani kwa wale wasafiri. Matokeo yake mtu badala ya kununua tiketi shilingi 23,000 ananunua shilingi 40,000 na huwezi kuzuia kwa sababu mabehewa ni machache. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesoma hotuba ya Waziri, amesema ameongeza mabehewa, lakini mengi ni ya mizigo, mabehewa ya mizigo kutoka 530 mpaka 704, lakini suala la mabehewa ya abiria ni shida kubwa. Pia tuongeze angalau route. Kwa kweli ni jambo la ajabu kuambiwa kwamba Wilaya ya Kaliua reli yote ya kati kituo kimoja, kwa wiki moja wasafiri watu 20, kwa kweli inasikitisha sana. Hatuwezi kukwepa suala la kuendelea kulanguliwa kwa tiketi kama hatuongezi mabehewa lakini pia kama hatuongezi angalau routes za treni tuweze kusaidia wananchi ambao treni pia ni tegemeo lao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyeki, suala lingine ni la mafao ya watumishi wa iliyokuwa TRC waliohamia RITES. Mwaka 2007 walipohama kutoka TRC kwenda TRL waliambiwa watalipwa mafao yao leo ni karibu miaka kumi hawajawahi kulipwa. Tunaomba Waziri wakati ana-wind up atuambie wale watumishi waliohamishwa kutoka TRC kwenda TRL mwaka 2007 mpaka leo hawajalipwa haki zao wanalipwa lini haki zao? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye barabara za Tabora. Mkoa wa Tabora mpaka tunapoongea umeunganishwa na mkoa mmoja tu, Mkoa wa Singida. Mwanza moja kwa moja mpaka Tabora bado, Mbeya bado, Shinyanya bado, Kigoma bado. Tunaomba sana, kuna barabara hii ya Nyahuwa – Chanya, ni kipande kidogo tu pale, kilometa 85.4 imetengewa fedha kidogo. Ni yale yale ninayoyasema, tukitenga fedha kidogo kidogo tunaleta gharama zaidi. Hebu tuhakikishe kwamba tunaweka fedha za kutosha barabara hii ikamilike ili angalau tuunganishe Dodoma na Tabora. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini barabara nyingine ni barabara ya Urambo - Kaliua. Ni barabara muhimu kweli kweli, imetengewa shilingi bilioni tano tu, sasa hizi ni za uchambuzi au za kufanya nini? Barabara ile ni fupi, kilometa 28, tunaomba Mheshimiwa Waziri aweke fedha ya kutosha angalau ikamilike. Leo ukienda pale una mimba changa inatoka, barabara hali ni mbaya sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara nyingine ni ya Kazilambwa - Chagu. Tunashukuru angalau kwa kipande kidogo imekamilika, kutoka Kazilambwa kuja Kaliua tayari, Kazilaumbwa kwenda Chagu kwa maana ya kuunganisha Tabora na Kigoma bado. Fedha iliyowekwa ni kidogo sana labda ni kwa ajili ya uchambuzi, sijui. Naomba barabara hii na yenyewe iweze kutekelezwa ndani ya bajeti hii ili angalau tuunganishe Mkoa wa Tabora na Kigoma. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara nyingine ni ya kuunganisha kutoka Mpanda – Ugala – Kaliua, Ulyankhulu – Kahama. Ni barabara muhimu sana kwa uchumi wa Kaliua, Mpanda na Kahama. Barabara hii imewekewa fedha kidogo ya uchambuzi, tunaomba kwa bajeti ya mwaka wa kesho ihakikishe inajengwa kwa lami, ni barabara nzuri sana kwa ajili ya uchumi wa nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye suala la viwanja vya ndege. Kiwanja cha Tabora ni matatizo, leo ni mwaka wa nne tangu kimetengewa fedha ya ukarabati, hakikamiliki kwa nini? Nashangaa Wabunge wanaosema kwamba ndege ni anasa, ndege siyo anasa, tunataka uchumi wa kati, tunataka wawekezaji. Leo unamtoa Mchina kutoka Dar es Salaam aingie kwenye makorongo afike Tabora saa ngapi? Angetaka apande ndege straight afike Tabora aangalie eneo la kuwekeza, arudi kwenye shughuli zake. Kwa hiyo, viwanja vya ndege ni uchumi wa nchi hii. Tunaomba Mheshimiwa Waziri akija atuambie kiwanja cha Tabora lini kitakamilika kwa gauge kubwa, kipanuliwe kiweze kuwa kiwanja ambacho kinaingiza ndege kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwanja kile ndege kubwa haziingii. Ndege ndogo, nauli kutoka Dar es Salaam mpaka Tabora ni shilingi 450, 000 nani mwenye uwezo huo? Gharama ni kubwa, wananchi wengi hawawezi. Kuna Mbunge kasema hapa tukiweza kuwa na viwanja vikubwa, ndege nyingi zikatua, zenye upana mkubwa hata gharama zinapungua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nichangie kidogo kuhusiana FastJet, Wabunge wanasema kwamba FastJet ni rahisi, FastJet ni gharama kuliko maelezo, ni aibu. Kwanza mimi niseme FastJet ni wezi, ni wezi kabisa. Leo unachangishwa begi shilingi 200, 000, maji nusu lita shilingi 3,000 hii ni aibu, ni wizi wa hali ya juu. Anakwenda kuchukua maji kwa jumla jumla shilingi 300 kwa nusu lita anakuja kuuza shilingi 3,000 huu ni wizi, hakuna gharama ya unafuu wa aina yoyote.
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Magdalena.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ninakushukuru kunipa nafasi niweze kuchangia hotuba ya Wizara ambayo iko mbele yetu. Kwa sababu ya muda nichangie moja kwa moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa miaka zaidi ya 15 sasa tumekuwa tunashuhudia tunajadili hapa Bungeni suala la makaa ya mawe, tangia sijawa Mbunge alikuwepo Profesa alikuwa anaitwa Profesa Mwalyosi ndani ya Bunge hili, kila akisimama ndani ya Bunge nilikuwa nasikia anazungumzia Mchuchuma, Liganga, makaa ya mawe miaka iliyopita, alikuwa ni Profesa wa mimea na mazingira. Leo nimeingia ndani ya Bunge miaka 10 tunazungumza makaa ya mawe, ni kwa nini tunashindwa kutumia makaa ya mawe kwa ajili ya nishati ya matumizi ya nyumbani? Tunaomba Mheshimiwa Waziri akija atueleze kuna tatizo gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi hii inaenda kuwa jangwa, hatuna means, kwa sababu umeme haushikiki, hata Mheshimiwa Waziri hawezi kupikia umeme. Mafuta ya taa hayashikiki, gesi haishikiki, tunachemshia vitu vidogovidogo tu, asilimia 80 tunatumia mkaa, nchi inakuwa jangwa. Kama kwa mwezi mmoja Dar es salaam peke yake wanatumia magunia 200,000 kwa takwimu za Waziri can u imagine nchi nzima tunatumia gunia ngapi kwa mwezi mmoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tusipoangalia tunaenda kuwa jangwa, lakini tunashangaa tumepewa makaa ya mawe ndani ya nchi yetu, kuna tatizo gani Mheshimiwa Waziri, tunaomba kesho utujibu hapa, kwa nini hatuoni umuhimu wa kutumia rasilimali hii tuliyopewa ndani ya nchi yetu tutoe nishati kwa ajili ya kuitumia, naomba sana Mheshimwa Waziri atuambie. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ilikwenda Likuyu - Namtumbo mwaka juzi, nilikaa pale Namtumbo karibu siku tatu, jambo la kushangaza niliona malori zaidi ya 100 kila siku yanabeba makaa ya mawe, kwanza napenda kujua yanapelekwa wapi cha kwanza, Mheshimiwa Waziri uniambie, yale makaa ya mawe, yanayotoka Namtumbo, malori 100 kila siku yanapelekwa wapi, kwa sababu kwa takwimu ambazo nilijaribu kuuliza wananchi pale wanasema wanakwenda Uganda nan mengine yanakwenda Kenya. Nikawa nashangaa kama malori 100 yanabeba makaa ya mawe kutoka Namtumbo, rasilimali ya nchi yetu, leo tunaendelea kuteketeza misitu yetu, are we serious?
Naomba uje utuambie yanakwenda wapi, na wale wananchi pale wananufaikaje na sisi kama Tanzania tunanufaikaje. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la Wizara ya Madini na Nishati kutoa leseni za kutafuta madini kwenye maeneo ya hifadhi…
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nilindie muda wangu, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwepo na utaratibu ambao kunakosekana coordination kati ya Wizara ya Madini na Nishati na Wizara ya Maliasili. Wizara ya Nishati na Madini inatoa leseni za utafutaji wa madini ndani ya maeneo ya hifadhi, kwa hiyo imeleta migogoro mingi sana. Kuna baadhi ya maeneo ya hifadhi ambayo mpaka sasa hivi kuna migogoro mikubwa sana mojawapo ni Hifadhi ya Manyara. Wamepewa leseni ndani ya hifadhi, hakuna coordination matokeo yake leo kuna migogoro ambayo haiishi. Kwa hiyo, tungependa wakati Wizara inatoa leseni za kutafuta madini kuwepo na coordination kati ya Wizara hizi mbili ili kuondoa migogoro ambayo inatokea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine nimeangalia kitabu cha Mheshimiwa Waziri, tuna madini ya Uranium ambayo tunachimba maeneo mengi sana ya Tanzania, napenda kujua haya madini ya Uranium maeneo gani yameanza kuchimbwa, maeneo gani yanafanya kazi, maeneo gani na tunanufaikaje na madini hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, nilitembelea Mgodi ule wa Uranium kule Likuyu Namtumbo, tuliona jinsi ambapo kuna Uranium nyingi iko nje, tulitembea pale wanaita yellow cake, iko peupe ni ya kukusanya. Kwanza ningependa kujua ule mgodi umeshaanza kufanya kazi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, tunanufaikaje kama Watanzania na lingine wananchi wa eneo lile wananufaikaje na ule mgodi kama umeshaanza kufanya kazi. Maana naona kimya, nilikuwa nategemea angalau tuone huku kwenye kitabu cha hotuba ya Waziri, sioni chochote ambacho kimeandikwa huku.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la REA, kiukweli kwenye sula la REA kwa kiasi fulani limesaidia sana umeme kusambaa, lakini bado changamoto zake ni kubwa sana. Suala la REA kila Mtanzania anashiriki kwa fedha ya REA, hata bibi wa kule kijijini kabisa akinunua lita moja ya mafuta ya taa tayari kasaidia mchango wa REA kuendelea kuwepo kwa kukatwa shilingi 150. Jambo la kushangaza kwa nini fedha zile hazielekezwi zote maeneo yaliyopangiwa?
Mheshimiwa Waziri hebu kesho utuambie, zile fedha ambazo hazikutumika kwa hii miaka mitatu hazikupelekwa kwenye REA zimeelekezwa wapi na ni kwa sababu gani? Kwa sababu kupanga ni kuamua, kama tumeamua kutengeneza mradi wa kusaidia umeme vijijini, tumeamua kama Watanzania, tunawakata kwenye mafuta, kwanye diesel, petrol, na kwenye mafuta ya taa. Tuwe na nidhamu basi ya matumizi ya hizi hela.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli kama Wabunge wengine walivyosema, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri alikuja kwenye Jimbo langu la Kaliua, namshukuru Mheshimiwa Waziri, kiukweli alikuta hali ni mbaya. Wakati anakuja katika Jimbo la Kaliua tulikuwa na asilimia moja tu ya usambazaji wa umeme wa REA katika Wilaya nzima mpaka alishtuka.
Nashukuru baada ya kuwepo kwake alisukuma watendaji wake angalau shughuli zimeanza kwenda lakini Mheshimiwa Waziri uliagiza tarehe 30 mwezi wa nne, umeme wa awamu ya kwanza na ya pili uwake, mpaka leo ni kijiji kimoja tu kinawaka umeme, hivyo, bado tunayo changamoto nyingi sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, REA inahitaji ufuatiliaji wa hali ya juu, siyo suala kwamba watendaji wa TANESCO wanawaachia wale makandarasi hapana. Nimeona mfano mmoja Kaliua, Mameneja walikuwa wamekaa ofisini hawafanyi kazi, walivyonyanyuka kutoka ofisini kuwafuata makandarasi leo kazi inafanyika.
Kwa hiyo, watu wa TANESCO watoke maofisini waende kwa makandarasi wahakikishe kwamba wanawasimamia, makandarasi wale wanapoachiwa peke yao wanafanya wanavyotaka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ukiangalia nguzo zinazopelekwa kwenye maeneo ya vijiji ni chache sana, wanasambaza barabarani mwa kijiji au makao makuu ya kijiji, vitongoji vyote hakuna umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo la Serikali na Watanzania ni kila Mtanzania anayetaka kutumia umeme atumie umeme, siyo maeneo ya barabarani, ni lazima pia umeme uende mpaka maeneo ya vijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni migodi mikubwa ya dhahabu kutolipa Kodi ya Mapato. Leo nimesikia kauli ya ajabu, eti wanasema watu wa migodi wamekuwa wanapata hasara endelevu. Sijawahi kusikia hasara endelevu. Hakuna mfanyabiashara yeyote duniani, hata kama ni mama ntilie akubali kupata hasara endelevu. Kama wanapata hasara endelevu, kwa nini waendelee kuwepo? Kama wanapata hasara endelevu, kwa nini waendelee ku-run? Wanakuwaje na watumishi? Wanakuwaje na kila kitu? Hapa ni wizi mtupu. Tunataka migodi yote ilipe kodi. Tumekuwa tunayabeba sana makampuni. Leo kama Tanzania hatunufaiki sana na migodi yetu ya madini kwa sababu wanabebwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hotuba ya Mwenyekiti wa Kamati, wametuambia kwamba kuna makampuni yanayodaiwa shilingi bilioni kadhaa. Makampuni ambayo hayakulipa Kodi ya Zuio yanadaiwa shilingi bilioni 89 lakini kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri anasema Acacia wamelipa almost karibu shilingi bilioni 13. Sasa hebu tujue, Mheshimiwa Waziri utuambie, kwanza haya makampuni mengine ambayo hayakulipa, umesema kuna makampuni matatu hapa ambayo hayakulipa, wamelipa tu Acacia kidogo, yale mengine tunayafanyaje, ikiwepo Mantra na hao wengine Tanzania One?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini hawakulipa na ni kwa sababu gani? Kwa nini Mheshimiwa Waziri hajatueleza kwenye kitabu chake kwamba wanafanywaje? Kwa sababu ametuambia tu wamelipa Acacia kiasi kidogo. Kwanza Acacia hawajamaliza, tunataka walipe kodi yetu yote, lakini yale ambayo hawajalipa, tunawafanyaje? Mheshimiwa Waziri, tuache kuwabeba, wanatunyonya, hii rasilimali ni yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni la wachimbaji wadogo wadogo. Kwenye Jimbo langu ninayo machimbo ya madini ya dhahabu kwenye eneo la Ulyankulu, machimbo ya Silambu. Tulikubaliana hapa Bungeni Serikali iwezeshe wachimbaji wadogo wadogo, kuwapatia maeneo lakini pia wapatiwe mitaji, pamoja na vitendea kazi. Bado halitekelezwi kama tulivyokuwa tumekubaliana, bado wana hali ngumu ya utendaji wao wa kazi, bado wanahangaika hapa pale, wamekuwa ni watu wa kufanyia kazi kama za utumwa, wanatumika tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa tunaomba sana, Serikali inajua na Mheshimiwa Waziri anajua, anawajua wote wako wapi na vitalu vyao, hebu wekeni utaratibu wa kuwawezesha, waweze kunufaika na ile kazi yao wanayoifanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine, ndani ya Wilaya yangu ya Kaliua, Kata ya Igwisi, Kijiji cha Twende Pamoja, kuna machimbo ya madini ya mawe, yanachimbwa na kampuni ya CHICO. Kampuni ya CHICO imechimba pale karibu miaka mitatu wanatengeneza kokoto, hawajawahi kulipa chochote kwenye kata ile wala kwenye kijiji kile, lakini kikubwa kuliko yote, kuna nyumba zaidi ya 25 hazijalipwa, baruti zinapasuliwa usiku na mchana, wananchi wale wengine wanateseka, wengine wanazimia, hawajaweza kuhamishwa, lakini wapo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilipofuatilia kwa CHICO anasema, sisi tuna-deal na watu wa madini. Sasa Mheshimiwa Waziri utusaidie, pale kampuni inapopewa mlima, pale ni mlima wamesambaratisha mlima wote umekwisha, wananchi wanateseka. Hakuna hata coin moja ambayo wamewahi kulipa. Tunaomba Mheshimiwa Waziri ukija kujibu utuambie, wale kampuni ya CHICO ambao mmewapa mlima wa pale Twende Pamoja, Igwisi, wamechimba miaka mitatu, wanatengeneza kokoto, kwa nini hawalipi ushuru unaotakiwa kwa kijiji husika na kwa Halmashauri? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ni kwa nini mpaka leo hawalipi watu haki zao? Wawaondoe pale. Nilishawahi kukuta mwanamke amezimia pale, mpaka kijiji kwa huruma, wakamhamisha wakampeleka sehemu nyingine. Wananchi wa kawaida, lakini Serikali ipo na sheria iko wazi kwamba pale unapotaka kutumia eneo kwa ajili ya matumizi mengine, lazima watu wapewe haki zao waondoke. Makanisa, mawe yanadondoka mpaka ndani ya kitanda cha mtu. Makanisa...
MWENYEKITI: Ahsante kwa mchango wako.
Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuchangia Taarifa zilizoko mbele yetu. Awali niwashukuru sana watoa hoja wote, Kamati zote mbili kwa taarifa zao nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda nitakwenda straight kwenye hoja. Naomba nianze kwa kusema kwamba, tunayo hifadhi moja tu Tanzania yenye urithi wa kipekee, hifadhi ambayo ina vivutio ambavyo haviko sehemu nyingine Tanzania, Afrika na hata Dunia nzima na ni Hifadhi yetu ya Ngorongoro. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hifadhi ambayo imekuwa inatuingizia kipato kikubwa sana kwa Taifa hili, lakini kwa karibu miaka 10 sasa, hifadhi hii isipoangaliwa kwa makini inakwenda kupotea ndani ya Tanzania. Hifadhi hii imewekwa ndani ya Urithi wa Dunia, imeingia kwenye Maajabu saba ya Dunia na imewekwa chini ya UNESCO, Shirika la Uhifadhi la Dunia, lakini Watanzania ambao tumepewa hadhi ya kuwa na hifadhi hii tumeshindwa kuitunza na sasa hivi hali ya hifadhi hii inakwenda kupotea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Ngorongoro inakabiliwa na tatizo kubwa la watu kulima ndani ya hifadhi, Ngorongoro inakabiliwa na watumishi kutafuna fedha za hifadhi, inakabiliwa pia na kuongezeka kwa mifugo. Jana nilikuwa nasoma vyombo vya habari, tayari Ngorongoro hata watumishi wanahamishwa wanakataa wanakwenda Mahakamani kushtaki. Najaribu kuelewa kwamba, miaka mitano ijayo tunayo Ngorongoro?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali, hadhi ya Hifadhi ya Ngorongoro iendelee kubaki kama Urithi wa Dunia kwa vizazi vya leo na vizazi vijavyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeunda Tume hapa Tanzania kwa ajili ya kupitia migogoro ya wakulima na wafugaji na kuweza kuondoa mauaji yanayotokea ndani ya nchi yetu. Hata hivyo napenda kujua, Tume hii imeshaanza kazi, itamaliza lini? Tume hii ambayo inahusu Wizara nne na wataalam kutoka Wizara nne wakati bado inaendelea na kazi bado kuna wataalam na watendaji wanaopita kwenye maeneo ya hifadhi na kuweka alama katikati ya nyumba za watu bila kushirikisha Ofisi za Wilaya, Wakurugenzi hata Wabunge kwenye maeneo yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba tujue, Serikali imeamua kuunda Tume, itekeleze kwanza jukumu la Tume. Tume ije na mpango kamili utakaoweza kutoa suluhu ya kutosha kuondoa migogoro ya wafugaji, kuondoa migogoro ya wakulima na migogoro ambayo watu wanapoteza maisha yao hapa ndani ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwamba, Wizara ya Ardhi wamefanya kazi nzuri; wamefungua kanda nne ndani ya Tanzania kuweza kurahisisha huduma za ardhi. Pamoja na kufungua Kanda nne ndani ya nchi yetu bado kuna tatizo kubwa katika Halmashauri zetu, manispaa zetu pamoja na majiji la kutokuwa na fedha za kutosha kuweza kupima maeneo. Tunayo shida kubwa sana Waheshimiwa Wabunge, nchi yetu haijapimwa, maeneo mengi hayajapimwa, migogoro inaongezeka kwa sababu pamoja na kwamba Wizara inajitahidi; na namshukuru Mheshimiwa Lukuvi anafanya kazi nzuri, lakini bado.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali iangalie namna ya kuweza kutoa fedha kama revolving fund kwenye manispaa zetu, kwenye halmashauri zetu pamoja na kwenye majiji, wapewe fedha wapime maeneo, wakishayapima wayauze wapate fedha, warejeshe fedha. Hiyo kazi ilianza kama miaka mitano iliyopita kwenye Manispaa za Dar-es-Salaam; Temeke, Ilala na Kinondoni, sikujua ule mpango uliishia wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunaomba, ule ulikuwa ni mpango mzuri, tuliusapoti lakini umeishia katikati. Ni mpango mzuri, Serikali iwezeshe, ipeleke watalaam wa kutosha kwenye halmashauri, ipeleke vifaa kwenye manispaa, kwenye majiji na halmashauri, lakini pia, itoe fedha waweze kupima kuhakikisha kwamba, nchi yetu inapimwa. Kutegemea Wizara peke yake tutachukua miaka mingi sana kuweza kupima maeneo yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunalo tatizo kubwa sana la makazi holela. Mimi kila nikiongea juu ya ardhi nazungumzia makazi holela. Tumekuwa kama Serikali hatujipangi. Leo kila ukienda watu wanaanzisha miji miwili, mitatu, baada ya miezi mitano, baada ya mwaka ni mji tayari. Tayari wanahitaji huduma za maji, barabara, na umeme. Serikali kwa nini isiwe na mpango? Watu waambiwe kajengeni pale? Kwa nini inasubiri wananchi wajiamulie wenyewe wakakae wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ukianza kutembea kuanzia Dodoma, elekea Morogoro unaenda Dar-es-Salaam, vijiji vinaanzishwa kidogo, kama utani. Serikali ipo, viongozi wapo, wataalam, lakini wanaona wananyamaza kimya. Leo tumekuwa na nchi ambayo haijapimwa maeneo mengi, miji yake ni ya kiholela na bado inazidi kuanzishwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri wa Ardhi ifike mwisho kuwa na mji usiopimwa, usiopangwa, miji ambayo ni ya kiholela. Nchi nzima tunakuwa na vichuguu, hatutaki kuwa na nchi yenye vichuguu. Kwa hiyo tunaomba, Wizara inafanya kazi nzuri lakini haijaweza kudhibiti ujenzi holela kwenye maeneo mbalimbali ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala pia, la National Housing. Nishukuru kwamba, wanafanya kazi nzuri, tatizo kubwa ni jukumu la Serikali kuhakikisha wananchi wake wanapata makazi bora. National Housing inafanya kazi kwa niaba ya Serikali, ni kwa nini Serikali haiwezi ku-subsidize nyumba za National Housing ili wananchi wa hali ya chini waweze kukaa na kuishi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini National Housing inunue simenti bei ileile, mchanga bei ileile, vifaa vya ujenzi bei ileile utegemee wakauze nyumba rahisi? Haiwezekani! Pia, wanapeleka huduma za maji wenyewe, umeme wenyewe, miundombinu wenyewe. Serikali inatakiwa iweze kutoa baadhi ya vitu kupunguza gharama, nyumba za National Housing zinufaishe wananchi wote wenye hali ya kawaida na wenye hali ya chini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasahivi nyumba za National Housing zinakaliwa na kununuliwa na watu wa hali ya juu, watu wa chini hawanufaiki kabisa. Kwa hiyo, hata ile maana ya kuwepo kwa National Housing yenyewe inakuwa haina tija kwa wananchi wa hali ya chini. Ni jukumu la Serikali kuhakikisha kwamba National Housing inakuwa na nyumba nzuri, lakini za standard ambazo mwananchi yeyote yule anayetaka kumudu anaweza kumiliki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunalo tatizo, TANAPA inajitahidi inafanya kazi nzuri. Naomba Serikali ihakikishe inafungua, inaweka miundombinu kwenye maeneo ya hifadhi za Kusini, tuweze kufungua hifadhi za Kusini. Leo ukiangalia Tanzania National Park inajitahidi lakini ni upande mmoja wa Kaskazini. Huku maeneo ya Iringa kuna vivutio vizuri, Kitulo, Mbeya, maeneo mengi. Serikali ni wajibu wake iweke miundombinu kwenye National Parks nyingine zilizoko nje na Kaskazini ili tuweze kuwa na utalii nchi nzima. Vivutio vipo, tatizo ni kwamba, maeneo hayo hayawezi kufikika kwa sababu hakuna miundombinu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lipo tatizo lingine. Tumekuwa tunazungumzia suala la concesion fees kwenye National Park. National Park wame-introduce concesion fees kwa maana ya tozo ya vitanda kwa hoteli ambazo ziko ndani ya hifadhi kwa miaka zaidi ya 10 sasa. Wanatumia zilezile za miaka 20 iliyopita, Dola tano mpaka Dola saba, wakati huo imewekwa hii tozo Dola tano mpaka Dola saba tulikuwa tunalipa kitanda Dola 150 mpaka Dola 200, leo kitanda kimoja National Parks ni Dola 500 mpaka Dola 1,000 lakini tozo iko palepale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua kwamba, Bodi haikuwepo, sasa Bodi imeshateuliwa tayari, naiomba Serikali mapema iwezekanavyo tozo mpya za National Parks ziweze kuwa introduced ili National Park ipate fedha za kutosha kuboresha miundombinu, lakini pia kuweza kusimamia utalii ndani ya hifadhi zetu za TANAPA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lipo suala la Loliondo. Tumeona migogoro mingi ndani ya Loliondo. Naiomba Serikali; kwa taarifa ambazo tumezipata ni kwamba, sehemu ambayo inagombaniwa mpaka Mkuu wa Mkoa Mheshimiwa Mrisho Gambo wametofautiana yeye na Mheshimiwa Waziri ni eneo la chanzo cha maji. Katika eneo lile wanaokuja kufuga kule ni watu wa kutoka nje ya nchi, wameleta mifugo kule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunaomba kwenye masuala ya uhifadhi na hasa kulinda vyanzo vya maji tusiweke siasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimezungumzia juu ya vyanzo vya maji. Nimesema eneo linalogombaniwa ni eneo ambalo linaonekana lina chanzo cha maji. Suala la kuwepo kwa chanzo cha maji haliangalii hifadhi au si hifadhi, ni chanzo cha maji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka mingi tumeshuhudia mifugo Loliondo inakufa wakati wa ukame kwa sababu maji yanakosekana. Leo hata wale wa Loliondo wenyewe wakishindwa kutunza vyanzo vyao vya maji wakati wa ukame mifugo itakufa tu. Kwa hiyo, nasema kwamba, tuangalie interest ya Taifa lakini pia, interest ya wafugaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ni chanzo cha maji kilindwe iwe nje ya hifadhi iwe ndani ya hifadhi!
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru pia kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia kidogo kwenye hotuba ya Waziri Mkuu ambayo iko mbele yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijaenda kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba nizungumze kwa uchache sana upotoshwaji ambao unafanya ndani ya Bunge na kwa Watanzania kuhusiana na suala la mgogoro wa CUF. Nashangaa sana kwa Wabunge wanaotumia muda wa Bunge kupotosha umma kumshambulia Msajili wa Vyama kwamba anaingilia migogoro ndani ya vyama wakati wao wenyewe wameshindwa kuijua, kuisimamia na kuiheshimu Katiba ya chama chao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wapo waliodiriki kusema kwamba Msajili wa Vyama ni karani tu anayekusanya na kutunza mafaili ya vyama vya siasa, hii ni aibu kubwa kwamba Mbunge hajui hata Sheria ya Vyama vya Siasa inasemaje juu ya majukumu ya Msajili wa Vyama. Msajili wa
Vyama anafanaya kazi ya kulea na kusimamia vyama vya siasa, kazi yake siyo karani, waende wakasome Sheria ya Vyama vya Siasa, majukumu na kazi za Msajili wa Vyama vya Siasa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Msajili wa Vyama vya Siasa hakuingilia mgogoro wa CUF peke yake, alipelekewa malalamiko na viongozi ndani ya Chama cha Wananchi CUF, chombo cha mwisho cha maamuzi ni Mkutano Mkuu wa Taifa, Wajumbe 324 walipeleka malalamiko kwa Msajili wa
Vyama juu ya uhuni uliofanyika ndani ya Mkutano Mkuu wa Chama uliofanyika tarehe 21 Agosti, hakuingilia alipelekewa malalamiko.
Mheshimiwa Naibu Spika, Msajili wa Vyama hajamteua Mheshimiwa Sakaya kuwa Kaimu Katibu Mkuu, Katiba ya Chama cha CUF, kipengele 93, Sura ya Tatu kinampa Naibu Katibu Mkuu wa upande wa Bara mamlaka ya kufanya kazi za Katibu Mkuu pale Katibu Mkuu anaposhindwa kutekeleza wajibu wake kama Katiba inavyomwongoza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Wabunge wasipotoshe Umma, wasipotoshe Bunge, wasitumie muda wa Bunge kwa ajili ya kudanganya Watanzania, wafanye kazi kwa ajili ya maslahi ya Watanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naungana na Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa wa Tabora kumpongeza na kumshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi nzuri aliyofanya kuweza kurekebisha Chama cha Ushirika cha Mkoa wa Tabora na ku-overhaul system nzima ya ushirika ya Mkoa wa Tabora, ni matumaini yangu kama watendaji wa Serikali watazingatia maagizo yaliyotolewa na Waziri Mkuu na kuyafanya vizuri nina imani kabisa kwamba kilimo cha
tumbaku cha Mkoa wa Tabora kitanufaisha wakulima kama tunavyotarajia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimesoma hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu hasa suala linalozungumzia suala la uchumi…
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la uchumi. Hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu inasema kwamba uchumi unapanda na umekua kwa asilimia saba lakini pia kwamba mfumuko wa bei
umepungua. Naomba Mheshimiwa Waziri Mkuu wakati wa ku-wind up atuambie, uchumi unapanda wakati hali ya maisha ya Tanzania inazidi kuwa mbaya, hali ya uchumi inazidi kuwa mbaya, pia wafanyabiashara wengi mitaji inazidi kuzama, wanafunga maduka yao, hali ya upatikanaji wa fedha kwa ajili ya maisha ya kawaida unazidi kuwa mbaya unazidi kuwa mdogo. Sasa huu uchumi unapanda, mimi sio mchumi, uchumi unaopanda wakati fedha mifukoni inazidi kupotea ni uchumi wa aina gani?
Mheshimiwa Naibu Spika, hali ya kupanda kwa bei ya gharama za vyakula, wakati tunaambiwa kwamba mfumuko wa bei unapungua lakini ukienda sokoni, leo nimekwenda sokoni na jana nimekwenda sokoni, kilo ya mchele shilingi 2,400, kilo ya unga shilingi 2,200, maharage
nimenunua leo shilingi 2,400 bei zinazidi kupanda. Kwa hali ya kawaida, Watanzania wengi kwa hali ilivyo sasa hivi hawana uwezo wa kuweza kula milo miwili ya uhakika kwa siku. Kwa hiyo, tunaomba Serikali lazima iangalie namna, kama vyakula vimefichwa vitoke vije ndani ya masoko ili bei zishuke. Kuambiwa kwamba bei zinashuka mfumuko wa bei unapungua wakati hali inazidi kubana, haiendani na hali halisi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la uwezeshaji wa vijana. Hotuba ya Waziri Mkuu inatuambia kwamba Serikali imetoa almost 1.5 billion kwa ajili ya kusaidia mfuko wa vijana na akina mama pia halmashauri zetu zimetenga fedha karibu shilingi bilioni 4.6 kwa ajili ya kuwezesha vijana na akina mama, kwa Mikoa yote ya Tanzania na Wilaya zetu karibu 140 bado ni fedha kidogo sana. Kwanza fedha inayotolewa na Serikali, shilingi bilioni 1.5 ni ndogo kwa sababu vikundi ni vingi na vingi havipati hiyo hela ya kukopeshwa. Halmashauri zetu ile asilimia tano haitengwi, wanatenga kidogo sana kwa sababu hali ya Halmashauri pia makusanyo siyo mazuri na wengine fedha zao ni kidogo, hawana uwezo wa kutenga asilimia tano kwa ukamilifu, matokeo yake vikundi vimeundwa vingi vya akina mama, vya vijana, hawapati mikopo wanafuatilia mwaka baada ya mwaka hawapati mikopo ya kutosha.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kwanza Serikali ihakikishe inaongeza fedha za mikopo ya vijana na akina mama za kutosha kwenda kwenye Halmashauri zetu. Pili, kuwepo ufuatiliaji wa kutosha, Halmashauri zitenge fedha za kutosha na kulipa, vikundi vinakopa zile fedha hazirejeshwi, matokeo yake inashindwa kuwa revolving fund ambayo kama ingekuwa inarejeshwa kwa wakati wengine wangepewa, matokeo yake Halmashauri hazirejeshi, vijana
wengine wanasubiri miaka miwili hawajapata mikopo. Kwa hiyo, suala la uwezeshaji wa vijana bado ni tatizo kubwa, fedha inayotolewa ni kidogo, haitoshelezi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la ajira, bado tatizo ajira ni kubwa ndani ya nchi yetu na vijana wengi bado wanazurura, wapo kwenye vijiwe, wapo mitaani. Ni kweli kwamba asilimia karibu 57 ya Watanzania wameajiriwa kwenye sekta binafsi, lakini mazingira wanayofanyia kazi
kwenye sekta binafsi ni magumu mno. Mishahara yao ni midogo, kwanza hawaingizwi kwenye mifuko ya jamii lakini wengine hawana likizo, hawana chochote, wanashindwa wafanye nini kwenye mashirika binafsi. Wengine wananyimwa mpaka haki zao za uzazi, mwanamke akipata
mimba akiwa kwenye mashirika binafsi au viwanda anaachishwa kazi kwa sababu tu kapata mimba, hata ile haki ya kuzaa ananyimwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba Serikali ifuatilie, ni kweli kwamba sekta binafsi zinasaidia sana kwenye ajira ya Watanzania lazima tuwapongeze, lakini lazima sheria za kazi zifuatwe. Kama Serikali imesema kima cha chini cha mshahara kwa nini kule wakatoe shilingi 100,000, 120,000 kwa mwezi. Kwa maisha ya sasa hivi kumpa mtu 120,000 kwa mwezi anaishije? Anafanya kazi zaidi hata muda wa saa za kazi wengine mpaka usiku. Pia wengine hawapewi mikataba ya kazi wanafanya kazi kama vibarua, miaka saba mpaka kumi wanaajiriwa kwa miezi mitatu, mitatu wanakosa haki zao za msingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali, wametuambia kwamba wanatengeneza Mabaraza ya Kazi, maeneo mengine hawaruhusiwi kutengeneza mabaraza ya kazi. Mimi nimeshuhudia kabisa makampuni yetu haya ya Kichina, hawawaruhusu kutengeneza Mabaraza ya Kazi, hata
sehemu ya kupeleka malalamiko yao hakuna. Kwa hiyo, ninaomba Serikali ihakikishe kwamba pamoja na kwamba wanatusaidia ni lazima pia wahakikishe kwamba wanaweza kutoa haki zinazostahili.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho ni suala la uzalishaji. Hatuwezi kuwa na uchumi wa viwanda kama hatusimamii vizuri suala la kilimo. Kilimo tusimamie kuanzia uzalishaji, utunzaji, usafirishaji mpaka kwenye masoko. Njia pekee ya kuweza kuwa na uhakika wa masoko ni kuwa na viwanda vidogo vidogo na viwanda vikubwa. Kila Mkoa Mungu ameubariki una zao la biashara, hebu Serikali iweke mkakati, nashukuru kwamba mashirika ya kijamii yameanza kuingia kwenye kutengeneza viwanda, wahakikishe kila Mkoa, tukianza na Mkoa wa Tabora, kiwanda cha tumbaku kijengwe mkoani Tabora, vijana wa Tabora wapate kazi ndani ya kiwanda cha tumbaku.
Mheshimiwa Naibu Spika, hapa Dodoma tuna zao la zabibu, tumeweka kiwanda kilichopo hapa kinachukua concentrate kutoka nje, tuhakikishe kila kiwanda kinachowekwa ndani ya Mkoa wowote kinatumia materials kutoka ndani ya mkoa wenyewe. Tukihakikisha kila Mkoa
tumekuwa na kiwanda, kutumia material ya kilimo yanayopatikana ndani ya mkoa ule, kwanza tutazalisha ajira kwa wingi pia tutaweza kuwainua wakulima kwa sababu watalima kwa tija wana uhakika na masoko yao. Vinginevyo ni tatizo kubwa tutaimba mpaka tuchoke wakulima
hatuwezi kuwainua na ukizingatia asilimia 80 ya Watanzania ni wakulima na wengi wako vijijini wanategemea kilimo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo, tuboreshe kilimo, pembejeo ziwepo kwa wakati, tujenge maghala ya kutosha. Tukihakikisha kilimo kimekuwa na tija nina imani kabisa Watanzania walio wengi watanufaika na tutaweza kuondoa umaskini kwa kiasi kikubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Ahsante.
Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia kidogo kwenye Mpango uliopo mbele yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii pia kuendelea kuwashukuru wananchi wa Jimbo la Kaliua kuendelea kuniamini kuwa mtumishi wao na kunipa tena fursa ya kuweza kuwepo ndani ya chombo hiki cha uwakilishi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitabu hiki nimekipenda sana kwa kuwa kina Mipango mizuri kweli kweli, tena sana. Nina imani kabisa kama itakwenda kutekelezwa vizuri nchi yetu itapiga hatua kubwa sana. Wasiwasi wangu ni wale wanaokwenda kutekeleza, juzi nilichangia kwa ufupi, tuna shida kubwa ya watendaji wa nchi yetu. Tumekuwa na gap kubwa, watu hawafanyi kazi kwa kuwajibika, hii Mipango yote haiendi kufanywa na robbot, inakwenda kutekelezwa na watu kwa kutumia brain zao, mikono yao na akili Mungu alizowapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesoma kwenye kitabu, kwenye mradi mmojawapo mkubwa ni kusomesha vijana wengi kwa mkupuo katika fani mbalimbali. Sijaona Mpango gani wa kwenda kubadili mindset za watendaji wa nchi hii na vijana wetu wakasome, wakielewa wanakwenda kusoma kwa ajili ya kwenda kufanya nini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna shida kubwa kama Serikali haitaangalia hili, Mipango yote hii iliyopo huku haina watekelezaji. Kwa hiyo, shida kubwa namna gani kwenye mipango yao ya kawaida ya Serikali lazima waliopo kazini, wanaoingia, waliopo mashuleni wakajengewe uwezo namna gani ya kujituma, namna gani ya kuwajibika, namna gani ya kujipima na kwenda kutekeleza miradi ya Kitaifa ambayo ipo kwenye mipango hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze suala kubwa tulilonalo ni suala la maji, tena niseme kwa uchungu mkubwa. Nchi yetu ina shida kubwa sana ya tatizo la maji na ni tatizo ambalo linawatesa watu, nina maumivu makubwa na zaidi kabisa kwa kina mama na watoto. Kina mama wengi wanakosa hata fursa za kuhudumia familia kwa sababu ya maji, lakini watoto wengi na hasa wa kike wanakwenda kufuata maji wanakosa hata muda wa vipindi kwenye madarasa wanachelewa shuleni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa miradi ya maji, nimesoma mingi huku, ninavyosikia Serikali inasema kwamba tutaendelea na utaratibu wa maji vijijini, ndiyo hadithi miaka yote. Nimekaa ndani ya Bunge hili miaka 10 tunaambiwa miradi ya maji, miradi ya World Bank, kwenye Wilaya yangu ya Kaliua, kati ya vijiji vyote vijiji vitatu tu vilipatikana na maji na yale maji hayakusambazwa popote, yameishia pale pale. Kwa hiyo, unavyosema kwamba tutaendelea na utaratibu wa kumalizia au kutekeleza Miradi ya Maji ya Vijiji 10 ya World Bank almost 70% ili-fail.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba lazima tunapokwenda kuangalia miradi ya maji tuone kweli inafanikiwa. Nimeangalia kwenye Mpango hapa, Mkoa wetu wa Tabora tulipata faraja baada ya kuambiwa kwamba kuna mpango wa kutoa maji Ziwa Victoria kuleta Wilaya zote za Mkoa wa Tabora, kuanzia Nzega kwenda Igunga kwenda Bukene mpaka Sikonge, Tabora Mjini mpaka Urambo, Kaliua haikuwepo. Nimeangalia hapa tena haipo kwenye Mpango wa mwaka huu, haipo kabisa, kwamba ule Mpango umeishia wapi? Ni miaka mitatu uchambuzi yakinifu unafanyika, miaka mitatu upembuzi unafanyika, miaka mitatu utafiti unafanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hotuba ya Mheshimiwa Rais hapa alisema ule uchambuzi na upembuzi yakinifu utakuwa haupo tena kwenye Serikali hii, mbona huu upembuzi unaendelea miaka mingi. Naomba sana kwenye mpango wa mwaka huu mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria kuleta Mkoa wa Tabora na Wilaya zake utimie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Wilaya yangu ya Kaliua Mpango wa Victoria haupo na mpango uliokuwepo kwenye Wilaya ya Urambo kuanzia mwaka 2013 ni kutoa maji kutoka Ziwa Ugala. Ni jambo la kusikitisha juzi nimesikia Mheshimiwa Waziri anasema hapa, mchakato bado unaendelea 2014 zilitengwa milioni 450 kufanya uchambuzi yakinifu na upembuzi, leo ni mwaka wa tatu bado uchambuzi unaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini bado Serikali ikaja na mpango wa kwenda kutoa maji Malagarasi, bado tunaambiwa uchambuzi yakinifu unaendelea. Naiomba Serikali, kwenye Mpango huu uwepo mradi wa maji katika Wilaya ya Kaliua wa kuondoa machungu na mateso kwa akinamama wa Kaliua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni kuendelea kushuka kwa shilingi ya Tanzania. Nilikuwa nazungumza, nitaendelea kuzungumza, ndiyo wajibu wangu kama mwakilishi. Tumekosa udhibiti wa shilingi yetu ya Tanzania kabisa kwa miaka yote na nimekuwa namlaumu hata Benno, Gavana Mkuu, ameshindwa kusimamia, kusimama kwa shilingi ya Tanzania. Ni Tanzania pekee, dola inatumika kununua vitu madukani, ni nchi gani utakayokwenda ukatumia Tanzania shillings kununua vitu madukani kwao. Tanzania tunatumia fedha ya nje kununua vitu, kutoa huduma kwenye maduka yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ni Tanzania pekee kuna utitiri wa bureau de change kila kona unakuta viduka vya kubadilisha fedha. Leo ukienda Kariakoo watu wana dola mikononi, mikononi tena Wamachinga watu wadogo, wanashika dola wanauza nchi gani hii! Kuendelea kushuka kwa shilingi ya Tanzania kumeendelea kushusha uchumi wetu, hili hatulifahamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda nchi nyingine kubadilisha fedha unaingia gharama kubwa unateseka kweli na wana centers Tanzania tunaongea hapa halifanyiwi kazi. Kwenye Mpango wa mwaka huu tunataka tujue mpango wa kudhibiti matumizi ya dola ndani ya nchi yetu, mpango wa kudhibiti maduka holela ya fedha hapa nchini na mpango wa kuimarisha fedha yetu ya Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatusafirishi chochote Tanzania, sisi ndiyo tumekuwa masoko ya wenzetu, tunauza kila kitu, ni masoko tu, masuala mengine hayajaleta viwanda vikubwa vya ajabu. Hivi kweli, tunahitaji kiwanda cha aina gani kutengeneza pamba stick, tunaagiza kutoka nje. Tunahitaji kiwanda cha aina gani kutengeneza toothpick ya kuchokonolea meno, tunaagiza kutoka nje, tunahitaji kiwanda gani kule kuleta ndani ya nchi yetu vibiriti, vitu vingine ni vidogo vinatutia aibu, ni Taifa kubwa, lakini hebu aibu hii iondoke. Vile vitu ambavyo tuna uwezo navyo ndani ya nchi yetu tusiagize, tumezidi kuwa masoko ya wenzetu, tunatoa ajira kwa wenzetu, sisi tunaendelea kunyanyasika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefurahi kusikia kwenye hotuba hapa, kwamba, kuna viwanda kuendana na jiografia ya nchi yetu. Tuna bahati kweli Watanzania, maeneo mengi almost karibu kila kanda ina vitu ambavyo Mungu ameweka. Mkoa wa Tabora tuna misitu, tunasafirisha mbao, kuna magogo, jambo la ajabu vijana wanadhurura, hawana ajira, lakini mbao zinapelekwa China zinakwenda kutengeneza furniture tunarudishiwa makapi, tunanunua. Tunaomba kwenye Mpango wa mwaka huu kuwepo kiwanda kikubwa Mkoa wa Tabora cha kutumia rasilimali ya mbao na magogo ya Tabora, badala ya kusafirisha yaende nje, vijana wapate ajira, lakini pia tuweze kuzalisha ndani ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilisema hapa Bungeni, itahakikisha samani zote za ofisi zinanunuliwa ndani ya nchi. Huu ni mwaka wa nne, Serikali wameshindwa wanaagiza, leo ukienda ofisi zote za Serikali ni samani za Kichina, wakati tunao vijana, tunazo mbao, tunayo magogo, miti ya thamani, mininga, mikongo mnapeleka China, tunaletewa makapi, tunanunua vitu ambavyo ni very low quality, this is shame! Naomba sana Serikali kwenye Mpango ihakikishe sasa ile mipango ya miaka mitatu, minne iliyopita hakuna kutoa kitu nje, tuwezeshe vijana wetu, tuwezeshe Magereza, tuwezeshe Jeshi ili tununue vifaa ndani ya nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la kilimo. Hili ni muhimu kwa hiyo, lazima tuligusie, lazima tuwe na kilimo cha uhakika, lakini pia lazima tuhakikishe kilimo chetu kinaendana na hali halisi. Leo kilimo chetu kimekuwa cha jembe la mkono kwa asilimia kubwa. Lakini pia utaratibu unaotumika kupata pembejeo sio mzuri, ni wizi unafanyika, Serikali kila mpango unaokuja nao hautekelezeki. Sasa tunaomba, tunapokwenda kwenye uchumi wa viwanda uende sambamba na uchumi na kilimo chenye tija. Umwagiliaji, pembejeo, mechanization, wawezeshaji wale watumishi wawe wa kutosha lakini pia wawe na ujuzi wa kutosha kuweza kutoa elimu kwa ajili ya kilimo chetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, ni suala la elimu. Nashukuru kwamba Mheshimiwa Rais ameamua kutoa elimu bure kwa Watanzania, ni jambo jema. Naomba suala la elimu bure liendane na miundombinu ya watoto, ukiwapa leo watoto elimu bure, wengi wanakaa chini, kwangu Kaliua kule watoto wanasomea chini ya mti. Mtoto anasomea chini ya gogo, kwanza hajui kama kuna elimu bure kwa sababu ananyeshewa na mvua, anapigwa na jua, lakini pia tuhakikishe watoto wetu wanakaa kwenye madawati yote.
Kwa hiyo, naomba kwenye Mpango huu, mwaka huu Serikali ihakikishe ndani ya mwaka mmoja, watoto wote wa Tanzania vijijini na mijini wanakaa madarasani, lakini pia wanakaa kwenye madawati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo, angalau kila mtoto atajua kwamba Serikali yake inamjali, atathamini sana elimu ambayo anapewa, lakini pia itamjengea uwezo. Leo tumekuwa tunapata kwenye taarifa zetu kwamba mtoto anamaliza shule hajui kusoma wala kuandika. Kwa sisi ambao tunatoka vijijini hushangai, kama mtoto anakaa chini ya mti, mvua inamnyeshea miaka miwili, mitatu, hajui kusoma…
MWENYEKITI: Mheshimiwa Sakaya muda wako tayari.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA:Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora) kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, pongezi kwa Waziri na Wataalam wake wote. Pamoja na hotuba yao nzuri, napongeza hotuba ya Msemaji wa Kambi ya Upinzani na Kamati ya Bunge.
Mheshimiwa Naibu Spika, rushwa ni adui wa haki. Wananchi wengi wanakosa haki zao za msingi karibu kila mahali hasa kwenye vyombo vya kutoa haki; Mahakimu wengi wanaongoza kwa rushwa, mahospitalini, kwenye kutafuta kazi; kwenye makampuni wapo wanaopoteza maisha sababu ameshindwa kutoa rushwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, TAKUKURU haina meno – haina mamlaka ya kushtaki, ni mpaka ipeleke faili kwa DPP. Serikali ieleze ni lini sheria ya TAKUKURU italetwa Bungeni ili wapewe meno?
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa MKURABITA kwa kiasi kikubwa haujaweza kusaidia wananchi wa chini (wanyonge). Pamoja na kuwa na dhamira nzuri, lakini bado wananchi wengi wanakosa mikopo Benki, pamoja na kuwa na nyumba ambazo hazina hati na viwanja ambavyo havijajengwa. Ni kwa nini wananchi hawa wanakosa mikopo kwenye Taasisi za fedha wakati kuna MKURABITA?
Mheshimiwa Naibu Spika, Wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki hawakulipwa mafao yao. Ni miaka 30 na zaidi sasa wanadai haki zao bila mafanikio. Serikali ya Awamu ya Tatu, Mheshimiwa Benjamini Mkapa, Rais Mstaafu aliwalipa robo. Serikali ya Awamu ya Nne iliwapiga mabomu wazee hawa walipokwenda Ikulu kudai mafao yao. Hii ni aibu kubwa kwa Taifa kuwapiga wazee waliotumikia nchi yao kwa uaminifu bila wizi wala ufisadi na wengi wao ni maskini. Serikali hii itawalipa lini wastaafu hawa mafao yao ambayo ni haki yao?
Mheshimiwa Naibu Spika, Mfuko wa TASAF umesaidia wananchi maskini na watoto, baadhi wameweza kwenda shule. Serikali itoe tamko na agizo kwa Kamati za Mfuko wa TASAF wanaoiba fedha za wahitaji. Utaratibu wa kuibua wahitaji kwenye mikutano ya hadhara usimamiwe na Serikali. Watendaji wanaweka watu/familia zao zenye uwezo. Familia zote maskini zipate nafasi katika Mfuko huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna Walimu wengi walioajiriwa mwaka 2014/2015, katika Wilaya ya Kaliua, hawajapata mishahara yao ya mwezi Mei na Juni. Orodha na majina yao yako Utumishi. Ni kwa nini hawalipwi mishahara yao?
Mheshimiwa Naibu Spika, pia suala la kuchelewesha mishahara ya Walimu inawakatisha tamaa na kuondoa moyo wa kazi na kwa kuzingatia mazingira ya kazi yao, ni magumu na mishahara ni midogo. Vile vile Walimu hawapandishwi madaraja kwa wakati na hivyo kutopandisha mishahara yao kwa wakati. Hakuna Taifa bila Walimu!
Mheshimiwa Naibu Spika, kitendo cha Serikali kuzuia Watanzania kuona Bunge Live ni kuwanyima wananchi haki yao ya msingi kuona/kutazama chombo chao cha Uwakilishi. Hili Bunge ni chombo pekee ambapo kila Mtanzania anawakilishwa, wana haki ya kujua nini kinaendelea. Kama suala ni bajeti ya Serikali ya TBC1; kuna vyombo vya binafsi. Kwa nini wanakatazwa kuonyesha? Serikali inaogopa nini? Inaficha nini? Hii ni aibu kubwa na huo utawala bora uko wapi?
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Kaliua kuna maeneo wananchi (Wasukuma) wanajichukulia hatua mkononi na kuwatoa Viongozi waliochaguliwa kwenye nafasi zao na kutaka kuwaua/kuwajeruhi na hakuna hatua za kiserikali zinazochukuliwa kwa watu hawa. Matukio yote yameripotiwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Kaliua na hakuna hatua yoyote inayochukuliwa. Serikali ichukue hatua mapema kuondoa kasumba hii.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuchangia kwenye hotuba iliyopo mbele yetu. Niliwasilisha maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani, sasa huu ndiyo mchango wangu mimi kama Sakaya, Mbunge wa Jimbo la Kaliua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendeleze kilio cha zao la tumbaku kwa sababu mengine sikuweza kuandika kwenye hotuba. Makampuni ya tumbaku yamekuwa na urasimu mkubwa sana kwa wakulima wa tumbaku. Mwaka 2014/2015 tulikaa kwenye kikao cha wadau tukakubaliana kupanga bei ya tumbaku kila kampuni inunue kwa dola mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo makampuni matatu; tunayo TLTC, Alliance One na GTI. Makampuni mawili ya TLTC na Alliance One walikataa kununua tumbaku kwa bei tuliyokubaliana kwenye kikao cha wadau. Kampuni ya TLTC walinunua kwa dola za Kimarekani 1.73; Alliance One walinunua kwa dola za Kimarekani 1.78, na GTI peke yake ndiyo waliokubali kununua kwa dola za Kimarekani mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, makampuni haya mawili yamesababisha hasara kubwa sana kwa wakulima wa Mkoa wa Tabora. TLTC peke yake, kwa mwaka 2015 kwa msimu mmoja tu wamesababisha hasara ya dola 3,953,558.3; Kampuni ya Alliance One imesababisha hasara kwa wakulima kiasi cha dola 2,537,800.10. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa pamoja makampuni haya yamesababisha hasara ya dola 6,491,758.40, sawa sawa na shilingi bilioni 13,665,676,156. Tumekaa kwenye mkutano wa wadau Mkoa wa Tabora tukakubaliana, hatuwezi kuruhusu makampuni haya kununua tena tumbaku msimu huu kabla hawajalipa hasara hii kwa wakulima wa tumbaku. Tunaiomba Serikali itusaidie, hasara iliyosababishwa kwa wakulima wa tumbaku kwa msimu mmoja tu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaposimama hapa Bungeni kulia kilio cha Wanatabora na tumbaku kwa ujumla, mtusikilize Mheshimiwa Waziri. Kama kwa msimu mmoja, makampuni mawili yanasababisha hasara ya shilingi bilioni 13 na ushee, rudi nyuma miaka yote ambayo wakulima wanalima tumbaku, ni hasara kiasi gani wanasababishiwa na makampuni? Naiomba Serikali itusaidie, makampuni haya yalipe fedha hii kwa wakulima kabla ya kuruhusiwa kununua tumbaku kwa msimu huu wa mwaka huu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaruhusu viwanda kujengwa ndani ya nchi yetu, kwa nia ya kuweza kusaidia mazao ya nchi yetu yaweze kupata masoko. Tunaomba kupata majibu kwa Serikali, tunavyo viwanda ndani ya nchi yetu; tukianzia na Kiwanda cha Mkoa wa Dodoma cha kutengeneza mvinyo ambapo hatumii zabibu ya Mkoa wa Dodoma, anatumia concentrate, anakwenda kuchukuwa juice toka nje anatengeneza mvinyo wakati Dodoma tunazo zabibu zinatembezwa mtaani na akina mama, hazina soko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini Serikali inaruhusu? Tulijua kiwanda kile cha mvinyo kingesaidia kuweza kununua mazao ya zabibu, leo akina mama wanaleta mtaani, zabibu haina soko la maana, lakini tunacho kiwanda ambacho kinachukuwa juice kutoka nje. Ni hasara kwa Serikali, ni hasara kwa wakulima. Kwa nini Serikali inaruhusu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunavyo viwanda vya maziwa, leo tunaruhusu viwanda vya maziwa vinaleta Powder, vinatengeneza maziwa vinakwenda kusambaza, Lita moja ya maziwa ya powder ni shilingi 4,000, lita ya maziwa ya kawaida ni shilingi 1,000, huu ni unyonyaji wa hali ya juu! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazo juice, leo tuna machungwa nchi hii yamejaa kila kona, nenda Mwanza, Muheza yamejaa, tunakubali juice za nje, viwanda viko ndani vina-pack juice ya concentrate kutoka nje, wanakwenda kuuza lita moja shilingi 4,000 huku machungwa yanaoza, hayana soko. Kwa nini tunashindwa kutumia viwanda vya ndani kuweza kununua mazao ya ndani?
Naomba kujua, nini hatima na Mheshimiwa Waziri? Atujibu hapo, ni kwa nini wanaruhusiwa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala linguine ni Serikali kuruhusu vipimo ambavyo siyo halali; kuruhusu mazao ya wakulima kununuliwa kwa vipimo ambavyo siyo halali kwa kutumia rumbesa. Wakulima wananyonywa kupita maelezo! Wafanyabiashara wanajinufaisha sana. Leo mkulima wa hapa Gairo, gunia moja la viazi linawekwa rumbesa, akifika Dar es Salaam anatoa magunia mawili wakati kanunua gunia moja! Kwa nini Serikali haina huruma na wakulima wa Tanzania? Kwa nini Serikali inaruhusu wafanyabiashara wanakwenda mashambani wanashindilia magunia mpaka wananulia gunia lingine wanafunika kwa juu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Waziri wa biashara akiwa Mheshimiwa Mama Nagu, tulimuuliza maswali hapa Bungeni na akaja na mpango wa kuhakikisha kwamba tunazuia vipimo ambavyo siyo halali tuje na mizani halisi. Baada ya muda mfupi wakaleta mpango wa mizani, then wakaja hapa Bungeni kwa Azimio wakaondoa ule utaratibu. Leo ni kilio kwa Watanzania, wakulima wanaumia, Serikali ipo inaona. Naomba kujua ni kwa nini hatuji na mizani kwenye mazao? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ng‟ombe wananunuliwa kwa kupapasa, hakuna mizani. Hatuwezi kwenda kwa namna hiyo! Pia naomba kujua, kwa nini Serikali haianzishi Tume ya Udhibiti wa Bei ili kila mazao ya wakulima yanunuliwe kwa bei ambayo ni halisi, mkulima anufaike na mfugaji anufaike! Hatuwezi kwenda kwa namna hii wakati 70 percent ya wananchi wetu wanategemea kilimo na mifugo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni matumizi ya viatilifu na madawa ya mifugo na mimea katika mazao. Hili ni tatizo kubwa. Tumekuwa tunaruhusu, sheria inasema baada ya ng‟ombe kuchomwa sindano, aidha, antibiotics au baada ya mazao ya mboga mboga kuwekewa dawa za kuzuia wadudu yakae siku 14 shambani au ng‟ombe akae siku 14 kabla ya kupelekwa butchery.
Sasa dawa inapulizwa leo, kesho mboga ziko sokoni; kesho nyanya ziko sokoni. Unanunua mboga zina dawa unaziona kwa macho huhitaji hata kutumia darubini. Tunaharibu afya za walaji wetu! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua na Serikali itueleze, wameweka utaratibu gani kufuatilia kuhakikisha mazao yanayokwenda sokoni ni bora na salama kwa walaji? Vinginevyo mimi nimekuwa najiuliza kila leo cancer zinazuka kila kona, kila leo mara figo zinaathirika, afya za wananchi wetu mpaka watoto wadogo! Hatuoni tatizo ni kwamba tunashindwa kudhibiti ulaji? Hatuoni tunashindwa kudhibiti mazao kwenye masoko? Tunaruhusu wananchi wetu wanakula vyakula, ambavyo haviwezekani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaporuhusu ng‟ombe aliyechomwa antibiotic jana, leo analiwa, ile sumu ya madawa bado iko ndani ya mwili wake, inakwenda straight kwa mlaji. Leo mwananchi anaugua, akitibiwa dawa hazifanyi kazi; UTI imejaa, malaria hazitibiki, typhoid imekuwa nyingi! Tunaomba Serikali itujibu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lipo suala linguine kuhusu matumizi ya hormone kwa kuku wa kisasa wanaofugwa, nalo ni tatizo kubwa sana. Unaweza kufikiria labda Serikali haipo! Hivi kweli kifaranga day one (chick) analelewa kwa muda wa wiki nne, ameliwa! Wiki nne, kuku anapewa hormone ananenepa, ukimkuta ana kilo moja au robo tatu ndani ya wiki nne. Huyu kuku ni salama? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo watoto wetu, nenda Dar es Salaam, watoto wa kiume wanaota maziwa, akina baba wanaota maziwa, Serikali haioni! Wanaruhusiwa wanauza wale Kuku. Angalau kuku wawe wamemaliza miezi miwili au miezi miwili na nusu. Kiukweli suala la afya ya Watanzania kwenye ulaji wa vyakula vya kisasa ni tatizo kubwa na hakuna udhibiti wa aina yoyote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia kujua, nimezungumzia suala la Vyuo vya Kilimo hapa nchini. Tunacho Chuo kimoja tu Tanzania kinachotoa degree zote kuanzia ya kwanza mpaka ya mwisho kwenye masuala ya kilimo na Mifugo, ambacho ni Chuo Kikuu cha Sokoine, Morogoro. Kwa miaka miwili Serikali imeshindwa kupeleka hata senti moja ya maendeleo, Chuo Kikuu kimoja tu!
Mheshimiwa Mwenyekiti, pale vyuoni kuna watalaam wana mifugo ya mfano, kuna mashamba ya mfano, watoto wanasoma, watoto wanakosa mpaka practicals, watoto wanasoma theoretical; tunataka kuboresha kilimo, tunataka kuboresha mifugo, watoto wetu wanasoma mpaka vyuo vikuu ni theory, hakuna practical! How can we move? Hatuwezi kwenda! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua, chuo kimoja tu! Kama tumeshindwa kukiangalia chuo kimoja; bahati nzuri Bunge lililopita tulikuwa tunasafiri tulikwenda nchi mbalimbali. Tulikwenda Indonesia, unapozungumzia habari ya drip irrigation unakwenda kuangalia vyuo vikuu, wanaonyesha kwamba drip irrigation ikoje na watu wanakuja kule kujifunza. Leo hapa tunazunguza vitu havipo. Naomba kujua, kama Chuo kimoja tunashindwa, kwa miaka miwili, miundombinu ni ile ile! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesoma Sokoine, mimi ni product… (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante kwa mchango wako.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini Serikali inaruhusu Shirika la ndege la FastJet hutoa huduma kwa kuwaibia wateja/abiria kwa kiasi kikubwa hivyo? Ndani ya ndege, maji nusu lita wanauza shilingi 3,000 wakati wanachukua kiwandani kwa bei ya jumla, nusu lita shilingi 300.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukikata tiketi ya go and return, ukipata dharura ukashindwa kusafiri tarehe ya tiketi hata ukiwapa taarifa saa 24 kabla ya safari, hela yako inakufa na tiketi imekufa. Begi hata kama lina nguo za mtoto, likizidi kilo moja unalipishwa kuanzia shilingi 100,000 mpaka shilingi 200,000; huu ni wizi mtupu wakati Serikali ipo na inaona. Tunaomba majibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano ya simu; katika Wilaya ya Kaliua kuna maeneo ambayo hakuna minara ya simu na hivyo, wananchi hupata shida kubwa ya mawasiliano. Kata ya Igwisi, kijiji cha Upele na vitongoji vyake vyote, kata ya Tugimlole mpaka kijiji cha Igombe. Kata ya Ulambi, Sigaga mpaka vijiji vya Usinga na Kotonko. Kata ya Igagala mpaka vijiji vya Wachawasome na vitongoji vya Kona Nne, Ukumbanija, Ufulaga. Kata ya Ugunga mpaka vijiji vya Mpilipili na vitongoji vya Kanyanya. Maeneo yote ya Kaliua kuanzia pale mjini mtandao wa Tigo ni wa shida sana.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia kwenye Mpango wa Maendeleo ulioko mbele yetu wa mwaka 2018/2019. Nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa uzima nikaweza kusimama tena mbele ya Bunge lako Tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru kwenye mpango wa Waziri ameweka vipaumbele vichache. Nami naomba nijaribu kuangalia vile vipaumbele kwa namna ambavyo vinaweza kuboreshwa zaidi. Kwanza naanza na hii ya kufungamanisha uchumi na maendeleo ya watu na hasa nikianza na suala la maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matarajio yetu Wabunge na ni matarajio ya Watanzania kwamba, angalau mpango wa bajeti ujao uweze kwenda kuondoa kilio cha maji cha muda mrefu, kwa sababu kilio kimekuwa ni cha kila mahali. Kila Mbunge ndani ya Bunge hili Tukufu ana kilio cha maji na kiukweli maji ni uhai, maji ni uzima. Tunapokwenda kugusa suala ambalo tunagusa uhai wa Watanzania tusitegemee tunaambiwa kwamba, tunasubiri kupata wafadhili au tunaomba wafadhili, tutenge fedha ya ndani kwenda kukamilisha miradi ya maji ambayo imeanzwa ili tuweze kupata maji ya uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye mpango ujao nategemea kabisa miradi mikubwa ile ambayo ilikuwa kwenye bajeti inafanyiwa upembuzi yakinifu na mambo mengine inakwenda kuwekewa fedha ya kutekelezwa ikiwepo mradi wa maji kutoka Malagarasi Mkoani Tabora kupeleka Wilaya ya Kaliua na Wilaya ya Urambo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana kwenye bajeti ijayo kuwepo na fedha ya kutosha kuhakikisha kwamba, mradi huu unakamilika kwa sababu, Serikali inajua kwamba, ndani ya Mkoa wa Tabora ardhi haina visima vya maji kwa hiyo, njia pekee ni Mradi huu wa Maji wa Malagarasi na Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria kuweza kupeleka katika Mkoa wa Tabora. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la usimamizi wa rasilimali ya misitu. Katika kipindi ambacho misitu yetu inateketea ni kipindi hiki. Nilitegemea kabisa kwamba, baada ya kuanzishwa kwa Wakala wa Misitu angalau lengo la Wakala wa Misitu, ilikuwa ni kuhakikisha kwamba, misitu inalindwa, inahifadhiwa, lakini inatunzwa kwa njia ambayo ni endelevu na matumizi endelevu. Sasa hivi tofauti na hapo Maafisa wa Misitu kwa maeneo mbalimbali kazi wanayofanya ni kugonga mihuri kwenye magogo, kwenye mbao, magogo yanaondoka tunabakiwa na vichaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana kwenye mpango ujao namna gani Serikali itahakikisha kwamba, inaweka mpango endelevu wa kulinda na kutunza misitu yetu, tunaenda kuwa jangwa. Leo tunapata madhara mengi sana ndani ya nchi yetu kutokana na mabadiliko ya tabianchi, hatujui chanzo ni nini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uchomaji wa mkaa umezidi na bahati mbaya sana leo Serikali imeweka mabango sehemu maeneo mbalimbali kuhalalisha mauzo ya mazao ya misitu wakati uvunaji wa misitu na utunzaji, kupanda miti ni tofauti. Tunapanda kidogo sana, hatutunzi, haikui, tunavuna kwa speed ya 100 percent, tuendako tunaenda kuwa jangwa. Naiomba sana Serikali tuhakikishe tunaweka mpango endelevu wa kutunza na kuhifadhi misitu yetu kwa sababu hali ni mbaya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia chanzo kikubwa cha uharibifu wa misitu ni ukataji wa mkaa na hatujawa na mpango mbadala wa matumizi ya nishati, tunasema kila siku. Nimeona kwenye Mpango wa Serikali kwamba, tunakwenda kuwekwa kiwanda cha makaa ya mawe ya Mchuchuma. Ni miaka 15 tunasikia makaa ya Mchuchuma – makaa ya Mchuchuma, kwa nini hautekelezwi, miaka 15?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pengine ingekuwa ni solution kuhakikisha kwamba, watu wanapata nishati ya kutumia kwa sababu, umeme huwezi kupikia, gesi wanatumia wachache, mafuta ya taa hayashikiki, ni kuni na mkaa. Asilimia 80 ya Watanzania wanatumia kuni na mkaa, hebu Serikali mwakani itujie na mpango namna gani Watanzania wanatumia nishati tofauti na mkaa, ili kulinda misitu yetu, tunakwenda kuwa jangwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la umeme. Nashukuru kwamba, umeme wa REA umeanza kusambaa maeneo mbalimbali, lakini ule umeme sasa hivi umekuwa ni ‘kimulimuli’ kwa sababu, ikinyesha mvua umeme hamna kwa sababu, speed yake ni ndogo na nguvu yake ni ndogo. Tunaiomba Serikali kwenye mpango wa maendeleo ujao uje na mpango mkakati wa kujenga sub- stations maeneo mbalimbali kwa ajili ya kupokelea umeme na kusambazwa maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ukienda Kaliua pamoja na kuwa walipata faraja wamepata umeme, lakini mvua ikinyesha unakatika, jua likiwa jingi unakatika kwa hiyo, hauna tija. Tunasema tunazungumzia uchumi wa viwanda, hatuwezi kuwa na uchumi wa viwanda kama umeme siyo wa uhakika. Kwa hiyo, naiomba Serikali ikiwepo kujenga kituo cha sub-station pale Kaliua pamoja na Urambo, mpango ambao umekuwepo tangu mwaka jana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba kwenye mpango ujao ukatekelezwe huu umeme wa REA ambao tunaendelea kuupata uweze kuwa na tija kuendesha viwanda vidogovidogo, lakini pia kuweza kusaidia wananchi kuweza kuutumia, usije ukawa ni kama mapambo, kama ambavyo sasa hivi unaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la Vitambulisho vya Taifa. Mpango huu umeanza tangu mwaka 2019, mpaka leo ni miaka tisa speed yake ni taratibu sana. Tunajua umuhimu wa Vitambusho vya Taifa. Kwanza ni uraia wa Mtanzania, lakini pili tunaweza kutumia kwa ajili ya kupata huduma mbalimbali. Leo ndani ya Taifa letu kuna watu wanaingia kinyemela kwenye mipaka wanaishi Tanzania kwa amani, kwa furaha, sio raia wa Tanzania. Hiyo ipo kabisa, ni nchi pekee ambayo unaweza kukuta kitu kama hiki. Kwa nini speed ya vitambulisho vya Taifa inaenda taratibu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulitenga fedha nyingi sana zaidi ya milioni 200 kipindi kile, lakini mpaka leo speed ni taratibu sana. Bahati mbaya sana sasa hivi wananchi wanadaiwa fedha, ili uweze kuandikishwa utoe sh.5,000/=, sasa hivi mtu ananunua hata uraia wake kwa kweli, is nonsense.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaiomba Serikali, kwanza suala la kuwalipisha wananchi kujaza fomu kwa ajili ya Vitambulisho vya Taifa liondoke, lakini pia mchakato huu ufike mwisho. Tuambiwe kabisa kwamba, idadi ya Watanzania wangapi mpaka leo wamepata vitambulisho vya Taifa, ni haki yao na siyo ombi. Tunaomba litekelezwe tuache kwenda speed ya taratibu kiasi hiki kwa suala la umuhimu kama kupata Vitambulisho vya Utaifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la uanzishwaji wa Bandari ya Samaki. Tumekuwa tunaongea na kwenye mpango wa Waziri haipo. Tumekuwa tunasema njia tunayopoteza mapato mengi sana ni njia ya bahari kuu, uvuvi wa bahari kuu almost ni shamba la bibi, wanakuja wanavuna wanaondoka; hatujui wamevuna wangapi, mafuta wanajaza hukohuko, tumekuwa ni rasilimali ambayo hatuilishi iko pale ni kuiuza, kuisimamia na kupata fedha, tumeshindwa Serikali. Tunaiomba kwenye bajeti ijayo Serikali ije na Mpango wa Kujenga Bandari ya Samaki tuweze kuhakikisha bahari kuu samaki wale wananufaisha Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuache kuwa wazembe kiasi hiki. Ni miaka mingi, lakini kila mpango ukija haipo. Kwa hiyo, ni matarajio yangu kwamba, mwakani kwenye mpango huu unaokuja Waziri atatujia na mpango mkakati, mpango maalum kuhakikisha kwamba, tunakuwa na Bandari ya Samaki tuweze kuongeza Pato la Taifa, lakini pia tunufaike na rasilimali ambayo wenzetu wananufaika nayo wanakwenda kutajirika, sisi tunaendelea kuwa ni maskini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kilimo. Ni kweli kilimo ni uti wa mgongo wa taifa letu, lakini kilimo chetu hakiendani na neno lenyewe uti wa mgongo. Kwanza kilimo cha Tanzania bado ni kilimo ambacho kinatumia jembe la mkono kwa kiasi kikubwa, lakini ni kilimo ambacho hata mazao yanayopatikana hayana masoko. Leo imekuwa ni kilio sasa mwananchi ananunua pembejeo mwenyewe, ananunua kila kitu mwenyewe, hata masoko ya mazao hakuna. Imekuwa ni maumivu makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ndani ya Mkoa wa Tabora particularly Wilaya ya Kaliua na maeneo mengine watu wanalia machozi, wamelima kwa jasho, wamevuna, leo tumbaku iko kwenye ma-godown haina soko, inaharibika, inashushwa thamani. Leo Serikali inasema habari ya kilimo, utasema nini kwa habari ya kilimo?(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba tuwe na mbinu na mikakati ya kuandaa masoko ya kilimo mapema kwa sababu, tunakwenda kwa takwimu ni lazima tujue tuna wakulima idadi gani, watazalisha kitu gani, tuwe tumejipanga kupata masoko ya uhakika kupitia kilimo cha mbaazi, kilimo cha mahindi, ni kilio kwa sababu tunahamasisha kilimo, lakini tuwe na mikakati ya masoko ya uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ni lazima tuhakikishe kwamba, kilimo cha Watanzania kinakuwa ni kilimo ambacho kinatumia mechanization siyo kilimo cha jembe la mkono ambacho ni cha muda mrefu na pembejeo zipatikane kwa wakati ili watu walime kwa tija na waweze kunufaika na kilimo ambacho asilimia zaidi ya asilimia 75 kubwa ya Watanzania inategemea kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango ujao ni lazima kila zao la biashara tuwe tumeambiwa kwamba, masoko yako wapi ya uhakika. Sasa hivi naiomba Serikali sana tatizo la tumbaku ambalo liko sasa hivi Serikali ihakikishe namna yoyote kuhakikisha tumbaku ile inapata masoko, pia itafute madawa ipeleke kwa ajili ya kwenda kuitunza isiendelee kuharibika na ikiwezekana Serikali iinunue iitunze kwenye ma- godown yake wananchi wapewe fedha waendelee na maisha yao. Leo watoto wao hawaendi shule, leo wameshindwa hata kumudu vyakula, lakini tumbaku iko ndani na ni zao ambalo walihamasishwa walime.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati mbaya sana majibu anayotoa Waziri wa Kilimo yanasikitisha sana kwamba, watu walilima bila kuwa na makisio na anajua ni kwa nini watu walilima bila makisio. Sio majibu ya Waziri ya kutoa. Kwa hiyo, tunaomba aje na majibu mazuri, Serikali ije na majibu mazuri ni kwa nini tumbaku ya wakulima Tabora na mikoa mingine hainunuliwi wakati walihamasishwa kulima na wamelima kwa nguvu zao peke yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la utafiti. Huwezi kuwa na nchi ya maendeleo endelevu, ukawa na kilimo endelevu, ukawa na viwanda, ukawa na elimu nzuri bila kuwa na utafiti. Tumekuwa wazembe kama Taifa kuwekeza kwenye utafiti. Tunaomba bajeti ijayo tuhakikishe tunawekeza vizuri kwenye utafiti, vyuo vyetu vya utafiti nchi nzima viko hoi, miundombinu imeharibika, tunao wataalam wako pale wana elimu nzuri, hatuwatumii kwa sababu, hatuwekezi kwenye utafiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni lazima kama Taifa tuwekeze kwenye utafiti tuweze kufanya kila kitu kwa kutumia utafiti, watu walime kwa utafiti, watu wauze kwa utafiti, watu wasome kwa kufanya utafiti. Suala la mwisho katika utafiti, vituo vyote vya utafiti vikarabatiwe pia, kuwepo na nyenzo na vitendeakazi elimu ambazo ziko pale na wataalam wale waweze kutumika vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni suala la mikopo kwa elimu ya juu. Kiukweli kuna matatizo makubwa na wananchi wa Tanzania, wonyonge, maskini, wanalia sana. Nilifikiria kwamba, Serikali iliposema kwamba, kila mtoto anayekidhi vigezo atakwenda kupata mkopo, ni kweli ingekuwa hivyo, lakini leo wako wengi wamekidhi vigezo, lakini wamekosa mikopo. Unaposema unawapa watoto elfu 30 wakati umeacha elfu 37, majority wamerudi mitaani wanakwenda kufanya nini, hakuna mitaji ya biashara, wameshamaliza kusoma Form Six, kilimo hakilipi, wakilima biashara hamna, wakilima masoko hamna. Kiukweli hawa asilimia zaidi ya 30,000 ni wengi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaiomba Serikali ifanye utafiti wa kutosha kila mwaka ihakikishe kwamba, mwaka ujao wana-pass wanamaliza vyuo wanafunzi wangapi, form six na wataingia wangapi, ili ijipange kuendana na idadi ya watu ambao wanakidhi vigezo vya kuweza kupata mikopo. Vinginevyo itaendelea kuwa ni vurugu kwa sababu, kila mwaka watoto wetu wanaandamana, wanapigwa kwa sababu, ni haki yao wanadai.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni kwa kuwa watoto wanatamani kusoma na kitu pekee ambacho mzazi au Taifa unaweza kumpa mtoto wako ni elimu, vingine vyote ni bure, ukishindwa kumpa elimu ni basi. Kwa hiyo, pale ambapo watoto wetu wanamaliza shule wana matarajio ya kupewa elimu, basi Serikali ijipange vizuri iweze kutoa mikopo, ili kila mtoto mwenye kigezo cha kuweza kupata elimu apate elimu kwa ajili ya maisha yake ya hapo baadaye. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi hii.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru nami kwa kunipa nafasi niweze kuchangia hoja ambayo iko mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi hakuna Mtanzania yeyote mwenye akili timamu, mpenda maendeleo ya Taifa lake, anayependa Taifa hili, anayeweza kupuuza juhudi zinazofanywa kwa ajili ya kusaidia kuokoa rasilimali za Tanzania, hakuna. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya Bunge hili wapo Wabunge ambao wana miaka 30, wengine 25, wengine tuna miaka 10. Kilio chetu, miaka yote ndani ya Bunge hili ni juu ya sekta ya madini kugeuzwa kuwa shamba la bibi miaka yote. Kwa miaka yote sekta hii imekuwa hainufaishi Taifa, tumekuwa tunaomba mikataba ije ndani ya Bunge hili miaka yote. Tumekuwa tunapewa majibu na Serikali ilizopita kwamba mikataba ya sekta ya madini ni siri kali. Tulikuwa tunauliza hii siri anafichwa nani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiangalia sekta hii na namna ambavyo Watanzania hata wale wanaozunguka maeneo ya madini wanavyonyanyasika, wanavyoumia hawana maji, barabara zinabomolewa hawatengenezewi ni suala la uchungu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, yale ambayo tuliyokuwa tunayaomba miaka yote hayafanyiwi kazi, nikiona leo anatokeza mtu, Rais anaweza kuyafanyia kazi angalau kwa hatua za mwisho, mimi binafsi napongeza, napongeza juhudi yoyote kuhakikisha kwamba rasilimali ya Watanzania inanufaisha Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachokiomba maamuzi yote, mapendekezo yote likiwepo la kuleta mikataba Bungeni ije haraka Wabunge tuipitie sisi ni wawakilishi. Unapoingia kwenye nyumba yako hata kwa maisha ya kawaida, ukikutana na changamoto huwezi kutatua zote kwa wakati mmoja unakwenda step by step. Kwa hiyo, tumeanza na hili hapa, ije mikataba yote tatizo kubwa ni kwenye mikataba ndiko tunapopigwa madini, mchanga wa makinikia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, imefikia hatua kuna mikataba ya madini imekwenda kuingiwa Ulaya, Karamagi hapa alipeleka mkataba Uingereza kwenda kusaini, una mbuzi wako baada ya kuita mnunuzi ndani ya nchi yako unambeba unampeleka kwenda kumuuzia nje ya nchi ulifanyika ufisadi. Kila aliyeweka kidole chake kiwe ni kidole kidogo, kikubwa chochote lazima ashughulikiwe vizuri ihakikishwe kwamba adhabu inatolewa ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye hotuba ya Waziri kuendelea kushuka kwa shilingi ya Tanzania. Katika hotuba ya Waziri tumeona kwamba shilingi ya Tanzania inaendelea kushuka na tumekuwa tunazungumza hapa Bungeni hatuoni mikakati kama Taifa, hakuna mikakati ya kuweza kudhibiti kuporomoka kwa shilingi ya Tanzania na kuporomoka kwa shilingi yetu kunasababisha mambo mengi yanakwenda vibaya, kunasababisha kupanda kwa vyakula na mambo mengine kama hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunashangaa ni Tanzania pekee ambapo dola ya Marekani inauzwa kama njugu mitaani, ni Tanzania pekee ambapo Bureau de Change, vioski vya kubadilisha fedha vipo kila kona kama vioski vya soda. Tanzania pekee unaweza kuona kwamba bidhaa zinanunuliwa kwa fedha ya nje, nendeni nchi nyingine hata hapa Kenya huwezi kutumia shilingi ya Tanzania kununua kitu Kenya huwezi! Tumejisahau kama Taifa na kwa kweli hapa nasema, Gavana wa Benki Kuu ameshindwa kabisa kusimamia kuporomoka kwa shilingi ya Tanzania, kabisa nasema kila siku, ni kwa nini tunashindwa kusimamia?(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri tunataka mikakati sio kila siku bajeti tunasema kwamba shilingi inaporomoka, tuilinde shilingi yetu tusikubali fedha za nje ije i- overhaul shilingi ya Tanzania. Tunaomba sana shilingi yetu iendelee kupanda ipande kwa sababu inazidi kushuka matokeo yake kama Taifa kiuchumi inaathiri uchumi pia inaathiri maisha ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hali ya uchumi, nimesoma kitabu cha Mheshimiwa Waziri cha hali ya uchumi wa Taifa, ukiangalia mazao mengi ambapo yalikuwa yanaingizia pato kubwa kwa Taifa hii, page 49, mazao mengi yamepungua sana kusafirishwa nje, tukianza na kahawa, kuna cocoa kuna mazao mengi kuna katani, kuna pamba. Kutokusafirisha mazao mengi ina maana uchumi wetu unazidi kwenda chini, kwa nini tunashindwa kusafirisha mazao kwa sababu tumepunguza mapato, mazao yapo kidogo ndani ya nchi yetu kwa sababu hatujaweza kuwekeza vizuri kwenye kilimo hiyo ni ishara tosha, kupungua kusafirisha mazao nje hatuwekezi vizuri na kama hatusafirishi sisi tunakuwa ni masoko kuonyesha kwamba tunauza vitu vya wenzetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima kama Taifa tuweze kuinua sekta ya kilimo hakuna namna nyingine. Tuinue sekta ya kilimo tuhakikishe kwamba mazao yote ambayo ukisikia leo Mkoa wa Kilimajaro umeendelea ilikuwa ni kahawa, leo Kagera Bukoba ni kahawa, ndizi, ukisikia Mbeya wameendelea ilikuwa ni cocoa, tumeyasahau yale mazao tumeyaacha. Leo mkulima wa kahawa anang’oa kahawa kwa sababu pembejeo ni ghali hawezi kununua, Serikali haiangalii, kwa hiyo hatuwezi kuinua kilimo kama tunashindwa kuhakikisha kwamba pembejeo zinapatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri amesema amebadilisha mifumo kwa ajili ya kutoa pembejeo, tulikuwa tunatumia mfumo wa voucher ukawa ni hasara kubwa wakulima hawanufaiki. Tukaja na mfumo mwingine Serikali ikasema itaunda vikundi then itoe dhamana benki vikundi vikakope benki, mfumo ule haukutekelezwa, matokeo yake mwaka uliopita mpaka ndani ya Wilaya yangu Kaliua watu hawakupata pembejeo kwa sababu Serikali haikupeleka pembejeo na waliopewa kusambaza pembejeo hawakupeleka kwa wakati. Kwa hiyo, lazima kama Taifa tuwe na mfumo ambao ni endelevu na ni wa uhakika kuhakisha kwamba wakulima wetu wanapata pembejeo kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta nyingine ni sekta ya mifugo, Tanzania ni nchi ya tatu Afrika kuwa na mifugo mingi, lakini kwa bahati mbaya sana mifugo yetu hatujaweza kuitumia vizuri kuongeza kipato cha Taifa. Leo wafugaji wamekuwa wanatangatanga hapa na pale, mifugo imeaachwa inazagaa karibu nchi nzima, hakuna maeneo yaliyopimwa kwa ajili ya wafugaji, hakuna malisho, hakuna viwanda, hakuna kuchakata mazao yao, hatujaweza kutumia sekta ya mifugo vizuri. Nilitegemea bajeti kama ya leo Waziri angekuwa anatuambia mifugo yenyewe inaingiza zaidi ya robo percent kwa sababu tunayo mifugo mingi inakufa tu, wakati wa ukame inateketea yote kwa sababu hatujaweza kujizatiti vizuri kwenye mifugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunazo ranchi za Taifa, ranchi zile Serikali haiwekezi chochote, ranchi zimekuwa ni mapori majengo yale yanaharibika, tunaiomba Serikali kama wameshindwa kuwekeza kwenye ranchi za Taifa wayagawe yale maeneo wawape wafugaji, waweze kufungua ranchi zao kule wafuge kisasa Serikali inufaike. Kuacha yale maeneo yanateketea wakati wafugaji wanasambaa nchi nzima, siyo sahihi na wala hatuangalii uchumi wa Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la Serikali kubana matumizi au udhibiti wa upotevu wa fedha za Serikali. Serikali imesema huku nyuma kwamba itahakikisha samani zote za Serikali za ofisini, samani zote za ofisi za Serikali kuanzia Serikali Kuu mpaka Local Government wananunua samani kutoka ndani ya nchi. Pia tumeambiwa huko nyuma kwamba watanunua magari ya bei ya kawaida sio mashangingi lakini leo yote hayo hayafanyiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunamwomba Mheshimiwa Waziri atuelekeze ni kwa nini Tanzania hii tuna mbao nzuri, tuna vijana wenye uwezo, tuna viwanda vidogo vidogo wanazalisha samani, Serikali inanunua samani za Kichina ambazo ni low quality ni expensive na hazina ubora, wakati huo tuna viwanda vidogo vidogo ndani ya nchi yetu wanashindwa kununua. Tunao Magereza, tunao JKT, tunao vijana wote wana capacity nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Mheshimiwa Waziri aje atuambie ni lini Serikali itaacha utaratibu wa kuagiza fanicha/samani kutoka nje ya nchi za Kichina na kuhakikisha kwamba zote zinanunuliwa ndani ya nchi yetu, ili tuweze kutoa ajira kwa vijana lakini pia tuweze kulinda viwanda vya ndani vidogovidogo na hivyo kuweza kuinua uchumi wetu ndani ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu sekta ya utalii, tunayo rasilimali nyingi sana tuna vivutio vizuri ndani ya nchi yetu, tatizo kubwa hatuwekezi vya kutosha. Ukiangalia hapa Ruaha National Park ni National Park kubwa kuliko nyingine zote Afrika, lakini National Park ile barabara ya kutoka Iringa tu kwenda Ruaha Serikali zaidi ya miaka 15 mmeshindwa. Matokeo yake watalii hawaendi kule. Hebu tuhakikishe tunawekeza kwenye utalii tunavyo vivutio vizuri, leo sio watu wa kushindwa na Kenya, inatushinda kwa ajili ya kipato cha utalii kwa sababu hatuwekezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huwezi kuvuna pasipo kupanda, lazima tupande tuweze kuvuna. Kwa hiyo, naiomba Serikali tuwekeze vizuri kwenye sekta ya utalii, tuweze kuvuna vizuri kwenye utalii. Nina imani kabisa kwamba kwa vivutio vyetu vilivyo vizuri kuliko nchi zote za Afrika tunaweza tukaingiza kipato kikubwa na hivyo kuongeza uchumi wa nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mabadiliko ya tabianchi, sijaona hotuba ya Mheshimiwa Waziri namna gani ya kuweza kudhibiti au kupambana na mabadiliko ya tabianchi ndani ya nchi yetu. Climate change ni suala la Kitaifa, nchi zote duniani wamejiwekea mikakati kwenye nchi zao kwa njia namna gani ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi, leo ndani yetu tunaona jinsi gani tutapata madhara makubwa kwa mabadiliko ya tabianchi, tumeona tetemeko kule Kagera limeua watu, mafuriko kila siku...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kunipa nafasi ili niweze kuchangia Hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Niungane na Waheshimiwa wa Bungeni na Watanzania wote kumshukuru Mungu kwa kukupa afya njema, tunaomba aendelee kukutetea na kukupigania katika majukumu yako.

