Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Amb. Adadi Mohamed Rajabu (68 total)

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Spika, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa leo kuniweka hapa.
Pili, ningependa kuwashukuru Wanamuheza ambao wakati wa kampeni niliwaomba wanilete kwenye jengo hili na wamenileta, nawashukuru sana tena sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono Hotuba ya Mheshimiwa Rais moja kwa moja kwa asilimia mia moja. Mheshimiwa Rais kwenye hotuba hiyo ameainisha mambo chungu nzima; nilikuwa nasoma mstari kwa mstari na nilikuwa na-underline, nilipofika mwisho wa kitabu
nikakuta nime-underline mistari yote kwenye kitabu hicho. Kwa sababu kila point, kila mstari ambao nilikuwa nauona, niliuona ni wa msingi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hotuba hiyo, lakini ningewaomba Waheshimiwa Wabunge waangalie namna Mheshimiwa Rais alivyokuwa anai-present hotuba hiyo, seriousness aliyokuwa nayo, commitment aliyokuwa nayo siku ambayo alikuwa anaiwasilisha hotuba hiyo na baada ya hapo matendo yake baada ya hiyo hotuba! Jamani mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais ameainisha matatizo ambayo sijui ameacha tatizo gani kwenye hii hotuba. Ameanzia na huduma za jamii, matatizo yote yapo pale, matatizo ya maji, umeme, barabara, kila kitu kiko pale. Tatizo moja kubwa sana ambalo wote
humu Waheshimiwa Wabunge tunalo, isipokuwa wananchi wa Muheza wanalo zaidi ni la maji.
Wanamuheza wana shida ya maji! Yapo matatizo ya umeme, lakini umeme umefanyiwa kazi kubwa sana, REA imefanya kazi kubwa sana! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba Serikali iangalie uwezekano, utaratibu ambao umetumika kwa REA, utaratibu huo utumike kwa maji vijijini. Wananchi wana taabu, sikupata nafasi ya kuchangia jana, lakini nina hakika Waziri wa Maji yuko hapa atahakikisha kwamba, kweli suala la maji linapewa kipaumbele kwenye bajeti inayokuja. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, bila kuangalia matatizo hayo; sasa hivi tunakwenda kwenye sera ya Tanzania ya viwanda. Hatuwezi kujenga viwanda bila kuangalia kwanza haya matatizo ya umeme na maji tuyashughulikie, matatizo ya barabara, hivyo viwanda vitakavyopelekwa
huko, barabara zitapita wapi. Naamini Mheshimiwa Rais kutokana na ahadi zake alizozisema, kutokana na commitment ambayo anayo kwamba ahadi alizozitoa zitatekelezeka. Tumeona ahadi zinaahidiwa nyuma, kuna barabara yangu kule ya Amani mpaka Muheza kilomita 40,
awamu mbili zilizopita zimeahidi kwa kiwango cha lami barabara hiyo, lakini hakuna lami iliyowekwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Amani wanavuna, sasa hivi kuna viungo, kuna chai ambapo sasa ni wakati wa kuvuna viungo hivyo, wanashindwa kuteremsha mazao hayo, wanapata taabu kila saa magari yanakwama. Naamimi kabisa kwamba Waziri wa Ujenzi yupo hapa na ataliangalia suala hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunazungumzia suala la viwanda, Tanzania ya viwanda, lakini naamini kwamba Waziri wa Viwanda ataangalia kiwanda kipi ambacho kinatakiwa kiwe wapi na mkoa gani ambao unatoa zao gani. Tuanze kufufua viwanda ambavyo vilikuwepo kabla ya kufikiria kuanza kujenga viwanda vingine, lakini Kiwanda cha Machungwa Muheza kianze kujengwa mapema. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Tanga kulikuwa na viwanda chungu nzima, viwanda vimekufa pale; ningefurahi sana kuona kwamba viwanda vile vinaaza kufufuliwa na wananchi wa Mkoa wa Tanga basi wanaanza kufaidika na viwanda hiyo. Kuna mazao chungu nzima ambayo yako Tanga na ambayo naamini kabisa kwamba kama viwanda hivyo vitafufuliwa basi tutakuwa na uwezo wa kujenga uchumi wetu vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo kuna mambo mengi ambayo yamezunguka Tanga, hapa imezungumzwa reli ya kati tu, reli ya Tanga - Arusha mpaka Musoma hadi Nairobi imesahauliwa kabisa. Ningefurahi na ningeshukuru kama ningekiona kitu hicho kwenye Mpango huu wa Bajeti ambao unakuja. Vivyo hivyo pamoja na Bandari ya Tanga, tunazungumzia mambo ya Bandari nyingine tunaacha Bandari ya Tanga ambayo ni bandari kubwa kabisa pale, kwa nini hatuizungumzii? Naomba Waziri anayehusika aliangalie hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la elimu; Serikali imeanza vizuri kabisa. Mheshimiwa Rais alitoa ahadi ya elimu bure na imeanza kutekelezwa. Lazima tuwe na pa kuanzia, matatizo madogo madogo yanaweza kuwepo, lakini lazima tuweke sehemu ya kuanzia. Tumeanza vizuri na naamini wananchi wote nchi hii wamefurahi kwamba elimu imekuwa bure. Hayo matatizo ambayo yanatokea hapo yatarekebishwa. Tusiikatishe tamaa Serikali hii kwa jinsi walivyoanza, tuwaunge mkono Waheshimiwa Wabunge. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi kuna shule nyingi ambazo zinaishia darasa la kumi na mbili (form four), lakini tuna shule chache sana za Serikali za kidato cha tano na cha sita.
Umefika wakati sasa hivi Serikali iondoe ukiritimba ambao upo wa kusema kwamba lazima shule za Serikali za form five na six ziwe boarding. Tunahitaji sasa hivi iwe day, watoto wetu waweze kusoma kwa sababu sasa hivi shule zimekuwa nyingi, lakini za form five na six zimekuwa ni chache, naomba mliangalile.
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine Mheshimiwa Rais ameongelea suala la wawekezaji, lakini ni lazima tuangalie na tukubali kwamba maandalizi yetu ya wawekezaji not friendly, bado kuna matatizo mengi sana EPZA, TIC, bado kuna ukiritimba mkubwa sana ndiyo maana
wawekezaji wanatoka hapa wanarudi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi Mabalozi tuna Sera ya Diplomasia ya Uchumi, tuliambiwa tulete wawekezaji, tunawaleta wawekezaji, wanarudi. Kuna leseni sijui karibu 18 mara ya mwisho nilipokwenda TIC pale au vibali ambavyo mwekezaji anatakiwa apewe. Unategemea
huyo mwekezaji atawekeza kweli, jamani tuangalie hilo suala na kama mnataka Mabalozi watekeleze kweli Economic Diplomacy, basi tuhakikishe kwamba huu ukiritimba na huu urasimu unaondoka.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna suala la utulivu na amani, Waheshimiwa Wabunge, lazima tukubali kwamba uchaguzi huu tumeufanya kwa utulivu na amani. Kama kulitokea uvunjivu wa amani, ni kidogo, lakini kazi ambayo wamefanya vyombo vya dola ni kubwa jamani. Ninyi hamuelewi namna ya kutuliza utulivu wa amani, ni kazi kubwa, vyombo vya dola vilikuwa havilali, ni lazima tuvipongeze na tuviunge mkono vyombo vyetu jamani.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Balozi muda wako umekwisha.
MHE. BALOZI. ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tu kumalizia kwa
kusema kwamba….
NAIBU SPIKA: Muda umekwisha naomba ukae tafadhali.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nashukuru kupata nafasi hii kuweza kuchangia bajeti ya mwaka huu. Kwanza napenda kukupongeza sana wewe kwa ujasiri ambao unao na katika hali ya sasa hivi jinsi ambavyo unaliendesha Bunge hili. Nakupongeza na haya matatizo ya wenzetu yasikupe tabu sisi tunaku-support moja kwa moja. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda pia kumshukuru Waziri, Naibu wake na wataalam wake ambao wameweza kutuletea bajeti nzuri ambayo haijawahi kutokea tangu tumepata uhuru. Ni bajeti yenye mwelekeo ambayo inajieleza yenyewe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi kifupi tu tangu Awamu ya Tano imeingia madarakani imeweza kukusanya mapato mengi sana ambapo nchi yoyote bila kuwa na mapato haiwezi kwenda vizuri. Mapato ni kitu cha msingi kwenye nchi yoyote. Hata ukiangalia wakati wa ukoloni ukusanyaji wa kodi ni kitu muhimu, kulikuwa na kodi za vichwa, kulikuwa na kodi za vipande na kodi za matiti. Zote hizo zilikuwa ni kodi ambazo zinakusanywa kwa lengo la kuweza kupata mapato ya Serikali na kuweza kufanya nchi iweze kuendelea, nchi iweze kutengeneza miundombinu mbalimbali. Ndiyo maana mpaka leo hata wenzetu wa Ulaya watu ambao wanakwepa kulipa kodi wanakwenda jela. Hapa tuna kesi ya mcheza soka bora duniani Lionel Messi ambaye yuko Mahakamani kwa kosa la kukwepa kodi. Sasa huo ni mfano tu wa kuonesha namna gani kodi ni muhimu katika kuendeleza maendeleo ya nchi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, bajeti hii kama ambavyo ilivyo asilimia 40 imekwenda kwenye maendeleo, ni kitu ambacho hakijawahi kutokea hapa nchini na imelenga kuleta maendeleo kwenye maeneo mbalimbali. Mheshimiwa Waziri pia kwenye bajeti hii ameweza kuangalia ni vitu gani ambavyo vinaweza kuboreshwa kwenye huduma za jamii, mambo ya maji, umeme, barabara na mambo mengine kwa lengo la kuweza kupata maendeleo ya haraka hapa nchini. Hii ni pamoja na bajeti ambayo imejikita zaidi kuondoa tozo mbalimbali kwa manufaa ya wakulima. Kuna tozo zimeondolewa, tozo za mazao ya korosho, chai, pamba na kadhalika. Sasa yote haya ni muono wa bajeti hii ambao kwa kweli naunga mkono kwa asilimia mia moja. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pamoja na yote hayo ningependa Mheshimiwa Waziri na wataalam wake wajielekeze kwenye baadhi ya maeneo ambayo ningependa kuyataja. Wakati tunachangia Wizara ya Maji, Wabunge wengi sana walisisitiza suala la Wakala wa Maji Vijijini. Suala hili lingepewa umuhimu wa kipekee kwa sababu tatizo la maji ni kubwa hapa nchini, hata Jimboni kwangu ndilo tatizo linaloongoza. Kwa hiyo, uanzishwaji wa Taasisi ya Maji Vijijini ni muhimu na naomba Mheshimiwa Waziri ajaribu kuliangalia aone kama anaweza kulipenyeza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili ni road toll. Road toll kwenye nchi hii naona halipewi umuhimu, nikiambiwa kwamba kodi yake imeongezwa kwenye mafuta lakini huwezi kuona impact hiyo. Nchi nyingi duniani kubwa na ndogo ukiangalia zimewekwa road toll barabarani. Nashangaa ni kwa nini sisi hatuwezi kuiga na kuona kwamba tunaweza tukapata mapato mengi kutokana na road toll. Naamini kabisa kwenye highway zetu pamoja na matatizo ya barabara zetu kuwa ndogo lakini tukianzisha road toll tunaweza kupata mapato ya kutosha. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la transit good, sasa hivi naambiwa kwamba meli nyingi zinakwepa kuja Dar es Salaam na meli nyingi sasa hivi zinakwenda Beira na Maputo kwa sababu ya VAT ambayo imewekwa kwenye transit goods. Ni vizuri Waziri akaliangalia eneo hilo kama ni kweli akaangalia namna gani anaweza kutoa hiyo VAT ya asilimia 18 ambayo inatukosesha malipo ya transit kwa mizigo ambayo inapita hapa nchini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni reli ya kati. Naipongeza kabisa kwamba bajeti hii imegusa reli ya kati kwa standard gauge, lakini nasikitika kwamba sijaona reli ya kwetu, reli ya Tanga sijaiona kwenye bajeti hii ambayo nilitegemea hata itaguswa pia. Pia nasikitika sijaona maboresho ya bandari ya Tanga ukitilia maanani bomba tumelipata kutoka Uganda. Kwa hiyo, labda Mheshimiwa Waziri aangalie namna atakavyoweza kupenyeza suala hilo ambalo ni muhimu ili vitu hivyo viende simultaneously, reli ya Tanga pamoja na reli ya kati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimefarijika sana kuona kwamba tutanunua ndege tatu, ndege ambazo naamini kabisa zitatuletea wawekezaji na watalii wengi. Nasikitika kuona kwamba kwenye suala la watalii Kodi ya Ongezeko ya Thamani imewekwa pale kinyume na wenzetu wa Rwanda na Kenya ambao wameondoa kodi hiyo. Kwa hiyo, hii ina maana kwamba watalii ambao watakuja wote wataishia Kenya ukitilia maanani kwamba wao usafiri wa ndege ni wa uhakika na wanao. Kwa hiyo, ni vizuri eneo hilo pia akaliangalia kama ambavyo ameweka kwenye page yake ya 49. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la uanzishwaji wa Mahakama ya Mafisadi ni muhimu na ambalo Mheshimiwa Rais ameliongelea tangu wakati wa kampeni. Mahakama hii inategemea sana ripoti au taarifa kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali. Katika kesi ambazo naamini zitapelekwa kwenye Mahakama hiyo robo au nusu ya kesi hizo zitatokana na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali. Ni kilio cha Wabunge wengi ambao wameongelea, hivyo ni vizuri wakaangalia eneo hilo, namna ambavyo wataweza kuwaongezea fedha. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna suala lingine la kodi ambayo imeondolewa hasa kwenye maduka ya vyombo vya ulinzi na usalama. Hivi vyombo vya ulinzi na usalama vilikuwa vimezoea maduka hayo na tozo hiyo imeondolewa hasa baada ya kuonekana kuna misuse kwa hao ambao wamepewa hizo zabuni za kupeleka vyombo hivyo. Nimesoma hotuba lakini haielezi mbadala kwamba ni shilingi ngapi watapewa hawa maaskari au walinzi wetu ambao wapo kwenye vyombo hivyo badala ya kununua hivyo vitu kwenye maduka. Kwa hiyo, ningeomba suala hilo pia liangaliwe litakuwaje. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeangalia pia suala la makato ya kodi za Wabunge lakini nimeliona kwamba halina mashiko kwa sababu halina basis. Kama suala hili la viinua mgongo vya Wabunge ambalo inatakiwa likatwe kodi mwaka 2020 sielewi kwa nini limeletwa wakati huu wa 2016. Ni vizuri suala hili likaletwa kwenye bajeti ya 2019/2020. Hapo ndiyo tunaweza tukalijadili kwa kina. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kumalizia kwa ushauri. Ukiangalia taarifa ya Kamati ya Bajeti inaonekana kuna msuguano au hakuna maelewano yaliyokuwepo kati ya Wizara na Kamati ya Bajeti. Ni vizuri wakikaa na kuona wanaweza kulitatua namna gani na kuangalia mawazo ya Kamati ya Bajeti ambayo wameyatoa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nimefarijika kuona kwamba bajeti hii isiwe tegemezi kwa wafadhili. Nimeona kwamba hela za nje ambazo zimetengwa ni shilingi trilioni 3.12 lakini ni vizuri kabisa kwenye bajeti ambazo zinakuja tujaribu kujifunza, tujaribu kuelewa kwamba tusitegemee fedha za wafadhili ambazo zinakuja na masharti kemkem. Kwa hiyo, ni vizuri kabisa katika bajeti hii hela za wafadhili ni kidogo, lakini katika bajeti zinazokuja suala hili linatakiwa tuliondoe moja kwa moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ambalo napenda kushauri ni hizi fedha ambazo zimetengwa. Tunategemea kwamba fedha hizi zitakapopitishwa na Bunge hili fedha hizo zote ziwe zinafika kwenye Wizara kama zilivyopitishwa. Vinginevyo kama zitakuwa zinakwenda nusu nusu au mwishowe unakuta kwamba fedha hizo hazifiki itakuwa ni mbaya sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kumalizia napenda waangalie hili suala ni kwa nini nchi yetu hatuwezi kutumia currency ya kwetu. Currency zinatumika hovyo hovyo tu, unaweza ukawa na dola au pound unakwenda hapo nje unabadilisha tu, wenzetu hawatumii hivyo. Naamini restrictions ambazo wenzetu wameziweka zinakuza uchumi kwa sababu tutatumia currency yetu. Kwa hiyo, naamini kabisa tutakapotumia fedha zetu tutakuwa na uwezo wa kukuza uchumi wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, ningependa kuunga mkono hoja na nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii na mimi kuchangia hoja hii ambayo ni ya muhimu sana kwa mwananchi wa kawaida na hata mwananchi yoyote wa hapa nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, napenda kumshukuru sana Rais Mheshimiwa Dkt. Magufuli na hususan Waziri Mheshimiwa Profesa Mbarawa. Kazi ambayo Wizara hii imeifanya katika kipindi kifupi ni kazi ambayo inatakiwa isifiwe na ni kazi ambayo kila mtu ameiona. Katika kipindi kifupi Serikali hii ya Awamu ya Tano imeweza kutufanyia mambo mengi, imeweza kuleta ndege hapa. Kuna ndege sita; mbili zimeshafika. Zaidi ya kuleta ndege hizi kuna nchi nyingine ndogo tu kama Mkoa hapa nchini, zina ndege kubwa na sisi nchi hii tumeshindwa kuleta ndege na Mheshimiwa Rais ameweza kuifufua ATCL. Kwa hiyo, tumpongeze sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, ameweza kuleta flyover. Flyover zimeanza kujengwa, zitapunguza msongamano mkubwa sana hapa nchini hasa ukichukulia maanani pia kwamba watu wote wanahamia hapa Dodoma sasa hivi, kwa hiyo, msongamano kule Mjini Dar es Salaam utapungua kwa kiwango kikubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, cha msingi zaidi ni kuweza kuleta treni ya standard gauge ambayo kwa kweli ni treni ya kisasa. Kule nchi za nje wenyewe wanaiita bullet train. Sasa umuhimu wa treni hii kwa kweli utakuja kuonekana hasa wale ambao wataingia Bungeni mwaka 2020; wataacha magari yao yote Dar es Salaam na kuingia kwenye hizi treni. Kwa hiyo, mambo haya pamoja na mambo mengine ya vivuko ambavyo vimewahi kufanyika na mambo mbalimbali ambayo yamewahi kufanyika kwa kweli napenda kumpongeza sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Profesa Mbarawa ametembea nchi nzima hii kwa ajili ya kukagua miradi, ametembea kote, amekuja Tanga karibu zaidi ya mara tatu, ingawaje bado Muheza hajafika, namsubiri. Lakini nangependa kumshukuru sana, yeye na wataalam wake kazi ambayo wameifanya kwa kweli ni kubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na juhudi zote hizo, lakini pia safari hii Wizara hii imeweza kuangalia Mkoa wa Tanga; tunajua tumepata zabuni ya kutengeneza bomba la mafuta kutoka Hoima kule Uganda mpaka kwenye Bandari ya Tanga, lakini kwenye kitabu hiki nashukuru sana Wizara imeanza kuboresha Bandari ya Tanga na tumefanikiwa kupata karibu shilingi bilioni 12 kwa ajili ya kutengeneza bandari hiyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, cha msingi ni kwamba Mheshimiwa Waziri amesahau kuangalia reli ya Tanga. Reli ya Tanga ndiyo chimbuko, tena reli ya Tanga imeanza kabla hata ya hii reli ya kati, lakini sijui kwa nini hakuigusia, hata kuiangalia. Namuomba aangalie kwa kadri atakavyoweza tukitilia maanani kwamba tuna bomba la mafuta, tuna kazi kubwa, Tanga inataka kufufuka, kwa hiyo, tunaomba aangalie atafanya namna gani ili na reli ya Tanga iweze kuwa kwenye kupata standard gauge. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo, pia kuna na barabara ambazo zimesaidia sana, zinataka kutoa vitu kutoka Mkoa wa Tanga ili viende kwenye Mikoa mingine. Mheshimiwa Waziri ametusaidia sana kwenye barabara ya Bagamoyo – Saadani - Pangani ambapo barabara hii kwa kweli ndiyo tumepata hela ambazo ni kianzio tu, lakini tunashukuru sana. Tunaamini kwamba baada ya barabara hii kutengenezwa basi Tanga inaweza kufunguka.
Mheshimiwa Naibu Spika, hapo hapo, ukitilia maanani pia tuna barabara ya Handeni - Kibarashi pamoja na Kibaya ambayo inakuja kutokea Singida. Barabara hii imewekewa hela ndogo, lakini tunaamini kwamba huu ni mwanzo tu, ataweza kuifikiria kuweza kuongezea. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la msingi zaidi ambalo limenifurahisha kwenye bajeti hii ni kuweza kuweka hela za kutengeneza barabara ya kutoka Amani mpaka Muheza kilometa 36. Barabara hii safari hii imewekewa hela karibu shilingi bilioni tatu. Najua ni mwanzo tu, najua kutokana na jinsi nilivyokuwa namghasi Mheshimiwa Waziri atatuongezea hela, lakini hii ni chachu! Barabara hii ni muhimu sana kwa maendeleo ya uchumi katika Wilaya ya Muheza na ninaamini kabisa kwamba wana Muheza hasa watu wa Amani kama wananisikia watafarijika sana kuona kwamba barabara hii safari hii imewekewa hela. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nami namwambia Meneja wa TANROADS, Engineer Ndumbaro ambaye yupo kule, anafanya kazi nzuri sana na mara baada ya hizi fedha kufika, basi barabara hii, kama watu wa Amani wananisikia, itaanzia Amani kuteremka mpaka Muheza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo, tuliahidiwa kilometa tatu na Mheshimiwa Rais alipokuja, alipata vumbi sana pale Muheza na akaahidi na tunazitegemea hizo kilomita tatu basi zitapunguza vumbi ambalo lipo pale Mjini Muheza.
Mheshimiwa Naibu Spika, iko barabara nyingine ambayo inatoka kwenye junction ya Pangani, Boza. Barabara hii ni muhimu sana kwa watu wa Muheza. Sasa hivi inashughulikiwa na TANROADS na tuliomba sana iingizwe kwenye mpango huu wa sasa hivi kwa sababu barabara hii inatoka Boza junction na inapita Muheza, inakwenda moja kwa moja mpaka inapita Misozwe, inakwenda mpaka Maramba. Sasa barabara hii tuliomba hata tupewe hela ziingie hata kidogo kwa ajili ya kufanyia upembuzi yakinifu tayari kwa kuwekewa lami. Tungeshukuru sana kama utasikia kilio hiki kwa sababu niliwahi kuiongelea barabara hii kwenye bajeti iliyopita na ninaamini kwamba hata safari hii utaweza kuangalia unaweza kuifanyia vipi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna barabara ambazo tuliomba zipandishwe hadhi na ziweze kushughulikiwa na TANROADS na barabara hizo tumeshazipitisha kwenye RCC. Barabara hizo zipo tano; kuna barabara ya Kilulu ambayo inakwenda mpaka Mtindiro inapita kwa Fungo. Tunaomba sana ipandishwe hadhi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna barabara ya Kibaoni - Misarai - Zirai inatoboa mpaka inakwenda Korogwe. Barabara hii ningefurahi sana kwa sababu inatoboa kwenye Jimbo la Profesa wangu Maji Marefu. Tumekuwa tunaipigia makelele sana; tungefurahi sana kama ingeweza kupandishwa hadhi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia barabara ya Potwe - Shambakapori na Amtiko inapitia Masuguru mpaka Kerenge. Sasa tutashukuru sana kama ungeweza kutuangalizia barua hizo ambazo tumeshapitisha kwenye RCC na tungeshukuru sana kama ungeweza kutusaidia hizi barabara zishugHulikiwe na TANROADS. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mawasiliano. Tarafa ya Amani ina matatizo sana ya mawasiliano, nilizungumzia bajeti iliyopita na nilishakuja Wizarani na nikatoa kilio hichi kwamba uchumi wa Muheza unategemea sana Amani, lakini sasa watu wenyewe kule hawana mawasiliano ya simu. Tulikuwa tunaomba kampuni moja ya simu ituwekee minara kule. Maeneo ya Misarai, Mbombole, Zirai, Kwemdimu, Tongwe na Kiwanda kote kule kuna matatizo sana ya mawasiliano ya simu. Kwa hiyo, ningeshukuru sana kama ungewaamuru hata kampuni moja tu iweze kutuwekea, ingewasaidia sana watu wa Amani. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la miradi, Wizara hii ina miradi mingi sana, lakini ningeshukuru sana kama miradi hii ingeanza kushirikiana na PPP. Watu binafsi ni watu muhimu sana. Nchi zote duniani sasa hivi zinashirikiana na watu binafsi na bila watu binafsi tutachukua miaka mingi sana kukamilisha hii miradi. Mmewahi kuona acha hii miradi mikubwa ya madaraja au barabara, lakini barabara zote sasa hivi, hata nchi zilizoendelea zinatumia road toll. Sasa huu mpango ambao unatumia sasa hivi wa kukata hela kidogo za mafuta hauna effect. Mimi ningeshukuru sana kama mngeanzisha road toll ili watu binafsi wajenge hizi barabara na mwingie makubaliano. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naamini kama Mheshimiwa Waziri ukisimamia vizuri huu urasimu ambao upo hapo treasury wa kuweza kutoa hizi zabuni kwa watu binafsi, ungeusimamia naamini kabisa kwamba sasa hivi tungekwenda kama rocket kwenye hii nchi. Kwa hiyo, uchukue hayo mawazo na uangalie kwamba utaweza kuyatekeleza kwa namna gani. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na ninaamini kabisa kwamba mambo yote ambayo Mheshimiwa Waziri ameyafanya, safari hii ameiona Tanga vizuri, lakini tunaomba aangalie kabisa suala la reli yetu ya Tanga na pia tunaomba aangalie kwenye kiwanja chetu cha ndege kwa sababu kitakuwa busy sana sasa hivi, tunategemea kupata Waziri wa Viwanda hapa, ndugu yangu ametuletea kiwanda kikubwa sana kule, sasa kutakuwa na mambo mengi sana Tanga, bandari inafanya kazi vizuri na imeshaanza kufanya kazi. Kwa hiyo, tunaomba uangalie kiwanja chetu na chenyewe kiweze kusaidiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, nashukuru sana na ninazidi kuipongeza Wizara hii kwa kazi ambayo imefanya. Wizara hii imekuwa ni kioo cha Wizara nyingine nyingi hapa. Kazi ambazo zimefanyika, zinaonekana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, napenda kushukuru na ninaunga mkono hoja. Ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Katiba na Sheria
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naunga mkono hoja na ningependa kuchangia suala moja muhimu. Jimbo la Muheza halina jengo la Mahakama ya Wilaya, bajeti iliyopita ilikuwa limepangwa kwenye mpango wa ujenzi na likaondolewa katika hatua za mwisho, mwaka huu katika bajeti hii limeondolewa kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Muheza tulikwishatayarisha kiwanja muda mrefu, jengo linalotumika halina hadhi ya kimahakama, hivyo tunaomba tufikiriwe katika mpango wa ujenzi wa kisasa. Nakushukuru.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nashukuru kwa kunipatia nafasi hii ili niweze kuchangia bajeti ya Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, napenda kumshukuru sana Rais wetu mpendwa, Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli. Napenda kumshukuru kwa jinsi alivyoanza kuendesha Serikali hii ya Awamu ya Tano kwa nguvu, kwa kasi na kwa weledi mkubwa na kwa vitendo na sio blah blah. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeshuhudia tukiwa na mipango mingi, miradi mingi, maneno mengi lakini sasa hivi tumepata mtu ambaye anaonesha vitendo. Rais ambaye anaonesha kitu gani ambacho kinatakiwa na sio kuzungumza blah blah. Kwa muda mrefu tumekuwa na sera nyingi lakini ndugu zangu mtakubaliana nami kwa kipindi kifupi mmeona vitendo ambavyo amefanya. Amechukua hela kutoka mafungu mbalimbali na kuyapeleka kwenye mambo muhimu ambayo yanawagusa wananchi wa kawaida kama mambo ya barabara, vitanda hospitalini, madeski ya shule na mambo kadha wa kadha. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ndugu zangu nimefurahi sana na nashukuru kupata mtendaji wa aina hiyo. Nchi yetu sasa hivi inataka kiongozi wa aina hiyo anayeweza kutoa amri, kutekeleza na kufuatilia. Naamini kama Rais Magufuli angekuwa amechukua mafunzo ya komandoo basi miezi sita tu hii nchi ingeweza kuwa kwenye mstari ambao unatakiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda pia kupongeza uongozi mzima kwa jitihada kubwa ambazo zimefanyika hivi karibu mpaka tumepata mradi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Kampala na kuyaleta kule kwenye bandari ya Tanga. Mradi huo ni mkubwa na lazima uende sambamba na sehemu ambazo bomba hilo litapita kwa kuonesha wananchi watafaidika namna gani. Bandari ya Tanga kama mlivyosikia ina kina kirefu kuliko bandari zote na ndiyo moja ya sababu iliyofanya tupate mradi huo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ningefurahi sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kama wangechambua sasa hivi hiyo bajeti ambayo ipo, wahakikishe kwamba wanaimarisha vitu vyote ambavyo vinahitajika kwenye bandari ya Tanga, kuna vifaa ambavyo ni vichakavu sana kwenye bandari ile. Vifaa vyote hivyo na mambo yote hayo ambayo yanatakiwa ni lazima tuhakikishe kwamba bandari hiyo inaimarika ili tuweze kukabiliana na huo mradi ambao unakuja.
Ningeshukuru sana kama reli ya Tanga na yenyewe ingewezwa kuimarishwa. Najua imewekwa kwenye bajeti lakini nitashukuru kama na yenyewe inaweza kuwa kwenye standard gauge ili iweze kuungana na reli ya kati iweze manufaa makubwa kwenye mradi huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitashukuru pia kama kiwanja cha ndege cha Mkoa wa Tanga kitaimarishwa kwa sababu sasa hivi kutakuwa na watu wengi, wimbi litakuwa ni kubwa, kwa hiyo, tunaomba uwanja huo na wenyewe uweze kuwekwa kwenye mpango huu na kuweza kuimarishwa kwa kupanuliwa tayari kwa kupokea wageni. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo, sisi Muheza bomba hilo litapita, tunataka kutayarisha kituo cha matunda (center ya matunda) kuhakikisha kwamba kwa mradi huo panakuwa na additional value ili kuona tunafaidika vipi na mradi huo. Kwa hiyo, tumeshatayarisha sehemu za wawekezaji kuhakikisha kwamba tunatengeneza sehemu ya matunda, tunataka Mji wa Muheza uwe mji wa matunda. Matunda yote ya Mkoa wa Tanga yaweze kupatikana kutokea Muheza. Tumeshaanza kukaribisha wawekezaji na tungeomba Serikali ituunge mkono kwenye hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo lakini vitu hivyo vinakwenda na miundombinu, ni lazima tuhakikishe kwamba tunaziimarisha barabara, mkoa wa Tanga tuna barabara ya Muheza kwenye Jimbo langu, barabara ambayo Serikali imeahidi kuiweka lami, barabara ya Amani mpaka Muheza. Amani kutoa vitu chungu mzima, kuna viungo, karafuu, pilipili manga, kuna vitu vingi sana na wakulima wa kule wanapata taabu sana kuleta vitu hivyo mjini. Pamoja na kuweka kituo cha matunda tuna mpango tuweke viwanda vya kusafishia viungo ili kuhakikisha kwamba Muheza inakuwa ni Muheza kweli kweli.
Mheshimiwa Naibu Spika, najua kuna tatizo la maji ambalo tumeanza kulishughulikia kwa kumuomba Waziri anayehusika lakini ningeomba liwekewe mkazo. Bila maji Muheza haiwezi kuendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda pia nichangie suala la utalii. Vivutio ambavyo tunavyo nchi hii haviendani na watalii waliopo. Hatuwezi kusema tunakadiria watalii milioni 1.2 wakati tuna National Parks karibu 15, uwiano wake haupo. Kuna nchi ambazo zina kivutio kimoja tu, mimi nilikuwa Zimbabwe wana Victoria Falls tu lakini wanaingiza watalii milioni 2.5 kwa mwaka, sasa ni kwa nini sisi tushindwe kufanya vitu kama hivyo? Naomba suala hilo liangaliwe na tuone tunaweza kufanya nini kuweza kuongeza watalii. Kuna sehemu nyingi sana za utalii, Amani kule Muheza ni sehemu mojawapo ya watalii ila wanashindwa kwenda vizuri kule kwa sababu ya barabara. Naamini tutakapoiweka lami ile barabara kutakuwa na ongezeko la watalii sehemu za Amani.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kilimo ni muhimu na linakwenda sambamba kabisa na sera ya Serikali ya Awamu ya Tano ya viwanda. Bila kilimo, mazao na malighafi hatuwezi kufika. Tuchukue mifano ya nchi nyingine ambapo wanawawezesha wakulima, wanawakopesha pembejeo, wanawapa mbolea bure halafu baadaye wanakuja kuelewana na Serikali namna ya kuwakata. Kwa hiyo, naamini tukifanya hivyo tutaweza kuhakikisha kwamba wakulima wetu wanaweza kufaidika na kilimo.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, napenda kuunga mkono bajeti hii ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ahsante sana.
Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017- Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nakushukuru sana kwa kupata nafasi hii kuweza kuchangia bajeti hii ya Wizara ya Viwanda. Pia nawashukuru wapiga kura wangu, Wanamuheza kwa kuendelea kuniamini na kuweza kunifanya niendelee kuongea hapa leo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Viwanda ni Wizara muhimu sana. Ni Wizara muhimu kwa sababu inaendana na malengo ya Awamu ya Tano; wananchi wa Tanzania wengi wana mategemeo makubwa sana na Wizara hii; wana mategemeo ya mabadiliko mengi sana kwenye Wizara hii; wana mategemeo ya kupata ajira nyingi kutokana na viwanda ambavyo Awamu ya Tano inategemea kuviweka. Kwahiyo, Wizara hii ni Wizara ambayo ni ya muhimu na Wizara ambayo tunaitegemea itakuza uchumi wetu, italeta ajira nyingi na itatuondolea umaskini kwa kiwango kikubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda ambavyo vilikuwepo tangu enzi za Mwalimu ni viwanda vingi, lakini vile viwanda vingi vimekufa. Sasa hivi kinachofanyika ni kutaka kuvifufua hivyo viwanda. Mkoa wa Tanga ulikuwa ni mmoja wa Mkoa ambao tulikuwa tunaongoza kwa viwanda hapa nchini.
Tuikuwa na viwanda karibu 180 na sasa hivi viwanda ambavyo viko ni 50 tu, ndiyo viwanda vikubwa na vidogo ambavyo tunaweza kusema kwamba ndio vinafanya kazi katika Mkoa wa Tanga. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama alivyosema Waziri kwenye hotuba yake kwamba malengo ya kwanza ni kuanza kuvifufua viwanda hivi, lakini hatuwezi kufufua viwanda hivi kama hatujajua vile vilivyokufa vilikufa kwa sababu gani. Kwa hiyo, tutakapovifufua viwanda hivi tutakuwa tunajua kwamba vile ambavyo vimekufa vimekufa kwa sababu gani, tusirudie hayo makosa tena. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Muheza ni sehemu mojawapo tulikuwa na kiwanda. Tulikuwa na kiwanda cha matunda. Matunda ambayo yanazaliwa Muheza ni matunda ambayo yanajulikana hii Afrika na ulimwengu mzima. Sisi tunaweza kutoa matunda tani 100,000 kwa mwaka. Ni matunda ambayo yanaweza kuwa ya pili au ya tatu katika Bara la Africa baada ya South Africa na Egypt.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Muheza tunatoa machungwa mengi, lakini sasa hivi hatuna kiwanda cha machungwa. Wanakuja Wakenya, wanajaa pale, wanajaza hoteli za Muheza, miezi miwili iliyopita ilikuwa ukija Muheza huwezi kupata nafasi kwasababu wamejaa Wakenya pale kuchukua machungwa yetu ku-cross kupeleka Mombasa kwenye viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nategemea Mheshimiwa Waziri, atakapokuja ku-wind up kwenye hotuba hii, atatoa matumaini ya kiwanda cha matunda cha Muheza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuhitaji kiwanda cha matunda Muheza, lakini pia tunazalisha viungo vingi kuna pilipili manga, hiliki pale baada ya Zanzibar, kuna karafuu na mdalasini. Wanakuja watu kutoka nchi za nje wanajaa Wilayani pale kwa ajili ya kuchukua malighafi hizo na kuzipeleka nje. Kwa nini tusiweke hata kiwanda kidogo pale? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri ame-present hotuba yake kwa nguvu sana na inaonekana inatoka moyoni kwake. Kwa hiyo, tunategemea utekelezaji wake utakuwa ni mkubwa ili wananchi wa Muheza na wenyewe waweze kufaidika na Mheshimiwa Waziri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunategemea kwamba viwanda hivi basi vitakapozalisha vitalindwa. Nimefurahishwa sana na Mheshimiwa Rais aliposema kwamba kuanzia leo basi furniture zote za maofisini ziwe zinatokana na malighafi yetu ya humu humu nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tuna kiwanda chetu cha kamba, kama unavyojua katani, ni zao letu kubwa Mkoani Tanga, ni zao letu kubwa Wilayani Muheza. Kiwanda cha Ngomeni cha kamba ambacho ni kiwanda kikubwa Afrika Mashariki na Kati, ni kiwanda kimojawapo ambacho watu wanalipa hela kabla hata hawajapata hayo mazao yake ambayo wanayataka pale. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunategemea kwamba kiwanda kile kinatakiwa sasa kisaidiwe na Serikali. Nilikwenda pale na kuongea na uongozi, wakaniomba. Wao wanaomba kitu kimoja tu, wanaomba Serikali iwape tender ya wao kutengeneza mazulia ya maofisi zote za Serikali kwenye nchi hii na uwezo huo wanao, ni suala la kubadilisha zile mashine zao pale na kuwapa mashine nyingine. Mheshimiwa Mwenyekiti, namtegemea Waziri ataweza kuwapa upendeleo kiwanda hicho, kukuza kiwanda hicho kiweze kuzalisha mazulia yote ambayo yanatengenezwa kwenye ofisi zote za Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niongelee suala la EPZA. Kwanza nawashukuru sana EPZA kwa sababu wameweza kujaribu kuweka maeneo ambayo wawekezaji wakija wanaweza wakaoneshwa, ni hatua moja nzuri sana. EPZA imejikita zaidi kwenye Foreign Direct Investment (FDI). Vitu vyote wanaelekeza nje, vinapelekwa nje; vikitoka kule, vinatengenezwa, then vinarudishwa hapa hapa. Sasa nilitaka wapanue wigo wa kuweza kuwafanya Watanzania na wenyewe waweze kuelimika na kuwa wataalam na waweze kufanya vitu hivyo wao wenyewe na kuviuza hapa hapa nchini; kuleta mashine ambazo zinaweza kufanya kila kitu hapa hapa nchini na kuweza kutoa mali ambayo inaweza kuwa ni nzuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanga tunataka tufaidike na bomba hili la mafuta la kwenda Kampala.
Kwanza tunaisifu sana Serikali kwa kuweza kupata hiyo zabuni ya kutengeneza hilo bomba la mafuta, lakini tunataka tuhakikishe kwamba tunaongeza value kwenye hilo bomba ili wananchi wa Tanga, wananchi ambao bomba hilo litapita sehemu zote, waweze kufaidika nalo. Wanaweza kufaidika nalo namna gani?
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja, ahsante.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJABU: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuunga mkono hoja, na ningependa kuchangia kama ifuatavyo:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza kwa changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika hoja hii. Elimu ndiyo msingi wa mambo yote hapa Duniani, yapo mambo ambayo yanatakiwa kuboreshwa ili tuzidi kuongeza ubora wa elimu yetu. Kwa mfano, mitaala yetu inabidi iangaliwe upya, tujaribu kuangalia mitaala ya nchi zingine zinazofanya vizuri ili tuiboreshe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitengo cha Ukaguzi cha Wizara inabidi kiimarishwe, sikumbuki au kusikia Wakaguzi wamekuja Muheza. Hawa ndiyo wanaweza kuboresha mambo mengi ni watu muhimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna upungufu mkubwa wa Walimu Muheza. Ingawa ni suala lililopo TAMISEMI shule za msingi na sekondari zote, ninaomba uliangalie kwa umuhimu wake, kuna shule zingne zina walimu wawili na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara sasa ni vizuri ifikirie kuanzisha mitihani mara mbili kama wenzetu wengi badala ya kungojea mwaka mzima kwa O- level na A- Level. Pia maslahi ya walimu yaangaliwe kwani inaonekana kama wamesahulika sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa msisitizo mkubwa naona Muheza High School ambayo ni hiyo tu Wilaya nzima ifanywe ya kutwa na bweni ili iweze kuhudumia ongezeko la wanafunzi wa „O‟ Level Wilaya nzima. Shule hiyo ilijengwa kwa nguvu za wananchi na ina uwezo mkubwa wa kuchukua wanafunzi wengi zaidi. Wizara isimamie TAMISEMI kuona vifaa vya maabara shule za sekondari vinapelekwa.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nashukuru sana kupata nafasi hii ya kuchangia kwenye bajeti hii ya mtoa hoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa ningependa kusema kwamba bajeti hii kwa kweli haikututendea haki Mkoa wa Tanga. Bajeti hii haiku-take into consideration kwamba sasa hivi tumepata tender, tumepata zabuni ya kutoa mafuta kutoka kule Ohima, Lake Albert - Uganda mpaka Tanga kwenye bandari ya Tanga. Lakini ukiangalia kitabu hichi hakizungumzi hata kidogo, hakuna hata mstari mmoja unaozungumzia kwamba Bandari ya Tanga itaboreshwa namna gani? Sasa hivi Bandari ya Tanga ina matatizo mengi, Bandari ya Tanga ina vitu ambavyo ni vichakavu, hata mashine za kubebea makontena ni taabu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hizi mashine za tag boats ambazo zinatakiwa kwenda kufunga meli baharini. Mashine ziko mbili, moja ni mbovu kabisa na nyingine tumekodisha kutoka Mombasa. Sasa sioni chochote ambacho kinaelezea mambo ya standard gauge kuhusiana na reli, sioni chochote ambacho kinaelezea kuhusiana na airport ya Tanga, mambo yote ambayo yanazungumzwa hapa ni standard gauge ya reli ya kati, au kwa sababu Waheshimiwa Wabunge wako kwenye mstari wa reli ya kati basi Tanga tunasahaulika? Kwa nini Tanga tunasahaulika?
Mheshimiwa Mwenyekiti, jana hapa Wabunge wa reli ya kati walikutana, sasa jamani Mheshimiwa Waziri nini sisi Tanga tumekukosea? Tumepata tender na hutaki kutupa chochote. Nimeona hapa maboresho ya Bandari ya Tanga ni shilingi milioni 7.6 kweli, are we serious? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nahamia sasa Jimboni kwangu kuna barabara kule, nimeangalia kwenye Hansard tangu mwaka 2000 barabara ya Amani - Muheza kilometa 40 imeanza kuzungumziwa, kwamba ijengwe kwa kiwango cha lami. Awamu ya Nne Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete aliahidi kuiweka barabara hiyo lami, Rais, Mheshimiwa Magufuli ameaihidi kuiweka lami barabara hiyo, Mheshimiwa Rais Mkapa ameiahidi kuiwekea lami barabara hiyo, na watu wote wa Amani wanategemea kwamba barabara hiyo itawekwa lami. Sasa hivi naangalia kwenye kitabu hapa naona shilingi milioni 250, nilitaka kuzirai Profesa, kwa sababu nitawaambia nini watu wa Amani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii inategemewa kule, uchumi wa Muheza unategea Amani, mazao ambayo yako Amani ni kitukingine. Amani kuna kila kitu, kuna si mambo ya utalii tu, mbao, karafuu, chai, hiliki, pilipili manga na mdalasini zote zinatoka kule.
Sasa mimi nitawaambia nini watu wa Muheza jamani? Nategemea kwa kweli Mheshimiwa Waziri utakapo-wind up jioni basi ueleze chochote ambacho kitahusiana na barabara ya lami ya Amani, Bandari ya Tanga, reli standard gauge tunataka Tanga na kiwanja cha ndege cha Mkoa wa Tanga utakifanya nini. Sioni chochote wala hata kugusiwa hakikugusiwa; na sasa hivi tunategemea kwamba mambo yatakuwa moto moto Tanga. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeahidiwa kilometa tatu, Rais, Mheshimiwa John Pombe Magufuli alifurahi wakati wa kampeni jinsi uwanja ulivyojaa, akasema Muheza mmenifurahisha nawapa kilometa tatu za lami vumbi limezidi, na hizo kilometa tatu mtazipata kabla ya mwezi wa sita; mpaka sasa hivi sioni kitu. Nimeangalia kwenye kitabu kuanzia page ya kwanza mpaka ya mwisho sioni chochote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri utakapokuja hapa kwa kweli utueleze na uwape matumaini watu wa Muheza hizo kilometa tatu za kuondoa vumbi Muheza utazifanya vipi, nitazipata namna gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna masuala mengine niliwahi kuwasiliana Mheshimiwa Waziri, hakuna mawasiliano huko Amani ambako ndiko kwenye uchumi wetu Muheza. Hakuna mawasiliano Amani, Zirai, Kwezitu, Mbomole kote kule huwezi kuongea na simu, ukiongea na simu mpaka upande juu ya miti ama kwenye kichuguu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana nategemea kwamba Mheshimiwa Waziri labda atakuja na majibu, ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nashukuru sana kupata fursa hii kuweza kuchangia hoja hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, nina mambo mawili, jambo la kwanza ningependa kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri Profesa Muhongo. Nampongeza kwa kazi aliyoifanya yeye na Watalaam wake ambao waliwezesha kupata tender ya kutoa mafuta kutoka kule Lake Albert Uganda mpaka Tanga bandarini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza kwa dhati kabisa, najua ilikuwa ni kazi kubwa, lakini mwishowe tumeipata! Pia nataka kusema tu kwamba Mheshimiwa Waziri tumepata hiyo kazi tunataka kujua kwamba tutafaidika vipi na hili bomba ambalo litapita kwenye Wilaya yangu na litaishia kwenye bandari yetu ya Tanga. Nafikiria kwamba ni vizuri wakajipanga na Waziri wa Uchukuzi kuona namna gani ambavyo wataweza kupanua bandari ya Tanga. Kuweka vitu vya kisasa kwenye bandari ya Tanga, kuhakikisha kwamba mafuta hayo basi, tunaweza kuyakidhi na kuyahudumia jinsi inavyotakiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ningefurahi sana kama Mheshimiwa Waziri angeitisha kikao ili tuone kwamba tutafaidika vipi, tu-sensitize na wananchi wetu tuweze kuona tunaweza kuongeza value gani kwenye hilo bomba na tunaweza kufaidika nini kwenye hilo bomba.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili, pia napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri kutokana na mradi wa REA. REA imetusaidia sana, REA imetusaidia kupata Majimbo haya na mpango huu ni mpango ambao unatakiwa uendelezwe hata kwenye Idara nyingine ambapo tutakuja kuchangia kwenye mada zinazofuata.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri Jimbo langu nafikiri linaweza kuwa ni Jimbo moja kubwa kuliko Majimbo yote hapa! Jimbo langu lina Kata 37, Vijiji 135, Vitongoji karibu 550, lakini mgao ambao umefanyika kwa REA awamu ya kwanza na awamu ya pili, vijiji ambavyo nimepata katika Jimbo la Muheza ni vichache sana! Namwomba Mheshimiwa Waziri aangalie kwa dhati kabisa aone kwamba hii awamu ya tatu, Jimbo la Muheza linaweza kufaidika namna gani. Nafikiri hatujazidi hata asilimia 40 kwenye mgao ambao tumepata! Vijiji vingi kwenye kila Tarafa, Jimbo lina Tarafa nne na kila Tarafa ina matatizo, kuna vijiji ambavyo havijapata umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Waziri aangalie, akitilia maanani pia Hale power station tunatoa karibu megawatts inaweza kuwa 20, pia ukijumlisha na Pangani tunatoa karibu megawatts 60. Kuna vijiji ambavyo viko karibu na power stations hizo, lakini usiku wao wanaangalia umeme kwa mbali tu. Kuna Vijiji vya Makole, Mhamba, Kwafungo na Songa vyote hivyo vinaangalia umeme usiku kwa mbali. Ningeomba aangalie kabisa aone ataweza kutusaidiaje!
Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu alipoteuliwa tu, ziara yake ya kwanza ilikuwa ni Hale na naamini aliweza kuwaona hao wanavijiji ingawaje Hale haiko kwenye Jimbo langu iko kwenye Jimbo la Korogwe. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri ningeshukuru na ningefurahi kama angeweza kuliangalia.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine sasa hivi Muheza tuna matatizo makubwa ya transformer, tunayo transformer ndogo na ambayo ni chakavu. Sasa Serikali inapata lawama kubwa sana ya umeme kuzimika zimika! Tungeomba Waziri atutafutie transformer kubwa, kwa sababu tunataka tufaidike na hilo bomba, tunataka tuifanye Muheza kiwe kituo cha matunda. Sasa kama hatutapata umeme wa uhakika ina maana kwamba hata hivyo viwanda ambavyo tunategemea kuvijenga Muheza vitakuwa ni matatizo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri tungeomba sana ajaribu kuliangalia suala hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la tatu ni Mkandarasi, nilishawahi kumwambia Waziri kwamba Mkandarasi Sengerema ana kazi nyingi sana! Speed anayokwenda nayo ni ndogo sana! Sasa nafikiri ni muhimu akampunguzia kazi ili tuweze kupata Mkandarasi mwingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana!
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Waziri kwa juhudi zake za kuhakikisha zabuni ya bomba la mafuta kutoka Ziwa Albert- Uganda hadi Bandari ya Tanga inafanikiwa. Namwomba aangalie uwezekano wa kusaidia vyombo mbalimbali bandari Tanga kwa sababu ni chakavu ili tupate vyombo vya kisasa zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nampongeza Waziri kwa mradi wa REA. Mradi huu ni moja ya sababu zilizotufanya tuingie Bungeni. Binafsi nina eneo la Jimbo kubwa kuliko Majimbo yote hapa Bungeni. Nina kata 37 na vijiji 135. Vijiji ambavyo nimefanikiwa kupata umeme ni asilimia ndogo sana ambayo haizidi asilimia 50. Namwomba sana Mheshimiwa Waziri REA III nipate mgao mkubwa. Nimetuma orodha ya vijiji 100 kwa kuanzia. Aidha, naomba anitatulie tatizo la transformer Mjini Muheza, kila siku umeme unakatika sababu ni uchakavu na ni dogo, limeelemewa.
