Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Additional Questions to the Prime Minister from Hon. Venance Methusalah Mwamoto (2 total)

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa majibu mazuri, lakini nilikuwa naomba ile sehemu kwa umuhimu uliopo, kwa kuwa wenzetu wanaweza kuja siku moja pale, kwa ajili ya kutaka kujua walipoishi; kwa kuwa ni sehemu ambayo ina kumbukumbu muhimu na viongozi wengi wakubwa walikaa, basi angalau Serikali ifikirie kujenga kitu kingine mbadala kwa ajili ya kuwaenzi na kuwakumbuka wale wenzetu wa Afrika Kusini. Ahsante.
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge ametoa ombi kwamba kwa kuwa eneo hilo la Kilolo lina umuhimu wa kuwa na shule nyingi za sekondari, ifikiriwe kuwa eneo hilo libadilishwe badala ya Magereza liwe elimu. Ni wazo zuri na ni ombi, tunaweza kuangalia ndani ya Serikali, lakini bado nilipokuwa najibu swali la msingi, nilisema eneo hilo la Kilolo linahitaji kuwa na taasisi za shule nyingi kulingana na idadi kubwa ya wanafunzi waliopo.
Mheshimiwa Naibu Spika, bado Halmashauri na wananchi wanahitajika kuweka mikakati ya ujenzi wa shule nyingine, huku Serikali ikiangalia umuhimu na uwezekano wa kubadilisha hilo Gereza kuwa elimu; lakini bado Magereza ni eneo muhimu na ni jambo la msingi pia kuwa na Gereza kwenye eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kadiri ambavyo Serikali tutafanya mapitio, tutawezakuwapa taarifa wananchi wote wa Kilolo.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO:
Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa majibu mazuri, lakini nilikuwa naomba ile sehemu kwa umuhimu uliopo, kwa kuwa wenzetu wanaweza kuja siku moja pale, kwa ajili ya
kutaka kujua walipoishi; kwa kuwa ni sehemu ambayo ina kumbukumbu
muhimu na viongozi wengi wakubwa walikaa, basi angalau Serikali ifikirie kujenga kitu kingine mbadala kwa ajili ya kuwaenzi na kuwakumbuka wale wenzetu wa Afrika Kusini. Ahsante.
WAZIRI MKUU:
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge ametoa ombi kwamba kwa kuwa eneo hilo la Kilolo lina umuhimu wa kuwa na shule nyingi za sekondari, ifikiriwe kuwa eneo hilo libadilishwe badala ya Magereza
liwe elimu. Ni wazo zuri na ni ombi, tunaweza kuangalia ndani ya Serikali, lakini bado nilipokuwa najibu swali la msingi, nilisema eneo hilo la Kilolo linahitaji kuwa na taasisi za shule nyingi kulingana na idadi kubwa ya wanafunzi waliopo.
Mheshimiwa Naibu Spika, bado Halmashauri na wananchi wanahitajika
kuweka mikakati ya ujenzi wa shule nyingine, huku Serikali ikiangalia umuhimu na uwezekano wa kubadilisha hilo Gereza kuwa elimu; lakini bado Magereza ni eneo muhimu na ni jambo la msingi pia kuwa na Gereza kwenye eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kadiri ambavyo Serikali tutafanya mapitio,
tutaweza kuwapa taarifa wananchi wote wa Kilolo .