Mheshimiwa Spika, niishukuru sana hiyo kauli ya Serikali ambayo imetolewa leo hapa Bungeni asubuhi kwa ajili ya kuwarejesha watumishi wa umma ambao waliondolewa kinyama kwenye kazi zao, kwa kweli nashukuru sana, tumerudisha imani na matumaini kwa wale watendaji.

Mheshimiwa Spika, mwaka juzi Serikali ilikuja na mkakati kuhakikisha kwamba watoto wote wa Kitanzania wanakaa kwenye madawati na ikawezekana. Hata hivyo, hivi tunavyoongea watoto wengi wa Tanzania kutokana na idadi kuwa wengi, wengi wao wanakaa nje, jua linawapiga, mvua yao, jua lao.

Mheshimiwa Spika, tunaiomba Serikali, kwa mpango ule ule iliyokuja nao 2016/2017 watoto wakaweza kukaa kwenye madawati wote, tunaomba Serikali ije na mkakati maalum kuhakikisha watoto wote wanakaa kwenye madarasa. Katika wilaya zote hakuna sehemu ambapo madarasa yanatosha na kiukweli mtoto anayesoma nje hata ufaulu unakuwa ni mdogo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni suala la vyakula mashuleni. Kutokana na tamko lililotolewa na Serikali kwamba elimu ni bure wazazi na walezi wameona kwamba hata jukumu la vyakula shuleni ni jukumu la Serikali, kwa hiyo watoto wengi sasa hivi hawali shuleni na mtoto ambaye ana njaa hafundishiki. Tunaiomba Serikali itoe ufafanuzi mzuri kwenye shule namna gani wazazi wahakikishe watoto wanakula shuleni.

Mheshimiwa Spika, ni ukweli kwamba tumepanda kielimu kwa maeneo mengi particularly kwenye Wilaya yangu ya Kaliua tumepanda vizuri sana na najua tumechangiwa na Walimu lakini pia watoto kula mashuleni na speed ya viongozi kufanya kazi; lakini sasa hivi wameacha kula tumeona trend yao imeanza kushuka.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tunaomba Serikali itoe ufafanuzi mzuri namna gani watoto waanze kula shuleni tukizingatia wengi wao wanatoka nyumbani hawajala mpaka jioni wana njaa, kwa hiyo hawawezi kufaulu vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni suala la mifugo. Nchi yetu ni nchi ya pili kuwa na mifugo mingi Afrika, lakini ukiangalia pato la Taifa ambalo linaletwa na sekta ya mifugo bado ni dogo sana. Tatizo ni kwamba pamoja na kuwa tunaongoza kwa kuwa na mifugo mingi, lakini mifugo yetu haina tija kwa sababu hakuna maeneo yanayopangwa popote kwenye mikoa wala wilaya kwa ajili ya malisho ya mifugo.

Mheshimiwa Spika, katika maeneo mengine mifugo inaonekana kama ni changamoto, wanaonekana wanazurura na kila siku wanakamatwa na wanapigwa risasi huko kwenye hifadhi. Hatujaweza kama Watanzania kutumia rasilimali ya mifugo kama uchumi wa Taifa.

Mheshimiwa Spika, naiomba sana Serikali lazima kwenye bajeti hii tuje na mpango mkakati namna gani kila mkoa na wilaya ambao wanaendeleza mifugo watenge maeneo kwa ajili ya mifugo.

Mheshimiwa Spika, lingine ni kwamba, hakuna malisho, wakati wa mvua nyingi malisho yanajaa, ikiondoka mvua mifugo yote inateketea, kwa hiyo Mfugaji anafuga wakati wa mvua wakati wa ukame mifugo yote imepotea. Tunaiomba Serikali ije na mpango wakati wa mvua tuwe na utaratibu wa kuvuna majani tutengeneze hay, tutengeneze silage tutunze vyakula ili tufuge kwa tija.

Mheshimiwa Spika, lingine tuwe na viwanda. Tulikuwa na viwanda vya kuchakata mazao ya mifugo. Tulikuwa na Tanganyika Packers leo hamna. Ni kweli sasa hivi tunajitahidi kuwa na machinjio ya kisasa, lakini hatuna viwanda vya kuchakata mazao ya mifugo.

Mheshimiwa Spika, bahati nzuri kwenye mifugo kila kitu ni mali. Kwato, ngozi, nyama, mifupa, kila kitu ni mali. Tukiweza kutumia vizuri sekta ya mifugo tutaweza kuhakikisha kwamba inaingiza pato zuri kwa Taifa letu na tukaweza kufanya wafugaji wakawa ni watu ambao wana tija siyo huku wananyanyaswa kila siku kwa sababu Serikali haijaweza kuweka mfumo mzuri wa mifugo kwenye nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni Mfuko wa Wanawake na uwezeshaji wa wanawake wa vijana. Tumeiona hapa Serikali imetenga fedha milioni mia saba themanini na tatu kwa ajili ya vijana ambapo vijana 840 kutoka halmashauri mbalimbali wamenufaika. Vijana 840 ni kijiji kimoja au viwili. Leo tuna vijana wangapi Tanzania, tuna wilaya ngapi, tuna kata ngapi, tuna vijiji vingapi? Kuja na vijana 840 mimi nashangaa.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali, fedha zinazotengwa kwenye halmashauri ni kidogo sana. Leo Kaliua tumetenga zaidi ya milioni mia mbili hamsini, vijana wenyewe wamekuja na vikundi hamsini, hatukuweza kuwapa wote tumewapa vikundi 15. Wanawake wamekuja na vikundi 56 tumewapa vikundi 30 na wanaomba milioni kumi unawapa milioni mbili, haitoshi.

Mheshimiwa Spika, ni kweli tunatenga lakini kwa kweli kama hatujajizatiti vizuri Serikali hatuwezi kusaidia vijana wakaweza kujiajiri, hatuwezi kusaidia wanawake wakaweza kujiajiri kwa sababu fedha tunayotenga ni kidogo. Halmashauri zetu tunafahamu uwezo wake, hawana uwezo wa kuweza kusaidia vikundi vyote vinavyoundwa. Kwa hiyo naiomba Serikali, lazima itenge fedha ya kutosha ili wanawake wawezeshwe, vijana wawezeshwe ili nchi yetu iondokane na kundi kubwa ambalo linakosa ajira na waweze kuendeleza familia zao.

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni suala la kilimo; nazungumzia kidogo kwa sababu nitazungumzia kwenye sekta ijayo. Tuna shida kubwa Taifa letu, hatujaweza kuwa na mizani ya kisasa kwenye manunuzi ya mazao, tumelia Bungeni na mimi binafsi nimeongea sana hapa. Leo bado wakulima wanakwenda kulaliwa kule vijijini, wakulima wanakwenda kununuliwa mazao yao bila mizani ya uhakika.

Mheshimiwa Spika, vile vile leo lumbesa inaendelea, pia kuna ndoo za Mozambique, mkulima analima kwa shida, anavuna kwa shida hata kwenda kuuza anaibiwa. Naiomba Serikali kwa nini tunashindwa kusimamia mizani ya kisasa kwa ajili ya kununua mazao? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa nini Serikali inaruhusu lumbesa mpaka hivi leo dunia ya leo, kwa nini Serikali inaruhusu Mozambique ndoo moja inachukua mpaka galoni saba, kwa nini inaruhusu? Hatuwezi kuwa na nchi ya viwanda bila kuwa na kilimo chenye tija. Pia tunahitaji wakulima wanufaike na wanachokilima, tunaiomba Serikali ije na mpango, ituambie kwa nini tumekubali wakulima waendelee kuibiwa wakati wakulima hao hao tunawategemea waendeleze Taifa hili.

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni maji; katika Wilaya ya Kaliua bado hatuna mpango mkakati wa kupata maji. Mpango wa Ziwa Victoria kutoa maji kutoka Mto Malagarasi ni mpango wa muda mrefu. Leo ni mwaka wa tano bado mpango huu uko kwenye upembuzi yakinifu. Naiomba Serikali kwenye mpango wa mwaka huu ituletee mpango wa muda mfupi kuwatua wanawake wa Kaliua ndoo kichwani.

Mheshimiwa Spika, leo mvua zinanyesha ukienda Kaliua akinamama angalau wanatulia, watoto wanaenda shule, njoo mwezi Agosti ni hatari. Kwa hiyo naiomba sana Serikali ije na mpango huu mwaka huu tuhakikishe kwamba tunapata maji wanawake wa Kaliua, watoto waende shule kwa wakati na tuondokane na shida.

Mheshimiwa Spika, mpango wa Maji Victoria haufiki Kaliua wala Urambo, kwa hiyo mpango pekee wa kuwapatia wana Kaliua maji ni kutoka Mto Malagarasi lakini mpango huu unaenda taratibu sana na fedha inayopangwa pale ni ndogo haitoshelezi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni afya; Kaliua tunaishukuru Serikali imetutengea fedha kwa ajili ya hospitali yetu ambayo tunategemea kujenga Kaliua, lakini pia Kaliua mpango wetu wa mwaka huu ni kuwa na vituo vya afya, tumeongeza vituo vya afya vinne, viwili Ulyankulu, viwili Kaliua, Jimbo langu.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali, wananchi sasa hivi wanacheka kwa speed kubwa Mheshimiwa Rais alivyofika Kaliua alitoa milioni kumi kwa ajili ya kituo cha Kaliua Usinge ambapo wengi wao wanatibiwa kule Nguruka.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali iongeze nguvu kwenye kituo cha Usinge ili wananchi ambao wanatibiwa Nguruka waweze kutibiwa pale kwenye kituo cha Usinge iongeze nguvu ya Rais. Mfuko wa Jimbo tumeongeza, wananchi wanachanga sana kila siku, Rais ameweka nguvu tunaomba na Serikali pia itusaidie mwaka huu tuhakikishe kwamba kituo kile kinakamilika ili wananchi wa Kaliua waweze kupata huduma za afya kwa karibu.

Mheshimiwa Spika, nizungumzie hata hapa Dodoma. Benjamin Mkapa wanafanya kazi nzuri sana ya kuokoa wananchi na pia Wabunge wenyewe, lakini Madaktari hakuna. Hivi sasa ninavyoongea kuna Mbunge amelazwa pale…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi nami niweze kuchangia kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, nianze na suala la barabara, lakini kwanza nianze na fedha iliyotengwa kwa ajili ya Mfuko wa Barabara kwa Mkoa mzima wa Tabora. Kwenye kitabu cha Mheshimiwa Waziri ukiangalia fedha iliyotengwa kwa Mkoa wa Tabora barabara za ndani ni milioni mia nane themanini na tano tu, lakini ukiangalia Mkoa wa Tabora kwa Tanzania ndio mkoa unaoongoza kuwa mkubwa kwa sasa hivi kuliko mikoa yote na ni mkoa ambao una mzunguko mkubwa sana wa barabara tofauti na maeneo mengine.

Mheshimiwa Spika, fedha iliyotengwa na hali ya barabara za Mkoa wa Tabora ni hatari sana kwa mwaka huu mzima. Iko mikoa mingine wamepata mpaka bilioni mbili, tatu, moja point, kwa Mkoa wa Tabora kuwapa milioni mia nane themanini na tano ni fedha kidogo sana.

Mheshimiwa Spika, tunaomba Wizara iuangalie Mkoa wa Tabora kwa jicho la pekee. Hivi tunavyoongea kuna maeneo ambayo hayapitiki kabisa wananchi wanaogelea, hali ya uchumi ni mbaya, mazao hayasafirishwi kwenda mjini kwa sababu barabara zile ni mbovu sana.

Mheshimiwa Spika, specifically nizungumzie barabara ya kutoka Kaliua na hasa eneo ambalo linatoka pale Kazilambwa Kaliua kwenda Chagu ambako ni mpakani mwa Uvinza Mkoa wa Kigoma. Barabara hii ni mbaya sana na nimekuwa nikiomba ipatiwe fedha za kujengwa kwa kiwango cha lami. Hivi ninavyoongea na wiki nzima iliyopita sikuwepo hapa Bungeni kwa sababu nilikuwa jimboni. Hali ni mbaya kweli kweli; watoto, wagonjwa, wazee wamekaa pale zaidi ya siku nne kwa sababu ya barabara.

Mheshimiwa Spika, TANROAD Mkoa wamejitahidi kurekebisha eneo moja, hilo ni eneo moja tu. Barabara hii imekatika maeneo manne tofauti, hivi tunavyoendelea huku ni bahari, huku ni bahari. Kwa mvua zinazoendelea barabara ile yote inaenda kuteketea mwaka huu. Ukiangalia barabara ya Mpanda imekatika, magari yamekuwa yakitumia kutoka Tabora kwenda Kaliua na kwenda Mpanda, leo haipitiki, Kaliua kwenda Tabora haipitiki, Watanzania watateseka sana.

Mheshimiwa Spika, tunaomba Serikali, nilikuwa naangalia pia kwenye kitabu, ukiangalia fedha iliyotengwa kwa fedha za ndani kwenye barabara kuu kwa Mkoa wa Tabora ni barabara mbili tu na mojawapo ni Kaliua kwenda Puge na fedha iliyotengwa ni milioni saba, inafanya nini kwa uharibifu ule?

Mheshimiwa Spika, naomba Mheshimiwa Waziri aangalie, kwa Kaliua kwa kweli inahitaji special priority mwaka huu, vinginevyo tutakuwa ni kisiwa. Barabara zote hazipitiki za ndani hazipitiki, barabara kuu hazipitiki, wananchi wale wako katika hali mbaya sana sana.

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni suala la kampuni hizi za ujenzi. Tumekuwa tunashuhudia kampuni za ujenzi zinapewa tender zinakwenda kuchukua material kwa ajili ya kujenga kwenye vijiji huko changarawe, mawe, mchanga lakini bahati mbaya sana wanapokabidhi kazi baada ya ujenzi hawatengenezi zile barabara wanaziacha zikiwa katika hali mbaya sana.

Mheshimiwa Spika, mfano mkubwa ni wa Kaliua, Kampuni ya Chico ilipewa mradi kutengeneza barabara ya Kazilambwa kuja Kaliua Mjini, wamekwenda kuchukua kokoto kutoka Igwisi; kwanza wamemaliza, tumepiga kelele sana kwenye halmashauri na hata hapa Bungeni, kwamba watengeneze barabara ya Igwisi kuja Kaliua, lakini wamemaliza kazi, wamekabidhi kazi barabara ile sasa hivi ni mashimo ni mahandaki, hakuingiliki na wameshaondoka tayari.

Mheshimiwa Spika, tunaiomba Serikali bado Chiko wamepewa kazi nyingine Mkoa wa Tabora, waelekezwe wakatengeneze barabara ya Igwisi kuja Kaliua, ni barabara ya uchumi lakini kwa hali ambayo imeachwa ni hali ambayo ni mbaya sana.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia TARURA wanapewa fedha ndogo, hazitoshi kutengeneza zile barabara ambazo zimeharibiwa na Chico lakini wameondoka wameachia madhara makubwa pale. Pia hata fedha ya wananchi wa Igwisi ambapo walichukua kokoto na mchanga pia hawakuwapa stahili zao kama walivyokubaliana kwenye mikataba yao.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali itoe agizo, kampuni zote zinavyopewa tender kabla ya kukabidhi kazi na kupewa certificate ya mwisho wahakikishe kwamba wanatengeneza barabara na kufukia mashimo ili waweze kuacha mazingira yale yakiwa katika hali nzuri.