Mheshimiwa Naibu Spika, mkandarasi Sengerema apunguziwe kazi. Kasi anayokwenda nayo kwenye mradi wa REA hairidhishi, anafanya taratibu sana. Aidha, utaratibu wa kuwekewa umeme usiruke kijiji kupunguza malalamiko ya vijiji vinavyorukwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la madini, ni kwa nini Serikali isianze mipango maalum ya kujenga kiwanda kikubwa cha kuanza kusafisha madini yetu hapahapa nchini. Mipango hii imekwishaanza nchi nyingine kama Zimbabwe, Botswana na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ni lazima iangalie uwezekano wa kuweka maeneo maalum ya madini ambapo wawekezaji wakija wanaweza kuonyeshwa moja kwa moja badala ya wawekezaji kuzungushwa. Aidha, wale walioshika maeneo bila ya kuyaendeleza wanyang‟anywe.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nashukuru sana kupata fursa hii ya kuweza kuchangia hoja hii ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Kwanza, napenda sana kumshukuru Mheshimiwa Lukuvi alikuja Muheza na alituletea ahueni kutokana na ziara yake hiyo. Wananchi wa Muheza wanamshukuru sana kwa sababu aliweza kurudisha mashamba karibu matano ambayo yanaonekana kwenye ukurasa wa 104 wa hotuba yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mashamba hayo ya katani yamekuwa ni ahueni sana kwa wana Muheza kwani yalikuwa yanawafanya wana Muheza wawe vibarua tu wa mashamba ya katani. Sasa hivi tunatengeneza mipango maalum ya kuhakikisha kwamba tunakuwa na master plan ya Wilaya ya Muheza ili kuhakikisha kwamba mashamba hayo ambayo tumeyapata yanakuwa kwa manufaa ya wana Muheza. Wananchi watagawiwa maeneo yao ambayo yapo na tutatenga maeneo maalum kwa ajili ya uwekezaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kitu muhimu sana ambacho tumekiweka na tunakisisitiza na tunahakikisha kwamba kwa kweli tunataka kuibadili Muheza. Nashukuru kwamba Waziri wa Viwanda yuko hapa, Waziri wa Kilimo yuko hapa, Waziri wa Miundombinu yupo hapa, Waziri anayeshughulika na TANESCO yuko hapa, Waziri wa Maji yuko hapa, tatizo sasa hivi linalotupata ni miundombinu, hatuna tatizo tena la ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua baadhi ya mashamba hayo yamevamiwa, lakini wana Muheza ni watu waungwana tutakaa chini, tutaongea na tutaona namna ya kutatua tatizo hilo. Kwa hiyo, tunamshukuru sana Mheshimiwa Waziri na tunataka kuhakikisha kwamba ardhi hiyo tunaitumia ipasavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu cha pili ni kwamba, yapo mashamba mengine ambayo bado hayajafutiwa hati. Mashamba ambayo yameshafutiwa hati ni kama shamba la Lewa, Bwembwera, Luhuwi, Kilapula, Kwa Fungo, Kihuwi lakini shamba la Kibaranga na Azimio bado sijayaona kwenye hiyo list. Kwa hiyo, tutashukuru kama mashamba hayo pia na yenyewe yataweza kufutiwa hati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo pia mashamba ambayo wanamiliki watu lakini hawalimi katani jinsi inavyotakiwa kulimwa. Wengine wanalima katani pembeni pembeni ili ukipita uone kwamba hili shamba linalimwa lakini ukienda katikati kuna pori kubwa sana. Nitampa Mheshimiwa Waziri list ya mashamba hayo na yenyewe pia tufanye mpango kwa wote ambao wanaweka mapori Muheza, mashamba hayo tuweze kuwanyang’anya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Mheshimiwa Waziri alipokuja alijionea mwenyewe watu walikuwa wengi sana, migogoro ya ardhi ni mingi sana na hii ambayo imeoneshwa kwenye page 33 kwamba ni migogoro sita ipo mingine ambayo sijaiona hapa na ambayo nitaiorodhesha na kumkabidhi. Hata hivyo, napenda kumshukuru kwamba migogoro hiyo imeanza kushughulikiwa. Mwezi uliopita timu yake ilikuwa Muheza na imeanza kutatua migogoro hiyo, napenda kumpongeza sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, migororo hii ya ardhi najua iko mingi, lakini nina hakika kwamba yote tutaitatua kwa wema tu na tutaelewana vizuri na wananchi wataelewa vizuri tu. Kwa hiyo, hii mingine iliyobaki Waziri pamoja na timu yake ningefurahi sana kama ningeambiwa watarudi ili waweze kushughulikia matatizo haya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Nyumba linafanya kazi nzuri ya kujenga nyumba, lakini kama walivyosema wenzangu tatizo kubwa ni bei zake, VAT iliyoko pale ni hela nyingi sana haina unafuu wowote kwa mwananchi. Sisi Muheza tumeshawapa eneo sehemu za Kibanda lakini tungeomba msukumo wa Waziri, tunataka wajenge nyumba za bei nafuu ili wananchi wa Muheza waweze kununua nyumba hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi Rais ameshatoa maelekezo haya mashirika yetu sasa yawekeze kwenye viwanda na mashamba na sisi tunayo mashamba na sehemu za kuweka viwanda. Ningependa shirika hili liwe mfano waje Muheza tuwape eneo waweke viwanda, tunataka kutengeneza kitu kinaitwa economic corridor ya Muheza. Kwa hiyo, nafasi tunazo na ningeshukuru sana kama National Housing watakuwa wa kwanza kuja kuwekeza Muheza na tunawakaribisha sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo kubwa ambalo tunalo pamoja na kuwa na mashamba hayo ni la vifaa kwenye Ofisi ya Ardhi, kwani vifaa hakuna kabisa inabidi tukodi labda kutoka Korogwe au Mkoani Tanga. Ningeomba Waziri awasaidie wale vijana wa pale ili wapate vifaa vya kupimia, tuanze kazi ya kuangalia tunapima namna gani kufuatana na master plan ambayo tutaitengeneza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, napenda kumwomba Waziri kwamba awasaidie TIC (Tanzania Investment Center) wawe na land bank inayoeleweka. Wana shida sana pale ya land bank. Wafadhili wanakwenda pale wanataka kuwekeza, wanataka kuleta mambo chungu nzima lakini land bank ambayo wanayo TIC ni ya watu binafsi. Kwa hiyo, ningeshukuru sana kama Waziri atashughulika na kuwasaidia TIC waweze kuwa na ardhi, mwekezaji anapofika anapelekwa moja kwa moja kwenye site na kuoneshwa kwamba ardhi hiyo hapo badala ya mwekezaji kuanza ku-negotiate na mtu binafsi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, namtakia Mheshimiwa Waziri kila la kheri na tunamkaribisha Muheza. Wana Muheza wanamkumbuka kwa jinsi alivyowaletea ufumbuzi na tunamhakikishia ardhi hiyo tutawagawia wana Muheza na tutaweka sehemu maalum za uwekezaji na tunawakaribisha sana. Nawashukuru sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kupata nafasi hii kuweza kuchangia hoja hii ya Wizara ya Maliasili na Utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja hii ni muhimu sana kwa sababu suala la Maliasili na Utalii ni kitu kimoja ambacho ni muhimu na kinachangia pato kubwa kwenye uchumi wa Taifa asilimia 17.3 siyo mchezo. Sasa kuna mambo mengi ambayo yapo ndani ya Wizara hii lakini mimi ningependa kujikita kwenye mambo ya hifadhi na pili kwenye suala la utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazo hifadhi nyingi sana lakini kuna hifadhi nyingine ambazo zimesahauliwa, kuna hifadhi ya misitu ya Amani kwa mfano, ni hifadhi kubwa ambayo ina hekta karibu 47,000 na ina mambo chungu nzima ndani yake. Kuna vitu ambavyo viko ndani ya msitu huo ambavyo havipatikani ulimwengu huu. Kuna vipepeo ndani ya msitu huo ambavyo huwezi kuvipata dunia yote hii, kuna kima weupe ambao wako mle, kuna nyoka wa ajabu ambayo mimi nilipata nafasi ya kuyaona pia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo ambayo yapo ndani ya msitu huo na ambayo naona kama Wizara hii haikuyaona kama ni muhimu na ndiyo maana msitu wa Amani imechangiwa kidogo sana kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri ukiangalia kwenye page 54, page 61, 62 na 63 ni kama imeguswa tu by the way. Lakini kuna mambo muhimu ambayo yapo huko kwenye msitu wa Amani ni msitu mkubwa na msitu ambao una mambo mengi sana kuna ua ambalo liko pale huwezi kulipata dunia nzima, kule Amani wanaliita Dungulushi. Hili ni ua ambalo lina harufu ambalo likichanganya na mambo ambayo yako kule Amani mambo ya hiliki, mambo ya karufuu sasa ile mandhari yake ambayo unaipata kule ni kitu tofauti sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Maofisa wa Mheshimiwa Waziri wamesahau kitu kama hicho kwamba Amani kuna vitu ambavyo ni muhimu, Amani kuna vitu ambavyo ni vya msingi na ingetakiwa waweke umuhimu sana kwenye hifadhi hiyo ya misitu. Pamoja na msitu huu kuwa na hekta 47,000, lakini pia umezungukwa na misitu mingine midogo midogo karibu sita ambayo ipo pembeni yake. Kuna misitu midogo kwa mfano msitu wa Derema, Lunguza, Tongwe Kwani, Nilo, Kambai, Manga, Mlinga yote ni misitu ambayo inazunguka pale Amani na kuufanya ule msitu uwe mkubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na mtafiti mmoja na mtalii mmoja ambaye alitembea hifadhi nyingi hapa duniani na alipofika pale Amani alishangaa sana namna ambavyo hatuupi ule msitu wa Amani. Aliulinganisha msitu wa Amani na Kisiwa kimoja kiko kule Amerika ya Kusini Ecuador, hicho kisiwa kinaitwa Galapagos muangalie kwenye ramani mtakiona. Kuna vitu ambavyo vina vutia zaidi sasa alipoangalia msitu wa Amani akaona msitu ulivyo jaa, ulivyo nona, akasema huu ni msitu kwa ulimwengu na hifadhi ambayo nimewahi kutembea huu unaweza kuwa wa pili duniani. Sasa hii ni kitu muhimu sana ambacho Mheshimiwa Waziri inabidi uangalie na uone umuhimu wa msitu huu ambao una kila aina ya vitu, viumbe mbalimbali ambavyo viko pale. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, msitu huu pamoja na kuwa ni wa asili kuna malalamiko ambayo wananchi wa Derema wako 1,128, ambao wamehamishwa kutoka kwenye ule msitu na kwamba tunaenda kuwapa maeneo mengine na wale wananchi fedha ambazo wamelipwa ni ndogo sana. Wananchi hawa wamezunguka wamekwenda Ikulu karibu sijui mara ngapi? Wamekwenda hapo Wizarani kwako Mheshimiwa Waziri sijui mara ngapi? Na mimi tu nilipokuwa Mbunge hii ni barua yangu ya tatu kukuandikia kwamba hawa wananchi 1,128 kwa nini wamepunjwa wamepewa hela kidogo mimea yao ambayo ilikuwa ndani ya hifadhi kama hiliki, karafuu ilikuwa ni mingi, lakini hela ambayo wamepewa wamekadiriwa ni kidogo sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, last week nimepokea barua kutoka Wizarani kwako inasema kwamba kufuatana na sheria hao walitakiwa walipwe sijui kila mche shilingi hizi, jamani, kila sheria general rules ina exception zake, kwa hiyo exception ambayo unaweza kuipa kutokana na umuhimu wa huo msitu mmeamua kuwahamisha hao watu jamani wapeni haki zao. Nitakuja kukuona Mheshimiwa Waziri, lakini ni muhimu sana uangalie namna gani mtaweza kuwapa hawa wananchi ambao wamelalamika, wamehangaika, wamekwenda kila ofisi wamekuja Dar es Salaam sijui mara ngapi kudai hizo haki zao lakini hawasikilizwi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hiyo tulisema kwamba hawa tunawahamishia kwenye shamba moja la Kibaranga pale ambalo shamba hilo ni haya ambayo yamerudishwa hati, lakini shamba la Kibaranga bado halijarudishwa hati na Mheshimiwa Lukuvi, Waziri wa Ardhi simuoni hapa lakini nilishamlalamikia kwamba tunasubiri hati inyang‟anywe ya shamba hilo tuweze kuwakabidhi hao wananchi wa Derema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana nasema kwamba kuna mambo mengine ambayo amesahau, kuna Pango la Amboni kule karibu na Muheza, Tanga pale. Sasa lile pango badala ya kuwa utalii limekuwa ni maficho ya magaidi, magaidi wako mle kila siku askari wanakwenda mle, kila siku wanawatoa, sasa sijui limesahauliwa kwamba siyo eneo moja la utalii au ni namna gani? Ninaomba Mheshimiwa Waziri suala hilo pia liangaliwe na hilo pango pia lipewe kipaumbele kwa sababu ni kitu kimoja muhimu sana. Kuna vitu ambavyo viko vya kihistoria kwenye vitu kama hivyo ambavyo tunatakiwa kuviangalia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Amani pamoja na kuwa na kutengeneza mbao za mitiki ni sehemu moja ambayo tunatengeneza mbao za mitiki, tuna mashamba makubwa sana ya mitiki pale. Mjerumani alitengeneza reli mpaka inafika Amani kwa ajili ya kuichukua mitiki, lakini hiyo reli imekufa na ndiyo maana nilikuwa napiga kelele kwamba ni muhimu tupate barabara ya lami ya kutoka Amani kilometa 40 mpaka Muheza. Kuna mambo chungu nzima ambayo yako pale ambayo yangeweza kuwa facilitated na huo mlima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niangalie suala la utalii kwa haraka haraka, utalii kama unavyoonekana kwa kweli haulingani, watalii ambao wanakuja hapa nchini hawalingani na vivutio ambavyo tunavyo. Tuna mbuga karibu zaidi ya 15 acha hizo hifadhi ambazo tunazo kubwa kabisa hapa ulimwenguni, nasikitika sana kusema kwamba utalii tunaingiza watalii milioni 1.1.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Victoria falls pale Zimbabwe wao Victoria Fall alone na wanaingiza watalii milioni mbili na nusu wanaingia pale kwa mwaka, tuna kila aina, jamani nafikiri Mheshimiwa Waziri inabidi uangalie namna gani ambavyo tunaweza kufanya au kuwafanya watalii waingie nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua njia moja ni hiyo kwamba hatuna ndege na ninashukuru sana kwa bajeti hii kuweka ndege. Watalii wengi wanapenda direct flight akitoka Ulaya moja kwa moja anatua hapa, kwa hiyo naamini kwamba hizo ndege ambazo zimepatikana mtazitumia vizuri na mtazipanga vizuri ili ziweze kutuletea watalii wengi hapa nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Mlima Kilimanjaro, ni muhimu sana mimi nilipata bahati ya kupanda Mlima Kilimanjaro mwaka juzi, mwezi Disemba. Ningefurahi sana mngetengeneza programu ya Waheshimiwa Wabunge wapande mlima huu ili waone huko njiani kukoje, lakini njiani hakulingani na hali halisi iliyopo huko Mlima Kilimanjaro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna vibanda ambavyo viko hapo Horombo, vingine vipo pale Kibo, watu wanalala kwa shida. Mheshimiwa Mbunge mmoja alizungumzia mambo ya vyoo, mimi nilipandia njia ya Marangu naomba viangaliwe. Vile vi-hut vimejengwa miaka sijui mingapi iliyopita, ukienda pale Kibo hut kuna vibanda ambavyo vimejengwa sijui lini? Sasa hii sijui kwa sababu labda viongozi hawapandi ule mlima na kuona matatizo ambayo yako mle, lakini ni vizuri wakayatatua....
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na muda kuwa mdogo, ningependa kuongeza mchango wangu niliozungumza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuwaombea wananchi 1,128 wa Derema wafikiriwe kuongezwa fidia, lakini bado hati ya shamba la Kibaranga tunapotegemea kuwahamishia haijapatikana, Waziri wa Ardhi anafahamu suala hili. Wizara ifikirie zaidi kuwaongezea vibali wanavijiji ambao wako karibu na shamba la Tiki. Wananchi hawa ambao ni vibarua wa shamba hilo la Derema wanalalamika kwa kupewa vibali vichache mno.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ifikirie kuanzisha Chuo cha Hifadhi ya Asili ambacho hakuna hapa Afrika Mashariki na Kati. Muheza tutakuwa tayari kutoa eneo la chuo hicho. Ili kuongeza watalii nchini, pamoja na kununua ndege tatu ambazo hakikisha kati ya hizo zilenge nchi zenye watalii wengi, ni vizuri kuongeza au kuwatafuta tour operators, ambao wanaweza kufungua ofisi hizo kwa wingi nje ya nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ifikirie kuboresha sehemu ya kituo cha Horombo ambacho ni njia ya kupanda Mlima Kilimanjaro. Iboreshe kukuza utalii wa ndani ili kuwawezesha wananchi kufika hapo kwa kuwa magari yanafika na wengi wanaweza kufika na kuona milima yote vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, askari wanyamapori waendelee kupata mafunzo zaidi na waajiriwe wengi kukidhi mbuga zote.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kupata nafasi hii adimu ya kuweza kuchangia hoja hii. Suala la maji ni suala ambalo linamgusa kila mtu katika ukumbi huu. Kila mtu katika eneo lake, katika Jimbo lake ana tatizo la maji na tatizo ni kubwa sana. Ningependa kuchukua ushauri ambao umetolewa hapa wa kuanzisha wakala wa maji vijijini. Ni ushauri muhimu na ni ushauri ambao ni lazima tujifunze na mafanikio ambayo yametokea au yamepatikana kwa REA. REA imetusaidia sana, imesaidia sana kwenye mambo ya Kampeni, sasa ni kwa nini tunashindwa kuanzisha huo Wakala wa Maji Vijijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tabu ambazo Jimbo la Muheza linapata katika suala la maji sijui naweza kufananisha na nini, sijui ni sugu au sijui ni nini, lakini wananchi wa Muheza wana matatizo makubwa sana ya maji. Kuanzia pale mjini mpaka vijijini akina mama wanapata tabu sana ya maji wanashinda kwenye visima, na ukiangalia hayo maji ambayo wanayashindia huku visimani huwezi ukaamini. Wakati wa kampeni nilikuwa nakaribishwa na ndoo na nikaoneshwa maji ni udongo mtupu, maji sio salama kabisa. Kwa hiyo, kuna mambo mengi ambayo yanafanyika ambayo unaona wewe mwenyewe kama binadamu kwa kweli unashindwa. (Makofi)
Mheshimwa Mwenyekiti, tunayo Hospitali teule pale, Hospitali teule ya Wilaya inashindwa kufanya operation kwa sababu hakuna maji, kwa hiyo maji ni tatizo kubwa sana Wilayani Muheza. Nimefarijika kuona kwamba kuna mpango ambao upo ndani ya kitabu cha Mheshimiwa Waziri kwamba mpango wa kutoa maji kutoka Mto Zigi ambao ni kilomita ishirini na mbili na nusu kutoka Muheza mjini mpaka mto Zigi Amani kule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanga wanatumia maji kutoka Mto Zigi na sisi wenyewe hatuna maji tulishakubaliana na watu wa Tanga kwamba na walishayapima kwamba maji hayo yana uwezo wa kutosheleza Muheza na Tanga yote na maji hayo kuna uwezo wa kuweza kukaa kwa miaka 30 ijayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo umefanyika utafiti wa mwanzoni, sijui imekuja Kampuni moja ya Hispania pale, EUROFINSA, Wizara ya Maji hii, Waziri kwenye bajeti iliyopita hapa Hansard nimeangalia ameahidi kabisa kwamba hao EUROFINSA watakuja na wataweka maji. Upembuzi yakinifu ulishafanyika na nimeona hapa kwenye miradi mikubwa 17 ya maji ambayo tunategemea labda, tunamwombea Mheshimiwa Waziri afanikiwe kupata hizo fedha ili huo mradi uweze kuanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru Mheshimiwa Waziri kwamba, anafahamu matatizo ya Muheza, amefika Muheza na ndiyo maana kwenye mradi huo ameuweka wa kwanza Muheza. Kwa hiyo, nataka wakati atakapokuja ku-wind up awahakikishie wananchi wa Muheza kwamba maji kutoka mto Zigi safari hii yatateremshwa. Awamu ya Tano imedhamiria na itateremsha maji hayo kutoka Mto Zigi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimefarijika kuona kwamba Mheshimiwa Waziri vijijini ametoa fedha ambazo ni karibu bilioni moja point moja na ushehe.
Kwa hiyo, fedha hizo namwomba zije zote, tutahakikisha kwamba maji vijijini Muheza kote wanaweza kupata na tutawachimbia visima na kuhakikisha kwamba maji hayo ni salama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeangalia kwenye kitabu cha Mheshimiwa Waziri sikuona fungu lolote la kusaidia maji Mjini Muheza. Ningeomba aangalie ataweza kunisaidia namna gani kuweza kuweka at least fedha kidogo katika maji Mjini Muheza, tuangalie uwezekano wa kuvuta maji kwenye visima ambavyo ni vingi na vinatoa maji kwa wingi, kuweza kuyasambaza kwa sababu ardhi ya Muheza ni chumvi kubwa sana ambayo iko pale kiasi kwamba hata ukichimba visima basi yatatoka magadi matupu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kitu ambacho Mheshimiwa Waziri anataka kufanya ni kuangalia vile visima vyenye maji mengi na kuangalia jinsi ya kuweza kuyatoa yale maji na kuyasambaza kwenye visima ambavyo viko karibu karibu. Nashukuru sana isipokuwa nilikuwa nashauri kwamba suala hili la maji hasa katika Jimbo la Muheza Mheshimiwa Waziri alipe kipaumbele kwa sababu 2020..
Mheshimiwa Menyekiti, naomba kuunga mkono hoja .
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kupata nafasi hii, kuchangia hoja hii ya Mambo ya Nchi za Nje. Nashukuru sana kwa sababu Wizara hii ni Wizara ambayo ni muhimu sana, Wizara ambayo inatuunganisha na mambo yetu huko nje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa tu kukuhakikishia kwamba Mabalozi ambao wako nje, Mabalozi ambao wameteuliwa na Mheshimiwa Rais huko nje wanafanyakazi nzuri sana. Wanafanya kazi nzuri na wanajenga, wanatoa sifa kubwa kwa nchi yetu ya Tanzania. Sisi ambao tumekuwa Mabalozi huko nje tunaelewa uthamini ambao tulikuwa tunapewa, heshima ambayo tulikuwa tunaipata huko nje na consultation nyingi nchi ya Tanzania, Mabalozi ambao wako nje walikuwa wanakuwa consulted kwa ushauri na kwa kila kitu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemshangaa sana Mheshimiwa Waziri Kivuli, anapotupiga critic na kutulinganisha na Wajumbe wa Nyumba Kumi Kumi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli unaweza ukanilinganisha mimi na Mjumbe wa Nyuma Kumi Kumi? Unaweza kumlinganisha Balozi Mahiga na Mjumbe wa Nyumba Kumi Kumi, amekuwa Balozi wetu kwenye Umoja wa Mataifa kwa miaka kemkem mpaka Katibu Mkuu mwenyewe Ban Ki –Moon, akasema kwamba, hapana wewe umefanya kazi nzuri akampa kazi Somalia. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimekuwa Balozi na kiongozi wa Mabalozi Zimbambwe kwa miaka chungu nzima, Mheshimiwa Msigwa unaweza kusema hivyo kweli? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi Mheshimiwa Msigwa nilikuonya nikakwambia kwamba, ushauri ambao tunakupa kwenye Kamati, usiuchukuwe ushauri huo ukaugeuza kwamba ndiyo critic na ndiyo ulichokifanya hicho. (Makofi/ Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri mwingi ambao umeuzungumza hapa ni ushauri ambao tumeupa Wizara kwamba vitu gani muhimu ambavyo wanatakiwa kuvifanya. Sasa yeye kazigeuza kwamba ndiyo critic, ndiyo madongo ya Wizara, hapana hivyo, hatuendi hivyo Mheshimiwa Msigwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kusema ni kwamba, kazi ambayo wanafanyika huko ni kubwa na heshima ambayo tunaipata huko nje ni kubwa na Mabalozi hawa msiwakatishe tamaa, wanafanya kazi nzuri sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia diplomasia ya uchumi, wameleta wawekezaji chungu nzima hapa. Mimi mwenyewe nimeshaleta wawekezaji chungu nzima hapa, wamekuza biashara chungu nzima na nchi yetu na nchi za nje. Jamani tusiwakatishe tamaa, tuzidi kuwaunga mkono, Mabalozi hawa kazi wanayofanya ni kubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachokisema sasa hivi, Foreign Policy ya kwetu inabidi ibadilike kwamba zamani foreign policy ilikuwa politically, inakwenda politically, lakini sasa hivi ni lazima twende na hali halisi inavyokwenda duniani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na tumeishauri Wizara kwamba, ni lazima waangalie wanapoanzisha Balozi sasa hivi waanzishe balozi sio politically, waangalie kwamba tunaweza kufaidika vipi kiuchumi na ndiyo maana sasa hivi unakuta kwamba Balozi wana mipango, ambayo tumeshauri, sisi tumeishauri Kamati kwamba ni lazima wahakikishe kwamba wanaanzisha Balozi kwenye zile nchi, ambazo wanaona kwamba tunaweza kupata wawekezaji, kukuza biashara zetu na tunaweza pia kuleta watalii wengi hapa nchini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na ndiyo maana sasa hivi Wizara ina malengo makubwa sana ya kuanzisha ubalozi kule Uturuki, Qatar, South Korea na sehemu nyingine nyingi. Kwa hiyo, ni suala ambalo tunatakiwa tuwaunge mkono na tuhakikishe kwamba, wanapata fedha za kutosha kwa sababu diplomasia…. aaha!
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, ahsante sana.
Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga hoja mkono na kuwapongeza sana Mawaziri wote kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya pamoja na kazi nzuri ya usimamiaji wa mazingira inayofanyika. Napenda Wizara itoe pia kipaumbele cha vijiji ambavyo vinazunguka vyanzo vya maji kuhakikisha vyanzo hivyo vinatunzwa na kulindwa vizuri na wananchi hao. Wananchi hao inabidi na wao wafaidike na vyanzo hivyo vya maji kwa mfano; maji ambayo yanatumika Mkoani Tanga yanatoka Mto Zigi Wilayani Muheza. Tarafa ya Amani wanavijiji wanaokaa maeneo hayo kama Amani, Zirai Misarai, Mbomole, Mashewa, kwendimu na kadhalika maji wanayotumia yanatiririka bila kuwekwa vizuri. Hawasaidiwi kuweka maji hayo kuwa safi na salama. Ni vizuri Wizara ikashirikiana na Wizara ya Maji ili wananchi hawa wasigeuke kuharibu mazingira ya vyanzo hivyo. Wapewe motisha na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na pigeni kazi na nashukuru Mheshimiwa Waziri kufika Mto Zigi.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017
MHE. BALOZI ADADI. M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nashukuru sana kupata nafasi hii ya kuchangia taarifa za Kamati hii. Kwanza nawapongeza Wenyeviti wote wa Kamati kwa mchanganuo mzuri na mambo mazuri, mapendekezo na maoni ambayo wameyatoa kwenye Kamati zao. Nitajikita kwenye Kamati zote mbili kwa kifupi sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Kamati ya Katiba nilitegemea sana wangeweka msisitizo pia pamoja na mambo mengine suala la msongamano na ucheleweshaji wa kesi Mahakamani. Kamati hii ya Katiba ina mwingiliano sana na Kamati yangu ya Mambo ya Nchi za Nje, Ulinzi na Usalama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati yangu imetembelea sana Magereza na imeona namna ambavyo mahabusu pamoja na wafungwa walivyosongamana ndani ya Magereza, ni tatizo kubwa sana. Tatizo hili linatokana hasa na makosa mawili tu au matatu. Utaona makosa ya mauaji na makosa ya madawa ya kulevya ndiyo ambayo yanachukua muda mrefu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mahabusu wako wengi sana wa makosa ya mauaji, madawa ya kulevya na Wahamiaji haramu. Sasa hawa watu wamekaa gerezani muda mrefu, mtu anakaa miaka miwili, mitatu, minne anasubiri apangiwe kesi Mahakama Kuu. Kwa hiyo unaona kwamba Kamati hii ilikuwa na uwezo wa ku-force Serikali hasa Mahakama Kuu kuangalia uwezekano wa kubadilisha taratibu zao, kanuni zao kuendana na wakati kwa sababu mahabusu wanakaa sana wakisubiri kesi zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kitu kinaitwa hiyo High Court Session. High Court Session inapangwa, inaweza kukaa miaka mitatu mahabusu wanasubiri High Court Session iweze kuitwa. Ni muhimu sasa hivi Kamati ipendekeze kwa Jaji Mkuu waangalie uwezekano wa kubadilisha kitu kinaitwa High Court session.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wafungwa kule ambao wamehukumiwa kunyongwa. Wamejaza Magereza na kama unavyojua ukihukumiwa kunyongwa hufanyi kazi yoyote, wanakula tu, wanasubiri kunyongwa. Kunyongwa kwenyewe hakujulikani watanyongwa lini. Sasa sijui mamlaka zinazohusika zinafikiria namna gani kwa sababu wanaendelea. Sasa hivi karibu miaka ishirini, thelathini kuna watu wamehukumiwa kunyongwa wako kule hawanyongwi, vifaa vya kunyongea vimekaa mpaka vimeota kutu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vizuri kama sheria hiyo mamlaka inaona kwamba haitekelezeki basi iletwe Bungeni tuifute, maana hata kwenye kupunguziwa adhabu wafungwa ambao wanataka kupunguziwa adhabu wale waliohukumiwa kunyongwa hawapunguziwi adhabu hata siku moja sasa sijui ni kwa nini. Ni vizuri suala hilo Kamati pia ingeshauri ili tuibane Serikali ili mamlaka zinazohusika zifikie maamuzi ya hawa watu ambao wamehukumiwa kunyongwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama mamlaka zinazohusika zinashindwa basi zirekebishe ziteremshe kwa Mwakyembe huenda atasaini watu wanyongwe, lakini vinginevyo kwa kweli wanajaa na wahamiaji haramu ambao wako mle wanajaa. Maafisa uhamiaji, mhamiaji haramu anakosa anamtupa jela hata bila kupelekwa Mahakamani. Ni vizuri Sheria hiyo pia iangaliwe na kuletwa hapa Bungeni tuweze kuiangalia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la ajali. Suala la ajali ni kubwa sana na zinaleta athari kubwa sana. Watu wanakufa sana kwa ajali, watu wanapata vilema kwa ajali. Nilitegemea pia tuungane na Kamati hii ya Katiba na Sheria tuweze kulazimisha Serikali ilete mapendekezo ya kubadilisha suala hilo, kwa sababu mambo mengi ambayo yanatokana na ajali ni mambo personal (mtu binafsi). Ajali ambazo zinatokea karibu asilimia 70 na ushee zinatokana na matatizo ya mtu binafsi. Ni vizuri Sheria hiyo tukaiangalia upya na iletwe Bungeni tuweze kuifanyia marekebisho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye Kamati ya Utawala Bora na Serikali za Mitaa, hii kitu inaitwa TAMISEMI. TAMISEMI ni jalala, limechukua kila kitu. Kwenye Majimbo yetu huwezi ukazungumza chochote bila kuangalia TAMISEMI. Ukiangalia afya TAMISEMI, sijui shule TAMISEMI, barabara TAMISEMI, matatizo ya maji TAMISEMI.
Mheshimiwa Mwenyekiti, TAMISEMI ina mambo mengi sana na kwenye Halmashauri inakuwa ni tatizo, kwa sababu tuna mipango mizuri ya kutekeleza bajeti hii ya TAMISEMI lakini hela hakuna, hela zimeanza kuja juzi. Nashauri tu kwamba, tuilazimishe Serikali hizi fedha zilizopangwa kwenye Halmashauri zetu ziletwe kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi Muheza tuna mipango mingi sana ambayo tumepanga kwenye bajeti, lakini mpaka sasa hivi sijui hata kama robo zimefika ambazo tumepokea kwenye mpango wa maendeleo. Kwa hiyo, naomba hela hizi ziletwe ili tuweze kukamilisha mambo ambayo yamepitishwa hapa Bungeni na mambo mengi ya maendeleo ambayo tumeamua kuyafanya katika kipindi hiki cha fedha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Madaraka ya Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa; suala hili sasa hivi linakwenda kubaya na nashauri Serikali iliangalie kwa kina. Hawa Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa wanaonekana hawajapata semina yoyote ya kuelewa madaraka ya ukamataji. Wao wanaelewa tu mtu mpeleke ndani. Mtu amekubishia kwenye mkutano unaamua akamatwe apelekwe ndani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, askari Polisi anachukua miezi sita kusomea namna ya kumkamata mtu, namna ya kuondoa haki ya mtu, sasa huwezi ukajibishana na mtu tu kwenye mkutano wewe Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa unaamua huyu mtu umweke ndani. Ni suala ambalo ni sensitive na ningeshauri Kamati suala hili tuwabane Serikali hawa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wapate semina, waelewe maana ya ukamataji, waelewe maana ya kuweka watu ndani vinginevyo itakuwa chaos hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa sana kupongeza suala la mradi wa mabasi wa DART, ni mradi ambao unatakiwa upongezwe. Kwa kweli huu mradi sijui kwa nini umechelewa, lakini haya mabasi yangeweza kuwa kwenye Jiji la Dar es Salaam sasa hivi naamini Dar es Salaam upungufu huu wa usafiri ungeweza kupungua kwa kiasi kikubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili suala ambalo ndugu yangu aliyesema la kutoa matairi alilosema Mheshimiwa Rais, zile ni mbinu za Askari, Rais amewashauri tu Askari namna ya kufanya kazi zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti kwa hiyo, si kutoa matairi ni vielelezo mojawapo ambavyo vitatolewa Mahakamani kuthibitisha huyu mtu alikuwa anaingia kwenye barabara ya mwendokasi. Ile ni barabara ya mabasi ya mwendokasi na yanapokukuta wewe ni maiti. Sasa ni lazima askari wawe wakali na wahakikishe kwamba kweli wanatekeleza hizo sheria inavyopaswa. Kwa hiyo, Rais alifanya kuwashauri tu askari, hiyo ni mbinu mojawapo ya kuwakamata hao watu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge ni suala ambalo tunatakiwa tulipongeze kwamba hawa wapanda bodaboda wanapoingilia haya mabasi kwa kweli waelewe kwamba ni kifo. Kwa hiyo, ni lazima kwamba Sheria iwe kali kwenye suala hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia napongeza sana suala la TASAF, suala ambalo linatujengea imani sana kwa wananchi. Kuna matatizo madogo madogo ambayo wanatakiwa wayarekebishe lakini huu mpango wa TASAF uongezwe na tunaunga mkono sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono mapendekezo yote na ningeshukuru mapendekezo haya ambayo tumeyashauri, basi yachukuliwe ili tuwabane Serikali vizuri, nakushukuru sana.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kupata nafasi hii
kuweza kuchangia hoja hii ya Kamati. Kwanza kabisa ningependa kupongeza sana Wizara hii
ya miundombinu, kwa kiwango kikubwa katika miezi sita hii ambayo tumekuwa nayo
imeonyesha dalala kweli kwamba kuna mambo ambayo yanaonekana kabisa na ni dhahiri
kabisa kwamba wamejitahidi kwa kadri ya uwezo wao. Waziri mwenyewe, Mheshimiwa Profesa
ametembea nafikiri nchi nzima hii nilikuwa kila nikiangalia television naangalia anapumzika
wakati gani lakini naamini kabisa amefika mikoa yote kwenye nchi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, utaona tu ni dhahiri kabisa ametuletea ndege zimeletwa hapa
bombardier mbili na nyingine zinakuja, mkataba wa reli umetiwa saini juzijuzi hapa, barabara
wametengeneza karibu kilometa 400 za lami, kuna flyovers ambazo zimeanza kuonekana pale
TAZARA, madaraja ya Coco Beach yameanza kushughulikiwa na magati mengi kule bandarini.
Kwa hiyo, ninachosema ni kwamba Wizara hii ya Miundombinu kwa kiasi fulani imejitahidi na
imetoa nuru ya Awamu ya Tano ni kitu gani ambayo inataka katika hiki kipindi cha miezi sita.
(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na mambo mengi ambayo imeyafanya especially
mambo ya reli, lakini utaona kwamba reli yetu ya Tanga kidogo imesahaulika na sijui ni kwa nini,
katika taarifa ya Kamati kwa kweli ingebidi na reli hii ya Tanga iangaliwe, hatuwezi kusubiri
mpaka reli ya kati imalizike ndiyo mipango wa kuanza kushughulikia reli ya Tanga ianzishwe.
Kwa hiyo, ningeomba vitu hivi viende kwa pamoja, simultaneously, huku inafanyika na huku
inafanyika kidogo.
Kuna suala la bandari pia, bandari Tanga sijaona kitu chochote ambacho kimefanyika
ukitilia maanani kwamba kuna bomba la mafuta ambalo linafanyika lakini mipango ya
kupanua ile bandari ya Tanga ili kuweza kukidhi mahitaji ya hili bomba ambalo linakuja bado
sijaiona. Kwa hiyo, ningeshauri Kamati iitake Serikali maandalizi hayo yaanze mapema ili n watu
wa Tanga waanze kufaidika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la barabara ambazo Wizara hii imejitahidi sana kwenye
kilometa 400 lakini barabara hasa jimboni kwangu, sijaiona na ninaomba Mheshimiwa Waziri
usisahau kuiingiza kwenye bajeti inayokuja barabara kilometa 40 ya Amani mpaka Muheza, ni
barabara muhimu sana na ambayo sasa hivi ina matatizo sana ya kuipitika. Kwa hiyo,
wananchi wa Muheza wanaamini kwamba safari hii barabara hiyo basi itawekwa kwenye
bajeti hii.
Vilevile kutokana na ukame ambao upo sasa hivi tunategemea kwamba ahadi zile za
Mheshimiwa Rais za kilometa tatu ambazo alituahidi pale Muheza basi zitatekelezwa kwa
sababu vumbi limekuwa kbwa na ukame umeongeza vumbi, basi tunategemea hizo kilometa
tatu tukipata lami kidogo tutapata ahueni ya lami. (Makofi)
Kuhusu mawasiliano, kuna tatizo kubwa, hasa kwenye Mlima wa Amani kule, ambapo
redio hazisikiki, simu hazisikiki na nilikwishamuomba Mheshimiwa Waziri ili aweze kuliangalia
tupate minara maana yake hatupati mawasiliano kabisa maeneo ya Amani, tarafa yote nzima,
vijiji vya Ngomole, vijiji vya Zirai, Vijiji vya Kwezitu, inakuwa mawasiliano ni matatizo makubwa
sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, labda nije kwenye Wizara ya Nishati na Madini; ishu ya bomba
la mafuta kutoka kule Hoima, Uganda mpaka Bandari yetu ya Tanga linasisimua sana pale
Mkoani Tanga na linasisimua sana hata Muheza. Lakini sijaona fukutofukuto lolote ambalo
wananchi wanaweza kusema kwamba sasa hivi hii kitu inafanyika, tunaona mkataba umetiwa
saini, lakini hatuoni…
Mheshimiwa Naibu Spika, REA Awamu ya Tatu…
NAIBU SPIKA: Muda umekwisha Mheshimiwa.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante
sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga hoja mkono. Aidha, naomba kuchangia katika maeneo mawili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ucheleweshaji wa kesi hususan za jinai Mahakamani ni tatizo kubwa sana ambalo linahusisha Wizara nyingine kuu za Mambo ya Ndani. Makosa ya mauaji ni moja ya makosa ambayo watuhumiwa wake wanakaa muda mrefu mahabusu. Nashauri Serikali iangalie upya utaratibu wa High Court Session ili kesi hizo zisichukue muda mrefu kama inavyochukua wakati huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mahabusu pia ambao wanahukumiwa kifo utekelezaji wake haufanyiki vizuri. Suala hilo likaangaliwe mawakili wa Serikali maslahi yao yaangaliwe upya. Mishahara na marupurupu yao ni midogo sana ukilinganisha na kazi zinavyofanyika.
Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB - MWENYEKITI KAMATI YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nashukuru sana kwa kupata nafasi hii kumalizia hii hoja. Hoja hii imechangiwa na Waheshimiwa Wabunge 29. Waheshimiwa Wabunge 23 wamepata nafasi ya kuzungumza na sita wameweza kuleta kwa maandishi. Mheshimiwa Mwenyekiti, nawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge michango yao yote tutaichukua na kuboresha kwenye maazimio yetu. Nawashukuru pia Waheshimiwa Mawaziri, Manaibu Waziri kwa michango yao ambayo ni muhimu sana kwenye Kamati hii ambayo inajumuisha karibu Wizara tatu na nne. Mheshimiwa Mwenyekiti, nawashukuru pia wana Kamati wenzangu, wamefanyakazi nzuri sana na wengine kwa kweli wamekuwa na roho ngumu; hata tulipoingia kwenye Magereza na kuwaona wafungwa na mahabusu jinsi walivyo, wengine machozi yaliwatoka. Nawashukuru sana kwa kuwa wavumilivu. Mheshmiwa Mwenyekiti, amani na utulivu katika nchi yoyote ile ni jambo la msingi sana. Tukichezea amani na utulivu, naamini hatuwezi kukaa. Kuna mifano mingi sana ambayo ipo kwenye ulimwengu huu. Nchi ambazo zimechezea amani na matokeo yake wanayaona na wasingeweza kukaa hata kwenye ukumbi wa Bunge kama hivi. Sisi kama Kamati yetu tutajaribu kwa kadri tunavyoweza kushauri Serikali namna ya amani na utulivu umuhimu wake unavyotakiwa. Mheshimiwa Mwenyekiti, majukumu haya ambayo yote yapo kwenye Wizara hizi; za Mambo ya Ndani na Mambo ya Ulinzi na Usalama yanahitaji fedha; lakini kwenye Wizara zote hizi tatu ambazo tumezizungumza zote zimeonekana kuna upungufu wa fedha. Fedha ambazo zimepitishwa na Bunge lako Tukufu hili, zimeshindwa kuwafikia wahusika ili waweze kufanya shughuli za maendeleo. Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati imetembea kwenye baadhi ya Magereza na baadhi ya Magereza mengine tumekuta wafungwa wanadai vyombo, zana za kufanyia kazi ya kilimo. Wanasema tunaomba matrekta, tuna ardhi iko hapo imejaa na tuna hela zetu. Ni Gereza la Songwe wanasema tuna hela zetu shilingi milioni 40 ziko kule kwenye akaunti, tupeni tununue matrekta. Sijui kwa nini, nafikiri Waziri wa Fedha na Waziri wa Mambo ya Ndani, atakuwa analisikia. Toeni hizo hela na kuacha huo urasimu, wapeni wafungwa walime.
Mheshimiwa Mwenyekiti, msongamano wa mahabusu kwa kweli ni tatizo kubwa sana. Kama nilivyosema kwenye taarifa yetu, kuna watu wamekaa Magerezani kwa miaka mine mpaka mitano kwa makosa ya mauaji na madawa ya kulevya; kitu ninachongojewa ni kitu kinaitwa High Court Session. Polisi na Mahakama zimefanya kazi nyingi sana za kesi ndogo ndogo, bado hizi kesi kubwa. Mahakama Kuu kuna nini? Kwa nini hambadilishi taratibu za kuangalia kubadilisha huu mfumo wa High Court Session ambao unawaweka mahabusu muda mrefu ndani ya Magereza? Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kuhusu, msongamano wa mahabusu ambao unaambatana na hiyo kwa kweli ni suala ambalo linatakiwa lishughulikiwe. Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje, Waheshimiwa Wabunge wamezungumza na tumetoa mapendekezo na maoni ambayo tunaona ni muhimu yaweze kuchukuliwa, isipokuwa cha msingi ni fedha ziende kwenye Balozi nje ya nchi. Mabalozi kule hawana hela. Hela tumepitisha lakini haziendi. Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa mabalozi watatumika sana kwenye diplomasia ya uchumi. Wao wana uwezo mkubwa sana wa kuleta Wawekezaji hapa na watalii. Tuwapelekee fedha, tuwawezeshe waweze kufanya hayo mambo. Hii ni pamoja na Mabalozi ambao wako hapa nje; nyumba nyingi tu; mfano huo wa Sweden ni mmoja, lakini nyumba nyingi za Mabalozi ziko kwenye hali mbaya na zinahitaji kuboreshwa. Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepata mchango wa Mheshimiwa Bilago. Warundi wamejaa kwenye Gereza la Kibondo, kwa sababu pale ni mpakani, huwa kuna utaratibu wa mikutano ya ujirani mwema. Waburundi wanakuja na sisi tunakwenda, tunanunua vitu na wao wananunua vitu. Sasa wanapokuja wale, unawakamata kwamba wameingia nchini isivyo halali, unawajaza kwenye Magereza, kwa kweli siyo haki. Waziri wa Mambo ya Ndani na Serikali iliangalie hilo ikafanye mikutano ya ujirani mwema kuondoa hilo tatizo. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, Polisi wanafanya kazi nzuri sana na mpaka sasa hivi wamepunguza uhalifu kwa kiwango kikubwa sana, tukichukulia uhalifu in totality; lakini hawana nyenzo. Bajeti ambayo tumeipitisha hapa kuwapa fedha, hawajapata hizo hela, au kama wamepata, zote zimekwisha. Sasa tusiwafanye Polisi wawe ombaomba, isipokuwa naitaka Serikali iangalie hilo suala na kuhakikisha fedha ambazo tumepitisha hapa, basi Polisi wale wanapewa. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, Madawa ya kulevya ni tatizo kubwa, watoto wetu wameharibika, Watanzania wanakamatwa sana huko nje. Sisi tunaweza kuwafuatia Nigeria sasa hivi. Kwa hiyo, wamejaa kwenye Magereza ya nje, ni vita. Nami naomba tutakaporudi kwenye Majimbo yetu tuwasaidie kutoa taarifa ya wote wanaohusika na madawa ya kulevya. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kusema, Makamanda wa Mikoani wa Polisi na Makamanda wa Wilaya, wana jukumu kubwa sana la kuwasaidia Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya. Ni lazima wafuate taratibu za upelelezi. Taratibu za upelelezi zipo wazi. Upelelezi ni profession jamani. Kuna doctorate ya investigation inachukuliwa. Upelelezi hauendi hivi hivi. Huwezi ukatoa upelelezi kwa kutaja watu majina, hakuna! Mimi sijawahi kuona kitu kama hicho. Kwa hiyo, ninachotaka kusema ni kwamba Makamanda wa Polisi na wa Wilaya, waangalie. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, zipo Police General Orders, Police Force Ordinance na Criminal Procedure Act ambazo zinaeleza kabisa namna ya Polisi kutekeleza majukumu yake. Kwa hiyo, kinachotakiwa ni kukaa pamoja na hao Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kuwasaidia. (Makofi) Waheshimiwa Wabunge, mtakumbuka wakati Mheshimiwa Lyatonga Mrema alipokuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, mimi nilikuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam na alifanya kazi kubwa sana, lakini kulikuwa na kazi nyingine anakwenda nje, kinyume. Nikasema tukimwacha Mheshimiwa Lyatonga aende hivi, ataharibu kesi Mahakamani. Ikabidi Wakuu wakae na Mheshimiwa Mrema, wakaelekezana taratibu za kufanya na Polisi walimpa support na mambo yakawa yanakwenda vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nashauri kwamba Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Wilaya wakae na Wakuu wa Mikoa wao na Wakuu wa Wilaya zao, waangalie na kuwashauri namna ya kugawanya hizi kazi. Hawa Makamanda wamesomea, wanaelewa. Wamekwenda kwenye vyuo mbalimbali, wanaelewa taratibu. Hatutaki waharibu hizi kesi nzuri au hii operation nzuri ambayo imeanza ili kesi hizi ziende kufa kule Mahakamani. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nawahakikishia Waheshimiwa Wabunge kwamba yote ambayo mmeyaongea na kushauri tutayachukua na tutaweka kwenye maazimio yetu na ninawahakikishia kwamba tutaunda Kamati Maalum ya kufuatilia yote ambayo tumeyasema ili kuhakikisha kwamba kabla hatujatoa report nyingine mwaka kesho, basi tutatoa utekelezaji wa maazimio haya. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, kwa niaba ya Kamati ya Mambo ya Nchi za Nje, Ulinzi na Usalama, napenda kuwasilisha taarifa yangu na naomba kutoa hoja.
Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.
MHE. BALOZI ADADI RAJABU: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuunga hoja mkono na kuwapongeza wote; Mheshimiwa Waziri, Naibu, Katibu Mkuu na Watendaji wote kwa kazi kubwa wanayoifanya. Naomba kuchangia kwenye maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Taasisi ya NIMR ni muhimu sana na ina sifa kubwa kwa tafiti mbalimbali za magonjwa ya binadamu Afrika na dunia kwa ujumla. Taasisi hii tawi lake lipo Muheza na lina mpango mahususi kabisa wa kuanzisha Chuo Kikuu kwa msisitizo wa masomo haya ya Tafiti za Binadamu, masomo ambayo hayapo hapa Afrika. Majengo yapo ila yanahitaji ukarabati kidogo huko Amani, Muheza. Sasa ni kwa nini Wizara haikutoa umuhimu wa kutenga fedha kwa ajili hiyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshatenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza. Tunaomba Wizara iangalie uwezekano wa kusaidia ujenzi wa hospitali ili isaidiane na Hospitali Teule ya Muheza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tunaomba Mheshimiwa Waziri aangalie uwezekano wa kupeleka CT- Scan na utengenezaji wa lift katika Hospitali yake ya Bombo, Tanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, magari ambayo yametolewa Kanda ya Ziwa, uwezekano wa magari hayo kutolewa kwenye Vituo vya Afya vya Muheza uangaliwe, maana kuna matatizo makubwa ya usafiri wa kuwapeleka wagonjwa kwa haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Chuo cha Mafunzo mbalimbali ambacho kipo maeneo ya Kiwanda, Muheza. Chuo hiki kipo chini ya Mheshimiwa Waziri lakini kimedharaulika kabisa, ni kama hakipo. Idara ya Ustawi wa Jamii imekisahau kabisa. Kina matatizo mengi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri atume wataalam wake ili tushirikiane tuweze kukubaliana tutakisaidia vipi Chuo hiki kisife?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa juhudi zao wote Wizarani.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja na nachangia kwenye maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, Kituo chetu cha TBC naomba kiimarishwe, hususan maeneo ya vijijini. Aidha, Redio ya Taifa na TV – TBC hazisikiki kabisa na TV za TBC muono wake sio mzuri. Kwa mfano, maeneo ya Tarafa ya Amani, Muheza yenye Kata za Mbomole, Misanai, Zirai, Kwezitu, Kweningoji na kadhalika Redio ya Taifa, TBC, haisikiki kabisa. Naomba mipango ifanyike kuimarisha sehemu hizo ili vyombo hivyo visikike na kuonekana.

