Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Bahati Ali Abeid (1 total)

MHE. BAHATI ALI ABEID: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo hili la fistula wanawake wanapolipata, huwa wanatumia pesa nyingi ili kupona. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kwa wanawake wanaopata tatizo hili wakatibiwa bure?
WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii. Nimshukuru sana Mheshimiwa Bahati Abeid, Mbunge wa Jimbo la Mahonda kwa swali lake zuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, sera yetu ya afya inasema mwanamke mjamzito ndiye anatakiwa kupata matibabu bure; na huduma hizi za fistula especially suala la upasuaji zinafanyika baada ya siku 40 baada ya mwanamke kujifungua. Kwa hiyo, niseme tu tumelibeba. Naomba nilipokee, haliko kisera, lakini kwa sababu kama unavyosema ni jambo ambalo linawaathiri wanawake wengi hasa wa vijijini, nitashauriana na wenzangu tuone ni jinsi gani tutatoa matibabu bure kwa wagonjwa wa fistula. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naishukuru sana Hospitali ya CCBRT, wao wanatoa matibabu bure kwa wagonjwa wa fistula. Kwa hiyo, ni changamoto kwetu sisi wa Serikali pia kuhakikisha kwamba na matibabu hayo bure ya fistula yanapatikana katika Hospitali za Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto kubwa ni kwamba ule upasuaji unachukua saa sita na daktari anatakiwa ainame kwa saa sita.
Kwa hiyo, tutaangalia ni jinsi gani tutakuja na incentive package ya jinsi gani ya kutoa motisha kwa Madaktari wetu bingwa wa magonjwa ya akina mama kuwafanyia matibabu haya bure badala ya kulipia, lakini nawashakuru sana CCBRT.