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni kuhusu uharibifu wa miundombinu barabani. Tumekuwa tunashuhudia barabara zetu zinatengenezwa kwa gharama kubwa sana lakini kiukweli zinaharibika sana sana na zipo taarifa za uhakika kwamba miundombinu yetu ya barabara inahujumiwa kwa namna ya kutumia kwamba ni screpa. Zipo taarifa kwamba vifaa vingi ambavyo vinaingia barabarani vinapelekwa kwenye scraper.

Mheshimiwa Spika, hebu Serikali tuangalie tunawezaje kuruhusu scraper mpaka zinapelekwa kwenye viwanda? Viwanda tunavijua, vinatengeneza chuma katika maeneo mbalimbali lakini vinatumika vifaa vya ujenzi barabarani, zinatumika alama za barabarani, ni miundombinu ya barabani. Leo haiwezekani kuendelea kutengeneza gharama kubwa hivi wakati inahujumiwa na tunajua.

Mheshimiwa Spika, ninazo taarifa kwamba nyingine zimefikia Serikalini lakini hazipatiwi taarifa, nitakuja kuongea na Waziri nimpatie takwimu ni namna gani ambavyo barabara zinahujumiwa na baadhi ya watu wanafahamika, lakini hatua hazichukuliwi.

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni kuhusu reli. Niipongeze Serikali kwa hatua ambayo imefikia ya kutengeneza reli kwa standard gauge kutoka Dar es Salaam mpaka Morogoro pia Morogoro mpaka Dodoma na nina imani kwamba itatoka Dodoma itakwenda Kaliua na maeneo mengine.

Mheshimiwa Spika, hivi tunavyoongea bado mabehewa ni machache sana. Pamoja na kuwa kweli reli hii ni reli ya uchumi, reli hii, kama tunavyosema hatuwezi kuacha barabara kuharibiwa kama hatutengenezi reli zikawa imara. Pia reli inaweza ikawa nzuri ikawa inapitika lakini bado ikawa na mabehewa machache, Kaliua mabehewa ni machache sana na nimeongea na Waziri na yeye amefika jimboni ameona, wananchi wengi wanashindwa kutumia reli kwa sababu ya uchache wa mabehewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaiomba Serikali, Waziri aliagiza kwamba ataongeza bajeti kwa ajili ya kununua mabehewa, nilikuwa nategemea niione huku bajeti tuongeze mabehewa ili usafiri huu wa reli uweze kunufaisha wananchi wa Kaliua, Mpanda na maeneo mengine. Kwa sababu sasa hivi wanahesabiwa watu 15 mpaka 20 wakati wengi wao wangependa kusafiri na reli lakini wanashindwa wanatumia barabara ambapo pia hazina uhakika sana.

Mheshimiwa Spika, lingine, ni pale wasafiri watakapotaka kusafiri reli imepata matatizo, wananchi wanashindwa kupewa taarifa kwa muda. Hivi wiki iliyopita wako wasafiri wamekaa Kaliua siku tatu mpaka wakaandamana kwenda kwa Mkuu wa Wilaya, kwenda kwa Mbunge kwa sababu wana njaa wameishiwa, hawaambiwi taarifa zozote ikawa ni matatizo.

Mheshimiwa Spika, tunaiomba Serikali, kwa kuwa kuna communication nzuri pale inapotokea tatizo kwamba miundombinu ya barabara labda reli imekatika mahali waelezwe, tusisubiri waandamane waanze kulia na watu wanakuwa wameshateseka sana na wanaumwa na mbu. Tuwape taarifa kwamba reli itakuwa tayari siku fulani prior, kabla ya kuteseka na tuhakikishe kwamba wasafiri wetu wanaweza kusafiri kwa muda. Pia tuharakishe lile tatizo ambalo limetokea ili wasiendelee kuteseka. Kwa kweli ukifika pale Kaliua wakati ambapo reli imeharibika utaona uchungu, watoto wamelala chini, wagonjwa wamelala chini ni mateso ya hali ya juu.

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni kuhusu mawasiliano ya simu. Kwanza nashukuru kwamba kiukweli, hata mimi mwenyewe na wananchi wengi hawajui kwamba kuna mpango wa fursa za mawasiliano kwa wote ambao unajenga minara nchini.

Mheshimiwa Spika, sisi tulifikiri kwamba minara mingi inajengwa na kampuni za simu, lakini kumbe tuna mpango mzuri wa mawasiliano kwa wote ambapo unajenga minara. Kwa hiyo, kwanza naomba, kwa kuwa sisi kama Taifa tuna mpango wa mawasiliano kwa wote, tunaomba wahakikishe kwamba maeneo ambayo kampuni hazifiki wanafika waweke mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, hivi ninavyoongea Wilaya ya Kaliua kuna maeneo mengi sana hakuna mawasiliano ya simu mpaka upande juu ya mti, juu ya paa ndipo upate mawasiliano. Maeneo ya Igwisi, Mloka, Usenye, Usinge na maeneo mengine, nikihesabu hapa vijiji zaidi ya 20 hakuna mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, tunaiomba Wizara hii ijue kwamba mawasiliano sasa hivi ni uchumi, kama hakuna mawasiliano hakuna uchumi; huwezi kufanya biashara kama hakuna mawasiliano. Kwa hiyo tunaiomba Serikali ihakikishe kwamba inapeleka mawasiliano maeneo yote ya Kaliua ambayo hayana mawasiliano ili wananchi waweze kupata mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la mawasiliano ya redio; yapo maeneo ambapo hakuna radio kabisa. Tunaomba Serikali ihakikishe kwamba mawasiliano ya redio yanakuwepo, kwa sababu dunia ya leo kama hakuna mawasiliano ya simu wala redio ni kwamba unakuwa kisiwani.

Mheshimiwa Spika, kuhusu magari kujaza kupita uwezo. Tumekuwa tunalalamika, ukiona barabara zetu zilivyokuwa na mabonde; ni hatari kubwa, lakini ninachoshangaa ni kwamba tunayo mizani, sasa inafanya nini? Kwa nini tunaruhusu magari kujaza kupita uwezo licha ya kwamba pia barabara zinaharibika kwa haraka pia zinasababisha ajali?

Mheshimiwa Spika,Leo ukiwa unaendesha kutoka Morogoro kuja Dodoma unakutana na milima ndani ya barabara ingawa tunayo mizani. Naiomba Serikali tuhakikishe magari yanatii sheria…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nikushukuru sana kunipa nafasi hii niweze kuchangia kwenye Mpango wa Bajeti ambayo ipo mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na suala afya. Tunashida kubwa sana sana ya huduma ya afya watumishi wa afya almost ni Tanzania nzima, kiukweli baadhi ya huduma zimeporeshwa na hata dawa zimeongezeka hospitalini lakini watu wanafika hospitalini hawapati kuudumiwa kutokana kwamba hatuna watumishi wa afya. Kwa hiyo, naomba kwenye Mpango wa Maendeleo ujao lazima Serikali iyakikishe tumepata Watumishi wa afya wa kutosha maeneo yote ya Taifa hili kwenye zahanati, zahanati moja inakuwa na wahudumu wawili au mmoja, tunasema tunapunguza vifo vya akinamama na watoto, tumeporesha zahanati, lakini mama anafika pale anajifungulia nje kwa sababu mhudumu ni moja akaangaike na wagonjwa wa kawaida, akaangaike na mama anayejifungua, ahaangaike na mama mwenye mimba ni shida, tunaomba Serikali ije na mpango namna gani kuwakikisha nchi nzima maeneo yote tunakuwa na wahudumu wa kutosha wa afya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwenye mpango ujao uoneshe kabisa namna kuakikisha kwamba hospitali zote za rufaa na hospitali mikoa zinakuwa na vifaa tiba muhimu vyote kila hospitali iwe na CT Scan ya hali ya juu, x- ray ya kisasa, iwe na ultrasound ya kisasa na iwe na MRI ya kisasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Muhimbili saiv inafanya vizuri kwa sababu ina vipimo hivyo, lakini watu ni wengi na siyo wote wanaweza kuja Muhimbili, wengine wanapata shida huko mikoani walipo.

Kwa hiyo, ili kuwakikisha kwamba Watanzania wanapata vipimo watibiwe vizuri kwa kutokana vipimo vyao na uchunguzi wa kutosha kwenye mikoa yote wahakikishe kwamba kuna vifaa tiba vya kutosha na tuhakikishe hili kwamba tunalinda afya ya Watanzania na watatibiwa siyo kwa kubahatisha bali kuhakikisha wamepata vipimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la utafiti, kiukweli katika miaka yote tunashauri hapa Bungeni hata kuingia mikataba na mataifa mengine kuweza kutenga fedha asilimia kumi ya pato la Taifa kwenda kwenye utafifi bado hatujaweza kufanya kama Taifa, huwezi kuwa na maendeleo endelevu bila kuwekeza kwenye utafiti. Ili uende kwenye kilimo vizuri lazima utafiti, ufugaji utafiti, uvuvi utafiti, huwezi leo suala la kilimo limezungumziwa sana siwezi kulizungumzia, lakini leo ukiangalia wakulima wengi wanalima kwa kubahatisha tunahitaji utafiti kwenye kilimo, utafiti kwenye pembejeo, utafiti kwenye mbolea, kwenye udongo, kwenye masoko kila kitu ni utafiti, kwa nini Serikali aitengi fedha asilimia moja kwenda kwenye utafiti? Kwa hiyo, mpango ujao uoneshe namna gani tunatenga fedha one percent la pato la Taifa kwenda kwenye utafiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine tunaomba kwenye mpango ujao uoneshe namna gani ya kuunganisha mikoa yote kwa barabara za lami, mikoa yote kwa barabara za lami mpaka sasa hivi kuna baadhi ya mikoa ambazo hakuna barabara za lami hazijaunganishwa mkoa kwa mkoa barabara za lami kwa sababu nchi yetu ni nchi ya kilimo wakulima wanapata shida sana kusafirisha mazao kutoka kwenye mkoa mmoja kwenda kwenye mkoa mwingine hakuna barabara za lami, leo kule Kaliua unakuta kuna mahindi ya kutosha, lakini mkoa mwingine kuna shida ya mahindi, kuyapeleka inakuwa ni shida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuhakikishe kwenye mpango ujao namna gani ya kuhakikisha mikoa yote ya Tanzania na kwa barabara za lami, kwa mfano, Kaliua kuna barabara inayoanzia Katavi inakuja Kaliua inakuja Kahama inakwenda mpaka Rwanda, leo tuna mahindi ya kutosha Katavi, mahindi ya kutosha Kaliua lakini Rwanda wanahitaji mahindi barabara ingekuwepo ya kutosha imeunganishwa ingeweza kusafirisha masoko huko kuliko kutegemea pale pale au pale ndani ya mkoa kwa hiyo lazima mpango ujao uoneshe hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine tunakwenda kwenye uchumi wa kati lakini uchumi wa viwanda, hatuwezi kuwa na uchumi wa viwanda kama hakuna umeme wa uhakika na kutosha tena umeme wenye nguvu. Ni ukweli REA inajitahidi kuweza kusambaza umeme lakini ule umeme una nguvu ndogo, transfoma zilizowekwa ni ndogo, mvua ikinyesha ime-shake hakuna, unakuta hata viwanda vidogo ambavyo viko size ya welding, kusukasuka na kunyoa bado wale vijana hawafanyi kazi kwa uhakika kutokana umeme hauna uhakika. Kwa hiyo, kwenye mpango ujao wa bajeti lazima tuhakikishe namna gani tunakuwa na umeme wa uhakika, tunakwenda kwenye uchumi wa viwanda huwezi kuzungumzia viwanda kama umeme ni wa aina hii ambao tunao sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Serikali ije na mpango namna gani ya kuhakikisha kwamba tunajenga substation zote za kupokelea umeme na kusambaza umeme, kwa mfano pale Kaliua na Urambo kuna sehemu ya kujenga substation, ilikuwa kwenye mpango wa bajeti uliopita tunaomba itekelezeke ili tuweze kupata umeme wa kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala mazingira pamoja na mabadiliko ya tabianchi. Nimeangalia kitabu cha Mheshimiwa Waziri kina sentensi moja tu inayoonesha suala la mazingira na mabadiliko ya tabia nchi, hili suala la mazingira, hili suala la mazingira ni suala gumu na ni suala ambalo ni very serious, lakini kiukweli Serikali haijawekeza kwenye mabadiliko ya tabianchi na kupambana na mazingira kabisa na hata ukiangalia kwenye bajeti zilizotangulia mwaka juzi/mwaka jana fedha inayotoka kwenye bajeti ya Wizara ya Mazingira ni kidogo sana asilimia kubwa inakwenda Muungano lakini bajeti ya mazingira ni kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania imeshakuwa bare maeneo mengi, misitu inazidi kuteketea, mbao zinaondoka, lakini hakuna mkakati lakini tuna desasters, tuna matetemeko ya ardhi, tuna baadhi ya visiwa vinazama, yapo matukio mengi kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi, lakini hatuoni fedha inatengwa na ukiangalia fedha inayotengwa kwenye bajeti za nyuma ni fedha ya nje kwa maana fedha ya ndani haitengwi ya kutosha na wakati mwingine haitengwi kabisa, lazima mpango ujao uoneshe namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kutunza mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nategemea sana mojawapo ya kitu kinachopoteza sana misitu ya Tanzania ni suala la uchomaji wa mkaa na Mawaziri wanaona wakipita kutoka Dodoma kwenda Morogoro, kwenda Dar es Salaam tunategemea makaa ya mawe itakuwa ni solution kutoa nishati kupunguza kukata mikaa kwenye miti, kuharibu misitu, lakini ukiangalia huku Mheshimiwa Waziri anasema makaa ya mawe, basi Serikali inaangalia kama mwekezaji huyo atakuwa na manufaa kwa Taifa. Miaka 20 kweli Serikali inaangaliaga tu? Miaka 20 makaa tunayo hapa hapa tuweze kuyatoa ni kuya-export na kuyatumia, lakini tunakuwa jagwa huku tunasubiria tunasubiria tunachukua muda mrefu sana kutekeleza mradi wa kimkakati ambayo ni muhimu kwa Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba hili suala la mazingira liangaliwe na huu mradi wa makaa ya mawe upewe kipaumbele cha kutosha ili tuweze kutumia nishati mbadala ili tuokoe misitu inayoteketea na tuweze kulitoa Taifa hili kwenye jangwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine tumekuwa tunaomba sana Serikali tuwe na vikosi makini vyenye uwezo wa kuweza kuokoa kwenye vyombo vya maji. Tumeona kipindi hiki jinsi tumepata shida, watu wameteketea kwa sababu hatuna kikosi makini cha kuokoa, tumeomba miaka mingi kwamba lazima kama Taifa kwenye vyombo vya maji, kwenye ukanda wa maziwa yote na ukanda wa bahari tuwe na vikosi makini vya kuokoa, lakini leo watu wamezama kwenye maji, tunaenda kutumia wavuvi siku mbili/tatu mpaka wengine wamepoteza maisha kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba kwenye mpango ujao Serikali iweke mkakati na mpango namna ya kuwa na vikosi makini vyenye uwezo na vifaa na weledi wa kutosha kuweza kusaidia kuokoa watu pale inapotokea tatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine suala la mifugo tunaiomba bajeti ijayo au mpango ujao uonyeshe vizuri namna gani ya kutumia rasilimali ya mifugo ya Taifa hili kuweza kuongeza uchumi wa Taifa kwa kiasi kinachotosha lakini pia kuweza kusaidia uchumi wa jamii ya wafugaji na Watanzania kwa ujumla. Pamoja na kuwa tuna rasilimali ya mifugo lakini bado hatujaweza kuitumia vizuri. Tunaomba bajeti ijayo ioneshe maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya mifugo, ioneshe viwanda kwa ajili ya mazao ya mifugo, ioneshe ruzuku ya Serikali kwa ajili ya kusaidia kwa ajili ya kusaidia mifugo...

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana ahsante.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante nakushukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ambayo iko mbele yetu. Awali ya yote, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa nafasi hii. Naomba niseme kwamba naipongeza Serikali kwa masuala ya afya kwa kuhakikisha kwamba wameweza kuimarisha huduma za uchunguzi wa magonjwa katika kufunga vifaa vya kisasa katika hospitali mbalimbali hapa nchini, lakini zaidi kabisa kuweza kufunga mashine za kisasa za MRI, CT-SCAN Digital X-Ray na Modern Ultrasound, katika Hospitali ya Moi Muhimbili.

Mheshimiwa Spika, nilisema tena wakati tumeletewa Mpango wa Bajeti na nikaiomba Serikali kitendo cha kuweza kufunga vifaa vya kisasa kwenye Hospitali ya Muhimbili kimeokoa sana sana watu wengi ambao walikuwa wanaumia na kupoteza maisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia kuweza kuimarisha huduma kwenye Taasisi ya Moyo ya JK Kikwete. Cha kwanza nipongeze sana utendaji mzuri wa Taasisi ya Moyo ya JK Kikwete. Kama hujauguliwa au hujaugua huwezi kujua umuhimu wa Taasisi hii. Kama umeuguliwa au umeugua unaweza kuona umuhimu wa Taasisi hii.

Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kumpongeza kwa dhati Director wa ile Taasisi, Profesa Jinabi na Dkt. Kitenge na watumishi wengine wote na Madaktari wote, kwa kazi nzuri wanayoifanya. Kama unataka kwenda kujifunza huduma ya upendo wa dhati, huduma inayomponyesha mgonjwa kabla hajaipata, basi watumishi waende Taasisi ya Moyo. Kwa kweli, nisiposema haya, mawe yatasimama yatasema na nitaonekana sina maana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninachoiomba Serikali, baada ya kuhakikisha kwamba kuna huduma hizi za msingi kwenye ya JK pamoja na Hospitali ya Moi na maeneo mengine, naomba vifaa vya kisasa viende kwenye hospitali zote za Mikoa ya Tanzania, tuwekeze kwa mara moja. Serikali imesema iwekeza karibu shilingi bilioni 12. Ukiwekeza shilingi bilioni kwa mara moja kwa miaka zaidi ya kumi ijayo hujapoteza chochote. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Magdalena Sakaya, kwa makofi haya yaliyopigwa humu ndani kuhusiana na Taasisi ya Jakaya Kikwete, basi kwa niaba ya Waheshimiwa Wabunge tutaandika barua rasmi ya pongezi kwa Uongozi na Wafanyakazi wa Taasisi hiyo kuwapa moyo kwa niaba yenu Waheshimiwa Wabunge wote. Endelea Mheshimiwa. (Makofi)

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nashukuru kwa hatua hizo. Naiomba Serikali tuhakikishe tunatafuta fedha tuwekeze kwenye vifaa tiba na vifaa vya kisasa kwenye Hospitali za Mikoa. Inakuwa ni ngumu mtu kutoka labda Ruvuma au kutoka Tabora mpaka Muhimbili kufuata vifaa hivi vya kisasa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tukiwekeza kwenye hospitali zote za Rufaa za Mikoa, tukihakikisha tumeweza kuweka vifaa vya kisasa kuhakikisha tunakuwa na uchunguzi wa kisasa, tutaweza kupunguza idadi ya watu wengi wanaokuja Muhimbili. Pia tutaokoa sana wananchi wetu ambao wengi walikuwa wanapoteza maisha.

Mheshimiwa Spika, leo tumeokoa gharama kubwa ambazo watu walikuwa wanaenda India na maeneo mbalimbali, lakini leo huduma ambazo zilikuwa zinapatika India leo ziko ndani ya Tanzania pale Hospitali ya Moi. Nashukuru sana kwa ajili ya hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali imesema kwamba inajenga hospitali katika maeneo mbalimbali, nami napongeza kwa hatua hiyo. Naomba juhudi ziendelee. Pamoja na kuwa tunaongeza vituo, katika hotuba Mheshimiwa Waziri amesema wameongeza vituo 441, lakini kwa speed ya ongezeko la Watanzania, speed yetu ni kubwa kweli kweli, tunaongezeka sana na niliwahi kuomba mwongozo hapa kwamba angalau tuweke standard ya watoto, Serikali ikasema imeachia free watu wazaane tu. Speed yetu ni kubwa sana. Kwa hiyo, tunavyozidi kuongezeka ndivyo mahitaji ya Vituo vya Afya, Zahanati na Hospitali zinahitajika.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba bado speed ya kuongeza vituo vya iendelee kuongezeka. Nashukuru kwamba Serikali ilitoa agizo kupitia TAMISEMI miaka kama miwili iliyopita kwamba kila baada ya Kata mbili wajenge Kituo cha Afya kimoja. Sisi Kaliua tumeanza kujenga vituo vinne kwa mpigo. Tunaomba Serikali iongeze nguvu kwenye vile vituo.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli alipokuja Kaliua, alitoa shilingi milioni kumi kama mbegu kupanda kwenye Kituo kimoja cha Afya cha Usinge. Kwa hiyo, naomba Serikali isadie vile vituo ambavyo vimeanzishwa ili yale maboma yasibaki wazi, likamilike tuendelee kuongeza huduma za afya lakini pia kupunguza vifo vya akina mama na watoto.

Mheshimiwa Spika, pia Serikali imesema kwamba inaendelea kujenga hospitali, imekarabati hospitali nyingi na ina hospitali nyingi sana kwa ajili ya kujenga. Wilaya ya Kaliua tunajenga hospitali ya kisasa ya Wilaya kwa fedha za ndani, iko karibu asilimia 60.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali, Mheshimiwa Makamu wa Rais alipokuja ametupongeza, Mheshimiwa Waziri Mkuu ametupongeza, Mheshimiwa Rais ametupongeza; naiomba Serikali iongeze nguvu pale kwenye ile hospitali. Tumemaliza jengo la OPD, la ghorofa tumemaliza, jengo la akina mama na mtoto la kisasa tumemaliza mwaka huu. Tunaiomba Serikali itusaidie, kuweza kujenga jengo la wanaume na jengo la uchunguzi ili huduma pale ziweze kufunguliwa, hospitali ile ifunguliwe kazi ziendelee. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nashukuru sana. La pili, naomba niende kwenye suala la mifugo. Watanzania tumejaliwa kuwa na mifugo mingi, lakini kiukweli hatujaweza kutumia fursa ya mifugo Tanzania kuongeza pato la Taifa inavyotakiwa. Hiyo ni wazi kabisa. Leo mifugo yetu mingi inakwenda kunufaisha Taifa la nje. Mimi mwezi wa 12 nilienda Nairobi kwa kutumia basi, kupitia Namanga. Nimefika pale Namanga niliweka mikono kichwani, nimekuta malori tisa yamebeba ng’ombe, mbuzi, kondoo.

Mheshimiwa Spika, nikawauliza wale watumishi wa pale, wakasema huu ndiyo utaratibu, kila siku malori tisa au kumi yanakwenda Nairobi. Sasa nikawa nasema mifugo kuanzia ngozi ni mali, kwato ni mali, damu ni mali, kila kitu ni mali. Leo yale yote yanakwenda kutoa faida kwenye Mataifa mengine, sisi tunabaki tu tunaambulia ile kodi kidogo inayotolewa pale.

Mheshimiwa Spika, bado tunahitaji kufanya mambo makubwa sana kwenye Sekta ya Mifugo, hatujaweza. Leo Mikoa ambayo inazalisha mifugo kwa wingi hatuna viwanda vya kuchakata masuala ya mifugo. Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alizindua machinjio ya kisasa pale Ruvu.

Mheshimiwa Spika, niiulize Serikali leo, naomba Mheshimiwa Waziri Mkuu tujue yale machinjio ya kisasa pale Ruvu ambayo yalipewa karibu shilingi bilioni mbili tangu mwaka 2008 mpaka leo yamebaki ni magofu, nini kinaendelea pale?

Mheshimiwa Spika, lazima tuwekeze kwenye viwanda vya mifugo, lazima tuhakikishe kwamba rasilimali ya mifugo inanufaisha Taifa. Leo kwa baadhi ya maeneo ya Mikoa mingine, mifugo inaonekana ni changamoto, inaonekana ni kero na siyo fursa, wakati hii ni mali. Tunatumiaje uwezo wetu Watanzania wa kuwa watatu kiafrika kuwa na mifugo mingi kuweza kuongeza pato la Taifa.

Mheshimiwa Spika, naomba sana kwenye Sekta ya Mifugo tuhakikishe tunawekeza vizuri. Leo Tanzania nzima, nilikuwa nazungumzia habari ya viwanda vya Tanganyika Packers, ni historia. Viwanda vyote ni historia. Mwanza kulikuwepo na viwanda vya nyama, leo ni historia.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali, ili tunufaike vizuri na pato hili; mimi nilijaribu kupiga mahesabu ya haraka haraka: Je, pale Kenya kwa kupokea magari tisa kwa siku, wanapata nini? Sisi tunakosa nini? Hiyo ni mifugo, bado maziwa, wanachukua. Sisi tumekuwa ni collecting Center. Pale Arusha ambapo kuna mifugo mingi imekuwa ni collection Center wanakusanya wanapeleka Nairobi.

Mheshimiwa Spika, tunakwenda kwenye uchumi wa viwanda, tunakwenda kwenye uchumi wa kati, hatuwezi kwenda huko kama hatuwekezi vya kutosha. Ndiyo maana nashukuru sana mchango wa mama yangu Mheshimiwa Anne Kilango, Sekta ya Uwekezaji, dada yangu Mheshimiwa Kairuki umepewa jukumu zito, ni lazima utumie nafasi hiyo kikamilifu.

Mheshimiwa Spika, nashukuru Mheshimiwa Rais alivyoweka hii Sekta chini ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Hii Wizara iliyoko chini ya Waziri Mkuu, Mheshimiwa Waziri Mkuu tunamjua utendaji wake wa kazi, tumwambie asimamie kikamilifu lakini walio chini yake wafanye kazi kikamilifu, wahakikishe wanaitendea haki Wizara hii. Hatuwezi kwenda kwenye uchumi wa viwanda, kwenye uchumi wa kati kama hatujaweza kusimamiwa vizuri suala la uwekezaji.

Mheshimiwa Spika, natoa mfano mmoja, kwanza tumekuwa wazito sisi Watanzania kwenye suala la uwekezaji na tumekuwa tuna vikwazo vingi, tumekuwa na urasimu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Nakuongezea dakika tano uweke vizuri uwekezaji huo. (Kicheko/Makofi)

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Tumekuwa na urasimu ambao saa nyingine hauna tija kabisa, urasimu ambao unakatisha tamaa wawekezaji, urasimu ambao unafanya mtu anazungushwa mwaka mzima; amekuja na mtaji wake au anakopa benki anataka awekeze, mwaka mzima anapigwa dana dana, nenda rudi nenda rudi, ameshapata ardhi, anaambiwa mpaka Environment Impact Assessment, inachukua miezi sita, anaambiwa sijui hiki, miezi sita.

Mheshimiwa Spika, wale wanaokuja kuwekeza wanakata tamaa, hawawezi kuwaambia walioko huko kwamba njooni. Kwa hiyo, ni lazima tuweke conducive environment kuhakikisha kwamba mwekezaji anapokuja tunampokea vizuri, akiwekeza anapiga simu, njooni Tanzania inawekezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka 2018 ulitutuma kwenda South Africa, bahati nzuri tukapata bahati ya kumtembelea Balozi wetu wa South Africa, tukajaribu kumwambia mojawapo ya tatizo katika nchi yetu, hatuna wawekezaji. Vile vile kazi mojawapo ya Mabalozi ni kuwa na diplomacy ya kuvutia wawekezaji kwenye nchi yetu. Wewe umefanya nini kuhakikisha kwamba tunapata wawekezaji kutoka South Africa?

Mheshimiwa Spika, alisikitika sana, akatuambia ndugu zangu mimi nasikitika sana. Nimepata wawekezaji South Africa. Kwanza alipata wawekezaji wanaotaka kuja kuwekeza Tanzania kwenye mashamba ya kulima parachichi Iringa, ametuma barua TIC mwaka mzima hakujibiwa. Wale wawekezaji wamesubiri mwisho wamekata tamaa wameondoka zao. Akapata wawekezaji wengine hata ile ku-reply kwamba tumepata barua yenu jamani tuna- respond, no response.

Mheshimiwa Spika, tunahitaji wawekezaji; lakini akapata wengine, akahangaika baba wa watu, kapata wawekezaji wa kuwekeza kwenye kiwanda cha ku-assemble Volkswagen hapa Tanzania, walitaka kuja hapa kuwekeza Tanzania. Walitaka kuweka kiwanda cha magari ku-assemble Volkswagen. Wamepigwa dana dana nenda rudi hawajibiwi; na wenzetu Wazungu wanakwenda kwa muda. Watu wana- invest kwa muda. Huwezi kuwa unataka uwekeze leo, unaambiwa kaingize mwakani. Mipango inabadilika, watu wanakwenda kwa malengo, ya jana siyo ya leo.

Mheshimiwa Spika, wamepigwa dana dana, Tanzania Investment Center imezubaa, haikujibu kwa wakati, wale wawekezaji wamekwenda kuwekeza kiwanda cha Volkswagen Kenya pale. Leo tayari uchumi ambao ungeingizwa na kile kiwanda kimoja cha Volkswagen, umekwenda Kenya.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hii ni mifano hai, ni namna gani ambavyo hatutumii fursa kama Watanzania. Kwa hiyo, Sekta ya Uwekezaji ni sekta muhimu sana. Hakuna Taifa lolote duniani linaweza kuendelea bila wawekezaji usidanganywe na mtu. Ukiona leo China imeendelea, ni wawekezaji, Malaysia, Singapore, kila mahali, hata Nairobi hapa ni wawekezaji.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ni lazima kama Taifa tuhakikishe kwamba tunaweka nguvu ya kutosha kwenye suala la uwekezaji ili lengo letu la kwenda kwenye uchumi wa viwanda, uchumi wa kati liweze kutimia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine ni suala la kilimo. Wenzangu wamechangia sana suala la kilimo, lakini kwa kuwa ni sekta muhimu sana kwenye uchumi wetu na hasa uchumi kwenda uchumi wa kati, kwenda uchumi wa viwanda, naomba nami niweke inputs zangu.

Mheshimiwa Spika, bado uchumi wetu hatujaweza kuwekeza kikamilifu. Nilikuwa nasoma hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, amesema kwamba benki yetu ya Tanzania Agriculture Development Bank imeweza kukopesha shilingi bilioni 100. Mimi naona ni kidogo sana kwa wakulima wa Tanzania nzima, ni kidogo bado. Kwa sababu kuna watu ambao wana ekari 1000, kuna watu ambao wana ekari 2000 mpaka ekari 100,000. Ukiangalia hii shilingi bilioni 100 ni kidogo kwa watu hao, lakini tunataka ku-transform kilimo chetu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE.MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara kwa kuandaa hotuba na kuileta hapa Bungeni. Kwa dhati nampongeza Waziri kwa mipango mizuri, utendaji mzuri na mikakati mizuri ya kuhakikisha ardhi ya nchi hii inatumika vizuri na kuwepo kwa mpango miji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwepo tabia ya wananchi kuanzisha miji midogo midogo kiholela pembezoni mwa barabara kuu kila kona. Ukipita barabara kuu kutoka Dar es Salaam kuja Dodoma kuna miji midogo mingi isiyokuwa na ramani yoyote. Naomba Waziri aeleze Bunge hili ni mikakati gani inapangwa kudhibiti uanzishaji miji kiholela halafu wanadai huduma za jamii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Kaliua, Kata ya Ushokola wananchi walichukuliwa mashamba yao ya asili kwa lengo la kupimwa viwanja kwa ajili ya makazi na huduma nyingine tangu mwaka 2000 mpaka leo hawajalipwa haki zao. Mashamba hayo yamepimwa viwanja na watu wanauziwa lakini wamiliki hawaambiwi hatma ya haki zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2011 watendaji wa TANROARDS waliweka mawe ya alama za barabara kwenye viwanja na miji ya watu. Mpaka leo hakuna lolote linaloendelea wala hawaambiwi lolote kuhusiana na mawe hayo yaliyowekwa. Maeneo yaliyowekwa mawe ni Kata ya Ushokola na Zugimlole.
Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro mingi ya ardhi inasababishwa na watendaji wabovu, wala rushwa katika ngazi ya Halmashauri za Wilaya na Manispaa. Maafisa Ardhi ndiyo chanzo cha matatizo kwani ndiyo wanauza viwanja mara mbili mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Morogoro unaongoza kwa migogoro ya ardhi. Afisa Ardhi Mteule pale Manispaa ya Morogoro ni chanzo cha matatizo kwa muda mrefu yupo pale na hachukuliwi hatua yoyote. Kwa nini Serikali inashindwa kuchukua hatua za nidhamu kwa watu kama hawa na kuwaacha kuendelea kuwatesa wananchi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mabaraza ya Ardhi kwa ngazi ya Kata na Wilaya ni muhimu sana kusaidia kutatua migogoro ya ardhi kwa gazi za Wilaya. Serikali ihakikishe Mabaraza ya Ardhi yanaundwa katika wilaya zote hapa nchini. Aidha, Wajumbe wa Mabaraza haya wapewe posho yenye tija ili wafanye kazi zao kwa ufanisi na waache utaratibu wa sasa wa kudai fedha kwa wale wenye matatizo ya ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo ya migogoro ya wafugaji na wakulima itakwisha kwa Serikali kuhakikisha kwamba makundi haya yanatengewa maeneo ya mifugo na maeneo ya kilimo. Maeneo hayo yakishatengwa yaheshimiwe na kulindwa kisheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Uwekezaji inaeleza wazi kuwa wawekezaji wote wanaofika nchini na kuhitaji ardhi kwa lengo la kuwekeza watapata ardhi kwa kufika Kituo cha Uwekezaji (TIC) lakini wapo wanaokwenda moja kwa moja vijijini wanawapa viongozi wa vijiji fedha, wanawapa ardhi ya wananchi tena bila kutumia mkutano na wananchi. Serikali itoe mwongozo wa maandishi kwa ngazi za vijiji, kata na wilaya kuhakikisha sheria zinafuatwa ili kuondoa migogoro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa ni wajibu wa Serikali kuhakikisha wananchi wake wanapata makazi na nyumba bora ni vyema sasa Serikalii ikaondoa VAT kwenye vifaa vya ujenzi kwa Shirika la NHC. Pia Serikali ipeleke miundombinu ili kupunguza gharama za nyumba ili wanyonge au wananchi wa kawaida waweze kuzimudu/kuzinunua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Serikali inapoona wananchi/mwananchi anajenga nyumba eneo ambalo siyo sahihi mara moja asimamishwe na sio kusubiri akamilishe ndiyo abomolewe. Suala la kubomoa linaathiri sana familia, watoto na kusababisha mzigo mkubwa wa mawazo na watu kupoteza maisha.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, uwepo wetu kwenye EAC utakuwa na tija kwa Taifa hili na watu wake ikiwa tutatambua na kuzitumia fursa zilizopo ndani ya umoja huo. Pamoja na Ibara ya 10 ya Itifaki ya Soko la Pamoja kuwahakikishia raia wanachama uhuru wa kupata ajira nchi zote za umoja wa EAC. Serikali itupatie takwimu ya Watanzania wangapi wameajiriwa kwenye ajira rasmi za Serikali katika nchi za Umoja wa Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu imekuwa ni masoko kwa bidhaa zinazotoka kwenye nchi za Kenya na Uganda. Hata kwa bidhaa ambazo tunatengeneza kwa wingi hapa nchini kama vyombo vya plastic, viatu vya plastic na kadhalika bado vinavyotoka nje ni vingi kiasi cha bidhaa za viwanda vyetu kukosa soko ndani ya chini. Serikali ieleze ni kwa namna gani tukalinde viwanda vyetu ndani ya nchi, kuna udhibiti wowote wa uingizaji bidhaa hizi ndani ya nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na nchi yetu kuwa na vivutio vingi ya utalii bado hatujaweza kuvitangaza kikamilifu ili tuweze kunufaika vizuri. Ni kwa namna gani tunatumia Balozi zetu zilizoko katika maeneo mengi kutangaza utalii na vivutio vyetu huko waliko?
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuwezesha Balozi zetu ni muhimu sana ili ziweze kutekeleza vizuri majukumu yao. Ni aibu kwa Maafisa wa Ubalozi kushindwa kulipia nyumba za kuishi na kubaki wakilalamika mara kwa mara kila tunapokwenda nje. Maofisa hawa wanalalamikia shida, tabu na kutelekezwa na Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuelekea kwenye kutumia sarafu moja kwa nchi zote za EAC. Tumejiandaa kiasi gani? Kwa sasa hiyo shilingi ya Tanzania ndio yenye thamani ndogo sana tofauti na fedha za wenzetu. Tusikubali mambo ambayo yatakuja kutuumiza kama hatujajipanga vizuri ndani ya nchi. Tusije tukawa wasindikizaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na nchi yetu kuwa na vyuo vinavyotoa mafunzo ya fani za utalii na customer care; bado mahoteli mengi makubwa na madogo watumishi wengi ni kutoka Kenya na wanatoa huduma nzuri sana na wanaipenda kazi yao. Naomba Serikali itueleze nini kinakosekana ndani ya vyuo vyetu hapa nchini au kwa vijana wetu wanaosoma fani hiyo kiasi cha kutokubalika kwenye hoteli zetu. Je, Serikali imefuatilia mitaala ya vyuo vya utalii vya Kenya na kuona upungufu wetu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge lipange utaratibu wa Wabunge wa EAC wawe wanatoa semina na mafunzo kwa Wabunge kuhusu yale wanayofanya ndani ya Bunge la EAC ili tupate uelewa mpana na up to date yanayoendelea kuliko kusubiri hotuba wakati wa bajeti ya Serikali.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana nami kunipa nafasi niweze kuchangia kidogo hotuba hizi mbili ambazo ziko mbele yetu. Sababu ya muda mdogo, naomba moja kwa moja nianze na suala la upungufu mkubwa sana wa watumishi na hasa kwenye Sekta ya Afya na Sekta ya Elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiukweli kati ya kitu sasa hivi ambacho kinadumaza elimu, pamoja na ongezeko kuwa la watoto katika mashule yetu, ni suala la upungufu wa walimu kwenye mashule yetu. Wakati enrollment inaongezeka, wakati madarasa yanaongezeka, wakati shule zinaongezeka, walimu hawaongezeki kwa speed ile ile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya yetu ya Kaliua, mwaka huu tumefungua shule nne za sekondari; mwaka huu huu tumefungua zahanati nne, mwaka huu huu tumefungua primary school mikondo sita. Walimu wanahamishwa kutoka kwenye maeneno yenye upungufu, wanapelekwa kwenye shule mpya. Kwa hiyo, kwenye tatizo unaongeza tena tatizo lingine, una-create gap pale, unawapeleka kwenye shule nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kweli tunataka watoto wetu wapate elimu nzuri, ni lazima tuhakikishe kwamba ongezeko la watoto linakwenda sambamba na ongezeko la walimu, ni muhimu sana. (Makofi)

Leo shule moja ina madarasa saba inakuwa na walimu tisa, wanagawanaje hayo masomo waweze kufundishwa? Zahanati inakuwa na watumishi watatu au wanne na wakati mwingine katika maeneo mengine mpaka watumishi wawili. Mmoja akiugua, au kama ni mtu na mke wake ameugua, au amesafiri, zahanati haifanyi kazi. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Waziri wa Utumishi, lazima tuwe na mpango mkakati kabisa wa makusudi ya dhati, kuongeza watumishi na hasa kada hizi mbili, elimu na afya, ni muhimu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, akina mama wengine, nilisema tena hapa, wanajifungulia kwenye zahanati, hakuna wahudumu; na mhudumu huyu anachoka. Yeye ni binadamu, anatumia damu, hatumii maji. Tunaomba suala la upungufu ya kada hizi mbili ni muhimu mno.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua mwaka 2018 wilaya yetu imepata watumishi 16; ni wachache sana sana kwenye kada ya afya kwa sababu wamekwenda kuongezwa, kwenye zahanati kulikuwa na wawili, akaongezwa mmoja. Kwa hiyo, bado tatizo liko pale pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi bado tunakwenda kuongeza kujenga zahanati, vituo vya afya, tunaongeza shule, tunaongeza madarasa, lakini tatizo la upungufu wa walimu ni kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la walimu wa sayansi. Hivi kwa kweli, sasa hivi sijui ni percent ngapi, sijafanya utafiti wa kutosha; lakini shule nyingi, tumejenga maabara na ni agizo la Serikali. Maabara zile hazitumiki, hakuna walimu wa sayansi. Tunakwendaje kwenye uchumi wa viwanda wakati hatuna walimu wa sayansi, hatuna walimu wa biology, walimu wa physics na chemistry? Haiwezekani kwenda kwenye uchumi wa viwanda wakati hatupeleki walimu wa sayansi kwenye mashule yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine mwaka jana, mwaka juzi 2017/2018 Serikali ilipendekeza shule moja katika kila wilaya kupokea watoto wenye mahitaji maalum kwa maana ya watoto walemavu, wenye mahitaji yote, walemavu wa viungo, viziwi wote wamepokelewa pale. Cha ajabu shule zile miundombinu ile siyo rafiki kwa watoto wale, wamepelekwa pale wanapata mazingira magumu sana, hawapati elimu kama watoto wenzao, hawajapelekewa vifaa vya kuweza kuwasaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikupe mfano mmoja, sisi Kaliua shule iliyopendekezwa ni Kaliua Primary School, ina watoto 2,295, shule moja, wale watoto wanatumia kaofisi kadogo tu kalikokuwa kakatahapo pembeni.Kwa hiyo ni tatizo. Sasa kama lengo lilikuwa ni kuwasaidia, maana yake kilio chetu hapa Bungeni ilikuwa ni kwamba, watoto wale wamesahaulika, wako majumbani, lakini ni Watanzania wanahitaji elimu kama wengine, Serikali ikaamua kuwasaidia kwa kuwa hatuna shule maalum nyingi kwenye mikoa yetu watenge shule moja. Akili yangu ilikuwa ni kwamba, Serikali ingepeleka nguvu kubwa kwenye zile shule, kujenga miundombinu, kuweka Walimu, kuweka vifaa wale watoto wapate elimu ndani ya maeneo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti,kwa kweli lengo lilikuwa jema, lakini leo kilichofanyika ni kuwaacha katika mazingira yale, kwa kweli hatuwatendei haki. Naiomba Serikali ihakikishe lengo lake lililokuwa la kuweka zile shule kuzitenga litimie kwa kuweka miundombinu ya kutosha, miundombinu rafiki, watoto wanatambaa chini kwenda kwenye zile mashule, wana-share vyoo na wale watoto wengine na wenyewe ni walemavu, siyo haki kabisa! Wengine walikuwa viziwi, wamekaa pale mpaka mwisho wameondoka hakuna Mwalimu wa kuwasaidia. Tuwatendee watoto hawa haki, hawakupenda kuzaliwa walemavu, ni Watanzania wenzetu, wana haki sawa kama watoto wengine ambao wamezaliwa bila kuwa na upungufu wowote.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la TASAF;nakumbuka TASAFthree ambayo tunaenda nayo sasa hivi ya kunusuru kaya maskini ilianza mwaka 2013, maeneo mengine kama Kaliua 2014. Huu mradi ulikuwa ni miaka mitano, tulivyokuwa tumeelezwa pamoja na upungufu kwamba kwenye hivyo vijiji ambavyo wamepewa wachache wengi pia hawapati lakini tulitegemea baada ya miaka mitano waingie wapate tena vijiji ambavyo vilikosa. Leo hakuna majibu yoyote tunayopewa na Serikali nimeuliza suala hili tangu Mheshimiwa Kairuki akiwa Waziri, hatupati majibu, ni lini vilevijiji ambavyo havijawahi kuingia kwenye TASAF vitaingia kwenye TASAF? Imekuwa ni double standard, kuna wazee ambao hawajiwezi kabisa, kuna walemavu hawajiwezi, wanaona kijiji jirani kuna msaada wanapata japo ni kidogo, yeye hapo alipo kijiji hicho hicho jirani hapo pembeni hapati chochote kwa miaka yote, kwa nini Serikali isione kwamba hii ni fursa kwa wote? Kama suala la kusaidia kaya maskini zipo kote, basi baada ya miaka mitano mradi huu ueleweke kwenye vijiji tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba sasa tupate majibu kwa Mheshimiwa Waziri atakavyokuja kujibu kwamba mradi wa TASAF ambao ulikuwa umalizike waweze kupeleka na kwenye vijiji ambavyo vilikosa, Kaliua tulipata vijiji 36 tu, tuna vijiji vingine kwa maana ya Jimbo la Kaliua 36 tu, bado vijiji vingine 26 hawajapata. Kwa hiyo tulikuwa tunategemea kwamba wangeweza kupata kama wengine, kwa kweli wanaumia wazee wale wanasikitika kwa sababu wanaona kwamba Serikali imewaona wenzao wa vijiji jirani wao imewasahau na ukizingatia hapa kwamba hakuna mpango wowote wa Serikali kusaidia wazee popote, hata wale ambao wana nguvu ya kufanya kazi, hakuna mfuko maalum wa kuwasaidia. Kwa hiyo tunaomba TASAF ihakikishe kwamba imeangalia wale wengine ambao pia hawakuingia kwenye Mfuko huu wa TASAF kwa awamu ile ya kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala langu lingine na la mwisho ni suala la lishe. Suala hili ni muhimu sana, nilikuwa nasoma kitabu cha Mheshimiwa Waziri; suala la lishe hapa Tanzania kwa takwimu za mwaka 2016/2017 watoto chini ya miaka mitano wenye udumavu ni watoto asilimia 34, ni wengi kweli kweli. Nilikuwa nategemea tupewe takwimu update, tupewe takwimu za 2017/2018, 2018/2019 tujue current situation, udumavu kwa sasa hivi ni asilimia ngapi. Hata kwa takwimu za miaka mitatu iliyopita asilimia 34 kwa watoto chini ya miaka mitano suala la lishe ni muhimu kuliko maelezo, mtoto anapodumaa akiwa chini ya miaka mitano, anadumaa totallykuanzia fikra zake, mawazo yake, uelewa wake,darasani hafundishiki, ni tatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, ukiangalia bajeti iliyotengwa na Serikali bado ni kidogo sana, haiwezekani tunatengeneza Taifa la kesho, hawa ndiyo Marais wajao, ndiyo Mawaziri wajao, ndiyo Wabunge wajao, Wakurugenzi wajao, wanakua wakiwa wanaudumavu wa akili, tunawapeleka wapi.(Makofi/)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka pia niseme kwamba suala la kuangalia suala lishe siyo kutoa matone ya damu, siyo kutoa matone ya vitamini A na dawa za minyoo tu, hapana. Suala la lishe ni chakula pia na bahati mbaya ukiangalia maeneo ambako watoto wamepata utapiamlo na udumavu wa akili kwa maeneo mengi hasa utapiamlo ni mikoa ambayo wanalima vizuri sana, wanafuga vizuri, leo Mkoa wa Kilimanjaro siyo mkoa ambao tunatakiwa tuwe na udumavu wa akili wala kuwa na utapiamlo, lakini ukiangalia utapiamlo upo mwingi, kwa nini hakuna elimu. Pia ukiangalia bajeti nzima ya Mheshimiwa Waziri hakuna sehemu wamesema watawekeza kutoa elimu namna gani wazazi wawape watoto vyakula vyenye kujenga lishe yao, hawaangalii.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali suala la kutoa matone ya vitamini A nakubaliana nalo, pamoja na kutoa dawa za minyoo, lakini suala kubwa kabisa ni chakula nyumbani. Ukimpa mtoto dawa ya minyoo kamanyumbani alivyokula vitaminiataendelea kudumaa tu, kwa sababu hiyo haimsaidii sana.Vile vile Mkoa wa Tabora tunalima mahindi, tunalima maharage, tunalima karanga, tunalima alizeti vyakula vyote vyenye vitamini vipo, iweje watu wapate utapiamlo au udumavu wa akili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kilimanjaro wanalima, Kilimanjaro wanafuga watu wanakula mayai, maziwa, lakini maziwa yanauzwa mtoto hanywi, mayai yanauzwa,mtoto hali, matokeo yake watoto wanadumaa.Tusiliangalie Mheshimiwa Waziri kama suala dogo, ni suala kubwa kwelikweli, ndiyo maana tunakuja kuwa na Taifa la watu ambao hawafikirii vizuri, hawawazi vizuri, hawawezi ku-deliver kwa sababu udumavu umeanzia kwenye utoto wake.

MWENYEKITI:Ahsante sana.

