Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:- Mgonjwa anapotoka Zanzibar na kupelekwa kwa matibabu nje ya nchi analazimika kupata rufaa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili licha ya kuwepo kwa Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja, Zanzibar ambayo ina madaktari wenye uwezo kama wale wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. (a) Je, kwa nini Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja haijapewa uwezo wa kutoa rufaa ya matibabu nje ya nchi? (b) Je, kuinyima uwezo huo Hospitali ya Mnazi Mmoja ni kutoiamini hospitali hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Afya, naomba kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka nyuma kulikuwa kuna utaratibu wa Wizara zetu mbili hizi kukutana na kubadilishana uzoefu na vikao hivyo vilivyokuwa vinafanyika vilikuwa vina tija ndani yake ambavyo vilipelekea Madaktari Bingwa kutoka Muhimbili kuja Zanzibar na kutoa ushirikiano mkubwa. Vikao hivyo sasa hivi havifanyiki kwa muda mrefu kidogo. Je, Serikali ina kauli gani kuhusu vikao hivyo?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba Serikali ina mpango gani na vikao hivyo? Vikao hivyo havijawahi kufutwa na havitofutwa kwa sababu Wizara hizi mbili (Wizara ya Afya ya Jamhuri ya Muungano na Wizara ya Afya ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar) zimekuwa na utamaduni huo na zinaona utamaduni huo ni mzuri na zitauendeleza. Hivyo, tutaendelea kuvihuisha ili viwe active zaidi kuliko ilivyokuwa katika mwaka huu mmoja wa uchaguzi uliopita. Lakini kuanzia mwezi Januari tayari tumekwisha kufanya kikao kimoja, naomba kumpa taarifa Mheshimiwa Ussi.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:- Mgonjwa anapotoka Zanzibar na kupelekwa kwa matibabu nje ya nchi analazimika kupata rufaa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili licha ya kuwepo kwa Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja, Zanzibar ambayo ina madaktari wenye uwezo kama wale wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. (a) Je, kwa nini Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja haijapewa uwezo wa kutoa rufaa ya matibabu nje ya nchi? (b) Je, kuinyima uwezo huo Hospitali ya Mnazi Mmoja ni kutoiamini hospitali hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante kwa kunipa swali kwenye Wizara ya Afya. Suala linalotokea Hospitali ya Mnazi Mmoja ni sawasawa kabisa na masuala yanayotokea katika Hospitali ya Rufaa ya Ndanda, Mkoa wa Mtwara. Mheshimiwa Waziri atakubaliana na mimi alipotembelea alitoa ahadi ya wafanyakazi wasiopungua 85; hivi ninavyoongea sasa hivi hospitali ya Rufaa ya Ndanda inakaribia kukosa hadhi ya kuitwa Rufaa kwa sababu kuna Daktari Bingwa mmoja tu. Je, Wizara yake ina mpango gani wa kuwawezesha watu hawa ili waendelee kutoa huduma kwa sababu ni hospitali ambayo ina vifaa vingi lakini inakosa wataalam wa kuvitumia?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba mpango tulionao ni kusubiri kibali kutoka kwa wenzetu wa utumishi kitoke, kitakapotoka tutaajiri Madaktari Bingwa kwa kiasi ambacho tutakuwa tumekasimiwa na kuwatawanya kwenye hospitali zote za Rufaa za Mikoa nchini ikiwemo Hospitali ya Ndanda.

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:- Mgonjwa anapotoka Zanzibar na kupelekwa kwa matibabu nje ya nchi analazimika kupata rufaa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili licha ya kuwepo kwa Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja, Zanzibar ambayo ina madaktari wenye uwezo kama wale wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. (a) Je, kwa nini Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja haijapewa uwezo wa kutoa rufaa ya matibabu nje ya nchi? (b) Je, kuinyima uwezo huo Hospitali ya Mnazi Mmoja ni kutoiamini hospitali hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Changamoto za mahospitalini zimekuwa nyingi na moja kati ya kero kubwa ambayo wananchi wanaipigia kelele ni kile kitendo ambacho mwananchi akiuguza mgonjwa wake na hatimaye akapoteza maisha haruhusiwi kuchukua mwili wa marehemu mpaka alipe gharama za matibabu ambazo kimsingi hazikumsaidia mgonjwa wake mpaka amefariki dunia. Kitendo hiki kinatengeneza taswira mbaya kwa wananchi kuonesha kwamba Serikali haijali utu na haithamini utu wa wananchi wake.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba endapo mwananchi atafiwa na mgojwa wake lile deni la matibabu asamehewe ili familia ijikite tu katika kushughulikia suala la mazishi?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba kwanza nakanusha kwamba Serikali haithamini utu wa Watanzania, hapana Serikali ina thamini sana utu wa Watanzania wote na ndio maana ikaweka utaratibu mzuri sana wa kutoa huduma za afya kwa watu wote hata wasiojiweza. Tanzania ni miongoni mwa nchi chache sana ambazo zinawapa usawa wa huduma tena bure kwa kuwahudumia takribani asilimia 67 ya wagonjwa wote hapa nchini bure bila gharama yoyote ile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa wale wachache ambao wanatengeneza hiyo asilimia 33 ya wanaochangia huduma za afya, kama itajitokeza kwa bahati mbaya baada ya kuhudumiwa akafariki halafu Sheikh Mtolea unasema sasa pale ndio utu wake unaanza, sio sahihi. Utu wa Mtanzania upo akiwa anaumwa, akiwa anahudumiwa kwenye hospitali na hata ikatokea bahati mbaya umauti ukamkuta utu uko pale pale. Lakini gharama za mtu ambaye amekwishahudumiwa iwe alipona ama kwa bahati mbaya alipoteza maisha; zipo pale pale ni lazima ziwe compensated na Serikali haiwezi kuziondoa.