Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Halima Ali Mohammed

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA ALI MOHAMMED aliuliza:- Takwimu zinaonyesha kuwa kuna kasi kubwa ya ongezeko la wagonjwa wa maradhi ya moyo, kisukari na vidonda vya tumbo (ulcers):- Je, Serikali ina mkakati gani kukabiliana na tatizo hili?

Supplementary Question 1

MHE. HALIMA ALI MOHAMMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa ya Naibu Waziri nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tafiti zinaonyesha kwamba wanawake wanaathirika zaidi na maradhi ya moyo kuliko wanaume.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wanawake hawa ambao ndiyo walezi wa familia hasa wale waliopo kule vijijini?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, Serikali ina mkakati gani wa kudhibiti uingizwaji wa vyakula vibovu ambavyo havina kiwango katika nchi yetu? Ahsante (Makofi)

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu maswali ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Swali la kwanza Serikali ina mkakati gani wa kupunguza kiasi cha magonjwa haya kwa wanawake ambao wanaathirika zaidi kuliko wanaume.
Mheshimiwa Naibu Spika, tofauti ya upatikanaji wa magonjwa haya, kwa jinsia kwa maana ya baina ya wanawake na wanaume ni ndogo sana na kwa maana hiyo, mkakati wa kupambana na kuenea kwa magonjwa haya hauwezi kutofautishwa kwa jinsia. Hivyo mkakati wetu utakuwa ni wa pamoja na tayari Wizara ya Afya imeanza kutekeleza mkakati huo, kwanza kwa kutia umuhimu wa kipekee kwenye kuimarisha Kitengo cha NCD yaani Kitengo cha Magonjwa Yasiyo ya Kuambukiza pale Wizarani chini ya Kurugenzi ya Tiba.
Mheshimiwa Naibu Spika, kitengo hiki tayari kimeishaaza mkakati wa kuandika mkakati wa kupambana na magonjwa haya na mkakati huu utawafikia hao akinamama wa vijijini na watu wote kwa ujumla wake kuanzia ngazi ya huduma za afya kule vijijini, kwa maana ya ngazi ya zahanati, ngazi ya vituo vya afya na ngazi ya hospitali za Wilaya, Mikoa na hata ngazi ya Kanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni kweli kumekuwa na hisia kwamba kuna vyakula visivyo na viwango vinaingia nchini mwetu kutoka nchi za mbali. Serikali kwa kushirikiana kwa maana ya Wizara yetu Wizara ya Afya, ambayo ina kitengo cha TFDA (Tanzania Food and Drugs Authority) ambacho kipo chini ya Wizara yetu ya Afya, pamoja na Kitengo cha Viwango (TBS), wanaendelea kushirikiana kwa pamoja, kukagua mizigo yote ambayo inaingia nchini kwa njia za halali.
Lakini pia vyombo vingine vya kusimamia Sheria kama Majeshi ya Polisi na Uhamiaji, wataendelea kuwa makini kwenye mipaka yetu yote, katika njia zilizo halali na hata zile ambazo siyo halali kudhibiti uingizwaji wa vifaa hivi ikiwemo vyakula na dawa ambavyo havijapitishwa kwa viwango vinavyostahili, kwa mujibu wa Sheria za nchi yetu. (Makofi)