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi hii.(Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kunipa nafasi kuweza kuchangia kwenye hotuba ya afya ya Mheshimiwa Waziri ambayo ipo mbele yetu. Narudia tena kwa mara nyingine nilisema kwenye bajeti ya Waziri Mkuu na baada ya kupongeza juhudi zilizofanyika kwenye hospitali ya Muhimbili kuweza kuweka vipimo vya kutosha na vifaa tiba nikaiomba Serikali ihakikishe imepeleka vifaa tiba vya kutosha na vya kisasa kwenye hospitali zote za kanda na hospitali zote za rufaa Mikoa Tanzania nzima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa tulipo sasa hivi, Hospitali yetu ya Kitete, ambayo ni Hospitali ya Rufaa na Hospitali ya Mkoa wa Tabora, ukienda pale haina sifa ya kuweza kuwa Hospitali ya Rufaa kwa sababu haiwezi kutoa huduma za Hospitali ya Rufaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wagonjwa wengi ambao wanakuwa referred kutoka kwenye Hospitali za Wilaya wanakwenda Bugando, Muhimbili na maeneo mengine. Sasa fikiria mtu atoke Tabora mpaka Bugando, atoke Tabora mpaka Muhimbili na maeneo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kuweza kufanya, naomba Serikali ihakikishe kwamba inaweza kuweka vifaa tiba vya kutosha katika Hospitali zote, Hospitali ya Itete na Hospitali nyingine za Tanzania nzima kwa kweli, tutaweza kusogeza huduma karibu wale wananchi masikini ambao hawana uwezo wa kupata hata nauli ya kutoka Tabora, kuweza kwenda mpaka Muhimbili au kuweza kwenda Bugando waweze kupata huduma kwa maeneo ambayo wapo na maeneo ambayo ni ya karibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tabora hata ile Hospitali ya Nkinga tu yenyewe inatoa huduma bora zaidi kuliko hata Hospitali ya Kitete. Kwa hiyo, naomba jicho la pekee kabisa kwenye Hospitali ya Kitete ya Mkoa wa Tabora ili wananchi wa Mkoa wa Tabora wanaopata rufaa kwenye Wilaya yetu waweze kupata huduma pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la huduma za afya kwa Wilaya ya Kaliua. Nashukuru kwamba tumetengewa fedha mwaka huu shilingi bilioni 1.5 ya kuweza kumalizia Hospitali yetu ambayo tumeijenga kwa fedha za ndani, tumekamilisha almost karibu nusu. Jengo la OPD tayari, jengo la akina mama na watoto tayari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachoiomba Serikali, najua kwamba miundombinu iko kwenye Wizara ya TAMISEMI, lakini kwa msukumo wa Mheshimiwa Waziri kwa kuwa alifika kule akaona kazi inayofanyika, naomba aweze kusukuma fedha hii itoke ili Hospitali ile ifunguliwe, kwa sababu mwenyewe alituahidi kwamba tukimaliza jengo la akina mama tunaweza tukapata kibali cha muda ifunguliwe tuendelee na majengo mengine. Naomba msukumo wa Wizara ili tuweze kufungua Hospitali ile wananchi wa Kaliua ambao kiukweli wengi wao wanapata huduma mbali na Wilaya waweze kupata huduma pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni dawa. Tumekuwa tunapata dawa na dawa zimeboreshwa kwenye Vituo vya Afya na kwenye Zahanati zetu, lakini kuna Zahanati ambazo zina idadi ya watu wengi sana ambapo ule mgao wa huduma ya Zahanati hauwatoshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Zahanati ya Usinge nimeshaleta maombi kwa Mheshimiwa Waziri na kwa Mheshimiwa Naibu Waziri. Zahanati ya Usinge ina tibu watu 35,000 kwa mwezi, inahudumia Kata mbili na pale hamna Kituo cha Afya. Tukawaomba Zahanati kama ile ya Usinge watu 35,000 kwa mwezi, Zahanati ya Igagala watu 28,000 kwa mwezi wapewe mgao wa Kituo cha Afya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu wananchi wanaona kabisa kwamba hawapati dawa kwa sababu zikiletwa ndani ya wiki mbili zimeisha. Kwa hiyo, wakienda wanaambiwa dawa hamna kwa sababu idadi ya watu wanaopata huduma pale ni kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri ahadi yake ya kuweza kutupatia Zahanati hasa hizi mbili; Zahanati ya Usinge na Igagala waweze kupata mgao wa dawa unaofaa kwa Kituo cha Afya ili wananchi walioko maeneo yale waendelee kupata huduma kwa quarter nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni huduma za wazee. Mheshimiwa Waziri ametuambia tuna Makazi ya Wazee 17 ya Serikali, lakini pia tuna makazi ya Wazee 14 ya Taasisi za Umma, Watu binafsi pamoja na Taasisi za Mashirika ya Dini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Makazi ya Wazee ya Serikali yana hali mbaya sana. Wazee wengi walioko kule wanateseka hawana huduma. Hakuna chakula na hakuna mavazi. Mfano mmoja mdogo, Wabunge wengi wanapita njia hii ya kwenda Tabora pamoja na Singida, ukipita pale Sukamahela, ule mlima pale, kuna wazee kibao wamekaa pale wanaomba barabarani. Wamechoka kukaa kule Kituo cha Sukamahela, wanakuja kukaa barabarani kuja kuomba. Ukiangalia mavazi waliyovaa, wako pale wanadonoa chawa kwenye nguo zao, kwa maana kwamba hata hali ni mbaya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mimi naomba kama mmeamua kuwaweka kwenye vituo, wapate huduma ili ukipita pale ukiwa na mkate uwape, ukiwa na maji uwape. Wale ni wazee ambao wamefanya kazi kwa muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri, kile Kituo cha Sukamahela kwa kweli kinatia huruma. Mimi mpaka siku nilienda kukitembelea japokuwa siyo Jimbo langu, nikasema hebu nikaone hao wazee wanakaa maeneo gani? Wanatia huruma, wategemee mkate wa barabarani kweli! Magari yapite na bahati mbaya pale ni mlimani, likiharibika gari pale ndiyo wapate chochote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wazee hawa wamefanya kazi kubwa. Leo tuko hapa kwa sababu walikuwepo hawa wazee huku nyuma. Naomba vituo vyote vya Serikali vihudumiwe vizuri. Ukienda angalau kwenye Taasisi za dini zina unafuu, kwa sababu wanapeleka misaada mbalimbali, watu wanaenda kutoa sadaka kule, lakini hivi vya Serikali havitembelewi mara kwa mara na watu ambao ni wasamaria wema. Kwa hiyo, naomba sana wazee hawa waweze kupata huduma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni huduma za wazee za Bima ya Afya. Serikali kwa muda wa miaka minne imekuwa ikisisitiza wazee wapatiwe vitambulisho vya kutibiwa bure, lakini bado speed za Halmashauri kutoa vitambulisho hivi ni ndogo sana. Mpaka leo wazee wengi hawana vitambulisho vya kutibiwa bure. Mojawapo ni Wilaya yangu ya Kaliua, tunasisitiza kila vikao wazee wapewe vile vitambulisho, lakini mpaka leo, zaidi ya robo tatu hawajapata vile vitambulisho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba msukumo wa Serikali, wazee hawa, wapate vitambulisho wawe na dirisha lao waweze kupata haraka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni migogoro ndani ya ndoa. Mheshimiwa Waziri ameeleza kwa umakini mkubwa sana kwenye hotuba yake, migogoro imekuwa mingi sana ndani ya ndoa na wanaopata matatizo ni wanawake. Leo migogoro ni kila siku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia imezuka tabia nyingine hapa Tanzania, mimi naishangaa sana. Wanawake wanaojifungua mapacha zaidi ya watoto watatu mpaka wanne waume zao wanawakimbia. Yaani baraka inakuja nyumbani, halafu wanawake ambao wamepata mapacha wanakimbiwa. Nimekuwa nafuatilia mpaka nashangaa. Wengi wanasaidiwa sana na watu kwenye mitandao, waanze kuchangiwa shilingi 100/=, shilingi 200/=.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali ituambie, wana mpango gani kwa watoto hawa wanazaliwa wanne mpaka watano kwa familia ambazo ni masikini halafu wanawake wanakimbiwa na waume zao. Wanaume wengine sijui ni mashetani! Unapata baraka, halafu unakimbia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano binti mmoja ambaye aliomba mimba kwa muda wa miaka minne hajapata mimba. Kapata mimba mwaka 2018 kajifungua mwaka huu watoto watatu, mwanaume kamwachia wale watoto kakimbia. Yaani mpaka unashangaa. Hivi huyu ni binadamu au mtu gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi naiomba Serikali, watoto ni baraka ya Taifa, watoto ndiyo raslimali, nguvu kazi ya Taifa. Watoto hawa wanaozaliwa kwa familia masikini, mapacha watatu, wanne, watano, Serikali inawasaidiaje? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati nakua nilikuwa nasikia kuna kitu ambapo ukijifungua watoto zaidi ya watatu Serikali inakusaidia kuela wale watoto mpaka inawasomesha. Siku hizi nadhani hicho kitu sijui hakipo! Kwa hiyo, naomba Serikali itusaidie sana katika kuhakikisha kwamba watoto hawa waliozaliwa kwenye familia masikini ambao ni mapacha waweze kupata huduma nzuri, waweze kuwa ni Taifa nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la Sheria ya Ndoa, migogoro imezidi, akina mama wana mizigo mikubwa ya kuweza kulea watoto wenyewe. Tunaomba Sheria ya Ndoa ije Bungeni, iliyopo imepitwa na wakati. Tumeongea sana muda mrefu kwenye Bunge hili. Kwa nini Sheria ya Ndoa haiji Bungeni tuifanyie marekebisho ili watoto wapate stahiki zao? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani akina baba wanawakimbia watoto. Ile Sheria ya Ndoa ukiangalia viwango vilivyoko kule ni vidogo. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri atusaidie Sheria ije Bungeni tuipitishe ili watoto wanaoachwa mzigo kwa akina mama wapatiwe huduma stahiki za kusoma za kula vizuri na huduma nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Ahsante. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi nikushukuru kunipa nafasi ili niweze kuchangia hotuba hii muhimu sana kwa uchumi wetu, ambayo ipo mbele yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi niungane pia na Waheshimiwa Wabunge kupongeza kazi nzuri ambayo inafanywa na Wizara, kwa kweli Mheshimiwa Waziri kuna kazi inayofanyika, tunaiona na inaonekana. Pamoja na kazi inayofanyika lakini bado kuna mambo ya msingi sana ambayo ni lazima Wizara iangalie tena kwa jicho la pekee sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye taarifa ya Mheshimiwa Waziri ametuambia kuhusiana na kiwango kikubwa sana cha utowekaji wa misitu, speed ya kutoweka misitu Tanzania ni kubwa sana. Mwaka 2015 na mpaka 2018 tumepoteza almost hekta 469,420; kwa mahesabu ya haraka haraka ambayo nimepiga kwa mwaka mmoja tunapoteza hekta 29,000 za misitu ambayo tayari ipo, wakati huo huo speed ya kupanda miti bado ni ndogo sana. Kwa hiyo, kwenye suala la misitu inayoteketea bado lazima tutafutie solution, kwa mwendo tunaoenda nao bado.

Mheshimiwa Naibu Spika, na leo hili linaloongelewa kwenye vitabu wala huhitaji hata kwenda shule sana, ukiangalia spidi ya kukata misitu inayoendelea na mkaa unavyopelekwa Dar es salaam na magunia ambayo yamejaa kila unakopita yamerundikwa inadhihirisha wazi kwamba hali ya misitu yetu inakwenda kuwa hatarini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninachoomba, naomba Wakala wa Misitu wapewe mamlaka. Leo tunazisifia TANAPA na Ngorongoro kwa sababu ni mamlaka, wanatumia sheria ya kuhifadhi ndiyo maana unaona wanafanya kazi kulikoni hata mamlaka nyingine. Kwa hiyo, ukipewa mamlaka unakuwa na nguvu ya kisheria. Naiomba Serikali ione umuhimu kuifanya TFS waweze kuwa ni mamlaka ili wasimamie kikamilifu matumizi ya rasilimali zote za misitu kwa ukamilifu wake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine, kuna tatizo kubwa sana la ukataji wa miti kwenye mashamba yaliyopandwa Iringa na Njombe, miti ambayo haijakomaa, na kwa lugha ya kule wanasema ni kubakwa kwa miti, ,miti inabakwa kabla ya wakati wake. Hili ni tatizo kubwa sana kwa sababu tunaingiza product za mbao kwenye masoko ambazo hazijakomaa; wananchi hatujui mbao ipi imekomaa na ipi ambayo haijakomaa, tunanunua, unakwenda kujenga nyumba siku mbili/tatu upepo ukija paa lote limeezuliwa, ni kwa sababu tumeruhusu miti inavunwa ambayo haijakomaa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunao wataalam wa misitu, nataka nipate majibu ni kwa nini wataalam wa misitu wanakubali mbao ambayo haijakomaa inaingia sokoni? Pia nijue mkakati wa Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nilikuwa nashangaa, huko nyumba ukienda kuuliza mbao ya Sao Hill gharama yake ipo juu sana, ukienda kwenye mbao nyingine gharama iko chini, nikawa nasema ni kwanini tofauti hii ni kubwa sana? Kumbe tatizo ni kwamba mbao ya Sao Hill inakomaa vizuri, mbao za wananchi kwenye mashamba hazikomai vizuri lakini zote ni product ambazo zinatakiwa ziwe zimekomaa vya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naomba nijue mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba kwanza ni namna gani wananchi watajua mbao isiyokomaa na iliyokomaa sokoni lakini nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba wanatatua tatizo hili ambalo ni kubwa sana ndani ya matumizi ya rasilimali ya misitu na hasa kwa ajili ya ujenzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni kuhusu TANAPA; wengi wamelizungumzia. Kiukweli Serikali isipoangalia, leo tunajivunia wanakuja wageni wataalii mara Waisraeli na Wachina wanakuja kuangalia vivutio vilivyohifadhiwa na havikuhifadhiwa kwa siku moja, imechukua muda kuvihifadhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa leo tusipoenda kimkakati tukaendelea kuweka majukumu mazito kwenye TANAPA wakati huo huo bajeti ya mwaka huu ya TANAPA tumeipunguza kwa asilimia 18, lakini wakati huo tumewaongezea majukumu hifadhi nyingine tano ambazo ni mapori yaliyokuwa yamechoka hayana kazi tena. Tumewapa wayahifadhi, waya-groom mpaka yaweze kuwa ni maeneo ambayo yanatembelewa; watengeneze miundombinu na wawe na watumishi wa kutosha kuhakikisha kwamba hifadhi zile pia zinapeleka watalii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ni lazima ikubali, kwa kuwa TANAPA wamepewa majukumu makubwa, ipunguze zile tozo na angalau lile gawio la asilimia 15 lipungue liende kwenye 10. Lakini TANAPA inafanya kazi kubwa kwelikweli, ukienda kwenye Land Use Plan ya Taifa, protection, miundombinu, ujirani mwema kote huko TANAPA inachangia. Kwa hiyo, kazi inazofanya nje ya kazi zake ni nyingi sana. Kiukweli kuendelea kupunguza bajeti yake na kuendelea kuwapa majukumu na tunategemea kwamba majukumu hayo yaweze kuwa na tija huko tuendako tunaenda kuiua TANAPA kama ambavyo tumeua mashirika mengine ambayo yalikuwepo ndani ya nchi hii miaka ya nyuma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Ngorongoro; Kamati tumewahi kuleta maoni ya kwa muda mrefu sana, kwamba sheria hii iliyotengeneza Ng’orongoro miaka hiyo inawezekana leo ikawa inahitaji maboresho. Leo ukienda kule Ngorongoro wananchi wanalalamika na ni hifadhi pekee nadhani duniani ambapo ni multiple plan land use ambapo wananchi, wanyama na mifugo wapo huko huko, ni kitu kizuri kwelikweli. Kwa nini Serikali haileti Sheria ya Ngorongoro tuweze kuifanyia mabadiliko ili Ngorongoro iweze kuwepo sustainably lakini pia jamii inayoishi kule iweze kuridhika na kuendelea kuishi vizuri na kuendelea kutunza huu utamaduni wa kuweza kuwepo na multiple land use kwenye eneo la Ngorongoro. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni suala la tasnia ya uwindaji wa kitalii. Kwa mwaka 2017 tasnia hii imeyumba kidogo na mpaka sasa hivi nadhani haijasimama vizuri kutokana na kwamba Serikali itaenda kuingiza mfumo wa kugawa vitalu kwa njia ya mnada katikati ya muhula wa uwindaji, matokeo yake vitalu vingi vikarejeshwa Serikalini.

Mheshimiwa Naibu Spika, tafsiri ya vitalu kurejeshwa Serikalini ni kwamba vile vitalu havina ulinzi, hakuna watu wanaovilinda kwa sababu sheria ni kwamba unapewa kitalu kwa ajili ya uwindaji pia unaweka askari kwa ajili ya kulinda rasilimali iliyopo kule. Sasa vile vitalu vyote ambavyo vimerejeshwa havipo salama lakini Serikali inakosa mapato and at the same time wale wanyama kule wanawinda kiholela kwa kuwa hakuna anayetunza.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba Mheshimiwa Waziri atakavyokuja ku-wind leo atuambie amefikia wapi kuhusu mchakato wa kuhakikisha kwamba tasnia hii ya uwindaji wa kitalii inakuwa sustainable, lazima tupate majibu. Tukiendelea ku-dilly-dally kwanza wale wawekezaji wanaondoka lakini pia yale maeneo yanakuwa hayapo salama sana kwa ajili ya kuhakikisha kwamba yanaendelea kuleta kipato lakini pia yaendelee kuwa eneo salama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kuhusu Suala la Migogoro ya Ardhi Kwenye Maeneo ya Wananchi na Maeneo ya Hifadhi. Hili ni lazima tuliseme kila siku kama wimbo kwa sababu ni kitu ambacho kinagusa jamii ya chini kabisa ya wananchi wetu. Mimi nashukuru kwa mara nyingine Mheshimiwa Rais ameunda tume; na mimi nashukuru kwamba hii tume ina Mawaziri ambao tuna imani nao. Sasa hivi tunaambiwa kwamba wamekamilisha kazi na wanaandaa ripoti, lakini maeneo mengi hawajafika.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ninasema kama Mawaziri hawa wataenda kukaa maofisini na watendaji wakapata taarifa za ofisini, tatizo la migogoro hii halitakwisha, watakuja na ripoti hapa still kule matatizo yataendelea kuwepo. Mimi nawaomba maeneo ambayo hawajafika, wafike wakaangalie haya maingiliano ya maeneo ya hifadhi waone ili watakapokaa mezani kutoa mapendekezo na kuandika ripoti wampelekee Rais kitu ambacho ni reality. Leo unakwenda kukaa na watu wa TAMISEMI wa Wilaya ambapo hao hao ndio wamesajili vijiji ndani ya hifadhi, unategemea kupata nini? Ukienda kukaa na watu wa mkoa ambao na wenyewe pia wameshiriki unategemea kupata nini? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hawatapata uhakika (reality) mpaka waende kwenye maeneo ambayo yana migogoro wakaongee na wale wananchi na wenyewe waone ule muingiliano, wanaweza kukaa chini wakatoa taarifa ambayo ni nzuri na itaweza kusaidia kuondoa migogoro hii ambayo imedumu kwa muda mrefu lakini pia kiukweli inaleta madhara makubwa sana kwa wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni suala la hoteli zetu. Tulikuwa na utaratibu huko nyuma ulianzishwa na nitapenda Mheshimiwa Waziri aje atuambie, ya kuweza ku- grade hoteli zetu. Lazima tuwe na grade ya hoteli zetu zote, tujue five star ikoje, four star, three star mpaka mwisho. Leo unaweza ukaenda kwenye hoteli unaambiwa hii ni hoteli haifanani hata na guest, unavyoenda kwenye hoteli ujue hii ni hoteli, hii ni lodge na hii ni guest house; lakini leo mtu anajiandikia tu, chumba cha ajabu hakina hadhi anakwambia hii ni lodge.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba Serikali ituambie utaratibu wa kufanya grading ya hoteli zetu zote, leo sasa tunaanza kupata wageni wengi, mgeni anaweza akaja akaingia kwenye chumba ambacho alijua ni hoteli, mazingira yale ya hoteli tu yatamfanya next time asije tena au picha anayopeleka kule ikawa siyo nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba zoezi la ku-grade hoteli zetu maeneo yote lilianzwa vizuri sana na Mheshimiwa Shamsi nadhani kipindi hicho, mpaka leo hatujui limefikia wapi. Naomba sana hoteli zetu zote zipatiwe grading kwa kuwa ni sehemu moja wapo ya utalii. Mgeni anavyokuja ukimwambia hii ni lodge ajue ni lodge, guest ama five star hotel. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa muda, yangu ni hayo machache, ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia kwenye hotuba ya Wizara ya Maliasili na Utalii iliyoko mbele yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue nafasi hii kulipongeza Shirika la Hifadhi la TANAPA na Ngorongoro kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuhifadhi rasilimali hapa Tanzania. Imekuwa ni kawaida pale ambapo Serikali inashindwa kuhifadhi maeneo mbalimbali kimbilio lake ni shirika lake ambalo linawapelekea na kwa kiasi kikubwa kwa kweli wameonekana wanajitahidi sana kulinda rasilimali zetu na vituo vyetu hapa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, zipo tetesi kwamba Serikali inataka kuhodhi mashirika haya, kuyarudisha mikononi mwake kwa hili napinga kwa asilimia zote. Kama ni kweli kwamba ziko taarifa Serikali inataka kuhodhi mashirika haya irudishe kwenye mikono yake, wawe wanaendesha wao ni uhakika kabisa kwamba tunakwenda kuua uhifadhi hapa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mashirika mengi hapa nchini yalikufa kwa sababu Serikali imeshindwa kuyasimamia. Yale machache ambayo iliamua kuyapa full authority yajiendeshe yenyewe ndiyo bado yapo. Leo TANAPA na Ngorongoro wanajiendesha wenyewe kwa asilimia 100 na bado wanapeleka ruzuku Serikalini na ni mashirika pekee ambayo Serikali haiweki ruzuku hata senti moja. Leo kama wanataka kuyarudisha ndani ya mikono yao tunakwenda kuua uhifadhi hapa nchini. Naomba kama mpango huo upo ufe kabisa haufai kuwepo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka jana pekee TANAPA imetoa shilingi bilioni 10 kama ruzuku Serikalini na bado inajiendesha. Tumekuwa tunalia kilio hapa kwamba Serikali ijenge angalau miundombinu ya kwenda kwenye vivutio, barabara kutoka Iringa kwenda Ruaha kwa miaka 10 Serikali imeshindwa kujenga, leo tunanyang‟anya mashirika haya mamlaka ya kujisimamia tunakwenda kuua uhifadhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine, kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri hapa nimeona tunayo mapori ya akiba zaidi ya 28, tunayo mapori tengefu zaidi ya 42, tunazo hizi hifadhi za TANAPA 16. Nataka nimwambie Mheshimiwa Waziri haya mapori ya akiba 28 na mapori tengefu 42, mengi yapo taabani na mengine hayapo, yapo kwenye vitabu kwenye ground hayapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, mapori haya yana hali mbaya, tumekuwa tunalia hapa, mapori haya mengine yamevamiwa miaka 35 iliyopita huko nyuma na wamejenga ndani ya hifadhi vijiji, hospitali na barabara. Tumekuwa tunalia hapa mapori haya yalivamiwa miaka mingi iliyopita Serikali haikuchukua hatua, wamesajili vijiji kisheria, wanapeleka huduma, leo Mheshimiwa Waziri anatuambia tuna mapori ya akiba 28, yako kwenye hali mbaya, mengine hayapo katika ground, yapo kwenye karatasi tu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Tabora peke yake tuna vijiji zaidi ya 50 ndani ya hifadhi vina vyeti vya usajili na kila kitu kipo mfano shule na hospitali. Ninayo taarifa hapa kamili ya Kiserikali, Mkoa wa Tabora wenyewe vijiji zaidi ya 50, Wilaya ya Kaliua peke yake tuna vijiji 21 vimesajiliwa kisheria ndani ya hifadhi. Wananchi hawa wamekaa kwa hofu miaka mingi, Serikali tunaiambia hapa miaka 10, lakini hakuna hatua inayochukuliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilitegemea hatua ya leo Mheshimiwa Waziri angekuja na mpango kamili namna gani watu hawa wanashughulikiwa ili waache kuishi kwa hofu, waache kunyanyaswa, wanauliwa mifugo yao, wanaharibiwa mashamba yao, ni shida, ni matatizo makubwa. Watu wa hifadhi wanachokifanya kwa watu ambao wamesajiliwa kisheria siyo halali ndani ya nchi ambayo tunaishi kwa kufuata Katiba na sheria. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa umuhimu naomba nitaje tu kwa ufupi vijiji ambavyo vimeathirika na suala hili. Tuna Vijiji vya Ukumbi Kakonko, Lumbe, Usinga, Ukumbi Siganga, Kombe, Kashishi, Uyowa, Seleli, Nyasa, Mwendakulima, Sasu, Kiwakonko, Nsimbo, Mpanda Mlowoka, Mwahalaja, Chemkeni, Kanoge, Ulanga, Mwendakulima, vijiji 21 miaka yote watu wanaishi kwa hofu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kujibu hapa atueleze nini hatma ya watu hawa na nini hatma ya shule ambazo zimejengwa kule? Hatuwezi kuacha wananchi waendelee kuishi kwa hofu miaka yote, wanashindwa kufanya shughuli za maendeleo, lakini Serikali ipo tu imetulia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende kwenye suala la TFS. Tulianzisha Wakala wa Misitu (TFS) kwa maana ya kuokoa rasilimali ya misitu inayopotea na ndiyo lengo letu kama Watanzania, Wizara na Wabunge. Watu wa TFS wamekuwa ndiyo chanzo kikubwa cha kuangamiza misitu kuliko tulivyokuwa mwanzoni. Leo watu wa TFS hawana mpango wowote makini wa kuja kuokoa misitu, wao wanakaa wanasubiri wachukue mbao, wagonge muhuri mbao isafirishwe. Serikali imeweka utaratibu, imefunga kabisa kutoa magogo kwenye miti ya asili pamoja na mbao kutoka kwenye misitu ya asili. Kwa nini Serikali inaweka malengo kwenye TFS? Kwa nini Maafisa Misitu wanapewa malengo ya makusanyo? Leo misitu yetu inateketea kwa kasi kubwa ya ajabu kuliko ilivyokuwa TFS haipo. Labda hawakupewa malengo, labda Serikali haikuwa na mipango, labda hawajaambiwa wanatakiwa wafanye nini. Hili ni tatizo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, chain saws zilizopo ndani ya maeneo ya misitu ya asili nyingi ni za watu wa TFS. Wao ndiyo wananunua chain saws wanawapa watu wao wanaenda kuweka kule kwenye misitu, kwa hiyo, hakuna tunachokifanya. Naomba Mheshimiwa Waziri akija hapa kuhitimisha atuambie nini hasa kazi na wajibu wa TFS. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, TFS walikuja Kaliua, wamekuja kufyeka mahindi ya wananchi kwenye Jimbo langu, tena leo naomba njaa ikija, muwe wa kwanza kuja kuwalisha chakula wananchi wa Kaliua. Mahindi yalishafikia karibu kuzaa, wanakuja wanaweka beacon ndani ya nyumba za watu. Nimeongea nao kwenye simu hamfanyi kazi kwa weledi? Hamna mpango shirikishi, Wilaya haijui, Mbunge hajui, Mkurugenzi hajui, wanakuja wenyewe wanakwenda kufyeka mahindi ya watu, hawana weledi wa kufanya kazi. Naomba Mheshimiwa Waziri akija hapa atujibu nini kazi ya TFS. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali ikija hapa itujibu, kuna Tume ya Kimahakama iliundwa na Mheshimiwa Rais wa awamu iliyopita, kutokana na ripoti ya Operesheni Tokomeza kwenda kuangalia madhara makubwa waliyopata wananchi nchi nzima, leo ni mwaka wa tatu iko wapi ripoti ile? Iko wapi? Wananchi wanateseka, watu waliuawa, watoto wananyanyasika, mifugo iliteketea, operesheni tokomeza ilikuwa ya kutokomeza watu. Tunaitaka ripoti ya Mheshimiwa Rais hapa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Bunge lako liagize tupate ripoti ya Tume ya Kimahakama ya Mheshimiwa Rais ili tuweze kuangalia namna gani ya kuwasaidia wale watu waliopata madhara makubwa sana na wengine walipoteza maisha. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, ni tozo kwenye hoteli za kitalii ambazo ziko ndani ya hifadhi. Kwa miaka mingi tumekuwa tunazungumzia suala hili la tozo. Tozo zinazotozwa sasa hivi na TANAPA ni za miaka 10 iliyopita wakati vitanda vikiwa vinatozwa dola 50 - 100, leo kitanda kimoja dola 300 - 500, tozo ni zile zile huu ni wizi, haiwezekani! Kwa nini concession fee iwe ya miaka 10 iliyopita? Leo maisha yamepanda, gharama zimepanda, vitu vyote vimepanda Serikali imenyamaza kimya kuna nini hapa? Naomba Mheshimiwa Waziri akija hapa atuambie, Mahakama imeshatoa rulings wale wafanyabiashara walishindwa kwa nini hatuletewi tozo nyingine zinazoendana na hali ya sasa?
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia kidogo kwenye mapendekezo ya mpango ambayo yako mbele yetu. Kwa sababu mengi yamezungumzwa na wengi sitazungumza sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri anasema kwamba pato la wastani la kila Mtanzania kwa mwaka 2015 ilikuwa ni Sh.1,918,928. Nimekuwa najiuliza kwamba takwimu kama hizi zimechukuliwa kutoka katika maeneo gani? Kwa sababu kwa sisi ambao tunaishi na wananchi wetu vijijini wale ambao hawana uwezo wa kupata hata laki kwa mwezi, hawana uwezo wa kupata milo miwili ya uhakika kwa siku, unaambiwa kwamba kila Mtanzania ana uwezo wa kupata milioni moja na laki tisa, nadhani ni lazima Serikali inapochukua takwimu ichukue takwimu vijijini ambapo asilimia 80 ya watu wanaishi kule. Wakichukua takwimu za mjini hawawezi kupata hali halisi ya maisha ya Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi tunavyoongea hali ni mbaya kwelikweli, ni matatizo matupu, ukiambiwa kwamba kila mtu ana milioni moja na laki tisa, unapata mashaka makubwa sana. Kwa hiyo, naomba kwenye takwimu nyingi za Serikali chukueni maeneo ambapo percent kubwa ya Watanzania inaishi kule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni la ongezeko la watu na nimekuwa nashangaa Serikali imekaa kimya sana kutokana na ongezeko kubwa la watu Tanzania. Ukiangalia kwenye sensa mwaka 2012 tulikuwa watu milioni 45 japokuwa wengine hawakuhesabiwa. Kwa takwimu za Mheshimiwa Waziri kwenye hotuba yake 2016 tuko watu milioni 50.1, prediction 2025 tutakuwa watu milioni 63.
Mheshimiwa Mwenyekiti, spidi ya ongezeko la watu haiendani na spidi ya Serikali kutoa huduma muhimu, ni jambo ambalo liko wazi, haiendani kabisa. Ndiyo maana unaona leo wanafunzi wanagoma, mikopo haitoshi, huduma za afya hazitolewi kwa uhakika, elimu bado ni matatizo, Serikali inaogopa nini kuanza kuweka mikakati ya udhibiti wa ongezeko la watu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu wa nchi nyingine, China walivyoweka kwamba mwisho watoto wawili kuna factor waliziangalia na maeneo mbalimbali wanaweka idadi kwamba angalau mtu awe na watoto watatu mpaka wanne ili kuweza kutoa huduma. Haifai na haileti tija watu wazaliwe mshindwe kutoa huduma, ni kama sehemu ya familia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mzazi ukiwa na watoto kumi huwezi kuwapa elimu nzuri, huwezi kuwavalisha vizuri, huwezi kuwapa huduma nzuri, unawatesa. Simple applied kwa Tanzania kuendelea kuona idadi ya watu inaongezeka kwa spidi kubwa lakini Serikali hatuzungumzi chochote ni kuendelea kuwafanya watu wateseke bila sababu. Watu tuwe na watoto ambao tunaweza kuwahudumia vizuri angalau kila mwananchi apate huduma anazostahili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana kwenye suala la kufungamanisha maendeleo ya uchumi na maendeleo ya watu litekelezwe kikamilifu kwenye bajeti ijayo. Nikianza na mpango wa elimu, Serikali kweli imeanza na mpango wa kutoa elimu bure, tunatembea kwenye shule zetu bado fedha inayotolewa kwa retention haitoshi, changamoto ni lukuki katika shule zote. Kila unapokwenda ni kilio, Walimu wanalia wanafunzi wanalia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tumetengeneza madawati, madawati maeneo mengi yako kwenye maturubai, yamewekwa shade kwa kutumia majani hakuna madarasa ya kutosha, lakini pia hakuna miundombinu ya nyumba za Walimu, hakuna vyoo, ukienda kwenye shule zetu bado changamoto ni nyingi sana. Kwa hiyo, kwenye bajeti ijayo lazima Mheshimiwa Waziri aje na mpango mkakati wa kuongeza miundombinu ya madarasa, nyumba za Walimu kwenye shule zetu za primary na secondary. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna suala la kujenga vyuo vya elimu ya mafunzo, kwa spidi ambayo tunaongezeka nayo na kwa sasa hivi Serikali ambapo inasema division one na two ndio inaenda vyuo vikuu wengine wanaenda vyuo vya kawaida, vyuo vya mafunzo, wanafunzi wengi wanabaki vijijini, tunaulizwa maswali hatuna majibu. Tunaomba mpango ujao Mheshimiwa Waziri aje na mpango maalum kuhakikisha tunajenga vyuo vya VETA kwenye Wilaya zetu na atueleze ni vingapi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeangalia kwenye mpango huu hapa amesema mpango ni kumalizia chuo kinachojengwa Mahenge, haitoshi! Tunataka Wilaya zote ambazo hazina vyuo vya ufundi ni lazima vipate vyuo hivyo. Hii iende sambamba na kuweka karakana zinazoeleweka na miundombinu yote ili wanafunzi wetu wapate angalau stadi za kazi waweze kujitegemea kule vijijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la afya. Njia pekee ya kuondoa vifo vya akinamama na watoto, wazee na makundi mengine Tanzania ni kusogeza huduma karibu na walipo. Tulikubaliana na Serikali karibu miaka kumi sasa kujenga zahanati kila kijiji, kituo cha afya kila kata mpaka sasa hivi mpango huo bado unakwenda taratibu. Kwa hiyo, kwenye mpango ujao Mheshimiwa Waziri tunataka atuambie zahanati ngapi zitajengwa, za kutekelezwa siyo za kwenye vitabu, ngapi zitajengwa Tanzania nzima? Ni vituo vya afya vingapi vitajengwa kwenye kata zipi, zianishwe na zitekelezwe kwenye mpango ujao ionekane. Pia kuhakikisha kwamba tunapata watumishi wa kutosha na huduma zote muhimu zipatikane na vifaa tiba na dawa ziwepo za kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni la maji. Watu wanaongezeka changamoto ya maji inaongezeka kila siku. Tunaomba kwenye mpango ujao lazima Waziri atuambie namna gani ya kuondoa changamoto za maji kuendana na ongezeko la watu. Tusingependa mwakani tuanze kushika hotuba ya mwaka huu na ya mwaka kesho hatutaki kama ambavyo Serikali zilizopita. Tunataka tujue yaliyopangwa kwenye bajeti ya mwaka huu yawe yamepita ya mwakani tuwe na mipango mipya inayotekelezeka, tunaomba sana hilo. Kwa hiyo, lazima mipango mikakati ya maji ya kutekelezeka iweze kuletwa ndani ya Bunge, ianishe wazi na ikatekelezwe siyo kuja kubaki kwenye vitabu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mikopo ya elimu ya juu. Nimeangalia hotuba ya Waziri anasema kwa mwakani wanategemea kutoa ruzuku kwa wanafunzi kama 124,243 hata wanaoomba mwaka huu ni wengi zaidi ya hao. Inawezekana Serikali haifanyi tathmini ya kutosha kuanzia sekondari, vyuoni kujua idadi ya wanafunzi wanaohitaji kupata ruzuku kwa ajili ya elimu. Tumekubaliana kwamba kila Mtanzania awe maskini awe tajiri, mtoto wa maskini asome wa tajiri asome. Kama wengi hatuwapatii mikopo wanapataje uwezo wa kusoma mpaka kufika vyuo vikuu na hao ni Marais watarajiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Mheshimiwa Waziri ahakikishe wanafanya tathmini ya kutosha mwakani wawe na uhakika kwamba watoto kadhaa wanakwenda kupata mikopo na wapate mikopo yao kwa ukamilifu. Mtoto wa maskini unampa asilimia 10 au 20 haimsaidii kitu, anaishi maisha magumu kweli shuleni, wanaishi kwa kula mihogo na magimbi. Tunaomba itengwe fedha ya kutosha kuendana na mahitaji ya watoto maskini ndani ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine hakuna mikakati mizuri ya kusimamia…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Hakuna mikakati mizuri ya kukusanya marejesho ya fedha za mikopo. Mimi nilisoma kwa kutumia mkopo wa Serikali, nimelipa miaka mitano iliyopita na nimekamilisha, juzi mwezi Agosti napata barua nadaiwa. Hii ikanipa picha kabisa kwamba hakuna mikakati ya kufuatilia mikopo, kama mtu amelipa miaka mitano iliyopita leo unampa barua anadaiwa, it seems kwamba hafuatilii mikopo inavyotakiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.
Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii ili nami niweze kuchangia kidogo kwenye mkataba ambao upo mbele yetu. Kwa sababu mengi yameshazungumzwa na wenzangu, nitazungumza machache sana.
Mheshimiwa Spika, kwanza linapokuja suala la maslahi ya Taifa lazima tusimame kama Taifa. Japokuwa tuna Umoja wa East Africa, lakini kila nchi ina levels zake za maendeleo ambayo ime-move. Kwa hiyo, tunapoenda kuangalia suala la maslahi ya Tanzania tuasianze kusema kwa nini fulani kasaini, kwa nini Uganda kasaini, kwa nini Kenya kasaini? Yapo mambo ambayo yamemvutia yeye kusaini huo mkataba. Kwa hiyo, kwenye masuala ya maslahi ya Taifa tusimame kama Taifa kuangalia maslahi ya Taifa letu.
Mheshimiwa Spika, ni jambo la kusikitisha kwamba mkataba ambao upo mbele yetu ukiusoma vizuri unaturudisha nyuma karibu miaka 50 tuliyotoka. Unakwenda kutupangia masharti wakati tumepigana angalau miaka 50 tunaanza kuweka sera za uchumi, sera za mapato na sera mbalimbali nzuri, inatuambia sasa kwamba tuache sera zote pembeni tufuate masharti ya EU, hatukubaliani na hilo.
Mheshimiwa Spika, leo tunazo sera ambazo sahihi jinsi ya kukusanya mapato. Mkataba unachambua, zipo changamoto na hasara ambazo tutazipata kutokana na kuingia mkataba huu.
Mheshimiwa Spika, nasema ili muweze kuondokana na hasara hizo, lazima mkae mrekebishe sera za mapato ndani ya nchi zenu, hivi kweli tupo sawa sawa? Cha kusikitisha sana, pia wanatuambia ili muweze kufidia hasara zitakazotokana na kuruhusu biashara free kuingia nchi yetu bila ushuru muweze kukaa muongeze VAT kwenye bidhaa ndani ya nchi yenu ili muweze kufidia hasara.
Mheshimiwa Spika, tukiongeza VAT kwenye bidhaa zetu, tunamuumiza nani? Tunawaumiza wananchi wetu, kwa sababu vyote wanaenda kulipa wananchi wetu. Kwa hiyo, tunalazimishwa sasa kwenda kuwabana zaidi Watanzania kwa sababu tu ya kukidhi matakwa ya Mkataba nchi za Ulaya.
Mheshimiwa Spika, kwenye suala kama hili kiukweli ni lazima tuwe makini, tuwe makini sana jamani. Juzi tulikuwa na bajeti mwezi wa sita, tunataka kwenda kwenye uchumi wa viwanda; ni nchi gani duniani ambayo imeweza ku-move kwenda kwenye industrialization bila kulinda viwanda vya ndani? Hakuna. Hata hao Ulaya ambao leo tunaona wame-move, walilinda viwanda vya ndani.
Mheshimiwa Spika, kwanza sisi mpaka hapa tulipo bado ni soko la bidhaa za wenzetu, ni soko la pamba-stick, ni soko la Wachina, ni soko la Wakenya, ni soko la wengine. Haitoshi tu tukafungue wazi, sisi tuwe kazi ni kuzalisha na kupeleka.
Mheshimiwa Spika, kama tunataka ku-move na mikataba kama hii na mikataba mingine naomba, kama Taifa lazima tuje tuwe na watu ambao tunapokuwa na mikataba kama hii waende ku-negotiate; negotiators wenye uwezo mkubwa. Kwa sababu mkataba kama huu haukutakiwa hata sisi kuja kuujadili; ulitakiwa uishie huko huko! Baada ya kuona kwamba hatuna maslahi nao, wanapiga pembeni, tunasonga mbele kwenda na mambo mengine ambayo yana maslahi kwa Taifa letu.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, lazima sisi Wabunge tuisimamie Serikali vizuri, tuje tuwe na watu wenye uwezo, capacity thinking nzuri ya kuweza kuwa negotiators kwenye mikataba kama hii hasa ya kitaifa ambayo tusipoiangalia vizuri, kipengele kimoja tu kinaweza kutu-switch tunajikuta kwamba tunaenda kuwa watumwa wa nchi nyingine badala ya ku-move kwenda mbele kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu.
Mheshimiwa Spika, naungana na wenzangu Wabunge wengine wote kwamba mkataba kama huu hautufai na hata kama utatufaa, ni huko mbeleni. Pengine miaka 50 ijayo tuwe tume-move kidogo tumekuta wenzetu. Kama Wakenya, leo Kenya ni nchi ndogo, lakini kila nchi pia ina factors zake. Leo Tanzania tupo karibu milioni 50. Wakenya wenyewe ni wachache, lakini pia sera zinatofautiana. Kwa hiyo, lazima tuangalie factors nyingi nyingi kuhakikisha kwamba mikataba ya Kimataifa kama hii tunaipitisha. Kila mkataba unaopitishwa, tuangalie maslahi yetu, tusiangalie East Africa kwa sababu kila mmoja anapambana kwenye uwanja wake.
Mheshimiwa Spika, kwa hayo machache, nakushukuru sana kwa nafasi hii. Ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Waziri kwa hotuba nzuri pamoja na watendaji wote wa Wizara kwa kazi inayoleta faraja kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi nzuri inayoendelea kufanywa yapo mambo yanayohitajika kufanyiwa kazi kuwa nguvu:-

- Wizara kuongeza speed ya kupima ardhi yote ya Taifa hili. Kiasi cha asilimia 15% ni kidogo sana, eneo kubwa bado halijapimwa.

- Kupima maeneo kwa ajili mifugo na malisho. Sheria ya Ardhi imeelekeza Waziri kutenga ardhi kwa ajili ya mifugo na malisho, kuyagazeti na kuyalinda.

- Serikali itueleze ni maeneo kiasi gani na wapi maeneo ya malisho yametengwa na kupimwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuongeza speed ya kuanzisha Mabaraza ya Ardhi katika Wilaya zote hapa nchini, ili kurahisisha usuluhishi wa migogoro ya ardhi. Mabaraza tuliyonayo ni 53 tu, yanayofanya kazi ni machache sana. Mabaraza haya yawezeshwe kifedha ili yaweze kutekeleza majukumu yao vizuri. Pia Serikali iwezeshe Wajumbe wa Mabaraza kwa kuwapa posho wanapokaa wafanye kazi yao vizuri. Serikali/Wizara kufanya follow-up kwa Maafisa Ardhi popote walipo watekeleze majukumu yao kwa kuwajibika na kuuza ardhi mara mbili (double allocation).

Mheshimiwa Mwenyekiti, Viongozi wa Vijiji wapewe elimu wafuate Sheria ya Ardhi katika kugawa ardhi ya wananchi. Viongozi wanakula rushwa wanauza maeneo makubwa bila kuitisha mikutano ya wananchi. Waziri atoe tamko hapa Bungeni lakini pia semina kwa viongozi wa Vijiji ni kiasi gani cha ardhi kinaweza kuuzwa na viongozi wa vijiji na kiasi gani hawaruhusiwi. Wafugaji wanapokelewa vijijini wanatoa fedha nyingi, wanapewa maeneo ya kufugia wakati wananchi wengine hawana habari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima kama Taifa tuwaze miaka 100 ijayo mbele. Leo tunajivunia Tanzania tuna ardhi kubwa, tusipopanga matumizi bora na hii ardhi tutakosa ardhi kwa matumizi muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mashirika na Taasisi zinazojenga majengo na nyumba za makazi wajenge nyumba kwenda juu (flats) na sio kwenda chini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wawekezaji wa miradi mbalimbali wapewe ardhi kuendana na mradi wao au eneo linalofaa kwa mradi huo. Maeneo ya kilimo yabaki kwa kilimo, maeneo ya malisho yabaki kwa malisho na maeneo ya ujenzi yasiwe ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la uanzishwaji wa miji kiholela bila utaratibu; maeneo mengi kila leo miji mipya imeanzishwa kando kando ya barabara, hakuna maelekezo yoyote, hakuna udhibiti, hayo yanakuwa makazi holela.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Watumishi House waongeze speed ya kujenga nyumba za watumishi, speed yao ni ndogo sana. Wafike kwenye wilaya mpya ikiwepo Kaliua wajenge nyumba za watumishi kusaidia makazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Nyumba (National Housing) waliahidi kuja Halmashauri ya Kaliua kujenga nyumba tangu mwaka 2016. Napenda kujua ni lini watafika na maeneo tulishayatayarisha ya kutosha na yapo mjini.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, tunajadili mapendekezo ya Mpango wa Bajeti ya mwaka 2017/2018 huku Serikali ikiwa haijatoa fedha za maendeleo kwa ajili ya miradi kwenye halmashauri na wilaya kwa sehemu kubwa na hivyo kusababisha miradi kudorora.
Mheshimiwa Naibu Spika, hotuba ya Waziri wa Fedha inaonesha wastani wa pato la kila Mtanzania ilikuwa sh. 1,918,928/= sawa na USD 96.5 mwaka 2015.
Hizi takwimu haziendi na hali halisi ya wananchi wengi zaidi ya 809 wanaoishi vijiji ambao hawana uwezo wa kupata hata 100,000 kwa mwezi. Wengi wanapata mlo mmoja tu kwa siku. Serikali itueleze ni maeneo gani ya nchi yetu ambapo takwimu hizi zinatolewa/zinachukuliwa ambapo hazitoi hali halisi za maisha ya watu wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ongezeko la watu ndani ya nchi yetu ni kubwa sana haliendani na uwezo wa Serikali kutoa huduma muhimu na za uhakika. Ikiwa sensa ya mwaka 2012 tulikuwa watu milioni 45 mwaka 2016 tunakadiriwa watu milioni 50.1 na mwaka 2025 tutakuwa milioni 63 hii ni hatari kwa ustawi wa watu wa Taifa letu. Kwa mikakati gani ya Serikali kudhibiti ongezeko na kasi kubwa ya ongezeko la watu kwa nini Serikali inanyamaza kimya wakati inaona hatari iliyoko mbele?
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima Serikali ihakikishe kipengele cha kufungamanisha maendeleo ya uchumi na maendeleo ya watu kinatekelezwa kikamilifu; mpango wa elimu bure umesaidia kupunguza machungu kwa wazazi na watoto wengi kuandikishwa mashuleni, bado fedha inayotolewa ni kidogo haitoshelezi mahitaji ya watoto na shule zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye mpango ujao lazima Serikali iongeze fedha ya capitation zinazopelekwa mashuleni baada ya kufanya tathmini na kutambua mahitaji ya wanafunzi ili wapate elimu nzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwenye mpango ujao ilete mpango kamili wa kujenga vyuo vya mafunzo ya ufundi (VETA) kwenye Wilaya zote hapa nchini ambazo hazina mahitaji ya vyuo vya VETA, ni muhimu sana kwa ajili ya kujenga stadi za kazi kwa watoto wanaofeli wanaokosa nafasi ya kujiunga na vyuo vikuu na vyuo vingine vya mafunzo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka mpango ujao uoneshe mikakati ya kujenga zahanati kila kijiji na vituo vya afya kila kata ili kuokoa maisha ya watu yanayopotea kwa sababu ya huduma za afya kuwa mbali na watu. Njia pekee ya kupunguza vifo vya watoto na wanawake, wazee na makundi mengine ni kutotekeleza mpango wa kupeleka huduma hizi jirani na wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, upatikanaji wa maji safi na salama; tatizo la ukosefu wa maji ni kubwa sana linazidi kukua kutokana na ongezeko kubwa la watu. Mpango wa mwaka 2017/2018 lazima Serikali ioneshe mkakati wa kuondoa tatizo la maji, miradi mikubwa ya maji, Mkoa wa Tabora kutoa maji Ziwa Victoria, mradi wa maji kutoka Malagarasi kwenda Kaliua na Urambo na miradi yote ya kimkakati katika maeneo mengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, mikopo ya elimu ya juu; mpango ujao kwanza tathmini ya uhakika ifanyike kuanzia mashuleni na vyuoni ili kubaini mahitaji halisi/wanafunzi wanaohitaji kunufaika na mikopo hiyo ili kutenga fedha za mikopo ya elimu ya juu kuendana na mahitaji na kuwezesha watoto wa maskini kupata elimu mpaka vyuo vikuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa mapato yote ya Serikali kuingizwa kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali kufuta utaratibu wa retention uangaliwe kwa mapana. Lisipoangaliwa vizuri kuna taasisi na mashirika ya Serikali yataathirika sana – mashirika yanayojiendesha yenyewe bila ruzuku ya Serikali na yanalipa kodi zote stahiki na asilimia zilizoelezwa na Serikali mfano mashirika ya uhifadhi mfano TANAPA, Ngorongoro, TAWA, TFS, NHC.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mifugo na Uvuvi
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, pongezi kwa Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na wataalam wote wa Wizara kwa kuandaa hotuba na kuwasilisha hapa Bungeni.

Mheshimiwa Spika, Tanzania ni nchi ya pili katika Afrika kwa kuwa na idadi kubwa ya mifugo, hata hivyo idadi hiyo haijaweza kuchangia kikamilifu katika pato la Taifa kutokana na changamoto nyingi zinazoikabili sekta ya mifugo. Wafugaji wa Taifa hili wamekuwa wanahangaika sana kwa kukosa malisho na huduma muhimu na hivyo kusababisha migongano ya wafugaji na wakulima na watumiaji wengine wa ardhi.

Mheshimiwa Spika, Sheria za Ardhi na Maliasili zinaelekeza Mawaziri watenge maeneo ya mifugo na kuyatangaza kwenye gazeti na kuyalinda. Sasa Serikali ieleze hapa ni maeneo gani yametengwa kwa ajili ya mifugo na malisho ya mifugo, yako mikoa na wilaya zipi?

Mheshimiwa Spika, wafugaji wamekuwa wanakamatiwa mifugo yao kwenye hifadhi za misitu, inapigwa mnada hata pale Mahakama inapotoa hukumu kwamba irudishwe kwa wenyewe. Waziri wa Mifugo anashughulikiaje suala hili ambalo limewafilisi wafugaji wengi na wamebaki maskini?

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango gani kuhakikisha nyakati za mvua vyakula vya mifugo vinaandaliwa na kutunzwa kwa ajili ya matumizi ya nyakati za ukame, Kilenge’s Silage na kadhalika?

Mheshimiwa Spika, kuna mpango gani wa Serikali kutengeneza na kuendesha kampeni za unywaji maziwa mashuleni na katika jamii nzima? Sote tunafahamu umuhimu wa maziwa na kwa ng’ombe tulionao Tanzania inawezekana kabisa kila shule kupata maziwa kwa watoto wetu.

Mheshimiwa Spika, viwanda vingi vya kuchakata mazao ya mifugo vimekufa hali inayopelekea wafugaji kukosa masoko ya uhakika kwa mifugo yao. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha viwanda vyote vya ngozi, nyama na kadhalika vinafanya kazi? Naomba Waziri aje na majibu ya nini mkakati wa kufufua viwanda hivyo.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia hotuba ambayo ipo mbele yetu; na nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa nafasi ya kuweza kusimama tena kwenye Bunge lako Tukufu. Naomba pia niungane na Wabunge kupongeza kazi ya REA inayofanyika maeneo mbalimbali ya kuweza kuongeza juhudi za umeme hapa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati Mheshimiwa Waziri anazindua REA III mwaka 2017 kwanza alisema kwamba itaenda speed, alisema hata kwa wakandarasi aliokuwa anawapa maagizo; na pia kwamba ile REA III itakwenda mpaka kwenye vitongoji tofauti na REA awamu ya kwanza na REA awamu ya pili. REA hii awamu ya tatu kwanza inakwenda taratibu sana; na ingawa Mheshimiwa Waziri anatembelea maeneo mbalimbali lakini akishafika kule akitoka bado speed inakwenda slow vilevile.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo langu la Kaliua tulipewa vijiji saba tu REA III, lakini mpaka napoongea huu ni mwaka wa pili kilichowaka umeme ni kijiji kimoja tu na imewekwa transfoma moja tu; vijiji vingine vitatu wamepeleka nguzo nyaya bado na vijiji vingine 3 bado kabisa hawajafika. Sasa kwa speed hii tunayokwenda nayo Mheshimiwa Waziri itachukua miaka mingapi hata kwa hivyo saba tu kukamilika? Achana na vingine ambavyo bado.

Mheshimiwa Naibu Spika, speed ya REA bado ni ndogo. Fedha hii ya REA ni ring fenced, iko pale, haifanyi kazi nyingine, lakini speed imekuwa ni ndogo sana kila siku kuna vikwazo. Kwanza walikuwa wanasema ni nguzo, nguzo zikija wanasema ni nyaya, nyaya zikija wanasema ni tranfoma, kwa hiyo kila siku ni matatizo. Namwomba Mheshimiwa Waziri, speed ile ambayo mlikuwa mmeanza nayo mara ya mwanzo kushinikiza wakandarasi wafanye kazi kwa muda wafuatiliwe wafanye kazi kwa muda. Mwaka jana wakasema ni mvua nyingi mwaka huu mvua haziko nyingi. Kwa kweli tunasikitika kwamba speed ya REA ni ndogo pamoja na kuwa fedha ya REA iko ring fenced kazi yake ni hiyo moja tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili, ndani ya Wilaya ya Kaliua umeme umekuwa ni kizungumkuti, imekuwa ni kumulimuli. Mheshimiwa Waziri kila siku ya kwa Mungu, hata leo, tunakosa umeme masa sita mpaka nane, kila siku. Kwa hiyo kwa maana nyingine ule uwepo wa umeme hauonekani, maana umeme ukiwepo usaidie jamii kunufaika, mashine zifanye kazi, welding wafanye kazi, saluni zifanye kazi, vile viwanda vidogovidogo vifanye kazi. Sasa kama wanafunga kwa muda wa masaa nane kwa siku hauna faida.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri tulikuwa na shida ya nguzo kwenye maeneo ambayo ni mbuga, ukaagiza tangu mwaka jana zibadilishwe; mpaka leo shida ya Kaliua katika umeme iko pale pale. Hivi navyoongea leo kuanzia saa moja asubuhi mpaka saa nane walikuwa hawana umeme; na huu ndio utaratibu, hiyo ndiyo historia ya Kaliua. Mheshimiwa Waziri umeme ni maendeleo, umeme ni uchumi; leo uchumi wetu hauwezi kupanda kama vijana kwa masaa nane kwa siku hawafanyi kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni suala la kujenga substation. Kwenye bajeti ya mwaka jana Mheshimiwa Waziri alituambia kwamba vinajengwa vituo viwili kati ya Kaliua na Urambo na Kaliua na Uvinza; na nina imani kabisa inawezekana kujenga hiyo substation ukaweza kusaidia angalau umeme labda wakapokelea pale kwenye hiyo ki- substation ukawa umeme wa uhakika. Naomba, vile vituo Mheshimiwa Waziri havikujengwa kwenye bajeti ya mwaka jana, mwaka huu unapokuja ku-windup utuambie, je, mwaka huu vitajengwa? Ili angalau tuweze kuondokana na shida ya umeme. Leo umeme ni uchumi lakini kwa mwendo tunaoenda nao Kaliua, maeneo ya Urambo na maeneo mengine bado hatuoni faida kubwa sana kwa sababu tunaona nguzo na nyaya tu lakini umeme hautumiki kama inavyotakiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala linguine, Mheshimiwa Waziri amekuwa anatamka hapa Bungeni, nje ya Bunge na hata ndani ya Bunge kwamba pale REA inapoishia TANESCO ipeleke umeme kwa shilingi 27,000 vijijini, lakini hilo halitekelezwi, sasa sielewi kwamba maagizo haya hawajapewa TANESCO? Wilaya ya Kaliua tuna zaidi ya watu 160 wameomba wafungiwe umeme, wamefanya wiring hawapelekewi umeme na shilingi 27,000 wanayo. Hiki kingine ambacho TANESCO wanasema kwamba lazima kuwepo na nguzo, Mheshimiwa Waziri inakuwa ni double standard.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama REA imepeleka umeme mpaka maeneo fulani halafu kuanzia pale mwananchi anaambiwa alipe nguzo 338,000, kama ni nguzo mbili ni 480,000, kama ni nguzo tatu ni 900,000 ilhali mwenzake hapa jirani tu kafungiwa umeme kwa shilingi 27,000; hiyo ni double standard. Naomba Mheshimiwa Waziri utuhakikishie unapokuja ku-windup kesho hapa, utuambie namna gani wananchi wa vijijiini maeneo ambapo REA imeishia wanaweza kupata umeme kwa gharama ile ile unayosema kila siku, 27,000, kwa sababu ni haki ya kila mmoja kuweza kupata umeme kwa bei ambayo ni standard na ambayo itakuwa ni haki kwa wengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, limekuwepo tatizo lingine kwenye uwekezaji kwenye sekta ya mafuta. Tumekuwa tunalalamika kwamba kuna vikwazo vingi vingi kwenye masuala ya uwekezaji hapa Tanzania kwenye maeneo mbalimbali. Hata kwenye sekta ya mafuta pia lipo tatizo la uwekezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, unapotaka kuwekeza kwenye sekta ya mafuta aidha kujenga kituo cha mafuta kuna milolongo mingi sana ya kupitia, pia kuna vibali vingi sana vya kupitia. Ukianza na NEMC wanachukua mwaka, ukienda halmashauri unaomba kibali miezi sita, ukitoka tena ukienda EWURA miezi 6, useme uende OSHA miezi sita. Miaka miwili na nusu unahangaika tu na kibali huujakipata uanze kujenga kwa mwendo huu mwekezaji yeyote aliyejiandaa ataweza? Hawezi kwa hiyo tunaomba kuwepo na one stop center, kama ni masuala yafanyike kwa pamoja ili mtu anapokuwa na lengo la kuwekeza aweze kuwekeza kwa kirahisi kwa sababu uwekezaji ndio uchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine pia ambalo ni tatizo ni faini kubwa sana wanazopigwa watu wa mafuta. Sekta hii unakuta kwamba wale ambao ni wakubwa ndio wanaoweza kuwekeza tu, wale wadogo wanaojichomoza hawawezi; kwa sababu mtu mkubwa ana mitaji mikubwa, anaweza akawa anasubiri vibali huku anaendelea na mambo mengine; lakini kwa yule ambaye anayechipukia ambao ndio tunaowalenga, Watanzania wa chini wenye uwezo mdogo, waweze kunyanyuka, wanakwama.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tunaomba; wakati mwingine kuna faini kubwa sana zinapigwa kiasi kwamba mtu ana mtaji wa milioni 10, anapigwa faini milioni 20, umemuulia pale pale na bado unamdai. Faini tulizokubali ziwepo pale mtu anapofanya kosa ziendane na hali halisi kwa sababu tunapenda hawa wenzetu ambao ni wa chini pia waweze kunyanyuka kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wanachangia uchumi na ni sehemu ya maendelo ya taifa lao.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni hizi criteria za kampuni za mafuta au watu wanaofanya biashara za mafuta. Kumekuwepo na criteria mbalimbali, kuna watu wanaitwa CODO, kuna wengine wanaitwa DODO, na wengine ni wale wa chini kabisa. Unakuta mtu ambaye anaagiza mafuta kwa jumla na yeye pia anaruhusiwa tena kwenda kuuza kwa rejereja. Kwa hiyo wale wanaoagiza mafuta kutoka nje wanakuja wanauziana kampuni madogo ndogondogo nao pia wanaruhusiwa kufungua vituo vidogo vya mafuta wanauza reje reja; kwa hiyo ile fair competition inakosekana. Wakati huo umemuuzia mtu mdogo mdogo reje reja pembeni yake wewe unakwenda kufungua tena kituo kwa bei ya reja reja. Kwa hiyo wewe una faida kwa sababu kwanza ulishauza kwa bei jumla, pili unawezo wa kupunguza bei kwa sababi tayari unapata faida mara mbili. Mheshimiwa Waziri, kwa nini Wizara inaruhusu haya? Matokeo yake wale ambao ni wadogo hawawezi ku-compete kwenye biashara, mara nyingi unakuta wameondoka.

Mheshimiwa Naibu Spika, na ndiyo maana ukisoma kwenye kitabu cha Mheshimiwa Waziri unakuta kuna mahali kuna vituo 73 baada ya mwaka vimefungwa vitano kwa sababu wanaofunga ni wale wadogo ambao wanashindwa ku-compete na biashara. Tunaomba hizi criteria ziheshimiwe; Kama mtu anaagiza mafuta nje; kama yeye ni mtu mkubwa na ana uwezo wa kuagiza mafuta nje abaki kuagiza mafuta nje. Mheshimiwa Waziri wale ambao ni CODO wanaoagiza mafuta nje akishamuuzia mwenzake na ile criteria nyingine waweze kuhakikisha kwamba wao wanawaachia kwenye sekta ile tena wauze. Wale wa chini kabisa kule ambao ndio DODO waweze kuwa na uwezo wa kuweza kuuza pia…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa kengele ya pili imeshagonga, ahsante sana.

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana ahsante.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Pia namshukuru Mwenyezi Mungu aliyetupa kibali sisi Wabunge wote na viongozi wote wa Bunge pamoja na Watumishi wa Bunge kuweza kufikisha Bunge hili la Kumi na Tisa, Mkutano huu wa mwisho.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue nafasi hii kutoa shukrani za dhati kwa viongozi wote wa Bunge, viongozi wa Serikali, viongozi wa taasisi mbalimbali, viongozi wa vyama vya siasa, wanachama wote nchi nzima pamoja na wananchi wote walioungana nasi kipindi cha msiba wa Katibu wetu Mkuu aliyetutoka tarehe 30 Aprili, 2020 Mheshimiwa Khalifa Suleiman Khalifa. Mungu awabariki sana kwa moyo wa upendo na Mungu aendelee kumweka mahali pema Peponi kiongozi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende moja kwa moja kwenye Wilaya ya Kaliuwa. Hospitali yetu ya Wilaya ambayo kwa asilimia 80 imejengwa kwa fedha za wananchi wa Kaliuwa, kwa maana ya mapato ya ndani kwa asilimia 80, mwaka 2019 tulipata usajili wa muda kwa maelekezo kwamba tukamilishe baadhi ya majengo muhimu kama theater majengo ya wazazi ili tupate usajili wa kudumu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2019 tulitengewa shilingi bilioni 1.5. Ninashukuru kwamba tumepata shilingi milioni 500 tu, mpaka sasa hivi shilingi bilioni moja hatujapata. Kwa kweli ninaiomba Serikali, kwa jicho la pekee waweze kukamilisha ile shilingi bilioni moja iliyobaki kabla ya mwaka huu wa fedha kwisha ili hospitali ile ya Kaliuwa iweze kukamilika na kupata usajili wa kudumu, wananchi waache kuhangaika kwenda Hospitali za Kigoma, Urambo, Tabora na maeneo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba suala la watumishi wa afya kwa Wilaya ya Kaliuwa, tatizo sugu kubwa sana; mwaka 2018 nililia hapa Bungeni, Mheshimiwa Waziri wa Utumishi akaniambia nilete maombi rasmi kwa Sekta ya Afya nikaleta maombi rasmi tuliokuwa na tatizo, lakini tulipewa watumishi sita tu tangu mwaka 2018 na bado wengine wanahama. Kwa hiyo, bado kilio chetu kiko pale pale. Tunaomba Kaliuwa tuangaliwe kwa jicho la pekee kwa suala la watumishi wa Sekta ya Afya. Tumejenga Zahanati na Vituo vya Afya; Zahanati ina watumishi wawili na Kituo cha Afya kina watumishi watatu. Ni tatizo! Kwa hiyo, naomba suala la watumishi lipewe kipaumbele cha kutosha katika Wilaya ya Kaliuwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Walimu wa Sayansi kwa Wilaya ya Kaliuwa ni tatizo. Tumehamasisha watoto wetu, wameanza kupenda kusoma sayansi, lakini pia tunaenda kwenye uchumi wa viwanda. Hatuwezi kwenda kwenye uchumi wa viwanda hatuna Walimu wa Sayansi. Walimu hawa ni wachache; shule inakuwa na Walimu wa Sayansi wawili, anachukuliwa mmoja anahamishiwa shule nyingine. Kwa hiyo, shule nzima inakuwa na Mwalimu wa Sayansi mmoja, ni tatizo. Tunaomba Serikali iangalie namna gani ya kuondoa changamoto kubwa ya Walimu wa Sayansi katika Wilaya yetu ya Kaliuwa na ninadhani pia ni suala la nchi nzima.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2019 Mheshimiwa Waziri wa Utumishi alitoa waraka kwa Halmashauri zote kuhakikisha kwamba walimu na watumishi wanapandishwa madaraja. Bado kupandisha watumishi madaraja ni tatizo. Wilaya ya Kaliuwa inaweza kuwa na tatizo kubwa zaidi, kwa sababu kuna walimu wamekaa tangu mwaka 2013 mpaka leo hajawahi kupanda daraja hata moja. Mwalimu huyu tunampa moyo gani wa kufanya kazi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2018 kuna waliopewa barua za kupandishwa vyeo. Wameenda kusoma, tena wamejisomesha au wamesomeshwa na Serikali, lakini wamerudi hawajapandishwa cheo chochote; siyo mishahara wala siyo cheo. Bahati mbaya mwaka 2018 wamepewa barua mwaka 2019 wamenyang’anywa zile barua za kupandishwa vyeo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa mwalimu kama huyu, mpaka wengine wameamua kuacha kazi kwa sababu hatuwatendei haki. Kwa nini Mtumishi wa Serikali apandishwe cheo kwa barua, halafu uje mnyang’anye ile barua ya kumpandisha cheo, ni Wilaya ya Kaliuwa tu au na wilaya nyingine?

Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali ifuatilie, ni kwa nini Wilaya ya Kaliuwa walimu hawapandishwi vyeo, hawapandishwi madaraja na kwa nini wale wengine walipewa barua za kupandishwa madaraja halafu wakaja wakanyang’anywa leo wana miaka mitano, wana miaka sita, wana miaka nane hawajapanda madaraja? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni suala la shule za Kata. Tunatambua shule za kata kiukweli zimesaida Taifa hili sana, kila mmoja ata-acknowledge hicho kitu. Watoto wetu hata wa maeneo ya vijijini wamepata elimu kwa mazingira hayo hayo, lakini angalau wamepata elimu. Tukumbuke waliosaidia shule hizi za kata 2007 ni walimu waliolelewa kwa mpango wa crash program; Walimu ambao walitolewa, wakaambiwa njooni mkafundishe watoto hawa. Wengine walikuwa na fani nyingine mbalimbali, wakaambiwa yeyote mwenye kutaka kuja kufundisha, aje akafundishwe kwenye crash program, wakafundishwa, wakaja kufundisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, 2007 wamefanya kazi miaka 10, mwaka 2017 wakaondolewa kama wezi, bila chochote. Kwa kweli Serikali hatukutenda haki. Hata kama kulikuwa na makosa, waliambiwa wajiendeleze, wengine walikuwa vyuoni wanasoma, wengine washajiendeleza, wengine walikuwa hawajachukua hatua yoyote; walioko mashuleni wametoka, wameshaondolewa kazini; waliokuwa wanajiendeleza wamefika degree, wengine wamefika mwaka wa pili ameondolewa kazini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hebu Serikali iangalie namna ya kuona juhudi walizofanya kuendeleza Shule za Kata kwa 10 years wanaondolewa kama vile wameiba, hawakutendewa haki. Wana familia, wamehudumu katika Taifa hili kwa moyo wao wote, wengine walitaka kuwa wafanyabiashara, wakaamua kuwa walimu. Tuwaangalie kwa namna ya pekee. Ninaiomba Serikali iangalie namna gani kuwatia moyo angalau wamalizie masomo yao waone jinsi ya kuweza kuwarudisha kazini waendelee kufanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni la TARURA. Napongeza kazi nzuri ya TARURA wanayoifanya, lakini barabara zetu zimebomoka sana, sana na fedha wanayopewa TARURA haitoshi. Kwa hiyo, bado tatizo ni kubwa. Wilaya ya Kaliuwa peke yake tuna mzunguko wa ndani barabara za udongo, barabara za TARURA 1,370.5, tunapata kwa mwaka mzima shilingi milioni 600.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2019 tulipata shilingi milioni 675, mwaka huu tumepata shilingi milioni 625, inazidi kupungua, lakini mvua ni nyingi na barabara zimekatika. Kwa hiyo, bado wananchi wanashindwa kupitisha mazao yao kwenye barabara mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeshaomba mara nyingi Bungeni namna gani TARURA iongezewe fedha, kiukweli wanafanya kazi bila kupewa fedha. Shida ni kwamba fedha hawapewi, ni kidogo sana na mzunguko wa barabara ni mkubwa. Kwa hiyo, wanashindwa kutekeleza wajibu sawa sawa na ile kazi ambayo wamepewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, niende kwenye suala lingine. Mheshimiwa Rais alitoa ahadi Wilaya ya Kaliuwa ya kilometa saba za lami katikati ya mji. Natambua ahadi za Mheshimiwa Rais zinatekelezwa na TAMISEMI. Kaliuwa huu ni mwaka wa tano, Mheshimiwa Rais anaenda kumaliza muda wake, hata robo kilometa hatujawahi kupata. Ninaiomba Serikali iangalie, kilometa saba, hata moja kweli! Hivi Rais anavyokuja wakati mwingine kuja kuomba ridhaa ya wananchi wale, atawaambia hata kilometa moja ameshindwa kuwapa kweli jamani! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali iangalie ahadi za Mheshimiwa Rais ambazo wengine wamepata angalau kilometa mbili, kilometa moja; Kaliuwa na wananchi wake nao wana haki ya kupatiwa japo kilometa chache ili angalau anapokuja Mheshimiwa Rais kwa ajili ya kuomba kura kwa wakati mwingine awe na cha kusema kwa wale wananchi ambao aliahidi hadharani na nina imani kabisa kwamba watakuwa wanamhoji maswali mengi kuhusiana na suala hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa muda nilioupata Naendelea kuwashukuru wananchi wa Kaliuwa kwa kunitia moyo na kuendelea kuniamini na kuwatumikia. Nami nina imani kwa kipindi hiki tukimaliza na Serikali isaidie kutekeleza ahadi ambazo ilikuwa imeahidi ili angalau tunapokwenda kwenye kampeni tuwe na ya kusema. Ahsante sana. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Taasisi ya Utafiti wa Kilimo, wa Mwaka 2016
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia kwenye Muswada ulioko mbele yetu na mchango wangu utajikita kwenye Muswada wa kuanzisha Taasisi ya Utafiti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Muswada huu nilipoenda kwenye lile jedwali namba tatu, nikaangalia maeneo ya utafiti nikaona almost tume-cover mambo mengi sana, ukiangalia karibu kila kitu, kwenye uboreshaji wa mazao, afya ya mimea, utafiti, mavuno, matumizi ya ardhi kilimo, usimamizi, mambo mengi yamekuwa covered. Nilipokuja kwenye namba 26 namna ya kupata fedha kwa ajili ya kutekeleza yote haya yaliyoko hapa karibu mambo 11 sioni dalili za kutekelezwa kwa mambo hayo kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ukiangalia source za fedha ni hiyo mikopo, ruzuku ya Serikali, kuangalia ruzuku itakayopangwa, posho, sheria hii tunataka ituambie namna gani fedha zitapatikana kutekeleza hapa. Mimi nina imani kwa kupitia sheria hii kama kweli tutapata fedha za kutosha, tumekuwa na magonjwa ya mimea ya muda mrefu, tuna magonjwa ya migomba kule Bukoba zaidi ya miaka 20 utafiti hautoi majibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna magonjwa ya machungwa leo hatusafirishi machungwa nje kutokana na kwamba magonjwa hayapatiwi majibu. Tuna magonjwa ya mihogo, tuna magonjwa ya nazi, hatuwezi kama hatuna namna ya kupata fedha za kutosha. Kwa hiyo, shida kubwa ya Muswada huu hakuna namna ya kupata fedha kutekeleza haya yaliyoainishwa yote kwenye hili Jedwali Namba Tatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa na Vyuo vyetu vingi tu vya utafiti hapa nchini vyuo vilikuwa 16 vyote leo tunaambiwa vitakuwa chini ya hii Taasisi ya Utafiti, Vyuo hivi siyo kama vilikuwa havina wataalam, vilikuwa na wataalam wa kutosha, wana majengo yao mazuri, tatizo ni financial support. Kuna wataalam wenye uwezo, kuna Madokta lakini tatizo hakuna fedha, hakuna vitendea kazi, hakuna madawa ya maabara, matokeo yake vimekuwepo kama ni picha. Kwa hiyo ni lazima kwanza sheria hii ituambie namna gani tunapata fedha za kutosha kuweza kuendesha Taasisi ya Utafiti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliweka utaratibu ndani ya nchi yetu kuhakikisha kwamba angalau asilimia moja ya mapato ya nchi ndani ya mwaka yanakwenda COSTECH hatujaweza kufika hata hapo. Kwa hiyo, hata tungekuja na sheria nyingi kiasi gani, kama hatutoi fedha, hakuna utafiti usiokuwa na fedha, hakuna mafanikio ya utafiti ambao haujawekezwa, kuwa na utafiti ni kuwekeza vya kutosha. Nimeona hiyo ndiyo kwanza shida kubwa sana kwenye Muswada wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana kabisa na maoni yaliyotolewa kwamba lazima tuje na Mfuko Maalum wa Utafiti, tuwe na nidhamu nao na uwe ring fenced tuhakikishe kwamba fedha inakuwepo. Leo hii tunaposema tunaingiza mpaka mambo ya mazingira, nimeshukuru sana kwamba angalau sasa tunaanza kuoanisha hata kilimo na mazingira, kilimo na mabadiliko ya tabianchi, kilimo na matumizi bora ya ardhi, ni mambo mengi lakini kwa namna gani? Naomba sana sheria hii ingeanza kwanza namna gani tunapata fedha, hapo ningejisikia burudani kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima Mheshimiwa Waziri hapa atuambie namna gani tunapata fedha ya uhakika, siyo tunasema tu kwenye bajeti ya Bunge, kwani miaka yote hatutengi, tunatenga lakini haiendi! Mara tozo haziendi, hivyo kwanza ni financial support namna gani tunawekeza kwenye taasisi hii iweze kuwa na mafanikio.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine nikienda kwenye Muswada wenyewe sasa kwenye baadhi ya vifungu, kwenye Kifungu cha nne (4), kinasema kuhamasisha matumizi ya uzalishaji mbegu. Hapa ni kweli tumekuwa na shida katika nchi yetu kwa muda mrefu, asilimia 60 ya mbegu za Tanzania zinatoka nje na ni makampuni ya nje, mbegu zetu nyingi zimedumaa, leo ukienda kwenye maduka ya mbegu za mazao wanakwambia kabisa tunataka mbegu fulani kwanza zile za nje ni expensive, watu hawawezi kuzimudu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia pamoja na hiyo wafanyabiashara wale wanakwenda mpaka vijijini kwenda kuhamasisha zinanunuliwa. Kwa hiyo ni expensive halafu nyingine zinafanyiwa majaribio kwa kuwa hakuna utafiti ambao unatangulia. Ningeshukuru sana, kwa kupitia Muswada huu nina imani sasa tutakuwa na uhakika tunazalisha mbegu ndani ya nchi yetu za kutosha, lakini pia wananchi wetu wahamasishwe watumie mbegu za ndani ya nchi yetu na hivyo tuhakikishe kwamba tunajitosheleza vya kutosha kwa kutumia mbegu za mazao kutoka ndani ya nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha tano (5) napendekeza wale Wajumbe wa Bodi lazima kuwepo angalau Mwakilishi kutoka kila Kanda, hii kusema kwamba Mwakilishi mmoja awakilishe wakulima sikubaliani nayo! Kwa sababu wawakilishi wa kila Kanda watasaidia, leo mkulima wa korosho kule Kanda ya Kusini hawezi kujua changamoto za mkulima wa tumbaku kule Tabora. Mkulima wa mahindi kule Mbeya hawezi kujua changamoto za mtu anayelima mwani labda yuko upande wa Pwani. Kwa hiyo, lazima kila Kanda itoe Mwakilishi wanapokaa kwenye Bodi kila mmoja aainishe changamoto za Kanda yake na mazao yanayozalishwa kwenye maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha saba (7) posho za Wajumbe. Huwezi kusema kama Wajumbe wapendekeze posho, Waziri aende aidhinishe hapana! Wanajipendekezea posho kwa nini? Lazima kuwepo chombo kinachopendekeza posho, leo Mjumbe wa Bodi hawezi kujipendekezea posho mwenyewe, lazima kuwepo na chombo kinachopendekeza washauriane na Waziri wakubaliane tusitoe loophole. Wanaweza wakasema kila mmoja milioni mbili kwa siku siyo wao wenyewe? Tusiwape loophole hiyo tunataka fedha nyingi ziende kwenye kazi husika siyo kwenda kulipana posho kwenye vikao mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha 10(4) pia napendekeza kwenye Baraza la Taasisi lazima kuwepo Wajumbe kutoka kila Kanda tofauti na wanavyosema hapa ni Mjumbe mmoja wa kuwakilisha Wakulima kwa maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha 22 kusajili miradi utafiti wa kilimo na utoaji wa huduma. Kifungu hiki ndicho kitakachosaidia sasa kuweza kupata watoaji wa huduma ya kilimo wenye uelewa na weledi. Leo tumekuwa na watu wanaosambaza mbegu za kilimo, wanasambaza mbolea ni business oriented, ni wafanyabiashara, hajasoma kilimo, hajui kilimo, hajui msimu, hajui ni madhara namna gani unavyochelewesha mbolea unaathiri nini, unapeleka mbolea muda ambao siyo unaathiri nini. Unapeleka mbegu muda umepita, unaathiri nini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kupitia Muswada huu na kifungu hiki, lazima tuainishe sasa watu wenye uwezo wenye weledi, wenye elimu kuweza kutoa huduma za mazao, huduma za kusambaza mbegu, mbolea, hata kwenye manunuzi, mtu ambaye anaona hiyo ni fani yake, tofauti na sasa hivi ambapo mara nyingi tumekuwa tukiwatumia watu ambao ni wafanyabishara, hawanufaishi wakulima, tunaishia kupata hasara, mwisho wa yote wakulima wetu wanakuja kuwa ni maskini wa kutupa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha 26 ningependa sana kuhusiana na namna gani, tuna vituo vingine kwa mfano pale Sokoine University, kuna taasisi ya TOSCI inayoshughulika kuhakikisha kwamba mbegu zinakuwepo za kutosha na ubora wa mbegu, sijaona imeguswa kabisa humu, namna gani sheria hii inashirikisha taasisi nyingine tofauti na vyuo kuweza kufanyakazi kwa pamoja?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima waone ni namna gani wanafanya kazi kwa pamoja kwa sababu kama mmesema sasa ni kama umbrella, taasisi nyingine zote lazima zishirikishwe na wataalam wale washirikishwe kuhakikisha kwamba mwisho wa siku tunaweza kuwa na tija nzuri kwenye sheria hii ambayo imekuja mbele yetu leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha 29(7)(a) kwa idhini ya kimaandishi ya Waziri anaweza kutumia fedha bila kujali kwamba matumizi hayo hayapo kwenye bajeti yoyote. Naomba kifungu hiki kiondolewe, tumekuwa tunasema hatuna nidhamu ya matumizi ya fedha, fedha tunaipeleka kwenda kwenye shughuli fulani, inatoka inaenda sehemu fulani, haiendi kwenye lengo, leo tunaweka sheria kwamba kwa maandishi ya Waziri anaweza kuagiza Bodi itumie fedha tofauti na bajeti iliyokuwepo. Lazima tuwe na nidhamu ya matumizi ya fedha, hapa tunaweka mwanya tunaweka upenyo namna gani Bodi itumie fedha za miradi bila kuwa na utaratibu wowote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kifungu hiki kiondoke kwa sababu hakitatusaidia, kwanza tutaleta matatizo, fedha zitaenda kutumika sehemu ambapo haikupangwa kwenda kutumika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, tumeambiwa kwamba pale mtu anaomba usajili akinyimwa aende kwa Waziri na Waziri awe ni namba ya mwisho. Hapa naomba Waziri asiwe namba ya mwisho. Inawezekana ikatokea figisu au utaratibu fulani wakamnyima tu huyu mtu kwa makusudi, akienda kwa Waziri na yeye asimsikilize. Kwanza ni muda mrefu wanasema siku 21 anaomba, Waziri ndani ya siku 30 hapo tayari miezi miwili imekwisha mtu anaomba usajili, siku 30 anasubiri majibu, miezi miwili imekwisha kwanza ni muda mrefu, lakini pia Waziri asiwe ni namba ya mwisho. Waziri ni binadamu. Naomba kiwepo chombo kingine.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hongera Waziri na timu yako yote ya Wizara kwa kuandaa hotuba hii na kuiwasilisha hapa Bungeni. Tunaipongeza Serikali kwa hatua za kuanza kuimarisha reli yetu hapa nchini pamoja na ile ya kati kwa kujengwa kwa viwango vya standard gauge ili kuhakikisha mizigo mizito inasafirishwa kwenye reli na kuokoa barabara zetu zinazoharibika sana. Tunashukuru Serikali kwa kutenga fedha za kumalizia kipande cha barabara ya Nyahua - Chaya kilomita 85.4 kwa mwaka huu ili kuunganisha Mkoa wa Dodoma na Tabora kwa maendeleo ya wananchi wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Urambo - Kaliua pamoja na fedha kupatikana tangu mwaka jana 2016 na Bodi ya Zabuni kukaa na kutangaza na Wakandarasi kuomba, mpaka leo haijaanza. Serikali ieleze ni kwa nini kipande hiki cha kilomita 32 ujenzi wake haujaanza mpaka sasa na ni lini hasa utaanza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Kaliua – Kazilambwa, kilomita 56 inayojengwa na CHICO ilitakiwa kukabidhiwa mapema mwaka 2017 kwa maagizo ya Waziri Mheshimiwa Profesa Mbarawa, aliyoitoa alipotembelea mradi huu mwaka jana 2016, mpaka leo ni Mei, 2017 bado haujakamilika pamoja na kuwa kazi inaendelea. Serikali itoe agizo kwa Kampuni ya CHICO kukamilisha ujenzi huu ndani ya muda uliopangwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ile Kazilambwa - Ilunde kilomita 48 ni mbaya sana sana na kipande hiki kinaunganisha Mkoa wa Tabora na Mkoa wa Kigoma. Mpango wa Serikali Kuiunganisha mikoa yote kwa barabara za lami. Pia barabara hii ni muhimu sana kwa uchumi na kusafirisha mazao. Ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa lami?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna barabara ya kuunganisha Mkoa wa Katavi na Tabora, barabara ya Mpanda - Kaliua - Ulyankulu kwenda Kahama. Hii ni barabara muhimu sana kwa kusafirisha mazao na biashara kwa mikoa hii mitatu. Mwaka jana Waziri alilieleza Bunge kuwa inafanyiwa upembuzi yakinifu. Serikali ieleze mchakato wake umefikia wapi na ni lini itaanza kujengwa kwa lami?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na uwepo wa reli katika Wilaya ya Kaliua wananchi wengi wa Kaliua wanakosa fursa ya kusafiri kwa treni kwa sababu ya kukosa tiketi na nafasi chache zinazotolewa kwa siku treni inapopita. Nafasi zinazotolewa ni kumi na tano tu kwa kituo na treni za express haisimami pale Kaliua na wananchi wengi wanakosa tiketi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mabehewa yanayopita Kaliua kwenda Kigoma na Mpanda ni machache sana na hayakidhi mahitaji ya wananchi, pia tiketi zinalanguliwa kwa bei kubwa sana, madalali wanakata tiketi kwa bei ya Serikali wanauza kwa bei ya kuruka na wananchi hawana namna wananunua. Mheshimiwa Waziri aliahidi kuongeza mabehewa mpaka leo bado tabu na adha inaendelea. Serikali ieleze mkakati wa kuongeza mabehewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wastaafu wa Shirika la Reli walioachishwa kazi wakati wa EAC mpaka leo hawajalipwa haki zao, Serikali ilete taarifa kamili za wazee kwa wananchi haki zao mpaka wamechoka na wengine wamekufa bila kupata haki zao. Hii kwa nini hawalipwi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano eneo kubwa la Wilaya ya Kaliua na hususani Jimbo langu hakuna kabisa mawasiliano ya redio, wananchi wanaishi bila kujua nini kinachoendelea ndani ya nchi yao pia hakuna minara ya simu. Kata zifuatazo mawasiliano ya redio ni magumu sana mpaka radio zifungwe kwenye miti juu sana:-

Kata ya Igwisi, Kijiji cha Mpanda Mlohoka na Igwisi Center; Kata ya Usimba karibu vijiji vyote havishiki redio; Kata ya Ushokola, Kijiji cha Makubi na Mwamashimba; Kata ya Zugimlole Kijiji cha Igombe na Luyombe; Kata ya Ukumbisiganga, Kijiji cha Usimba na Ukumbi Kakonko; Kata ya Usinge, Kijiji cha Kombe; Kata ya Usonye; Vijiji vya Luganjo mtoni, Shela na Maboha. Kata ya Ugunga Vijiji vya Mkuyuni, Mpilipili na Limbula.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji vyote hivi mawasiliano ya simu ni ya tabu sana kwani minara iko mbali na eneo lao pia mawasiliano ya redio ni kwa tabu sana na kwingine hakuna kabisa. Naomba Serikali ieleze ni lini wananchi hawa watapelekewa huduma hii muhimu.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mikakati gani kuanzisha Mfuko wa Wazee utakaowezesha wazee wasiokuwa kwenye ajira rasmi kujiajiri kwenye shughuli za uzalishaji mali? Wapo wazee wenye nguvu na uwezo wa kuunda vikundi kwa ajili ya uzalishaji na shughuli za ujasiriamali tatizo kubwa hawana mtaji. Umri wa ujana unaishia miaka 45, wazee kuanzia miaka 46 kuendelea ambao hawana pensheni wanaishi kwa tabu sana vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imetenga baadhi ya shule za msingi kwenye Halmashauri ya Wilaya na Miji kwa ajili ya kusajili watoto wenye mahitaji maalumu (walemavu). Nini mkakati wa Serikali kuwezesha miundombinu ya shule hizi kuwa rafiki kwa ajili ya watoto hawa walemavu wa aina mbalimbali? Nini mpango wa Serikali kupeleka walimu wenye ujuzi na taaluma ya kufundisha watoto hawa wenye mahitaji maalum ili waweze kunufaika na elimu kama wanafunzi wengine?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la vijana kutokuwa na ajira linaendelea kila siku na kila mwaka vijana wanamaliza vyuo vikuu, vyuo vya kati katika fani mbalimbali. Ni vijana wachache sana wanapata ajira Serikalini na kwenye sekta binafsi. Nini mkakati wa Serikali kuwezesha vijana wengi kujiajiri kwa kuwapatia mitaji na vifaa/mashine za kufanyia kazi za ujasiriamali kwenye viwanda vidogo vidogo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kilimo ni sekta inayoajiri watu wengi ni maeneo yapi na wapi yametengwa katika Mikoa mbalimbali ili kuwezesha vijana kujishughulisha na uzalishaji mashambani?
Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuchangia kwenye Wizara hii ambayo iko mbele yetu. Kwa sababu ya muda niende haraka; pamoja na juhudi ambazo zinafanywa na Serikali na kwenye Hotuba ya Mheshimiwa Waziri tumeiona ametusomea tumeona mengi yaliyofanyika, lakini kiukweli bado tatizo la afya katika nchi yetu halijafikia katika standard ambayo tunaweza tukajisifia, hakuna.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba katika nchi yetu maeneo mengi sana wataalam, watumishi wa afya, maeneo yote kuanzia hospitali kwenda kwenye zahanati, vituo vya afya, bado ni wachache sana. Kwenye maeneo yetu, mfano tu ukienda Wilaya ya Kaliua vituo vya afya, kwanza tunavyo vichache, viko viwili tu, lakini kuna wahudumu watatu mpaka wanne; hebu niambie kwa eneo ambalo lina watu karibu laki tatu, wanahudumiwaje? Vile vile zahanati zina Mganga mmoja au Nesi mmoja akiugua mmoja wapo au wote wakiugua, zahanati imefungwa na watu hawapati huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, akinamama wajawazito wanakaa zahanati kuanzia saa kumi na mbili asubuhi mpaka jioni hospitali imefungwa, hakuna huduma. Kwa hiyo namwomba Mheshimiwa Waziri pamoja na juhudi zote lakini lazima kuhakikisha kuna watumishi wa kutosha kwenye maeneo yetu ya vituo vya afya, zahanati pamoja na hospitali zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vituo vingi vya afya kwanza havina Madaktari, lakini pia havina vifaa tiba vya kupimia malaria na magonjwa mengine. Leo Kaliua mtu akiwa na malaria, mpaka aende Urambo, vituo vya afya havina hata vipimo vya kupima magonjwa madogo tu mpaka aende Wilaya ya Urambo. Kwa hiyo naomba, kwa kuwa lengo ni kupunguza vifo vya Watanzania vituo vya afya vyote viwe na vipimo vile vya kawaida kama vile vya kupima malaria na BP viwepo; vinginevyo hatuwezi kupigana na suala la vifo vinavyotokea ambavyo ni vingi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine, Wilaya ya Kaliua hatuna Hospitali. Kwa nguvu za wananchi na fedha za ndani tumeanza kujenga jengo la OPD, lile ni jengo la ghorofa moja na lina vyumba vyote vya muhimu, tumejibana kwelikweli kwenye mapato ya ndani. Naiomba Serikali, sasa hivi tupo kwenye hatua za mwisho, tumeshapaua, bado kupiga rangi, kuweka milango na vitu vingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hebu Serikali iweke mkono wake pale, itusaidie pale tulipofikia tuweze kuhakikisha kwamba tunakuwa na Hospitali ya Wilaya. Kutoka Kaliua kwenda Urambo ni zaidi ya kilomita 35, lakini pale hakuna huduma ya operesheni hakuna chochote kinachofanyika. Mtu ambaye hali yake ni mbaya na barabara hakuna kutoka Kaliua mpaka Urambo, wengi wanajifungulia njiani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunaomba Mheshimiwa Waziri atusaidie, hospitali ile ambayo tumeshaanza OPD iongezewe fedha za kutosha ili iweze angalau ndani ya muda mfupi tuweze kuhakikisha kwamba ndani ya Wilaya yetu ya Kaliua tunakuwa na Hospitali ya Wilaya tuweze kuokoa maisha ya akinamama na watoto ambayo yanapotea kila kukicha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la kuwepo na vituo vichache. Sera inasema na ni Sera ambayo tunatamani itekelezwe; kwamba kila Kijiji kiwe na zahanati, lakini mbona mpango huo hauzungumziwi? Kila kata iwe na kituo cha afya, mbona mpango huo hauzungumziwi? Leo tunasema tunaokoa akinamama wajawazito na watoto, tunawaokoaje wakati unakuta vijiji kati ya 100 labda zahanati ziko tano au kumi? Leo Kaliua ina vijiji 101, zahanati hazizidi 20. Si kila kitu wananchi wanaweza kukifanya; ni kweli wanafanya na tunawahamasisha wanafanya, lakini ni ngumu kwa wananchi kujenga kuanzia mwanzo mpaka mwisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunawaomba ile Sera ya Serikali itekelezwe ili tuweze kuwa na zahanati kila kijiji, tukaweza kuwa na kituo cha afya kila kata. Naomba Mheshimiwa Waziri atusaidie, mwaka jana tumepata mwongozo kwenye vikao vyetu vya Halmashauri, Mheshimiwa Waziri alituma barua kwamba kila kata mbili ziandae maeneo kwa ajili ya kujenga vituo vya afya, tumeshaandaa yale maeneo, tukashauriana kila kata mbili zikaandaa eneo la kujenga Hospitali. Hebu atuambie, ni lini ujenzi au maandalizi ya kuanza kujenga vituo vya afya utaanza?

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: …Kwa sababu maeneo yametengwa yako pale na yako kwenye Wizara.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nampongeza Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote kwa kuandaa hotuba hii na kuleta hapa Bungeni.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kazi nzuri ya kupunguza ajali za barabarani hapa nchini bado ajali za pikipiki zinatishia uwepo wa vijana na nguvukazi ya Taifa. Kwa takwimu zilizopo kwa miaka 10 tu, watu waliopoteza maisha kwa bodaboda ni 8,000, bado majeruhi, walemavu, yatima, wajane, wagane na jamii inayozunguka. Lazima Serikali kuja na mkakati mahsusi wa kupunguza/ kuondoa ajali za bodaboda zaidi ya mafunzo na elimu wanayotoa.

Mheshimiwa Spika, fedha inayotengwa kwenye vituo vya polisi kwenye wilaya zetu kuendesha shughuli za kila siku ni ndogo sana na kusababisha polisi kufanya kazi katika mazingira magumu sana. Polisi wanapewa lita tano za mafuta kwa siku kwa patrol kwenye eneo kubwa kama Kaliua haiwezi kukidhi kabisa kazi zao kwa siku – matokeo yake matukio ya uhalifu yanatokea pembezoni, taarifa zinafika kituoni kwa muda lakini askari hawawezi kwenda kufuatilia kwa sababu hawana mafuta. Polisi wanaomba mafuta kwa watu binafsi au kwenye ofisi za halmashauri, wakipata waende, wakikosa wakae kimya. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha mafuta yapo?

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Zimamoto kwenye wilaya nyingi hawana ofisi wala magari ya zimamoto, hawapo kabisa. Matukio ya moto yanatokea mara kwa mara nyumba zinateketea bila msaada wowote. Nini mpango wa Serikali kuhakikisha wilaya zote zina ofisi za zimamoto na magari ya zimamoto yapo?

Mheshimiwa Spika, Wilayani Kaliua Jeshi la Magereza limechukua eneo la kujenga gereza la ekari 12 katika Kata ya Ushokora, Kijiji cha Pozamoyo kwa miaka sita sasa hakuna chochote pale kilichofanyika, hata watu waliohamishwa kwenye maeneo yao na kuacha mashamba yao hawajui hatma yao. Serikali ina mpango gani kuhusu eneo hili lililotengwa tangu 2012? Wananchi waliohamishwa maeneo yao nini hatma yao mpaka leo hawajui/ hawana pa kuishi, lini watalipwa fidia za maeneo yao?

Mheshimiwa Spika, spidi ya utoaji wa vitambulisho vya uraia inakwenda taratibu sana na gharama za utekelezaji wa mradi huu zinaongezeka kila mwaka kwa namna ambayo muda unakuwa mrefu. Kwa kuwa mradi huu ulitengewa fedha nyingi tangu mwaka 2012 kwa sababu ya umuhimu wake na kuhakikisha Watanzania wanapata vitambulisho vya uraia. Serikali ieleze Bunge time limit/ time frame ya zoezi hili muhimu kwa usalama na haki za raia wote wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, Tanzania ni nchi pekee ambayo mipaka yake mingi iko wazi na watu wa nje wanaingia kinyemela na wengi wanaishi humu ndani kama raia bila vyeti vya uraia. Wengine wamegombea nafasi za uongozi ndani ya nchi na wanaongoza watu leo. Vitambulisho vya uraia ndiyo mwarobaini wa tatizo hili, kila Mtanzania apate kitambulisho cha uraia.
Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mkoa wa Tabora watumishi wa sekta ya afya ni wachache kwenye maeneo yote na hili ni tatizo la muda mrefu, wanaopoteza maisha kwa kukosa huduma ni wengi. Vituo vya afya vina wahudumu watatu mpaka wanne tu na wanafanya kazi usiku na mchana. Zahanati nyingi zina nurse mmoja na mganga mmoja tu. Ikitokea akapata dharura hakuna huduma na maeneo mengine wanatoa huduma wasio na taaluma za afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itoe kipaumbele kwa Mkoa wa Tabora kupelekewa watumishi wa afya kwani uhaba huo, hata takwimu za kitaifa zinaonyesha miaka zaidi ya minne iliyopita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kaliua hakuna Hospitali ya Wilaya; tumeanza kujenga OPD kwa kutumia fedha za ndani na nguvu za wananchi. Tumejenga jengo la ghorofa moja kubwa lenye vyumba muhimu vyote na sasa tuko kwenye hatua za mwisho. Serikali iko tayari kutoa fedha kusaidia kuongeza nguvu kwenye jengo hili ili likamilike na Hospitali ya Wilaya ianze?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Kaliua lenye kata 13 lina vituo vya afya viwili tu. Serikali mwaka wa jana ilileta barua Wilayani ya kutaka kila kata mbili ziandae maeneo ya kujenga vituo vya afya, maeneo hayo yameshaandaliwa. Ni lini ujenzi wa vituo hivyo utaanza maana bajeti hii Waziri hajasoma lolote kuhusu mpango huo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la bima ya afya limehamasishwa na wananchi wengi wamejiunga, tatizo kubwa ni pale wanapokwenda hospitali, vituo vya afya, zahanati wanakosa dawa. Kwa nini Mfuko wa Bima ya Afya hauboreshwi sambamba na uwepo wa dawa zakutosha?

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la sekta ya afya kutaka kuwa watoto under five years, wajawazito na wazee zaidi ya miaka 60 kupata huduma bure halijatekelezwa katika maeneo mengi sana. Wazee wakienda vituoni bila pesa hawapati huduma. Pamoja na Waziri/Serikali kutoa kauli hapa Bungeni mara ngapi mbona bado ni tatizo? Leo Mheshimiwa Waziri atoe kauli ambayo itatekelezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado wanawake wengi na watoto wanapoteza maisha kwa kukosa huduma ya mama na mtoto. Kuwepo kwa zahanati chache, vituo vichache na kukosekana kwa mobile clinic ni chanzo cha kupoteza wanawake wengi na watoto bila hatia. Wilaya yangu ya Kaliua hakuna kabisa mobile clinic na hakuna gari la kupeleka chanjo kwenye maeneo ambayo hakuna vituo. Serikali inaokoaje maisha ya akina mama wa Kaliua kwa kupeleka gari moja tu katika Wilaya ya Kaliua na kwa kuzingatia kwamba jiografia ya eneo la Kaliua ni kubwa na mapori mengi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lipo tatizo kubwa sana kwa wananchi kununua dawa zinazotembezwa barabarani na makampuni mbalimbali na kutibu magonjwa bila kufanyiwa vipimo wala kujua vipimo sahihi na mbaya zaidi wanakuwa hawana ujuzi wowote ni kama njugu. Je, Serikali inaliona tatizo hili? Bahati mbaya kuna nyingine ni za kunywa/kumeza. Kwa nini Serikali inaruhusu biashara huria ya dawa kwenye mabasi, vilabuni, njiani na barabarani? Afya ya wananchi inalindwaje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hizi Hospitali za Mission kama vile KCMC ambazo Serikali inawekeza nguvu ili wananchi wapate huduma kama hospitali ya Serikali, je, sera ya afya kwa makundi yale muhimu kupata huduma bora inatekelezwa kwenye hospitali hizi? Wapo watoto waliopewa rufaa kwenda KCMC kupata matibabu walipofika kule wakaambiwa KCMC si hospitali ya Serikali hivyo huduma zote ni kulipia. Serikali itoe ufafanuzi kwa hospitali zote za aina hiyo.
Azimio la Bunge la Kumpongeza Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Job Yustino Ndugai kwa Uamuzi wake wa Kulifanya Bunge Kutekeleza kwa Vitendo Dhana na Bunge Mtandao (e-Parliament)
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Nami pia naungana na Waheshimiwa Wabunge kumpongeza Mheshimiwa Spika pamoja na Sekretarieti ya Bunge ikiongozwa na Katibu wa Bunge kufanikisha utumiaji wa e-Parliament ndani ya Bunge letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nikiwa kama Kamishna wa Bunge pamoja na wewe na wengine kwa muda mrefu sana tumekuwa tunashauri namna gani ya kuweza kuhakikisha kwamba Bunge letu linakuwa la kisasa, linaendeshwa kwa e-Parliament kama Mabunge mengine. Ukiangalia almost Mabunge yote ya nchi za Afrika ni Bunge letu pekee lilikuwa limebaki bado tunatumia karatasi na hivyo kuwa na malundo ya makarasi kwenye madawati yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa hatua tuliyofikia tunashukuru sana na tunamshukuru pia Katibu wa Bunge maana alipewa order kabisa. Mheshimiwa Spika alifika mahali akatoa order kwamba ifikapo Bunge hili la mwezi Novemba kama Wabunge watakuwa hawajapata tablets kwa kweli hapataeleweka na aliweza kutumia muda huo mfupi kuhakikisha kwamba anafanikisha azma hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naungana na Wabunge kuwashukuru sana Sekretarieti na hasa watumishi wa Idara ya IT kwa kazi kubwa waliyoifanya kuwezesha Wabunge kutumia teknolojia hii mpya. Wametumia muda wao mwingi ndani na nje ya Bunge kutuelimisha ili kila Mbunge aweze kutumia kifaa hiki na kuhakikisha kwamba tunafuatilia shughuli za Bunge kwa ukamilifu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa hivi tablets hizi bado zinatumika ndani ya Bunge peke yake lakini kwa maelekezo ya Mheshimiwa Spika pia kifaa hiki kiweze kutumika vizuri Wabunge wote ku-access information kwenye tablet zao nje ya Bunge na hata majimboni mwetu. Kwa hiyo, ni matumaini ya Wabunge kwamba ifikapo mwakani kila Mbunge ataweza kutumia kifaa hiki akiwa ndani ya Bunge, nje ya Bunge na jimboni kwake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Naunga hoja mkono, ahsante. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, pongezi kwa Mheshimiwa Waziri, Naibu wake na watendaji wote kwa kazi na kuandaa hotuba hii.

Mheshimiwa Spika, nchi yetu na Serikali tumekuwa na kasumba ya kutokuwekeza kikamilifu fedha ya kutosha kwenye michezo na hilo suala la kuwezesha michezo mbalimbali kuachwa kwa wahisani, mashabiki na wapenda michezo.

Mheshimiwa Spika, tumekuwa tunashuhudia tunapeleka team kambini kwa maandalizi ya mashindano ya Kimataifa lakini wachezaji wanalalamika hata chakula wakiwa kambini hawapewi inavyostahili, hii ni aibu kwa Taifa huwezi kuvuna bila kupanda.

Mheshimiwa Spika, miaka ya nyuma michezo mashuleni ilipewa uzito na kipaumbele kwa maana tangu primary school tulijengewa misingi mizuri ya kuifahamu vizuri mchezo, lakini pia kusaidia wanafunzi kwa sasa shule nyingi hasa shule za umma hakuna jitihada zozote za kuendeleza michezo na hakuna walimu wa michezo.

Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha tunajenga vipaji vya watoto bado mapema, Serikali ieleze Bunge mikakati ya kuhakikisha kwenye mashule yote kuna Walimu wa michezo wenye ujuzi wa michezo. Serikali ieleze mikakati ya kupeleka vifaa vya michezo kwenye shule za umma ili watoto wapate fursa ya kushiriki michezo na kujenga afya na akili zao.

Mheshimiwa Spika, viwanja vingi vilivyotengwa kwa michezo maeneo mbalimbali vimevamiwa na kujengewa makazi na Serikali inalijua hili, Serikali ieleze Bunge viwanja vyote vya michezo nchini vinalindwaje, visivamiwe lakini pia ni mikakati gani ya Serikali kurejesha viwanja vilivyovamiwa.

Mheshimiwa Spika, tumekuwa tunashuhudia watoto wakitumika kwenye michezo ya maigizo na hivyo kuwapotezea ndoto zao lakini pia kuwajengea taswira hasi kwa michezo inayotisha. Serikali itoe maelezo ya kutosheleza ni kwa nini watoto wanatumika kwenye maigizo?

Mheshimiwa Spika, katika Taifa letu maeneo mengi ya pembezoni mwa nchi, usikivu wa redio ni hafifu sana na maeneo mengine hakuna kabisa, mawasiliano ya redio. Je, kuna mpango gani wa Serikali kuhakikisha mawasiliano ya redio yanafika pande zote za Taifa hili ili kila Mtanzania apate haki ya kusikia na kujua yanayojiri ndani ya nchi yake.

Mheshimiwa Spika, katika Jimbo langu la Kaliua yapo maeneo ya Kata nyingi ambayo usikivu ni hafifu sana na pengine hakuna kabisa. Kata hizo ni Kata ya Igwisi-Kijiji cha Igwisi, Kijiji cha Mpanda mlohoka; Kata ya Usimba-Vijiji vya Usimba; Kata ya Ushokola-Kijiji cha Ukikubi; Kata ya Zugimlole- Vijiji vya Igombe na Luyombe; Kata ya Ukumbi Siganga-Vijiji vya Usinga na Ukumbi kakonko; Kata ya Usingi, Kijiji cha Kombo na Luganjo; Kata ya Usonye, Vijiji vya Luganjo, Mtoni, Shela na Maboha; na Kata ya Uganga-Vijiji vya Mkuyuni, mpilipili na limbula. Serikali ieleze kuna mipango gani mahsusi kuhakikisha mawasiliano na usikivu katika maeneo haya unapatikana.