Mheshimiwa Spika, wasanii wanafanya kazi kubwa lakini inaonekana haki zao (copyright) hawazipati kama inavyostahili; ni vizuri kuweka mikakati madhubuti ya kuwasaidia kupata haki zao. Aidha, wote wanaofanya uhalifu huu wakamatwe na kufikishwa mbele ya sheria.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kutungwa Sheria hivi karibuni ya Vyombo vya Habari, lakini maslahi ya waandishi wa habari hawapewi. Wapo waandishi wengi hawalipwi mishahara na wanaendelea kuwa vibarua. Suala hili liangaliwe kwa umakini mkubwa.

Mheshimiwa Spika, naipongeza Timu yetu ya Serengeti Boys, ni vizuri timu hii ikaangaliwa vizuri na isipoteze wachezaji hao ili baadaye wawe Taifa Stars. Taifa Stars imeshindwa kabisa kutuletea sifa katika nchi kwa sababu mbalimbali ikiwemo kutokuwa na kocha bora na wacheaji wengi wa Taifa wana umri mkubwa.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuchangia kwa kusema, naomba kuendelea kuchangia kwa maandishi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuzuia kukata miti kwenye Hifadhi ya Msitu wa Amani naomba lipewe kipaumbele. Miti inakatwa na baadhi ya viongozi wa vijiji maeneo hayo wanasimamia, wanatumia misumeno ya chainsaw. Tumepeleka FFU mara mbili lakini wakiondoka tu kazi inaendelea wanaharibu vyanzo vya Mto Zigi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri humbly mhamishe kikosi cha wanyamapori kihamie moja kwa moja kupunguza gharama. Nakuhakikishia Mheshimiwa Waziri ukidharau usishangae msitu huu wa Amani ukaisha, hamishia kikosi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba uangalie uwezekano wa kusaidia Ofisi za Ubalozi wetu zenye uwezo wa kuleta watalii. Kuna wakati Wizara yako ilisaidia sana Ofisi zetu za Kibalozi na walisaidia sana kuwakilisha nchi mbalimbali ambazo mlishindwa kuhudhuria. Fikirieni kuweka fungu maalum.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sina uhakika kama njia na sehemu za kupumzika wakati wa kupanda Mlima Kilimanjaro, nilipopanda Mlima huo mwaka juzi hali ilikuwa mbaya. Naomba viboreshwe tafadhali.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuwa mchangiaji wa kwanza mchana huu. Kwanza napenda kuwashukuru sana Waziri na Naibu wake kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya ya kuweza kutuletea watalii wengi. Wizara hii ni muhimu sana ambayo inaingiza pato la Taifa kama alivyosema mwenyewe Mheshimiwa Waziri kwenye asilimia 21; asilimia 17.5 ikiwa utalii na misitu asilimia 3.9. Nitakuja kuongelea suala hilo baadaye lakini ningependa kuanza mchango wangu na Hifadhi ya Amani (Amani Natural Reserve). (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Misitu ya Amani ni mikubwa sana na kama nilivyoongea kwenye mchango wangu mwaka jana ni misitu ambayo ina mambo mengi ndani yake. Ukiacha mambo ya miti yenyewe ambayo ipo pale pamoja na vivutio mbalimbali au scenario ambayo ipo au pamoja na vipepeo, maua na kila kitu ambavyo viko pale lakini ni reserve ambayo inatakiwa iangaliwe kwa uangalifu. Ni reserve ambayo inatupa chanzo cha maji kutoka Mto Zigi. Kwa hiyo, reserve hii sasa hivi ina hatari ya kuharibiwa na ina hatari ya hata chanzo cha maji kuharibiwa kabisa kwa sababu hivi karibuni tu maji ya Tanga yote yalikuwa ni tope. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, juhudi zimefanyika kimkoa, Mkuu wa Mkoa amejaribu kupeleka watu kule kwa ajili ya kuzuia ukataji wa miti kwenye hifadhi hiyo. Mkuu wa Wilaya pamoja na Halmashauri tumekuwa tukipeleka Askari wa Field Force lakini nguvu inakuwa ni ndogo. Ningeshauri ili kuweza ku-preserve Amani Nature Reserve, Mheshimiwa Waziri hawa Askari wa Wanyamapori ambao wapo kwa ajili ya kuangalia nafikiri wako pia kwa ajili ya kuangalia hifadhi zetu, tafadhali ahamishe hata unit moja immediately vinginevyo hii reserve itapotea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, reserve hii ni ya maana sana na iliwahi kulinganishwa kama ni moja ya maajabu ya dunia na mwanahistoria mmoja ambaye alikwenda kwenye Kisiwa cha Galapagos kule Ecuador Pacific. Sasa tutakapoachia reserve hii iweze kuharibika tutakuwa tumefanya makosa makubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni kuhusu wakulima wangu wa Derema 1,128. Wakulima hawa wameshapewa maeneo kwenye shamba la Kibaranga lakini bado hawajahama. Kama nilivyosema kwamba bado wanahitaji kifuta jasho ambacho Mheshimiwa Waziri aliahidi kwamba atakiangalia, naomba akiangalie ili wakulima hawa waweze kuhama mara moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la tatu ni kuhusu Mnada wa Miti ya Tiki. Mheshimiwa Waziri alikuja kuhudhuria Mnada wa Tiki pale Lunguza. Mnada huu umekuwa na malalamiko mengi sana kwani umekuwa ni kilio kwa wafanyabiashara na wenye viwanda pale Muheza kwa sababu tangu hii system ya mnada imekuwa introduced kuna viwanda karibu kumi vimefungwa pale Muheza. Hii ni kwa sababu matajiri wanakuja pale na hawa wenye viwanda vidogo vidogo hawawezi kushindana na hawa matajiri, utakumbuka kwenye mnada uliopita tajiri mmoja alichukua karibu vitalu vyote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka Mheshimiwa Waziri aangalie system hii ya mnada ijaribu kuboreshwa na kuangalia watu ambao wapo wanazunguka wanaangalia hizi hifadhi. Tiki zinapandwa vizuri sana, huyu Meneja wa Shamba la Lunguza Abdallah anafanya kazi nzuri sana na kila tiki inapokatwa unakuta amekwishapanda. Sasa wafanyakazi na wakulima wanafanya kazi nzuri, itakuwa siyo busara wao kuwanyang’anya sasa kwa sababu hawa matajiri wanaponunua hivi vitalu wanapakia magogo yote wanakwenda kupasulia Dar es salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka Waziri aangalie ili hawa wazawa ambao wamefungua hivi viwanda pale waweze na wao kupata hizi tenda za kuweza kupasua haya magogo, vinginevyo itakuwa shida. Kwa sasa viwanda karibu kumi vimefungwa, wafanyakazi karibu 1,000 wale wanaokaa pale wamepoteza kazi. Kwa hiyo, ni lazima kuwawekea masharti, kama hao matajiri lazima wafungue viwanda pale ili wafanyakazi wa pale waweze kupata kazi ya kufanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo nilikwishamwomba Katibu Mkuu ni kwamba tunategemea barabara ile sasa hivi kuiweka lami, lakini pale kuna malighafi (moram) ambayo ipo kwenye msitu huu lakini ipo pembeni. TANROAD wameomba sana kutumia hiyo malighafi kwa ajili ya kutengenezea hiyo barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ombi hili liweze kuzingatiwa kwa sababu kipindi kijacho tumeshaingizwa kwenye mpango kwa ajili ya kuwekewa lami kipande kidogo. Naomba kabisa mfikirie tutumie hiyo moram ambayo ipo pale iweze kutengeneza barabara hiyo ya Amani. Barabara hii itasaidia sana kuleta watalii ambao wataongezeka ili kupanda kwenye Milima ya Amani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la Mbuga ya Saadan ambayo ina upungufu sana wa wanyama. Mbuga hii sisi Muheza tuna interest nayo kwa sababu inapita Bagamoyo, Pangani na inatoboa mpaka Muheza inakwenda mpaka Amani. Sasa tulikuwa tunaomba waongezwe wanyama pale iweze kusaidia ili siku zijazo watalii watatoka Sadaan wanakwenda Pangani, Amani wanarudi Pangani kupumzika. Ni suala la muhimu sana ambalo naomba mzingatie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nakuja kwenye utalii. Kama nilivyosema, utalii unaingiza pato kubwa la Taifa lakini ukiangalia idadi ya watalii wanaoingia hapa nchini sasa hivi imeongezeka tuna milioni 1.2 ukilinganisha na mwaka jana ambayo ilikuwa milioni 1. Hata hivyo, bado idadi hii haitoshi kabisa ukiilinganisha na nchi nyingine. Kwa mfano, Victoria Falls Zimbabwe, pale ni hizo falls tu zenyewe lakini watalii ambao wanaingizwa pale ni wengi kuliko hawa wa kwetu, ni zaidi ya milioni 2.5 kama sikosei.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna umuhimu wa kujaribu kuongeza vivutio vya kuwafanya watalii waweze kuja kwa wingi na tumeona katika Afrika tupo kwenye namba 10 au
11. Kwa hiyo, bado tupo nyuma na tunahitaji kuongeza juhudi ili kuongeza watalii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, watalii hawa unawaongeza namna gani? Kuna masuala ya matangazo (advertisements). Suala hili ni muhimu sana na ukiangalia hapa hela ambazo zimetolewa kwa ajili ya advertisement ni ndogo sana. Nakumbuka kuna wakati mimi nilikuwa Denver kule Marekani na nilifarijika sana nilipoona kwenye TV moja ya Fox wanaonesha migration Serengeti na baada ya ule mkutano Wazungu wengi sana walionesha interest ya kuja kuangalia hii migration huku Tanzania. Sasa advertisement kama zile zinasaidia sana, ni lazima tuweke umuhimu sana kwenye mambo ya advertisements. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na advertisements kuna masuala ya tour operators. Tour operators wamesahauliwa sana na sijaona wakitajwa kwenye kitabu cha Mheshimiwa Waziri. Hawa ndiyo watu wanaleta watalii, hawa ndiyo wanafanya mipango, tour operators ni watu muhimu sana. Ukiangalia kwa mfano hao Victoria Falls ambao wanaletewa watalii wengi sana, wengi wanatoka South Africa na Zimbabwe wamefungua Ofisi kule (tour operator), wengi wanawachukua wanawaleta mpaka wanajaa, ni vizuri sana tukawapa umuhimu watu hawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tu nilikuwa naangalia kwenye gazeti moja la wananchi kwamba Kenya Airways inatoa ndege mara tatu sasa hivi kutoka Cape Town - Victoria Falls – Nairobi. Ni muhimu sana kuangalia tour operators ambao tukijumuisha pamoja na direct flights ambazo ni muhimu sana Mheshimiwa Waziri azipate, Wizara hii ina uwezo wa kununua au kukopa ndege yake ili kuwatoa watalii direct, watalii wanapenda direct flights.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kwa mfano kama Zanzibar, Zanzibar wanapata watalii wengi sana, lakini tatizo la Zanzibar sikumbuki sasa hivi kama wamesharekebisha ile mikataba yao ya zamani ambayo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Balozi.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
MHE. BAL. ADADI M. RAJABU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kupata muda huu kuweza kuchangia hii hoja muhimu sana ya viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kumshukuru sana Mheshimiwa Rais na Awamu yake ya Tano, kwa kuweka msisitizo mkubwa sana kwenye viwanda. Viwanda ni kitu muhimu sana kwenye nchi yoyote na ndiyo vinavyokuza pato la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na shukurani hizo lakini mtakumbuka kwamba viwanda vingi kwenye hii nchi vilikuwa Tanga. Tanga ilikuwa ni kitovu cha viwanda, lakini viwanda sasa hivi Mkoa wa Tanga vimekufa kabisa. Sasa nilitegemea Mheshimiwa Waziri alipoingia madarakani kitu cha kwanza kingekuwa ni kufufua vile viwanda vya Tanga ambavyo vilikuwa zaidi ya 1000. Kwa hiyo, tulitegemea kuna mikakati madhubuti ya kufufua vile viwanda. Kulikuwa na viwanda vingi tu vya chuma, sabuni, mbolea na vitu vingi tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka sasa hivi sijaona juhudi zozote za kufufua vile viwanda, lakini namshukuru kwa kutuletea kiwanda kikubwa sana ambacho kitaweza kutoa tani milioni saba kwa mwaka, Kiwanda cha Hengya na nimeambiwa kufuatana na taarifa yake kwamba wawekezaji wenyewe wako hapa Bungeni. Nawashukuru sana na nawahakikishia kwamba, wawekezaji hao waje Tanga na hawatapata matatizo yoyote na najua kabisa Mkuu wetu wa Mkoa wa Tanga yuko China kwa ajili ya ku-facilitate kiwanda hicho kiweze kuja Tanga. Karibuni sana Tanga. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Muheza sasa hivi sisi tumeshajitayarisha, tuna ardhi kubwa sana. Tuna ardhi ambayo sasa hivi tunasubiri mtuletee viwanda, tunafanya juhudi kubwa sana za kutafuta viwanda vya matunda; kutafuta wawekezaji wa viwanda vya mihogo pamoja na viwanda vya kuwekeza mipira, hizi pilipili manga pamoja na karafuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ardhi tunayo na nilishamwambia Mheshimiwa Waziri na tujitahidi kwa uwezo tuweze kupata wawekezaji wa kuweza kusaidia kupata hivi viwanda hasa vya matunda pamoja na mihogo. Juhudi bado zinaendelea na mazungumzo bado yanaendelea na insha Allah pengine tunaweza kufanikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamefunguliwa viwanda vingi hapa karibuni, viwanda vya matunda, lakini ningependa kumshauri Mheshimiwa Waziri kwamba, wawekezaji wanapokuja asiwaelekeze kwenye sehemu moja tu, ajaribu kuwaelekeza kwenye sehemu zile ambazo zao linatoka. Zao la matunda linatoka Tanga (Muheza). Kwa hiyo, ningeshukuru sana alete wawekezaji au wa mihogo Muheza, tunayo ardhi kubwa sana kwa ajili ya viwanda na kulima. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, TIC au EPZA. Vituo hivi ni muhimu sana kwenye nchi yoyote ile. Vituo vya TIC, EPZA, panapotokea ukorofi, ucheleweshaji wowote kwenye vituo hivyo, wawekezaji hapa ndipo wanapoweza kutoroka na kuondoka kwa kuwa vituo hivi ndivyo vinavyopokea wawekezaji. Sasa, niliwahi kuzungumza mwaka jana hapa kwamba, Kituo cha TIC lazima pawe na Land Bank, mwekezaji anapokuja hataki usumbufu, yeye anataka kuambiwa maeneo ni haya, ni haya, ni haya, wekeza hapo. Sasa utaratibu wa kusema watu binafsi ndio wawekeze pale, una land yako unakwenda kuingiza kwenye TIC inaleta usumbufu. Ni lazima Serikali sasa hivi kuptia Wizara ya Ardhi itoe ardhi TIC, ni lazima itoe ardhi EPZA ili mwekezaji akija aende moja kwa moja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mara ya mwisho mimi kwenda TIC baada ya kupeleka wawekezaji pale, kulikuwa na vibali zaidi ya kumi na tano. Sasa sijui sasa hivi hivyo vibali vimepunguzwa kwa kiasi gani, lakini unaposema One Stop Centre ni lazima iwe One Stop Centre kweli kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nenda Mauritius Enterprise, wao wana-time frame; mwekezaji anapokwenda pale ilikuwa 2400Hrs lakini wamepunguza mpaka 0600Hrs; kwamba kila kitu Residence Permit, Working Permit, viwanda, sijui leseni vyote vinafanyika katika siku moja. Sasa mwekezaji anataka kitu kama hiki na ndiyo maana kwenye ripoti za transparent international dhidi ya good governance na corruption, Mauritius na Botswana wamekuwa wanaongoza kwa miaka mingi na ni kwa sababu ya TIC yao, Mauritius Enterprise, ukienda Botswana TIC yao, hakuna usumbufu watu wanapata vibali mara moja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ningeshauri kwamba, Mheshimiwa Waziri aangalie vibali gani pale vinaleta usumbufu, atoe vile vibali weka vibali vichache. Mwekezaji hapendi usumbufu atoke hapa aende sijui biashara, atoke hapo aende sijui immigration, atoke hapo aende wapi! Anataka kila kitu akikute pale pale na hapo ndipo tutakapoweza kupata wawekezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi kuna taarifa wawekezaji wanaondoka, ni kweli? Ningependa hiyo taarifa labda Mheshimiwa Waziri aje ui-clarify wakati atakapokuja ku-wind up kama kweli wawekezaji wetu wanaondoka kwa sababu ya huu usumbufu ambao ni unnecessary ambao upo sehemu mbalimbali? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka jana nilimwomba Mheshimiwa Waziri kwamba Kiwanda cha Kamba, Tanga kina mashine nzuri na kinatoa mali ambazo zinanunuliwa hata nchi jirani. Nikaomba kwamba, Serikali sasa hivi basi iwape zabuni wale Kiwanda cha Kamba, wanatengeneza mazulia mazuri sana, ili mazulia yote ambayo yanatengenezwa, basi wapewe zabuni Tanga ili waweze kuzalisha na kuweza kuinua kile kiwanda. Sasa hivi kinatoa vizuri na kinataka kuleta mashine nyingine ambazo ni nzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho ningependa kushauri tu kwamba, ili kuleta wawekezaji, najua kwamba wanatumia Mabalozi nje, lakini ni vizuri wakaweka ma-trade attachee kwenye sehemu zile chache ambazo wanaona kwamba, kuna wawekezaji wengi ambao wanakuja. Wapeleke hawa ma-trade attachee watakaa kwenye Ofisi za Ubalozi na watakuwa specifically kazi yao iwe ni hiyo na wawape assignment kubwa, tutakuwa hatupati hasara, lakini nina hakika kabisa kwamba kuwepo kwa ma-trade attachee kwenye Balozi zetu kutasaidia sana badala ya kuwaachia hilo jukumu Mabalozi.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naomba kuunga hoja na nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja na kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri na Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kazi nzuri ambazo wamekuwa wakizifanya. Umuhimu wa kilimo hauna maelezo, kwani unachangia asilimia 29.1 ya pato la Taifa na kuleta ajira kwa asilimia 65.5 kutokana na asilimia kubwa hususan vijijini kujishughulisha na kilimo. Aidha, napongeza kodi/tozo ambazo zimeondolewa, hiyo itawapa afueni kubwa wakulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasikitika sana na kushangaa kutokana na fedha za maendeleo kupelekwa kidogo mno, yaani asilimia 3.31 ya fedha zilizoidhinishwa. Naomba tuweke umuhimu na kuhakikisha fedha hizo zinapelekwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Tanga tunalima mazao mengi ya biashara kama katani, nazi, korosho machungwa, viungo na kadhalika; lakini pamoja na Serikali kufuta hati za mashamba ya mkonge Wilayani Muheza, bado Wizara haijaonesha juhudi za kufufua zao la katani na kulifanya kuongeza pato la Taifa kama zamani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juhudi zinaendelea kufanyika kwa Maafisa Kilimo kuendelea kutoa elimu Wilayani Muheza, namna bora ya kulima machungwa, minazi na viungo vya chai na kadhalika wakati tunaendelea na mihogo kutafuta wawekezaji wa viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefurahishwa sana na ulimaji wa korosho ambapo Serikali imewapa wakulima pembejeo bure, jambo ambalo litaongeza ari ya kulima kwa bidii. Tunaomba Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho afanye mipango ya kutuletea mbegu Wilayani Muheza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ifikirie namna ya kutoa mbegu na mbolea bure kwa baadhi ya mazao, hii itawaongezea motisha wakulima. Kwa mfano, kuna wakati nchi ya Malawi ilifanya hivyo na walivuna mahindi mengi sana na kuongeza pato lao la Taifa. Aidha, nchini Zimbabwe pia waliwahi kuwakopesha wakulima zana za kilimo na wakaongeza uzalishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ubora wa mazao, pia Wizara inabidi isaidie sana wakulima. Ubora wa mazao yetu ukilinganisha na nchi nyingine kwa baadhi ya mazao, bado tunahitaji wataalam wetu walifanyie kazi. Kwa mfano, zao la pamba tunakosa kupata bei nzuri kutokana na ubora na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Chuo cha Kilimo cha Mlingano cha Utafiti kinakufa, kwani Chuo hicho hakipelekewi fedha kabisa na mambo mengi yako ovyo. Tunaomba wapelekewe fedha chuo hicho kifufuke. Muheza tunafuga sana ng’ombe. Kiwanda cha Tanga Fresh kinategemea sana maziwa kutoka kwa wafugaji wa Muheza, namshauri Mheshimiwa Waziri atutumie wataalam wake wawasaidie wafugaji hawa kuongeza maziwa kitaalam na pia namna ya kuwapatia mikopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umwagiliaji bado tupo nyuma sana. Inabidi tufanye kazi tuweze kuwa na mashamba makubwa na ya kisasa. Tutumie zana za kileo za umwagiliaji. Tukitaka kuwa na kilimo, ufugaji, uvuvi na viwanda, ni vizuri Mawaziri husika kuwa na mawasiliano ya mara kwa mara kama Waziri wa Kilimo, Ardhi, Maji, Nishati, Umeme na Fedha.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza Mawaziri wote wawili kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya pamoja na matatizo ya upungufu wa fedha. Bajeti ya mwaka 2016/2017, fungu la maendeleo walitengewa Sh.915,193,937,771 lakini walipata Sh.181,209,813.609, sawa na asilimia 19.8. Mwaka huu 2017/2018 wametengewa Sh.623,606,748,000, pana tofauti ya Sh.291,587,189. Upungufu huu ni mkubwa na ningeshauri kiwango kikubwa kiongezwe kabla ya Juni katika kipindi hiki.

Sioni mantiki ya kuongeza fedha kwa tarakimu badala ya kupeleka fedha ambazo zimepitishwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la maji Muheza bado ni kubwa sana. Ndoo moja ya maji ni Sh.800 hadi Sh.1,000/= mjini, bado huko vijijini. Ukombozi wa maji Muheza Mjini ni maji kutoka Mto Zigi kilometa 22.7. Mradi huu ni kati ya miradi 17 ya mkopo wa India (ukurasa wa 173) lakini kila siku tunaambiwa financial agreement bado. Tunaomba ishughulikiwe ili fedha hizo, dola milioni 14.754 zitolewe ili kazi ianze.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji kutoka Pongwe mpaka Mjini Muheza tenda zilikwishafunguliwa lakini bado wakandarasi hawajateuliwa. Tunaomba mradi huu unaoshughulikiwa na Tanga UWASA tupate majibu haraka ni nini kinachoendelea. Nawashukuru Mawaziri wote kwa ubunifu wa mradi huu na Tanga UWASA.

Mheshimiwa Naibu Spika, mfumo wa maji Muheza pia miundombinu ni mibovu. Hivyo, miradi yote miwili ikikamilika bila kurekebisha miundombinu hiyo miradi hiyo itakuwa haijakamilika kikamilifu. Hivyo, nashukuru kwa kuwekewa shilingi bilioni tano kwa ajili ya mifumo ya maji mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, maji vijijini, nashukuru kwa kutengewa shilingi milioni 931.373 ingawaje zimepungua kutoka zile za mwaka 2016/2017. Ningeshukuru kama zingerudishwa ambazo ni Sh.222,105,000/=.

Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji ambavyo vinazunguka vyanzo vya maji vya Mto Zigi inabidi visaidiwe kupata maji safi na salama kwa kuwekewa mabomba na dawa kwenye maji yote yanayotiririka kutoka milimani, hususan Tarafa za Amani, Mbomole, Zirai, Kwezitu, Mbarai, Kisiwani, Moshewa, Kwemidimu na kadhalika. Wakisaidiwa naamini wataendelea kuvitunza vyanzo hivyo na kuwafanya wasichafue vyanzo hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nashauri yafuatayo:-

(i) Suala la maji litolewe kabisa TAMISEMI na lishughulikiwe moja kwa moja na Wizara kama umeme;

(ii) Tozo inayotozwa ya Sh.50 kwa ajili ya Mfuko wa Maji iongezwe na kuwa Sh.100, hii itasaidia kupunguza tatizo la maji hapa nchini; na

(iii) Ni muhimu tuanzishe Wakala wa Maji Vijijini kama REA, huenda ikasaidia kupunguza tatizo hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata fursa hii ya kuweza kuchangia hoja hii ambayo ni muhimu sana ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami naungana na wenzangu kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kwa hatua ambayo ameichukua, hatua ambayo imedhihirisha madini yetu yalikuwa yanatoroshwa sana na yalikuwa yanaibiwa sana na ni hatua ambayo inadhihirisha kauli yake kwamba nchi hii ina mali nyingi sana. Kwa hiyo, ningependa kumpongeza sana kwa hatua hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ningependa kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri na Naibu wake na Katibu Mkuu pamoja na Wakurugenzi wote kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya. Viongozi hao wamedhihirisha kwamba kweli wana nia ya kuondoa malalamiko mengi ya ardhi ambayo yalikuwa yamejaa kwenye nchi hii; wamezunguka takribani nchi mzima. Mheshimiwa Waziri amekuja Muheza takribani mara mbili, yote ni kwa ajili ya kutatua matatizo ya ardhi pale wilayani Muheza. Nampongeza sana Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ardhi ni suala muhimu sana. Katika wiki iliyopita tulikuwa na hoja ya Wizara ya Viwanda na Biashara. Katika hoja hiyo issue ya ardhi ndiyo ambayo wawekezaji wote wanataka wakija hapa nchini wakute ardhi iko sawasawa. Sasa vituo vyetu vya TIC na EPZA vina matatizo makubwa sana ya ardhi na sina uhakika kama Wizara hii imeweza kuwasaidia kwa kiwango gani ili waweze kuwa na ardhi pale waweze kuwa na land bank ili wawekezaji wanapofika wasipate matatizo yoyote. Kama hawajawa-approach ni vizuri wakati wanagawa ardhi kwa kweli kuangalia hivi vituo viwili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TIC na EPZA ni kitovu cha wawekezaji na ni kitovu cha maendeleo. Mwekezaji akija anahitaji hoteli, anahitaji kuweka viwanda lakini lazima awe ardhi. Hatutaki wawekezaji waje hapa na waanze kusumbuka kuanza kutafuta ardhi wao, wanatakiwa wakute ardhi ipo hapo. Kwa hiyo ni vizuri wakiwasiliana na Mawaziri wanaohusika ili kuhakikisha kwamba kwa kweli ardhi inakuwepo na wakati wanagawa ardhi Wizara hii kweli vituo hivyo visikose ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri amekuja Muheza na alikuja mara mbili. Mara ya kwanza kukabidhi mashamba ambayo yamefutiwa hati, takribani mashamba saba na mara ya pili akaja tena kwa suala hilo hilo kwa sababu kulikuwa na shamba moja ambalo lilisahaulika la Kibaranga na akaja akatukabidhi hati, kwamba Mheshimiwa Rais amefuta hati ya hayo mashamba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mashamba yale, ukichukulia hili shamba la mwisho la Kibaranga, tulikuwa tumewawekea tunataka kuwahamisha wanakijiji takribani 1,128 ambao walikuwa kwenye hifadhi ya Amani kule Delema; ilitakiwa tuwahamishie pale na tumeshawaamisha pale sehemu kwenye hilo shamba la Kibaranga. Tatizo ambalo linajitokeza ni kwamba wananchi wa pale Kibaranga wanahoji kwamba utawapaje ardhi hawa kabla ya sisi wakazi wa hapa hamjatugawia?

