Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Godfrey William Mgimwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kalenga
Primary Question
MHE. GODFREY W. MGIMWA aliuliza:- Tatizo la mawasiliano ya simu katika Jimbo la Kalenga bado ni kubwa. Je, ni lini Serikali itapeleka minara ya simu kwenye vijiji vya Kaning‟ombe, Ikungwe, Lyamgungwe, Igunda na Ikuvilo?
Supplementary Question 1
MHE. GODFREY W. MGIMWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kuweka minara kwanza niipongeze sana Serikali kwamba imeendelea kupeleka minara katika Jimbo la Kalenga kwa kasi zaidi. Tatizo ninalolipata ni kwamba baada ya kusimikwa ile minara upatikanaji sasa au uanzaji wa kuanza kupata mawasiliano unatumia muda mrefu sana. Ningependa kujua Serikali ina mkakati gani ili mara baada ya kuwekwa ile minara mawasiliano yaanze kupatikana kwa muda unaostahili. (Makofi)
Swali langu la pili, narudi tu kwenye majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba amesema vijiji vilivyotamkwa hapa mwishoni vya Kaning‟ombe na Ikuvilo vitapita katika utaratibu wa kupitia UCSAF lakini katika tovuti ambayo nimekuwa nikiipitia ya UCSAF nitoe tu statistics kidogo inaonyesha kwamba kwa mwaka 2015 zilitangazwa zabuni175, Kata zilizopata wazabuni 116 hii kwa ni Tanzania nzima, idadi ya vijiji 156, miradi kuanza ilikuwa ni Mei, 2015. Lakini katika orodha hii yote hakuna vijiji ambavyo tayari vilishaanza kupatiwa mawasiliano ni zero, kupitia mradi ya UCSAF.
Ningependa kujua Serikali ina mikakati gani kuhakikisha kwamba inaipa pesa UCSAF ili kwamba miradi ambayo imeorodheshwa iweze kukamilika kwa wakati? Ahsante.
Name
Eng. Edwin Amandus Ngonyani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mgimwa naomba nikiri kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuwahangaikia watu wake, anafanya hivyo katika maeneo mengi ambayo Wizara yetu inaisimamia ikiwa ni pamoja na barabara, mawasiliano hayo ambayo leo ameyauliza na masuala mengine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie kwamba yale tunayomweleza anapofuatilia ofisini tunamthibitishia kwamba tutayatekeleza. Nimhakikishie kwamba Awamu hii ya Tano ya Serikali ya Dkt. John Pombe Magufuli inatenda inachoahidi. Mkakati wa kuhakikisha minara ambayo inajengwa inaanza kufanya kazi tutaifuatilia, kwa hili aliloliuliza nadhani ameuliza tu kuongezea utamu, tumemwambia kwamba mnara huo utaanza kufanya kazi mwishoni mwa mwezi Juni kama tulivyoongea, ni kweli na tutafuatilia. (Makofi)
Kuhusu mirafi ya UCSAF, naomba nimhakikishie kama nilivyosema hii Serikali inatenda inachoahidi, katika mwaka huu wa fedha hizo zilizotengwa miradi iliyotangazwa tutahakikisha inakamilika. Lakini usisahau kwamba miradi mingine tuliyoongelea hapa haitekelezwi na UCSAF peke yake mingine inatekelezwa na TTCL na Viettel ambayo katika tangazo hili miradi hiyo hutaiona.
Name
Seif Khamis Said Gulamali
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Manonga
Primary Question
MHE. GODFREY W. MGIMWA aliuliza:- Tatizo la mawasiliano ya simu katika Jimbo la Kalenga bado ni kubwa. Je, ni lini Serikali itapeleka minara ya simu kwenye vijiji vya Kaning‟ombe, Ikungwe, Lyamgungwe, Igunda na Ikuvilo?
Supplementary Question 2
MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali fupi kwa Naibu Waziri.