Mheshimiwa Spika, miaka ya nyuma mchakato wa kumpata Miss Tanzania ulikuwa unavutia na waliochaguliwa walituwakilisha vizuri Kimataifa. Kwa kuwa kwa sasa suala hili limepoteza mvuto na kuendeshwa kwa rushwa kubwa na udhalilishaji. Serikali ifute uwepo wa zoezi hili kwa heshima ya Taifa.
Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari za Mwaka 2016
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha 20 (2) kabla ya Mwandishi wa Habari kuondolewa au kukoma kuwa Mwanahabari kwa kosa lolote atakuwa amekiuka sheria hii, ni lazima kuwepo chombo huru kitakachothibitisha pasipo shaka kuhusu adhabu hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha 20(3) Mwanahabari aliyepatikana na kosa apewe fursa ya kukata rufaa pia apate fursa ya kujitetea kwenye chombo hicho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha 14(1) maneno kwa idhini ya Waziri yaondoke na badala yake yawekwe maneno kwa kushauriana na Waziri wa Habari. Ni vizuri sana na muhimu Bodi ya chombo hiki ikawa huru bila kuingiliwa majukumu yake, wala kuamuliwa nini cha kufanya ili iweze kutekeleza majukumu yake kikamilifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria ianishe wazi kwenye Bodi uwiano wa wajumbe wanawake na wajumbe wanaume ili mawazo yanayowagusa wanawake yapate nafasi kwenye Vyombo vya Habari na kwenye jamii kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha 7(2) ni vizuri habari zinazoandikwa zisihatarishe usalama wa nchi. Swali muhimu hapa ni chombo gani kinachothibitisha kwamba, habari iliyoandikwa inahatarisha usalama? Isije kutokea mtu mmoja tu akaibuka na hoja itakayokandamiza uhuru wa habari. Hivyo, ni vizuri sheria iainishe wazi chombo kinachothibitisha habari na kiwe huru.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia kwenye hotuba iliyoko mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na Wizara kufanya kazi kubwa Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri na Watendaji wake, kwa sababu ya muda nijielekeze tu kwenye eneo la Wilaya ya Kaliua na changamoto zinazotokana na hifadhi kwa sababu Kaliua imezungukwa na hifadhi maeneo yote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napata mashaka, naendelezea alipomalizia Mwenyekiti wa Kamati yetu. Napata mashaka kama Serikali ina dhamira ya dhati kuondoa migogoro ya wananchi ndani ya Tanzania, napata mashaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napata mashaka kwa sababu huu ni mwaka wangu wa 12 kuwepo ndani ya Bunge hili, tumeunda Kamati nyingi sana na Kamati ya mwisho ambayo nilijua itaondoa migogoro ya wafugaji na wakulima; ya hifadhi na wananchi ni Tume Teule ya Bunge ambayo mimi nilikuwa Mjumbe wake, ilikuwa ina Maazimio tisa muhimu sana, nilijua kuanzia pale tunaondoa kabisa migogoro ya wananchi Tanzania. Bahati mbaya hakuna kinachofanywa, ukiangalia yale Maazimio tisa ya Tume Teule ya Bunge hakuna hata moja ambalo limefanyiwa kazi mpaka sasa hivi.

Leo tumeunda tena Kamati nyingine. Tume ambayo inahusisha Wizara nne na wataalam, jambo la kusikitisha wakati Wabunge tunasubiri tupate majibu namna gani ya kuondoa migogoro hii, tupate ushauri wa ile Kamati, huku wananchi wetu wanateswa, wanapigwa, wananyanyaswa, wananyang’anywa mifugo yao. Nataka Mheshimiwa Waziri atwambie leo, kulikuwa na umuhimu gani wa kutengeneza ile Kamati ambayo ilitumia fedha za walipa kodi wakati majibu hatutajapata ya uhakika? Naomba nipewe majibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili; Serikali hii ndiyo imesajili vijiji ndani ya hifadhi, Wilaya ya Kaliuwa ina vijiji 21 ndani ya hifadhi. Wamekwenda kwenye vile vijiji watu wa maliasili wamekwenda kunyang’anya certificate za usajili wa vijiji. Naomba Mheshimiwa Waziri aniambie vile vyeti vya vijiji walivyong’anywa, watu wake wamekuja kuchukua ndani ya vijiji vyetu, viko wapi? Kwa nini hawarudishiwi? Kwa sababu Serikali ni moja, unless niambiwe leo kwamba ndani ya Tanzania kuna Serikali mbili. Serikali inayosajili vijiji na inayokuja kunyang’anya certificate! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba leo Mheshimiwa Waziri unipe majibu vile vyeti virudi kwenye vijiji, vimesajiliwa viko kwenye GN ya Serikali na vitongoji vyake. Naomba vyeti vyao virudi, msijidanganye kuwanyang’anya ili muendelee kuwaadhibu, hatukubali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimezungumza hapa Bungeni wiki iliyopita, bahati mbaya sana hata Mheshimiwa Waziri nimezungumza naye siyo mara moja siyo mara mbili, jamani mimi kwanza ni Mhifadhi by professional, lakini uhifadhi wa kutesa watu, kuumiza watoto, kulala kwenye mvua, kuchomewa vyakula, kuchomewa nyumba, hii siyo Tanzania tunayoiamini Tanzania ya amani, siyo kabisa. Wale siyo wakimbizi, kwa nini wakimbizi ndani ya Taifa hili wanaishi vizuri? Kama mlikosea Serikali ikaenda likizo, wakakaa ndani ya hifadhi mkawasajili, watoeni kwa utaratibu, kwa nini mnawatesa watu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri nimeongea na wewe mara nyingi suala hili, bahati mbaya sana huchukui hatua zinazotakiwa. Leo Mkuu wa Wilaya anakuwa na power ya kuruhusu watu wakanyanyaswe, nimeongea na wewe hufanyi kazi. Hujafuatilia suala hili hata kidogo! Naongea na watu wa Kanda wanasema hatujui, ukiongea na mtu wa Kaliua anasema hatujui, naongea na Waziri anasema napiga simu kule. Mheshimiwa Waziri wale watu mtuambie mliowasajili ndani ya hifadhi kule Kaliua ni Watanzania au? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtuambie leo, nataka majibu hapa leo, Mheshimiwa Waziri tutagawana mshahara wako leo hapa, hatuwezi kukubali watu waendelee kuteseka kila siku. Bahati mbaya sana ukiuangalia mjadala wa maliasili kila mwaka, almost nusu unajadili migogoro. Nafikiri mngejidhatiti mkaiondoa migogoro wakati wa bajeti tukawa tunajadili namna gani ya kukusaidia Mheshimiwa Waziri kuendeleza utalii, kuendeleza uhifadhi…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri na watendaji wote wa Wizara hii kwa kuandaa hotuba hii na kuileta hapa Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumelalamika sana hapa Bungeni juu ya mateso na maumivu yanayosababishwa na utendaji mbovu wa baadhi ya watendaji wako na hasa Game Rangers. Wilaya ya Kaliua na Jimbo la Kaliua imezungukwa na hifadhi, zaidi ya vijiji 30 vimesajiliwa kisheria, Serikali imepeleka huduma muhimu kama shule, zahanati na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Serikali imeunda Tume kuangalia namna ya kutatua tatizo sugu la migogoro ya ardhi na hifadhi, Askari wa Wanyamapori na Misitu wamewachomea nyumba, vyakula, mazao wananchi wa Kagome, Lumbe, Usinga, Luhembe - Iga na kuwaacha hawana chochote. Watu wa misitu kuweka beacon za mipaka kati ya wananchi na hifadhi kwenye maeneo hayo hadi kwenye nyumba za wananchi bila kuwashirikisha kwa lolote. Wanaingia, wanawapiga, wanawatupia vitu nje, wanaweka alama (beacon), wanakamata mifugo ya wananchi na kupiga mnada, wanakuja na wanunuzi wanawaacha wananchi maskini hana hata ndama wala mbuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanapora vitu vya wananchi na kwenda kuuza ikiwepo simu, solar panel, pikipiki, baiskeli, kuku, majembe ya kulimia kwa ng’ombe. Askari wa Wanyamapori wanakwenda kijiji cha Shela, kata ya Usenye, wanachukua mifugo katikati ya kijiji na kuwaswaga kupeleka hifadhini na kuwapiga faini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo cha wanyamapori kilichopo eneo la Kagome, Lumbe, kata ya Zugimlolo, askari (Games) walioko pale wote ni wezi, wanawafilisi wananchi. Mheshimiwa Waziri aeleze Bunge hawa Games wanapewa kazi ya kulinda wanyamapori au kupora mali za wananchi na kupiga minada mifugo ya wananchi, kuuza majembe, solar panel za wananchi, simu na kadhalika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji vilivyosajiliwa ndani ya hifadhi vilipewa vyeti vya usajili wa vijiji vyao. Maafisa Wanyamapori walivichukua vyeti hivyo kutoka vijijini tangu mwaka 2014 na mpaka leo hawajavirudisha. Waziri aeleze vyeti hivyo viko wapi na lini vitarudishwa kwenye vijiji hivyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ieleze kwa nini inasuasua kurekebisha gharama za concession fee za hoteli zilizopo ndani ya hifadhi zetu ziendane na hali halisi ya sasa. Ni lini hasa fee hizo zitafanyiwa marekebisho?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Sheria ya Uanzishwaji wa Hifadhi ya Ngorongoro imepitwa na wakati na inahitaji maboresho ili kuendana na hali ya sasa. Ni lini italetwa hapa Bungeni turekebishe? Hifadhi ya Ngorongoro imekuwa inawahudumia wananchi wanaoishi ndani ya hifadhi kwa chakula, elimu, afya na kadhalika, Serikali itaweza kufanya hilo jukumu kwa muda wote? Kwani watu wanaongezeka na huduma inaongezeka mwisho jukumu la hifadhi litapungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, misitu mingi ya asili imeteketea kwa sababu ya ukataji wa miti kwa kuchoma mkaa. Wanaokata mkaa hawapandi miti hata mmoja, pamoja na kuwa malundo ya magunia na mikaa imejaa barabarani na viongozi wanaona, hakuna juhudi za kuwaelimisha wapande miti na kuwaelimisha kuhusu mkaa endelevu. Ni mikakati gani ya Serikali inafanya kupunguza matumizi ya mkaa na kuokoa misitu yetu?
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Waziri na wataalam wote wa Wizara hii kwa juhudi kubwa wanayoifanya ya kuleta mabadiliko kwenye Wizara hii muhimu na kuinua ubora wa elimu hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilieleza Bunge kuwa wataboresha shule za umma kuanzia miundombinu, vitendea kazi, walimu na kadhalika ili ziweze kutoa elimu bora na kurejesha heshima ya shule za sekondari. Kwa muda wa mwaka unaoishia Juni, 2017 ni shule ngapi zimeboreshwa na jukumu hilo limefikia wapi kwa jumla?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilianzisha vikao na wadau wa shule binafsi ili kuweka standards za ada za shule za private ambazo ni kubwa mno na kila shule inatoa ada kwa utaratibu wake na hakuna control yoyote. Zipo shule zinatoza ada shilingi milioni tatu kwa mwanafunzi kwa mwaka bado kuna bus fee na michango mingine. Serikali ituletee hapa Bungeni taarifa ya vile vikao vimefikia wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna tatizo kubwa sana la upungufu wa miundombinu kwenye shule za msingi na sekondari. Watoto wanasoma zaidi ya 100 kwenye darasa moja, lakini wapo wanaosoma kwa shift, wanaingia saa 2.30 asubuhi wanatoka saa 6.30 mchana na wengine saa 7.00 mchana mpaka saa 10.00 jioni. Watoto hawapati muda wa kutosha kupata masomo na vipindi vya michezo, dini na mazoezi. Hakuna nyumba za walimu, wengi wanakaa kwenye nyumba za udongo huko mitaani, wengine wanakaa walimu watatu mpaka wanne kwenye nyumba moja hata ule uhuru wa kibinadamu hakuna. Walimu wanakatishwa tamaa na mazingira wanayofanyia kazi na yale wanayofundishia. Serikali itueleze mpango wa muda mrefu kuhakikisha walimu wanafundisha kwa moyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iboreshe na kuimarisha Ofisi za Ukaguzi wa shule za msingi na shule za sekondari kwa kuwapa magari ya ukaguzi kila Wilaya kwa ajili ya Mkaguzi wa Shule ya Msingi na gari lingine kwa shule za sekondari; Halmashauri za Wilaya iweke mafuta kwenye magari hayo ili muda wote wawe field na motisha uwepo kwa walimu wote hasa wale walio kwenye mazingira magumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeweka sheria ya kurejesha mikopo kwa elimu ya juu na kuweka asilimia 15 kila mwezi. Japokuwa ni sheria, lakini hii sheria inaumiza sana walimu ambao mishahara yao ni midogo. Ni vema waangalie utaratibu wa kuwasaidia walimu walipe kwa asilimia 7 kwa muda mrefu, lakini waweze pia kumudu maisha yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, madai ya walimu ni vilio na ni kero ya muda mrefu. Natumaini uhakiki umeisha na wenye vyeti fake wametambuliwa. Kuna walimu wa Kaliua waliajiriwa mwaka 2014 hawakulipwa mishahara kwa mwezi Mei na Juni, 2014 (miezi miwili) huku wamo waliolipwa mishahara yao. Pia malimbikizo ya madai yasiyokuwa ya mishahara ni mengi sana hayajalipwa kwa miaka zaidi ya saba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na kuwepo kwa mkanganyiko wa ubora wa vitabu vitakavyotumiwa na wanafunzi hasa primary school na zile za mchepuo wa kiingereza na uwepo upungufu mkubwa kwenye vitabu hivi vya shule za awali ambapo ndipo eneo watoto wanapata msingi wa elimu yao, Serikali itueleze mikakati iliyopo ya kuhakikisha vitabu vyote vinavyotumika mashuleni vimefanyiwa uhakiki na kuondoa changamoto iliyojitokeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatuambia nini kuhusu uwepo wa Mamlaka ya Udhibiti wa Vitabu (TEA) lakini wameshindwa kufanya kazi ya udhibiti wa elimu yetu hasa shule za msingi. Nashauri kuwepo na taasisi binafsi zinazotengeneza vitabu vya shule na visisambazwe mashuleni kabla ya kupitiwa na kuhakikiwa na mamlaka za Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la adhabu kwa watoto wa shule ni jambo jema kwa lengo la kumrekebisha mtoto na kumweka kwenye njia nzuri. Serikali inajua kuwa walimu wanatoa adhabu kubwa sana kupita kiasi? Watoto wanavuliwa nguo zote mpaka za ndani, wanachapwa mpaka wanalazwa na wengine wanapoteza maisha. Serikali itoe tamko leo Bungeni la kupiga marufuku adhabu za aina hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Chuo Kikuu cha Sokoine ni chuo pekee cha kilimo hapa nchini kinachotoa elimu ya juu kwa masuala ya kilimo, ufugaji wa kisasa, nutrition, misitu, mazingira, tafiti mbalimbali na fani nyingine. Serikali kwa miaka mingi haijabadilisha miundombinu ya chuo hiki pamoja na kwamba kila mwaka udahili unaongezeka na wanafunzi ni wengi. Nini mpango wa Serikali kuboresha chuo hiki tunapoelekea kwenye uchumi wa viwanda ambapo tutafika huko kwa njia ya kilimo?
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana kunipa nafasi ili niweze kuchangia hotuba iliyoko mbele yetu. Niungane na Waheshimiwa Wabunge wote na Watanzania kuwapa pole wazazi wa watoto wetu ambao wametutoka kule Arusha, Mwenyezi Mungu awape faraja na awapumzishe watoto wetu kwa amani.

Mheshimiwa Naibu Spika, natamani sana akinamama tungeungana leo, ukiwepo na wewe Mheshimiwa Naibu Spika, kwa dakika moja angalau tuangue kilio kwenye Bunge hili kwa niaba ya akinamama wa Taifa hili wanaoteseka na kuhangaika kwa adha ya maji kwenye nchi nzima.

(Hapa baadhi ya Waheshimiwa Wabunge walitoa sauti ya kilio kwa niaba ya akinamama wanaohangaika kwa adha ya maji)

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania shida ya maji ni kubwa kupita maelezo. Ukiangalia hivi vitabu vya maji kwa miaka karibu mitatu, minne iliyopita unakuta mambo mengi yanayojirudia ni yale yale.

Kiukweli ni jambo la ajabu, Watanzania wanaongezeka kwa milioni moja kwa mwaka. Wakati watu wanaongezeka, mahitaji ya maji yanaongezeka, bajeti ya maji inashuka; haingii akilini kabisa. Kwa mwaka mmoja tunaongezeka watu milioni moja Tanzania na Mheshimiwa Waziri kasema, yaani hata ule uwezo wa ongezeko la watu, tofauti na namna ya kuweza kumudu gharama za huduma kwa wao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini mahitaji yanaongezeka wakati huo bajeti inapungua? Wale wanaoongezeka hawahitaji kunywa maji? Hakuna kitu muhimu kwa Mtanzania na mwananchi yeyote wa Tanzania na binadamu yeyote kama maji. Kwa hiyo, tunaomba sana suala la bajeti ya maji iongezwe, hakuna discussion, liongezwe kwa sababu watoto wa Tanzania wengi hawaendi shule kwa sababu ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, akinamama wanaamka saa 10.00 ya usiku kufuata maji visimani, wengine wanabakwa. Huwa tunasema, hatufichi, wanabakwa usiku wakifuata maji kwenye visima; watoto wanachelewa shule hawapati elimu wanayostahili. Suala la maji lazima Serikali ije na mkakati maalum wa namna ya kuhakikisha akinamama wa Tanzania wanapata maji ya uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji wa Malagarasi. Nimewahi kusema Bungeni hapa mara nyingi, karibu miaka mitano sasa. Ardhi ya Kaliua na ardhi ya Mkoa wa Tabora haiwezi kuchimbwa maji kwenye ardhi yakapatikana, ndiyo maana kwa Kaliua nzima na hata Urambo hatukunufaika na mradi wa World Bank kwa sababu, visima vingi vilivyochimbwa havikutoa maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haijasema njia pekee ya kutupatia maji Kaliua, Urambo na Nguruka ni kutupatia maji ya Malagarasi. Tangu miaka mitatu iliyopita, kuanzia 2014 tunaambiwa utafiti unafanyika, leo tunaambwa kwamba mpango unafanyika ili kumpata mshauri mwelekezi haweze kufanya environmental impact assessment, wakati huo akinamama Kaliua hawana namna.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa nategemea angalau wangetuambia mwaka huu tumetenga angalau kuanza zile hatua za awali; lakini Mheshimiwa Waziri hata shilingi. Bahati nzuri hata nimeongea naye hata kabla ya bajeti hii; anasema wanategemea kutafuta fedha. Miradi inayotegemea sana fedha kutoka nje nyingi haitekelezeki. Kwa adha wanayopata akinamama wa Kauliua, Nguruka na Urambo ningetegemea Serikali itoe kipaumbele kwa fedha ya ndani ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kuwa Serikali imezindua miradi miwili ya Mkoa wa Tabora, Mradi wa Victoria na ule Mradi wa pale Mabama, Kaliua na Urambo hawamo, sisi hatumo kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa taarifa ripoti aliyoandikiwa Mheshimiwa Waziri, pengine ameandikiwa hakujua; kwamba mradi uliozinduliwa pale Mabama unalisha wilaya zote saba za Tabora si kweli, ni pale Uyui tu na ni baadhi ya vijiji, siyo vyote, lakini ripoti inasema Wilaya zote saba zitanufanika na mradi uliozinduliwa Mabama, kitu ambacho siyo kweli na kama ni kweli basi watuambie ndani ya Kaliua ni vijiji vingapi vimeingia kwenye mradi wa pale Mabama na pale Uyui?

Mheshimiwa Naibu Spika, inasikitisha, tutalia mpaka lini hapa Bungeni, ni kweli tulikuwa tunategemea mwaka huu uwe ni mwaka wa matumaini kidogo kwa wananchi wa Kaliua. Kweli naomba Mheshimiwa Waziri bajeti hii ikiisha twende na yeye Kaliua akawambie Wanakaliua wanapata maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mifumo ya Maji Taka na Safi. Ni kweli kwamba kwa maeneo ambayo yameunganishwa na maji taka mifumo yake imechakaa na mingine imeoza. Nikianzia hapa Dodoma, wananchi wanalipa gharama kwa ajili ya maji taka kila bili inapokuja lakini mabomba yamepasuka yanavuja ovyo na bahati mbaya sana wakiitwa kuja kurekebisha wanachukua zaidi ya miezi miwili, miezi mitatu, wananchi wana adha kubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua zile fedha zinazolipwa kwenye kila bili kwa ajili ya maji taka nilijua ni kurekebisha mifumo iliyooza, kuondoa mabomba yaliyochakaa kuweka mabomba mengine lakini mabomba ya miaka thelathini yako pale pale tunalipa gharama tunapata usumbufu kila siku ni gharama.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri atakapo-wind up atuambie kwamba lini mifumo ile ya maji chafu kwenye maeneo ambayo kumeunganishwa system ya maji chafu itaondolewa na kuwekwa mingine kwa sababu ile iliyopo imechoka imeoza na inaleta shida kwa wananchi karibu kila siku.

Mheshimiwa Naibu Spika, Upotevu wa Maji. Hotuba ya Mheshimiwa Waziri anasema upotevu sasa hivi ni asilimia 38 na hivyo imepungua. Upotevu wa maji ni mkubwa kweli kweli na kwa bahati mbaya bomba linaweza likapasuka katikati ya barabara Mawaziri wanapita pale, viongozi wanapita pale, inachukua almost miezi mitatu wakati maji yanatiririka, yanapotea Watanzania wengine wana-share maji na ng’ombe kwenye vijiji vya maeneo mbalimbali. Nikikutana na maji yanayomwagika mahali huwa naumia sana; kwa sababu nawaangalia wananchi wangu wanavyotesa nikikuta maji yanamwagika huko barabarani roho inauma sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo bado Serikali lazima inatakiwa iweke mifumo. Standard inayotakiwa kitaifa upotevu wa maji ni asilimia 14, kwa hiyo sisi asilimia 38 bado ni kubwa sana. Maji mengi tunayagharamia lakini yanapotea barabarani wakati huo huo kilio cha maji kinaongezeka kila kukicha; kitu ambacho ni hasara kwa Serikali na ni maumivu kwa Watanzania ambao hawana maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Gharama za Kuunganisha Maji. Gharama hizi zinazidi kuongezeka kila siku na zinakuwa kubwa kiasi kwamba mwananchi wa kawaida; kwa mfano hapa Dodoma gharama za kuunganisha zimezidi kuongezeka. Mwanzo utaratibu ilikuwa Mwananchi ananunua vifaa anakwenda kulipa gharama kule DUWASA anakuja kufungiwa maji.Leo unaambiwa ukalipe moja kwa moja kila kitu kule. Nimejaribu kwenda mimi mwenyewe, unajaribu kuangalia gharama ulizoandikiwa milioni moja na ushee wananchi wangapi wa hali ya chini wanaweza kuvuta maji? Ni wachache.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile ukiangalia vile vifaa bei ya madukani na bei ambayo umeandikiwa pale ni tofauti. Kwa hiyo, naomba suala la maji si biashara, maji ni huduma. Kila Mtanzania apate maji. Kwa hiyo tatizo la kuweka gharama kubwa wananchi wengi wanashindwa kugharamia ni maumivu kwa Watanzania lakini pia tunafanya huduma ya maji kuwa ni biashara na si huduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la mwisho, Madawa ya Kutibu Maji. Tumekuwa tukilalamika hapa Bungeni miaka mingi gharama za madawa ya kutibu maji inakuwa ni kubwa kiasi kwamba kuna maeneo mengine kuna wakati inafika maji yatoka machafu, yanatoka yananuka, yanatoka yana udongo kwa sababu halmashauri na miji zinashindwa kumudu gharama, matokeo wanaweka dawa kidogo wananchi wanakunywa maji machafu. Kwa hiyo naiomba Serikali, kwa kutambua umuhimu waweze kupunguza gharama za kutibu maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, ahsante.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi hii adimu sana. Naungana na Waheshimiwa Wabunge kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu wake na Watendaji wote wa Wizara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siri kubwa ya mafanikio ya Wizara hii, wanasikiliza tatizo, wanakwenda site, wanalishughulikia na wanaweka mifumo ya kuhakikisha kwamba tatizo halijirudii. Hongera sana Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri spirit aliyotumia ya kuweza kutatua migogoro maeneo mbalimbali, aje Kaliua akishirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii atatue migogoro ambayo inawasumbua wananchi wa Kaliua kwa muda mrefu na kuondokana na mateso na maumivu wanayopata wananchi wa Kaliua kwa sababu ya migogoro ya ardhi ya kati ya wananchi na hifadhi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni la upimaji wa ardhi. Speed ya kupima ardhi bado ni ndogo, asilimia 25 ni ndogo sana. Tunatamani kwamba mwananchi anapohitaji ardhi aweze kupewa kiwanja ambacho tayari kimepimwa. Kwa hiyo, naomba sana kwenye Mfuko wa Kupima Ardhi lazima kuhakikisha kwamba kuna fedha ya kutosha. Iwepo fedha ya kutosha na vifaa vya kupima ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Ardhi imeweka kipengele kwamba Waziri atatenga eneo la mifugo; eneo litapimwa, litakuwa gazetted na pia litalindwa. Kwa hiyo, naomba wakati wa kupima ardhi kwenye maeneo mbalimbali, Mheshimiwa Waziri ahakikishe anatenga maeneo ya mifugo na pia maeneo yawe gazetted na yaweze kulindwa. Ndiyo inayosababisha migogoro mikubwa sana ndani ya nchi yetu kutokana na migogoro ya ardhi kwa wakulima na wafugaji na hifadhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine naomba ahadi ya National Housing; pamoja na kazi nzuri wanayoifanya, wafike Kaliua. Ni Wilaya ambayo ni mpya, lakini inakwenda speed sana kwa maendeleo, waje wawekeze ndani ya Wilaya ya Kaliua, kujenga nyumba nzuri nasi tuweze kuwa wa kisasa kama ambavyo Wilaya nyingine wameweza kujengewa nyumba na National Housing.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, hawa watu wa Mfuko wa Kujenga Nyumba za Watumishi (Utumishi Housing), usambae uende maeneo mengi, ufike mpaka Kaliua. Watumishi wetu hawana nyumba, wamepanga nyumba ndogo ndogo za vijijini huko. Tunaomba na wenyewe waje Kaliua wapanuke katika maeneo mengi; sasa hivi wame- concentrate kwenye maeneo machache sana. Mfuko uongezwe ili watumishi wetu wa maeneo mengi waweze kupata nyumba za watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine. Migogoro mikubwa ya ardhi inasababishwa na uelewa mdogo pia wa Wenyeviti wa Vijiji na Watendaji wa Vijiji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Mheshimiwa Waziri atoe elimu kwa Viongozi wa Vijiji. Viongozi wa Vijiji wanatoa maeneo makubwa sana. Sheria inaruhusu ukomo wa kutoa eneo la kijiji, lakini wanatoa mpaka hekta 1,000 au 2,000 na wanapokea rushwa, wanaleta watu bila hata wananchi kujua. Kwa hiyo, naomba itumike busara viongozi wapewe semina na mafunzo waweze kutumia Sheria ya Ardhi kugawa maeneo ndani ya vijiji vyao ili kuondokana na migogoro inayosababishwa na kugawa ardhi bila kufuata Sheria ya Ardhi.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Waziri Mkuu, Mawaziri na Naibu Mawaziri walioko Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kuandaa hotuba hii na kuiwasilisha Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu; ongezeko kubwa la wanafunzi mashuleni haliendi sambamba na kuongezeka kwa miundombinu ya madarasa, ofisi za Walimu, matundu ya vyoo na kadhaili. Serikali iweke mkakati maalum wa ujenzi wa madarasa ili watoto wote wakae madarasani katika shule za primary na secondary.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kauli ya Serikali kwamba elimu ni bure na hivyo hakuna michango inayoruhusiwa mashuleni inapokelewa kwa uelewa tofauti na wazazi na hata vyakula mashuleni Serikali inatoa. Serikali itoe ufafanuzi kuhusu kauli yake kwa kuwa kwa sasa wanafunzi wengi hawapati vyakula mashuleni kwa sababu wazazi au walezi hawataki kuchangia vyakula kwa watoto wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtoto mwenye njaa hafundishiki, hali hii inatishia uelewa wa wanafunzi na hivyo kushusha elimu. Walimu wengi kutopandishwa madaraja kwa wakati katika mashule ya primary na secondary katika Wilaya ya Kaliua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ni nchi ya pili Afrika kwa kuwa na mifugo mingi, lakini pato/mchango wa sekta ya mifugo katika pato la Taifa bado ni mdogo sana. Sheria ya nchi inaelekeza maeneo ya malisho ya mifugo kutengwa, kulindwa na kutangazwa kwenye magazeti ya Serikali. Viwanda vya kuchakata mazao ya mifugo (processing plants) ili kutoa masoko ya uhakika kwa wafugaji. Maafisa ugani (mifugo) wenye weledi na vitendea kazi ili watembelee wafugaji mashambani na watoe elimu. Kuwepo na mashamba darasa ya mifugo katika wilaya zote na kata zinazofuga ili wafugaji wafuge kisasa kwa ubora na si kwa wingi usiokuwa na tija.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunamwomba Mheshimiwa Waziri Mkuu awaagize Wizara ya Maliasili na Utalii kurejesha vyeti vya vijiji 26 katika Wilaya ya Kaliua ambavyo vilisajiliwa Kisheria ndani ya hifadhi za misitu na baadaye Afisa wa Maliasili walifika kwenye vijiji hivyo na kupora vyeti vya usajili wa vijiji hivyo vyote. Suala hili linaathiri sana wananchi wa vijiji hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka huu 2018 kampuni za ununuzi wa tumbaku kama vile JTI, TLTC na Alliance one wametoa maelekezo kwa vyama vya msingi kwenye vijiji hivyo 26 kwamba hawatawapa makisio ya ununuzi wa tumbaku yao (mikataba) kwa vijiji ambavyo hawana vyeti vya usajili kwa sababu hawawezi kutekeleza mpango shirikishi wa utunzaji wa misitu (CBFM). Hili litaumiza uchumi wa Wilaya ya Kaliua na wakulima wa tumbaku wa Kaliua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakurugenzi wa Wilaya walipewa waraka na Serikali kwa kuwatoa kazini Watendaji wa Vijiji na Kata walioajiriwa tangu mwaka 2004 wenye elimu ya darasa la saba. Ni vyema Serikali ikaliangalia agizo hili kwa jicho tofauti ili kuondoa matatizo yanayoendelea kutokea ikiwa ni pamoja na Serikali kupelekwa Mahakamani na kupoteza fedha nyingi na muda mwingi kwa kushughulika na kesi wakati tuna mambo ya msingi ya kuyashughulikia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ya Kaliua wanaondolewa walioajiriwa tangu miaka ya 2001. Watendaji hawa wana barua za ajira walibaki kuthibitishwa, walipelekwa mafunzo kwenye Chuo cha Hombolo na maeneo mengine, pamoja na kupewa semina mbalimbali. Watendaji hawa hawatendewi haki, wengine ni wazee lakini pia wana familia zimeathirika sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kaliua na Jimbo la Kaliua tumepanga kuongeza vituo vya afya viwili katika Kata ya Usinge na Kata ya Ukumbi Siganga katika bajeti ya mwaka 2018/2019. Wananchi wanaendelea kuchangia ujenzi huo na pia Mheshimiwa Rais alipofika Kaliua alichangia shilingi milioni kumi ku-support Kituo cha Afya cha Usinge. Tunaiomba Serikali itenge fedha ku-support nguvu za wananchi katika ujenzi wa vituo vya afya viwili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la maji katika Wilaya ya Kaliua halijapatiwa ufumbuzi na hakuna mikakati ya muda mfupi kwa Serikali kuwapatia Wanakaliua maji safi na salama. Mradi wa maji mkubwa wa kutoa maji katika Mto Malagarasi ni wa muda mrefu, leo ni mwaka wa nne tangu uanze lakini bado uko kwenye hatua ya upembuzi na usanifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba mwaka huu 2018/2019 Serikali ilete mpango mkakati wa muda mfupi wa kuwatua wanawake wa Kaliua ndoo kichwani, watoto wa kike wapate muda wa kuhudhuria masomo shuleni na si kusaka maji kwenye madimbwi.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara kwa kazi nzuri ya kuandaa hotuba hii na kuiwasilisha vizuri Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuelekea kwenye uchumi wa viwanda kwa hakika tunahitaji wanasayansi wengi zaidi Tanzania, tuna tatizo kubwa sana la upungufu wa walimu wa sayansi katika shule zote. Wanafunzi wanaochukua mchepuo wa sayansi wamekuwa wanakatishwa tamaa, pia wengi wamekuwa wanafanya vibaya kwenye mitihani ya mwisho. Tumejenga maabara hakuna walimu wa kufundisha practicals na theories pia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kaliua karibu shule zote za sekondari za kata zina mwalimu mmoja tu na nyingine hakuna kabisa. Naomba Serikali isaidie upatikanaji wa mabweni ya wanafunzi katika shule ya Kiliua High School ambayo ndiyo shule pekee ya high school kwa Kaliua. Inawachukua wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali, lakini hakuna mabweni ya kutosha. Baadhi ya wanafunzi wanatumia madarasa kama mabweni kwa sababu ya shida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lipo tatizo kubwa sana la kukosekana kwa nyumba za walimu hasa kwa shule za vijijini. Walimu wengi wanapangwa kufanya kazi, wanapokuta hakuna nyumba na mazingira magumu ya kufundishia wanaondoka kwenye vituo walipopangwa na wengine wanaacha kazi. Tunaomba Serikali ilete mpango maalum kuhakikisha miundombinu mashuleni inaboreshwa hasa nyumba za walimu, vyoo na maktaba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miundombinu ya vyuo vikuu vya umma ina hali mbaya, udahili wa wanafunzi unaongezeka kila mwaka lakini miundombinu yake haiboreshwi ikiwepo library, madarasa, maabara na kadhalika. Matokeo yake wanachuo wanasimama madarasani huku wakifundishwa pengine wanafanya shift ku-share lectures room.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iweke kipaumbele kwa Chuo Kikuu cha SUA, Morogoro, chuo pekee Tanzania kinachotoa elimu ya juu kwa masuala ya kilimo na mifugo. Asilimia 75 ya Watanzania wote ni wakulima, wafugaji, tunakwenda kwenye uchumi wa viwanda, kilimo lazima kipewe kipaumbele. Waziri Profesa Ndalichako naomba utupe mkakati maalum kwa chuo hiki ili wanafunzi wanaotoka pale walete impact kubwa kwa wakulima na wafugaji Tanzania nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ubora wa elimu wa vyuo wa elimu ya juu; TCU ina jukumu la kuhakikisha vyuo vikuu hapa nchini vinakidhi vigezo vya udahili wa wanafunzi kutoa ithibati, kuhakikisha ubora wa elimu na kuidhinisha programu zinazofundishwa vyuoni. Katika kutekeleza majukumu TCU imekuwa inachelewa ufuatiliaji wa vyuo vya private na matokeo yake wanashtuka baadae ambapo wanafunzi/wanavyuo wameshadahiliwa, wameanza masomo na hata wamefanya mitihani ya mwisho. TCU inachukua hatua too late wakati wanafunzi wameshalipa ada wanafunzi wamefanya mitihani ya mwisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepata taarifa ya TCU kugundua madhaifu makubwa katika Chuo cha Mount Meru wanafunzi kupewa vyeti wakati walifeli, walimu zaidi ya asilimia 75 kuacha kazi kwa kutolipwa mishahara kwa miezi zaidi ya sita. TCU imeagiza wanafunzi wale warudi chuoni ndani ya miezi mitatu wafanye mitihani upya, hapa wazazi watalipa fedha nyingine. Hili ni tatizo kubwa, tunaomba maelezo ya kutosha wakati chuo hiki kinaendesha mitihani mpaka kutoa vyeti walikuwa wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kila Wilaya kuna chuo cha VETA; vyuo vya VETA vipatiwe vitendea kazi vyote muhimu na walimu wenye ujuzi wa kutosha kusaidia kufundisha watoto wetu wapate stadi na ujuzi wa kuendesha maisha yao na kuendeleza Taifa. Fedha inayotolewa na waajiri kwa ajili ya kukuza vipaji na kutoa mafunzo ya vitendo, Skill Development Levy (SDL) itolewe iende VETA ifanye kazi iliyokusudiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na juhudi za Serikali kuongeza fedha za malipo ya vyuo vikuu na kufikia idadi ya wanafunzi 122,623 bado wanafunzi wanaopata mikopo ni michache na wanaohitaji ni wengi zaidi. Serikali iongeze zaidi fedha ya mikopo kwa wanafunzi ili kila mtoto wa Kitanzania aweze kupata elimu ya juu.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nakushukuru sana kwa nafasi uliyonipa niweze kuchangia kwenye bajeti muhimu sana ambayo iko mbele yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kilio cha maji kwa Watanzania ni kilio kikubwa sana na ukiangalia hata siku ambayo maswali ya maji yanazungumziwa humu ndani ya Bunge hili almost karibu robo ya Bunge wanasimama kwa ajili ya kuuliza masuala ya maji. Hii inaonesha ni jinsi gani Taifa kwa ujumla tuna shida kubwa ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, jaribu kuangalia jinsi taratibu za kutatua changamoto ya maji na hii kampeni ya kwenda kumtua mama maji kichwani sioni kama inaenda sambamba na fedha zinazotolewa. Ukiangalia kwa kweli kwa asilimia 54 inayotengwa, tutenge shilingi bilioni karibu 623, tutoe shilingi bilioni 349 kwa speed hii kampeni itafanikiwa lini? Hili ni tatizo. Lazima Serikali iamue kwa uhakika kwamba tunataka sasa kuondoa tatizo la maji nchini, kama tulivyopanga kwa masuala ya umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo tunazungumzia habari ya vijiji karibu zaidi ya asilimia 80 zinaenda kupata umeme, hivyo hivyo kwenye maji lakini speed ni ndogo leo na kila siku tunalia hapa Bungeni ni shida.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa speed tunayoenda nayo kama hatuna mkakati maalum kuja na Wakala kama walivyosema Waheshimiwa Wabunge wenzangu na naunga mkono Wabunge waliozungumza suala la wakala. Hatuwezi kuondokana na kero ya maji na akina mama wanateseka, hawaingii kwenye shughuli za maendeleo, hawaendi kulima hawaendi kwenye miradi yao midogo midogo, watoto wetu wa kike hawasomi kwa muda wanaenda kufata maji kisimani ndiyo waje waingie darasani, hatuwezi kuwatoa Watanzania mahali walipo kwa speed hii tunayoenda nayo ni ndogo sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni suala la umwagiliaji. Serikali tumekuwa na malengo, almost karibu miaka mitano sasa kuweza kuwa na heka milioni moja kwa ajili ya umwagiliaji. Lakini nenda kwenye vitabu, leo mmeona vitabu vyote hapa karibu vinne vya miaka minne mfululizo angalia inayotengwa yaani kwa mwaka mmoja tuna hekta 6.7, 7.2 ni aibu, kwa nchi ambayo inategemea kilimo kwa hatua kubwa. Tunakwenda kwenye uchumi wa viwanda, tunafahamu tunataka kwenda kwenye umwagiliaji kwa speed hii tunayoenda nayo itachukua muda wa miaka karibu, nilikuwa nafanya mahesabu ya haraka hapa, kwa speed tunayoenda nayo, ukiangalia 2016 hekta za umwagiliaji tunaenda 7000.02; mwaka 2017 ni hekta 6,712 kwa hiyo ukiangalia trend hiyo ili tuweze kufika milioni moja hekta tunahitaji karibu miaka 50, hivi tutakuwepo?(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali lazima tuamue tunakwendaje kwenye uchumi wa viwanda wakati hatuwekezi vya kutosha kwenye umwagiliaji, bado ni tatizo kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni la upotevu wa maji, ukiangalia speed ya upotevu wa maji wakati tunalia hatuna maji, hata mijini watu hawana maji, vijijini watu hawana maji asilimia 33 ya maji yanapotea, hayatumiki na mengine tumeshaingia gharama za walipa kodi. Kwa hiyo, naiomba Serikali lazima ije na mpango maalum, waweke utaratibu maalum wa kuboresha miundombinu mingi imechoka, miaka 20, miaka 30, miaka 50 leo ukienda baadhi ya maeneo unakuta maji yanamwagika barabarani. Inaumiza wananchi wako wanapokuwa hawana maji unafika maeneo unakuta maji yanamwagika barabarani hayatumiki, ni tatizo kubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lazima Waziri aje na mkakati, awe na utaratibu maalum, regularly mpango wa kurekebisha mabomba yaliyochakaa kuhakikisha kwamba maji hayapotei yanayopatikana yakatumike kwa Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni suala la charge za maji. Kwenye gharama za maji tumeweka kitu kinaitwa service charge kama ilivyokuwepo kwenye umeme hizi Mheshimiwa Waziri hazimsaidii Mtanzania, zinamuumiza. Hizi service charge kwenye maji wakati tayari bili analipa bili nzima na kama analipa maji taka yapo, leo mnaweka tena na service charge tunaomba iondolewe kama ilivyoondolewa kwenye umeme ili kupunguza gharama za maji kwa Watanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni suala la maji kutoka Mwanza kuja Mkoa wa Tabora. Tulifurahi sana tukajua kwamba sasa Mkoa wa Tabora japokuwa haifiki Kaliua na Urambo angalau shida kubwa ya maji inaondoka. Lakini jaribu kuangalia kwa miaka mitano tumetekeleza kwa asilimia 17 ya utekelezaji wake, ili mradi huu ukamilike utahitaji karibu miaka mingapi, karibu miaka labda kumi. Hivi kweli kama ni mpango mkakati, kama ni mradi wa kimkakati kwa speed hii ya asilimia 15 ya utekelezaji, nasikitika sana kwa kweli hii pengine hatutakuwepo wakati huo.

Naiomba Serikali kwa kuwa huu ni mradi ambao unaenda kulisha karibu Wilaya tano za Mkoa wa Tabora na kilometa 12 pande zote ambazo bomba linapita iwekewe fedha ya kutosha ili speed yake iongezeke na itengewe muda maalum, tuambiwe sasa kwamba mradi huu utakamilika lini? Lakini kwa asilimia inayokwenda nayo bado ni ndogo sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niongelee Kaliua, mimi nasikitika na kiukweli natamani kupiga yowe hapa kwenye hili Bunge. Ninaongea kila siku habari ya Kaliua, nimesoma hiki kitabu page by page, line by line Kaliua huku haimo, Mheshimiwa Waziri huoni hata huruma, Kaliua haimo, hivi Kaliua hawaishi watu? Mradi pekee ambao umetoka Kaliua ambao hauonekani wanasema kwamba Mradi wa Maji Kaliua, kata mbili, Kaliua na Ushokora mradi unaotekelezwa na Mkoa. Fedha haionekani, kuptoka wapi haionekani, wala ni lini haijulikani.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tulikuwa na mradi Waziri mwaka jana alisema kutoa maji Malagarasi kuleta Kaliua na Urambo, ukiangalia imetengewa shilingi milioni 500 na nimeongea na Waziri akasema siyo mradi wa leo wala kesho. Sasa mpango wa kupatia maji wananchi wa Kaliua uko wapi? Leo kama unazungumzia habari ya kata mbili za Kaliua na Ushokora. Kaliua ina Kata 28, ina vijiji 101, ina vitongoji karibu 460, leo unazungumzia habari ya kata mbili na hakuna mradi mwingine wowote hatuko kokote, kwenye visima hatumo, kwenye mabwawa hatumo, kwenye miradi ya quickwins hatumo, kwenye miradi ya mkakati hatumo, miradi mikubwa hatumo, hivi Kaliua wanaishi watu wa aina gani?(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri ukija unijibu kwa nini kwenye kitabu hiki Kaliua umewasahau, kuna baadhi ya Wilaya nimeangalia huku mpaka inauma. Wilaya ina miradi yote kwenye visima wamo, kwenye mabwawa wamo kila mahali wamo.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka jana walikuja mradi wa kuchimba visima pamoja na mabwawa, wakaainisha maeneo ya kimkakati kuweka mabwawa saba, nimeshangaa huku hamna hata bwawa moja, hii kwa kweli muone aibu Serikali. Naomba Mheshimiwa Waziri uniambie kwa habari ya Kaliua kama wanawake wa Kaliua wataendelea kuteseka na maji miaka mingapi nijue, hata kama mimi siyo Mbunge lakini wana Kaliua wana haki ya kupata maji, wanalipa kodi kama Watanzania wengine, akina mama wale wanataka wafanye shughuli za maendeleo, lakini kwa speed hii mimi nakataa kwamba Kaliua haijatendewa haki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana Mheshimiwa Waziri na nikuombe bajeti ikiisha twenda Kaliua ukaone mateso wanayopata wale watu, kwa kweli ni maumivu makubwa sana, yaani hata bwawa jamani ni kweli kwamba ardhi yetu haina maji chini na hata visima vya Mradi wa World Bank hatukunufaika navyo kabisa kwa sababu hatuna maji chini. Hata kutuwekea mabwawa ili mvua zinaponyesha tukusanye tuyatumie, inasikitisha, inaumiza sana, sijui nitumie lugha gani!(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilijua kwa kilio changu miaka yote inakwenda kwa Waziri tungeangaliwa angalau mwaka huu lakini inasikitisha sana, kwa kweli inaumiza sana. Mradi wa Malagarasi haujulikani, Mheshimiwa Waziri ukija hapa Bungeni na mimi nang’ang’ania shilingi yako mpaka nijue wannchi wa Kaliua wanapatiwaje maji, karekebishe bajeti, haujatutendea haki.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia kidogo kwa dadika hizi nilizopewa kwenye Wizara hii muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kusema kwamba kama kweli tunataka kwenda kwenye uchumi wa viwanda ambapo asilimia kubwa inategemea mazao ya kilimo, lazima Serikali kujidhatiti kikamilifu kwenye suala la kilimo. Ukiangalia dhamira tuliyonayo na ukiangalia tunakokwenda havioani! Hatuwezi kuwa tunaenda kwenye uchumi wa viwanda wakati huo huo kwenye kilimo tunawekeza kidogo, hatuwezi kwenda. Pia najiuliza swali pamoja na hicho kidogo tunachopa hiyo bajeti ndogo tu, Waziri umeweza kusimamia kipi kikaonekana kwa uhakika? Hicho kidogo tunachokipata, mimi naona tunalo tatizo la msingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwenye utafiti, hatuwezi kwenda kwenye kilimo cha tija kama hatuna utafiti. Tulisema kwenye Bunge hili na imetengwa kwamba tuhakikishe kwenye bajeti ya Serikali tunatenga asilimia moja kwenda kwenye utafiti, leo ni karibu miaka kumi haiendi! Lini Serikali itafikia hatua ya kutoa one percent ya bajeti iende kwenye utafiti, hatuwezi kwenda huko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna mazao mengi ndani ya nchi hii yana magonjwa sana kwa miaka zaidi ya 20 hayapatiwi ufumbuzi kwa sababu hatutoi fedha kwenda kwenye utafiti. Kuna mazao ya kilimo cha ndizi kule Bukoba hayaendi nje kwa sababa ya magonjwa hayaponi, tuna mazao ya mihogo, tuna machungwa yenye magonjwa, tuna maembe yenye magonjwa, tuna minazi hata vyuo vyetu vya utafiti hatuvipi uwezo viweze kutumia rasilimali zetu kwa ajili ya utafiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunazalisha, kama hatuna uwezo wa kusafirisha mazao hayo nje tunazalisha kwa ajili ya nini, ukiona maembe yetu wakati wa maembe yanaoza, yanadodoka chini, ukiangalia mengi yana wadudu, kwa nini kwa miaka 10/15 tushindwe kuja na solution ya magonjwa yanayosumbua mazao yetu hatuwekezi? Kwa hiyo, kwanza kabla hatujaamua kuingia kwenye utafiti hatuwezi kutoka, tutalima lakini bado hatutavuna vizuri kwa sababu nguvu zinatumika nyingi za wananchi lakini bado hatutoi kwa tija wala haturuhusiwi kusafirisha nje kwa sababu ya udhaifu wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni upatikanaji wa mbegu. Kwa miaka yote mpaka leo tunapozungumzia habari ya uchumi wa viwanda, bado tunazalisha mbegu ndani ya nchi kwa asilimia 20 peke yake, asilimia 80 tunatoa nje. Hii ni aibu kwa nchi ambayo asilimia 80 tunategemea kilimo ni aibu! Kwa hiyo, lazima Serikali ihakikishe kwamba inawekeza. Bahati mbaya hata mbegu hizi za nje bado siyo bora mimi mwenyewe nimejaribu mbegu za nje, lakini mbegu za ndani bado siyo nzuri watu tunaenda kwenye mbegu za nje sababu ndiyo zinazalisha vizuri. Kwa nini tunashindwa kujengea uwezo mamlaka zetu za ndani za mbegu zizalishe mbegu nzuri za kutosha na kwa bei nzuri, hili nalo ni tatizo kubwa sana.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Dkt. Charles Tizeba, Waziri wa Kilimo ukija hapa utuambie umefanya kazi gani kwa miaka ambayo umewekwa kwenye hiyo Wizara kuweze kumsaidia Mheshimiwa Rais kwenda anakotaka, uje utuambie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kilimo ni suala la mzunguko, kilimo ni mashambani, kilimo ni maghala, kilimo ni usafirishaji na kilimo ni masoko. Kama kwenye mashamba hatuwekezi vizuri, Waziri anazungumzia juu ya uagizaji wa mbolea kwa bulk na kwa urahisi. Nikuambie mbolea hizi haziji kwa wakati, hata bei zake hazieleweki wanasema kwamba ni bei elekezi siyo kweli. Wilaya ya Kaliua mwaka jana tumenunua mbolea mpaka shilingi 140,000 wakati bei elekezi ni shilingi 75,000, wengine shilingi 90,000, mahali pengine shilingi 100,000, shilingi 120,000, shilingi 140,000, bahati mbaya sana mbolea ya Serikali iliyokuja imekuja wakati tunavuna wakati ni mbolea ya kupandia, leo iko kwenye maghala haina kazi, kwa hiyo, liko tatizo la msingi Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu amekuwa anafanya kazi kubwa sana kuisaidia Wizara hii. Kiukweli inapofika mahali panaonekana kitu, Mheshimiwa Waziri anafanya kazi kubwa hata kurekebisha zile AMCOS pamoja na ushirika wetu. Najiuliza swali kama Waziri Mkuu asingekuja Tabora kutusaidai WETCO leo angalau ina mabadiliko tungekuwa wapi na kwa nini Waziri Mkuu atoke alipo aje mpaka Tabora akaangalie kuna shida gani wakati Waziri yupo? Pengine Waziri hatoshi hili ni tatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni muwazi lazima tuseme, Wizara hii inahitaji mtu ambaye ni very straight, very aggressive, mchapa kazi anayeweza kutusaidia tunakokwenda tuweze kufika, lakini kwa Waziri aliyepo naona kama tunalo tatizo ambalo inabidi Mheshimiwa Rais aliangalie kwa karibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakulima wa Mkoa wa Tabora tunalima tumbaku kwa kiasi kikubwa mwaka jana 2017 tumepa hasara ambayo haijawahi kutokea. Tumbaku yetu tani milioni tano imeuzwa kwa bei ya makinikia, bei ya makenikia kutoka bei elekezi dola mbili tumeuza dola 0.0... (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote kwa kuandaa hotuba na kuleta hapa Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, makampuni ya tumbaku Mkoa wa Tabora yanaendelea kupunguza makadirio/makisio ya tumbaku kila mwaka. Msimu wa mwaka 2017/2018 makisio yalishuka kutoka tani 13 hadi tani 10, na msimu huu wa mwaka 2018/2019 zipo dalili za makisio kushuka zaidi wakati wakulima wameshakopa benki, wakapata pembejeo na sasa wanakosa soko kwa kukosa makisio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali/Waziri inasaidiaje wakulima wa tumbaku inayoendelea kuvunwa wakati hawana uhakika wa soko?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeelezea juu ya kununua mbolea kwa pamoja na kusambaza kwa bei ya ruzuku. Pamoja na kuja na mfumo huu, bado tatizo la upatikanaji wa mbolea kwa wakati na kwa bei elekezi na ya kutosha ni tatizo kubwa sana. Serikali itueleze ni mfumo gani umewekwa kwenye Wilaya zetu wa kuhakikisha mbolea hii ya ruzuku inawafikia wakulima na kwa wakati kwa bei elekezi na ya kutosha?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2017/2018, tumbaku ya Kaliua zaidi ya tani milioni tano zimeuzwa kwa bei ya makinikia, USD 0.073 hadi 0.070 baada ya bei elekezi ya USD 2 hadi 2.5. Wakulima wengi wamebakiwa na madeni makubwa ya benki na taasisi za fedha. Wengi wao wameshindwa kuingia kwenye kilimo cha tumbaku na wana hali mbaya. Tunaiomba Serikali iwasaidie wakulima hawa ili waweze kunyanyuka tena na kuingia kwenye kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali mwaka jana iliruhusu chini ya tani wanunuzi wa mazao chini ya tani moja wasilipe kodi, hili limekuwa ni tatizo na pia kunyima mapato Halmashauri za Wilaya zinazotegemea kilimo na mazao kama chanzo cha mapato. Wanunuzi wanasafirisha gunia 10 mpaka 15 bila kulipa ushuru hivyo wanabeba kidogo kidogo ili wasilipe ushuru. Serikali mnasaidiaje Halmashauri za Wilaya kupata mapato kupitia ushuru wa mazao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kila Mkoa kuna mazao ya kimkakati ya biashara ambayo ndiyo yaliyosaidia kuinua uchumi wa mikoa hiyo. Mazao mengi yaliyotegemewa yamedorora na mengine hayalimwi kabisa kwa kukosa msukumo wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kahawa-Kilimanjaro, kokoa- Mbeya, minazi-Pwani, korosho-Kusini, ndizi-Bukoba, zabibu- Dodoma, tumbaku-Tabora, mawese-Kigoma na kadhalika. Serikali itupe maelezo ni mikakati gani ya uhakika kuhakikisha maeneo haya yanayotegemewa kuinua uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wapo kandarasi waliongia mkataba na Serikali kwa ajili ya kujenga ma-godown kwa ajili ya mazao, wengine hawajalipwa tangu mwaka 2016. Wapo waliojenga ma-godown saba tangu mwaka 2016 mpaka leo hawajalipwa na wanadai kwa miaka yote bila kulipwa. Pia mawakala wa kusambaza pembejeo za kilimo hawalipwi kwa wakati. Serikali ilieleze Bunge mpango wa kulipa madeni yote ya kandarasi waliokopwa miaka mingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna kilimo cha uhakika bila ushirika wenye nguvu. Serikali iweke utaratibu endelevu wa kukagua Vyama vya Ushirika (AMCOS) mara kwa mara ikiwezekana kila robo ya mwaka. Waziri apewe taarifa za ukaguzi wa ushirika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, mafunzo yatolewe kwa uongozi wa ushirika ili waongoze AMCOS/ushirika kwa ufanisi na uaminifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imejipangaje kuongeza uzalishaji wa mazao kwa kuhakikisha tunaongeza hekta za umwagiliaji kufikia hata hekta milioni moja kwa mwaka 2020? Tangu mwaka 2013 mpaka leo hata nusu hatujafika. Kilimo chetu kwa asilimia zaidi ya 80 tunategemea mvua. Kuna mabadiliko ya tabianchi, mvua hazieleweki. Serikali itueleze inajipangaje kwenye sekta ya umwagiliaji na kuwasaidia wakulima kuelekea uchumi wa viwanda?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu masoko, Serikali inahamasisha wananchi walime, wanaingia benki wanachukua mikopo, wanaweka nyumba zao bond, wakizalisha hakuna masoko. Ili kupata masoko ya uhakika, tunahitaji wataalam ambao watatembea duniani kuangalia fursa za masoko kwa mazao ya aina mbalimbali. Kuna mpango gani wa haraka kuhakikisha mazao ya mahindi, karanga pamoja na mbaazi ambayo yamekosa soko yanapata masoko.
Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Sasa hivi kwa taarifa za Mheshimiwa Waziri suala la utalii wa uwindaji umeanza kupungua. Hata ukiangalia kwenye taarifa ya Mheshimiwa Waziri mapato ya utalii yameanza kupungua, ukiangalia vitalu vingi vya utalii vimeanza kurudishwa na pia kuna mchakato unafanyika nchi za nje kuhakikisha kwamba wanazuia, kwa mfano sasa hivi kuna maeneo ambayo nyara za tembo zimezuiwa kuingia, nyara za simba zimezuiwa kuingia, kwa hiyo, lazima kujikita zaidi kwenye utalii wa picha ambao ndiyo utalii wenye faida kubwa na endelevu. Ndani ya Wami Mbiki kuna Mto Wami unapita pale katikati, una samaki wa kila aina lakini kuna uwanda wa aina mbalimbali, kuna eneo unakuta tembo peke yake, unakuta twiga peke yake, unakuta swala pala (impala) na vitu vya aina hiyo. Kwa hiyo, ningependa sana kwa location ya eneo lile WMA hii iwe chini ya TANAPA.

