Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 17 | Sitting 6 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 77 | 2019-11-12 |
Name
Lucia Ursula Michael Mlowe
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ANATROPIA L. THEONEST (K.n.y. MHE. LUCIA M. MLOWE) aliuliza:-
Njombe ni kati ya Mikoa mikubwa ya Kilimo na ina mashamba darasa ambapo wanafunzi wa maeneo mengine wanakuja kujifunza:-
Je, ni lini Serikali itaanzisha Chuo cha Kilimo katika Mkoa wa Njombe?
Name
Omary Tebweta Mgumba
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Morogoro Kusini Mashariki
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Lucia Michael Mlowe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua mchango wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ikiwemo Mkoa wa Njombe katika uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara. Kutokana na umuhimu huo Serikali ilianzisha vyuo vitatu vya Kilimo katika Nyanda za Juu Kusini ambayo Mkoa wa Njombe umo, ili kuzalisha wataalamu wa Ugani watakaotoa huduma za ushauri kwa wakulima katika mikoa hiyo. Vyuo hivyo ni MATI Uyole, Igurusi na Inyala vyenye uwezo wa kudahili wanafunzi takribani 700 kwa wakati mmoja. Hata hivyo, vyuo hivyo vinadahili wanafunzi chini ya uwezo kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo uchakavu wa miundombinu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilianzisha Chuo cha Wakulima cha Ichenga mkoani Njombe kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wakulima. Kwa sasa Serikali haina nia ya kuanzisha chuo kipya cha kilimo katika Mkoa wa Njombe wala kwenye kanda yoyote ile, badala yake Serikali ina mpango wa kuviboresha vyuo vya kilimo vilivyopo, kikiwemo Chuo cha Wakulima cha Ichenga kwa kuvikarabati na kuviwezesha kifedha, ili viweze kuchukua wanafunzi na wakulima kwa ajili ya mafunzo ya rejea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali itaendelea kushughulikia changamoto katika vyuo vya kilimo ili kufikia lengo la kuwa na wataalamu wa kilimo wa kutosha na hivyo kufanikisha mapinduzi ya kilimo hapa nchini. Vile vile, Serikali inafanya ukarabati kwa chuo cha MATI Inyala kwenye Kanda ya Nyanda za Juu Kusini ambapo Mkoa wa Njombe upo.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved