Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dua William Nkurua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. DUA W. NKURUA aliuliza:- Katika ujenzi wa barabara ya Mangaka - Mtambaswala na Mangaka - Nakapanya, wapo wananchi ambao walishafanyiwa tathmini ya fidia ya kupisha ujenzi huo hawajalipwa na wengine wamepunjwa. Je, Serikali italeta lini wataalamu wa kuhakiki fidia hizo ili kila mwananchi apate haki yake?

Supplementary Question 1

MHE. DUA W. NKURUA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika wale ambao walifanyiwa tathmini ya awamu ya kwanza, wapo ambao mpaka sasa hawakulipwa, Majina yao yalirukwa katika Kijiji cha Misawaji, lakini pia wapo ambao walifanyiwa tathmini kwamba nyumba zao zitabomolewa nusu lakini zimebomolewa zote na hivi ninavyokwambia wamechanganyikiwa kabisa.
Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kutuma watu tumuoneshe watu ambao wameathirika ili wapate haki yao?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa barabara kutoka Masasi mpaka Mangaka imekamilika, hadi sasa magari yenye uzito mkubwa kutoka Songea kuelekea Masasi yanatumia hiyo barabara.
Je, Mheshimiwa Waziri haoni umuhimu wa kuleta mizani katika Mji wa Mangaka ili kuokoa barabara ambayo Serikali imetumia gharama kubwa?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana nae kwamba tutatuma watu waende wakalichunguze hilo suala na hatimaye tuweze kulipatia ufumbuzi stahiki. Ninachoomba kumhakikishia tu ni kwamba Serikali hii inafuata sheria na yeyote mwenye haki ya kulipwa fidia atalipwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali lake la pili nadhani anafahamu kwamba hizo barabara anazoziongelea bado hazijakamilika na hivi karibuni nimepiata katika eneo lake ingawa kwa bahati sikumjulisha kwa sababu ilikuwa ni dharura wakati natokea Jimbo la Namtumbo. Ninamhakikishia mara barabara hizi zitakapokamilika na umuhimu utakapoonekana kwamba kuna umuhimu mkubwa wa kuweka mizani, Serikali itafanya maamuzi stahiki. (Makofi)

Name

Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DUA W. NKURUA aliuliza:- Katika ujenzi wa barabara ya Mangaka - Mtambaswala na Mangaka - Nakapanya, wapo wananchi ambao walishafanyiwa tathmini ya fidia ya kupisha ujenzi huo hawajalipwa na wengine wamepunjwa. Je, Serikali italeta lini wataalamu wa kuhakiki fidia hizo ili kila mwananchi apate haki yake?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa barabara ya kutoka Sumbawanga kwenda Mpanda takriban kilometa 50 zimeshatengenezwa na magari makubwa ya mahindi zaidi ya tani 60, 70 yanapita kuelekea Mpanda. Nimeshamwomba Waziri wa Ujenzi kupeleka gari ya mizani ili kudhibiti uharibifu wa barabara kabla wakandarasi hawajakabidhi kwa sababu barabara inaanza kuharibika kabla haijakabidhiwa. Je, ni lini Serikali itapeleka gari ya mizani ili kudhibiti barabara hiyo isiendelee kuharibika?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchukua nafasi hii kumhakikishia Mheshimiwa Keissy na wananchi wa Sumbawanga hadi Mpanda kwamba barabara ile kwanza tutaikamilisha kuijenga. Tutakapoona umuhimu wa kuweka mizani kutokana na tathmini ya wataalam tutakaowapeleka kufanya shughuli hiyo tutaweka mizani hiyo.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. DUA W. NKURUA aliuliza:- Katika ujenzi wa barabara ya Mangaka - Mtambaswala na Mangaka - Nakapanya, wapo wananchi ambao walishafanyiwa tathmini ya fidia ya kupisha ujenzi huo hawajalipwa na wengine wamepunjwa. Je, Serikali italeta lini wataalamu wa kuhakiki fidia hizo ili kila mwananchi apate haki yake?

Supplementary Question 3

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Naitwa Alex Raphael Gashaza, Mbunge wa Jimbo la Ngara.
Kwa kuwa barabara ya Murugarama – Rulenge – Nyakahura yenye kilometa 85 ni barabara ambayo iliahidiwa na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mwaka 2008 kwamba itaweza kujengwa kwa kiwango cha lami na miaka miwili iliyopita wananchi wa Jimbo la Ngara walikuwa wakielezwa kwamba tayari upembuzi yakinifu wa barabara hii umeanza.
Naomba kumuuliza Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi ni lini mkandarasi atakuwepo site kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hii? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tumepata taarifa kutoka kwa Waziri mwenyewe wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano juu ya upatikanaji wa fedha za kulipa madeni ya wakandarasi, kama jana mlimsikia alisema ni karibu shilingi bilioni 419 zimeshatolewa. Kwa hiyo, katika lile deni la shilingi trilioni 1.268 sasa tumeshuka tuko kwenye shilingi bilioni 800 na zaidi. Naomba kuchukua nafasi hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba mara fedha zitakapopatikana kwa mradi huo, barabara yake itashughulikiwa kama ilivyoahidiwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.