Mheshimiwa Spika, lakini pia tunasisitiza sana utalii wa ndani. Eneo la Wami Mbiki ni eneo ambalo mtu anaweza kutoka Dar es Salaam akafanya utalii, Mbunge anasafiri kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam ana-spend siku moja pale anakwenda Dar es Salaam, eneo lile kwa potentiality yake nashauri Serikali ilifanye liwe chini ya TANAPA liweze ku- utilize vizuri rasilimali ambazo ziko pale ndani ya WMA ya Wami Mbiki.

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni vitalu. Tulipitisha hapa sheria mwaka 2009, tulibadilisha Sheria ya Wanyamapori kwa sababu tasnia ya utalii wa uwindaji ilikuwa inamilikiwa na wageni kwa asilimia 100. Tukasema haiwezekani tasnia hii iwe ndani ya mikono ya wageni peke yao na ili Watanzania waingie tukarekebisha sharia. Tukaishauri Serikali Watanzania wenzetu wawezeshwe kimitaji ili waweze kuingia kwenye tasnia hii. Pia kuwepo na masharti nafuu kwa Watanzania ili waweze kuingia kwenye tasnia hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, yote haya hayakufanyika, hakuna mitaji waliyopewa na bahati mbaya kwenye utalii wa uwindaji kuna investment kubwa sana, uwekezaji wake ni mkubwa bila kuwezeshwa kimitaji hawawezi. Matokeo yake wamechukua vitalu, wameshindwa kuviendesha, vimerudi Serikalini.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naiomba Serikali bado tuna ulazima wa kuhakikisha kwamba Watanzania wanashiriki kwenye tasnia ya utalii. Nachoomba tuwawezeshe kimitaji na tuwape masharti nafuu. Bahati nzuri wale Watanzania wenzetu wakinufaika na utalii ule wanawekeza ndani ya nchi, wenzetu wale wa nje wanakwenda kuwekeza kwao. Kwa hiyo, suala la sekta ya utalii wa uwindaji tunaomba sana Serikali iingilie kati isaidie wazawa waweze kushiriki kikamilifu kwenye tasnia ya utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna Hifadhi ya Mikumi ambayo iko karibu sana hapa, barabara kubwa inayotoka Morogoro kwenda Kilosa na kwenda Kusini inapita pale, lakini wanyama wanauwawa sana kila mwaka. Kila siku tembo na twiga wanauawa, ukipita barabara ile utaona huruma. Ninachoshangaa tulipendekeza angalau kuwepo na geti mwanzoni na mwishoni mwa ile barabara, nasikia TANROADS wamekataa hakuna kuweka geti, watu wanapita pale wanatalii bure bila kulipa chochote. Hata shilingi 1,000 kwenye basi moja kwa siku, tungeweza kupata fedha za kuendelea kutunza eneo lile lakini Serikali imekataa.

Mheshimiwa Spika, lakini pia tulipendekeza barabara ile ichepuke ipite mbele ya hifadhi lakini bado imeshindikana. Sasa rasilimali zetu wenyewe Watanzania ni za kutusaidia sisi wenyewe iweje tuwe na hifadhi ile katikati yetu hapo hapo Mikumi tunashindwa kuiwekea mazingira ya kuingiza zaidi kiasi kwamba mpaka sasa hivi inategemea hifadhi nyingine kwa ajili ya kujiendesha.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali iangalie suala la barabara ile ambayo inaua sana, pale speed inatakiwa 50 wanapita kwa 120 au 140, matokeo yake wanaua wanyama hata wakilipishwa lakini bado wanaendelea kuua. Kwa hiyo, ili tuweze kunufaika na ile hifadhi, naiomba Serikali iweke utaratibu wa kuwa na geti mwanzoni na mwishoni. Mimi nimetembea mpaka nchi za nje, huwezi kupita katikati ya hifadhi bure, haiwezekani, ni hapa kwetu nashangaa. Hata ukienda Namibia barabara zote hata kama ni za udongo maadamu inapita katikati ya hifadhi lazima kuna tozo fulani inayotozwa ili hifadhi ile iendelee kulindwa.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nakushukuru sana kunipa nafasi niweze kuchangia kidogo kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri, hotuba ya Serikali ambayo iko mbele yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye vitabu vyote vya Mheshimiwa Waziri; kitabu cha hotuba hata kitabu cha hali ya uchumi wa Taifa, uchumi wa Tanzania umekua kwa asilimia 7.1 tofauti na mwaka 2017 ambapo ulikua kwa asilimia 7 mwaka 2016. Ukijaribu kuangalia hivi vitabu vinavyosema na ukienda kwenye actual ground kule chini kwenye maisha ya watu ni tofauti sana. Uchumi tunaosema kwamba umekua kwenye vitabu kule chini bado hauendani. Nami nakubaliana kabisa na hotuba ya Kamati kwamba tumeshindwa kuoanisha uchumi na hali ya wananchi kule chini, tumeshindwa kuoanisha kukua kwa uchumi kwa kufungamanisha na hali ya maisha ya Watanzania kule waliko chini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi tunavyoongea kilo ya dagaa Sh.10,000 tena wa Mwanza. Hivi tunavyoongea jana sato Sh.10,000 kilo moja hata hapa kantini tunakula haijalishi ni mdogo au mkubwa. Ukiondoa mazao ya nafaka, mazao mengine yote gharama ni juu. Kwa hiyo, kwa mwananchi wa kawaida ukimwambia uchumi umekua hakuelewi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tukienda pia kwenye vifaa vya ujenzi, cement wiki iliyopita ilikuwa Sh.14,500 leo asubuhi ni Sh.15,500. Sasa uchumi umekua umekuaje? Miezi miwili iliyopita nondo milimita 16 ilikuwa Sh.19,500 mpaka Sh.20,000 leo nenda duka la dawa vifaa vya ujenzi ni Sh.38,000 imepanda almost mara mbili. Nashindwa kuelewa, mimi siyo mchumi ni mtu wa maliasili na mazingira, Waziri atuambie uchumi ukikua unaupima wapi? Unaupima juu au kule kwa wananchi walioko kule chini? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali lazima tuhakikishe kukua kwa uchumi kunaendana na hali kule chini. Hivi tunavyoongea watu wanazidi kuuza mashamba na viwanja vyao, mabenki yanatangaza kila siku kapiga minada nyumba za watu, watu wameacha kukaa kwenye nyumba zao walizokuwa wamejenga wameziuza wameenda kupanga nyumba, sasa hii kusema uchumi umepanda umepandaje? Kiukweli kusema uchumi umepanda wakati hatuuoni huko chini tunaoishi na wananchi bado kuna walakini mkubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni uzalishaji wa mazao. Ukienda kwenye Kitabu cha Hali ya Uchumi kwenye page 134, kuna baadhi ya mazao ambayo siku za nyuma ndiyo yalisaidia uchumi wa Taifa hili kukua ikiwemo kahawa, pareto, katani, tumbaku, mkonge, pamba, korosho na chai . Leo ukisoma kitabu kinasema mazao haya yamepungua tena kwa asilimia kubwa na sababu zilizotolewa hapa ni kwamba, kwanza mvua za kutosha zimekosekana lakini pili, wakulima wameshindwa kununua pembejeo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunazungumzia habari ya uchumi wa viwanda, bado tunategemea mvua ambazo hazina uhakika. Hatuwezi kuzungumzia uchumi wa viwanda wakati mazao ambayo yalikuwa yanainua uchumi wa Taifa hili, ukisikia Kagera wameendelea ujue ilikuwa ni ndizi na kahawa; Kilimanjaro wameendelea ni kahawa, kule Mbeya cocoa, Tanga viwanda vilikuwa zaidi ya mia ni katani ilisaidia sasa leo yale mazao hayapo, yamekuwa ni mapori, tunazungumzia habari ya uchumi wa viwanda, vinatoka wapi hivyo viwanda? Kwa hiyo, tukitaka kwenda kwenye uchumi wa viwanda lazima tujizatiti kwenye kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tulikubaliana miaka mitano iliyopita kwamba tutahakikisha tuna angalau hekta 1,000 za umwagiliaji. Kwenye hotuba ya Waziri wa sekta nilisoma mpaka sasa hivi ni hekta 460,000 hata nusu kwa miaka mitano hatujafika, hatuwezi kwenda na leo tena mabadiliko ya tabianchi, global warming na mambo mengine mengi. Kwa hiyo, hatuwezi kwenda kwenye uchumi huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sababu ya pili tumeambiwa ni wakulima kushindwa kutumia pambejeo. Zao kama kahawa leo ukisema mkulima anunue pembejeo hawezi, ni very expensive. Kwa hiyo, kwenye mzao kama haya lazima Serikali itoe ruzuku kuwaachia wakulima ni vigumu. Wengine wanang’oa wanapanda maharage, migomba kwa sababu hawawezi kuendelea kumudu kununua pambejeo. Kwa hiyo, naomba tuangalie hisotoria ya nyuma, Mwalimu Nyerere alifanya kazi kubwa sana, mazao ambayo ndiyo yalikuwa kielelezo cha Taifa letu tusiyaache. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hata kwa mazao ambayo yapo sasa hivi, kwa mfano, suala la tumbaku Mkoa wa Tabora tunalima lakini bado wakulima wake wameendelea kuwa maskini. Bei za mazao yetu bado ni tatizo. Hivi navyoongea masoko ya jana na juzi bei imeshuka kutoka Sh.4,000 mpaka Sh.4,500 kwa kila sasa wanauza kilo nzima ya tumbaku kwa Sh.181, hayo ni masoko ya jana. Sasa mkulima kama huyu ambaye amenunua pembejeo kwa Sh.90,000 mfuko mmoja wa kilo 50 mpaka Sh.140,000 kwa wale waliokosa ruzuku lakini bei ya Serikali Sh.90,000, mkulima huyu akauze tumbaku Sh.181 wakati amekwensda kukopa benki, anadaiwa kwenye taasisi za fedha, ananyanyukaje huyu? Kwa hiyo, hata kwa mazao ambayo yanasaidia bado Serikali hatujaweza kusimamia bei nzuri ya mazao yetu, hili ni tatizo kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine, Mkoa wa Tabora umelima tumbaku lakini bado kiwanda kipo Morogoro. Tumepiga kelele sana hapa kwa nini Kiwanda cha Tumbaku hakijengwi Mkoa wa Tabora? Majibu tunaambiwa kwamba tunatafuta wawekezaji lakini juzi mwaka uliopita amekuja mwekezaji wa Kiwanda kingine cha Tumbaku amejenga Morogoro. Naomba Serikali na Waziri aje na majibu, tunataka Kiwanda cha Tumbaku kiende kikajengwe Mkoa wa Tabora na mtuambie namna gani mtafanya kiwanda kile kiweze kujengwa vinginevyo kiukweli vijana wale hawana ajira lakini tumbaku inalimwa kwao tena asilimia 60 ya tumbaku ya Tanzania inalimwa pale Mkoa wa Tabora. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukienda kwenye kitabu pia cha Mheshimiwa Waziri ukurasa wa 92 utaona namna gani ambapo tunaingiza sana bidhaa ndani kuliko kupeleka nje kwa hiyo, tunauza kidogo, tunaingiza sana, hili ni tatizo. Kuna vitu vingine ambavyo hatuhitaji kuingiza kutoka nje, kwa mfano, toothpick, pamba za kwenye masikio, viberiti lakini tuna-import kutoka nje, fedha tunayokusanya tunapeleka nje kutengeneza ajira kwa vijana wao, sisi tunabaki ni masoko ya bidhaa za wenzetu, hatuwezi kupiga hatua, hili ni tatizo kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Tabora tunalima mbao, tena quality mbao, mninga na mpogo safi unaupata Tabora. Serikali ilisema itahakikisha samani zote za Serikali zinatoka ndani ya nchi lakini leo tunapeleka magogo, mbao, Wachina wanakwenda kuchukua, tunakwenda kununua bidhaa za Kichina very weak, hazina ubora kwa gharama kubwa. Kwa nini Serikali inashindwa kusimamia vitu ambavyo tunaweza kutengeneza hapa ndani ya nchi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi kweli kwa ule Msitu wa Sao Hill pale Iringa, kuna haja ya kwenda kununua kiberiti nje? Hata mtoto wa darasa la saba anatengeneza kiberiti, hata mtoto wa darasa la pili anatengeneza toothpick, tunayo pamba, vitu vingine ni sisi tunajitakia. Fedha ambayo tunaipeleka nje inakwenda kujenga kule nje kumbe tunaweza tukaitumia ndani ya nchi yetu ikazunguka humu humu, tuka-invest ndani ya nchi yetu. Kitendo cha Serikali kuruhusu hata vitu vidogo vidogo vikaingizwa ndani ya nchi ni kushindwa kusimamia nchi yetu lakini pia ni kushindwa kusimamia namna gani vijana wetu wapate ajira, tuna- create ajira kwa Wachina na kwa wengine huku vijana wetu wakiwa watanga tanga bila ya kuwa na ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi nyingi kwa Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na wataalam wote wa Wizara hii kwa kazi nzuri na kuandaa hotuba hii na kuleta hapa Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge limekuwa linatenga fedha nyingi sana kwa ajili ya NIDA kuendesha zoezi la kuandikisha raia ili kupatiwa vitambulisho vya uraia. Zoezi hili lilianza mwaka 2011 na lilitegemewa kukamilika ndani ya miaka miwili. Leo ni zaidi ya miaka nane (2011-2018), naomba Serikali ieleze Bunge zoezi hili limefikia hatua gani? Watanzania wangapi wamepatiwa vitambulisho mpaka sasa na ni lini zoezi hili litakamilika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, askari polisi wamekuwa wanapanda madaraja wanakaa miaka mingi bila kupandishwa mishahara yao na maslahi mengine. Wapo askari waliopanda madaraja tangu 2010, 2015 mpaka leo hawajaboreshewa mishahara yao. Jambo hili linawanyima haki zao lakini pia linakatisha tamaa ya kiutendaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lipo tatizo kubwa sana la watuhumiwa kuwekwa lock-up za polisi/mahabusu kwa zaidi ya saa 48 kinyume na sheria. Polisi wanawaweka watuhumiwa mahabusu siku 7 - 14 bila kuwapeleka mahakamani. Serikali ilieleze Bunge na kutoa kauli kuhusu tatizo hili ambalo tunalisemea kila leo lakini bado linaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Zimamoto halitengewi fedha za kutosha kuweza kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. Jeshi hili halina ofisi/vituo wilayani bado wamo kwenye ofisi za mikoa kwa maeneo mengi. Hakuna vitendea kazi vya kuokoa na kupambana na majanga ya moto, magari ni machache na hata pale wanapoitwa wanafika hawana maji. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha Jeshi la Zimamoto linakuwa na vituo katika wilaya zote hapa nchini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kaliua hatuna nyumba za kutosha za askari polisi. Askari wengi wanakaa mitaani jambo ambalo ni hatari sana kwa usalama wao na familia zao. Serikali haijawahi kujenga nyumba za polisi Wilaya ya Kaliua kwani chache zilizopo ni juhudi za viongozi wa Kaliua na wananchi. Serikali sasa itenge fedha za kujenga nyumba za askari pale Kaliua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Polisi Kaliua hakina vitendea kazi vya kutosha. Gari ni moja, pikipiki ni mbili tena mbovu, hakuna komputa hata moja na mafuta yanayotengwa kwa ajili ya gari hilo ni kidogo mno. Wilaya ya Kaliua ni kubwa sana hivyo matukio ya uhalifu ni mengi sana. Serikali itoe kipaumbele kwa Wilaya ya Kaliua kupatiwa vitendea kazi ili wafanye kazi kwa ufanisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Polisi hutumia nguvu kubwa sana hasa wakati wa kukamata wahalifu wasiokuwa na silaha. Wanaumizwa kwa vipigo wakati hawajathibitishwa kama wamekosea. Wapo raia wengi wameumia na wengi wamepoteza maisha kwa sababu ya matumizi ya nguvu kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Kaliua, Kata ya Ushokora tuelekezwe kutenga eneo kwa ajili ya kujenga gereza. Tangu 2014 mpaka leo hakuna lolote linaloendelea pale. Wananchi waliokuwa wanatumia eneo hilo walinyimwa kutoliendeleza hata kwa kilimo. Serikali itueleze nini hatma ya eneo lile na nini mkakati wa Serikali kuhakikisha Kaliua panajengwa gereza?
Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kunipa nafasi nami niweze kuchangia hotuba za Mawaziri hawa wawili. Pia niungane na Waheshimiwa Wabunge kuwapongeza Mawaziri kwa kazi nzuri wanayoifanya na hasa Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Jafo na timu yake nzima kwa kusaidiana na Katibu Mkuu kwa kweli kazi inaonekana. Japokuwa Wizara ni pana sana lakini kwa kwenda field kwenda kuona kazi zinazofanyika kule wanaweza kutatua kiasi kikubwa sana cha changamoto ambazo zinaikabili Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana Serikali imetenga shule moja ya msingi katika kila Wilaya kuweza kupokea watoto ambao wana mahitaji maalum kwa maana ya watoto walemavu. Kwa bahati mbaya sana shule hizi miundombinu yake siyo rafiki kwa watoto hawa. Pia shule hizi hazina Walimu wenye uwezo wa kufundisha hawa watoto ambao wana mahitaji maalum na kwa sababu watoto wale kuna wengine ni vipofu, kuna wengine ni walemavu wa viungo, wengine ni usikivu wote wamekusanywa pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaiomba Serikali na fedha ya capitation kwa ajili ya shule hizi hazitoshi kufanya chochote kuboresha miundombinu, Serikali ihakikishe inaboresha miundombinu katika hizo shule ili watoto waliopelekwa pale waweze kupata elimu sawasawa na watoto wenzao wanaopata elimu maeneo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni upungufu wa Watumishi. Kiukweli tuna shida kubwa ya watumishi katika sekta zote. Ukienda elimu, ukienda afya, ukienda ugani, ukienda Watendaji wa Kata kila kona, kwa hiyo TAMISEMI bila kuwa na watumishi wa kutosha wananchi hawawezi kupata huduma. Tunaomba Serikali ihakikishe inaongeza watumishi, Mheshimiwa Mkuchika ahakikishe tunaajiri watu, bahati nzuri wasomi tunao, wako wamesoma wako vijijini, wako mijini wanahangaika hawana kazi, kwa nini hatuajiri?(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya Wilaya ya Kaliua Sekta moja tu ya afya tuna upungufu wa asilimia 76, hujaenda elimu hujaenda kokote. Tunaomba sana Serikali iongeze watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lingine ni suala la watumishi kutokupanda madaraja kwa wakati. Leo Walimu wanakaa miaka minne hadi sita hawajapanda madaraja. Swali la kujiuliza watakuja kupandaje madaraja kwenda na wakati? Wakati anatakiwa miaka mitatu apande daraja, leo anapokaa miaka saba hajapanda daraja, anapandaje madaraja? Tunaomba watendaji wapande madaraja kuendana na wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la watumishi wa Kaliua walihama kutoka Urambo tangu mwaka 2013, mpaka leo mwaka wa sita hawajapata stahiki zao. Mwaka wa sita kuhamishwa na haki zao zote, leo wapo Wilaya ya Kaliua lakini tangu wakiwa Wilaya Urambo mpaka wamehamia Wilaya Kaliua leo miaka sita hawajapata stahiki zao. Waziri Mkuu alikuja Kaliua, akaagiza wapewe haki zao, leo ni mwaka wa sita hawajapewa. Naomba watumishi hawa wa Kaliua ambao walitoka Urambo wapatiwe stahiki zao kutokana na majukumu yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la Hospitali ya Wilaya. Wilaya yetu ya Kaliua ambayo ina takribani wananchi laki nne hatuna hospitali ya Wilaya. Tuna vituo vinne tu vya afya, tumeweka kipaumbele chetu ni hospitali ya Wilaya kwa mwaka huu, tukaiomba Serikali itusaidie bahati mbaya sana nimeangalia hiki kitabu hatupo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana tumeanza kama Halmashauri tumejenga jengo la OPD lenye ghorofa moja, mara nyingi nimeongea hapa Bungeni tumekamilisha tuko kwenye finishing, tukawaomba Serikali itusaidie majengo mengine, tunamwomba sana Mheshimiwa Waziri aiangalie Wilaya ya Kaliua kwa jicho la pekee. Tunazo Kata 26 tuna vituo vya afya vinne (4), tuna vijiji 101 vituo vya afya ni vinne.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wanafuata huduma za upasuaji wa akinamama Urambo, tunafuata Kigoma. Naomba sana kwa mwaka huu Kaliua iangaliwe kwa jicho la pekee, kama imesahaulika naomba iingizwe tupate hospitali wananchi wa Kaliua, tuokoe vifo vya akinamama na watoto vinavyotokea kwa kukosa huduma za afya.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la uwezeshaji wa vijana na kina mama. Tumeongea sana hapa Mheshimiwa Jenista alituambia tuna mifuko 17. Nashangaa kama kuna mifuko 17 mbona katika Wilaya yangu ya Kaliua kwa miaka mitatu tumepata vikundi vya SACCOS vimeletwa vinne tu, vijana viwili, akinamama viwili. Fedha nyingine yote ambayo tunawapa vikundi ni ya ndani ya Halmashauri, hii mifuko 17 inasaidia watu wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pengine mgawanyo wake siyo sahihi, pengine mgawanyiko hauna uwiano kwenye Wilaya mbalimbali, inawezekana kuna maeneo ambayo zinakwenda zaidi wengine wanakosa. Naomba sana hata fedha inayotengwa na Halmashauri ni kidogo haitoshi, akinamama vikundi viko zaidi ya mia, hatuwezi kuwapatia mtu anaomba milioni 10 unampa milioni mbili!

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilichangia kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu, lakini bado hapa kwa umuhimu wa Wizara hii na kwa kuwa Mheshimiwa Jafo anajua tukiwawezesha akinamama, tumewezesha familia, tumewezesha jamii, haiwezekani kuendelea kusema tunawawezesha wakati ambapo tunawapa kidogo na hatuwezi kuwasaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni TARURA. TARURA anafanya kazi nzuri shida hawana fedha nimeongea jana hapa barabara zimeharibika nyingi TARURA wako ofisini hawana fedha ya kufanya kazi. Nakubaliana na Waheshimiwa wengine kwamba tuwape TANROAD asilimia 50 na TARURA asilimia 50 kwa sababu barabara za vijijini ndiyo barabara za uchumi, mazao yanatoka kule, wananchi wako kule. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkuu wa Wilaya, nyumba imeanza kujengwa tangu mwaka 2013, mpaka leo imekuwa ni pagale haiendelei, imeota majani tunaomba sana nyumba ya Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya wa Kaliua imaliziwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho ni suala la kuendelea kuwepo mishahara hewa. Nimeangalia kitabu cha CAG kuendelea kuwepo na mishahara hewa, hivi jamani ndani ya miaka yote na juhudi zote, bado Halmashauri zaidi ya 29 zinaendelea kulipa mishahara hewa. Tunalia habari ya watumishi, tunalia hatuna watumishi wa kutosha lakini fedha zaidi ya milioni 329 wanalipwa mishahara hewa. Huu ni udhaifu kwa kweli wa hali ya juu!

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba sana tatizo la mishahara hewa watu waliokufa wanalipwa mishahara, liwe ni mwisho. Ni aibu kuendelea kuonekana kwenye vitabu vya CAG na anashauri anasema mapendekezo anayotoa hayafanyiwi kazi, Serikali amkeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nami nikushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia kwenye taarifa mbili za Kamati. Nazipongeza taarifa zote mbili ile ya Kilimo na ile ya Maliasili ambayo mimi ni Mjumbe wake.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais ameona kilio cha wakulima na wafugaji ambapo wamenyanyaswa sana hasa wafugaji na wameonewa kwa miaka mingi na ametoa tamko na ameagiza Mawaziri walishughulikie suala hili kwa haraka. Tamko hili linaweza kuchukuliwa tofauti na likichukua muda bila kufanyiwa kazi watu wataingia ndani ya hifadhi na kuharibu uhifadhi wakisema kwamba walikuwepo miaka mingi. Kwa hiyo, tunaomba Mawaziri waliopewa jukumu hili wachukue hatua za haraka kuhakikisha kwamba tamko hili la Mheshimiwa Rais linafanyiwa kazi kwa haraka ili kuokoa uhifadhi.

Mheshimiwa Spika, tunapoongea yapo maeneo ambapo watu walikuwa wametoka miaka mingi kwa mfano Bonde la Kilombero lakini baada ya lile tamko tunaona wanarudi kule kwenda kulima kwa matreka usiku na mchana. Kwa hiyo, hili litakuwa ni tatizo kama hatua za haraka hazitachukuliwa, tutakuwa tunakwenda kuharibu uhifadhi. Naomba tamko hili lifanyike kwa uhakika ili migogoro ya wakulima na wafugaji iweze kuisha na waweze kupata maeneo ya kufugia na kulima.

Mheshimiwa Spika, niende kwenye National Housing. Kwa miaka mingi National Housing imefanya kazi nzuri na baada ya kuwepo kwa Mkurugenzi Mkuu aliyeondoka, Ndugu Mchechu. National Housing kwa mwaka 2010 mpaka 2018 wameweza kutengeneza mtaji kutoka shilingi trilioni 4.3 na walikuwa na projection ya kwenda kwenye shilingi trilioni 7 mwaka 2025 lakini National Housing leo ni kama iko stacked, imetulia. Walikuwa na miradi mingi ya strategic kama Mradi wa Kawe na Morocco lakini miradi ile imesimama wakati wameshawekeza fedha nyingi na mingi iko zaidi ya 40% ya utekelezaji wake.

Mheshimiwa Spika, tunaiomba Serikali kwa kuwa wamezuiliwa sasa kuchukua mikopo kuendeleza miradi ile Serikali ione mikopo iliyowekezwa pale inazalisha riba waweze kutoa kibali waweze kuiendeleza ili kuokoa fedha ambayo imewekwa pale lakini pia National Housing iendelee. Tusipoangalia Shirika ambalo tumelipongeza miaka mingi litakufa kwa sababu tu ya watu ambao walikuwa wana maslahi yao.

Mheshimiwa Spika, tunajua wako watu wengi sana walitamani National Housing, miaka mingi lilikuwa ni shirika ambalo linamilikiwa na watu, nyumba zilikuwa hazijulikani, ni kama lilikuwa si shirika la umma, walikuwa wanamiliki watu mikononi. Baada ya kuonekana kwamba nyumba sasa zimetambuliwa ni nyumba za umma, shirika linafanya kazi, linapendezesha miji yetu mikubwa, watu walipiga vita kubwa sana na wamefanikiwa. Serikali iangalie, si kila ushauri waupokee waangalie ushauri ambao unawezesha kupiga hatua kwenda mbele. Wengine walitamani tu kwamba viongozi waliokuwa wanasimamia Shirika lile wakae pembeni ili waendelee kupiga deal na huu ndiyo uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie shamba la miti la Sao Hill. Tumekwenda Sao Hill na nashukuru TFS kwa kazi nzuri sana lakini zipo changamoto. Tunaiomba Serikali, kuna utitiri mkubwa wa kodi zaidi ya 32 kwa wafanyabiashara. Tunajua wafanyabiashara wa Taifa hili ni wadau wakubwa wa maendeleo na Mheshimiwa Rais kila siku anasema, tunaomba kwanza kodi zile zipungue.

Mheshimiwa Spika, lakini kingine, kuna kodi moja ambayo inaitwa kodi ya cess. Bungeni mwaka jana tulibadilisha sheria ya cess kutoka 5% kwenda 3% lakini Mkoani Iringa bado cess ya mazao bado ni 5%. Si hilo tu wanatoza mara mbili; mti ukiwa porini unatozwa cess 5% na ukitolewa mbao unatozwa cess 5%, Halmashauri na Sao Hill wote wanatoza. Wafanyabiashara wanaumizwa na hawa ndiyo wadau wa maendeleo. Tunaomba kwanza cess iwe moja lakini pia kodi zipungue ili waweze kuchangia vizuri maendeleo.

Mheshimiwa Spika, tumekwenda pale kwenye kiwanda tumeangalia, zaidi ya malori 20 yana nguzo za REA yamekaa mwezi mzima yamezuiliwa kuondoka kwa sababu TANESCO inatakiwa kulipa cess kwa mara ya pili wakati nguzo hizo zimelipiwa cess zikiwa kule Sao Hill. Sao Hill inakusanya zile cess inatoa percent inapeleka kwenye Halmashauri. Leo mbao ziko kiwandani tayari kusafirishwa Halmashauri inasema hakuna kutoa nguzo mpaka ilipwe tena cess nyingine, kwa nini kuwe na double taxation? Tunaiomba Serikali ihakikishe kunakuwa na cess moja lakini pia kodi ziondolewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni la LMD, kuna fedha ambayo wafanyabiashara wenyewe wamemua kuchanga…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
Azimio la Bunge la Kuridhia Ubadilishaji Hadhi Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi, Ibanda na Rumanyika – Orugundu kuwa Hifadhi za Taifa
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi uliyonipatia pia niweze kuchangia azimio ambalo liko mbele yetu. Niishukuru pia Serikali kwa kuweza kusikiliza ushauri wa Kamati na kuweza kupandisha mapori haya ya akiba kuweza kuwa chini ya TANAPA.

Mheshimiwa Spika, ni matarajio ya wananchi wa maeneo yale kwa sababu maeneo haya yalikuwa ni mapori kutokana na kwamba Serikali ilikuwa haiwekezi kwenye mapori haya ya akiba na yalikuwa ni mapori kiasi kwamba ndiyo maana Wabunge wanasema kwamba yalikuwa ni vichaka vya majambzi na vichaka vya wezi. Matarajio sasa ya wananchi wa maeneo yale kwamba baada ya mapori haya kupandishwa kuwa hifadhi za Taifa watanufaika kikamilifu sana na uwepo wa hifadhi hizi jirani yao.

Mheshimiwa Spika, naomba pia niipongeze TANAPA kwa kazi nzuri wanayoifanya chini ya Mkurugenzi wake Mkuu na Watumishi wote wanafanya kazi kubwa sana lakini kwa mazingira magumu sana. Tunapowaongezea majukumu, lazima pia tuangalie namna ya kuwawezesha wapate finance ya kutosha kuweza kuwekeza kwenye mapori hayo. Kama TANAPA hawatawekeza kwenye mapori haya yakaweza kuwanufaisha wananchi wa maeneo yale kiukweli itakuwa ngumu sana kwa mapori haya kuweza ku-success kwa sababu bado ujangili utaendelea katika maeneo yale kwa sababu hawataweza kufanya doria za kutosha.

Mheshimiwa Spika, pia TANAPA wana miradi ya out reach, wana miradi inaitwa miradi ya “ujirani mwema” ambapo wanawawezesha wananchi wa maeneo yanayowazunguka kuwajengea miundombinu mbalimbali ya elimu, ya afya na mambo mengine kiasi kwamba inawafanya wananchi wanaona sasa maeneo yale ni maeneo yao. Kwa hiyo kama TANAPA wasipowezeshwa waweze kutoa miradi ya ujirani mwema wananchi hawa hawataona umuhimu wa kuweza kuyatunza maeneo haya. Kwa hiyo naiomba sasa Serikali wakati wanaiongezea TANAPA mzigo wa majukumu ya kazi pia waangalie namna ya kuwawezesha ili waweze kufanyakazi hii kwa ufanisi zaidi.

Mheshimiwa Spika, TANAPA pamoja na kufanya kazi yao vizuri, kutunza mapori 16 na sasa hivi wameongezewa mengine na wanaendelea kuongeezewa, lakini pia wanalipa kodi zote stahiki kwa Serikali. Naiomba Serikali, kwa kuwa tunaiongezea TANAPA majukumu, TANAPA iliambiwa kulipa 10 percent ya mapato yake yote kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali, kwa kuwa sasa tunaiongezea TANAPA majukumu mazito zaidi, tupungue ile asilimia inayokwenda kwenye Serikali Kuu ili sasa wabaki nayo kwa ajili ya kuwezesha mapori haya ambayo tunawapa. Tuangalie Ruaha imeshindwa hata kutengeneza barabara vizuri kutokana na kwamba kipato chao ni kidogo.

Mheshimiwa Spika, mapori haya haya tuliyoyafanya kuwa chini ya TANAPA, sasa pia yanahitaji utangazaji, lakini pia yanahitaji kuweza kuhakikisha kwamba miundombinu yake kule ndani inakuwa mizuri. Kwa hiyo pamoja na nia nzuri ya Serikali, kama mapori haya hayatawezeshwa, lakini pia wananchi wale waone faida zake kuhakikisha kwamba hakuna migogoro. Leo TANAPA kuweza kuondoa migogoro kwenye maeneo kama Mikumi, hakuna migogoro kabisa na maeneo mengi wametumia rasilimali kubwa, wamefanya kazi kubwa kwa hiyo migogoro ya ardhi, maeneo ya jirani yakiwa kila siku haiishi bado TANAPA watakuwa na mzigo mkubwa wa kushindwa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Mheshimiwa Spika, naiomba sasa Serikali kwanza ifanye kazi kubwa kuhakikisha kwamba maeneo yale ambayo wananchi wale wamezunguka ihakikishe kwamba inasaidiana na TANAPA kuweza kuhakikisha kwamba wananchi wale wanakubali maamuzi yale yaliyofanywa na Serikali ili waweze kukubali kwamba maeneo yale yatakwenda kuwanufaisha lakini siyo kwa maneno, waone kwa vitendo kwenye maeneo yao. Waone hospitali zinajengwa, waone shule zinajengwa, waone vituo vya afya vinajengwa, waone miundombinu yao inawezeshwa ili wawe part and parcel ya maeneo haya ambayo yameweza kupandishwa hadhi kuweza kuwa hifadhi za Taifa.

Mheshimiwa Spika, naunga hoja hii mkono kwa malengo kwamba Serikali ihakikishe kwamba TANAPA inawezeshwa vya kutosha na hasa ile 10 percent ya mapato makubwa kwenye Mfuko wa Serikali ipungue iwe five percent ili percent inayobaki iende kuwekeza kwenye mapori ambayo tunaipa TANAPA mzigo wa kuweza kuendesha.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, na mimi nakushuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia hoja muhimu sana ambayo ipo mbele yetu. Hoja ya maji ni hoja ya uhai na kiukweli mtu unaweza ukaishi bila chochote, lakini huwezi kuishi bila kupata maji. Kitendo cha Serikali kuendelea kutoa fedha kwenye kidogo kwenye Wizara ya Maji kwa asilimia 51 zilizotolewa kwa bajeti iliyopita, kwa mwendo huu hatuwezi kutatua tatizo la maji na ile spirit ya kumtua mama wa Tanzania ndoo kichwani haitafikiwa na spirit ya kutaka mtoto wa kike wa Kitanzania asome, apate full education, awe mtu wa maana haitafikiwa. Vile vile pia spirit ya kuona kwamba kila Mtanzania au wananchi wote wanaenda kwenye shughuli za maendeleo na kuachana na shughuli za kusaka maji haitakaa iishe. Kwa hiyo kwanza ni lazima kwenye Sekta ya Maji fedha inapotengwa kwenda kufanya kazi ya kuleta maji itoke kikamilifu ikafanye kazi ya kuleta maji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niunge mkono Wabunge wote waliosimama kusema kwamba Mfuko wa Maji uongezewe; Mfuko wa Maji lazima uongezwe. Hatuna namna nyingine zaidi ya kuhakikisha kwamba kuna fedha ya kutosha kupeleka maji kwa wananchi wetu. Tumeona mfano mdogo wa REA, sasa hivi kila Mbunge akisimama anagusia REA japo sio vijiji vyote angalau kuna kazi imefanyika imeonekana. Kwa hiyo, naiomba Serikali na naomba niungane na wale wote waliosema patachimbika Jumatatu hapa kama fedha ya Mfuko haitaongezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kaliua tuna shida kubwa sana ya maji; mwanamke wa Kaliua anateseka sana, mtoto wa Kaliua hata shuleni wanakwenda kuvamia kwenye nyumba za watu kutafuta maji ya kunywa; nyumba za walimu na wananchi waliopo jirani. Wilaya ya Kaliua tunaomba kipaumbele cha hali ya juu.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kaliua kwanza kabisa jiografia yake na Mkoa wa Tabora hatuna maji ardhini, kwa hiyo Miradi yote ya Maji ya World Bank na visima hatunufaiki navyo kwa sababu hatuna maji ardhini. Kingine jiografia ya maeneo yetu hakuna mito kama ambayo inatamkwa Morogoro, Kaliua, Tabora hatuna mito hiyo, tuna Mito ya Igala na Malagarasi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali ilikuwa na mpango wa kutoa maji Malagarasi kuleta Kaliua na Wilaya ya Urambo, lakini pia mradi mwingine ni kutoa maji Victoria kuja mpaka Igunga, Nzega, Tabora na Uyui. Ule mradi wa Malagarasi ambao sasa hivi ni mwaka wa nne ulikuwa umetengewa fedha kidogo kidogo ya kuanza kufanya usanifu yakinifu…. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Sakaya…

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: mpaka leo hakuna chochote ambacho kimefanyika…

SPIKA: Mheshimiwa Sakaya kidogo…

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: mwaka huu Serikali imekuja na mpango kwamba…

SPIKA: Mheshimiwa Sakaya kidogo tu, Waheshimiwa Wabunge hebu tupunguze sauti, hata sisi wenyewe tunaweza kusikia hasa upande huu wa CCM, kwa nini CCM hatusikilizi? Tutulie kidogo hata kama unaongea na mtu, ili mjadala uwe na maana, lakini sasa maeneo haya, ni kama mikutano ya hadhara kabisa. Endelea Mheshimiwa.

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Spika, baada ya kuona kwamba mradi ule wa Malagarasi utakuwa na gharama kubwa, umekuja na mpango mwingine wa kuweka Kaliua na Urambo kwenye mradi wa miji 29. Nashukuru kwa kuwa tumewekwa kwenye huu mradi wa miji 29 ila kwa hamu kubwa ya maji ambayo tunayo, tunaomba huu mradi uende haraka tuweze kufanikiwa kupata maji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia nimeangalia kwenye kitabu cha Mheshimiwa Waziri, Wilaya ya Kaliua imewekwa kama ni sehemu ya Urambo, nakubaliana kweli Wilaya ya Kaliua tulizaliwa kutoka Urambo lakini ni Wilaya inayojitegemea, inayosimama, tuandikwe kama Wilaya na sio mtoto wa Urambo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuwa tumepata mradi huu ambao ni wa miji 29, lakini bado kwa mradi alivyosema Mheshimiwa Waziri ni kwamba, utalisha kilomita 12 kutoka barabarani kuja Wilaya ya Kaliua. Jiografia ya Wilaya ya Kaliua ni kubwa sana, kutoka Makao Makuu ya Wilaya kuna mwananchi anayeishi kilomita 120, kilomita 90, kilomita 60, kilomita 30 mpaka unafika. Kwa hiyo, mwananchi huyo ambaye anaishi kilomita 60 atapata wapi maji? Huyu wa kilomita 90 na kilomita 120 watakunywa wapi maji? Naomba waifahamu jiografia ya Kaliua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninachoomba pamoja na mradi huu ambao wa miji 29, lazima uwepo mradi mwingine wa kuweza kutoa angalau maji kutoka Mto Ugala ambao ni mto pekee ambao tunao Kaliua uweze kulisha wananchi ambao wapo mbali ambao hawatanufaika na mradi wowote, aidha ni Malagarasi hautawafikia au ni huo wa kutoka Mjini Tabora hautawafikia. Kwa hiyo, ni lazima kuwepo na mpango wa kuhakikisha wale ambao hawanufaiki na mradi huu uliopo wanapataje maji kwa sababu na wenyewe ni Wanakaliua na ni Watanzania, wana haki ya kupata maji na kupata maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nishukuru pia kuna mradi mdogo ambao unaendelea pale Kaliua Mjini ambao ni wa Kata ya Kaliua na Kata ya Shokora, naomba pia Serikali itoe fedha kwa wakati mradi huo ambao ni mradi wa Kata mbili tu uweze kukamilika.

Mheshimiwa Spika, pia kuna mradi mwingine ambao tunaomba Serikali itusaidie, tumepata kisima kimoja kimechimbwa na GTI pale Kijiji cha Usindi, Kata ya Ushokola. Maji yale ni mengi sana, tunaomba Serikali isaidie kuyasambaza yaweze kulisha eneo kubwa, kwa sasa hivi yamelisha kijiji kizima cha Usindi. Tunaomba iwekwe nguvu ya kutosha na GTI wapo tayari kusaidiana na Serikali uweze kusambazwa, uweze kulisha angalau kata nzima, inawezekana na ni kisima cha kwanza katika Wilaya ya Kaliua kuweza kuchimbwa kikawa kina maji ya kulisha angalau kata nzima. Kwa hiyo, naomba Serikali iweke nguvu zake pale. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niende kwenye Wakala wa Uchimbaji; mwaka 2016/2017, Wakala wa Uchimbaji wa Visima na Mabwawa walikuja Kaliua wakafanya utafiti katika maeneo mengi, wakaainisha maeneo tisa ya kuchimba mabwawa na wakasema kutokana na jiografia yetu, watafanya haraka kuweza kuja kutusaidia kuchimba mabwawa ili tukusanye maji ya mvua, lakini mpaka leo ni mwaka wa tatu hakuna kilichofanyika. Kwa hiyo, naiomba Serikali wale Wakala wa Uchimbaji Visima na Mabwawa waje Kaliua, tayari walishakuwa na mpango ule, waweze kuhakikisha kwamba maeneo yale yaliyoainishwa yanachimbwa mabwawa tuweze kukusanya maji ya mvua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni uvunaji wa maji. Bajeti ya mwaka 2017/2018, Serikali ilikuja na mipango mizuri sana hapa Bungeni kwamba ilikuwa imetoa maagizo kwenye Halmashauri zote nchi nzima na kutunga sheria ndogo kuzitaka taasisi za kijamii, asasi na watu binafsi kujenga miundombinu ya kuvuna maji. Pia wakati huo huo ikatuambia kwamba Serikali ilikuwa imetoa mafunzo kwa wananchi karibu 795 kwa ajili ya kutumia mbinu sahihi na nyepesi kuvuna maji.

Mheshimiwa Spika, pia Serikali ikasema ilikuwa imejenga matenki makubwa 29 na 59 na ukubwa tofauti kukusanya maji katika Wilaya mbalimbali. Sasa nategemea Waziri akija ku-wind up atuambie huu mpango umefikia wapi? Wananchi wangapi wameendelea kupewa elimu na matenki mangapi yameendelea kujengwa? Pia tujue kwamba maagizo yaliyotolewa kwenye Halmashauri mbalimbali yametekelezwa kwa kiasi gani.

Mheshimiwa Spika, ni aibu kwa mtu anayetoka nje kuiona Tanzania, akiona mvua zinaponyesha maji yanavyosambaa yanavyoharibu miundombinu akisikia tunalia maji hapa Bungeni, atatuona kama tumechanganyikiwa kiasi fulani kwa sababu hakuna juhudi ya kukusanya maji haya, hatuyakusanyi kabisa, yanakwenda kuharibu barabara, nyumba na kila kitu lakini kilio cha maji kipo pale pale. Kwa hiyo, kwa maana nyingine lazima Serikali ijipange kikamilifu kukusanya maji ya mvua, hii ni neema wakati mwingine, tuitumie kuhakikisha kwamba tunapunguza tatizo la maji. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kunipa nafasi nami niweze kuchangia kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri ambayo iko mbele yetu. Pia nimshukuru Mungu pia kunipa kibali kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu kwa ajili ya kuendelea kuwatumikia wananchi na kutumikia taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeweka sera ya kuwasaidia kujenga uwezo kwa makandarasi wa ndani kwa maana ya kwamba zile barabara ambazo ziko chini ya kilometa 30 wanapewa wakandarasi wa ndani ili kujenga uwezo wao, pia kuendelea kuenzi kazi zao za ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa na tatizo kubwa sana la udhaifu mkubwa sana la utekelezaji wa kazi zinazofanywa na wakandarasi wa ndani. Na hapa ninasema kwamba hatuwachukuii wakandarasi wa ndani tunawapenda, lakini tunaangalia matatizo tuliyokuwa nayo pia miradi ambayo inapangwa iende kwa muda na kazi iende kwa muda unaotakiwa. Leo kazi ya mwaka mmoja inafanyika kwa miaka mitatu, wapo wakandarasi ambao kiukweli ni dhaifu uwezo ni mdogo na unapoambiwa kwamba washirikiane na wenzao pia wanakuwa ni wagumu, ninaomba Serikali ituambie tutaendelea kuwabeba wakandarasi wa aina hii mpaka lini? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wantanzania wanapata shida mfano mmoja ni barabara Kaliua Urambo, kilometa 28 tu wamepewa wakandarasi wamepewa mwezi wa 4 mwaka 2017 ilikuwa ni kazi ya mwaka mmoja, leo ninapoongea na wewe na hapa Bungeni hata robo haijafika na wako site, na visingizio kila siku mara mvua, mara jua mara hiki ukienda pale kazi inayofanyika haieleweki, lakini wakati huo huo wenzao wa nje, wenzao wa CHICO walipewa kandarasi pamoja wamejenga barabara ya Neuya hapa kwenda Tabora kila siku wako kazini na kazi yao ni nzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali ituambie tutaendelea kuwabeba hawa wa ndani mpaka lini? Kama lengo ni kuwasaidia tunawatesa wananchi, tunawaonea wanachi. Kaliua ni Wilaya yenye uzalishaji kubwa sana asilimia 60 ya tumbaku yote Tanzania inatoka Kaliua mazao mengi mpunga, mahindi, karanga, lakini ukiona barabara ambavyo magari yanapita unaona huruma, pia Kaliua sasa hivi hatuna hospitali ya Wilaya, ukiona mtu akipewa rufaa akienda Tabora unamuonea huruma ile barabara jinsi ambavyo ni mbaya.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali ituambie sasa baada ya mkandarasi wa pale barabara ya Kaliua Urambo kuongezewa muda tena karibu mwaka mzima ni lini ile barabara itakamilika kwa kiwango kinachotakiwa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara nyingine ni barabara inayoungasha Mkoa wa Tabora, na Katavi pamoja Shinyanga, barabara inayoanzia Katavi inakuja Kaliua inakwenda Uliyankulu inakwenda mpaka Kahama, barabara hii ni barabara muhimu sana kwa uchumi na pia ni barabara kuu ni barabara ambayo iko kwenye TANROADS, lakini kuna kilometa 60 kutoka Kangeme kwenda mpaka kilometa 120 kwa maana ya mpakani haijaguswa wala kufunguliwa kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri atuambie ni lini sasa kile kipande cha kilometa 60 kutoka Kangeme, kwenda mpaka pale mpakani mwa Katavi itafunguliwa? Kilometa 60 zingine zimefunguliwa, lakini barabara hii ni lini sasa itatengezwa kwa kiwango cha lami sababu ni barabara ya uchumi, barabara kuu, barabara ya Mkoa kati ya Mkoa na Mkoa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni suala la barabara zilizopo pale Kaliua Mjini ahadi Mheshimiwa Rais ambaye alituahidi wakati uchaguzi, pia ameahidi 2017 alifanya ziara Kaliua kwamba kilometa saba za pale Mjini zijengwe na aliagiza kwa haraka mpaka leo barabara hizo bado hazijajengwa. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa waziri atakapokuja ku-windup atuambie barabara za pale kilometa saba za pale Mjini zitajengwa lini?