Mhesheshimiwa Mwenyekiti, tulileta malalamiko hayo pamoja na mipango yote ya mashamba yote namna tutakavyogawa sehemu mbalimbali za wawekezaji, hospital, ofisi, shule na kila kitu, na barua hiyo nilimkabidhi Mheshimiwa Waziri. Ni muhimu sana barua hiyo iweze kujibiwa kwa sababu sasa hivi tumeanza kupata wawekezaji na tumeanza kuwaonesha maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunategemea kwamba baada ya kupata majibu ya barua hiyo tutaanza kupanga na kutekeleza namna tutakavyogawa mashamba hayo kwa wananchi, wawekezaji na namna tutakavyoweza kupanga mambo mbalimbali ya maendeleo katika Wilaya ya Muheza. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri namwomba sana, kwamba tukipata majibu ya barua yetu hiyo itatusaidia sana sisi kuweza kupanga mipango yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni kwamba, sisi ardhi tunayo sasa hivi hatuna shida ya ardhi, tuna shida tu ya kutafuta wawekezaji Muheza. Hata hivyo, tatizo kubwa ni kwamba tuna upungufu sana la Wapima Ardhi; wapimaji hakuna; tuna mpimaji mmoja ambaye sasa hivi amekwenda kusoma. Sasa kila tukitaka kufanya mipangilio inabidi tuombe Mkoani Tanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilimwomba Mheshimiwa Waziri kwamba at least atusaidie wapimaji wawe pale ili tuweze kukamilisha hii kazi ya upimaji pale wilayani ambayo tunaamini kwamba kwa kiasi kikubwa sana itaweza kutusaidia kuweza kupima na kuweza kupanga (master plan) ya pale wilayani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mwisho nataka kuongelea suala la National Housing. National Housing wamefanya kazi nzuri sana na wanaendelea kufanya kazi nzuri sana, wamejenga majengo mengi sana na sasa hivi wako kwenye mikakati ya kujenga nyumba za bei nafuu. Mheshimiwa Waziri naomba; National Housing tumewapa eneo pale Muheza la sehemu za Chatuu Kibanda pale, wameshalipia na wananchi wa Muheza walikuwa wanategemea kwamba ujenzi wa hizo nyumba nafuu ungeanza wakati wowote ule. Hata hivyo, mpaka wakati huu hatuoni dalili zozote, tunajiuliza hawa National Housing vipi, wamesahau kwamba tuliwapa eneo pale Muheza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri kwamba aweke msisitizo ili National Housing sasa hivi waje waanze ujenzi pale. Eneo lipo na wananchi wa Muheza wako tayari na wengine wako tayari wanaulizia namna ya ununuzi. Sasa tunamwomba sana aangalie uwezekano wa kuja kusaidia na kuwaamuru National Housing waanze kujenga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, yangu leo yalikuwa machache na nakushukuru sana na naomba kuunga mkono hoja hii.
Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Spika, nami nashukuru sana kupata nafasi hii kuchangia hoja hii ya bajeti ambayo ni muhimu sana.

Mheshimiwa Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na Katibu Mkuu na Wataalam wake kwa kutuletea bajeti hii ambayo ni muhimu sana. Bajeti hii kwa kweli imelenga hasa watu wa chini na wanavijiji. Tofauti na mwaka 2016 ambapo Mheshimiwa Waziri alikuwa anasita kidogo, lakini baada ya kusikia kilio chetu kikubwa, ameweza kuifanyia marekebisho bajeti hii kwa kiwango cha hali ya juu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuondoa tozo na ushuru mbalimbali, lakini bajeti hii ingekuwa na umuhimu zaidi katika suala la maji ambapo Mheshimiwa Waziri amelisahau kwa kiwango kikubwa sana. Bajeti iliyopita ya mwaka 2016 kwa kweli fedha za maendeleo kwenye Wizara ya Maji zilitolewa kwa kiwango kidogo sana. Kiwango cha asilimia 19 na point something ni kidogo sana. Sasa safari hii tulitegemea kwamba Wizara ya Maji itaongezewa na itapata kwa kiwango kikubwa sana fedha ambazo zingeweza kutosha hasa vijijini.

Mheshimiwa Spika, kwa kweli nakubaliana kabisa na mapendekezo ambayo yametolewa na Kamati ya Bajeti ambayo kwa kweli ilishauri kwamba asilimia 70 ya mapato ambayo yanakwenda kwenye mfuko, yaende kwenye Mfuko wa Maji. Suala hili lingeweza kusaidia sana maji vijijini. Kwa hiyo, nashauri Mheshimiwa Waziri aangalie suala hilo, ahakikishe kwamba atleast asilimia 70 katika Mfuko wa Maji unaongezewa ili wananchi wa vijijini waweze kuwa na maji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili, ni suala la miradi 16 ambayo ilijadiliwa, tulipewa mkopo wa Dola milioni 500 kutoka India.

Naamini kwamba fedha hizi zikiweza kupatikana, zitaweza kuondoa matatizo ya maji kwa kiwango cha hali ya juu. Kwa sababu miradi 16 na miradi ambayo imesambaa nchi nzima, kila siku tunaambiwa kwamba kuna financial agreement ambayo inatakiwa isainiwe, tangu mwaka 2016. Mheshimiwa Waziri tafadhali sana, suala hili lipo kwenye mikono yake na kwenye Wizara yake, ahakikishe hiyo financial agreement inasainiwa ili kazi hii iweze kufanyika kwa bidii.

Mheshimiwa Spika, nilishauri wakati nachangia suala la bajeti ya madini na nishati kwamba sasa hivi ni lazima tuanzishe kiwanda cha kusafishia haya makinikia. Bila kuanzisha kiwanda hiki, Bunge halitaonekana linaunga mkono vizuri juhudi za Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Spika, jana kwenye mapendekezo ya Kamati, suala hili limetolewa kwamba atleast lazima tuwe na kiwanda hicho hapa, sasa huo ni mlango wa kutokea. Kwa hiyo, namshauri Mheshimiwa Waziri aangalie bajeti yake, ajaribu kuifumua kuhakikisha kwamba tunakuwa na hiki kiwanda tuweze kuondoa haya matatizo mengi kwa sababu taarifa ambayo imetolewa jana, kwa kweli inasikitisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Kampuni inafanya kazi hapa bila kuwa na leseni, kampuni imechukua madini chungu nzima, kuanzia miaka ya nyuma, matrilioni ya hela. Kwa kweli ni very absurd, sikutegemea kwamba kitu kama hicho kingeweza kutoka kwenye ripoti hiyo. Wametuachia mashimo! Wametuachia mahandaki! Kwa kweli sasa hivi never, never, never ever again, hatuwezi kukubali kuendelea kuwa na mahandaki humu ndani wakati tuna uwezo wa kufanya kila kitu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni muhimu Mheshimiwa Waziri aangalie suala hilo la uanzishwaji wa kiwanda na ni vizuri hata kama tutabaki na haya mahandaki, tubaki na haya mahandaki na mali zetu ziwe chini, lakini hatutakubali tena sasa hivi kutoa michanga kwenda nje kama alivyosema Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Spika, kwa kweli kama kuna hizo kesi sasa hivi, sisi ndiyo tuna hoja. Sisi ndio tunatakiwa, kama wakikataa kukaa kwenye makubaliano, sasa hivi tuna hoja ya kuwashtaki sasa kuhusiana na fedha zote ambazo wameiba. Ni lazima tuhakikishe kwamba zinarudi.

Mheshimiwa Spika, suala la utalii utaona kwamba mchango kwenye pato la Taifa umepungua katika mwaka 2015/2016. Tumechangia kwenye asilimia 14 ukilinganisha na asilimia 17.5 ya mwaka uliopita. Hii ni kwa sababu ya VAT. Sasa ni vizuri Mheshimiwa Waziri akaliangalia hilo suala na kuhakikisha hii VAT ambayo inachajiwa. Hili tumelipigia kelele sana kwenye bajeti iliyopita. Kwa hiyo, ni vizuri kuiangalia, pia tuondoe hiki kitu, tupate watalii wengi ili tuweze kuchangia kwa kiwango kikubwa kwenye pato la Taifa.

Mheshimiwa Spika, lingine ni reli ya Tanga - Arusha na Musoma. Reli hii sasa hivi tunasubiri taarifa ya feasibility study ili iweze kuiuza kwa wafadhili kwa njia ya PPP. Sasa bado haijalipwa hela na Kamati ya Bajeti imeshauri vizuri kwamba fedha za kulipa feasibility study, basi zitoke kwenye Mfuko wa Reli ili tuweze kulipa mara moja. Kwa hiyo, ningeshukuru sana kama suala hilo lingetiliwa maanani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwisho, suala zima la bajeti, bajeti ni nzuri lakini tunaomba utekelezaji wake, bajeti ikitekelezwa kwa kiwango ambacho tutaipitisha hapa basi itakuwa na maana, lakini kama bajeti tunapisha na haitekelezwi, kwa kweli inasikitisha sana. Sasa ni vizuri kutengeneza bajeti ambayo tunaweza kuipitisha. Tutakapoipitisha, itakuwa ni vizuri sana na papo hapo ni muhimu kuweka maanani kwamba siku hizi nchi nyingi hazi-include suala la wafadhili ambao wana-support kwenye bajeti.

Mheshimiwa Spika, ni vizuri ufadhili ambao unatolewa usiingie kwenye bajeti kwa sababu mara nyingi unakuta wanapoahidi kwamba watachangia bajeti, kwenye hatua za mwisho utakuta hawachangii bajeti. Sasa ile inavuruga mipangilio yote. Ni vizuri tuweke bajeti yetu ambayo tunaweza kutekeleza kutokana na hela zetu na hizo fedha za wafadhili zije kama ni kitu cha baadaye. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo,naomba kuunga mkono hoja. Ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2017/2018
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi nashukuru sana kupata nafasi ya kuchangia Wizara hii ambayo ni muhimu sana ya Nishati na Madini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kitendo chake cha kuzuia yale makontena pale bandarini na nampongeza sana kwa kuunda ile Tume ya kuanza kuangalia kiini hasa cha utoroshaji wa madini hapa nchini. Ripoti ya Tume inabidi Waheshimiwa Wabunge tuipongeze sana kwa sababu pale ndiyo mwanzo wa kuanzia, madini ya nchi hii yamekuwa yakitoroshwa kwa muda mrefu sana na kwa kiwango kikubwa.Tumeshuhudia baadhi ya migodi hapa nchini inatengeneza mpaka viwanja vya ndege ndani ya mgodi. Tumeshuhudia baadhi ya migodi hapa nchini inaweka kampuni za ulinzi kutoka nje kwenye migodi ya hapa nchini, maana yake ni nini hiyo? Maana yake ni utoroshaji kwamba wanatayarisha viwanja vya ndege, wanatayarisha ulinzi kutoka nje ili sisi tusiweze kuona na baadaye madini hayo yanaondoka kwa kiwango kikubwa. Sasa hii ripoti inadhihirisha kwamba tumeibiwa muda mrefu sana.

TAARIFA .....

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Mimi mwenyewe nimeviona hivyo viwanja na nimeona hizo kampuni kwenye migodi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja hapa Waheshimiwa Wabunge lazima tushikamane, hii ni hoja ya Serikali, sasa hizi hoja za kupinga ambazo zinatolewa aidha, madini hayo ni mengi au siyo mengi lakini kuna dalili za utoroshaji jamani, lazima tushikamane. Sasa tunapotoa hoja hapa ooh tutashtakiwa, ngoja twende tukashtakiwe, kwani tunaogopa kwenda International court, tunaogopa kwenda kwenye arbitration, twendeni tukashtakiwe na tutatoa arguments, tuna ushahidi ambao umeonekana na Kamati imedhihirisha. Waheshimiwa Wabunge hiki ni kipindi ambacho tunatakiwa tushikamane kwa sababu tutakapofanikiwa kudhibiti madini yetu maendeleo yatakuwa kwa kasi sana, kwa hiyo, nawaomba tushikamane. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti hii sijaona Mheshimiwa Waziri akizungumzia suala la ujenzi wa Kiwanda cha Kusafisha Madini. Namuomba aipangue bajeti yake na ahakikishe kwamba anaweka huo msimamo wa kuweka hela za Kiwanda cha Kusafisha Madini. Wakati masuala haya yanaendelea kushughulikiwa ngoja tuanze mchakato wa kujenga kiwanda chetu hapa kama tukishindwa basi tuingie ubia na watu binafsi kwa maslahi yetu lakini lazima tuhakikishe kwamba kiwanda hicho tuna ki-manage sisi tusije kufanya makosa tena na kuibiwa. Namshangaa ndugu yangu Mheshimiwa Lissu juzi wakati anaongea alipokuwa ana-criticize ya kuongelea case ya Bulyanhulu, naifahamu case hiyo nimeishughulikia na wakati huo Mheshimiwa Lissu alikuwa anatetea sana wachimbaji wadogo na namna makampuni makubwa ambavyo yanataka kuwadhulumu wachimbaji wadogo mali zao. Jana akawageuka tena anaponda mimi nimeshangaa sana. Kwa hiyo, nasema tushikamane ili tuondoe hili tatizo ili tuweze kupata hela nyingi za kuweza kuleta maendeleo hapa nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nizungumzie REA III, REA wamefanya kazi nzuri sana ila katika kipindi hiki hawakufanya kazi nzuri ukilinganisha na kipindi cha nyuma. Sasa sijui ni kwa sababu gani lakini mipango ambayo wameiweka kwenye REA III tunategemea waanze kutekeleza vizuri. Pale Muheza kwenye Jimbo langu Mheshimiwa Waziri unajua umenipa REA III vijiji 44, list ya mkandarasi ambayo umenikabidhi ina vijiji 37, nakuomba urudishe vile vijiji vyangu saba ili wananchi wa kule ambao wameanza kufunga nyaya waweze kupata umeme. Vijiji hivyo ni vya Kwakope, Kibaoni, Magoda, Mbambala, Kitopeni, Masimbani, Msowelo vyote hivyo wananchi wameshajitayarisha na wako tayari kwa ajili ya kufungiwa umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho napenda kupongeza sana juhudi ambazo zinafanyika kwa ajili ya bomba la mafuta la kutoka kule Hoima Uganda mpaka Tanga. Tunaamini hii ni chachu na wananchi wa Tanga wanategemea sana kwamba bomba hilo litawaletea maendeleo makubwa ya viwanda na vitu vingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja na nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
MHE. BALOZI ADADI M. RAJABU: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuunga mkono na kumpongeza Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara kwa kazi nzuri mnayoifanya. Nachangia katika maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu ambao umefanywa wa kugawa vifaa vya maabara katika shule za sekondari unapaswa kupongezwa sana, ila katika mgao uliopita Wilaya ya Muheza tulipata mgao wa shule saba tu. Naomba kwenye mgao huu Muheza tuongezwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Muheza hatuna Chuo cha VETA. Naomba tuone uwezekano wa kujenga. Kipo Chuo kimoja maeneo ya Kiwanda Potwe ambacho kipo chini ya Ustawi wa Jamii. Chuo hiki hakifanyi vizuri na uongozi wa Wilaya utaomba kifanywe VETA. Ombi hilo likifika naomba lishughulikiwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliwahi kuleta ombi la Muheza High School iweze kuangaliwa na iruhusiwe kuwachukua wanafunzi wa kutwa. Hii itasaidia wanafunzi waliofaulu na kukosa nafasi, maana shule hiyo imejengwa kwa nguvu za wananchi.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nashukuru sana kupata nafasi ya kuchangia kwenye huu Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa mwaka 2018/2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mipango mizuri ni ile mipango ambayo inatekelezwa, tumekuwa tunatengeneza mipango mizuri sana miaka mingi sana na utekelezaji wake unakuwa sio kwenye asilimia 100.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini kwamba hii mipango ambayo imeandikwa kwa mwaka 2018/2019 kama utekelezaji wake unakuwa kwa ukamilifu, basi tunaweza tukawa na uchumi ambao utapaa vizuri sana. Mipango mizuri inayotekelezwa inaongeza uchumi na inapunguza mfumuko wa bei.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona mipango mingi baadhi ya mipango ya 2017/2018, 2016/2017 imeanza kutekelezwa kwa uzuri kabisa. Tumeona standard gauge ya central line ikianza, tumeona ndege bombardier zikianza kuingia, tumeona umeme kule Rufiji - Ruaha ukianza, kwa kweli inatia matumaini na tumeona bomba la mafuta ambalo linatoka kule Hoima - Uganda mpaka kwetu kule Tanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vitu hivi kwa mfano kama Bomba la Mafuta la Tanga la kutoka Hoima mpaka Tanga inabidi tuongeze thamani yake, value adition. Kwamba bomba hili sehemu zote ambazo litapita watafaidika namna gani, kuna mipango gani ambayo ipo ya kusaidia kuona kwamba linaweza kuongeza thamani kwenye maeneo yote ambayo bomba hili linapita na wananchi ambao watafaidika ambao bomba hili linapita wanafaidika kiasi gani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye huu mpango sioni central line, sioni mpango wowote wa kuanza kutengeneza SGR ya central line na nimeangalia kwa makini, lakini sijaona. Naamini kabisa kwamba Tanga line pamoja na central line zikienda simultaneously basi tunaweza tukapata mendeleo mazuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi juzi Rais alikuja Tanga na aliambiwa tatizo hili na akaamuru bandari iongezewe fedha. Nilikuwa naona kwamba tusingoje mpaka Rais aje kwa sababu nchi ni kubwa, lakini ninyi Mawaziri mnapaswa kumsaidia kwenye maeneo yale ambayo ni muhimu. Sikuona namna ambavyo Kiwanja cha Ndege cha Tanga kinaweza kupanuliwa na sijaona namna ambavyo bombardier imeelekezwa kutua katika Kiwanja cha Ndege cha Tanga kwa sababu sasa hivi kutakuwa na hekaheka nyingi sana. Naomba Waziri aliangalie hili kwa makini sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Tanga line nakumbuka kikao kilichopita tulikubaliana kwamba aliyefanya upembuzi yakinifu atalipwa fedha zake na akilipwa fedha zake basi mpango huo utaingia kwenye PPP. Wapo wawekezaji kutoka Marekani ambao wameshughulika sana kupata huo mchoro ili waanze kuleta mapendekezo ya kuanza kutengeneza Tanga line, lakini mpaka sasa mchoro huo unakuwa ni hadithi. Kwa hiyo, naomba kabisa Waziri a-take note kama tuliamua kwamba msanifu alipwe kutokana na Mfuko wa Reli basi alipwe mara moja ili huo mchoro upatikane na tuanze kuuza hiyo biashara kutengeneza Tanga line mara moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilizungumza katika bajeti iliyopita, hili suala la PPP, suala la road toll, duniani kote sio Marekani, Ulaya na baadhi ya nchi hapa Afrika wanatumia road toll. Hizo nchi ambazo zimeendelea zinatumia road toll sisi kwa nini hatutaki kutumia road toll? Naamini kabisa mapato ambayo yatapatikana kwenye barabara…

MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, naomba mpunguze sauti tumsikilize mchangiaji, zungumzeni taratibu.

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mapato ambayo yatapatikana kwenye barabara ni makubwa na mfano upo wa Daraja la Kigamboni ambalo limeingia PPP na NSSF, mapato ambayo yanapatikana pale Kigamboni yangeweza pia yakapatikana kwenye barabara zetu kama tungeanzisha mpango wa road toll. Naamini kabisa kama Mataifa makubwa wanatumia road toll kwa nini hapa tusitumie, tuna tatizo gani? Mheshimiwa Mpango naomba kabisa hili suala aliangalie kwa makini sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la maji tumelizungumza na kila mtu hapa ndani ana tatizo la maji, viwanda na kilimo haviwezi kupatikana bila maji. Kuna mpango upo wa miradi mikubwa 17, kuna mradi wa dola milioni 500 kutoka China lakini sasa hivi imekuwa ni hadithi tu tunaambiwa financial agreement, sasa financial agreement mpaka lini? Naambiwa financial agreement ipo Wizarani kwake Mheshimiwa Mpango. Naomba kabisa atakapokuja ku-windup atuambie kwamba hii miradi na hiyo financial agreement imefikia wapi, kwa nini haianzi? Mimi ni mdau na Muheza ipo kwenye huo mradi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo, ukiangalia ukurasa wa tisa tumeambiwa kuna ongezeko kutoka asilimia 2.7 mpaka 3.1, hili ni ongezeko dogo sana. Naamini mkazo mkubwa tungeweka kwenye kilimo sasa hivi tungeweza kuwa mbali sana. Mheshimiwa Mpango ningependa sana wataalam wa kilimo watembelee hata hapo Zimbabwe na South Africa ili waone mashamba ya kisasa ambayo yapo, waone system za umwagiliaji ambazo zinatumika kule boreholes na kadhalika, unakwenda kwenye shamba wewe mwenyewe hutaki kutoka kwa raha ambayo unaoina pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unakwenda kwenye shamba unakuta kuna viwanda vidogo vidogo kama tumbaku hii ambayo tunasema wanakausha, wana viwanda vidogo vidogo ndani ya mashamba. Tumbaku ikitoka pale inakwenda moja kwa moja airport na maua yakitoka shambani yanakwenda moja kwa moja airport. Vitu kama hivi ndiyo vya kujifunza, naamini kabisa kwamba tutakapopeleka wataalam na Serikali ikiweka nia kwenye kilimo tutakuwa mbali sana.

Mheshimiwa Spika, hapa juzi nchi moja hapa chini tu walitoa bure mbolea na mbegu wakawapa wakulima na mazao ambayo wamevuna huwezi kuambiwa kwa sababu yale mavuno yalikuwa ni mengi mwisho ikabidi wawauzie WHO. Kwa hiyo, vitu kama hivyo ni muhimu sana kuweza kujua kwamba unawawezesha wakulima, unawapa mikopo ya vifaa vya kisasa, hatuwezi kuendelea kulima na jembe mpaka leo, kuna ma-harvester na kila kitu.

Mheshimiwa Spika, hapa kamati yangu ilikwenda Songwe, Mbeya kule, wapo wafungwa wanasema hatuna trekta, hatuna vifaa tuleteeni vifaa, Songwe ndiyo ambayo inalisha Mbeya yote ile, tuleteeni vifaa tulime na ardhi ipo. Tukaweka kwenye bajeti kwani walipata hata senti tano? Hivi ni vitu vya kuangalia kwa sababu vina umuhimu wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kuna tatizo kubwa sana kwenye zao la chai. Kule Amani sisi tunalima chai sana lakini tatizo ambalo linajitokeza sasa hivi ni kwamba wale walimaji wanatakiwa wa-export hiyo chai moja kwa moja au waingie kwenye mnada Mombasa, hawaruhusiwi ku- blend wala ku-pack, parking na blending vyote vifanyike nje, sasa hii nini? Wanakwenda Mombasa kwenye mnada, Kenya wananunua chai yetu wana-pack Kericho, Kericho wanaleta chai hiyo hiyo hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, hili suala siyo sahihi tunasema tulime na tu-dd value sasa hawa hawaruhusiwi, ni suala la kuliangalia. Nimeongea na Waziri wa Kilimo na nime-set appointment naye ili tuweze kuona tutafikia wapi lakini ni muhimu suala hilo liangaliwe kwa umakini wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vivyo hivyo na pamba, nchi kama Zimbabwe inalima pamba kidogo sana ukilinganisha na sisi, lakini grade ya kwake ni kubwa ukilinganisha na grade ya kwetu hapa. Ni kwa sababu ya utunzaji na ulimaji wake ambao unafanyika kwa umakini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mwisho ambalo nataka kuongelea ni la kuhamia Dodoma. Wizara zimeshahamia Dodoma, Dodoma imeshakuwa makao makuu lakini sijaona kwenye mpango namna ya kutengeneza huu Mji uonekane kweli ni makao makuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, miji mingi ambayo imehamiwa Serikali inakuwa na mipango, nenda Rwanda na Abuja kaangalie, wanakuwa na mipango kabisa wameshapanga kwamba wanajenga site fulani, wana- prepare certain site, wanaweka kila kitu nyumba na maofisi everything. Sasa hapa sijaona chochote kwenye mpango huu namna gani ambavyo tutaboresha Makao Makuu ya Dodoma iweze kuonekana kweli ni makao makuu kama nchi nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nakushukuru sana.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB – MWENYEKITI KAMATI YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA: Mheshimiwa Naibu
Spika, kwanza ningependa kuwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge ambao wamechangia na Waheshimiwa Mawaziri kwenye hoja yangu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wabunge 10 wamechangia kwenye hoja hii, watano kwa maandishi na watano kwa kuongea na Mawaziri, nawashukuru sana.

Waheshimiwa Wabunge waliochangia kwa maandishi ni Mheshimiwa Rhoda Kunchela, Mheshimiwa Lucia Mlowe, Mheshimiwa Zainabu Amiri, Mheshimiwa Mary Muro na Mheshimiwa Cosato Chumi. Mengi ambayo wameongea ni maoni ambayo tutayapeleka Wizarani kwa ajili ya kushughulikiwa na kwa mfano Mheshimiwa Rhoda amezungumzia mambo ya vitambulisho kwamba NIDA waweze kupewa uwezo waweze kutoa vitambulisho kwa haraka.

Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri Waziri wa Mambo ya Ndani yupo hapa tutampa hiyo hoja na Mheshimiwa Lucia Mlowe amezungumzia mambo ya crime ambayo matukio ya kupotea watu ambayo nimeyazungumzia kwa kirefu sana na kuwataka polisi basi hao watu ambao wanapotea na kutekwa na watu wasiojulikana basi wajitahidi kuhakikisha kwamba hao watu wanaofanya vitendo hivyo wanajulikana na wanakamatwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kukamatwa Wabunge ndani ya Bunge limeshughulikiwa vizuri na sasa hivi nafikiri polisi wana hayo maagizo kwamba ni lazima waripoti kwa Katibu wa Bunge kabla ya kuendelea kutekeleza hiyo kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia suala la ucheleweshaji wa kesi ambayo limezungumzwa kwa kirefu na kwenye taarifa yangu/kwenye hoja yangu nimeeleza mbinu mbalimbali ambazo kamati imeona Jeshi la Polisi inatakiwa zichukue ili kuharakisha upelelezi wa makosa mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Zainabu amegusa mambo ya kuongezewa zimamoto nyenzo na kuweza kulipwa kupewa fedha kwa ajili ya maendeleo kama ambavyo tumezungumza kwenye hoja yangu. Mheshimiwa Mary Muro kazungumzia msongamano wa Mahabusu na Wafungwa ambao ameuzungumzia kwa uchungu lakini na kwenye taarifa yetu, kwenye hoja yetu tumeelezea na kuwataka Serikali kuhakikisha kwamba basi kesi ambazo ziko Mahakamani zinasikilizwa kwa haraka inavyowezekana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Cosato Chumi ameshauri ufunguzi wa Balozi mbalimbali kule Lubumbashi na Guangzhou, China ambapo kwa kweli kwenye Kamati tumelizungumzia suala hili kwa makini sana na kumshauri Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa aweze kulichukua suala hili, kwa sababu hizi sehemu ni sehemu za biashara. Lubumbashi Watanzania wengi sana wanakwenda kwa ajili ya kufanya biashara, pamoja na Guangzhou wanakwenda wengi sana ni lazima tuwe na Balozi ndogo kwenye hizo sehemu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge watano wamechangia kwa kuongea tukianza na Mheshimiwa Katani ambaye amezungumzia suala la ulinzi wa Wabunge ambaye ame-support issue hiyo akihusisha na kupigwa risasi kwa Mheshimiwa Tundu Lissu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwamba kwenye ile hoja yangu kwenye taarifa hiyo nimeongea kwa kinaga ubaga kwamba kuna suala la mlinzi na kuna suala la ulinzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesisitiza sana suala la ulinzi, Jeshi la Polisi ni lazima lihakikishe kwamba basi linatoa ulinzi kwa Waheshimiwa Wabunge kwenye makazi na kwenye maeneo ambayo wanaishi. Haina maana kwamba watoe mlinzi, kwa hiyo kuna mbinu mbalimbali ambazo wanazotakiwa kufanya kama kufanya doria na kadhalika, kama ambavyo ameelezea Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, isipokuwa suala la usajili wa gari nimelieleza kwa ufafanuzi mkubwa kama mamlaka inahusika itaridhia basi ingekuwa ni vizuri ili usajili wa magari ya Wabunge basi yaonekane kama ni MB so, so, so au Viti Maalum so, so! Kwa hiyo, suala hilo ni la muhimu isipokuwa hapo ni lazima Wabunge waangalie kwamba gari gani hiyo ambayo unataka kuiwekea inazunguka na bendera. Kwa hiyo ni lazima uangalie na nafikiri taratibu zingine zitafuatwa namna ya kushughulikia.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Dkt. Ishengoma ametaja mambo ya amani na ulinzi ambayo kwa kweli ni Jeshi la Polisi linatakiwa liongezewe tu nyenzo na fedha ili liweze kukabiliana na uhalifu mbalimbali ambao unatokea hapa nchini.

Mheshimiwa Msigwa ametaja tukio la Mheshimiwa Tundu Lissu kwamba waliomba vyombo vya kimataifa vije kuchunguza tukio hilo, lakini ninavyofahamu ni kwamba ni lazima pana conditions zake kabla ya kuleta vyombo vya kimataifa. Ukianzia kwanza na tukio lenyewe, hilo kosa lenyewe linakuwa regarded kama nini, ni international crime, ni organize crime au ni domestic crime. Sasa na hawa wapelelezi ambao unataka kuwaleta je, tuna mahusiano nao kwa kinchi. Kwa hiyo, ni suala ambalo linatakiwa liangaliwe na sio kuwaleta wapelelezi kutoka nje kwa kienyeji.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la immigration mimi niliwakilisha kamati kwenye kupokea passport mpya hizi za e-immigration sasa na Mheshimiwa Rais pale alisema kabisa kwamba wamejaribu kuokoa kutoka kwenye wajanja walikuwa wameweka bilioni 400 pale lakini wametengeneza huo mradi wa hizi passport mpya kwa bilioni 50. Sasa hebu angalia hapo ni kiasi gani fedha ambazo zimeokolewa. Lakini nachosema hivyo ni kwamba sasa sidhani kama hizo taarifa ambazo anazo Mheshimiwa Msigwa zina ukweli kiasi gani kwa sababu mpaka Mheshimiwa Rais atangaze pale sidhani kama watu wanaweza wakampa taarifa ambazo ni za uongo.

Mheshimiwa Mwambalaswa ameelezea usalama wa Wabunge ambao nimeshaufafanua kwa kirefu lakini amesisitiza suala la ujenzi wa nyumba za Wabunge kwa sababu tuko Dodoma hapa Wabunge ni lazima watakuwepo kwa hiyo, ni muhimu sana Ofisi za Bunge zikafikiria namna ambazo zinaweza zikatengeneza Kijiji cha Wabunge ambacho kitakuwa na urahisi wa kuwalipa.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Mheshimiwa Nape Nnauye limefafanuliwa vizuri na Mheshimiwa Waziri wa Nchi na sijui kama kuna umuhimu wa kuileta Bungeni hiyo Sheria ya Usalama wa Taifa kwa sababu kazi za Usalama wa Taifa zinajulikana na ni intelligence informations na kushauri taasisi mbalimbali. Lakini nimeshindwa kuelewa hapa ilivyohusishwa na EPA pamoja na Diplomasia ya Uchumi ambayo kila watu na mikataba wako wataalam kwenye hizo sehemu.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema, kutoa ufafanuzi huo naomba sasa kutoa hoja ili mapendekezo yote na maoni ambayo nimeyaeleza yaweze kukubaliwa na Bunge hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nashukuru sana kwa kunipa fursa hii kuchangia hoja hii ambayo ni muhimu sana ya hotuba ya Waziri Mkuu. Hotuba ambayo ni hotuba mama, hotuba ambayo ina-cover shughuli zote zile za Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, napongeza sana juhudi ambazo anafanya Mheshimiwa Rais, tumeona maendeleo mbalimbali. Nampongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu, siyo siri tumemuona jinsi ambavyo anazunguka nchi nzima kwa ajili ya kuiletea maendeleo nchi yetu. Mheshimiwa Waziri Mkuu hongera sana na Mawaziri wote kwa shughuli ambazo wanazifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona miradi mikubwa, tumeona SGR ya reli ya kati ikianza, tumeona ufufuaji wa ATCL, tumeona flyovers, tumeona ujenzi wa vyanzo vipya vya umeme, tumeona miradi ya Mkulazi ambayo ni maendeleo makubwa sana kwa kilimo na pia tumeona bomba la mafuta la kutoka kule Hoima mpaka Mkoani Tanga. Juhudi ambazo nazipongeza kwa hii miradi mikubwa, hii inaongeza uchumi kupanda ndiyo maana kwenye hotuba ya Waziri Mkuu anaonesha kuna viashiria vikubwa vya kupanda uchumi wetu kwa asilimia 6.8. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la bomba la mafuta la Tanga tunaamini kabisa kwamba, shughuli hiyo imeshaanza na kwa kweli, itatusaidia sana Mkoa wa Tanga. Aidha, suala la ujenzi wa reli ya Tanga, mpaka sasa hivi ninafahamu kwamba upembuzi yakinifu umemalizika na juhudi zinafanyika za kuweza kuingia kwenye PPP, lakini tunaiomba Serikali Mheshimiwa Waziri Mkuu, suala hili ulipe kipaumbele. Najua upembuzi yakinifu wa Tanga – Arusha umemalizika, lakini upembuzi yakinifu wa Arusha – Musoma ndio unaendelea. Sasa ni vizuri tukaanza kutangaza hii tender ili ianze kushughulikiwa. Naamini kabisa wapo wawekezaji ambao watajitokeza kama alivyojitokeza juzi kwenye ujenzi wa viwanda vya madawa. Kwa hiyo, naomba suala hili lipewe umuhimu kwa sababu, wenzetu majirani pale Kenya SGR yao ambayo inakuja mpaka bandarini kwao Mombasa, wanatupa changamoto kubwa sana kwa hiyo, ningeshukuru na hii iende sambamba na SGR ya reli ya kati. (Makofi)

Miradi mikubwa imeshughulikiwa kwa kiwango kikubwa sana, lakini sasa naona kwamba msisitizo mkubwa twende vijijini. Naamini kabisa tutakapokwenda vijijini tutapunguza umaskini ambao uko mwingi kwenye vijiji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kilimo; tumeona kabisa juhudi ambazo zimefanyika kwenye suala la korosho, lakini hatujaona juhudi ambazo zinafanyika kuinua zao la katani. Sasa hivi zao la katani liko bei kubwa sana kwenye soko la dunia. Ni hivi majuzi tu Waziri wa Kilimo amekuja Tanga kuanza kufufua, lakini ningeshukuru kama Waziri Mkuu utaingilia kati na kujaribu kuona tutalifanya vipi soko la katani liweze kukua. Katani ndiyo imetukuza Tanga, miradi mingi sana imetokana na katani, sasa katani inadharaulika, haijapewa ule umuhimu ambao unatakiwa. Waziri Mkuu na Waziri wa Kilimo naamini kabisa suala hili mtalipa umuhimu wa kipekee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la maji; maji ni muhimu sana, sasa hivi tunashindwa kupata Wawekezaji Muheza pale kwa sababu ya maji, tuna tatizo kubwa sana la maji. Ninamshukuru sana Waziri wa Maji, tumepata mradi wa kutoa maji Pongwe, mradi wa kutoa maji Pongwe unakwenda vizuri sana Mheshimiwa Waziri Mkuu, lakini mradi huo ambao tuliutegemea umalizike mwezi ujao mwishoni umechelewa kwa mwezi mmoja na umechelewa kwa sababu ya ujenzi wa tenki ambao utaanza baada ya wiki mbili zijazo, lakini inanipa wasiwasi kwenye mifumo ya kufumua Mji wa Muheza ambao tulitengewa bilioni tano, sasa bado hatujaruhusiwa kutangaza hili suala. Ningemuomba Waziri wa Maji aliangalie ili utakapofika wakati basi mradi huu usiweze kuchelewa kwa sabau, maji yatakapotoka kule ni lazima tufumue hii mifumo ya Mjini Muheza. Hata hivyo namshukuru sana kwa juhudi zake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la miradi mikubwa 17 ambalo tumeambiwa kila siku linakwama shauri ya financial agreement haijasainiwa. Miradi hii 17 itakapoanza itasaidia sana tatizo la maji kwenye nchi hii, lakini kila siku tunaambiwa financial agreement. Najua kuna technical ground iliyoko pale, naamini kabisa kwamba, Waziri wa Fedha yuko hapa na Waziri wa Maji yuko hapa, suala hilo mtaweza kulitatua kabla ya bajeti ya Wizara ya Maji haijasomwa. Nitashukuru sana na pia kwenye bajeti ya maji itakaposomwa basi ile shilingi 50 ambayo tuliipigia kelele sana wakati uliopita nategemea itakuwepo kwenye bajeti ya Waziri wa Maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la afya, tunajenga Hospitali ya Wilaya ya Muheza na hapa nimeona kwamba, kuna hospitali zitajengwa 67 nchi nzima. Namtegemea Waziri wa Afya na au TAMISEMI, Waziri wa TAMISEMI naamini kama tumeonesha juhudi basi naamini hizo bilioni 1.5 na Muheza tutapewa ili tuweze kukamilisha hii hospitali yetu ya Wilaya. Lakini pamoja na hayo tunawashukuru sana TAMISEMI na Waziri wa Afya kwa kutupa milioni 400 kwa ajili ya kujenga kituo cha afya ambacho tumekianza kule Mkuzi. Tunategemea pia kujenga vituo vingine vitano vya afya ambavyo ambapo juhudi za wananchi wameanza kule Muhamba, wameanza kule Ngomeni, wameanza kule Tongwe, wamenza Potwe na wamenza Ubwari ambacho tunaendelea kukiboresha na wameanza kule maeneo ya Amani - Msarai, zote hizo wameshaanza kuweka misingi, naamini kwamba, tutakapofika juu basi Serikali itakuja iweke mkono wake pale.

