Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:- Kwa muda mrefu walemavu wa ngozi (albino) wamekuwa wakiishi kwa hofu katika nchi yao kutokana na kuuawa na kukatwa viungo vyao kwa imani za kishirikina ikiwemo kwa ajili ya kushinda uchaguzi au kujipatia mali:- Je, Serikali ina mpango wa kuwalinda na kuwahakikishia usalama wa maisha yao watu hao wenye ulemavu wa ngozi?

Supplementary Question 1

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri aliyonijibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni kesi ngapi zilizolipotiwa kwa kipindi hiki cha mwaka wa uchaguzi?
Mheshimiwa Naibu Spika, pia ni kwa nini kesi zinacheleweshwa wale walemavu hawapi haki zao kwa haraka?
Na je, ni mikoa mingapi inayoongoza kwa mauaji ya maalbino? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kuhusu Mikoa ambayo inaongoza ni Mkoa wa Mwanza, Mkoa wa Shinyanga na Kigoma.
Swali lake la pili anauliza kwamba ni kesi ngapi, takwimu halisi zilizotokea baada ya kumalizika uchaguzi naomba nimpatie baadaye lakini ninachoweza kusema ni kwamba toka mauaji haya yameanza mwaka 2006 mpaka mwaka jana takribani watu wanakadiriwa kwenye 40 mpaka 43 wameweza kufariki, lakini watuhumiwa karibu 133 na kati ya hao watuhumiwa ambao wamehukumiwa kwa adhabu ya kifo ni 19 tayari ambao wameonekana wana hatia. Kwa hiyo, hizi takwimu za baada ya uchaguzi mpaka saa hivi, hizi naomba nikupatie baadaye. (Makofi)

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:- Kwa muda mrefu walemavu wa ngozi (albino) wamekuwa wakiishi kwa hofu katika nchi yao kutokana na kuuawa na kukatwa viungo vyao kwa imani za kishirikina ikiwemo kwa ajili ya kushinda uchaguzi au kujipatia mali:- Je, Serikali ina mpango wa kuwalinda na kuwahakikishia usalama wa maisha yao watu hao wenye ulemavu wa ngozi?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa matatizo yaliyoulizwa na Mheshimiwa Mgeni kwenye swali namba 106 yanafanana kabisa na matatizo yaliyoko Jimbo la Geita Vijijini. Takribani wanawake wazee wanne kwa mwezi wanauwawa kwa kukatwa mapanga kwa imani ya kishirikina na Jeshi la Polisi halijawahi kufanikiwa kuwakamata wakataji mapanga hao kwa kuwa jiografia ya kutoka Geita kwenda eneo husika ni mbali.
Je, Serikali inajipangaje kupeleka gari maalum na kuunda Kanda Maalum kwa ajili ya kuokoa akina mama wanaokatwa mapanga kwenye Jimbo hilo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi linajitahidi sana kuweza kukabiliana na mauaji haya, lakini kama ambavyo nimezungumza wakati nikijibu maswali wiki iliyopita kuhusiana na changamoto ambazo zinakabili Jeshi la Polisi. Naomba nichukue fursa hii kuweka sawa kidogo takwimu wakati nilikuwa najibu swali la Mheshimiwa Selasini juzi, nilieleza kwamba moja katika changamoto inakabili Jeshi letu la Polisi ni kwamba idadi ya polisi tulionao ni kidogo na kiukweli kihalisia takwimu zinaonyesha kwamba ukiangalia takwimu za kidunia polisi mmoja anatakiwa ahudumie kati ya watu 400 mpaka 450 takriban na siyo 300 mpaka 350. Sisi hapa nchi yetu polisi mmoja kwa upande wa Tanzania Bara anahudumia watu kwenye 1000 mpaka 1200. Kwa hiyo utaona ni tofauti kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa changamoto hizi na changamoto nyingine ambazo tumekuwa tukikabiliana nazo hatua kwa hatua kama hii ya usafiri, nataka nimhakikishie tu Mheshimiwa Musukuma kwamba tumekuwa na changamoto ya usafiri kwa muda mrefu lakini tumepata magari takribani magari 387 ambayo yameweza kugawiwa katika maeneo mbalimbali. Tutaangalia eneo hilo kama halijafika gari tuone ni jinsi gani na uzito wa hali yenyewe ilivyo tushauriane tuone ni nini tutakachofanya ili tuweze kukabiliana na tatizo hilo. Lakini mengine ni changamoto ambazo tunaenda nazo kadri ya uwezo wa bajeti unavyoruhusu.