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni suala la mitandao, maeneo mengi ya Kaliua tena maeneo ambayo yana uchumi mkubwa wa kilimo hayana mawasiliano ya simu hivi tunayoongea kuna watu wanapanda kwenye mti ili aongee hata aseme shida yake apande juu ya mti aongee ndiyo Mhehimiwa Mbunge aweze kupata shida yake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tuambiwe maeneo mbalimbali ya Kaliua yatapata mitandao ya simu lini? Mheshimiwa Waziri nimezungumza sana kwa habari ya maeneo haya, maeneo ya Pandamloka ambapo mchele mwingi unaolimwa Kahama unapatikana Pandamloka, hakuna mawasiliano ya simu, Pandamloka, Mwahalaja, Kombe, Shela, Maboha, Luenjomtoni, Usinga, Ukumbi Kakonko, Mkuyuni, Mpilipili, Igombe maeneo yote haya ni muhimu kwa uchumi, yanalima sana lakini kwa miaka yote kiukweli wanateseka.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana maeneo haya yaingie kwenye bajeti. Naomba tuambiwe sasa ni lini minara itajengwa maeneo yale ili wananchi wa Kaliua ambao wanalima sana, wanachi wa maeneo mengi ya nchi hii waweze kupata mawasiliano na waweze kuwa na huduma nyingine kama wananchi wengine? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi hii. Ahsante sana. (Makofi)
Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba Kigosi Kuwa Hifadhi ya Taifa Kigosi pamoja na Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji wa Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba la Igalla Kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki (Minamata Convention on Mercury)
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru pia kunipa nafasi ya kuweza kuchangia kwenye maazimio yaliyoko mbele yetu na nita- concentrate sana kwenye maazimio mawili, Maazimio ya Maliasili ambayo ni lile la kupandisha mapori ya Akiba mawili kwenye maeneo ya Tabora kuweza kuwa National Parks.

Mheshimiwa Mwenyekiti, dhamira kubwa ya maazimio haya natambua kabisa kwamba ni ya kuimarisha ulinzi wa maliasili zetu, lakini pia kufungua fursa za utalii kwenye maeneo ya Kanda ya Magharibi jinsi ambavyo tumekuwa na mkakati huo kuweza kupanua wigo wa utalii zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mapori mengi ya Mkoa wa Tabora yakiwepo haya ambayo yanaenda kuwa National Parks ikiwepo pia na mapori ya misitu mengi sana kutokana na kukosa ulinzi kwa miaka mingi iliyopita yalivamiwa na watu na baadaye baadhi ya maeneo vijiji vilisajiliwa kisheria na watu wakaendelea kuishi kule kisheria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kwa mfano eneo linaenda kuwa Ugalla National Park ambalo kilometa 2065 ambazo zitaungana na zile kilometa 1800 kuweza kuwa National Park hizi kilometa 2065 zinatoka kwenye Msitu wa Ugalla North na kwenye huu msitu wa Ugalla North ndiyo eneo ambalo Kaliua wananchi vijiji vitatu vimo mle ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kijiji cha Zugimlole ambacho kuna vitongoji vyake, Kijiji cha Uyumbu na Kijiji cha Igombe na mwaka 2017 hapa Bunge liliagiza Wizara kuweka mipaka ya maeneo ya hifadhi na wakaanza ule utaratibu wa kuanza kuweka mipaka, lakini hawakushirikisha wananchi, nilivyolalamika Bungeni hapa wananchi wenyewe, Wabunge wengi wanalalamika Bunge likaagiza zoezi lile lisitishwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mipaka ile ilikuwa imewekwa kwenye miji ya watu na hivi tunavyoongea sasa hivi yaani zile beacon ziko kwenye miji ya watu, kwa hiyo tunakwenda kupitisha azimio hili lakini kuna baadhi ya maeneo kwenye Ugalla North ambapo bado wananchi wapo mle ndani, lakini ukiangalia pia hata maeneo ya Kigosi kuna watu walikuwa wanafuga misitu huku nyuki, kitu ambacho ni friendly na mazingira na kwa taarifa za Mheshimiwa Waziri peke yake ni kwamba kuna watu wamefuga kwa muda mrefu na kwa mwaka jana tu kuna watu waliosajiliwa mle ndani, watu wameweza kuvuna tani 701 ambazo zina thamani ya shilingi bilioni saba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, lengo langu ni kwamba maeneo haya tunakwenda kuyapitisha kuwa National Park lakini bado kuna agizo la Rais pia ambalo aliagiza maeneo yote ambayo wananchi walikuwa wanabughudhiwa kwanza tutulie na akaunda Tume yake kuweza kuhakikisha kwamba maeneo haya yanapitiwa tuweze kupata majibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo langu naomba, pamoja na kuwa inaenda kupita, lakini lazima Wizara ituambie namna gani watu hawa ambao bado wako mle ndani watahakikisha kwamba waondolewa kiutaratibu ili wasibughudhiwe, kiukweli hatupendi maumivu haya yaendelee, hatupendi kabisa maumivu haya yaendelee kwa sababu ni kilio chetu cha muda mrefu na mpaka Mheshimiwa Rais amefikia hatua ya kuweza kuunda Tume anajua watu kabisa wako ndani ya Hifadhi, lakini waliingia baada ya kuwa mipaka ile ilikuwa pollars ilikuwa pia...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mimi naomba sana kwamba hilo liangaliwe, lengo letu ni kwamba kweli tuihifadhi kwa kupanua wigo wa utalii lakini pia wananchi wetu wasije wakateswa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaenda kuwapa pia TANAPA mzigo mkubwa sana kwa sababu tukianza....

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa.
Muswada wa Sheria ya Upatikanaji wa Habari wa Mwaka 2016
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa nafasi hii ya pekee nami niweze kuchangia kidogo kwenye muswada ulioko mbele yetu. Kabla sijaenda kwenye muswada naomba nitumie dakika zangu chache niwatoe wapiga kura wangu wasiwasi. Wapiga kura wangu wa Jimbo la Kaliua na wananchi wote wa Tanzania niwatoe wasiwasi kuwa taarifa ambazo zimetolewa kwenye media na kwenye mitandao ya kijamii kwamba Mbunge wao kasimamishwa Ubunge, hizo siyo taarifa za ukweli, ni taarifa za uzushi, ni propaganda waachane nazo. Mimi Mbunge wao Magdalena Sakaya niko hapa imara na ninawajibika kwenye majukumu ya kazi waliyonituma kwa uaminifu wa hali ya juu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, muswada uliopo mbele yetu inawezekana ulikuwa una malengo mazuri sana lakini malengo hayo mazuri hayawezi kufikiwa kwa namna ambavyo muswada huu umeandikwa. Ukiangalia kuanzia mwanzo wa muswada mpaka mwisho kuna milolongo mingi ambayo mingine unaona kabisa haina sababu, kwa hiyo, inawezekana ile tija halisi ambayo tulikuwa tunaitegemea isifikiwe kutokana na kwamba kuna milolongo na kiukweli ni urasimu mkubwa ambao hauna sababu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukipiga mahesabu ya kawaida kwa nini sasa hivi kwa Wizara ya Ardhi kwa mfano, kupata hati unachukua mwezi mmoja, kwa nini kupata taarifa ichukue karibu miezi mitatu? Wakati tunataka sasa hivi turahisishe mambo, twende kwa mwendo wa kisasa tuachane na kuishi kwa mazoea huku nyuma. Tunaomba ili muswada huu uweze kuwa na tija ni lazima kuhakikisha kwamba tunauandika kwa namna ambayo utakwenda kukidhi mahitaji na malengo yaliyotarajiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye kifungu cha 4(e) sheria inaweka kinga kwa wanaotoa taarifa njema zenye maslahi kwa Taifa. Ni kwa namna gani ningependa kujua sheria hii kuna watu ambao wamekuwa wanatoa taarifa mbalimbali kwenye taasisi mbalimbali kwa mfano taasisi zinazozuia uhalifu kwenye vyombo vya polisi, matokeo yake taarifa zile zinatolewa na watu wale wanadhuriwa maisha yao, wapo walipoteza maisha kwa sababu tu wametoa taarifa ambazo zina maslahi kwa Taifa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunamlindaje mtu kama huyu ambaye ametoa taarifa polisi au kwenye vyombo vya dola kwa nia njema ya kuokoa Taifa wanamzunguka wanaenda kutoa taarifa zile kwa wale ambao ni wahalifu wanakuja kumjeruhi au kujeruhi familia yake. Sheria hii ituambie watu kama hawa wanakwenda kulindwaje? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kwa wale ambao wanatoa taarifa za informers kwenye public, watu kama hao na wenyewe sheria hii inakwenda kuwaba namna gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kipengele cha 5(4) namna sheria pia inatoa fursa kwa mamlaka yoyote kutunga sheria itakayotaka mamlaka ya umma kutoa taarifa. Tunalo tatizo sugu sana, namna gani sheria hii wana-harmonize na Sheria ya Local Government. Kwa sababu tuna tatizo kubwa Sheria ya Serikali za Mitaa inasema kwamba lazima Serikali za Mitaa, Vijiji, Vitongoji, Kata mpaka Wilaya kila mwaka wawe na mikutano minne ya wananchi kutoa taarifa za mapato na matumizi, nchi nzima ni tatizo sugu. Taarifa hazitolewi, wananchi wanahoji hawaambiwi na bahati mbaya Mwenyekiti wa Kijiji na Mtendaji ndiyo wanatakiwa waitishe mikutano, kwa sababu wanaiba fedha za wananchi, wanakula hela za maendeleo, hawaitishi mikutano. Ningependa kujua sheria hii itawasaidijiaje wananchi kupata zile taarifa kwa wakati?(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kila baada ya miezi mitatu wahakikishe kwamba mikutano ya hadhara imekuwepo, wasomewe taarifa za mapato na matumizi, waambiwe fedha zao zimepatikana kiasi gani na zimetumikaje, halifanyiki. Kwa hiyo, ningependa sheria hii wa-harmonize na Sheria ya Local Government ili wananchi wale waweze kupata taarifa za maendeleo ya miradi yao na fedha wanazochanga kwa ajili ya shughuli zao za maendeleo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ni Kifungu cha 11, ukikiangalia kifungu hiki cha 11 kimeletwa muda mrefu sana, ni vigezo gani vimetumika kuweka siku 30 kwa nini tunaweka siku 30, kwa sababu kitendo cha kuweka muda mrefu kinaweka uwezekano wa taarifa ambayo ingepatikana kwa muda wa siku mbili kuchukua siku 30, ni kwa nini hakuna categorization?
Kwa hiyo, ningependa kwanza watuambie ni kwa nini wamefikia kuweka siku 30 na siyo siku chache labda mbili au wiki, inapolazimu ndiyo mtu asogezewe muda, kwa nini ni siku 30; kwa hiyo hilo nalo tunaomba tupatiwe ufafanuzi wa kutosha wakati Mheshimiwa Waziri Dkt. Mwakyembe anakuja kutujibu hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 11(3) mwombaji wa taarifa atathibitisha vipi kwa sababu kifungu hicho kinasema kwamba ikiwa mmiliki atathibitisha kwamba taarifa hiyo haipo, ningependa kujua mwombaji wa taarifa atathibitisha vipi kwamba kweli taarifa ile haipo na kwamba hajanyimwa? Kuna chombo gani kimeandaliwa kuweza kuhakikisha kwamba wanaomba taarifa wanatendewa haki. Maana yake ukiangalia sheria hii imemlinda sana mmiliki wa taarifa lakini yule anayeomba taarifa hajalindwa kwa lolote, sasa tungependa kujua nani anayethibitisha kwamba kweli taasisi fulani, taarifa inayotafutwa mle haipo. Kwa sababu mmiliki anasema haipo na wewe umeandika barua siku 30 unajibiwa haipo, nani anayethibitisha kwamba kiukweli taarifa hiyo haipo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 19 pale ambapo Mkuu wa Taasisi anakuwa ndiye mmiliki wa taarifa unaomba taarifa kwa Mkuu wa Taasisi na yeye mwenyewe ndiye mmiliki na anakataa kutoa, sheria inasema lazima ukate rufaa kwa Mheshimiwa Waziri. Naona hii ni kuendelea kuweka mlolongo wa mambo mengi, hivi Waziri atapokea taarifa za watu wangapi, atapata rufaa ngapi, kwa nini tusiweke sheria kumlazimisha mmiliki wa taarifa kuweza kutoa taarifa pale inapotakiwa kwa wakati? Kwa nini mpaka tuseme kwamba akikataa kutoa mmiliki twende kukata rufaa, Waziri ataacha ku-concentrate kwenye mambo mengine, tunaomba sheria hii imbane yule mmiliki wa taarifa ahakikishe kwamba anapotakiwa kutoa taarifa anaitoa na asipate loophole ya kuweza kukatalia taarifa zinazotakiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 20 kwenye version ya kiswahili inasema kwamba Waziri anaweza kutengeneza kanuni naomba itoke Waziri „anaweza‟; iseme Waziri atatengeneza kanuni nimeona kwenye version ya kiingereza ni nzuri „shall make’ lakini ukija kwenye kiswahili inasema Waziri anaweza, maana ya kusema kwamba anaweza au asiweze, ni option, asipewe option ni lazima atengeneze kanuni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 21, kinasema kwamba mmiliki wa taarifa kutoza ada iliyowekwa nani anaweka viwango vya ada kwa sababu kama mmiliki hataki taarifa itoke anaweza kuweka viwango vikubwa ili mhitaji wa taarifa ashindwe kumudu. Kwa hiyo, ni nani anayeweka viwango vya tozo za kuweza kupata taarifa zile lazima iwekwe wazi kwamba who is going to make this option kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tozo zitakazowekwa ziendane na hali halisi ili anayehitaji taarifa aweze kuzipata kwa gharama ambayo ni affordable kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kifungu cha 23, kinahusu kinga kwa mtoa taarifa. ukiangalia sheria yote hii, utaona kwamba mtoaji wa taarifa amelindwa sana kama nilivyotangulia kusema lakini muhitaji wa taarifa au mwombaji wa taarifa hajalindwa kwa lolote kwa maana nyingine ni kama vile unampa mtu haki kwa mkono wa kushoto, unaichukua kwa mkono wa kulia unaiweka mfukoni kwa muda wote haiwezi kupatikana hiyo haki. Kwa hiyo, ni lazima sheria ieleze kwamba mmiliki wa taarifa analazimika kutoa taarifa kwa muda unaotakiwa kwa viwango vinavyotakiwa, ili kweli malengo ya sheria hii yaweze kutekelezwa na yaweze kufikiwa kama kweli dhamira ni Watanzania wapate taarifa kwa ajili ya maendeleo yao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru.
Muswada wa Sheria ya Reli wa Mwaka 2017
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia kidogo kwenye muswada uliopo mbele yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nishukuru sana kwa namna ambavyo Serikali imeanza kuona umuhimu mkubwa wa kuboresha huduma za reli hapa nchini na hivyo kuweza kuja na muswada ambao utatunga sheria ya kuweza kusimamia masuala ua usafiri wa reli hapa nchi. Tukitambua kabisa kwamba reli ndio njia pekee ya uhakika ya usafiri wa mizigo hapa nchini lakini pia reli ndio njia pekee ya usafiri wa uhakika kwa wananchi wetu na hasa wale ambao ni maskini.

Mheshimiwa Naibu Spika, muswada huu ni muhimu sana, na kama ukitekelezwa vizuri nina imani kabisa utaenda kusaidia sana kwenye suala zima la usafiri hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaunganisha mashirika mawili sasa RAHCO pamoja na TRL tuweze kuwa na shirika moja kubwa. Ningependa kujua, kwanza wakati watumishi wa TRL wanahamia RAHCO wapo ambao mpaka leo hawajapata haki (stahiki) zao. Kwa hiyo, wakati mnaenda kuanzisha shirika jipya, je, stahiki za wale watumishi ambao walikuwa hawajalipwa mpaka leo wanaendelea kulalamika, zitalipwa kwa namna gani?

Mheshimiwa Naibu Spika, pia ukiangalia madhumuni ya muswada huu ni mazuri, moja wapo unaenda kulinda miundombinu lakini pia kwenda kuweka demarcation katika ya maeneo yetu. Tumekuwa na tatizo kubwa, na hapa niungane na Kamati pamoja na taarifa ambayo imesomwa na upande wa upinzani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wengi sasa hivi wanalalamika sana, wamejenga kwenye maeneo ambayo kwa miaka mingi hawakujua kwamba ni maeneo ya railway. Wengine walipewa mpaka hati kwenye maeneo hayo lakini leo wanakwenda kubomolewa. Suala lingine ni yale maeneo yanatofautiana kati ya eneo na eneo. Ukiangalia Mkoa wa Tabora, eneo la Tabora Mjini, eneo ambalo wanaambiwa ni hatua 80, ukija Kaliua ni hatua 120. Kwa hiyo, kiukweli ni wananchi wengi sana wataathirika. Tumekuwa tunauliza kwamba kwanini kuwepo na tofauti hii. Kama barabara ni mita 60 na tunategemea pia kuwa railway ambayo ni standard gauge lakini haiwezekani kutofautiana Tabora Mjini na Kaliua tofauti na Urambo tofauti.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na sheria hii inayokuja, tungependa tupate uhakika kwamba haswa upana wa reli ya standard gauge ambayo inategemewa kujengwa ni ya aina gani? Lakini pia wale wananchi ambao walikuwa wamejenga miaka mingi na leo wanaenda kubomolewa, nini watasaidiwa na Serikali?

Mheshimiwa Naibu Spika, hatukatai kuwepo na miundombinu hii lakini pia wananchi hawakatai pia kuhama yale maeneo lakini kiukweli kuna maeneo ambayo wengine wana hati na wanaambiwa kwamba wamejenga kwenye railway, ina maana hapo nyuma kulikuwepo na udhaifu mkubwa. Maeneo ya railway kwa kutokuwepo na alama za uhakika yaligawanywa na Wizara ya Ardhi, watu wakajenga lakini leo wananchi ambao ni innocent, walipewa hati wanakwenda kubomolewa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, pamoja na sheria hii tungependa Serikali iangalie wananchi ambao kiukweli si makosa yao na wakati huo kulikuwa hamna alama lakini leo wanakwenda kunyanyasika. Leo ukimbomolea mtu nyumba hana mahali pa kwenda, ndani ya Kaliua peke yake zaidi ya nyumba 200 zitabomolewa na wananchi ambao ni maskini hana uwezo hata wa kufanya chochote leo hapo alipo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwenye sheria ni ukweli kwamba Mkurugenzi tunaona anapewa mamlaka makubwa sana, kitu ambacho hakiwezekani, mpaka anaambiwa kwamba aweze kuteua kwa dharura na hivyo kutokufuata sheria za uteuzi wakati anapofanya kuweza kuteua mtu anaetakiwa kwenye nafasi maalum.

Mheshimiwa Naibu Spika, hapa tusiweke mwanya, lazima taratibu zifuatwe kwenye uteuzi, hakuna uharaka wa kumteua mtu ambaye anaenda kushughulikia suala ambalo ni la muhimu anakwenda kutumika kwenye kazi ambako ni husika kwa kutegemea dharura.

Mheshimiwa Naibu Spika, masuala ya dharura yamekuwa yanatuumiza sana, kwa hiyo, tunaomba mamlaka makubwa aliyopewa mkurugenzi yaondoke yaende kwenye bodi. Vilevile linapotokea suala la uteuzi sheria zifuatwe na si kuteua hivi hivi, tutajikuta tumeondoka kwenye lengo halisi la muswada huu na kuja kuweka watu ambao ni dhaifu au ku-create mwanya ambao utaleta utendaji ambao ni utendaji mbovu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni suala la nauli. Kwamba wamesema pia muswada utasimamia pia masuala ya nauli na masuala ya usafiri kwa ujumla. Sasa hivi tuna shida kubwa sana, na hii inatokana na kuwepo kwa uchache wa mabehewa. Tatizo la kuwepo kwa uchache wa mabehewa limesababisha wananchi wengi kushindwa kutumia usafiri wa reli.

Kwa hiyo ninaomba, pamoja muswada huu wa sheria pia suala la uwepo wa mabehewa ya kutosha liende sambamba, kwa sababu sasa hivi wananchi wengi wanalipa bei double. Kama nauli kutoka Kaliua kwenda Dar es Salaam shilingi 23,000 leo wanalipa mpaka shilingi 50,000 kutokana na kulinguliwa zile tiketi.

Kwa hiyo tunaomba kwanza mabehewa yawepo ya kutosha lakini pia utaratibu wa nauli uwe standard, ijulikane kabisakwamba nauli kutoka Kaliua kwenda Dodoma kiasi gani, kutoka Kaliua kwenda Dar es salaam ni kiasi gani ili kuondoa tabia za walanguzi kwenda kulangua tiketi na matokeo yake wananchi masikini wanaotaka kutumia barabara ya reli wanashindwa kutumia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia tulikuwa na maeneo ya magenge yaliyohusiana na suala la ulinzi wa barabara ya reli. Bila kuwepo kwa ulinzi wa uhakika hii miundombinu haiwezi kulindwa. Mwanzoni tulikuwa na magenge barabarani kwa ajili ya kulinda miundombinu ya barabara ya reli, leo yale yote yamekufa hakuna anaeyaangalia, vile vyuma vimepotea na watumishi waliokuwepo kule kwanza hawakulipwa haki zao waliondolewa lakini pia hakuna anayeangalia miundombinu hiyo sasa hivi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo sambamba na kuwepo kwa sheria hii pamoja na muswada huu, tunaomba pia wale wananchi ambao waliondolewa kwenye yale magenge, waliokuwa wanafanya kazi ya kulinda miundombinu ya reli na hawakulipwa na mpaka leo wapo mtaani kwanza wakapewe haki zao lakini pia magenge yale yaboreshwe ili miundombinu hii ambayo ni ya gharama kubwa sana iboreshwe na kulindwa ili iweze kuwepo leo, kesho na kesho kutwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana, naomba nirudie tena Serikali iangalie kwa namna ya pekee suala la wananchi ambao watabomolewa maeneo yao ili kupisha upanuzi wa barabara ya reli kwa kuwa wananchi wale kiukweli wana hali mbaya na vilio ni vingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli kama wataachwa kama ilivyo sasa hivi watateseka sana na mwisho wake wengine wataishia kupoteza maisha kwa sababu hawana namna ya kufanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, ahsante.
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 5) wa Mwaka 2017
MHE. MAGDALENA H SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru nami kunipa nafasi niweze kuchangia kidogo kwenye Muswada ulioko mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii sheria ya ardhi inayosema kwamba ardhi zinaweza kutolewa kama dhamana kwa ajili ya kupata mkopo kwa ajili ya kuendeleza imekuwa inatumika sana kwenye mashamba makubwa. Kwa Tanzania ardhi ambayo zina hati kabisa benki hazikubali kutoa mikopo kama hakujaendelezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa sheria ipo na 120A; kwa nini mabenki yanakataa kutoa fedha mikopo kwa kutumia viwanja (plots) ambazo tayari zina hati na mpaka viendelezwe, lakini kwa mashamba ambayo hayajaendelezwa wanatoa tena fedha ambazo ni nyingi. Kwa hiyo ningependa kwanza sheria hii ambayo ipo 120A iweze kutekeleza benki zikubali hati na kutoa fedha ili wananchi waweze kuendeleza yale maeneo kwa ajili ya maisha ya watoto wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini, tumekuwa na mapori mengi sana Tanzania ambapo ukiyafuatilia mengi unakuta ni mapori kwa sababu fedha ilichukuliwa kweli ilienda kuendeleza maeneo mengine. Nakubaliana na Serikari kwamba mashamba ambayo yalichukuliwa hati, ilichukuliwa mikopo, mikopo itumike kwa ajili ya kuendeleza maeneo ya pale pale kwa sababu sasa hivi mapori ni makubwa kwa sababu fedha ilichukuliwa na watu wengine pengine hata wako nje ya nchi lakini mapori yako pale fedha inafanya kazi maeneo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa swali ya kujiuliza, kuna baadhi ya mapori ambayo yameshindwa hata kufuta zile hati kwa sababu benki zinadai. Sasa atakapokuja ku-wind up Mheshimiwa Waziri hapa atuambie; yale mashamba ambapo tayari benki zinadai na wameshindwa kufuta hati kwa sababu zinadaiwa hatima yake ni nini. Yataendelea kuwa ni mapori au Serikali inafanyaje, au italipa sasa mikopo kwa benki zile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ni suala la kuongeza mmekuja na Muswada hapa wa utumishi kuongeza miaka kwa ajili ya wahadhiri, madakatari, proffesors na watu wengine. Tunafanya hivi kwa sababu hatuna watu wa kutosha ku-fit nafasi hizo kwa wakati huo. Nina imani aliyeweka miaka 60 compulsory kuweza kustaafu alifanya utafiti wa kutosha. Kwa mtu unayefanya kazi kwa kujituma kwa miaka 60 kwa mazingira ya Tanzania unakuwa umechoka, kiukweli kabisa; unahitaji upate muda wa kufanya yale mambo yako mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunapoongeza muda mpaka miaka 65 are we sure kwamba hawa watu wako tayari kufika huko? Tunahitaji ufanisi kwenye utendaji. Kwa hiyo, nadhani tungekuja na mpango ambao utakuwa na ufanisi zaidi kuliko kuongeza miaka, anaweza akawepo tu kwa sababu kuna mkataba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maprofesa wengine wakifika miaka 55 wameshachoka. Wana elimu yao ya kutosha, wameshawekeza wangependa watoke nje ya utumishi, lakini kwa kuwa tunawahitaji kama Serikali wanalazimika kukaa kwenye utumishi. Kwa hiyo, naomba Serikali tuwe na succession plan katika kuhakikisha kwamba tuna watu kwenye nafasi hizo. Tuhakikishe kwamba kila mwaka tunajua wanaostaafu ni kiasi kadhaa ili tuweze kuwa na mpango wa ku-cover zile nafasi zao. Kwa hiyo hata tulicholetewa leo ni mpango wa muda mfupi, ni miaka 65 baada ya hapo je? Bado shida iko pale pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kwenye hili la watumishi lazima Serikali ije na succession plan ya namna wahadhiri wanapostaafu nafasi zao zinakuwa covered na wale madaktari bingwa. Leo ukianza ku-compare daktari bingwa wa Tanzania na wa Zimbabwe au Zambia ni tofauti kabisa. Daktari wa Ulaya anahudumia watu 15 mpaka 25 kwa siku, daktari bingwa wa Tanzania watu 40 mpaka 100, definetely atakuwa amechoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mazingira ni tofauti, utumishi ni tofauti, posho ni tofauti. Lazima mazingira yetu tuyaangalie na tuwaangalie watu wetu, tuweze kuhakikisha kwamba tunawapa package ya kutosha wafanye kazi vizuri kwa ajili ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.
Muswada wa Sheria ya Bodi ya Kitaalam ya Walimu Tanzania wa Mwaka 2018
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami pia nikushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuchangia Muswada ambao uko mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuwepo kwa chombo hiki cha kudhibiti taaluma za walimu binafsi naona siyo tatizo. Tatizo kubwa ambalo naliona mimi ni kuwepo kwa vyombo vingi vinavyozungumzia masuala ya walimu na kusababisha mzigo kwa walimu kwa sababu, ukiangalia kila chombo kinachoanzishwa lazima mwalimu anatakiwa alipe ada, kwa hiyo, hilo ndio tatizo kubwa. Kwa hiyo, kila kinachoanzishwa lazima mwalimu ahusike, ndiyo maana Wabunge wengi wanasema kwamba, angalau tuwe na vyombo vichache ambavyo vitaangalia masuala yote kwa pamoja ili mwalimu awe amepunguziwa mzigo mkubwa. Tatizo kubwa hapa ni kwa nini kunakuwepo na vyombo vingi vya masuala ya walimu? Kwa nini tusiwe na chombo kimoja ambacho ni imara, very strong, cha kuweza ku-accomodate masuala yote ya walimu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Muswada huu ambao uko mbele yetu kuna masuala mengi ambayo yanaingiliana sana. Ukiangalia majukumu ya Tume ya Walimu pamoja na ya Bodi hii inayoanzishwa kuna masuala kwa mfano, Bodi inasajili na Tume inasajili; Bodi inatoa namba ya usajili, Tume na yenyewe pia inatoa namba ya usajili; Bodi inaadhibu, Tume na yenyewe inaadhibu. Sasa swali la kujiuliza hii sheria ikipita hapa ikisainiwa tayari inakuwa ni sheria, wakati huohuo Tume inaendelea na kazi zake kama kawaida. Swali la kujiuliza je, nani atakaye-step down? Nani atakayeacha kufanya shughuli zake maana Tume itakuwa inafanya shughuli zake kama kawaida wakati huohuo na Bodi imeshasajiliwa iko kisheria inaanza kufanya kazi zake? Kwa hiyo, kuna mwingiliano, Mheshimiwa Waziri atufafanulie atakapokuja ku-wind up, kwenye masuala haya yanayoingiliana baada ya Muswada kupita kuwa sheria haya masuala yatakuwaje kwenye utekelezaji wake? Hilo ni suala ambalo tungependa kupata ufafanuzi baadaye wakati wa ku-wind up. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia zipo taarifa kwamba, kuna utaratibu mpya umekuja kwa ajili ya kupandisha madaraja ya ualimu. Kwa taarifa ambazo tumezipata ni kwamba, sasa hivi utaratibu utakuwa siyo kwa kufuata miaka aliyoajiriwa mtumishi, utakuwa kwa kuangalia utendaji wake, nidhamu kazini na mambo kama hayo. Sasa wakati utaratibu huu unakuja walimu wana malalamiko ya muda mrefu, ya miaka mingi, wanafanya kazi bila kupandishwa madaraja zaidi ya miaka 10. Wengine wameenda kusoma walikuwa Diploma level, wameingia Degree level, wako palepale. Wengine walikuwa Certificate ana Diploma yuko palepale. Mwingine ameenda kusoma alikuwa na Degree ameenda Masters yuko palepale. Badala ya kuwapandisha kwanza tunaleta tena utaratibu mwingine kwamba, tutakuwa tunawapima kwa kuangalia uwajibikaji, nidhamu na mambo kama hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kweli hili ni sahihi na tunaamua kwamba sasa utaratibu wa walimu wa kuwapa madaraja itakuwa ni hisani ya mtu anayemsimamia kazi, nina imani kabisa wapo walimu ambao hawatakaa wapandishwe madaraja kabisa kwa sababu, ni hisani ya mtu. Nayekupima kwamba unafaa kupandishwa au haufai ni mimi Sakaya, mpaka ukidhi vigezo ambavyo navitaka ni hisani yangu. Naomba kama utaratibu huu kweli upo lazima Serikali iangalie mara mbili-mbili. Jamani walimu hawa ni fani muhimu mno, ni daraja muhimu mno, lakini mambo tunayowawekea inakatisha tamaa. Leo tusingekuwa hapa kama siyo walimu, lakini kila kitu mwalimu ni shida. Kwa hiyo, kama hilo lipo naomba Serikali itoe macho zaidi ya mawili kwenye sekta ya ualimu, walimu wapewe moyo, wawe promoted kwa wakati, tuweke utaratibu ambao kila mwalimu atapanda kwa wakati wake na siyo kwa ajili ya hisani ya mtu, itakuwa ni shida kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine, nikienda kwenye Muswada sasa kifungu cha 29, kinasema kwamba, mtu hatafanya kazi yoyote ya ualimu au kuajiriwa mpaka awe registered. Swali ambalo naomba kuuliza nipatiwe majibu, wakati mwingine watoto wetu wa form six na form four wanapokuwa wamemaliza shule wanasubiri kwenda vyuoni wanakwenda kujitolea kwenye shule ambazo hatuna walimu labda wa sayansi, jografia au historia, wanatumia ule muda wao wa kupumzika nyumbani kwenda kujitolea shuleni kusaidia wadogo zao na walikuwa wanasaidia sana. Sasa naomba kujua, baada ya sheria hii kupita hawa waliokuwa wanajitolea wakati mwingine bure kabisa, wakati mwingine walimu wale wanawaangalia kutoka kwenye mifuko yao au wazazi wanawaangalia, je, huu utaratibu huu umekufa au utaendelea kuwepo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wapo pia wanafunzi ambao wanamaliza form four shule shikizi kama Kaliua na maeneo mengine. Wale walikuwa wanachukua watoto ambao wamemaliza form four wanasaidia kutoa elimu maeneo ambapo hakuna walimu, wazazi wamejenga shule zao wenyewe na kwa kweli wamesaidia maana maeneo yale ilikuwa hakuna kusoma, mtoto hasomi kabisa, lakini leo wamewasaidia watoto wale wanasoma, kwa elimu yao ya form four wanawasaidia watoto wale na baadaye wanakua wanakwenda shule za kawaida ambazo ni shule za Serikali. Naomba kujua kwa sheria hii sasa, je, wale walimu waliokuwa wanajitolea hata kwenye zile shule shikizi za
primary ambapo ni baby class na darasa la kwanza na la pili, hawataweza kufanya kazi hii tena au itakuwaje? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine nikienda tena kwenye kifungu cha 35, kinazungumzia kuhusu Bodi kufuta usajili. Bodi inaweza kutoa jina kwenye usajili, wameweka mambo mengi pale, lakini naomba nizungumzie suala lile la kwanza tu ambalo linasema kama atashindwa kulipa ada.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshazungumzia kwamba, kwanza walimu wana mzigo mkubwa. Kwa hiyo, naomba hiki kifungu kiangaliwe, ameshindwa kulipa ada kwa muda gani? Je, kuna sababu ya msingi imemfanya ashindwe kulipa ada? Je, alikuwa mgonjwa au anauguliwa? Naomba kifungu hiki pia kiseme kushindwa kulipa ada kwa muda kadhaa na kwa sababu ambazo hazina msingi, lakini tukisema tu kwamba, ameshindwa kulipa ada halafu ndiyo anaondolewa kwenye usajili, hili ni tatizo. Haya mengine nakubaliana nayo, lakini hili la kwanza ni lazima tuweke muda, kama hiki kifungu cha 37 ambacho kimesema angalau mtu anapewa miezi 12, ilivyo hivi ni kwamba akipitiliza hata mwezi mmoja tayari anafutiwa kwa sababu, anaweza akawa na sababu. Kwa hiyo, naomba hili liwekewe consideration kwamba uwepo muda maalum kuhakikisha huyu mwalimu aliyeshindwa kulipa ada na ufanywe uchunguzi wa kutosha kwa nini ameshindwa kulipa ada, ameuguliwa, anaumwa au ana sababu zipi za msingi ambazo zimemfanya kushindwa kulipa ada kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kile kifungu cha 43, kinahusu Bodi ya ku-appoint committee ambayo itakuwa inashughulikia masuala ya hii Bodi. Ningeomba kabisa kwenye sheria tuone gender hapa, tuone wanawake. Kati ya wale watano lazima tuseme at least wawili wawe wanawake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka kila sheria inayopita hapa Bungeni, iwe ni bodi, iwe ni kamati, iwe ni chochote, lazima jicho la mwanamke lionekane. Kwa hiyo, naanza kwenye kamati hii na kwenye ile Bodi inayoundwa lazima at least kati ya watu watano walioko hapa kwenye hii kamati itakayoundwa wawili wao wawe wanawake na iwe kwenye sheria, siyo kwenye regulations. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni kifungu cha 52 cha kuruhusu hii Bodi kuweza kukopa. Nakubaliana na Kamati kabisa kwamba haiwezekani Bodi ikaanze kukopa kwa discretion zao wenyewe, lazima kiwepo chombo kingine kinachodhibiti hata kama ni Waziri, consultations ziwepo na kuwepo mtu anayeruhusu, waombe kibali cha kuweza kukopa. Vinginevyo walimu watabambikiwa madeni makubwa, wataambiwa walipe kwa sababu Bodi inakwenda kukopa kwa niaba ya walimu. Kwa hiyo, kama hawajapata idhini, wakajikopea wanavyotaka tu, leo tutakuja kushangaa kwamba walimu hawa ambao wameundiwa hiki chombo itakuwa kwao ni maumivu zaidi ya kunufaika na chombo hiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maoni yangu ni hayo machache, nakushukuru sana.
Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania wa Mwaka 2018
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia kidogo kwenye Miswada hii miwili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, muda ni mdogo sana na kiukweli kwa kuwa Bunge ni chombo cha kutunga sheria, Miswada muhimu kama hii imepewe muda wa kutosha. Dakika kumi na tano kwa Miswada miwili naona kama Bunge hatupati muda wa kutosha kutunga sheria ambazo zitakuwa nzuri na kwa ajili ya kutumia kwa muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianza na huu Muswada wa kuunda Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini, siku za nyuma tumekuwa tukilalamika sana kuhusiana na suala la bodaboda kusababisha ajali nyingi sana barabarani, kiukweli japokuwa hapa sheria imezungumza kwamba ni habari ya mabasi na mabasi makubwa, lakini sasa hivi ajali nyingi barabarani, karibu hata kwenye asilimia sabini au sitini zinasababishwa na bodaboda kutokufuata sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujua hii sheria inawezaje kusaidia bodaboda waweze kufuata sheria barabarani? Bodaboda hawajui sheria kabisa, wana- overtake kushoto badala ya kulia, kwenye traffic light taa nyekundu inawaka wanatembea na nimeuliza swali hapa Bungeni na wakasema kwamba wanaleta sheria, lakini nimeangalia sheria hii sijaona mahali hapo imeeleza kudhibiti motorcycle barabarani waweze kufuata sheria na kupunguza ajali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi tunavyoongea bodaboda wanabeba watoto wa shule mpaka wanne/ watano wakipata ajali wanapota wote. Bunge lilipitisha sheria bodaboda zitumike kwa maana ya mizigo na abiria kwa maana ya kutoa ajira kwa vijana lakini sasa hivi imekuwa ni kinyume chake, wanaopoteza maisha ni wengi. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri anapokuja ku-windup atusaidie namna gani sheria hii inaweza kusaidia bodaboda wafuate sheria na kuweza kuokoa maisha ya watu yanayopotea barabarani kila kukicha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni ukaguzi. Tulipenda sana tulipoonyeshwa ile mizani pale Vigwaza kwa sababu tuliambiwa ni digital na itakuwa fast lakini ukiangalia muda mwingi sana unapotelea kwenye mabasi wanavyoingia kwenye mizani. Kwa hiyo, japokuwa kunajengwa mizani za kisasa lakini bado hazifanyi kazi kwa speed inayotakiwa. Kwa hiyo, pale muda unaopotelea kwenye mizani kukagua magari wanakwenda kufidia barabarani matokeo yake wanasababisha ajali. Kwa hiyo, ni namna gani mizani zetu ambazo zimejengwa na zinaendelea kujengwa zinaweza kufanya kazi kwa speed kama mizani za nchi za nje ili muda uweze kuokolewa, watu wafike kwa wakati na pia madereva wasiongeze mwendo barabarani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la ukaguzi wa magari. Tumeshuhudia kipindi cha sikukuu Polisi wanakagua magari wakati abiria tayari wako kwenye mabasi, muda mwingi unapotea na kusababisha watu kusafiri mpaka usiku. Sheria inatusaidiaje ukaguzi wa magari ufanyike siku moja kabla ya safari, kwa sababu ukaguzi ni kazi ya kila siku lakini kwa maana ya ukaguzi mkubwa ufanyike siku moja kabla ya safari tofauti na kwamba leo ni asubuhi saa kumi na mbili ndiyo pale stand Askari wametinga wanakagua muda mwingi unapotelea pale matokeo yake watu wanachelewa safari zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine pia ameliongelea Mheshimiwa Mbatia kwa kiasi kidogo. Tunapenda sheria iweze kuainisha Mamlaka hii ya LATRA na Mamlaka ya Polisi. Ijulikane kabisa LATRA wanafanya sehemu gani na Polisi wanafanya sehemu gani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tumekuwa tunalalamika suala la Polisi barabarani kusimamisha magari barabarani kwa ajili ya ukaguzi, unakuta msururu mkubwa, hakuna maeneo ya kufanyia ukaguzi. Kwa hiyo, Polisi akiamua tu anasimamisha gari barabarani, matokeo yake kama juzi kuamkia jana nilipokuwa nakuja, barabara ya Morogoro nimekuta magari karibu 15 yako barabarani yanakaguliwa, pale kwanza muda unapotea mwingi lakini pia siyo sehemu sahihi. Kwa hiyo, nashauri ukaguzi ufanyike maeneo ambapo ni sahihi kuweza kuokoa muda, lakini pia kuweza kuepusha ajali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niingie kwenye Muswada wa Mamlaka ya Hali ya Hewa, kwanza nishukuru huu Muswada ni muhimu sana kwa sababu kwa nchi za wenzetu huwezi kutoka nyumbani kwako asubuhi kabla hujaangalia Mamlaka ya Hali ya Hewa inasemaje siku hiyo. Ili kuboresha Mamlaka ya Hali ya Hewa kwa nchi yetu ili iweze kutoa takwimu sahihi na iweze kutoa taarifa kwa wakati ni kwanza kwa maendeleo ya nchi lakini pia kwa miradi mbalimbali. Leo wakulima wetu wa Tanzania tunalima kwa kubahatisha hujui mvua itanyesha au hainyeshi, lakini tukiwa na Mamlaka nzuri na ambayo ni efficiency itaweza kutoa takwimu sahihi ili mkulima alime kwa tija, ajue muda gani wa kulima, muda wa kupanda na hata muda wa kuvuna.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata wavuvi, tumeshuhudia kwamba watu wanapata ajali baharini kutokana na Mamlaka kutowaambia leo hali ya hewa ikoje baharani. Kwa hiyo, nafurahi kwamba Mamlaka hii ikiweza kuboreshwa itaweza kufanya kazi kwa ufanisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachoomba itolewe elimu ya kutosha kwa Watanzania wote. Kiukweli watu wachache sana wanatumia Mamlaka ya Hali ya Hewa. Kwa hiyo, lazima pia sheria hii ijielekeze kutoa elimu kwa Watanzania tuweze kutumia Mamlaka ya Hali ya Hewa lakini ni kama taarifa zake zitakuwa sahihi na zitatolewa pia kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa jumla sheria zote mbili lazima gender izingatiwe, wasemaji wengine wamezungumzia, kila bodi inayoundwa at least wanawake watatu wawepo kwenye hizo bodi maana hawaja-specify. Naomba iwepo kwenye sheria kwa kila bodi inayoundwa lazima wanawake wawepo siyo chini ya watatu kuhakikisha kwamba tumezingatia gender balance.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la adhabu. Kiukweli Miswada yote hii miwili imeweka adhabu kubwa sana, shilingi milioni hamsini na kifungo miaka mitano. Lengo la adhabu ni kurekebisha lakini hiyo adhabu ya shilingi milioni 50 kwa mtu ambaye amekiuka ni kubwa sana kiasi kwamba inakuwa ni mateso na siyo adhabu tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafurahi kwamba hii Sheria ya kuanzisha Mamlaka ya Hali ya Hewa imehusisha watu wengine wa nje na Serikali kwa maana ya kuweka private sectors. Sheria pia inasema pale ambapo vifaa vya meteorological vitakavyokuwepo lazima viwe examined na Mamlaka hiyo yenyewe. Kwa kuwa mmeamua private sector washiriki na nchi zote zimeweka private sector kwenye masuala yote ya maendeleo, lakini kusiwepo na urasimu. Ni lazima basi kuwe na vituo vya kutosha kwenye Mikoa na Wilaya ili pale ambapo mtu ametaka labda kuingiza vifaa vya meteorological aweze kukaguliwa kwa muda unaotakiwa. Mkiweka one stop center labda mamlaka ya kukagua iko Dar es Salaam halafu mtu yuko Arusha au Tabora, yuko mbali na Dar es Salaam itakuwa ni urasimu kwa maana kwamba hawataweza kufanya kazi kwa wakati kutokana na urasimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa private sector wanafanya kazi kwa wakati na wengi ni wafanyabiashara basi kuwepo na kurahisishwa namna ya kuweza kukagua vifaa hivi. Kiukweli lazima viweze kudhibitiwa ili tuhakikishe tunatumia vifaa ambavyo vimetathminiwa na kwamba vina ubora wa kutosha lakini kusiwepo na urasimu wowote ili hao wanaojiunga kusaidia Taifa letu kwa ajili ya masuala ya hali ya hewa wafanye kazi kwa wakati na kuleta tija kwa Taifa letu na kwa nchi nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.
Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Ardhini wa Mwaka 2018
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia kidogo kwenye Miswada hii miwili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, muda ni mdogo sana na kiukweli kwa kuwa Bunge ni chombo cha kutunga sheria, Miswada muhimu kama hii imepewe muda wa kutosha. Dakika kumi na tano kwa Miswada miwili naona kama Bunge hatupati muda wa kutosha kutunga sheria ambazo zitakuwa nzuri na kwa ajili ya kutumia kwa muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianza na huu Muswada wa kuunda Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini, siku za nyuma tumekuwa tukilalamika sana kuhusiana na suala la bodaboda kusababisha ajali nyingi sana barabarani, kiukweli japokuwa hapa sheria imezungumza kwamba ni habari ya mabasi na mabasi makubwa, lakini sasa hivi ajali nyingi barabarani, karibu hata kwenye asilimia sabini au sitini zinasababishwa na bodaboda kutokufuata sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujua hii sheria inawezaje kusaidia bodaboda waweze kufuata sheria barabarani? Bodaboda hawajui sheria kabisa, wana- overtake kushoto badala ya kulia, kwenye traffic light taa nyekundu inawaka wanatembea na nimeuliza swali hapa Bungeni na wakasema kwamba wanaleta sheria, lakini nimeangalia sheria hii sijaona mahali hapo imeeleza kudhibiti motorcycle barabarani waweze kufuata sheria na kupunguza ajali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi tunavyoongea bodaboda wanabeba watoto wa shule mpaka wanne/ watano wakipata ajali wanapota wote. Bunge lilipitisha sheria bodaboda zitumike kwa maana ya mizigo na abiria kwa maana ya kutoa ajira kwa vijana lakini sasa hivi imekuwa ni kinyume chake, wanaopoteza maisha ni wengi. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri anapokuja ku-windup atusaidie namna gani sheria hii inaweza kusaidia bodaboda wafuate sheria na kuweza kuokoa maisha ya watu yanayopotea barabarani kila kukicha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni ukaguzi. Tulipenda sana tulipoonyeshwa ile mizani pale Vigwaza kwa sababu tuliambiwa ni digital na itakuwa fast lakini ukiangalia muda mwingi sana unapotelea kwenye mabasi wanavyoingia kwenye mizani. Kwa hiyo, japokuwa kunajengwa mizani za kisasa lakini bado hazifanyi kazi kwa speed inayotakiwa. Kwa hiyo, pale muda unaopotelea kwenye mizani kukagua magari wanakwenda kufidia barabarani matokeo yake wanasababisha ajali. Kwa hiyo, ni namna gani mizani zetu ambazo zimejengwa na zinaendelea kujengwa zinaweza kufanya kazi kwa speed kama mizani za nchi za nje ili muda uweze kuokolewa, watu wafike kwa wakati na pia madereva wasiongeze mwendo barabarani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la ukaguzi wa magari. Tumeshuhudia kipindi cha sikukuu Polisi wanakagua magari wakati abiria tayari wako kwenye mabasi, muda mwingi unapotea na kusababisha watu kusafiri mpaka usiku. Sheria inatusaidiaje ukaguzi wa magari ufanyike siku moja kabla ya safari, kwa sababu ukaguzi ni kazi ya kila siku lakini kwa maana ya ukaguzi mkubwa ufanyike siku moja kabla ya safari tofauti na kwamba leo ni asubuhi saa kumi na mbili ndiyo pale stand Askari wametinga wanakagua muda mwingi unapotelea pale matokeo yake watu wanachelewa safari zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine pia ameliongelea Mheshimiwa Mbatia kwa kiasi kidogo. Tunapenda sheria iweze kuainisha Mamlaka hii ya LATRA na Mamlaka ya Polisi. Ijulikane kabisa LATRA wanafanya sehemu gani na Polisi wanafanya sehemu gani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tumekuwa tunalalamika suala la Polisi barabarani kusimamisha magari barabarani kwa ajili ya ukaguzi, unakuta msururu mkubwa, hakuna maeneo ya kufanyia ukaguzi. Kwa hiyo, Polisi akiamua tu anasimamisha gari barabarani, matokeo yake kama juzi kuamkia jana nilipokuwa nakuja, barabara ya Morogoro nimekuta magari karibu 15 yako barabarani yanakaguliwa, pale kwanza muda unapotea mwingi lakini pia siyo sehemu sahihi. Kwa hiyo, nashauri ukaguzi ufanyike maeneo ambapo ni sahihi kuweza kuokoa muda, lakini pia kuweza kuepusha ajali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niingie kwenye Muswada wa Mamlaka ya Hali ya Hewa, kwanza nishukuru huu Muswada ni muhimu sana kwa sababu kwa nchi za wenzetu huwezi kutoka nyumbani kwako asubuhi kabla hujaangalia Mamlaka ya Hali ya Hewa inasemaje siku hiyo. Ili kuboresha Mamlaka ya Hali ya Hewa kwa nchi yetu ili iweze kutoa takwimu sahihi na iweze kutoa taarifa kwa wakati ni kwanza kwa maendeleo ya nchi lakini pia kwa miradi mbalimbali. Leo wakulima wetu wa Tanzania tunalima kwa kubahatisha hujui mvua itanyesha au hainyeshi, lakini tukiwa na Mamlaka nzuri na ambayo ni efficiency itaweza kutoa takwimu sahihi ili mkulima alime kwa tija, ajue muda gani wa kulima, muda wa kupanda na hata muda wa kuvuna.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata wavuvi, tumeshuhudia kwamba watu wanapata ajali baharini kutokana na Mamlaka kutowaambia leo hali ya hewa ikoje baharani. Kwa hiyo, nafurahi kwamba Mamlaka hii ikiweza kuboreshwa itaweza kufanya kazi kwa ufanisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachoomba itolewe elimu ya kutosha kwa Watanzania wote. Kiukweli watu wachache sana wanatumia Mamlaka ya Hali ya Hewa. Kwa hiyo, lazima pia sheria hii ijielekeze kutoa elimu kwa Watanzania tuweze kutumia Mamlaka ya Hali ya Hewa lakini ni kama taarifa zake zitakuwa sahihi na zitatolewa pia kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa jumla sheria zote mbili lazima gender izingatiwe, wasemaji wengine wamezungumzia, kila bodi inayoundwa at least wanawake watatu wawepo kwenye hizo bodi maana hawaja-specify. Naomba iwepo kwenye sheria kwa kila bodi inayoundwa lazima wanawake wawepo siyo chini ya watatu kuhakikisha kwamba tumezingatia gender balance.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la adhabu. Kiukweli Miswada yote hii miwili imeweka adhabu kubwa sana, shilingi milioni hamsini na kifungo miaka mitano. Lengo la adhabu ni kurekebisha lakini hiyo adhabu ya shilingi milioni 50 kwa mtu ambaye amekiuka ni kubwa sana kiasi kwamba inakuwa ni mateso na siyo adhabu tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafurahi kwamba hii Sheria ya kuanzisha Mamlaka ya Hali ya Hewa imehusisha watu wengine wa nje na Serikali kwa maana ya kuweka private sectors. Sheria pia inasema pale ambapo vifaa vya meteorological vitakavyokuwepo lazima viwe examined na Mamlaka hiyo yenyewe. Kwa kuwa mmeamua private sector washiriki na nchi zote zimeweka private sector kwenye masuala yote ya maendeleo, lakini kusiwepo na urasimu. Ni lazima basi kuwe na vituo vya kutosha kwenye Mikoa na Wilaya ili pale ambapo mtu ametaka labda kuingiza vifaa vya meteorological aweze kukaguliwa kwa muda unaotakiwa. Mkiweka one stop center labda mamlaka ya kukagua iko Dar es Salaam halafu mtu yuko Arusha au Tabora, yuko mbali na Dar es Salaam itakuwa ni urasimu kwa maana kwamba hawataweza kufanya kazi kwa wakati kutokana na urasimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa private sector wanafanya kazi kwa wakati na wengi ni wafanyabiashara basi kuwepo na kurahisishwa namna ya kuweza kukagua vifaa hivi. Kiukweli lazima viweze kudhibitiwa ili tuhakikishe tunatumia vifaa ambavyo vimetathminiwa na kwamba vina ubora wa kutosha lakini kusiwepo na urasimu wowote ili hao wanaojiunga kusaidia Taifa letu kwa ajili ya masuala ya hali ya hewa wafanye kazi kwa wakati na kuleta tija kwa Taifa letu na kwa nchi nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.