Suala REA Muheza ina Kata nyingi sana, kata 37 kwa hiyo, nina vijiji karibu 135 ambavyo vingi bado havijapata umeme. REA imeanza kuingia, survey imefanyika kwa vijiji vingi, lakini kazi ilikuwa haijaanza ni wiki iliyopita tu Waziri alipopita pale, ambapo ningependa kumshukuru sana Mheshimiwa Waziri Dkt. Kalemani kwamba baada ya kufika basi kazi zimeanza, nguzo zimeanza kuletwa, lakini ninachoomba ni suala hili lifanyike kwa haraka kwa sababu vijiji vyangu vingi havijapata umeme. Survey ilipofanyika tu kwenye vile vijiji wananchi wenyewe wameanza kufurahi, wameanza kushukuru. Mimi nimekula mbuzi na kuku wengi tu wananipa, lakini bado hawajapata umeme, lakini mbuzi hao wenu nimewala pamoja na kuku wengi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la barabara, barabara yangu ya Amani na Muheza kilometa 36 ipo kwenye bajeti shilingi bilioni tatu, lakini mpaka sasa hivi bado sijaona dalili zozote za TANROADS kuja kuanza kuishughulikia. Ningeomba Mheshimiwa Waziri Mkuu na Waziri wa Ujenzi basi suala hili muliangalie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni suala la Watendaji wa Vijiji na madereva ambao walimaliza darasa la saba, kwa kweli inasikitisha. Sisi tumeendeshwa na madereva wa darasa la saba kwa miaka yote, miaka mingi na wamefanya kazi kwa bidii. Juzi wakati hilo zoezi linafanyika tulikuwa tuna ziara ya kwenda wapi, naambiwa magari yako pale Halmashauri madereva hawapo wamesimamishwa, nini? darasa la saba. Mheshimiwa Waziri Mkuu tuwe na imani, wamefanya wameendesha gari bila ajali zozote zile miaka yote, wanakuja mwisho wanakaribia kustaafu tunawafukuza. Tuwe na ubinadamu tuangalie na hawa watu ningeshauri kabisa Mheshimiwa Waziri Mkuu basi warudishwe waendelee kufanya kazi kwa miaka yao ambayo imebaki. Wakati wanaajiriwa watu hawa wakati huo darasa la saba lilikuwa lina umuhimu wake, lakini sasa hivi wasomi wengi! Lakini hatuwezi kuwa tumewapata wasomi basi tuwaache wale. Naomba kabisa Serikali iangalie na ione namna ya kurekebisha. (Makofi)

Baada ya kusema hayo, naunga hoja mkono na ninakushukuru sana kunipa nafasi hii.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nashukuru sana kwa kupata nafasi ya kuchangia hoja hii muhimu ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda sana kuusifu uongozi wa Mheshimiwa Rais na Mheshimiwa Profesa Mbarawa na wasaidizi wake wote, kwa sababu Wizara hii ni Wizara mojawapo ambayo imeonesha kwa kweli ni kitu gani Awamu ya Tano inataka. Miradi mikubwa mingi sana imeanza kutekelezwa, tukianzia kwenye barabara, SGR, madaraja, bomba la mafuta la Tanga, flyovers, vivuko na mengineyo mengi. Hata hivyo nimefurahishwa sana na hotuba ya Mheshimiwa Waziri hasa hasa kwenye miradi hii mikubwa. Isipokuwa nimesikitika sana baada ya kuona kwamba reli ya Tanga imeachwa kabisa. Nimeangalia nimesoma kwa haraka haraka, lakini sijaona reli ya Tanga ikizungumziwa. Najua upembuzi yakinifu umemalizika kati ya Tanga mpaka Arusha na sasa hivi unafanyika upembuzi yakinifu wa Arusha mpaka Musoma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ningeshauri kwamba hii reli ya Tanga ambayo upembuzi yakinifu umeshafanyika wa Arusha mpaka Tanga basi ingeanza kutangazwa kwa njia ya PPP ili wawekezaji waanze kufanya kazi hiyo. Naamini kabisa wawekezaji wa PPP watakapoarifiwa mradi huu unaweza kuanza mara moja. Nafahamu wapo na wanategemea Serikali itaanza kuutanga hivi karibuni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo tunategemea bandari. Nimeona kwenye ratiba hapa Bandari ya Tanga ambayo ni bandari kubwa na sasa hivi kutokana na bomba la mafuta ambalo linategemewa kuanza tunategemea kwamba kazi itaanza. Mwaka uliopita ilitengewa fedha lakini naona kazi inakwenda kwa kusuasua, sasa nategemea kwamba basi wakati huu itatengenezwa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nakuja kwenye jimbo. Barabara yangu ya Amani - Muheza kilometa 36 mwaka 2017 tulitengewa shilingi bilioni tatu. Nilitegemea kwamba kazi ingeanza lakini naona kwenye maandiko ya Mheshimiwa Waziri kwamba anatafutwa mkandarasi na kila nikimuuliza Meneja wa TANROADS Tanga vipi umefikia wapi ananiambia tunashughulikia. Sasa tutashughulikia huyu mkandarasi sijui atapatikana lini na fedha hizi zinaweza kurudi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona kwamba nimetengewa tena shilingi bilioni tano, sasa naamini kabisa shilingi bilioni tatu zangu zile na shilingi bilioni tano hizi nikijumulisha pamoja ni shilingi bilioni nane naamini nitapata karibu kilometa 20.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Mheshimiwa Waziri nakuomba sana fedha hizi zije ili hii kazi iweze kuanza. Nashukuru sana kwamba barabara ya Tanga mpaka Pangani mtaanza kuitengeneza na nimeona hapa mmeitengea hela kwa hiyo, nakushukuru sana na nategemea kwamba barabara hiyo yenyewe itaanza kutengenezwa kwa sababu barabara hiyo inapita pia kwenye jimbo langu. Namshukuru sana Mheshimiwa Elias Kwandikwa, alikuja na aliiona barabara hii na aliona matatizo yake. Kwa hiyo, naamini kabisa kwamba kazi itaanza mara kwa sababu waliwapa matumaini wanachi wa Amani kwamba kazi hii itafanyika na sasa hivi wanategemea kwamba kazi hiyo itaanza kufanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mawasiliano ya eneo hilo hilo la Amani, tuna tatizo kubwa sana la mawasialiano. Nafikiri sasa hivi imefika wakati kwamba kukimbilia kwenye mapaa ya nyumba au kupanda kwenye miti kwa ajili ya mawasiliano iwe imekwisha. Sasa naamini kwamba nimempa list Naibu Waziri ambaye aliuliza maeneo ambayo mawasiliano hakuna; na nimempa list ya Tarafa yote ya Amani, Muheza; Tarafa yote ya Bwembwera ambako mawasiliano yanakuwa ni tabu sana kwenye baadhi ya vijiji. Kwa hiyo, nategemea kwamba katika kipindi hiki basi atazituma hizi kampuni za simu kuja kusaidia kwenye haya mawasiliano, vinginevyo suala la TARURA bado hatujaona matunda yake. Muheza hawajaletewa hela kabisa na hii TARURA, hata shilingi moja; sasa inakuwa taabu na kuwa- control hawa TARURA, najua ni TAMISEMI lakini inakuwa taabu sana kwa sisi kuweza kupata mawasiliano ya kujua kama wamepewa hela au hawakupewa hela, wao wapo wapo tu. Sasa naomba wapewe hela ili waweze kuonesha hiyo kazi ambayo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nashukuru sana kupata nafasi hii ya kuchangia kwenye hoja hii ya kilimo ambayo ni muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaposema kilimo kipewe kipaumbele ni muhimu sana, na ningeshauri kwamba kipaumbele hiki kiende sambamba na ujezni wa viwanda, tuwe wabunifu kwenye mambo mbalimbali yaweze kuweza kukuza kilimo chetu ili kumuondoa mkulima kulima na jembe. Sasa twende kwenye ubunifu wa ulimaji ambao ni wa kisasa, ulimaji ambao ni wa umwagiliaji, ambao utaleta manufaa makubwa kwa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa sana kuishauri Serikali kwamba kuna mifano mingi ya nchi nyingi, hili suala la mbolea, suala la mbegu, hebu Serikali ijiangalie, itoe mbegu bure, itoe mbolea bure. Tutakapotoa hivyo, kuna mifano ya nchi jirani ambayo imewahi kufanya hivyo, kwa hiyo nafikiri tutakapotoa hivi vitu bure na baadae tunakuja kuwachaji wakulima kwenye faida ambayo watapata baada ya kuuza hayo mazao yao. Nafikiri ni muhimu tuchague baadhi ya mazao ambayo tunaona kwaba yanaweza kuwa na manufaa kwa nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kule Tanga, Amani, tunalima sana chai, kuna kiwanda kimoja cha EUTCO, wanalima sana chai, lakini wana tatizo moja ambalo nimeshawahi kumwambia Mheshimiwa Waziri, kwamba hawa watu wanalima chai, wanatakiwa wa-brand, wanatakiwa wa-pack, wanatakiwa wauze, lakini hawaruhusiwi, wao wanalima baadaye wanaambiwa kwamba baada ya kuchakata wakauze mnadani kule Mombasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunawapa faida hawa watu wa Mombasa, watu wa Kenya, kwa nini hayo mambo tusiyafanye hapahapa nchini? Hawa watu wako tayari kabisa kufungua kiwanda, na ndiyo maana tunataka kwamba tuweke viwanda kwenye hii nchi viwe vingi. Sasa hivi vikwazo ambavyo vinawekwa hapa, naomba Mheshimiwa Waziri uliangalie sana hili, hii ni mara ya pili nakwambia, naomba uliondoe, waruhusiwe hawa watu, wachakate, wa-brand na wauze hapa hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni katani, naona vipaumbele vingi vinapewa kwenye korosho na pamba, lakini katani sasa hivi ina bei kubwa sana kwenye Soko la Dunia, lakini haipewi kipaumbele na sielewi ni kwa nini kwa sababu mashamba yametaifishwa lakini hakuna kiongozi ambaye anakuja kushawishi kuweza kusema kwamba tulime katani. Sasa naomba kabisa kwamba suala la katani lipewe kipaumbele, kwa sababu katani yenyewe si kamba tu, ina mambo mengi pale kwenye ule mti. Huwezi kutupa katani, inatengeneza mpaka umeme; kwa hiyo naomba kabisa kwamba Mheshimiwa Waziri suala hili la katani lipewe kipaumbele cha hali ya juu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri sana na ninaunga mkono Kamati ambayo imeshauri kwamba Mheshimiwa Spika na uzuri yuko hapa, atengeneze Kamati ya Bunge ambayo inaweza kushauri hili suala la kilimo, vinginevyo hatuelewi tunakwenda wapi, mbele, nyuma, bajeti inazidi kuteremka.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii na mimi kuchangia hoja hii ya maji ambayo ni muhimu sana. Tatizo hili sijui kama ni sugu au ni donda ndugu au ni nini, lakini ni tatizo kubwa sana hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano imefanya mambo mengi sana katika kipindi cha miaka miwili na nusu. Tumeshuhudia mambo mengi kwenye sekta mbalimbali za afya, miundombinu, lakini sekta ya maji bado Awamu ya Tano haijashughulikiwa ipasavyo. Nashauri sasa hivi mwelekeo uende kwenye maji. Suala hili sasa hivi ni tatizo siyo katika Jimbo la Muheza tu, Jimbo la Muheza naweza kusema sijui ni sugu au ni donda ndugu, lakini ni tatizo kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu juhudi ambazo zinafanywa na Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu na Wakurugenzi wote wanashughulika sana kutatua tatizo la maji, lakini hawana hela. Mipango ambayo ipo kwenye kitabu hiki kama ingetekelezwa ninaamini kabisa tungeweza kupunguza sana tatizo la maji. Kama mambo ambayo yametajwa kwenye kitabu hiki fedha zingeenda kutolewa, basi tatizo hili tungeweza kulipunguza kwa kiasi kikubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naona aibu sana kwa sababu Tanga sasa hivi kuna miradi mikubwa ambayo inakuja na unapopita kwenda Tanga huachi kupita kwenye Jimbo la Muheza, ni lazima upite Muheza. Ninyi ni mashahidi Waheshimiwa Wabunge, unapopita Muheza unapopita
Lusanga unakwenda Mkanyageni, Ngomeni, Kilapula unakaribishwa na madumu ya maji barabarani. Madumu ya maji watu wanasubiri kwenda kuchukua maji Tanga. Sasa hii kitu inanisononesha sana na ninaona aibu sana. Kwa kweli suala hili ni gumu na ninaomba sana Wizara iweze kuliangalia kwa sababu ndiyo miradi ipo mingi, lakini inachelewa kutekelezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana Wizara kwa kuanzisha mradi wa Pongwe. Pongwe mpaka Muheza tumechukua maji na huo mradi umeanza kufanya kazi. Nawashukuru sana tena sana kwa sababu mradi huu tuliutegemea tuufungue mwezi huu, lakini naona itashindikana labda baada ya miezi miwili au mitatu ijayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nashukuru kwa sababu Mheshimiwa Waziri wenyewe na Maofisa wake wote kwa kweli wanashughulika sana ili kuhakikisha kwamba haya maji yanafika Muheza Mjini kama ilivyopangwa ili wananchi wa Muheza waweze kupata maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nawashukuru Wizara kwa kuweza kuangalia vyanzo, vijiji vingi vya Mashewa kule Amani ambavyo vinazungumza Mto Zigi vimeweza kupata maji, ninawashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi bado nina miradi ya vijijini, najua nimepangiwa hela hapa karibu shilingi bilioni
1.169 na ninaamini kabisa kwamba kuna miradi ambayo tuliipanga kwenye mwaka uliopita haikutekelezwa. Mradi wa kutoa maji kutoka Mto Pangani wa Kirongo, Mradi wa Umba – Ngomeni, Mradi wa Mkwakwa – Mafleta na mradi wa Tongwe. Hii miradi ipo kwenye hatua za kuwekewa sign. Sasa tunaamini kabisa kwamba haitasita na tutaendelea ili iweze kukamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kimoja ambacho nimesikitika sana ni hii miradi 17. Miradi 17 ya mkopo wa India dola milioni 500 imekuwa kama ni kichekesho sijui ni sindimba au ni nini. Miaka miwili iliyopita tumeambiwa hapa, Waziri Mkuu wa India amekuja ameweka saini Ikulu pale, miradi 17 Muheza ikiwemo, sasa hivi hapa Mheshimiwa Waziri kwenye taarifa yake anasema majadiliano yanaendelea. Mwenyekiti wa Kamati anasema issue ipo kwenye vetting kwa Attorney General. Sasa sijui tuamini ipi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda Mheshimiwa Waziri atakapokuja ku-windup atuhakikishie kwamba kweli hiyo financial agreement imeshasainiwa? Maana yake tatizo lilikuwa ni financial agreement, kila siku financial agreement, sasa imeshasainiwa ili tuweze kujua kama ni nini? Kama ipo kwa Attorney General, hiyo issue ya vetting, Attorney General imefikia wapi? Hiki kitu miaka miwili na nusu inazungumzwa hapa! Ninaamini miradi hii ingeanza, ingeweza kupunguza sana tatizo la maji kwa sababu ni miradi ambayo ime-cover karibu nchi nzima mpaka Zanzibar, sasa kwa nini haitekelezwi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, ni suala la tozo ya mafuta. Hili suala ni la muhimu sana kwa sababu takwimu zinaonesha kwamba hizi tozo hata Hazina hawaziingilii, zinakwenda moja kwa moja na Wizara ya Maji wanazishughulikia hizi. Ukishapeleka hati mara moja tu unapewa hela zako. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nafikiria kwamba Waheshimiwa Wabunge tuunge mkono wazo lililotolewa na Mwenyekiti wa Kamati, lazima tozo hii ya shilingi 50 iongezwe iwe shilingi 100. Kwa kweli bila kufanya hivyo Mheshimiwa Waziri na Waziri wa Fedha wakati wa kupitisha Financial Act hapa itakuwa ni matatizo. Hatutakaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naona muda haupo kwangu, nakushukuru sana na ninashukuru kwa kupata nafasi hii na naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia hoja hii na naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo inabidi kipewe kipaumbele sambamba na ujenzi wa viwanda. Wizara inabidi iendelee kubuni mipango ya kisanyansi kama tunataka tutoke katika jembe la mkono, kwa mfano, kilimo cha umwagiliaji, mabwawa na visima viimarishwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zao la chai ni moja ya mazao ambayo sisi Amani – Muheza linalimwa kwa kiwango kikubwa. Makampuni yanayolima chai Amani ni EUTCO lakini wana tatizo kubwa, wanalima chai hawaruhusiwi ku-pack, ku-brand na kuuza. Wanachokifanya ni kuchakata na kwenda mnadani Mombasa kutafuta soko. Kwa nini twende mnadani nje ya nchi? Kwa nini msiruhusu hawa wenye uwezo ku-pack, ku-brand na kuuza nchini na nje Mombasa, Kenya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanga tunalima katani kwa kiwango kikubwa sana lakini zao hili halijapewa umuhimu wa kipekee ili kuweza kusaidia ulimaji wa zao hili na uuzaji wake ambao kwa sasa soko lake ni zuri kwenye soko la dunia. Aidha, tuna kiwanda cha pamba ambacho kinanunua katani kwa wingi lakini hawana soko kubwa ndani na nje ya nchi. Mipango ifanywe ili kuzuia bidhaa kutoka nje, kukuza soko na kufanya wananchi waweze kulima sana katani. Kampuni hii ya Katani Limited imeingia mikataba na wakulima wadogo wadogo kulima katani na kuwauzia wao kwa bei ndogo. Mikataba hii wananchi wanaumizwa, iangaliwe vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ingeangalia utaratibu wa kutoa mbegu na mbolea bure kwa wananchi. Nimeona mfano kwenye nchi moja jirani ambapo wananchi walivuna mahindi mengi hadi wakaamua kuwauzia WFP/ WHO. Sio lazima Serikali itoe kwa nchi nzima, ingechagua baadhi ya mikoa michache kwa majaribio. Aidha, mikopo ya zana za kilimo itolewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kulima pamba kwa wingi hapa nchini tatizo kubwa lililoko ni ubora (quality) ya pamba yetu bado iko chini ukilinganisha na nchi zingine ambapo grades za pamba zao ziko juu. Nashauri tuangalie uwezekano wa kuona tutawasaidia namna gani wakulima wetu kuweza kulima pamba yenye ubora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasifu sana mradi wa Mkulazi. Mradi huu ingawa sijafanikiwa kuuona lakini ni mradi wa mfano. Tuwe na miradi mingi kama hii itatuvusha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Wizara ijipange na kuona itasaidia namna gani kuzuia panya wakubwa Mkoani Tanga ambapo walikula mahindi yote. Tafadhali angalieni namna ya kusaidia.
Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na ningependa kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nawapongeza kwa kazi kubwa mnayoifanya hususan katika sekta ya utalii. Nashauri mtumie vizuri ndege hizi ambazo zinakuja/zilizonunuliwa na Serikali kuongeza idadi ya watalii. Aidha, utumiaji wa Tour Operators zilizopo (ama zianzishwe) nje ya nchi ni muhimu zitumike.

Mheshimiwa Spika, eneo la Amani – Muheza ambalo Waheshimiwa Mawaziri wote mmefika ni eneo zuri ambalo linaweza kuwa kivutio kizuri kwa watalii. Naomba uliboreshe, kuna miti mirefu kuliko sehemu nyingi duniani, majoka makubwa, maua na kadhalika, kuna vipepeo ambao ni vivutio na pia ni biashara kwa wanakijiji wa Fanusi – Amani, ambao wanapeleka vipepeo hao nje kwa wingi.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo tangu Serikali ipige marufuku usafirishaji wa wanyama hai nje ya nchi wananchi wa Fanusi wameathirika. Mheshimiwa Waziri uliahidi kuboresha mazingara ya utunzaji wa vipepeo hao lakini bado wakala wa misitu amesahau naomba kukumbushia.

Mheshimiwa Spika, mgogoro wa watu 1,028 wa Derema bado haujamalizika. Tumeanza kuwapatia maeneo kwa kushirikiana na Wakala wa Misitu lakini bado kuna suala la upungufu wa fidia zao. Tumeongea jana na Naibu Waziri na Katibu Mkuu na naomba ulishughulikie.

Mheshimiwa Spika, miti ya tiki ambayo inalimwa Lunguza – Muheza bado tatizo la kuruhusu wakazi wa Muheza au wanunuzi kuwa na uwezo wa kushindana nadhani halijatatuliwa. Tunaomba utaratibu wa zamani (kwa maboresho kidogo) mgao wa wananchi urudishwe na waweze kupatiwa fursa ya kufunga viwanda vidogo vidogo hapo hapo Muheza badala ya matajiri wachache kununua vitalu vyote na kutoa miti hiyo nje ya Muheza.

Mheshimiwa Spika, lipo tatizo lingine kubwa dhidi ya Maafisa Misitu la utoaji wa vibali vya kukata miti hovyo. Kwa mfano Afisa Misitu wa Muheza juzi Baraza la Madiwani limearifiwa kukatwa mivule 100 nje ya utaratibu. Sasa pamoja na wazo la kuanzishwa Mamlaka ya Misitu lakini Maafisa Misitu pia wangehamishiwa chini ya Katibu Mkuu wa Wizara.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
MHE. BALOZI ADADI M. RAJABU: Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja na napenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watumishi wote kwa kugeuza Wizara na kuifanya iwe bora. Nawapongeza kwa kuondoa utapeli wa viwanja, migogoro mbalimbali na kuweka nidhamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawashukuru kwa kuanzisha mradi wa nyumba ambazo zinajengwa na NHC kule Chatur
- Muheza. Mradi huo umeanza vizuri na Wakandarasi wapo
site.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Muheza hatuna Baraza la Ardhi na malalamiko na migogoro ya ardhi inaongezeka kila siku. Wananchi wa Muheza inabidi waende Tanga. Tafadhali naomba tuangalie uwezekano wa kuanzisha Baraza la Ardhi hapo Mjini Muheza kwa msaada wa Wizara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza miradi mbalimbali ambayo inajengwa na shirika letu la NHC. Miradi hiyo ni mingi, ila bei za nyumba bado ni kubwa. Pendekezo la kuondoa VAT kwa nyumba wanazouziwa wananchi inabidi liendelee kupendekezwa. Kuondolewa huko kutafanya nyumba hizo zinunuliwe kwa wingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Ofisi ya Ardhi Muheza isaidiwe fedha ikarabatiwe, hususan chumba cha kutunza kumbukumbu/takwimu haiendani na vifaa vilivyoletwa. Mheshimiwa Naibu Waziri ameona. Tafadhali naomba liangaliwe, vinginevyo nawapongeza.
Makadilio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kupata nafasi hii kuchangia hoja hii ya Maliasili na Utalii ambayo ni muhimu sana. Kwa sababu ya muda nitakwenda moja kwa moja kwa utalii na vivutio vya utalii ambavyo viko jimboni kwangu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwanza Mawaziri wote Mheshimiwa Waziri na Naibu wake wameweza kuja katika Jimbo la Muheza na kuweza kuona vivutio vya utalii ambavyo viko maeneo ya Amani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kule Amani kama walivyoona ni kwamba kuna mambo mengi sana ya vivutio vya utalii, acha pamoja na mambo ya kuwa na miti mirefu hapa duniani, pamoja na kuwa na majoka makubwa hapa duniani na mambo mengine mengi, lakini kitu kimoja ambacho Mawaziri hawa wameweza kukiona kule ni namna ya wananchi wa Fanusi maeneo ya Amani ambapo wanachuma/wanavuna vipepeo. Vipepeo ambavyo vinawaletea hela nyingi na kukuza uchumi sio Muheza tu na hata Mkoa mzima wa Tanga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa tatizo ambalo lilitokea kwenye uvunaji wa hawa vipepeo ni kwamba waliingia kwenye kundi la kuzuiwa kusafirisha vipepeo hivi nje ya nchi. Ni kwamba Serikali ilipiga marufuku kusafirisha wanyama pori hai nje ya nchi basi wakachukua na vipepeo. Lakini sidhani kama lengo la Serikali lilikuwa ni kuzuia vipepeo hawa kuzuia vipepeo hawa kusafirishwa nje ya nchi. Naamini kabisa Serikali ilikuwa na nia ya kuzuia wanyama wakubwa faru na wanyama wengine kwenda nchi za nje, lakini sio vipepeo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri wote wawili mliahidi mtalishughulikia suala hili, lakini siku zinavyozidi kwenda na wale wavunaji na wenyewe wanakata tamaa. Naomba suala hili Mheshimiwa Waziri utakapokuja ku-wind up jioni ulitolee maelekezo kwa sababu ni suala muhimu sana katika maendelezo ya uchumi pale Muheza, kwa sababu linaingiza fedha nyingi sana na pia uliahidi kuboresha yale maeneo kuwaboreshea wale wavunaji yale maeneo bado suala hilo bado Wakala wa Misitu hajalishughulika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili ambalo ni mgogoro wa muda mrefu pale Derema. Kuna wakulima ambao walikuwa kwenye hifadhi karibu 1,028 mgogoro huu ni wa muda mrefu tangu miaka kumi umeukuta na wote mlipokuja mliwaona wale wananchi walivyokuwa wanalalamika. Sasa hivi Muheza tumeanza kuwagawia viwanja kuwatoa pale wameshaondoka lakini tunawagaia viwanja eneo la Kibaranga ili waweze kuondoka vizuri. Lakini kuna fidia ambazo mapungufu ambayo wanadai na ni muda mrefu sana, sasa naomba suala hili pia Mheshimiwa Waziri utakapokuja ku-wind up jioni naomba ulishughulikie ili ulielezee/ulitolee tamko kwa sababu hata wiki iliyopita tu walikuwa hapa Dodoma hawakupata nafasi tu ya kuwaona. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la tatu ni suala la tiki, sisi tunalima tiki, tunalima tiki katika Afrika tunaongoza, tiki yetu iliyoko pale ni the best in Africa. Sasa suala hili Serikali inaelewa kabisa, kulikuwa na mpango ambao ulikuwepo ambao wakulima wa tiki ilikuwa inagaiwa kwenye vitalu. Sasa vitalu ilikuwa inawawezesha wafanyabiashara ya Muheza au kutoka nje kununua vile vitalu na kuweka viwanda pale Muheza. Sasa baadae mmeanzisha mtindo wa mnada, mnada ambao anakuja tajiri mmoja ananunua vitalu vyote kiasi kwamba ilisababisha viwanda karibu 10/12 vyote vya wilaya ya Muheza kufungwa.

Sasa mlipokuja mliwaona na Mheshimiwa Waziri uliahidi kabisa kwamba suala hilo unalirekebisha na wananchi wa Muheza watafaidika sasa kuanza kununua vile vitalu. Naomba hiyo ahadi yako itekelezwe ili tuweze kuweka viwanda ambavyo ni viwanda vingi kwa ajili ya uchumi wa Muheza.

Mheshimiwa Spika, na mwisho ni suala la Maafisa Misitu. Maafisa Misitu kupewa madaraka ya kukata au kutoa vibali vya misitu katika hizi Halmashauri. Suala hili limetokea hapa juzi Muheza ambapo Afisa Misitu wa Muheza ameamuru karibu misitu mia na ushee kukatwa. Sasa suala hili ni kubwa sana ambalo Baraza la Madiwani liliamua kabisa kupendekeza hawa watu wasimamishwe kazi.

Sasa ni vizuri hawa Maafisa Misitu ili kuweza ku-protect misiti yetu na wenyewe wawe answerable moja kwa moja kwa Katibu Mkuu. Kama vile Rais alivyoamuru maafisa/ wahandisi wa maji na watu wa ardhi wote waripoti moja kwa moja kwa Waziri Mkuu nafikiri Mheshimiwa Rais amesahau hii kitengo cha misitu na wao waende moja kwa moja wawajibike ili waweze kushughulikiwa kwa haraka pale panapotokea matatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, kwa sababu muda ni mdogo ningeomba kuunga mkono hoja na nakushukuru sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja na napenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napongeza juhudi zote Serikali inazochukua za kudhibiti utoroshaji wa madini yetu kama uimarishaji wa mifumo ya ulinzi sehemu mbalimbali zenye madini; uboreshaji wa mikataba mbalimbali ya madini na sheria; na uboreshaji na kuinua biashara ya madini.

Mheshimiwa Naibu Spika, pongezi kwa ukuta wa Mererani ambao umesaidia kudhibiti madini ya tanzanite, ila CCTV cameras ijengwe kuanzia sehemu ya ulipuaji; kituo kimoja kitakachokidhi mambo yote kwa pamoja kijengwe hapohapo karibu na mlango wa kutokea, pawepo na benki na sekta zote muhimu. Aidha, mnada wa tanzanite uboreshwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa kiwanda cha kusafisha/kuchakata madini ufanywe kwa haraka ili kuongeza thamani ya madini yetu badala ya kupeleka India.

Mheshimiwa Naibu Spika, Muheza maeneo ya Amani – Sakale, Kata ya Mbomole kuna madini ya dhahabu na wananchi kila mara wanakamatwakamatwa na kufukuzwa. Nimemuomba Naibu Waziri, Mheshimiwa Doto, wiki iliyopita anitumie wataalam tujue tuna madini kiasi gani, je, yapo Milima ya Sakale? Je, yapo katika Mto Kihara? Kama ni hivyo tutengeneze utaratibu mzuri wananchi wa Muheza waanze kuchimba huko Mlimani Sakale.
Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Spika, namimi nashukuru sana kupata nafasi ya kuchangia hoja hii ambayo ni muhimu sana.

Mheshimiwa Spika, hoja hii ni muhimu kwa sababu Wizara ya Fedha ndiyo Wizara ambayo inategemewa kwa mambo mengi na Wizara hii inatakiwa ijikite na ijiweke sawasawa kwenye mambo mbalimbali. Mipango ambayo inatakiwa ifanywe na Wizara hii kwa ajili ya shughuli za maendeleo hapa nchini ni muhimu sana. Na ni muhimu kwa sababu ni mipango ya kimkakati ya maendeleo ambayo inaweza kutufanya kuinua uchumi wetu.

Sasa ukiangalia kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri, Tume ya Mipango ambayo imeanzishwa kisheria chini ya Sheria ya Mipango ikiwa kwenye Fungu 66 Tume hiyo imeondolewa sasa hivi, imeingizwa moja kwa moja kwenye Fungu 50 la Wizara ya Fedha.

Mheshimiwa Spika, sasa nchi yoyote suala la mipango, suala la research, suala la plan ni muhimu sana. Sasa unapoondoa Tume ya Mipango unaiondoa unaiweka chini ya Wizara yaani ile mipango bwana mipango naye anatungenezea mipango aripoti kwa Waziri au kwa Katibu Mkuu, si atatengeneza mipango ambayo anaitaka. (Makofi)

Sasa hili ni suala moja na ambao Kamati ya bajeti imependekeza huo mpango kuondoa hili suala la Tume ya Mipango lirudi mara moja. Tunashauri sana ni muhimu sana, kwa sababu bila mipango hatuwezi kuwa na uchumi mzuri, hatuwezi kusema kwamba tunaendelea na mipango mizuri, uchumi unakua Tume ya Mipango lazima iwe independent na miaka yote imekuwa chini ya Ofisi ya Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni lazima hii irudi chini ya Ofisi ya Rais maana yake baadaye tutakuja kuisema CAG nayo iende chini ya Wizara haitakuwa independent, kutakuwa na check and balance za aina gani. Kwa hiyo, hilo ni wazo moja ambalo nashauri na Wizara iweze kulichukua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili ni suala la utoaji wa fedha za mifuko ring fence, hapa tumeona fedha mbalimbali ambazo zimewekwa kwa kisheria kabisa kwamba fedha hizi ziende kwenye mambo ya maji, fedha hizi ziende kwenye mambo ya reli, kwenye mfuko wa reli, fedha hizi ziende kwenye labda korosho, fedha hizo zinakwenda badala zinachukuliwa zinakaa palepale BOT. Sasa inakuwa ni muda mrefu kuna kitu kinaitwa letters of credits, letter credits (LCs), Benki Kuu inafungua tangu lini? LCs zinatakiwa zifunguliwe kwenye matawi kule. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa tumeona hapa ucheleweshaji wa fedha za REA ambao baada ya Kamati kuingilia ndiyo haya mambo yameanza kuingiliwa. Sasa tumeona ucheleweshaji pia wa Mfuko wa Reli na baada ya Kamati kuingilia mambo hayo yameanza kutekelezwa. Sasa huu urasimu tunataka Wizara iuondoe na tufuate sheria, hizi fedha zinatajwa hizo zitakatwa kwa kufuata sheria. Kwa hiyo, tunaomba fedha hizi ziende kwa misingi ya sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la tatu ni suala la michezo hii ya kubahatisha, hili suala la michezo ya kubahatisha sasa hivi limechukua kasi sana na ni nzuri sana kwa sababu Serikali inapata kodi. Lakini tatizo moja kubwa ni watoto ambao ni chini ya miaka 18. Sasa hivi wamekuwa wanachukua hela za wazao wao kuingia kwenye hii michezo. Sasa ni lazima Wizara iangalie namna gani inaweza kudhibiti hawa watoto wasiweze kuingia kwenye hii suala la kuingia kwenye michezo ya kubahatisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine ambalo namuomba Waziri alitolee ufafanuzi ni suala la shilingi milioni 50 za kila kijiji. Hili limeleta matatizo sana village empowerment, sasa suala hili katika bajeti ya mwaka 2016/2017 limetengewa shilingi bilioni 60, bajeti ya mwaka 2017/2018 shilingi bilioni 60. Lakini hakuna hata senti moja imetoka, sasa ni vizuri Waziri akikaa pale jioni atuambie kwamba kweli hizi fedha zipo au huu mpango upo kwa sababu ni kazi kubwa kwenye 2020.

Mheshimiwa Spika, mifuko ya PSPF, jana Naibu Waziri alijibu swali la askari wa magereza kwamba wamelipwa. Lakini ukweli na malalamiko mengi ya askari polisi ambao bado wako kambini hawajalipwa mafao yao kuanzia mwaka 2016/17 na 2017/2018. Juzi tu wiki iliyopita wakati naweka mafuta hapa mjini askari mmoja akanifuata afande mimi ni fulani fulani akaniambia; “mimi nimestaafu tangu mwaka jana ambapo ilikuwa ni mwaka 2016/2017 hatujalipwa” na wako kambini. Sasa wako Kambini ina maana kwamba wanasema hawawezi kutoka kwenye kambi kama hawajalipwa hizi hela zao vinginevyo hatapata kabisa. Sasa niliomba Mheshimiwa Waziri suala hili ulifuatulie kwa makini sana kwasababu haya malalamiko yao na hizi PSPF hawajalipa hizi fedha kwa kipindi cha miaka miwili, hawa askari walipwe hela zao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la rufani za kodi, pamekuwa na mashauri mengi, report zinaonesha karibu mashauri 320 lakini katika mashauri hayo ni asilimia 31 tu ambayo mashauri haya yamesikilizwa. Sasa mashauri ya kodi, rufaa kwenye Baraza la Kodi yanakuwa ni mengi na hayasikilizwi kwa wakati, sasa ni vizuri Waziri aangalie utaratibu gani ambao utafanyika hizi kesi ziweze kusikilizwa na kwanini rufaa za kodi zinakuwa ni nyingi.

Mheshimiwa Spika, ningeshauri kwamba ni vizuri kuanzia kwenye utaratibu wa negotiations badala ya kuanza kukimbilia kwenye Mabaraza ya Kodi au kwenye makesi kwa sababu hawa ni walipa kodi ambao wanatakiwa waangaliwe kwa uangalifu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni Msajili wa Hazina; pale tumeona kwamba kwenye report changamoto ambazo zimekuwepo ni baadhi ya wawekezaji ambao walikabidhiwa, walinunua mali za ubinafsishaji, bado mali zile zipo tu. Pamoja na juhudi kubwa na kelele nyingi za Serikali lakini hawa watu bado hizi mali wanazo na hakuna utaratibu wowote wa kuwanyang’anya, kama wamenyang’anywa basi ni kidogo sana. Ufanyike utaratibu, Msajili wa Hazina apewe madaraka, Msajili wa Hazina hata ukiangalia kwenye mafungu ambayo amepewa, amepewa hela ndogo sana. Sasa suala hilo Msajili wa Hazina akaangaliwa na kuweza kupewa hela ambazo zinatosheleza.

Mheshimiwa Spika, na suala la mwisho ni suala la ubia (PPP). Hiki kitengo ambacho kipo pale cha PPP hakijapewa umuhimu kwa sababu kitengo hiki kina maandiko mengi ambayo yanafanywa lakini mpaka sasa hivi pamoja na miradi mingi mikubwa ambayo inaonekana kufanyika hapa nchini lakini hiki kitengo ukiangalia fedha ambazo kimepewa ni kidogo sana na ni kitengo ambacho kinatakiwa kipewe nguvu, kipewe hela, kiweze kuingia kufanya lobbying na watu kiweze kuhakikisha kwamba tunaingia miradi mikubwa mikubwa hii kwa njia ya PPP.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo nakushukuru sana na naunga mkono hoja.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Spika, nami nashukuru sana kwa kupata nafasi hii ya kuchangia hoja hii ambayo ni muhimu sana ya Hali ya Uchumi na Mpango wa Maendeleo pamoja na Bajeti ya mwaka 2018/2019. Kwanza nampongeza sana Waziri wa Fedha, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu, Wakurugenzi wote na Watendaji wote wa Wizara ya Fedha. Najua kazi kubwa wanayo, lakini kutuletea bajeti hii ni kitu kimoja ambacho wamefanya usiku na mchana na kwa kweli bajeti imeonekana na ni nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Rais hasa kwa kipindi hiki kifupi cha miaka miwili na nusu kuweza kuja na miradi mikubwa, ya kisasa na ya kileo ambapo kwa kweli miradi hii itakapomalizika, naamini kabisa kwamba uchumi wa nchi yetu utakuwa mkubwa sana. Miradi hii imeorodheshwa vizuri kabisa. Miradi kumi ambayo ameiorodhesha Mheshimiwa Waziri kwenye kitabu chake cha mpango ambayo ukianzia na reli, mambo ya ndege, mambo ya bomba la mafuta, umeme, Mkulazi na kadhalika, ni mizuri sana na imechukua matrilioni ya hela, lakini hii itakuwa ni historia ambayo Awamu ya Tano itaiweka katika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, bajeti hii ni ya tatu ya Awamu ya Tano. Kwa kweli ukiiangalia bajeti hii ni nzuri sana na imelenga hasa kulinda viwanda vya ndani. Mheshimiwa Waziri ameeleza kwenye hotuba yake hapa, ameongeza kodi nyingi sana kwa bidhaa ambazo zinatoka nje kwa ajili ya kuingia ndani. Kwa kweli tunampongeza sana kwa sababu kutoka page 48 - 52 ameorodhesha bidhaa zote hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Waziri na hii ni hatua nzuri ambayo inaonekana kutoa mwanya sasa kwa wawekezaji kuweza kuweka viwanda hapa nchini, kuongeza ajira na kufanya mambo mengi ili ku-discourage importation kutoka nje. Suala hili la ku-discourage importation kutoka nje lilifanyika na nchi nyingi tu; India wanafanya sana, hawataki bidhaa kutoka nje au vitu kutoka nje na wanatumia vitu vyao vya ndani, South Afrika na nchi nyingine nyingi. Kwa hiyo, hii ni hatua na mwenendo mzuri sana ambao naamini kabisa utatupa faida sana kwenye hii nchi.

Mheshimiwa Spika, napenda sasa nianze kuchangia pia kwenye mambo ya mfumo mpya wa kodi za Electronic (Eletronic Tax Stamp - ETS). Mpango huu ni mzuri sana na ni mpango ambao unatutoa kwenye manual system na unatupeleka kwenye electronic. Ni mpango ambao utaweza kujua ni bidhaa gani zinazalishwa na kupata takwimu sahihi ambazo zinatoka kwenye viwanda.

Mheshimiwa Spika, mpango huu pia wameuchukua kwenye nchi nyingi ambazo wamewahi kufanya. Wameuchukua kutoka Kenya, Morocco, Uturuki, Malaysia na Switzerland. Nchi zote hizo ambazo zimechukua mpango huu, wamekwenda kwenye mambo ya sprits; bia, vinywaji vikali na sigara. Sasa sisi mpango huu tumejumuisha vinywaji vikali, bia, sigara, maji na soft drinks. Kitu ambacho nina wasiwasi na Kamati ina wasiwasi ni kwamba huenda tukaweka burden kubwa sana kwa mnunuaji, mtumiaji wa vitu hivi.

Mheshimiwa Spika, naona kwamba mpango huu ni mzuri na unatakiwa uanze mara moja, lakini ni vizuri Wizara ikajitathmini kwamba itakapochukua vitu vyote hivi in totality hasa maji na soft drinks, huenda mzigo mkubwa ukaenda kwa mtumiaji. Ni vizuri iangalie kwa makini kwa sababu siyo ajabu kwa mpango huu vitu hivyo vikaongezeka bei, ingawa kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri amesema kwamba bei hazitaongezeka kwenye bidhaa hizo, lakini nina uhakika kwamba wataongeza bei hapa. Kwa hiyo, naomba aangalie vizuri sana.

Mheshimiwa Spika, la pili, mpango huu, hiyo Kampuni ya SCIPA ambayo imepewa imeonekana kwamba itakuwa self financing, lakini sidhani kama itakuwa self financing. Hakuna biashara ambayo inafanyika bila kupata faida.

Mheshimiwa Spika, ni bahati mbaya tu kwamba vitabu vya hotuba yetu havijafika, lakini kuna mchanganuo ambao umetoa na unaonekana kwamba huenda kampuni hii ikapata faida kubwa sana. Wasiwasi uliopo ni kwamba, kampuni hii tumeipa miaka mitano. Kwa nini tuipe miaka mitano? Kwa nini tusipunguze? Tumeweka mkakati gani wa kuweza kuangalia kwamba tutafanya vipi kuweza ku-train watu wetu ili baada ya huo muda tuweze kuendelea wenyewe na huo mpango? Kwa hiyo, niliona tujaribu kuangalia hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine nataka tuangalie system hii ya Akaunti Jumuifu ya Hazina (Treasury Single Account). Tumekwenda vizuri sana kwenye Mifuko. Mfuko wa Maji umekwenda vizuri sana na umesaidia sana, kwa sababu ulikuwa ring fenced kwamba huruhusiwi, umezuiwa na Hazina walikuwa wamefanya vizuri sana wanapopata fedha zile moja kwa moja wamezipeleka kwenye maji na umesaidia sana kuleta maendeleo ya maji na miradi mingi ya maji. Hii ni pamoja na REA na barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hivi tumekwenda tunataka tuanzishe hii Treasury Single Account, kwamba sasa hii Mifuko yote inaweza kufa. Itakapokufa, majukumu yote yanakuwa kwa Wizara. Sasa hii ni issue ambayo ni muhimu sana Waheshimiwa Wabunge tuiangalie. Kweli Wizara imejitayarisha kupokea hela zote na kuhakikisha inazigawa hela zote kwa wakati? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hapa ni muhimu sana kuangalia; Wizara imejitayarisha namna gani? Ni vizuri kama wanajitayarisha, wajitayarishe kwa E-system ili kuweza kutoa hizo fedha kwenye maendeleo. Kwa sababu kuna miradi mingi ambayo imeshaanza, imetiwa saini, lakini hakuna uhakika wa kwamba hii system itakapoanza wakati huu, hiyo miradi itaendelea namna gani?

Mheshimiwa Spika, hapa tunaona hela za maendeleo zimechelewa sana kupelekwa kwenye mikoa. Sasa tunakuja kwenye E-system, hii miradi ambayo tumeshasaini mikoani itakuwaje? Ni vizuri Mheshimiwa Waziri atakapokuja ku-wind- up aweze kutoa ufafanuzi wa hili suala kwa sababu ni muhimu sana na nashauri kwamba tujitayarishe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine ni suala la PPP. Ni muhimu sana kitengo hiki kikaimarishwa kwa sababu miradi mingi na mikubwa, ni vizuri ikafanyika kwa njia hii. Naamini kabisa ile miradi ambayo feasibility study imeshafanyika, basi itangazwe. Itakapotangazwa, nina uhakika wawekezaji watatokea. Tumefanya hivyo kwenye hivi viwanda vya madawa na watu wengi wametokea. Sasa hii miradi mingine, kwa mfano road toll, barabara ya Ubungo - Dar es Salaam – Morogoro, Mheshimiwa Spika, kwa nini tusiingie kwenye road toll? Ni kitu cha muhimu sana, naomba sana tuangalie. Au feasibility study ya reli ya Tanga, imeshamalizika, kwa nini wasiitangaze sasa wawekezaji watokee? Naamini kabisa kwamba tutakapochukua uamuzi huu, mambo haya yataweza kwenda kwa haraka sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, kuna suala moja ambalo sekta binafsi inalalamika sana kuhusu malipo yao ya fedha za VAT. Wanadai shilingi bilioni 600, haya mambo ya wawekezaji kwenye mambo ya sukari. Naamini kabisa Serikali italiangalia kwamba umechukua hizi hela 15%, basi hakikisha unazirudisha kama ambavyo umeamini.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, mengine nitaandika, nakushukuru sana kwa muda huu.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nashukuru sana kupata nafasi hii kuchangia hoja hii muhimu sana. Ni hoja muhimu kwa sababu ni madini ambayo yanaongeza pato la Taifa. Kwanza napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa hatua mbalimbali ambazo amezichukua kuweza kuboresha sekta hii ya madini na mpaka sasa hivi tunaanza kuona faida yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kipindi kifupi sana utaona Wizara hii kazi ambayo imefanya ni kubwa sana kwa sababu imeweza kuongeza pato la Taifa kwa asilimia 4.8. Hii ni kutokana na uimarishaji wa mifumo mbalimbali ya madini ambayo imefanyika kwa haraka sana, uangaliaji wa mikataba mbalimbali ambao umefanyika pia kwa haraka sana na utungaji wa sheria mbalimbali ili kuweza kuendana na hali ambayo inaweza kurahisisha kufanya mchango huu wa madini uweze kuongeza pato la Taifa na uboreshaji wa biashara hii ya madini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais ameunda Tume mbalimbali kwa lengo la kuweza kusaidia uimarishaji huu ambapo kwa kweli manufaa yake yanaanza kuonekana sasa hivi. Utoroshaji ulikuwa ni mkubwa sana na sasa hivi udhibiti ambao umefanyika ni mzuri sana. Nashauri Wizara na Mheshimiwa Waziri muendelee na kazi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili ambalo napenda kushauri ni kuhusu tanzanite kule Mererani. Nafahamu kwamba ukuta umejengwa, ni kazi nzuri sana ambayo imefanyika. Kwa kipindi kifupi tu cha miezi mitatu ukuta ule umeweza kujengwa ambao ni mkubwa sana na umeweza kuzaa matunda kwa sababu sasa udhibiti wa tanzanite umeanza kuonekana. Tanzanite ilikuwa unatoroshwa sana na kama unaona takwimu ambazo zimetokea kwenye mitandao mbalimbali India imeonekana kuna tanzanite nyingi sana, ikifuatiwa na Kenya na sisi ambao ndiyo wazalishaji hatuna tanzanite au kiwango chake ni kidogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ningeshauri kama nilivyoshauri Kamati kwamba camera’s ziwekwe na ziwekwe kuanzia kwenye ulipuaji kule chini ili kila kitu kiweze kuonekana. Hivi ni viboresho ambavyo vitaongeza udhibiti pale pamoja na ule ukuta.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini si hivyo tu, kuna suala la kujenga kituo ambacho kinakuwa one stop pale pale kwenye mlango pale kwamba baada ya kutoka waingie kwenye kile kituo waweze kukaguliwa au kukabidhi kama ni leseni au ni export license, kama ni masuala ya benki yaweze kufanyika pale pale. Kwa hiyo, hicho kituo ni muhimu sana vinginevyo wanaweza wakatoka pale halafu ikaingia mjini. Kwa hiyo, tunataka ikitoka tanzanite pale Mererani basi moja kwa moja inakwenda airport kwa ajili ya usafirishaji. Hilo ni suala muhimu sana ambalo ningeomba Waziri aliangalie na liko kwenye mapendekezo ya Kamati.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ambalo napenda kulizungumzia ni ujenzi wa kiwanda cha ku-add value kwenye madini yetu ambayo yanapatikana, si tanzanite tu bali hata dhahabu na almasi. Nimeona kwenye hotuba ya Waziri na hotuba ya Waziri wa Viwanda, lakini ni muhimu suala hili likajengwa haraka ili liende sambamba na hizi juhudi ambazo zinafanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ambalo napenda kuliongelea ni kwenye Jimbo langu Amani. Kule tuna aidha dhahabu, kwa sababu watu wengi sana wanakwenda kuchimba na imekuwa ni tabu sana kwa sababu wananchi wa Amani, Muheza wanasumbuliwa mara kwa mara kukamatwa na kufukuzwa. Kule kuna safu za milima ya Sakale, tunaamini kabisa kwamba kwenye hiyo milima ya dhahabu, ndio maana wananchi wanakwenda wanafukuzwa na wanayapata.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimewahi kuongea na Naibu Waziri, Mheshimiwa Doto, nafikiri analifanyia kazi. Ni muhimu tupate wataalam waende wakakague ili waweze kuwashauri wananchi wa Muheza waweze kujua kwamba tunachimba dhahabu na iko kiasi gani na waweze kupata leseni kihalali kabisa badala ya kukamatwa kamatwa na kusumbuliwa kama inavyofanyika sasa hivi.

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, kuna maeneo ambayo watu wameyahodhi, mengi tu na wengine wana leseni na wanalipia lakini hawayafanyii kazi. Wengine wanayaweka kwa lengo ya kuyauza, sasa wanapokuja wawekezaji wanataka kuwekeza inakuwa ni tabu kwa sababu wanakosa ardhi, wanakosa sehemu ya kuwekeza na inaleta matatizo sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakumbuka niliwahi kuleta wawekezaji na wakaambiwa hakuna sehemu yenye madini, sasa inakuwa ni tabu, ukitaka muone mtu fulani. Sasa ni suala ambalo linatakiwa kuangaliwa. Hili shirika letu la STAMICO lipewe huo uwezo, wawe na maeneo ambayo ni maalum kabisa mtu ambaye anataka kuwekeza anakwenda STAMICO anaambiwa nenda mahali fulani utalikuta hilo eneo, kaangalie, kapime endelea na hiyo kazi. Kwa hiyo, ni muhimu kuwa na maeneo maalum ambayo yataweza kuwasaidia wawekezaji whether ni wa hapa nchini au wa nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja, ahsante sana.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nashukuru sana kwa kupata nafasi hii kuchangia Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 2019/2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kusifu sana juhudi ambazo Serikali ya Awamu ya Tano imezifanya katika kipindi cha miaka mitatu. Imefanya mambo mengi ambayo yatakuwa ni historia. Napenda sana kusifu hasa miradi mikubwa ambayo imeanzishwa na ambayo inaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mpango wa mwaka 2017, kuna mambo mengi ambayo ni ya msingi ambayo yameachwa hayakuorodheshwa kwenye Mpango wa mwaka huu na mapendekezo hayo Kamati ya Bajeti imeorodhesha vizuri sana katika page namba 13. Pamoja na mapendekezo hayo, napenda kujikita zaidi kwenye mambo mawili ambayo naona ni ya msingi sana na napenda kujua kwa nini yameachwa kwenye mapendekezo ya mpango wa mwaka huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni barabara ya Chalinze Express Way. Barabara hii naona imeachwa na sijui kwa nini imeachwa. Cha msingi tunaona ni muhimu kwenye mapendekezo haya barabara hii ikaingizwa kwa sababu mapato mengi sana yanategemewa kwenye mambo ya road toll.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimekuwa nikizungumza suala la road toll tangu mwaka 2017 lakini naona bado Mheshimiwa Waziri hajaona umuhimu wake, lakini road toll ni muhimu sana kwa sababu Mataifa mengi duniani sasa hivi unapoenda unakuta kwamba kuna mageti ambayo yanakusanya mapato na mapato yanaweza kupatikana kwa urahisi zaidi. Najua inawezekana sababu mojawapo ni uanzishwaji wa SGR, lakini SGR ni kitu kingine na mambo ya barabara ni kitu kingine kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni suala la Bandari ya Bagamoyo. Bandari ya Bagamoyo imeachwa kabisa na sijui ni kwa nini imeachwa. Bandari hii imeshughulikiwa kwa kiwango kikubwa sana. Nakumbuka mpaka MoUs ambazo tumewahi kuzisaini kati ya Serikali yetu na Serikali ya Oman pamoja na Serikali ya China tulifanya sherehe kubwa sana kule kwenye Ubalozi wetu Oman kusherehekea mradi huu, lakini sasa hivi naona kama mradi huu haupewi umuhimu ambao unatakiwa. Nashauri kwamba mradi huu na wenyewe uweze kuingizwa kwenye mapendekezo ya mipango ya mwaka 2019/2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kiwanda pia cha kuchakachua au kusafisha madini sijaona mpango huo kwenye Mapendekezo ya Mpango huu ya Mheshimiwa Waziri. Ningefurahi sana kama na suala hilo pia lingeweza kuingizwa kwenye mpango huu wa 2019/2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni uchimbaji wa gesi asilia. Suala hili naona pia limesahauliwa na sijui ni kwa nini, lakini utakumbuka kwamba gesi yetu asilia tulikuwa na wawekezaji wengi sana kule Mtwara na Lindi, lakini wawekezaji wale wameondoka na sasa hivi wamehamia kwenye nchi jirani tu pale, lakini suala hili halijapewa umuhimu wa kipekee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nikisoma kwenye mitandao taarifa fulani nikaona kwamba wawekezaji ambao walikuwa wawekeze kule, moja ni Kampuni ya Shell sasa hivi imeenda kuwekeza kule na imejenga mitambo ile ya LNG Canada kule British Columbia kwa gharama kubwa sana. Sasa tunaona tunampoteza mwekezaji mkubwa kama yule na ilikadiriwa kwamba mitambo hii ambayo ingewekwa hapa nchini, kwa mwaka tungeweza kupata zaidi ya trilioni 10 na kuendelea. Ni vizuri hayo mazungumzo ambayo yamekwamisha wawekezaji kuweza kuendelea kuwekeza kwenye suala hili yakapewa umuhimu ili yaweze kufanyika na kufikia muafaka mzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo Kamati ya Bajeti imependekeza ni suala la magofu kwenye shule, maabara na zahanati. Kuna magofu mengi sana na mwaka jana kwenye bajeti tulipendekeza kwamba hela nyingi ziwekwe kwa ajili ya kukamilisha magofu haya, lakini naona kwenye mapendekezo ya mwaka huu hayapo. Ni vizuri aka- take note ya mambo hayo ambayo ni muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni miradi ya mikakati. Suala hili ni zuri sana kwa sababu najua miradi ya mikakati ambayo ilipitishwa kwenye mwaka wa fedha 2017/2018 ni 17 tu, lakini ni vizuri miradi hii ikasambazwa kwenye kila Halmashauri, kwa sababu najua ni source kubwa sana ambayo ingeweza kuleta mapato mengi kwa Serikali kama miradi hiyo itaweza kuwekwa kwa wingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi hii ni vizuri ikagawiwa kwa usawa kwa sababu utakuta ile miradi 17 ambayo imegawiwa, mikoa mingine imepata miradi miwili, mitatu wakati mikoa mingine haijapata mradi hata mmoja. Ni vizuri iangaliwe ili tuweze kupata usawa katika ugawaji wa miradi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kilimo linatakiwa liongezewe fedha. Kwa kweli Wajumbe wengi wameongea hapa na ni muhimu likaangaliwa. Fedha ambazo zinatengwa kwenye sekta ya kilimo ni ndogo sana na ni vizuri fedha hizo zikaongezwa ili tuweze kusonga mbele kwa sababu kazi kubwa ya Watanzania wengi iko kwenye kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la maji pia ni vizuri liangaliwe. Sasa hivi tumefanya vizuri sana kwenye mambo ya miundombinu, lakini suala la maji bado ni tatizo kubwa, linaleta matatizo mengi sana kwa wapiga kura wetu na wananchi wote wa Tanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi huu mpango wa certificate, tumepeleka certificates kule, wakandarasi wamefanya kazi, certificates zimekwama kule karibu miezi sita. Sasa Wizara ya Maji sijui inatuambia nini kwa sababu linakwamisha na jinsi unavyomkwamisha mkandarasi anaongeza interest kwenye ule mradi kufuatana na mkataba ambao upo. Ni vizuri suala hilo likaangaliwa kwa undani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la REA pia ni vizuri likaangaliwa kwa sababu wakandarasi wapo na kila siku kule wanakwambia kwamba tunasubiri vifaa. Mheshimiwa Dkt. Kalemani amefika Muheza na ameona hali ya kule, mkandarasi yule uwezo wake ni mdogo kabisa, ameweka vijiji viwili tu mpaka sasa hivi. Tangu Mheshimiwa Waziri amekuja kuzindua, hajaendelea tena, ukimwuliza anakwambia bado vifaa vinakuja, hivyo vifaa vitakuja lini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ni suala la motisha kwa watumishi wa Serikali. Kwenye Mpango huu sijaona kuongezwa mishahara ya watumishi. Mishahara ya watumishi ni kitu cha muhimu sana, hatuwezi kukaa na watumishi miaka mitatu hatujawaongeza mishahara, pamoja na mambo mengine, lakini hawawezi kuelewa. Kwa hiyo, naomba kabisa kwenye Mapendekezo ya Mpango huu kwenye bajeti ijayo mishahara iweze kuongezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nashukuru sana kwa kupata nafasi hii ya kuweza kuchangia hoja hii muhimu sana ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Kwanza, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu pamoja na Mawaziri wote kwa jinsi Mheshimiwa Waziri Mkuu alivyo- present hoja yake kwa weredi mkubwa sana, kwa sababu ametumia system ya PowerPoint na mambo yote mazuri ambayo alikuwa anayasema tulikuwa tunayaona pale. Kwa hiyo, nampa hongera sana. Nategemea na Waheshimiwa Mawaziri wengine basi na wenyewe wata-present kwa system ya PowerPoint ili tuweze kuona kazi nzuri ambazo zinafanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kazi nzuri ambazo zinafanywa na Serikali ya Awamu ya Tano, tumeona kazi nzuri sana na nyingi sana ambazo hazijawahi kufanyika katika nchi hii katika kipindi kifupi. Tumeona mambo ya kisasa ambayo yanakwenda na ambayo yanafanyika kwa weledi mkubwa sana na miradi mikubwa sana. Sasa pamoja na kazi hiyo, nilitaka kuchangia kwenye sekta zifuatazo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nitaanza na suala la uchumi. Hivi karibuni Mheshimiwa Rais aliwaelekeza TRA kuangalia uwezekano wa kupunguza mapato kwa sababu kodi ambazo wanatoza ni kubwa sana to the extent kwamba wananchi wa kawaida wanashindwa kulipa kodi na badala yake wanatumia njia mbalimbali za kukwepa kodi au kukimbia nje ya nchi ili mradi tu waweze kuona kwamba watafanya vipi kukwepa kodi?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Rais aliposema TRA ni lazima waangalie namna gani wanaweza kupunguza kodi, wananchi wasiweze kukimbia kulipa kodi. Hivi karibuni tulikwenda Kampala kuangalia wenzetu wanafanyaje kwenye Treasury Single Account. Kule Kampala pamoja na mambo mengine tulikutana na Watanzania wengi. Watanzania ambao wanatoka hapa wanakwenda Kampala kununua bidhaa na kuzirudisha hapa, bidhaa hizo hizo zimepita kwenye bandari yetu hapa hapa na zimekwenda na baadaye wale wale wanazifuata kuzirudisha hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hii system kwa kweli ni kitu ambacho Mheshimiwa Rais alikuwa anasema. Kwa sababu hapa ilikuwa ni kama hub, ilikuwa ni kana Dubai, tuna bandari sisi. Walikuwa wanakuja wafanyabiashara wengi, Afrika Kusini, Zimbabwe, Malawi, Zambia, wote walikuwa wanakuja hapa. Sasa wamehama wote, tumewakuta kule. Sasa ni vizuri suala hili likaangaliwa. Tuliongea na Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwenye Kamati na aliahidi kutuma watu ili kuangalia kwamba tutaweza kulirekebisha namna gani?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni muhimu sana watu waende kwa sababu tunafanya mambo mazuri sana juu kule, miradi mikubwa sana inafanyika, lakini bado sasa hivi tuangalie namna gani tunaweza kupunguza kodi, namna gani tunaweza kufanya wananchi wetu kulipa kodi bila ya kukimbia au bila kufanya mchezo mwingine. Kwa sababu hapa karibuni tu kule Tanga kuna kiwanda kikubwa sana cha Pembe ambacho ni cha ngano; jamaa kafunga kiwanda kwa sababu ya kukimbia kodi. Kafunga kiwanda na kageuza mambo mengine; kwa mfano, magari yake sasa yanasomba mchanga au kitu kingine chochote. Kwa hiyo, ni suala muhimu sana ambalo naomba liangaliwe kwa undani wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili ni suala la hizi ndege zetu ambazo zimekuja. Tunategemea ndege hizi zifanye, nimeona faraja sana kwa sababu tulikwenda na Airbus mpaka Kampala na tukaja kuchukuliwa na Airbus hiyo hiyo. Kwa kweli tulipofika KIA ilijaa kabisa ile ndege. Kwa hiyo, ni fahari kubwa kwamba hizi ndege zina umuhimu wake na zitasaidia sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika taarifa ya Mheshimiwa Waziri Mkuu sikuona akitaja uwanja wa ndege wa Tanga. Tunategemea nasi tupate ndege ya Bombardier iweze kushuka pale. Sasa nategemea wakati Wizara itakapokuja kutoa taarifa zake, basi itaona kwamba Tanga sasa hivi kwa sababu ya umuhimu wake, wawekezaji wengi wanakuja, basi nasi tuweze kupata ndege ambayo itakuwa pale Tanga. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la tatu ambalo nataka kuchangia ni wawekezaji. Ni kweli ukiangalia kwenye taarifa ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kwenye World Investment Report ya mwaka 2018, sisi tunafanya vizuri sana hapa Afrika Mashariki. Pamoja na kufanya vizuri, inabidi tuangalie kituo chetu hiki cha TIC. Tunategemea TIC tumeita ni lakini ni lazima tuhakikishe kwamba ni kweli real One Stop Center kwa ajili ya kuwaweka hawa wawekezaji ili mwekezaji akifika pale, hana sababu ya kuzunguka kwenda mahali pengine popote. Ni kuhakikisha kweli vibali vyote, leseni na vibali vyote vya kuishi nchini vinapatikana bila matatizo yoyote. Bila kufanya hivyo, itakuwa ni delays ambazo hazina umuhimu. Mara nyingi sana wanapofanya assessment hasa za mambo ya corruption na uboreshaji wanaangalia hizi systems, wawekezaji wanakuwa handled namna gani? Unatoa leseni kwa muda gani? unachelewesha kwa muda gani? Je, kuna land bank pale kwenye kituo chetu? Kwa sababu mwekezaji hawezi akaja ukamwambia basi nenda katafute ardhi sehemu nyingine, kuna huyu jamaa uende ukaongee naye. No, inatakiwa akija pale kweli ni One Stop Center, anakutana na kila kitu; kama ni ardhi anaoneshwa, unataka hapa au hapa? Basi yeye ni juu yake kuangalia kwamba anataka sehemu gani?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni muhimu sana kurekebisha vitu kama hivyo. Ni muhimu kwenye Wizara ya Mambo ya nchi za Nje ikafungua kitengo kabisa. Sasa hivi Mabalozi nje kule wamehamasishwa sana na wanatafuta wawekezaji kwa bidii sana. Sasa itakuwa wawekezaji wanatafutwa, wanakuja pale, halafu Foreign Affairs wanakuwa hawana kitengo au department maalum ya kuwashughulikia au kupokea wawekezaji, badala yake Balozi atoke nje aje nao mpaka hapa, aanze kuzunguka kwenda huko.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni jukumu ya Foreign Affairs kuweka mazingira mazuri na ni jukumu la TIC kuweka mazingira mazuri. Ninaamini kabisa kwa sababu imekuwa ni Wizara maalum, basi Wizara hiyo itashughulikia mambo haya yaweze kwenda vizuri tuweze kupata wawekezaji wazuri zaidi. Ni vizuri ndege yetu hii Dreamliner sasa ikaanza kufanya kazi, kwa sababu itategemea kwa sababu hakuna mwekezaji ambaye anafurahia kwenda na direct flight. Hakuna mtalii ambaye anafurahia kupata ndege ya direct flight badala kuingia kwenye transit kwenye Miji mingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni vizuri hizi ndege zianze kufanya kazi tuweze kupata watalii wengi na tuweze kupata wawekezaji ambao ni wazuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho ambalo nilitaka kuchangia ni suala maji. Maji hasa Muheza ni siasa. Juzi juzi Kamati walikwenda kule na wenyewe watanisaidia kudhihirisha kwamba tuna tatizo kubwa la maji Muheza na tuna tatizo kubwa la maji sehemu mbalimbali hapa nchini. Kuna mradi ule wa shilingi bilioni 500 ambao ofcourse nitakuja kuongelea nikipata nafasi kwenye Wizara ya Maji. Suala hilo tunamsubiri Mkandarasi Mshauri (Consultant) kutoka India. Sasa tumekuwa tunamsubiri na taratibu nyingine, sasa sijui ni miezi mingapi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba Wizara ya Maji, kama ni kumsubiri, kwa nini tusitume mtu mara moja kwenda India na kurudi na hivyo vitu ambavyo vimebakia?

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kupata nafasi hii kuchangia kwenye Wizara hizi mbili ambazo ni muhimu sana; Wizara ya TAMISEMI na Wizara ya Utumishi na Utawala Bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nawasifu sana Mawaziri wote wawili kwa kazi nzuri ambazo wanazifanya. Namsifu sana Mheshimiwa Mkuchika na Naibu wake Mheshimiwa Mary kwa kweli tangu amehamishiwa kwenye wizara hiyo, wizara imetulia. Pia ningependa kuvisifu vyombo vya ulinzi na usalama kwa sababu kazi ambazo wanazifanya sasa hivi za usalama sio siri kwamba uko vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napongezakwa dhati kabisa kazi zinazofanywa na Mheshimiwa Rais na napongeza kabisa kazi ambazo wanafanya Mawaziri wa TAMISEMI hasa Mheshimiwa Jafo, Mheshimiwa Kandege na Mheshimiwa Mwita Waitara. Kwa kweli kazi ni nzuri na kwa kweli wanastahili sifa kubwa sana. Wamezunguka sana kwenye hii nchi na wamezunguka sana hasa kwenye Wilaya yetu; nakumbuka Mawaziri wote hao ninaowataja wamefika Muheza na wameona kazi za Muheza ambazo wanazifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Muheza tumefaidika sana kwa sababu tumepewa kwanza bilioni 1.5 kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya na kwenye mpango wa mwaka huu pia tumeongezewa milioni 500 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. Pia tulipewa karibu milioni 400 kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Mkuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tunajenga vituo vya afya kwenye kila Tarafa; kwenye Tarafa ya Amani, Misarai tunajenga kituo cha afya, Tarafa ya Bwembera tunajenga Potwe na Mhamba na kwenye Tarafa ya Ngomeni tunajenga Umba. Nakumbuka nilikuja ofisini na Mheshimiwa Waziri aliniahidi katika vituo vyote hivyo atajitahidi kadiri anavyoweza kuhakikisha kwamba kituo kimoja ananipa milioni 400 kwa ajili ya jiografia ya Jimbo lenyewe kwa sababu ya ukubwa wa Jimbo lile. Hata hivyo, nimeangalia kwenye kitabu bahati mbaya sijaona kituo chochote ambacho kimepangiwa wakati huu, lakini namwomba Mheshimiwa Waziri ajaribu kufikiria kutokana na ukubwa wa Jimbo la Muheza ambalo ni kubwa sana lenye kata karibu 37 na vijiji karibu 135.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la maboma na madarasa, tunashukuru sana Muheza tumepata milioni 225 kwa ajili ya kukamilisha maboma ya shule za sekondari na tumeweza kuanza kazi hiyo karibu kwenye sekondari tisa. Kazi hiyo inaendelea vizuri, isipokuwa tunalo tatizo kubwa sana ambalo ni la maabara, tuna maabara karibu shule zote za sekondari, karibu sekondari 21. Haya ni maboma ya maabara ambayo tulitegemea kabisa Serikali itusaidie kukamilisha maabara haya, hii imeleteleza tatizo linafanya hasa wanafunzi wa sekondari katika Wilaya ya Muheza kutokusoma sana masomo ya sayansi. Kwa hiyo, tunawashukuru sana na tunaomba sana kwa msisitizo mkubwa kwamba tuletewe fedha nyingine za maboma ya maabara ili tuweze kumaliza hili tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la upungufu wa watumishi pamoja na Walimu; suala hili ni kubwa sana na nitamwandikia barua Mheshimiwa Waziri kumpa takwimu sahihi ambazo zinaonesha upungufu ulivyo mkubwa hasa kwenye masomo ya sayansi na hisabati. Tuna upungufu mkubwa na upungufu hasa wa Wauguzi pia na Madaktari kwenye zahanati na hiki kituo chetu cha afya ambacho tunategemea kukifungua karibuni. Kwa hiyo, tunategemea kwamba upungufu huu utaweza kukamilika na kuweza kusaidiwa kuweza kupata Walimu hasa wa sayansi na hisabati kwenye sekondari.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna upungufu mkubwa pia kwenye shule za msingi. Shule nyingi za msingi zina Walimu kuanzia wawili, watatu, wanne; huwezi kutegemea Walimu wachache na shule ziweze kufanya vizuri. Matokeo yetu ya mitihani ya shule za sekondari na msingi sio mazuri kutokana na kuwa na Walimu wachache. Kwa hiyo, nashukuru kwamba tuweze kuangaliwa na kupewa Walimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala ambalo wenzangu wameliongelea la Madiwani, Madiwani tunawategemea sana kwenye hii miradi ambayo inaendelea sasa hivi. Wanafanya kazi kubwa sana Madiwani kwa sababu hasa Force Accountkwenye vituo vya afya na madarasa wanajituma sana na wanakuwa ni wahamasishaji wakubwa sana kwa wananchi wetu, ni vizuri suala lao la posho likaangaliwa ili waweze kuongezewa posho waweze kupata posho ambazo ni nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la TARURA, wenzangu wameolingelea kwa wingi sana lakini fedha ambazo wanapewa TARURA kutokana na kazi yao kubwa ni ndogo sana. Ni afadhali sasa hivi badala ya ile 70kwa30 basi ikaongezeka kidogo. Sisi kwenye Kamati ya Baajeti tunajitahidi kwa kadiri ya uwezo wetu kuhakikisha kwamba kwa kweli pendekezo hili linaweza kuchukuliwa kwa sababu TARURA kazi wanazofanya ni kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la miradi ya mikakati; miradi ya mikakati sisi Muheza tunategemea kujenga stendi ya kisasa na tumeleta maombi yetu yote na tunaamini yametelekezwa kwa ukamilifu kabisa, lakini tumeangalia pia hapa sikuona Muheza ikipewa chochote. Nilikuwa nafikiria Waheshimiwa Mawaziri wajaribu kwa kadiri ya uwezo waowaangalie kwamba wanaweza kutusaidia vipi, tunaamini kabisa kwamba tutakapopata fedha hizo za kujenga stendi mpya pale Muheza, basi tutaweza kujikimu na kuweza kujishughulikia na mambo yote ambayo tunayaweza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nakushukuru sana na naunga hoja mkono. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nakushukuru sana kupata nafasi ya kuchangia hoja hii ambayo ni muhimu sana na ni tatizo kubwa sana mpaka sasa hivi hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Waziri na Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na Wakurugenzi wote kwa kazi nzuri ambazo wanazifanya. Pia nawapongeza Mkurugenzi wa Tanga-UWASA pamoja na ma- engineer wa Muheza, Eng. Bakari na Eng. Elikana ambao wanafanya kazi kubwa sana kuhakikisha kwamba maji kwenye Jimbo la Muheza yanapatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kwanza, sisi Muheza tuna mradi, ukiacha mradi mkubwa lakini uko mradi ambao unatoa maji kutoka Tanga (Pongwe) na kuyaleta Mjini Muheza ili kuondoa tatizo la maji Muheza. Mradi huu ulitegemewa umalizike tangu Mei 2018 lakini mpaka sasa hivi mradi huo bado unaendelea kujengwa na uko kwenye asilimia 70.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi kubwa inafanyika lakini mradi huu ambao tunautegemea ulikuwa kwenye Quick- Wins ili kupunguza tatizo pale Mjini Muheza. Sasa hivi kama nilivyosema imebaki kitu kidogo sana ni asilimia 30 ili maji haya yaweze kutiririka pale Muheza ingawa haitakidhi sehemu kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo ambalo limebaki ni kufumua mabomba yaliyochakaa pale Mjini Muheza na kuweka mapya. Suala hili limesitishwa kidogo ili tusubiri mradi mkubwa wa maji wa kutoka India wa Dola milioni 500. Nimeongea na Waziri na nasisitiza sana kwamba waruhusu sasa hivi ili mabomba yale yaanze kufumuliwa kwa sababu tenki ambalo lilikuwa linachelewesha limekwishatengenezwa na limekaribia kumalizika. Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri na Katibu Mkuu mmefika kule na mmeona kazi kubwa ambayo imefanyika ya kutoa tenki kubwa Pongwe na mabomba yameshalazwa. Nashukuru sana hivi karibuni mmetoa fedha kwa wakandarasi na sasa hivi mabomba ya chuma yanalazwa kupelekwa kwenye chanzo kikubwa cha maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sasa hivi maji hayawezi kwenda kwa sababu bado hiyo sehemu ndogo ambayo imebaki ifumuliwe. Nimeona kwenye bajeti mmepanga karibu shilingi milioni 700, Mheshimiwa Waziri naomba uruhusu, wakati tunasubiri mradi mkubwa, mabomba ya Muheza Mjini yaanze kufumuliwa ili mkandarasi aanze kazi hiyo na maji yaanze kupatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, nashukuru sana kwamba tumepewa fedha kwa ajili ya maji vijijini, karibu shilingi bilioni moja na zaidi. Ipo miradi mingi sana pale ambayo imebuniwa, kwa kweli nawashukuru sana ma-engineer wa maji pale Muheza ambapo tumebuni na mmekwisharuhusu tutangaze zabuni kwa ajili ya kutafuta wakandarasi, kuangalia uwezekano wa kuanza kujenga Miradi ya Kwemdimu, Zaneti na Tongwe. Hii miradi ni maji ambayo yanachirizika kutoka milimani yaweze kusafishwa na kusambazwa kwa wananchi kule vijijini.

Kwa hiyo, nashukuru sana isipokuwa nashauri tupunguze urasimu wa kutoa vibali uliopo pale Wizarani. Baada ya kutangaza basi mruhusu moja kwa moja ili wapatikane wakandarasi na watie saini badala ya tena irudi Wizarani kuomba kibali kingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la tatu ambalo nataka kuongelea ni mradi huu wa India wa Dola milioni 500. Najua Mheshimiwa Waziri unatupa taarifa, maendeleo yanavyokwenda kila mara lakini mradi huu ni muhimu sana na una-cover miji karibu 29 hapa nchini. Mradi huu ukikamilika utapunguza sana tatizo la maji hapa nchini. Pamoja na kwamba suala hili lipo kwenye mchakato lakini unachukua muda mrefu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Waziri aangalie uwezekano wa kuona huu mchakato utafupishwa namna gani, umekuwa ni mrefu. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri naomba uweke jitihada sana kwenye suala hili kwa sababu watu wengi tumeliongelea kwenye majukwa ya kisiasa kwmaba mradi unakuja mpaka sasa hivi tunashindwa kueleza kwamba mradi unakuja namna gani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la nne, ni kama walivyosema Kamati kuhusu tozo ya maji ya shilingi 50. Suala hili limepigiwa kelele sana, miaka mitatu sasa na Kamati imependekeza hapa kwamba tozo ya shilingi 50 inatakiwa iongezwe ili ifikie shilingi 100. Hii ni kutokana na fedha ambazo zinapatikana kwa sababu fedha ambazo zinalipa wakandarasi sasa hivi inaonekana zote zimetoka kwenye Mfuko wa Maji wa Taifa. Mfuko huu umesaidia sana kuonekana kwamba Wizara haina fedha. Kutokana na Mfuko huu kuwa ring fenced, imesaidia sana kulipa malipo mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini fedha hizi hazitoshi, wewe mwenyewe Mheshimiwa Waziri umetembelea miradi mbalimbali hapa nchini na umeona kabisa wakandarasi wengine wamesimama kutokana na kutokulipwa fedha. Kwa hiyo, ni vizuri kilio cha Wabunge ambacho wengi tangu miaka hiyo tumekuwa tunasema tuongeze shilingi 50 ili tozo hii ya mafuta iweze kuwa shilingi 100 ili iweze kusaidia kidogo kupunguza tatizo kubwa la maji. Naamini kabisa kwamba tutakapoongeza fedha hizo basi inaweza kusaidia kwa kiwango kikubwa kuweza kufikia lengo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ni Uanzishwaji wa Mamlaka ya Maji Vijijini. Wazo hili ni zuri sana na tunategemea linaweza likasaidia sana kupunguza tatizo la maji kwenye vijiji vyetu. Hata hivyo, ni vizuri tuangalie tumeipangia kiasi gani na tutapata wapi fedha za kuanzisha Mamlaka hii kwa ajili ya kutatua matatizo ya maji vijijini? Tumeanzisha TARURA lakini fedha ambazo zinakwenda TARURA ni ndogo sana. Kwa hiyo, ni vizuri sana kuangalia uwezekano wa kupeleka fedha ili Mamlaka hii itakapoanza basi ianze kwa bidii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja na nakushukuru sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuunga hoja mkono na kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watendaji wote kwa kazi nzuri inayoonekana. Hata hivyo, bado ningependa kushauri na kujua hatima ya uanzishaji wa Chuo cha Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) maeneo ya Amani -Muheza. Majengo ambayo Mheshimiwa Waziri ameyaona yanazidi kuharibika bila kutumiwa, ningeshukuru kama suala hili litapewa umuhimu wa kipekee. Aidha, bado tunakumbushia suala la gari la wangonjwa, (Ambulance) ambapo katika Jimbo la Muheza hatuna kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la dawa ya nyoka kupewa bure kwa wananchi naomba lizingatiwe kwani bei ya dawa hizo ni ghali sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja na kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza kwa kazi nzuri Mheshimiwa Waziri, Naibu Katibu Mkuu, Wakurugenzi na Watendaji wote.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie suala la shamba la mpira Muheza na Kiwanda cha General Tyre, Arusha. Napongeza kwa kuonekana kwa dalili za kupatikana kwa mwekezaji za kupatikana kwa mwekezaji wa kiwanda cha matairi. Nimefika na Kamati ya Bajeti na kuona kiwanda hicho, kwa kweli hakuna kiwanda pale, maana mwekezaji mwenyewe anapaswa kutoa mashine zote za zamani na atapaswa kuweka mashine nyingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kushauri kwamba kutokana na Muheza kuwa na shamba kubwa la mpira ambalo hapo awali lilikuwa linalisha kiwanda hicho bora, kiwanda hicho kijengwe kwenye maeneo hayo hayo ya shamba husika. Tutakuwa tayari kutoa eneo kubwa kwa ujenzi wa kiwanda hicho. Naomba wazo hili lipewe uzito wake au atafutwe mwekezaji mwingine atakayewekeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni kuhusu biashara. Hivi karibuni Kamati ya Bajeti ilikuwa Kampala, Uganda. Kule tulikuwa wafanyabiashara wengi wa Kariakoo na wengine wa nchi jirani, wakinunua vitu mbalimbali na kuvirudisha nchini au nchini mwao. Wafanyabiashara wote hao walikuwa na biashara zao Kariakoo na sasa wamehamia Kampala.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri kwamba Wizara ijaribu kuchunguza kuona ni jambo gani lililowafanya wafanyabiashara hao kuhama? Vile vile iangalie uwezekano wa kuwarudisha.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja na ninapenda kupongeza juhudi kubwa za viongozi wote kwa mbinu mbalimbali inazofanya kuongeza ujio wa watalii nchini. Aidha, ninapenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, bado naleta hoja ya kuruhusu vipepeo hai viruhusiwe kwenda nje kibiashara na kitalii hapa nchini. Vipepeo ambao wanavunwa na kutunzwa na baadhi ya wananchi wangu maeneo ya amani ingewaongezea kipato. Aidha, ni ubunifu wao binafsi; sasa ni ubaya gani wanaofanya wa kupeleka nje ya nchi kwa biashara? Nchi nyingine wanafanya hiyo biashara. Vipepeo si hao wanyama kama ambao Serikali imefanya vizuri kuzuia. Nashauri leteni hiyo sheria Bungeni ifanyiwe marekebisho kwenye maeneo kama haya ya vipepeo. Haileti mantiki kulinganisha vipepeo na faru n.k.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaishukuru Wizara kwa juhudi kubwa (TFS) inazofanya kumaliza tatizo la wananchi wa Derema (1,028) ambao walihamishwa katika hifadhi. Kwa sasa tunamalizia wachache waliobakia kuwapatia ekari tatu tatu ila bado wanalalamikia wapunjo ya fidia ambayo bado hayajashughulikiwa. Naomba suala hili lishughulikiwe ili kuondoa haya malalamiko. Uhakiki na taarifa nzima ilikwishatumwa hapo Wizarani. Pamoja na Naibu Katibu Mkuu kuja na kufanya kikao na wahusika, bado tatizo hilo halijatatuliwa, naomba lipewe umuhimu tumalize hili tatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Muheza tuna sehemu nzuri ambayo watalii wameanza kuja kwa wingi sana, sehemu ya Magoroto. Ni muhimu sasa hivi wataalam wa Wizara watembelee eneo hilo washauri namna bora na hatimaye waliingize kitaifa kama ni moja wapo ya vivutio hapa nchini kupata matangazo mengi.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Spika, napenda kuunga mkono hoja na kuwapongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watumishi wote kwa kazi nzuri zinazoonekana kufanyika.

Mheshimiwa Spika, napenda kujua hatma ya maeneo ya Jimbo langu ambalo kuna dhahabu. Eneo hilo lipo Sakale, Amani na Mheshimiwa Waziri amefika eneo hilo na kuzungumza na wananchi. Nakushukuru ulituma wataalam wa sekta zote ambazo walifika eneo hilo, lakini bado hawajatoa taarifa yao. Namhakikishia Mheshimiwa Waziri pamoja na madini hayo kuwa karibu na chanzo cha maji ya Mto Zigi, lakini naamini tunaweza kukubaliana njia bora na ya kisasa kuweza kuchimba utajiri huo kitaalam. Naomba alipe umuhimu suala hili ambalo linanipa tabu sana Jimboni.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kupata nafasi hii kuchangia hoja hii ambayo ni muhimu sana katika nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza sana Mheshimiwa Waziri Kamwelwe na Manaibu Mawaziri, Mheshimiwa Kwandikwa na Mheshimiwa Nditiye (Mzee wa Minara), Katibu Mkuu na Wakurugenzi wote pamoja na Wakurugenzi wa ATCL, TTCL, TCRA, TANROADS na wengine wote. Nawashukuru sana kwa sababu Wizara hii kazi ambazo inazofanya ni nzuri sana na nafikiri kila mtu anaziona, katika sekta zote ambazo nimezitaja.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara hii imebeba Wizara nyingi sana na imefukia mashimo ya Wizara nyingi kutokana na kazi zake nzuri ambazo wanazifanya. Siyo siri kwamba miradi hii mikubwa imeipa sifa sana nchi yetu na ni miradi ambayo itabadilisha kabisa taswira ya Tanzania. Ni Wizara ambayo inatakiwa ipongezwe kwa sababu kwanza, Mawaziri na viongozi wake sasa hivi wanafanya kazi kubwa sana. Mawaziri hawa wametembea nchi nzima na wameona miradi ambayo iko kwenye mikoa yetu na wamejitahidi kwa kadri ya uwezo kutatua changamoto zilizopo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kuzungumzia Jimboni hasahasa barabara yangu ya Amani - Muheza kilomita 36. Barabara hii imekuwa inatengewa fedha tangu mwaka juzi, shilingi bilioni 3, mwaka jana shilingi bilioni 5, mwaka huu karibu shilingi bilioni 2 lakini tatizo ambalo lipo ni la mkandarasi kutopatikana. Najua Meneja wa TANROADS Mr. Ndumbaro anafanya juu chini lakini kila ukimuuliza anakwambia hapana, bado kidogo, kuna mchakato wa mzabuni. Zabuni hii imetangazwa mara tatu, mara ya kwanza mkandarasi hakupatikana, mara ya pili mkandarasi hakupatikana na hii mara ya tatu ndiyo naambiwa sijui kama atapatikana na naambiwa mambo yote yako kwa Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ndiyo uchumi wa Muheza. Muheza tunategemea barabara hii iwe kwenye kiwango cha lami ili iweze kuteremsha mazao kutoka Amani kwenda Mjini Muheza mpaka Dar es Salaam kwa ajili ya mauzo. Kwa hiyo, naomba uitolee maamuzi ili kabla mwaka huu wa fedha kuisha basi mkandarasi awe site. Nakumbuka Mheshimiwa Waziri nilikuona na nikakuomba kwamba fedha ambazo zimewekwa mwaka huu ni kidogo na ujaribu kuangalia namna ya kuweza kuziongeza. Nakushukuru sana kwa kupokea ombi hilo ambalo naamini utalishughilikia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na matatizo haya ya barabara ya Amani pia tuna matatizo ambayo tumeomba katika miaka hii miwili, mitatu iliyopita, kufanyiwa upembuzi yakinifu katikati ya barabara ya Pangani, junction ya Boza mpaka Muheza (kilomita 42) pamoja na Muheza – Maramba (kilomita 45) kwa matayarisho ya kuwekewa lami. Sikuona kwenye kitabu lakini naomba uangalie uwezekano ili ziweze kufanyiwa upembuzi yakinifu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni mawasiliano. Nimewasiliana sana na Mheshimiwa Nditiye, Naibu Waziri anayeshughulika na mawasiliano, kwa sababu mpaka wakati huu kiwango hiki tulichokifikia kuwa na sehemu ambazo hakuna mawasiliano ni tatizo kubwa sana. Tarafa ya Amani mawasiliano ni tabu sana, ukiangalia Kata zote za Amani yenyewe, Mbomole, Zirai, Kwezitu, Misarai, Magoroto pamoja na sehemu za Kwebada mawasiliano ni mabovu sana. Jana tu nilikuwa naongea na wewe Mheshimiwa Naibu Waziri na ukanihakikishia kwamba utashughulikia. Napenda niliongelee hilo ulishughulikie ili na wananchi wa maeneo ya Amani waweze kusikia kwamba kweli suala hilo linashughulikiwa na mawasiliano hivi karibuni yatakuwa ni mazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la SGR, nimeona hapa kwenye kitabu cha Mheshimiwa Waziri kwamba mpango wa kuweka SGR kutoka Reli ya Tanga - Dar es Salaam - Arusha – Msoma upembuzi yakinifu ulishafanyika na sasa hivi mikakati inafanyika ya kumtafuta mkandarasi kwa njia ya PPP ili na sisi reli ya Tanga tuweze kuwa na SGR. Suala hili ni la muhimu sana kwa sababu suala la PPP marekebisho yake tulishayafanya kipindi kilichopita na tunategemea kwamba suala hili lingeanza sasa hivi kutangazwa kwa sababu upembuzi yakinifu umeshafanyika ili tuweze kupata SGR Tanga line. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwamba Bandari ya Tanga inaendelea kufanyiwa ukarabati. Kwa hiyo, suala hilo ni muhimu sana liendelee na liweze kufanikiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala la ndege kwenda Tanga - Pemba, tulisikia kwamba sasa hivi bombardier itatua Tanga na itakwenda Pemba na kurudi Dar es Salaam. Mpango huo mpaka sasa hivi naona kimya, ningeshukuru sana kama Mheshimiwa Waziri utakapokuja hapa ku-wind up, basi utuambie kwamba na sisi Mkoa wa Tanga hii ndege ya bombardier itaweza kutua kwenye uwanja wetu kwa sababu sasa hivi kiuchumi tunakwenda kwa kasi kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho ambalo nataka kuongelea ni suala la express way, hili suala ni la msingi sana. Kila mwaka naongelea kwa nini hatuanzishi road toll kwenye barabara zetu. Ulimwengu mzima sasa hivi unakwenda na road toll, hakuna nchi ambayo utakwenda usikute imefungwa inatengenezewa road toll au kuna watu ambao wanalipa road toll. Hii ni njia mojawapo ya kuinua uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, juzi tulikuwa Kampala, tumeteremka Entebbe pale, Entebbe mpaka Mjini Kampala kuna express way wameshatengeneza wenzetu, mtu anachagua apite kwenye express way au aende kwenye barabara ya kawaida. Hivi vitu ni vya msingi na ni muhimu sana sijui kwa nini hii barabara ya Chalinze tusianzishe express way? Kama atapatikana mtu ambaye ana uwezo wa kutengeneza, akaweka road toll yake, kwa nini tunakataa vitu kama hivi? Nashauri sasa hivi tuangalia umuhimu wa kuanzisha road toll, express ways ni muhimu sana kwa maendeleo ya miji yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho ni suala la SGR ambalo mwenzangu Mheshimiwa Silinde hapa amelizungumzia lakini tunajua kwamba hawa watu wetu wenye viwanda vya vyuma, kweli hivi vyuma vilikuwa vinatoka nje lakini wewe mwenyewe Mheshimiwa Silinde utakubali kwamba wamekuja tangu juzi kwenye Budget Committee na wamekiri wameanza kupewa kazi hizo za kuweza ku-supply vyuma kwenye reli hii ya SGR. Hayo ni mafanikio kwamba sasa hivi wameanza na unajua kabisa kwamba Kamati ya Bajeti sasa hivi inashughulikia namna ya kufufua Mchuchuma-Liganga na jana tulikuwa na…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Kengele ya pili imeshagonga Mheshimiwa.

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kupata nafasi hii ya kuchangia Mpango huu wa Taifa ambao ni muhimu sana. Kabla sijaanza napenda kutoa pole kwa wananchi wa Muheza kwa mafuriko ambayo wameyapata pamoja na Mkoa mzima wa Tanga na kuwahakikishia kwamba Serikali inashughulikia matatizo yao na athari zote ili kurudi kwenye hali ya kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Waziri Dkt. Mpango kwa kutuletea Mpango mzuri na ambao hata ukiuona unaona kweli uko kwenye mwelekeo mzuri. Mimi sitakwenda kwenye takwimu ambapo naona tunakwenda vizuri kwenye ukuzaji wa uchumi ambao kwa sasa tuko kwenye asilimia 7.2 na tunategemea 2020/2021 tufikie asilimia 10 na hata mfumuko wa bei uko vizuri tu kwenye asilimia 3. Kwa hiyo, nitajikita kwenye miradi ambayo imeanza na inaendelea kutekelezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kilimo limezungumzwa kwa bidii sana na wachangiaji wengi lakini na mimi napenda kuongeza kwamba tunategemea kwenye Mpango huu ambao utakuja basi suala hili lipewe umuhimu wa kipekee. Tunaamini kabisa kwamba kilimo ambacho Watanzania wengi wanafanya na kinatoa ajira karibu asilimia 65 tunategemea kwamba kitatuinua. Ni suala la kuweka mipango vizuri kuhakikisha kwamba suala la umwagiliaji linapewa kipaumbele, suala la uanzishwaji wa mabwawa linapewa kipaumbele na naamini kabisa kwamba tukiweka fedha nyingi kwenye kilimo basi tutaweza kuendelea kwa haraka sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na mambo hayo, kuna masuala mengine ambayo yako kwenye kilimo kwa mfano suala la chai. Nimefarijika sana hapa nilipomsikia Naibu Waziri asubuhi akisema kwamba wana mpango wa kuanzisha mnada hapa nchini na kuondokana na suala la mnada wa Mombasa. Suala hilo sisi Muheza limetuathiri sana kwa sababu kampuni kubwa ambayo inalima chai pale inapeleka chai yake kwenye mnada Mombasa na Mombasa wananunua na wanafanya packaging na kurudisha tena kuuza hapa hapa nchini. Suala hili kiuchumi kwakweli linatuathiri sana na ni vizuri liangaliwe kwa uhakika na umakini kabisa ili tuanzishe mnada wetu hapa tuondokane na kupeleka haya mambo Mombasa. Vivyo hivyo ni vizuri pia kuangalia mazao mengine na kuanzisha hasa mazao ya viungo na mazao ya machungwa ili tuweze kuwa na bei elekezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Kitengo cha TMX ambacho Kamati ya Bajeti ilitembelea, kitengo hiki ni kizuri sana ambapo kikitumika vizuri basi Serikali inaweza ikawa na mazao mengi elekezi kwa bidhaa nyingi sana. Naomba kabisa Mheshimiwa Waziri Kitengo hiki kitumike ipasavyo. Tulikwenda pale lakini tumeona kwamba kitengo hiki hakitumiki kama inavyopaswa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile limeongelewa suala la uvuvi, Bandari ya Uvuvi ni muhimu sana. Bandari hii ilianzishwa kwenye bajeti iliyopita na ilitengewa fedha, nakumbuka mwaka 2017 kuna fedha ambazo zilitengwa lakini haijapewa umuhimu wake. Tunaamini kabisa kwamba tukifungua Bandari ya Uvuvi basi tutakuwa tumefika mbali sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la PPP ambalo nimekuwa nikiliongelea kila mara na naamini kabisa juhudi ambazo zinafanywa na Serikali sasa hivi, miradi hii mikubwa yote, SGR, ndege, umeme kwenye Bwawa la Nyerere naamini kabisa haya yangeoana na PPP sasa hivi hapa Tanzania tungekuwa tuna-boom. Kwa hiyo, naamini kabisa kwamba tumepitisha sheria hapa mwaka jana lakini mpaka sasa hivi hatujaona utekelezaji wake. Mheshimiwa Waziri tumekuwa tukisisitiza na naomba kusisitiza kwamba tangaza hiyo miradi ambayo tumeichagua. Tuliiona hapa miradi kumi ambayo bajeti iliyopita mlitusomea, tafadhali itangazwe ili watu wajitokeze na kama hawatajitokeza tuone tuna tatizo gani lakini ni suala ambalo linatakiwa lipewe umuhimu mkubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ATCL tumepita, nashukuru ndege zimefika lakini cha msingi hapa ni kuhakikisha kwamba tunaboresha na tunaanzisha route nyingi zenye tija ili kuweza kuleta watalii na wawekezaji hpa nchi kwetu. Tunataka Airport ya Dar es Salaam iwe hub, tuhakikishe kwamba hii Terminal III ambayo ipo inatumika kikamilifu. Sasa Terminal III bado ndege ziko chache lakini tunaamini kabisa kwamba wanaohusika watafanya juhudi kuweza kushughulikia na kuhakikisha kwamba Airport yetu inakuwa changamfu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la bandari ni muhimu sana. Uboreshaji wa bandari umekuwa mzuri, Bandari ya Dar es Salaam inaboreshwa vizuri, vilevile ya Tanga na Mtwara. Nimefarijika sana kwamba sasa hivi Bandari ya Tanga inachimbwa ili kuweza kupata kina kikubwa na naamini baada ya kazi hiyo kukamilika basi meli kubwa zitaweza kutua pale badala ya kwenda kutua Mombasa ambapo ilikuwa zinatua kule na baadaye zinaweza kuletwa hapa nchini. Kwa hiyo, suala hili ni la kupongezwa na tunaomba kabisa muendelee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wa bajeti nilizungumzia kiwanda kimoja kikubwa sana ambacho kinatarajiwa kujengwa na Wachina kule Tanga Hengia. Kiwanda hiki cha saruji tunategemea kitakuwa kikubwa na kuleta ajira kati ya 4,000 mpaka 8,000. Kiwanda hiki tunategemea kitoe tani karibu milioni saba kwa mwaka lakini nilipopita mara ya mwisho Tanga sioni chochote ambacho kinafanyika naambiwa tu mazungumzo bado yanaendelea kuweza kuwaruhusu Wachina hawa waweze kuweka hiki kiwanda. Kiwanda hiki ni kikubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapopata wawekezaji kama hawa inabidi na sisi tuchangamke wasije wakatupokonya. Kwa hiyo, naamini kabisa wakati wa winding up na nashukuru Waziri wa Uwekezaji yupo hapa watupe msimamo kiwanda hiki kimefikia wapi. Hawa Wachina wanazunguka karibu miaka miwili hapa na vibali mara hiki mara kile, mara incentives sasa tunaomba tupate uhakika nini kinaendelea. Huyu ni mwekezaji mkubwa na tunaamini kwamba atakapoweka kiwanda kile basi mambo yatakuwa vizuri sana siyo kwa nchi hii tu bali hata kwa Mkoa wa Tanga mambo yata-boom.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo nataka kulizungumzia, la mwisho ni suala la Soko la Hisa pale Dar es Salaam (Dar es Salaan Stock Exchange) tulifika pale lakini soko hili limeonekana limeduwaa kidogo haliko very active na tunaona haliko very active kwa sababu watu wengi hawajaliorodhesha, nataka Mheshimiwa Waziri ahakikishe kwamba Sheria ilishapitisha mashirika yote haya ya communication kwamba wajiandikishe kwenye soko la hisa, lakini mpaka sasa hivi ni Vodacom tu ambao wamejiandisha, sasa haya mashirika mengine ya simu kwa nini hayajajiandikisha? Nataka Waziri akija hapa aeleze ili tuweze kujua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ni kwamba Soko la Hisa la Dar es Salam lilikuwa linachangamshwa sana na haya mashirika ya kijamii. Sasa baada ya kuunganisha haya mashirika ya kijamii, tangu uunganisho huo umefanyika, shirika hili letu la sasa hivi halijajiandika tena pale wala halijapeleka kununua hisa wala kuuza hisa. Tunaomba shirika hili ambalo limejumuisha mashirika yote ya kijamii basi lijiandikishe ili liweze kufanya lile soko la hisa liweze kuwa very active, baada ya kusema hayo nakushukuru sana na naunga mkono mpango huu. Ahsante sana. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati Hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nashukuru sana kupata nafasi hii ya kuchangia hoja hizi za Wenyeviti wote wawili. Kabla sijaendelea, napenda kuungana na ndugu na Waheshimiwa Wabunge wote kumwombea ndugu yangu, rafiki yangu na jirani yangu ambaye alikuwa anakaa hapa ambaye ametangulia mbele ya haki. Tuzidi kumwombea ili roho yake iende peponi huko alikotangulia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Rais na Mawaziri na Maofisa wote ambao wameshughulika kwenye mapatano ya mkataba wa Barrick ambao naamini kabisa kwamba utatuongezea pato la Taifa katika siku za hivi karibuni. Mkataba huo ni mzuri na ni vizuri mikataba kama hiyo basi ikafanyika kwenye sekta nyingine na siyo madini tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, napenda kumpongeza Waziri na Maofisa wote kwa kuweza kugawa vizuri mapato na fedha ambazo wanazipata Wizaran, pamoja na kuwa hazitoshi, lakini wameweza kuzigawa katika mpango ambao ni mzuri na ambao unapaswa kupongezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, tumpongeze pia Kamishna Mkuu wa TRA ambaye anafanya kazi nzuri, anaendelea kuleta mapato mazuri na siyo siri kwamba mwezi uliopita tu wa Desemba, tumeweza kupata karibu shilingi trilioni 1.9 ambazo hatujawahi kupata katika nchi hii. Ni vizuri Kamishna Mkuu akaendelea na moto huo huo ili kila mwezi basi atupe mrejesho na kuonekana kwamba mapato yanaendelea kupatikana kwa uzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, pia napenda tumpongeza Gavana wa Benki Kuu ambaye ameweza ku-stabilize dollar. Mtakumbuka dola ilikuwa inaporomoka kwa kasi kubwa sana, lakini governor na maofisa wake wameweza kukaa vizuri na kui-stabilize mpaka sasa hivi iko kwenye kiwango ambacho kinaridhisha kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nampongeza sana TR, Msajili wa Hazina kwa namna ambavyo ameweza kusimamia mashirika haya na kuweza kutoa dividends ambazo hazijawahi kupatikana katika nchi hii. Ni sifa kubwa sana, nanyi mmeona mabilioni ya fedha ambazo mashirika haya yameweza kuyatoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati imeshauri mambo mbalimbali katika Wizara ya Fedha. Mambo mengi yamechukuliwa na mengine hayakuchukuliwa. Mengi yaliyochukuliwa matunda yake yameonekana, lakini yapo mengine ambayo hayakuchukuliwa na ningependa kushauri Wizara ya Fedha iweze kuyaangalia vizuri ili kuhakikisha kwamba basi wanayachukua kwa lengo la kukuza uchumi wetu na kuongeza pato la Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna miradi ambayo inabidi Serikali izidi kuifanyia kazi sana. Mradi wa Liganga na Mchuchuma, umekuwa ni kero. Siyo kero tu, Kamati tumejadili kwa kina na Mheshimiwa Waziri anajua kwamba viwanda vya chuma hapa nchini ambavyo viko 11 au
17 vyote vinachukua malighafi kutoka nje. Naamini kabisa mradi huu wa Liganga na Mchuchuma ungekuwa unafanya kazi, basi kusingekuwa na haja ya viwanda hivi kuagiza malighafi hizi kutoka nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni muhimu sana maamuzi ya mradi huu yafikie mwisho. Ni mradi mkubwa na utaona kwenye Mpango wa Maendeleo, Serikali ina mpango pia wa kujenga SGR ambayo itatoka bandarini Mtwara na kuweza kufika mpaka huko Liganga na Mchuchuma. Sasa ni vizuri Serikali ikaweka umuhimu na kuona kwamba mradi huu ni muhimu sana. Nimewahi kuona mradi wa makaa ya mawe kule Zimbabwe njia ya kwenda Victoria Falls, ni mradi mkubwa na unatoa ajira nyingi sana na uchumi wa nchi ya Zimbabwe unategemea sana mradi wa makaa ya mawe ambao uko kule Midlands.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nashauri Serikai iliangalie, tumelipigia kelele sana na tunaomba basi uamuzi ufikiwe. Isitoshe, kuna mradi kwa mfano wa kiwanda kile cha General Tyre Arusha, kila siku hapa Bungeni tumekuwa tukiongea suala hilo. Ni vizuri ikafikia mwisho, maana sioni kitu gani ambacho NDC wanafanya kwenye ule mradi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo, tumekuwa tukipendekeza na hata kwenye bajeti iliyopita kuhusu ujenzi wa bandari ya uvuvi. Najua colleagues wangu wameongea hapa asubuhi na tukaambiwa kwenye bajeti kwamba iliyopita kwamba Serikali ina mpango wa kuanza kujenga bandari ya uvuvi, sasa sijui ni ujenzi huo umefikia wapi? Ni vizuri tukapewa ufafanuzi kutoka kwa Waziri mhusika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati ilipata fursa ya kutembea kwenye baadhi ya nchi, tulikwenda Rwanda pamoja na Uganda ambapo kwenye hiyo study tour lengo lake ni kuangalia namna gani Treasury Single Account (TSA) inafanyakazi. Sisi tulikwenda Uganda na kwa kweli tuliona mpango huo unaendelea vizuri na unafanya kazi vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi hizo ambazo zinafanya, tulijiongeza na kwenda kutembea mjini na tuliona mambo ya ajabu ambapo tulikuta bidhaa nyingi sana ambazo zinapita hapa hapa kwetu, zinakwenda mpaka Kampala na Kampala kule unakuta Watanzania wengi na sio Watanzania tu, pamoja hata na wa nchi jirani wanakwenda Kampala kwa ajili ya kununua wengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wengi wa nchi jirani walikuwa wanakuja kwetu Kariakoo sasa hivi wamehamia kule Kampala. Sasa tuliongea na Mheshimiwa Waziri na tuliona kwamba ni muhimu tuangalie tumekosea wapi? Ni kitu gani ambacho tunatakiwa tukifanye? Kwa nini bidhaa zitoke hapa, zipite hapa, ziende Kampala na watu wetu wa hapa watoke hapa waende kununua kule wazirudishe hapa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hapa kwenye transit kuna ushuru ambao unatakiwa ufanyike na tumemshauri Mheshimiwa Waziri atengeneze Kamati ndogo iweze kukaa na kuona kwamba huu ushuru utafanya nini ili tuweze kuwa vizuri? Kwa hiyo, naamini kabisa Mheshimiwa Waziri atalichukua hilo na kuweza kuona kwamba tunafanya nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti,...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Adadi. Kengele ya pili imelia.

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naunga mkono hoja ya Mwenyekiti.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi ningependa kushukuru sana kupata nafasi hii kuweza kuchangia hoja hii ambayo ni muhimu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ningependa kumpongeza sana Waziri na Naibu wake pamoja na Katibu Mkuu na watendaji wote; kazi ambayo wanaifanya kwa kweli ni kubwa sana na inahitaji kupongezwa. Nakumbuka wiki iliyopita nilikuwa na Waziri kwenye kijiji change kimoja ambacho aliloa tope kabis akutokana na mvua, lakini aliweza kudiriki kuweza kuwasha umeme kwenye baadi ya vijiji. Nakushukuru sana, na namshukuru pia Naibu Waziri ambae ni mwenyeji sana Muheza na tumempa kadi pale kwa hiyo karibu sana na wametembelea sana Jimbo langu la Muheza.

Mheshimiwa Naibu Spika, REA awamu ya tatu Muheza tulibahatika kupata vijiji 19 lakini nasikitika kusema, na Naibu Waziri na Waziri wana habari kabisa kwamba mkandarasi ambaye yuko pale Radi ni mkandarasi ambaye ni mbovu sijawahi kuona. Kati ya vijiji 19 katika muda wa miezi 10 ameweza kuwasha umeme kwenye vijiji vitano tu. Kwakweli inasikitisha lakini Mheshimiwa Waziri nilikumbuka na nilikuambia kwamba tafadhali sana naomba vijiji vingine ambavyo vingekuja labda kwenye awamu ambayo itakuja Awamu ya Pili, REA III vijiji 28 basi uweze kuniwekea na uweze kunitafutia mkandarasi ambaye kwakweli ni mzuri. Nitakushukuru sana endapo utatimiza ahadi hiyo. Isipokuwa nakushukuru sana kw ajuhudi za kuweza kum-force huyu mkandarasi aweze kuweka umeme kwenye sehemu mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni vizuri kwenye Awamu ya III ya REA round ya pili hii mikataba ya hawa wakandarasi ikaangaliwa vizuri; na ni vizuri kama masuala ya transformer, masuala ya nguzo na nyaya basi ikanunuliwe moja kwa moja kwenye makampuni ambayo yanahusika badala yake kunakuwa na mikataba mingi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo ningependa kujikita sasa kwenye mradi wa kuchakata na kusindika gesi asilia (LNG), mradi huu ni mkubwa na muhimu sana, Mheshimiwa Waziri na Wizara yako ni vizuri sasahivi mkajielekeza kwenye gesi asilia kwenye huu mradi wa LNG. Serikali haijaipa uzito unaostahili mradi huu. Mradi huu ni muhimu sana, na mimi nakumbuka kabisa kwamba mradi huu unaweza ukainua uchumi wa nchi hii kwa nafasi kubwa sana. Makampuni ambayo yalikuwa kwenye huu mradi baadhi yao wameshaondoka na wamekwenda Msumbuji.

Mheshimiwa Waziri, Msumbiji, mradi huu wa LNG sasahivi Msumbiji wanauzindua mwezi ujao tarehe 18, iko kwenye press, na mradi utakuwa ni plant moja kubwa sana katika Afrika na Ulaya. Sasa hatuwezi kuacha hiyo nafasi tukaanza kucheza mradi huu. Nakuomba kabisa Mheshimiwa Waziri elekeza nguvu sasa kwenye huu mradi wa LNG tuweze kuinua huu uchumi kwa bidii sana…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Kengele imeshagonga Mheshimiwa. Ahsante sana.

MHE. BALOZI. ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kupata nafasi hii ya kuweza kuchangia hoja hii muhimu sana ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Kwanza, napenda kushukuru sana Serikali ya Awamu ya Tano na hasa Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa ambayo anaifanya hususani kwenye mambo ya miradi mikubwa ambayo inaendelea. Napenda pia kumsifu Mheshimwa Waziri Mkuu pamoja na Mawaziri na Naibu Mawaziri wote ambao wapo katika Ofisi yake, wanafanya kazi kubwa na tunashukuru sana.

Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza na kumshukuru Mheshimiwa Waziri kwa kufanya ziara yake Muheza, katika Mkoa wa Tanga. Naamini alipokuja ziara imeweza kufufua mambo mengi na wananchi wa Muheza hawawezi kumsahau hususan kwenye suala la maji ambapo aliongozana na Waheshimiwa Mawaziri na Naibu Waziri. Kwa kweli kuja kwake kulifanya tenki kubwa ambalo linajengwa pale Muheza la lita laki saba liweze kujaa maji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, najua Mheshimiwa Waziri Mkuu aliacha kiporo lakini yale maji kwenye lile tanki la lita laki saba bado yamejaa. Tunaamini kabisa kwamba atakaporudi basi ataweza kuyafungulia na wananchi wa Muheza waweze kupata maji. Nakushukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia napenda kukupongeza hasa katika kuingia kwenye digital, sasa hivi tunatembea na tablet. Hata hivyo, tulikuwa na mawazo kwamba basi Bunge lijalo watakaorudi waweze kuwa na screen katika table zao ingekuwa ni vizuri sana. Tunakushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, baada ya hayo, napenda kuchangia mambo yafuatayo. Pale kwa Waziri Mkuu kuna Kitengo cha Maafa lakini kwa kweli hakipewi umuhimu unaostahili. Kitengo kile naamini kabisa kina upungufu mkubwa wa fedha na ni vizuri kikaimarishwa kwa sababu mafuriko ambayo yametokea wakati huu wataalam wanasema hatujawahi kuyapata katika kipindi miaka 15 au 20 iliyopita. Kitengo kile kikiimarishwa naamini kitaweza kusaidia sana.

Mheshimiwa Spika, sisi tuliathirika kwa kiwango kikubwa sana kule Amani ambapo kwenye ziara ya Waziri Mkuu pia tulikuwa tumpeleke Amani lakini tulishindwa kumpeleka kutokana na barabara. Mafuriko yaliharibu sana barabara za kule na mpaka sasa hivi barabara za kule vijijini kuna sehemu kata huwezi kupita. Kwa hiyo, tunaomba kabisa kwamba Kitengo kile kiimarishwe na TARURA ambao wanashughulika na barabara za vijijini waweze kuongezewa fedha kwa sababu kazi wanayofanya TARURA ni nzuri, lakini uzuri wake hauonekani kwa sababu ya ufinyu wa bajeti ambayo inapatika.

Mheshimiwa Spika, napenda pia kushauri kwenye Kitengo cha Uwekezaji cha TIC. Utaona kwamba Kitengo kile kina Mkurugenzi Mkuu mzuri sana na kuna kitu kile wanakiita One Stop Center lakini Maafisa ambao wamewekwa pale hawana uwezo. Maafisa ambao wamewekwa pale kutokana na Wizara zao ili waweze kukifanya kile Kitengo kiwe the real One Stop Center hawa uwezo wa kutoa vibali, leseni, kuangalia ni vitu gani ambavyo mwekezaji anatakiwa kupewa bila kupata consultation tena kutoka Wizarani, sasa hiyo inakuwa siyo One Stop Center. Inatakiwa Maafisa ambao wanapelekwa pale wawe na uwezo wa kuamua, wawe na uwezo wa kutoa vibali na kufanya mambo yote yanayohusiana na mwekezaji. Anachotaka mwekezaji akifika TIC apate vibali vyote pale siyo aambiwe tena aende Labour au TRA, hapana, ule ni usumbufu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni vizuri tuangalie uwezekano wa kukiongezea nguvu. Waheshimiwa Mawaziri ambao wako kwenye Wizara zinazohusika wapeleke Senior Officers pale ambao wanaweza kutoa maamuzi, hapo ndiyo tunaweza kukifanya kiwe One Stop Center.

Mheshimiwa Spika, nilitoa mfano kwamba twende Mauritius, ni nchi ambayo One Stop Center yake wanaiita Mauritius Enterprise, ina lead. Pale mwekezaji akienda, at the time naondoka pale ilikuwa three days anakuwa amepata kila kitu sasa hivi naambiwa ni some hours.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Waziri mhusika kwanza namshauri sana aende Mauritius, aangalie One Stop Center yao iko vipi, Mauritius Enterprise, naamini atajifunza. Hapa tunasema kwamba mtu anapata vibali siku saba lakini mwekezaji anakuja hapa na siku saba hizo anakuwa hajakamilisha kupata vibali vyake. Sasa tutakapokamilisha mambo haya nafikiri yatasaidia sana.

Mheshimiwa Spika, kuna kitu kinaitwa roadmap ambacho amekiongelea Waziri kwenye Kamati na pia blueprint. Ni vizuri hiyo blueprint basi itoke maana imekuwa ni kama kizungumkuti, kila siku inasemwa iko tayari lakini haitoki. Kwa hiyo, ni vizuri mambo haya yaweze kurekebishwa.

Mheshimiwa Spika, kuna miradi mikubwa ambayo imekwama hasa ukiangalia Mradi wa Bomba la Mafuta, umeanza kwa nguvu sana sasa hivi naona mambo yamepoapoa sijui kwa nini. Vilevile LNG Project nayo ilianza kwa nguvu sana imepoapoa. Twende Mchuchuma na Liganga nayo ilianza kwa nguvu sana nayo imepoapoa. Hivi vitu unaambiwa kwamba bado majadiliano yanaendelea, ni vizuri hayo majadiliano yaendelee na yamalizike na kama pia kuna compensation ambazo watu wanatakiwa walipwe basi walipwe.

Mheshimiwa Spika, la mwisho ni Corona ambalo kwa kweli ni janga kuu Waheshimiwa Wabunge wameliongelea kwa hisia tofauti na kubwa sana. Ni vizuri basi Serikali ikatenga fungu maalum, kwa sababu tumeangalia kwenye Mpango halikuwepo, lakini ni vizuri ikaja hapa na mpango, tusingoje hali ikawa worse tutashindwa kuizuia. Ni afadhali sasa hivi Serikali ije na mpango ambao utaeleza, najua kuna Kamati ambayo imeundwa, lakini Kamati haijaja na taarifa yoyote ambayo inaelezea ni kitu gani hasa ambacho kinatakiwa, kama ni suala la financial basi zitengwe.

