Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. ULEGA aliuliza:- Je, ni hatua gani madhubuti Serikali itachukua kwa kampuni zinazoshinda tender (zabuni) za ununuzi wa korosho lakini haziwalipi wakulima kwa wakati?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Naomba kwa namna ya kipekee kabisa wakati nikijielekeza kuuliza swali hilo niipongeze sana Serikali yetu ya Awamu ya Tano kwa kazi nzuri inayofanya ya kuwalinda wakulima wetu na wananchi wetu wa hali ya chini. Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hiyo pia nimpongeze Mkuu wetu wa Mkoa Engineer Evarist Ndikiro kwa kazi nzuri aliyoifanya mwaka wa jana wa kuyalazimisha Makapuni mawili ya Alpha Choice na Kaisari ambayo yaligoma kuwalipa kwa wakati wakulima wa korosho wa vijiji vya Msonga, Kalole, Mkuranga mjini na Kimanzichana Kusini. Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jibu la msingi la Mheshimiwa Waziri anaeleza kwamba wanapochelewesha…
MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Ahsante sana. Wanapochelewesha kulipa malipo ya wakulima wa korosho huchelewa. Je, Serikali ipo tayari sasa kuhakikisha inawasimamia ipasavyo na madhubuti kabisa wanunuzi hao ili wawe wanaondoa mazao yao katika maghala yetu mapema iwezekanavyo ili mzigo mwingine wa wakulima uingie kwa wakati na waweze kupata pesa za kuinua maisha yao?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaona zao la korosho kama mfano wa namna ambavyo tunaweza tukafanya kilimo chetu kifanikiwe. Mafanikio makubwa na ya kihistoria ambayo yamepatikana katika korosho katika msimu uliopita ni kielelezo tosha cha namna Serikali ya Awamu ya Tano inavyotaka kushughulikia changamoto za kilimo. Kwa hiyo, hatutakubali mtu yoyote aje avuruge mafanikio yetu na ndiyo maana hizo kanuni zimeweka wazi kama unaenda ku-bid kununua korosho ni lazima kuweka dhamana. Hiyo inatusaidia kuwashughulikia wanunuzi wababaishaji ambao wanaenda ku-bid lakini baadaye korosho zinahifadhiwa halafu baadae wanakuja kulalamika kwamba zimepoteza sifa. Kwa hiyo, kwa sasa haiwezekani tena na niwahakikishie tu wakulima na Waheshimiwa Wabunge kwamba mtu yeyote ambaye ameshinda tender ya kununua korosho atalazimika kulipia na haiwezekani baadaye akaja kuleta malalamiko mengine, kwa hiyo, hilo halitatokea.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. ULEGA aliuliza:- Je, ni hatua gani madhubuti Serikali itachukua kwa kampuni zinazoshinda tender (zabuni) za ununuzi wa korosho lakini haziwalipi wakulima kwa wakati?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti nashukuru sana. Tatizo hili la wazabuni kushinda tender na baadae kuchelewesha huduma kwa Watanzania kwa muda uliokusudiwa imekuwa tatizo kubwa katika nchi yetu. Mifano ya wazi zipo katika Halmashauri za Wilaya ya Mbulu kwa miradi ya maji na miradi ya afya. Mifano hiyo ni kama ambavyo kupewa tender makampuni ambayo hayana uwezo na hatimaye baadaye kuchelewesha huduma hizi. Je, Seriakli yetu sasa kutokana na hali hii ambapo tenda hutolewa na wataalam ndani ya Halmashauri, inachukua hatua gani kuhakikisha kwamba Watanzania wanapata huduma kwa wakati uliokusudiwa kutokana na muda wa mikataba?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba nilichozungumzia kwenye korosho ni zile taratibu ambazo tumeweka kwa ajili ya korosho, lakini ukweli wa mambo, kuna utaratibu wa kawaida wa kisheria kuhusiana na mambo ya tender. Sheria yetu ya manunuzi inaweka wazi namna tender inavyotakiwa kuendeshwa, lakini vilevile inaweka masharti kuhusiana na utekelezaji wa miradi kwa yule ambaye ameshinda tender na kwa vyovyote vile hairuhusiwi kisheria mtu ambaye ameshinda kutelekeza ile kazi kama kuna mapungufu ambayo yametokea ni vizuri kuangalia katika kesi zenyewe ili wale ambao wamehusika waweze kuchukuliwa hatua za sheria.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ABDALLAH H. ULEGA aliuliza:- Je, ni hatua gani madhubuti Serikali itachukua kwa kampuni zinazoshinda tender (zabuni) za ununuzi wa korosho lakini haziwalipi wakulima kwa wakati?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Moja ya sababu zinazofanya ucheleweshwaji wa malipo ya korosho ni pamoja na tamko la Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, alitamka kwamba korosho zote za Mkoa wa Lindi na Mtwara zipitie Bandari ya Mtwara kitendo ambacho bandari ya Mtwara ilishindwa kusafirisha korosho hizo kwa wakati na wanunuzi wakaacha kulipa kwa sababu korosho zao mpaka ziingie kwenye maji ndipo waendelee kufanya malipo. Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hivyo tu, sababu ya pili; ni kwamba hata hayo makampuni mnayosema kwamba mnayadhibiti pale ambapo yanakuwa yanachelewesha kulipa lakini bado kuna mtindo wa hayo makampuni kubadilisha majina. Unalifutia jina kampuni hili, mwenye kampuni ni yule yule anatengeneza kampuni nyingine…
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Je, Serikali inatoa kauli gani namna ya kukabiliana na matatizo hayo?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kama alivyosema kwamba kitendo cha kuelekeza korosho ipelekwe nje kupitia Bandari ya Mtwara ilikuwa ni moja kati ya sababu ambazo zilipelekea ucheleweshwaji wa malipo na kuvuruga kwa kiasi fulani soko la korosho. Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo nimueleze Mheshimiwa Mbunge kwamba Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa na Serikali kwa ujumla walifanya hivyo kwa nia njema. Tulitaka vilevile kujenga Bandari ya Mtwara kama moja kati ya bandari zetu, kwa hiyo, ilikuwa ni kwa nia njema. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile hata ilipotokea changamoto ile ya mizigo kurundikana bandarini, Serikali ilikuwa rahisi kuchukua hatua na kuruhusu ipitie Bandari ya Dar es Salaam. Kwa hiyo, baadae tatizo hilo liliisha. Kuhusu hili la makampuni kutumia majina mbalimbali, ni tatizo kubwa, tunatambua kwamba unakuta mtu mmoja au watu wale wale wanakuwa na kampuni zaidi ya kumi, wana-bid katika soko lile lile. Lakini nikueleze tu kati ya mabadiliko makubwa ambayo tumefanya ni hilo la kuleta kanuni na utaratibu ambao ni lazima kuweka security bid ili baadaye ukishashinda tender baadaye huwezi kukimbia na kusema kwamba sitakuja kuchukua korosho. Kwa sasa ni lazima uchukue kwa sababu usipochukua, fedha zako tayari ulishaziacha na Serikali itawalipa wakulima.