Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. RICHARD M. NDASSA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa ujenzi wa bomba la maji ya Ziwa Victoria kutoka Magu - Sumve - Malya utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza naomba nisahishe jina langu hapa inasomeka Ngassa, siyo Ngassa ni Ndassa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na maelezo mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini naomba Serikali itambue kwamba suala la maji ni suala kila Mtanzania, kila mwananchi anahitaji maji na ndiyo maana unaona Wabunge wote wanasema kuhusu maji.
(a) Swali langu, kwa sababu Serikali katika mwaka 2000 na 2004 iliamua, maamuzi magumu yenye tija, kuyatoa maji ya Ziwa Victoria kuyapeleka Kahama, Shinyanga. Je, Serikali ina mpango gani mrefu wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria katika Mikoa tisa ili maji hayo yawanufaishe Watanzania na mikoa hiyo ni Mwanza, Mara, Kagera, Simiyu, Singida na Dodoma. Serikali ina mpango gani kwa sababu mahitaji ya maji ni makubwa na maji ya Ziwa Victoria yapo hayana kazi nyingine. Je, Serikali ina mpango mkakati gani wa kuhakikisha kwamba maji yanafika katika maeneo hayo?
(b) Mheshimiwa Waziri wa Maji, wananchi wa Jimbo la Sumve katika Kata ya Nkalalo na Mabomba wanashida kubwa ya maji, naomba nikuombe pamoja na maelezo haya utembelee tuende ukajionee mwenyewe jinsi wananchi wa Tanzania wa Jimbo la Sumve wanavyopata taabu ya maji katika Jimbo langu.

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimezungumza jana kwamba tumeleta mapendekezo ya mwongozo kwa kutengeneza mpango wa miaka 2016/2017 na nilisema katika sekta ya maji tumetoa ahadi kwamba katika miji yote ya Mikoa inayozungukiwa na Ziwa Victoria tutahakikisha tunachukua maji ya kutosha kuyafikisha kwenye maeneo husika kwa kiwango ambacho tumeshasema kwenye Ilani, kwamba Miji Mikuu ya Mikoa ipate asilimia 95 ikifika 2020 na ipate asilimia 100 ikifika 2025.
Kwa hiyo, naomba nilihakikishie Bunge hili kwamba azma hiyo ambayo pia Mheshimiwa Rais wetu ameahidi tutakwenda kufanya, tutaomba Waheshimiwa Wabunge muweze kutuunga mkono katika kupanua vyanzo vya upatikanaji wa fedha hasa kuongeza Mfuko wa Maji ili tuweze kutekeleza miradi yote hii ambayo kila Mbunge ameomba Serikali iweze kufanya, ahsante. (Makofi)

Name

Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Primary Question

MHE. RICHARD M. NDASSA aliuliza:- Je, ni lini mradi wa ujenzi wa bomba la maji ya Ziwa Victoria kutoka Magu - Sumve - Malya utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Naibu Spika, jina langu naitwa Mussa Mbarouk, Mbunge wa Tanga Mjini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali ilianzisha mpango wa maji safi na salama vijijini katika mradi uliofadhiliwa na World Bank na mradi ule umekwama. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha katika Halmashauri ya Jiji la Tanga ili kuondoa kero ya maji katika Kata za Mabokweni, Chongoleani, Kilale na Marungu?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali ilianzisha mradi wa vijiji 10 kupitia progamu ya Benki ya Dunia na mradi huo ungali unaendelea. Katika mradi huo tulikuwa na miradi 1,855 kama nilivyotoa taarifa ya awali kwamba katika miradi hiyo miradi 1,143 imekamilika na miradi 454 inaendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na tatizo la fedha ndiyo lililofanya hii miradi isikamilike kwa wakati lakini nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika eneo lako la Tanga kufuatia juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kukusanya fedha, fedha zimeanza kutoka na nikupe tu taarifa Mheshimiwa Mbunge kwamba wiki iliyopita tumeletewa shilingi bilioni 10 kwa ajili ya kuendelea kulipa miradi hiyo mingi ambayo ilikuwa imesimama na siyo Tanga tu, ni karibu Mikoa yote miradi ilikuwa imesimama.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nikuhakikishie kwamba Serikali inatoa fedha kuhakikisha miradi hiyo inakamilika ili katika progamu ya pili tuanze kuweka tena miradi mingine. (Makofi)