Mheshimiwa Spika, hata wewe kwenye Kamati ya Uongozi uliongelea hata Bunge lenyewe lichangia na Wabunge tuchangie lakini tukasema aah, aah. Hata hivyo, ni vizuri pia ukafikiria tena ili tuone kwamba na sisi mchango wetu kama Wabunge, siyo kama ulivyosema siku ngapi zile hata siku moja, siku mbili.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo nakushukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)
The Written Laws (Miscellaneous Amendment) Bill, 2016
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nashukuru sana kwa kupata nafasi hii ya kuchangia kwenye marekebisho ya sheria hizi ambazo zimewasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Kwanza nampongeza sana kwa sababu mabadiliko hayo ambayo ameyaleta, ni muhimu sana kwa wakati huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitajikita kwenye hii Mahakama ya Division ya Mafisadi, Mahakama hii sasa hivi ni muhimu sana jinsi ambavyo imeanzishwa na ni dhamira ya Awamu ya Tano kuanzisha Mahakama hii. Mahakama ya Division ya Mafisadi ambayo inategemewa kuanzishwa, ukiangalia mabadiliko ambayo yamefanyika, yametoa Mahakama ya uhujumu uchumi na kuweka Mahakama hii ya Division ya Mafisadi. Sasa provisions kifungu cha tatu ambacho kimerekebisha kifungu cha pili na kifungu cha tatu ambacho kimeweka makosa ambayo Mahakama hii ya Mafisadi itashughulikia, utaona pamekuwa na msururu wa makosa mengi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la kuanzishwa kwa Mahakama hii ni kuangalia zile kesi nzito, kesi kubwa kubwa ambazo zinatakiwa ziende kwenye hii Mahakama na siyo lengo la kuweka msururu wa kesi nyingi nyingi. Kwa hiyo, utaona kwamba, makosa ambayo yalikuwepo kwenye Sheria ya Uhujumu Uchumi (Economic and Organized Crime Act), mengi ni kama yamehamishwa sasa kwenye Mhakama hii ya Division ya Ufisadi. Ndiyo maana nasema pamekuwa na msururu mkubwa pamoja na kuwekewa kiwango cha bilioni moja kwamba kesi zote ambazo zitakuwa zinakwenda kule ziwe zimefikia bilioni moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, utakuta makosa mengine ambayo yanakwenda kwenye Mahakama hiyo, gharama ambazo zinapatikana ni gharama za mitaani (street value), kwa mfano makosa ya madawa ya kulevya, thamani yake inachukuliwa kama street value ya mitaani ndiyo ambayo inawekwa pale. Kwa hiyo, hakuna gharama halisi ambayo unaiweka pale ya kusema kwamba, kweli madawa haya au meno haya ya tembo, basi gharama yake ni bilioni moja. Wenzetu nchi za nje sasa hivi wameondoka kwenye suala la kufikiria gharama bali wanafikiria uzito, kwamba madawa haya ya kulevya uzito wake ni kilogram ngapi? Ni kontena ngapi au pembe hizi za ndovu ni kontena ngapi? Uzito wake ni kiasi gani na siyo kufuata gharama.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo hii gharama ambayo imewekwa hapa, ningemwomba Mwanasheria Mkuu ajaribu kuangalia kwamba tuzingatie sasa hivi uzito badala ya kuangalia gharama. Nasema hivyo kwa sababu, Kamati yangu tumekwenda katika Magereza mbalimbali na imegundua kwamba makosa ya madawa ya kulevya, watu ambao wako magerezani kule utakuta uzito wa kesi ambazo wanazo ni mdogo, kwa mfano, ambao wanaambiwa wamesafirisha madawa ya kulevya. Kusafirisha madawa ya kulevya mtu ambaye amemeza yale madawa, anashtakiwa kwa kosa la kusafirisha madawa ya kulevya whatever grams ambazo wanazo, lakini zimeshaingia tumboni, sasa anaambiwa kwamba, basi hili tumbo ni kontena wewe umesafirisha haya madawa, kwa hiyo, ni lazima ushtakiwe chini ya Sheria ya Uhujumu Uchumi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ukiangalia pia kwenye mabadiliko haya ambayo yameletwa hawa watu ambao wamekamatwa kamatwa wamemeza madawa au wamekutwa na gram ambazo zimekutwa kwenye viatu au kwenye mabegi, wote hawa pamoja na gram zao kuwa ndogo utakuta kwamba wanashtakiwa chini ya Sheria ya Uhujumu Uchumi. Sasa kitu ambacho kitatokea sasa, kwa sababu hawa ni wasafirishaji wameweka kwenye makontena, wameweka kwenye viatu, wameweka kwenye matumbo yao, wamekamatwa wanaambiwa wao ni wasafirishaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la Mahakama hii ni kupeleka wale watu ambao wana makontena. Sasa tukiipeleka jinsi ilivyo, patakuwa na msururu mkubwa kweli kwenye hiyo Mahakama na lengo lake ambalo liko pale utakuta kwamba halitafikiwa. Kwa hiyo utaangalia hapa kwenye presentation ambayo ametoa Attorney General, msururu wa makosa nauona ni mkubwa sana, ni makosa mengi sana, kiasi kwamba hii Mahakama sasa tutaichosha, badala yake itakuwa kazi ambazo inazifanya zitakuwa sio tulizokusudia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, hebu angalia kuna kosa hapa za kupatikana na silaha, yaani gobore ni silaha, sasa gobore mtu amekamatwa na gobore itabidi aende kwenye hiyo Mahakama ya Ufisadi. Sasa hiyo Mahakama itakuwa na maana gani kwa sababu hizi kesi zote ndogo ndogo zitakwenda. Kwa hiyo, nafikiri kwamba Serikali iangalie tena kwamba ni kesi gani na hasa zile nzito ndiyo zinatakiwa ziende kule. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili ninaloliona ni suala la zile kesi ambazo zimetoka kwenye Economic and Organized Crime Act ambazo zimeonekana ni ndogo ndogo, maana siyo zote ambazo zimehamishiwa hapa, haiku-specify hapa kwamba zile kesi zitapelekwa wapi au zitasikilizwa kwa utaratibu gani na Mahakama hii inatakiwa ianze kazi kwa kesi gani? Ni fresh cases ambazo zinakuja au nyinginezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kuanzishwa kwa Mahakama hii, ingekuwa ni vizuri kwamba, baada ya sheria hii kupita, wale wadau stakeholders wote wapate semina, wapate mafunzo maalum kuanzia Wapelelezi mpaka Majaji na Waendesha Mashtaka ili kuweza kuwa na uwiano mzuri wa usikilizaji wa kesi hii katika Mahakama hii ambayo tunategemea kwamba, iende kwa uharaka jinsi inavyotakiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, nategemea kwamba uanzishwaji wa Division hii basi utakuwa ni mzuri, utaratibu mzuri kama vile ilivyokuwa Division ya Biashara, Commercial Court au Division ya Kesi za Ardhi. Utaratibu ambao utakuwepo pawe na jengo lake kwa sababu utaratibu ambao ulikuwa unafanywa katika kesi za uhujumu uchumi kama alivyosema Mwanasheria Mkuu kwa kweli haukuwa utaratibu, ni Majaji wale wale tu kama kuna kesi ya wahujumu uchumi, basi jaji huyo huyo anahamia hapo hapo anaanza kusikiliza hizo kesi. Kwa hiyo, unakuta kwamba msongamano wa kesi unakuwa mkubwa. Kwa hiyo, hapa tunategemea kwamba Divisheni hii itakuwa na jengo lake maalum, Majaji wake maalum, wafanyakazi maalum kama ilivyo kwenye Commercial Court, pamoja na Ardhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo ningependa kuunga mkono hoja kwa marekebisho ambayo nimeyaeleza. Nakushukuru sana.
Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma ya Mwaka 2016
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nashukuru sana kupata nafasi hii kuchangia hoja hii ambayo imeletwa na Waziri wa Fedha. Kwanza, nampongeza kwa kuleta mabadiliko ya hoja hii ambayo ni muhimu sana. Suala la manunuzi ya umma Serikalini ni kitu cha msingi na muhimu sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, ununuzi wa umma ni kipimo cha namna Serikali inavyoendesha shughuli zake, inavyofuata sharia, uwazi na namna ambavyo inadhibiti vitendo vyovyote vya rushwa kwenye zabuni. Zabuni ni eneo ambalo linaleta rushwa sana. Zile rushwa kubwa kubwa zinazozungumzwa zinatoka kwenye zabuni kubwa, mikataba mikubwa, yote inatokea hapa kwenye hii kitu inaitwa zabuni na ndiyo maana asilimia 70 ya bajeti inakwenda huko kwenye suala la mchakato wa zabuni.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria yetu ya Public Procurement, Cap 410 ina historia ambayo imeanzia tangu 1990, tukaja kwenye ya 2011 pamoja na regulations zake lakini pamoja na sheria zote hizo utaona kwamba bado haijakidhi matakwa yale ambayo yanatakiwa ili sheria hii iweze kuwa nzuri na itekelezeke vizuri. Kwa hiyo, mabadiliko yanatokea na ndiyo maana sheria hii sasa hivi imeletwa hapa kufanyiwa mabadiliko.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sheria hii ambayo bado haijafanyiwa marekebisho imesaidia kwa kiwango kikubwa hasa kwenye udhibiti wa corruption. Imedhibiti rushwa kwa sababu imekuwa na Kamati nyingi sana pamoja na changamoto ya urasimu na muda lakini kwa njia moja au nyingine imesaidia kuweka transparency kwenye suala zima la mchakato wa hizo zabuni. Pia sheria hii ambayo tunataka kuibadilisha imesaidia sana kutoa opportunities za kutoa zabuni za kimataifa ambazo sasa hivi tunazifanyia mabadiliko.
Mheshimiwa Naibu Spika, hii sheria ambayo sasa hivi imeletwa hapa ina umuhimu sana kwa sababu imeingiza kitu ambacho kinaitwa value for money ambacho ni muhimu sana na kimewekwa mpaka kwenye hii preamble ambayo ipo kwenye haya mabadiliko. Ukiangalia kifungu cha 3 au cha 2 kimeweka hiyo preamble ambayo inaonyesha kwamba sasa sheria hii itaangalia value for money na sasa hivi ndiyo sheria nyingi za zabuni zinakwenda kwenye mwelekeo huo. Nilikuwa naangalia Sheria ya Manunuzi ya World Bank pamoja na EU zote hizo zimeingiza kitu kinaitwa value for money. Pia imejaribu kuondoa mlolongo mzima wa michakato hii na kupunguza hizi Kamati ambapo kila Kamati ikikaa inapewa hela, sasa mlolongo wote huo umeondoka.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna kitu kimoja kimewekwa ambacho wenzetu pia wamekiweka badala ya kulenga tu bidder yule ambaye ana bei ya chini inaangalia huyu mzabuni pamoja na kuwa na bei ya chini, je, vitu vyake vina ubora kiasi gani? Sasa hicho ni kitu muhimu, kuangalia ubora na siyo kuangalia tu thamani kwamba hii ni thamani ndogo basi huyu mpe kwa sababu thamani ndogo ameshinda hiyo tenda. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kitu cha msingi ambacho nimekitafuta kwenye marekebisho haya sikukiona ni suala la negotiations kwamba huyu ameshinda, je, kuna utaratibu gani umewekwa ambapo wanaacha mambo ya kwenda kwenye bei ndogo wanaingia kwenye majadiliano na wazabuni kuweza kuangalia ubora irrespective ya bei ambayo ameitenda? Kwa hiyo, ni kitu cha msingi naomba Mheshimiwa Waziri aeleze amekiweka wapi kwenye hizi provisions ambazo zipo.
Mheshimiwa Naibu Spika, na-support kabisa suala ambalo limewekwa kuanzia kifungu cha 55A, 55B, 55C na 55D ambapo inawakata makali wageni na kuwaruhusu wazawa kushiriki kwenye zabuni hizi. Suala hili limekuwa likiathiri sana zabuni nyingi kwa sababu utakuta wanapewa watu wa nje na wanaleta wataalamu wao na wengine hata hawana utaalam wanajaa kwenye hizo zabuni wanafanya kazi na watu wetu wanakosa kazi za kufanya. Hii itasaidia sana kwa sababu watu wetu watapata nafasi ya kufanya kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni suala la ushindani wa zabuni, kwenye zabuni lazima pawepo na ushindani lakini pawepo pia na zabuni ambazo hazina ushindani (single source) lakini hizi single source pia ni lazima zirekebishwe ziendane na wakati. Nimeangalia kwenye kifungu cha 65A na 65C na nimeona ushindani huu wa single source ameachiwa Waziri kutengeneza hizo regulations. Hapa ni lazima tuwe waangalifu sana vinginevyo tunaweza tukarudi kwenye suala lile lile ambalo liko chini. Single source ni muhimu na lazima tui-encourage kwa sababu kuna mifano mingi ambapo zabuni unaweza ukanunua moja kwa moja kutoka kiwandani na ikaanza kufanya kazi. Kwa hiyo, ningeshukuru kama suala hili litapewa umuhimu wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna suala la zabuni maalum wakati wa athari au panapotokea chochote kile ambacho ni cha dharura hapo tena huwezi ukasema kwamba unaanza mambo ya tenda itachukua mlolongo mrefu. Ni lazima sheria iruhusu vitu vya wakati huo kwamba sasa hivi vitu vya dharura viruhusiwe mtu aweze kwenda moja kwa moja kwenye single source na kuanza kufanya manunuzi. Hiyo special provision lazima iwepo na ionekane.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala kubwa ambalo linatakiwa kwenye zabuni ni uaminifu na uadilifu na namna watumishi wa Serikali watakavyofanya kazi hiyo. Naunga mkono hoja hii kwa sababu imejaribu kutaja mambo mengi ambayo ni muhimu. Cha msingi hasa ambacho sijakiona na napenda Waziri atuthibitishie, wakati wazabuni wanaingia kwenye majadiliano, suala la kui-inflate rate ni kitu cha muhimu sana. Watumishi wengi wa Serikali wanaongeza bei pale kwenye zabuni na ile kuongeza bei inawapa tabu sana hata wapelelezi namna ya kuchunguza na kujua hii kitu bei yake ni shilingi ngapi. Kwa hiyo, ni vizuri wakati wa zabuni tuwe na assessment ya kujua kwamba chombo hiki ambacho tunataka kiingie kwenye zabuni au gharama ya kutengeneza hii barabara inaweza kuwa shilingi ngapi? Atleast tukiwa na maximum evaluation itasaidia kuondoa hii thinking ya kuongeza bei jinsi anavyotaka mtu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana na naunga mkono hoja hii na nashukuru kwa kupata nafasi hii.
Muswada wa Sheria ya Usimamizi wa Wanataaluma wa Kemia wa Mwaka 2016
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nashukuru sana kupata nafasi hii kuweza kuchangia Miswada hii miwili ambayo ni muhimu sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, Miswada hii muhimu kwa sababu ni Miswada ya kitaalam na watendaji wake wengi ni wataalam wa fani mbalimbali. Mkemia Mkuu wa Serikali amekuwa akifanya kazi nyingi sana za kitaalam. Nimebahatika kufanya kazi na Mkemia Mkuu wa Serikali kwa miaka mingi, kwa kweli wanafanya kazi nyingi sana za upelelezi na Idara ya Upelelezi inamtegemea sana Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kutoa taarifa mbalimbali za kitaalam za matukio mbalimbali ya makosa ya jinai.
Mheshimiwa Naibu Spika, Idara ya Upelelezi kwa muda mrefu imekuwa ikishirikiana na Mkemia Mkuu na inaendelea kushirikiana nayo kwa ajili ya kupata taarifa mbalimbali ili kukamilisha upelelezi wa makosa mbalimbali ya kemikali. Idara ya Upelelezi inayo Forensic Unit ambayo ina-cover mambo ya kitaalam kwa mfano utaalam wa maandishi, ballistic, finger prints, cyber crime na utaalam mbalimbali lakini hivi karibuni idara hiyo pia imeanzisha utaalam mwingine zaidi wa mambo ya kemikali, toxicology na mambo mengine mengi ya bombing na drugs. Ili kupunguza workload ya Mkemia Mkuu wa Serikali anapaswa kusaidia kwa kiwango kikubwa kabisa maabara nyingine ambazo zitakuwa zinafanya kazi za kimaabara hapa nchini ikiwepo na maabara iliyo chini ya Idara ya Upelelezi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumepata mafunzo kwa matukio makubwa ambayo yamewahi kutokea hapo nyuma na hata ukichukulia tukio hili la sasa hivi lilitokea huko Kagera la tetemeko la ardhi. Mwaka 1998 Ubalozi wa Marekani ulilipuliwa hapa nchini na ulipolipuliwa Watanzania walikufa pale na viungo vyao vilitawanyika kwa sababu lile bomu liliwatawanya kwa hiyo utaalam wa DNA ulihitajika lakini tulikuwa hatuna huo utaalam. Tulikuwa hatuna utaalam wa bombing kujua kwamba bomu ambalo lilipiga Ubalozi wa Marekani lilikuwa kubwa kiasi gani, lilikuwa na uzito kiasi gani hivyo hivyo tukio hili la tetemeko la ardhi ambalo limetokea huko Kagera hatujui ukubwa wake ni kiasi gani. Labda kwa mfano tetemeko hili la ardhi lingekuwa limetawanyisha viungo ingebidi sasa hivi navyozungumza wataalam wa DNA wanatakiwa wawe kule Bukoba.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kupata lile tukio kwa mfano la 1998 ilikuwa ni fundisho kubwa sana kwa Idara ya Upelelezi hapa nchini ambapo tulikuwa ni weupe kabisa kwenye mambo ya kitaalam ya DNA na hata ilikuwa ni fundisho kwa Mkemia Mkuu wa Serikali.
Nashukuru sana baada ya pale Idara ya Upelelezi ya FBI ilitushauri na ikasisitiza kwamba Forensic Units za Polisi ambazo ziko duniani ni lazima ziwe zina-cover maeneo yote haya ambayo ni muhimu ya toxicology, DNA na kadhalika ndiyo inakuwa imekamilika kwa sababu itasaidia wataalam kwenda kwenye matukio haraka na wataweza kusaidia kurahisisha kazi za Mkemia Mkuu. Namna ya kuchukua vielelezo pale, namna ya kuchukua sampuli mbalimbali yote hiyo ni utaalam ambao unatakiwa na ni utaalam ambao unatakiwa usaidiwe sana na Mkemia Mkuu wa Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, sheria hii imekuja wakati muafaka na nashauri kabisa Waziri atakapokuja ku-wind up aonyeshe nia kweli kwamba Mkemia Mkuu wa Serikali yuko tayari kusaidia maabara nyingine ambazo ni muhimu kabisa ili kuweza kurahisishia kazi. Sasa hivi kuna kesi nyingi sana za mauaji, za drugs, kama Kamati tumetembelea kwenye magereza mbalimbali na kule ambapo zimekwama unakuta labda wanasubiri taarifa ya Mkemia kuhusu mauaji au drugs hizo. Kwa hiyo, sheria hii inatakiwa itoe nguvu kwa maabara hizi nyingine ili ziweze kusaidia kazi hizi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeangalia kwenye vifungu mbalimbali ambavyo viko katika Sheria hii ya Mkemia Mkuu wa Serikali na nimeona kwamba mambo mengi yameguswa lakini kuna mambo mengine ambayo yanatakiwa kuguswa kwa mfano hilo la kuhakikisha kwamba Mkemia Mkuu ana-support maabara nyingine, ni muhimu liwe wazi na liwe na kifungu chake maalum cha kuhakikisha kwamba Mkemia Mkuu anasaidia maabara nyingine hapa nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini napata pia wasiwasi kwenye kifungu cha 4 ambacho kinatoa supremacy na referral. Sijapata lugha sahihi ya kuweka katika kifungu hiki, lakini labda Mheshimiwa Waziri angetusaidia, Mkemia Mkuu yeye ni operational, regulator sasa itakuwaje tena awe supremacy na at the same time yeye ndiyo apelekewe rufaa? Ningeshauri labda kifungu hiki kingehamishwa aidha kipelekwe kwenye Bodi ile iweze ku-oversee maabara zote nchini ikiwepo na hii ya Mkemia Mkuu kama kuna tatizo lolote ambalo linatokea. Kwa hiyo, natashukuru kama suala hilo lingeangaliwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kifungu cha 5 pia nina wasiwasi nacho ambacho kinakwenda sambamba na kifungu cha 4 pale kinaposema kwamba results shall be final and conclusive. Hii final na conclusive inanipa wasiwasi kidogo kwa sababu ripoti ambazo zinatolewa na Mkemia Mkuu ni za utaalam chini ya Sheria ya Ushahidi pia ambapo ripoti hiyo inaweza kutolewa na utaalam mwingine.
Kwa hiyo, ni lazima kuangalia badala ya kuweka final and conclusive inaweza ikasema labda taarifa ambazo zinatolewa ni unreliable. Kwa hiyo, labda Waziri angekiangalia kifungu hicho na kukirekebisha ili ku-come up na good provision.
Mheshimiwa Naibu Spika, kifungu kingine…
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.
Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari za Mwaka 2016
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi napenda kuungana na wenzangu kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri Nape na Mheshimiwa Naibu Waziri pamoja na Mwenyekiti wa Kamati kwa kazi nzuri ambayo wameifanya kuweza kuchambua muswada huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, muswada huu ni muhimu sana. Taswira ya habari hapa nchini ni kitu ambacho humu ndani hakuna hata mmoja wetu ambaye anaweza kusema kwamba waandishi wa habari au taswira ya habari ni mbovu. Waandishi wa habari kwenye nchi hii wamefanya kazi nyingi sana; wanafanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ndiyo maana kila siku asubuhi unaangalia kwenye television kutaka kujua kuna habari gani? Kuna kitu gani leo? Kila mtu kila saa ana-google au ana-whatsapp kila leo, lakini yote hayo ni mahusiano ya habari. Hizi habari zinatafutwa. Hawa waandishi wa habari hawaokoti hizi habari, wanazitafuta kwa bidii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashangaa kabisa, nimesoma huu muswada, ni mzuri sana. Kama ni marekebisho yanahitajika kufanyika, ni kidogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 58 kinawatambua na kuwathamini waandishi wa habari. Kimewapa bima, kimewafanya wawe na mifuko. Hawa waandishi wa habari imefika hatua wanaitwa mapaparazi, wengine hawana mishahara, wengi tu. Wanafanywa kama vibarua, wanalipwa kwa story, kwa mistari. Ukiangalia kwenye vyombo vyote vya habari, karibu nusu ya hao waandishi wa habari hawalipwi na hawana barua za ajira; lakini wanavumilia na hawataki kutoa hizo taarifa kwa sababu wanajua wakitoa tu watafukuzwa kazi na watakuwa hawana cha kusema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka kusema kwamba wamiliki wa vyombo vya habari na watu wengine wawe waangalifu, wasikazanie kusema kwamba muswada ni mbaya ili hawa waandishi wa habari wanaopata taabu kila siku wasipate haki zao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, uhuru wa habari hapa nchini, mimi nimeangalia kwenye google, Tanzania ni nchi mojawapo ambayo ina uhuru mkubwa sana wa vyombo vya habari. Nimetembea, nimeona nchi mbalimbali, sijawahi kuona nchi ina magazeti kama hapa nchini, lundo la magazeti. Hapa huwezi ukasema unaweza ukanunua magazeti yote ambayo yanatoka kwa siku, ndiyo maana magazeti yote yanafanya kubandikwa, mtu unaangalia hii heading ngoja ninunue hili na hili. Uhuru ni mkubwa, vyombo vya televisheni viko vingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninachosema ni kwamba uhuru wa vyombo vya habari ni mkubwa hapa nchini na ambao inabidi uangaliwe na hawa watu wanaotupa habari tuwaangalie maslahi yao jamani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ngoja niende kwenye sheria, kwenye muswada wenyewe unavyosema. Mwandishi wa habari ni nani? Pale imesema, a journalist is the one who has been accredited, lakini inategemea kwamba Mheshimiwa Waziri atakwenda further na kufafanua kwamba huu ni muswada wa waandishi wa habari, kwa hiyo, ni lazima afafanuliwe nani ni mwandishi wa habari?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona kwenye media inasema ina-include na social media. Kulikuwa na utata hapa kwamba labda blogs au social media basi siyo media. Nilikwenda nikaangalia baadhi ya kesi kwenye commonwealth; Mahakama Kuu ya Australia, New Zealand kulikuwa na huo utata kwamba social media labda siyo media na imetolewa uamuzi kwamba blogs zote ni social media. Ipo na nenda mwangalie kwenye Mahakama Kuu za Australia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninachosema ni kwamba, kwenye accreditation ni lazima Waziri aseme vigezo gani ambavyo atavitumia kuweza kumfanya huyu mtu aweze kuitwa Mwandishi wa Habari. Hatuna maana kusema basi wale ambao hawatakuwa accredited, basi hawatafanya kazi za uandishi wa habari. Ni lazima Waziri atambue kwenye kanuni atakapozitengeneza, ahakikishe kwamba anawatambua mpaka ma-repoter, ma-photographer, waandishi, ma-digital waandishi, waandishi wanaoandika makala mbalimbali ni lazima wote wa-appear kwenye kanuni. Hii tunataka kuifanya profession ya uandishi wa habari iwe kama profession nyingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo wanasheria wote ni mawakili. Tunao wanasheria wengi lakini pia tunao mawakili. Kwa hiyo, tunataka waandishi ambao wako accredited ili waweze kutambua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nitakwenda kifungu cha 20(3) kimeshakuwa amended ambacho kinasema kwamba journalist yeyote ambaye amekuwa suspended basi asifanye hizo kazi. Kilikuwa ni kifungu kibaya sana, lakini nakushukuru kwa kufanya hiyo amendment na kuhakikisha kwamba basi atasimamishwa kwa miezi mitatu na aendelee na kazi zake. Kilikuwa ni kifungu kibaya ambacho kingeendelea kuleta taswira mbaya sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 18 ambacho kinatambua waandishi wageni, hiki ni muhimu sana. Nimekiona na kimeleta madhara makubwa sana. Waandishi wa habari wageni ni lazima wadhibitiwe. Kama wanapewa vibali ni lazima wahakikishe kwamba wanakwenda kwenye hiyo specific area ambayo wameambiwa waka-cover hiyo habari. Hatuwezi kukubali nchi hii waruhusiwe tu waandishi ambao ni foreigners waingie nchini kiholela holela, hatuwezi kukubali. Kwa hiyo, nakipongeza sana kifungu hicho na kuhakikisha kwamba ni lazima tukidhibiti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria hii imetambua mambo mengi. Sheria hii imetambua pamoja na kujua mwandishi wa habari ni nani, lakini imekwenda further na kutengeneza hiyo Bodi ya Ithibati, Mfuko wa Waandishi wa Habari, imetengeneza Baraza la kudhibiti ethics za waandishi wa habari na pia imempa Waziri madaraka ya kuthibiti mambo mbalimbali. Jamani hatuwezi kutengeneza sheria bila kumpa madaraka Waziri ya kuangalia mambo muhimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo mengi sana kwenye mambo ya uhandishi wa habari, ni lazima pawepo na msimamiaji. Yuko pale kwa nia njema tu. Waziri atatengeneza kanuni ambazo zitakwenda sambamba na uandishi wa habari. Yeye ni binadamu, hataki kuua hii kitu ya uandishi wa habari, anataka kuendeleza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeangalia makosa katika sheria hii, hasa makosa ya uchochezi. Makosa mengi yametolewa kwenye Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976; seditious offences. Makosa ambayo yameorodheshwa kwenye sheria hiyo ambayo Sheria ya Magazeti, imeifuta, yale makosa ya kwenye Kifungu kuanzia cha 50, kwenye sheria ile yalikuwa ni lazima yapate kibali cha Mkurugenzi wa Mashitaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria hii imeondoa kibali cha Mkurugenzi wa Mashtaka na kuwapa madaraka polisi wote wakamate hayo makosa na kuyafikisha mahakamani. Mheshimiwa Waziri ni muhimu madaraka ya Mkurugenzi wa Mashtaka dhidi ya seditious offences madaraka hayo yarudishwe. Itasaidia sana kuweza kudhibiti makosa hayo ambayo yataonekana yanatokana na uchochezi hapa nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, napenda kumpongeza tena Mheshimiwa Waziri na timu yake kwa kazi nzuri ambayo wameifanya, lakini nitashukuru wakifanya marekebisho hayo ambayo nimeyasema ili tuweze kwenda sambamba na sheria hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haki za waandishi wa habari lazima zitambuliwe, waajiri lazima wawekewe vifungu pale tuwathibiti waweze kuwalipa vizuri waandishi wa habari. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga hoja mkono.
Muswada wa Sheria ya Huduma ya Msaada wa Kisheria wa Mwaka 2016
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kupata nafasi hii kuchangia Muswada huu ambao ni muhimu sana. Kwanza natoa pongezi kwa Chama changu kwa kuweza kupiga magoli mengi kule magoli 19 kwa 1 na pia nawapongeza Wabunge wote hasa ndugu yangu Juma ambae ameweza kushinda kwa kishindo kule Unguja-Dimani. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Muswada huu kwa kweli ni muhimu sana na Muswada huu kama walivyosema wenzangu kwa kweli umechelewa sana. Ni Muswada ambao unalenga watu ambao hawana uwezo wa kupata huduma za kisheria. Ni Muswada ambao utaweza kusaidia watu wengi sana masikini, walemavu na kila watu na wafungwa ambao hata wako kule Magerezani ambao wanashindwa hata kuandika nanihii za kukata rufaa ambao wamejaa na ambao huwezi kusema kwamba kweli wote wamefungwa kwa makosa hayo lakini wana-right ya kukata rufaa lakini wanashindwa kutumia rufaa hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwamba Muswada huu umepanua wigo na umepanua wigo wa kuleta watu wengi kuweza kudai madai yao kwa kufuata sheria hii na nasema umepanua wigo kwa sababu ukifuata sura, Muswada ambao ulikuwa unatoa mamlaka kama haya kwenye sura ya 21 ambayo ni sheria ambayo ni The Legal Aid ambayo ilikuwa inatoa kwa ajili ya sheria ya makosa ya jinai pekee sasa hivi Muswada huu umepanua wigo na unatoa siyo makosa ya jinai ya mauaji tu au wale ambao wamehukumiwa kifungo bali unakwenda mpaka kutoa kwenye kesi za madai. Pia Muswada huu siyo kwamba utatoa huduma Mahakama Kuu tu, lakini Muswada huu unakwenda mpaka kwenye Mahakama za Wilaya, kwa hiyo ni Muswada ambao unatakiwa kupongezwa na ambao ni lazima tuangalie namna ya kuupitisha. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na mambo yote hayo, lakini nimepata wasiwasi wa mambo kama matatu hivi ndani ya Muswada huu. Ukiuangalia Muswada huu utaona kwamba mara utakapoanza kutumika wananchi wengi sana watakuja kudai huduma hiyo. Wananchi wengi watataka huduma za Mawakili, watataka huduma za hizo Taasisi ambazo zimeandikishwa kwa ajili ya kutetea haki zao. Sasa najaribu kuangalia wigo wa kesi ambazo ziko katika Mahakama zetu, wigo wa kesi chukulia kesi ambazo ziko Mahakama ya Wilaya tu au chukulia kesi ambazo ziko Mahakama kuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa watu wengi ambao wako pale watataka hiyo huduma ya Wakili ambao atakuja kunanii sasa utaona kwamba kuanzia kifungu cha 21 mpaka 36 nimejaribu kukiangalia lakini sijaona sehemu ambayo Muswada huu umeelekeza ni makosa ya aina gani ambayo yatataka kupata msaada huu. Sasa ukiacha hiyo vinginevyo itakuwa ni chaos kwa sababu kila mtu atataka kupata msaada huo na makosa ambayo yanatakiwa yapatikane msaada huo hayakuainishwa kwenye sehemu yoyote ile. Kama ni lengo la Serikali kwamba makosa ambayo yataainishwa yawe yanatakiwa kupata msaada yatatengenezwa kwenye kanuni, sijaona pia Mamlaka (provision) yoyote ambayo imeipa bodi, kuishauri kutengeneza hizo kanuni ili kuainisha ni makosa gani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ningependa kuishauri kwamba ni lazima basi pawepo na provision ambayo itaipa Mamlaka Bodi ya kuhakikisha kwamba inachambua ni makosa gani ambayo yanahitajika kutolewa msaada huu vinginevyo itakuwa ni chaos na itakuwa ni watu wengi ambao watahitaji huo msaada.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, kwa sababu niliangalia sheria mbalimbali na nikakuta sheria ya Afrika Kusini ambayo imetoa uwezo kama huo kwamba imetoa uwezo kwa bodi na bodi ile wametengeneza regulations, wame-identify makosa gani ambayo yanatakiwa yapewe msaada na ndiyo ambayo yanafuatwa, kwa hiyo na hapa ningeshauri pia na sisi tungeiga hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika la tatu, ambalo naliona, ukiangalia sheria ya 21 ambayo imefutwa, sheria ile imetoa madaraka kwa Mawakili ili Msajili wa Mahakama Kuu ndiyo ambaye anaweza kuchagua ofisi yoyote ya Uwakili kumwakilisha yule ambaye ameomba kuomba huduma hiyo ya msaada ambao anautaka. Kwa hiyo, ofisi yoyote ya Wakili ambayo imeandikishwa basi ilikuwa ina utaratibu kwamba hata kama ni Wakili wako mikoani walikuwa wanaamriwa kwenda kutetea hizo kesi za mauaji au zile ambazo zina adhabu ya vifo sasa ilikuwa centralized, registrar alikuwa na madaraka hayo, lakini ukiangalia kwenye hii sheria inasema kwamba mtu ambaye anahitaji kutoa huduma za kusaidia basi inabidi aombe kwenye bodi. Kwa hiyo, ina maana kwamba Taasisi zote ambazo zinataka kutoa huduma, ofisi za Mawakili ambazo zinataka kutoa huduma hii inabidi ziombe kule kwenye bodi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tatizo ambalo naliona ni kama ofisi hizi zisipotaka kuomba itakuwaje kwa sababu sasa hivi sheria ambayo ipo ya sura ya 21 Mawakili hawaombi, wanaamriwa kwa sababu ni Maafisa wa Mahakama wanaamriwa kwenda na bado hapo hapo wanakwenda kwa kinyongo kwa sababu fedha ambazo wanalipwa ni kidogo sana kwa kila kesi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ukiangalia sura hii utakuta kwamba Wakili sasa hivi analipwa kwa kesi elfu 40, elfu 60 sasa utakuta kwamba ni hela ndogo sana na hakuna motivation ya kuwafanya Mawakili au ofisi hizo ziombe. Sasa kitu gani ambacho sheria hii imekifanya ambacho kitawafanya Mawakili waweze kuomba au Taasisi zinaweza kuwafanya kwamba wakimbilie kuomba ili kutoa huduma kwa hawa ambao watatakiwa kupewa hiyo huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni suala ambalo linatakiwa liangaliwe kwa sababu hawezi wakili akapoteza muda wake wote pale hajui atalipwa nini ndiyo anayekwenda kutoa msaada lakini analipwa nini? Kwa hiyo sheria hii haikugusa chochote. Naomba kwamba Waziri aliangalie hilo na atakapokuja ku-sum up aweke kipengele hicho vinginevyo nitaleta mapendekezo ya marekebisho. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la nne, ni suala ambalo sasa hivi hii itakuwa ni ofisi kubwa sana, itakuwa ni institution kubwa sana. Haitakuwa kwenye kiwango cha bodi kama hivi ambavyo sheria inasema, haitakuwa kwamba ni mwakilishi mmoja tu kama ni Paralegal ambao wako kule wilayani basi hao hao ambao watafanya kazi. Sasa hiki ni kitu ambacho kinatakiwa pawe na independent board, institutions ambayo itashughulika kabisa na suala hili la kutoa hizi huduma. Hapa amezungumza Msemaji wa Kambi ya Upinzani ambayo ni mifano ambayo iko kwenye nchi nyingine. Nchi nyingine South Africa wana-independent board, institutions kabisa ambayo inatoa hii misaada kwa watu wote ambao wanahitaji huduma za kisheria. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hatuwezi kusema kwamba tunaweka ki-board tu au Wakala tu, ni lazima pawe na ofisi special office ambayo itatoa hizi huduma vinginevyo tutakuwa tunafanya masihara masihara tu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, nashukuru na naunga mkono mapendekezo ambayo yametolewa na Mwenyekiti wa Kamati kwamba ufafanuzi wa baadhi ya mambo ya Mwanasheria ni nani? Paralegal ni nani? Sheria hii ita-cover Mahakama zipi? Lazima ufafanuzi huo utolewe kwa sababu imeacha wazi, mtu anaweza kusema nataka kwenda hata Primary Court, jinsi mapendekezo haya yalivyo ina maana ana-cover mpaka Primary Court, kwa hiyo ni lazima ufafanuzi huu utolewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja baada ya marekebisho hayo. Nakushukuru sana.
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2017.
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nashukuru sana kupata dakika kidogo za kuweza kuchangia Muswada huu ambao ni muhimu sana. Kwanza ningependa sana kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa uamuzi wake wa kuleta Miswada hii ya jana na leo hapa Bungeni. Ni Miswada muhimu sana na kwa kweli ni uamuzi mgumu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Hati ya Dharura ilibidi suala hilo liweze kuletwa hapa Bungeni, imeletwa kwa Hati ya Dharura kutokana na mambo ambayo yalikuwa yanafanyika hapo nyuma, mambo ya wizi, mambo ambayo hatuna faida nayo dhidi ya madini yetu ambayo tumeanza kuyachimba kwa muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jana tulipitisha Miswada miwili ambayo ni ya muhimu sana, Miswada ambayo imeweka rasilimali za nchi hii katika mikono ya wananchi, Miswada ambayo imetoa uwezo wa kuangalia mikataba yote ambayo imeingiwa hapo nyuma na ile ambayo itafanyika hapo mbele kuweza kuiangalia. Miswada ambayo pia imeipa Bunge uwezo wa kupitia Miswada hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo tuna Muswada ni wa muhimu sana, Muswada wa Marekebisho Mbalimbali ya Sheria za Madini na Gesi hapa nchini. Muswada huu ni muhimu nami nimeuwekwa kwenye categories mbili, kwanza ni Muswada ambao ukiangalia kifungu ambacho kimetoa hisa ambacho ni muhimu sana katika Muswada huu. Kifungu hiki ni kifungu ambacho kitatupa faida pia ni kifungu ambacho kinaweza kikaangalia maslahi yote ya madini ambayo tunayo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia kifungu hicho ambacho kiko kwenye Kifungu cha 10, ni kwamba Serikali uitakuwa na asilimia kuanzia 16 mpaka 50 na Wawekezaji watachukua hiyo 50. Sasa nataka Mheshimiwa Waziri atakapokuja ku-wind up atoe ufafanuzi makini kabisa kwenye kifungu hiki. Kwanza kwa sababu kuondoa zile hisia za kusema kwamba wawekezaji wanatakiwa asilimia 30 kuweka kwenye soko la hisa na baadaye mwekezaji atabakiwa na asilimia 20. Sasa hii notion ni lazima ui-clarify ili kuonesha kwamba wawekezaji wasiwe na wasiwasi wowote, ni suala la marekebisho ambayo na wao wenyewe watakuwa na faida. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pili nataka akija kuhitimisha Mheshimiwa Waziri atoe ufafanuzi kwamba suala la udhibiti mapato, kwa sababu tumeona kwamba wawekezaji wamekuwa wakileta ripoti zote ambazo ni loss, loss! Tunataka kuona kwamba vifungu gani ambavyo nimeangalia kwa haraka haraka lakini nimeona madaraka hayo yako kwenye Commission. Sasa ni vifungu gani ambavyo vinawabana hawa Commission kuhakikisha kwamba kweli na sisi tumeweka udhibiti kwenye kuangalia hizi hisa ambazo tunazipata, alternatively ni kuhakikisha kwamba kwenye suala la utawala wa wawekezaji hao basi na sisi tunakuwa na mtu wetu kwenye finance department ambae ataangalia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tatu ni suala ambalo limezungumzwa na Mheshimiwa Masele hapa na ni suala ambalo tumelizungumza kwenye Kamati. Ni lazima suala hili lianzie kwenye leseni, kwa hiyo nategemea kwenye marekebisho ambayo utayaleta kwamba wachimbaji au waombaji wawekezaji ni lazima tuanzie kwenye leseni.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ni Kifungu cha 21. Kifungu cha 21 ambacho kinaunda Tume hii ya Madini, kwa kweli nimefurahi sana kwa sababu kime-take into consideration watu wote ambao wanahusika na mambo haya. Pia hata wachimbaji wadogo wadogo wako included naamini kwenye marekebisho ambayo hatujayaona atayaweka. Nataka kuona kwamba ni kwa nini Katibu Mkuu wa Madini na Nishati hakuwekwa kwenye hii. Nategemea nipate ufafanuzi ambao ni muhimu sana kwa sababu naamini Katibu Mkuu wa Nishati na Madini ni muhimu awepo kwenye Tume hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni Kifungu cha 100B suala hili ni zuri sana kwa sababu naamini kwenye mapendekezo au marekebisho ya Mheshimiwa Waziri ataingiza kusimamia kuanzia mining, sorting na hata kuendelea mpaka kwenye uuzaji na kuthamini. Kwa hiyo, kuwepo kwa Maafisa wetu kwenye ushiriki huo ni muhimu sana kwenye hicho kifungu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kifungu cha 102 pia nashukuru kwamba makampuni ambayo …

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)
Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya wa Mwaka 2017
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi nashukuru sana kunipa nafasi hii ili niweze kuchangia Muswada huu ambao ni muhimu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nampongeza sana Kamishna Jenerali Siang’a kwa sababu tangu ameteuliwa kwa muda mfupi sana ameonesha kweli ana nia ya kupambana na barons wa dawa za kulevya. Pili nashukuru kwa Muswada huu kuja ili kuangalia na kujaza yale mapengo ambayo yanaonekana kwamba yanaweza kuathiri hizi kesi za dawa za kulevya mahakamani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vifungu ambavyo vimeongezwa, moja ya kifungu ambacho kimeongezwa kwa kweli ambacho kilikuwa ni tabu sana; hizi kesi ndogo ambazo zilikuwa zinajaza msongamano wa mahabusu kule magerezani sasa hivi utaona kwamba at least vimewekewa viwango na zile kesi ndogo ambazo zilikuwa ninangojea mahakama Kuu kuweza kusikilizwa basi zinasikilizwa na Mahakama za Hakimu Mkazi au Mahakama za Wilaya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hiki ni kitu cha kupongeza sana kwa sababu kamati yangu ilipokwenda kutembelea kwenye magereza, kesi nyingi ambazo zilikuwa zinasubiri kusikilizwa zilikuwa ni kesi za mauaji na za dawa za kulevya. Kwa hiyo, muswada huu umekuja kwa wakati ambao ni mzuri sana na ninaamini kabisa kwamba utapunguza msongamano ambao umejaa kule magereza wakisubiri High Court Sessions ili kesi hizo ziweze kusikilizwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niende kwenye vifungu. Kifungu cha 15 ambacho ni para eight, kifungu hiki kimeanisha makosa ambayo watuhumiwa wakionekana na hatia basi watakwenda magerezani maisha.

Sasa kifungu cha 15(1)(iii) ambacho kimetaja makosa ambayo watakwenda magerezani, utaona pale kwenye kifungu hicho ukianzia mwanzo kwamba narcotic drugs, pyschotropic substances ambazo zinazidi kiwango cha gramu 200 basi huyo mtu atakwenda kufungwa maisha. Pia kuna precursor chemicals or substances ambazo zitazidi lita 100 na yenyewe atakwenda kufungwa maisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, wasiwasi wangu unakuja pale cannabis na khats ambacho wanasema kwamba ukikutwa na cannabis (mirungi) au bangi zaidi ya kilo 50 ni trafficking lakini unakwenda kufungwa maisha. Sasa imenipa wasiwasi kwamba huku tumeondoa kesi zile ndogo na inanipa wasiwasi kwamba tunapoingiza kifungu hiki maana kilo 50 za mirungi na bangi trafficking ni kiwango kidogo sana ambacho watu wengi sana watakamatwa na tutarudia makosa yale ya kupeleka watu gerezani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nilitaka wahusika waangalie kifungu hicho kwa makini kwa sababu kitarudisha tena msongamano na ile mantiki ya kupunguza msongamano na kuweka madaraka kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi itakuwa imepungua.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa hiyo, nilitaka hilo liangaliwe na liweze kuonekana kwamba ni kitu cha muhimu sana. hii ni kwa sababu ukiangalia kwenye 15A imeeleza kabisa kwamba less than 50 kilograms kwamba basi RM’s Court zitaendelea kusikiliza hizo kesi. Kwa hiyo labda ingeendelea iangalie ifanyiwe marekebisha ya kifungu 15A kuweza ku-accommodate cannabis pamoja na khats kwa sababu kimejumlisha hizi hard drugs na hizi drugs nyingine za kawaida.

Mheshimiwa Naibu Spika, hard drugs maana yake ni hizi cocaine, heroin, mandrax na kila kitu; sasa zile effects zake ni kubwa sana na pia bei zake ni kubwa sana ukilinganisha na mirungi na bangi, kwa hiyo ni vitu viwili tofauti ambavyo sasa vimekuwa grouped kwenye sehemu moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lingine ambalo ninaona ni la muhimu sana ni kwenye para ya 22 kifungu cha 48(2) ambacho kimetoa madaraka of course kwenye rekodi ya interrogation au interview, caution statement kuchukuliwa na kuweza kukubalika ukiongezea uzito na hiyo electronic equipment ambayo itaongeza uzito.

Mheshimiwa Naibu Spika, isipokuwa niliona kwamba kui-separate ile alternative ya caution statement kwa sababu caution statement inataratibu zake ambazo kama imetolewa kwa inducement au threat basi trail within a trial inabidi iingie na inaweza kuwa na process ndefu. Kwa hiyo, tutakapoweka paragraph nyingine tofauti ambayo itampa Kamishna Jenerali au yule afisa kuchukua maelezo kama ni alternative ili iweze kukubalika moja kwa moja mahakamani.

Mheshimiwa Naibu Spika, para nyingine ambayo nimeiona ina matatizo ni para ya 31 kifungu cha 53 ambacho kinampa uwezo Commissioner General kuweza ku-forfeit any illegal properties ambazo anaziona kwamba labda zimepatikana kwa njia isiyo ya halali. Kwa hiyo, niliona kwamba illegal properties ambazo zimepatikana through drugs labda kuongeza na abandoned ambazo zimeweza kutupwa au wenyewe wamekimbia bila kuwa na wenyewe basi na yenyewe apewe madaraka aweze kuzi-forfeit kwa Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lingine ni suala la mali ambazo zipo nje ambazo zinaonekana zimepatikana kwa njia ya drugs. Hili suala of course linatakiwa ku-invoke registration ya mutual assistance ambayo lakini hii inahitaji sana bilateral agreements ambazo itakuwa ni ngumu sana lakini nimeona kifungu kimoja ambacho kinaonyesha ushirikiano na other law enforcing agencies.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni vizuri Commissioner General ajaribu kuingia kwenye MOUs na hizi law enforcing agencies ambazo already zina contact nje ili kama inapobidi kuweza kurudisha au kuzichukua hizo mali waweze kuwasiliana na wao ambao wana contact nyingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la mwisho ni suala la huku kwenye schedule kuna mabadiliko mbalimbali ambayo yanaweza kuwa ni makosa tu sababu ya kazi nyingi, lakni nilitaka yaangaliwe kuanzia fomu ya kwanza, pili, tatu na ya nne. Isipokuwa hii fomu ya nne nilitaka kwa seizer wale watuhumiwa ambao wanameza madawa ya kulevya na kuyatoa basi eneo la kuonyesha kwamba kuna shahidi ambaye ameshuhudia kwamba ameona huyo mtuhumiwa akitoa hizo nanii ili iweze kuongezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi wa Mwaka 2018
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru sana kwa kunipa hii na mimi kuchangia muswada huu ambao ni muhimu sana. Muswada wa marekebisho ya sheria ya Ubia baina ya sekta ya umma na sekta binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, muswada huu ni muhimu na naona kama umechelewa sana, umuhimu wake unajidhihirisha na miradi ambayo kama tunayo hapa nchini ya ubia wa PPP na sekta ya umma. Kama miradi hiyo ipo basi ni michache sana, ndiyo maana marekebisho haya naamini yamekuja ili kuweza ku-facilitate kuweza kupata wawekezaji ambao tunaweza kuingia nao ubia na tuweze kuwa na miradi kama hii. Miradi ambayo ipo hapa ni michache sana na mfano ambao unaweza kuutolea siuoni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia Mradi wa DART wa mabasi upo, lakini ukiangalia Mradi wa Daraja la Kigamboni upo, lakini utaona kwamba imekwenda kwenye sekta ya umma kwa sekta ya umma. Ni muhimu sana marekebisho haya yameletwa kwa wakati muafaka ili kuweza kuangalia namna gani ambavyo tunavyoweza kuleta wawekezaji waweze kuingia kwenye miradi mikubwa na midogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Bara la Afrika tu, kwa sababu miradi kama hii iko kote duniani. Nilikuwa nasoma juzi Marekani wana miradi ya PPP mingi sana, Ulaya mingi sana na kama hapa Afrika, South Africa ndiyo ambayo inaongoza kuwa na miradi mingi na ambayo imekuwa successful. Kule wana miradi zaidi ya 400 mikubwa na hii midogo midogo hii kwenye provinces zao ambazo ni kama Halmashauri za kwetu hapa. Ukiangalia mikubwa iko zaidi ya 100, kwa hiyo ni nchi ambayo utakuta kwamba wanafanya vizuri sana kwenye mambo haya ya miradi ya PPP, ndiyo maana naona kwamba ni muhimu na hata watalaam wetu waende kujifunza South Africa, waende kujifunza Mauritius ili waweze kuona namna gani ambavyo miradi kama hii inaweza kufanyika kwa ufanisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi mingi kama hii ambayo imefanikiwa hasa ni kwenye mambo ya transportation, road tolls, unakuta ni mingi sana na telecommunication na electricity, lakini miradi kama ya maji kwenye mambo kama haya imekuwa na bahati mbaya kuweza kufanikiwa. Sasa ni vizuri kwamba, sasa hivi miradi hii na amendments hizi zimekuja mpaka miradi mingine ambayo ni midogo kuanzia karibu, unaweza ukatoka zero mpaka kwenye milioni 20; kwa hiyo ni vizuri hata Halmashauri zetu zinaweza kuanza kufanya mazungumzo na kuanza kuingia kwenye miradi kama hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukija kwenye marekebisho ya sheria utaona kwamba kuanzia kwenye kifungu cha pili mpaka kifungu cha 7C yote hii imezungumzia namna gani ya kuweza ku-facilitate miradi hii iweze kufanyika na kuondoa urasimu ambao unaweza kuwa pale na kuleta matatizo. Nimeweza kuleta kitengo maalum ambacho kitaweza kushughulikia PPP, kitengo hiki kimetoka kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu ambacho ilikuwa very dormant sasa hivi iko pale kwa Waziri wa Fedha ambayo tunaamini ya kwamba itafanya kazi nzuri sana chini ya Mheshimiwa Waziri, imeondoa urasimu na imejaribu kuweka uwazi kwenye zabuni ili kuweza kuona kwamba zabuni zinafanyika kwa haki na usalama kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo imeweka muda maalum kwenye hivi vipengele vyote vinne ambavyo vinatakiwa vifuatwe, imewekewa muda maalum kwamba wewe PPP Center unapewa siku 21, wewe Steering Committee umepewa 21, Waziri unapewa siku 21, kwa hiyo ni njia ya kuweza kufanya hii yote iweze kwenda kwa wakati kwamba wawekezaji waweze kufanya kazi yao kwa bidii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utaona kwamba kuna solicited contract pale na unsolicited. Kwa hiyo, utaona kwamba hata kwenye upande wa ubunifu wa wawekezaji wao wenyewe ambao wanaweza kubuni miradi yao pia wamewekewa masharti yao ambayo yako very clear ambayo tumeyajadili kwa kirefu sana kwenye Kamati na kuona kwamba kwa kweli tunaweza kupata wawekezaji wote solicited ambao wataingia ubia na Serikali pamoja na hawa unsolicited ambao pia wanaweza wakaingia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo kubwa sana ambalo lipo ni hawa watalaam wetu ambao watakuwa hapo kwenye PPP Center. Nchi nyingi sana miradi hii imeshindwa kwa sababu ya drafting ya legal contracts. Uandikishaji wa mikataba umefanya kwamba miradi hii iweze ku-fail, kwa hiyo ni muhimu sana Mheshimiwa Waziri hili alizingatie kwamba uandikishaji wa mikataba tutakapofika kwenye hatua ya kuandika mikataba ni lazima kupata uzoefu, lazima kuwa na watu wanasheria ambao wamebobea na siyo siri kwamba hata tukipata watalaam kutoka nje, vinginevyo sheria hii/mabadiliko haya yatakuwa hayana umuhimu wowote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uandikishaji wa mikataba, tumepata fundisho kwenye IPTL. IPTL mradi ule ulikwenda na ulifanyika kienyeji ingawaje uliweza kusaidia 100 megawatts ambazo tumeingia mkataba kwa njia ya
kuweka umeme kwa njia ya dizel lakini madhara yake tumeyaona. Kwa sababu mkataba haukufanyika kwa uwazi na umeletea gharama kubwa sana Serikali, ambayo sasa Serikali ilitakiwa ilipe IPTL mamilioni ya hela kila mwezi kiasi kwamba mpaka Awamu ya Tano imeamua kuyafunga. Kwa hiyo, suala la uandikishaji wa mikataba, legal drafting ni lazima lipewe umuhimu wake wa kipekee vinginevyo mabadiliko haya hayatakuwa na maana yoyote na yataturudisha kule ambako tupo.

Mheshimiwa Mwenyekit, naamini kabisa kwamba kama tutapata committed people ambao watakuwa pale kwenye PPP Center, wakafanya kazi kwa uadilifu, suala la corruption litaondoka, naamini kabisa tunaweza tukapiga hatua kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la msingi pamoja na hayo, baada ya sheria hii ya mabadiliko haya kupita Mheshimiwa Waziri lazima atangaze sasa priority zote ambazo zinatakiwa Serikali inataka ubia na miradi ipi, lazima itangazwe na itangazwe siyo kwenye gazeti tu lakini tumia media zote, tangaza miradi yote ambayo unaona ya kwamba sasa hivi Tanzania tuko tayari kuingia kwenye ubia wa PPP na miradi ifuatayo ni hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashangaa sana mpaka sasa hivi nchi hii kukosa mradi wa PPP kwenye road toll, sijatembea kwenye nchi yoyote duniani nikakuta kwamba hakuna mradi wa road toll ambao nchi imeingia na nchi nyingine. Marekani wenyewe wanafanya road toll, Ulaya kwenyewe kuna road toll, sasa hapa kwa nini hakuna road toll.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunategemea kwamba hii miradi mingine barabara yetu hii ya Chalinze nategemea SGR sasa hivi ya Tanga, tangaza mradi wa Tanga wawekezaji wapo watajitokeza mimi nawajua.

Kwa hiyo, naamini kabisa marekebisho haya yakifanyika vizuri tutapiga hatua tena kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni hayo tu nilitaka kuchangia na nashukuru sana, lakini mapendekezo ambayo tumeyapendekezo ambayo tumeyatoa yazingatiwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2018
MHE. BAL. ADADI M. RAJABU: Mheshimiwa Spika, nami nashukuru sana kwa kupata nafasi hii ya kuchangia hii Finance Bill ambayo ni sheria muhimu sana. Kwanza napenda kumpongeza sana Waziri wa Fedha pamoja na wasaidizi wake wote. Waziri wa Fedha amefanya kazi kubwa sana kwa sababu, mapendekezo ambayo yamekuja kwenye Muswada huu na vifungu ambavyo vimekuja kwenye Muswada huu kwenye Kamati ya Bajeti ni vingi, lakini Waziri wa Fedha amekuwa very flexible.

Mheshimiwa Spika, hoja nyingi ambazo Kamati imeweka, zimekubalika. Hoja nyingi amekubali kuzirekebisha na ndiyo maana amekuja na hii schedule of amendment ambayo iko hapa. Ni hoja chache ambazo Kamati imemshauri kama mlivyoona kwenye ripoti ili Wizara ikae ijaribu kuzirekebisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwanza nitaanza na Treasury Single Account, Cap 34(a). Mwanzoni nilipata bahati ya kuchangia Wizara ya Fedha na nilifikiri kwamba mfumo huu unakusanya fedha zote unapeleka kule Hazina au Benki Kuu ndiyo wanaanza kugawa. Baada ya kukaa kwenye Kamati na kwa muda mrefu sana na ku-present hoja mbalimbali, Waziri huyu wa Fedha amekubali kubadilisha mambo chungu nzima. Tulifikiri kwamba hela zote mpaka kwenye Halmashauri zetu zinakwenda na zote zinachukuliwa na huu Mfumo wa Treasury Single Account na kweli aliweka kwenye sheria, lakini amebadilisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukiangalia Kifungu cha 11B(1)(c), Waziri wa Fedha ame-delete, ameondoa kile kifungu ambacho kilikuwa kinachukua mapato yote ya Halmashauri, own source na kupeleka kwenye Mfuko wa TSA. Sasa hilo ningependa kumshukuru sana na mambo mengi ambayo ameyafanya pale. Nilifikiri pia hii Mifuko ya Special Accounts inakwenda kwenye TSA, lakini mifuko hiyo ni mifuko ambayo iko ring fenced; Mifuko ya Maji, Barabara, Reli na mifuko yote ambayo ni special ambayo imeelezewa kwenye Katiba 135, Subsection (2), yote iko vilevile. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwa hili nashauri Waheshimiwa Wabunge kwamba mfumo huu una matatizo madogo madogo ambayo yameonekana na tulikubaliana kwamba mfumo huu basi uanze tarehe 30 Septemba, 2018 ili kipindi hiki cha miezi mitatu, Mheshimiwa Waziri aweze kurekebisha mambo ambayo yapo. Kwa hiyo, mfumo huu kama ambavyo upo, mwanzoni pia tulifikiri kwamba unavunja Katiba, lakini hakuna kitu kama hicho. Mfumo huu hauvunji Katiba na uko sawasawa kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili, ni suala la ku-repeal Plan Commission. Suala hili tunaelewa kabisa sababu za Planning Commission ni think tank, lakini Serikali imeamua kufuta. Wameleta Muswada wa kufuta hii Cap. 314, kuondoa kabisa.

Mheshimiwa Spika, Kamati baada ya majadiliano marefu imeona kwamba kwa kweli kama Serikali inataka kuendelea kufuta kama ambavyo imewasilisha, basi wasifute sheria, ibaki jinsi ilivyo. Kama ni kufuta basi waangalie administratively wahamishe watu, wahamishe Ofisi, lakini sheria isifutwe ibaki vile vile, kwa sababu kesho na keshokutwa tutakuja kuiona umuhimu wake hii sheria.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, bado tunasisitiza kwamba sheria hii isifutwe kwa sababu kwanza imeletwa katika Finance Act, siyo kwa utaratibu. Hii ilitakiwa ije kwenye miscellaneous kwa sababu haihusiani kabisa na mambo ya fedha na Finance Bill. Nashauri kwamba sheria hii isiwe repealed, naunga mkono mawazo ya Kamati na mambo mengine ya utawala kama Serikali inataka kuendelea, basi iendelee. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la tatu ambalo nataka kushauri ni suala la ukusanyaji wa kodi za majengo. Suala hili pia Kamati imeliangalia sana na imeona ile Part XI ambayo iko kwenye sheria ambayo imeletwa, baada ya mawasiliano marefu, Waziri amekubali kuondoa vipengele vyote vya Part XI na kuacha suala la ukusanyaji wa kodi ya majengo libaki vile vile kwa Halmashauri. Kwa hiyo, kutuondolea kifungu cha 38 – 47, yote yamekuwa deleted na iko kwenye amendment yake ambayo amei-present hapa. Kwa hiyo, suala hili limekuwa handled vizuri.

Mheshimiwa Spika, lingine ambalo nataka kushauri ni suala la Road and Fuel Toll, Cap. 220. Kamati imependekeza sana kwamba ongezeko la Sh.50/= kwenye mafuta ya petroli ili iweze kuongeza Mfuko wa Maji, suala hili tumelizungumza kipindi kilichopita lakini halikuweza kupita.

Mheshimiwa Spika, safari hii tunasisitiza kabisa ni muhimu suala hili la hizi Sh.50/= kwamba zitoke kwenye mafuta zikatunishe Mfuko wetu wa Maji, tulipitishe kwa sababu ni suala muhimu ambalo tunaliona kwamba linaweza likasaidia tatizo la maji. Serikali ya Awamu ya Tano imefanya mambo mengi sana, lakini kwenye Sekta ya Maji bado kunasuasua. Kwa hiyo, tunaona kwamba labda hizi hela zikiongezeka pale zinaweza kusaidia kwa njia moja au nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la gaming, tumekwenda na mahojiano mbalimbali na Mheshimiwa Waziri na hiyo ukiangalia kwenye Cap. 41 na kwenye proposal za amendments, Mheshimiwa Waziri amekwenda mpaka kupunguza asilimia 25 kwenye hii Michezo ya Bahati Nasibu, lakini Kamati inazidi kusisitiza baada ya kuongea na wadau tumeona kwamba ni vizuri basi Waziri aka-consider tumeleta mapendekezo iwe kwenye asilimia 20 isipokuwa kwenye mambo ya Casino, basi iendelee kwenye asilimia 15 badala ya kwenda kwenye asilimia 18.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunashukuru sana kama marekebisho hayo yataweza kuchukuliwa na tunamshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa kufanya consideration kwa mapato yote kwenda kwenye GGR. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna suala la mgao wa zile fedha kwenye Halmashauri. Baada ya ushauri mkubwa, Mheshimiwa Waziri amekubali mawazo ya Kamati na nimeona schedule of amendments nyingi za Waheshimiwa Wabunge hapa, badala ya kwenda kwenye fifty fifty kwa vijana na wanawake, basi ameleta schedule of amendiment ambayo itakuwa kwenye 40 vijana, 40 wanawake na 20 kwa walemavu. Kwa hiyo, hayo ni mambo mazuri ambayo ameyafanya Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Spika na Waheshimiwa Wabunge, kwa hiyo, nashauri kwamba ziko amendments chache ambazo
zimeletwa ambazo Kamati imeleta. Kwa hiyo, tumeshukuru sana kama Wizara ingeweza ku-consider na ku-come up na hiyo solution.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nakushukuru sana.