Ni lini sasa maeneo ya kata za Mwashiku, Ngulu, Uswaya na Igoweko yataweza kupata mawasiliano kama ambavyo Mheshimiwa Naibu Waziri ameweza kujibu swali la Mheshimiwa Mgimwa? Ahsante.
Name
Eng. Edwin Amandus Ngonyani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Gulamali ni mfuatiliaji sana, siyo wa masuala ya mawasiliano peke yake, bali ni pamoja na barabara zake zile mbili ambazo viongozi wetu wakuu walitoa ahadi, na nyakati zote wakati akifuatilia hiyo miradi nimekuwa nikimhakikishia kwamba Serikali hii ya Awamu ya Tano inatenda inachoahidi. Mheshimiwa Gulamali nikuahidi katika yale uliyoyafuatilia vijiji hivi sikumbuki kama ulinitajia. Kwa hiyo, nitafuatilia ratiba ya utekelezaji wa makapuni yote yanayotuletea mawasiliano nchini kuona kama hivi vimeshaingizwa katika ratiba na kama vitakuwa havijaingizwa namhakikishia tutaviingiza.
Name
Khadija Nassir Ali
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. GODFREY W. MGIMWA aliuliza:- Tatizo la mawasiliano ya simu katika Jimbo la Kalenga bado ni kubwa. Je, ni lini Serikali itapeleka minara ya simu kwenye vijiji vya Kaning‟ombe, Ikungwe, Lyamgungwe, Igunda na Ikuvilo?
Supplementary Question 3
MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika nashukuru kwa kuniona, kwa kuwa tatizo la Jimbo la Kalenga linafanana kabisa na tatizo la Mkoa wa Kusini Unguja;
Je, ni lini Serikali itapeleka minara ya simu kwenye vijiji ambavyo bado havijafikiwa na huduma hii kwenye Mkoa wangu?
Name
Eng. Edwin Amandus Ngonyani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Khadija Ali anafahamu kwamba tumefungua ofisi Unguja ambayo kazi yake kubwa ni kuhakikisha mawasiliano yanakamilishwa katika vijiji mbalimbali Unguja na Pemba. Naomba nimhakikishie akitembelea hii ofisi atapata uhakika wa eneo hilo analoliongelea ratiba yake ikoje.
Name
Selemani Jumanne Zedi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukene
Primary Question
MHE. GODFREY W. MGIMWA aliuliza:- Tatizo la mawasiliano ya simu katika Jimbo la Kalenga bado ni kubwa. Je, ni lini Serikali itapeleka minara ya simu kwenye vijiji vya Kaning‟ombe, Ikungwe, Lyamgungwe, Igunda na Ikuvilo?
Supplementary Question 4
MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, pamoja na kuwepo kwa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kwa lengo la kuchangia gharama za ujenzi wa minara maeneo ya vijijini, lakini bado speed ya ujenzi wa makampuni haya umekuwa mdogo sana, kulikuwa napendekezo kwamba sasa Mfuko wa UCSAF ugharamie asilimia 100 ya ujenzi wa minara katika maeneo ya vijijini ambayo hayana mvuto kwa biashara.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefikia wapi katika kuona umuhimu huu wa kwamba Mfuko wa UCSAF ugharamie minara ya vijijini kwa asilimia 100 badala ya kuyaachia makampuni ambayo kwa kweli yamekuwa mazito kupeleka minara vijijni kwa sababu hakuna mvuto wa kibiashara?
Name
Prof. Makame Mnyaa Mbarawa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkoani
Answer
WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, mfuko wa mawasiliano kwa wote unagharamia kuanzia asilimia kumi mpaka asilimia 100; inategemea eneo na eneo. Kama eneo hilo halina mvuto wa kibiashara kabisa mfuko wa mawasiliano kwa wote unagharamia asilimia 100. Kuna tatizo ambalo limejitokeza ni kweli makampuni ya simu yamechelewa kujenga minara ya mawasiliano kwenye maeneo mbalimbali na kwa kulijua hilo sasa Serikali itapiga faini makampuni ya simu yote ambayo yamechelewa kupeleka mawasiliano kwenye maeneo hayo. Ahsante.