Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 18 | Sitting 6 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Mifugo na Uvuvi | 72 | 2020-02-04 |
Name
Neema William Mgaya
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. PROF. NORMAN A. S. KING (K.n.y. MHE. NEEMA W. MGAYA) aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itajenga kiwanda cha maziwa Wilayani Makete?
Name
Abdallah Hamis Ulega
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkuranga
Answer
NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema William Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Njombe una ng‟ombe wa maziwa 19,759 na idadi kubwa ya ng‟ombe hawa wapo katika Wilaya ya Makete ambapo wanakadiriwa kufikia 8,310.
Katika mwaka 2018/2019 uzalishaji wa maziwa kwa Mkoa wa Njombe ulifikia lita 8,846,496 zinazokadiriwa kuwa na thamani ya shilingi 6,596,925,230/= na wastani wa bei ya maziwa ulikuwa kati ya shilingi 670/= hadi 1,000/= kwa lita moja. Mwaka 2018/2019 Wilaya ya Makete ilizalisha maziwa lita 1,241,550 zinazokadiriwa kuwa na thamani ya shilingi 1,241,550,000/= na kuifanya Wilaya hii kuwa ya tatu kwa uzalishaji wa maziwa katika Wilaya za Mkoa wa Njombe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ujumla Wilaya ya Mekete inazalisha lita 103,462.5 kwa siku moja. Kwa takwimu hizi ni wazi kwamba maziwa ni bidhaa muhimu kwa kuongeza kipato cha wananchi wa Wilaya ya Makete na Mkoa wa Njombe kiujumla .
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Njombe una kiwanda kimoja cha Maziwa cha Njolifa kilichopo Njombe Mjini chenye uwezo wa kusindika maziwa lita 20,000 kwa siku na mwaka 2018/2019 kilisindika lita 1,620,000. Ni wazi kwamba kiwanda hiki kina uwezo mdogo wa kusindika maziwa ukilinganisha na ma ziwa yanayozalishwa na wafugaji kwa Mkoa wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti kwa kutambua umuhimu wa tasnia ya maziwa kwa wananchi wa Wilaya ya Makete na nchi kwa ujumla, Serikali ya Awamu ya Tano imeendelea kuhamasisha wawekezaji katika Wilaya ya Makete na eneo nzima la Ukanda wa Nyanda za Juu Kusini. Kwa sasa kiwanda cha ASAS kipo katika hatua za mwisho za upanuzi wa kiwanda chake kipya Wilayani Rungwe.
Mheshimiwa Mwen yekiti, Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara na Kituo cha Uwekezaji tunaendelea na kampeni ya kuhamasisha uwekezaji katika viwanda vya maziwa kwa eneo la ukanda huu ili kuweza kutumia maziwa yote yanayozalishwa Mkoani Njombe ikiwemo Wilaya ya Makete. Hivyo, Wizara inaendelea na jitihada za kuhakikisha mwekezaji mahiri anapatikana ili kuhakikisha maziwa yote yanayozalishwa na Mkoa wa Njombe ikiwemo Wilaya ya Makete na maeneo yanayouzunguka Mkoa huu yanapata soko la uhakika kupitia kiwanda au viwanda vitakavyojengwa.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved