Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:- Mkoa wa Shinyanga na Simiyu inaunganishwa kwa barabara ya vumbi, tofauti na mikoa mingine ambayo imeunganishwa kwa barabara za lami. (a) Je, Serikali itaunganisha lini mikoa hiyo kwa barabara ya kiwango cha lami kwa kumalizia kilometa 102 zilizobaki katika barabara ya Lamadi - Mwigumbi kupitia Bariadi? (b) Je, Serikali itaona umuhimu wa kuunganisha makao makuu ya Wilaya za Mkoa wa Simiyu kuunganishwa kwa barabara za kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa vile nchi yetu ina uhaba wa majengo ya shule, zahanati na vituo vya afya, je, Serikali iko tayari kumuagiza mkandarasi ambaye sasa hivi yuko site kujenga majengo ya kudumu ili baada ya mradi kukamilika majengo hayo yaweze kutumika kwa ajili ya matumizi ya shule, zahanati na vituo vya afya? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa barabara za Mkoa wa Simiyu zinaunganishwa na barabara za vumbi na kwa sasa hazipitiki kutokana na mvua zinazoendelea.
Je, Serikali iko tayari kutenga fedha kutoka kwenye Mfuko wa Barabara ili kuweza kutengeneza barabara hizo na ziweze kupitika kwa urahisi tofauti na ilivyo sasa? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, mkandarasi aliyeko site mkataba wake ulishasainiwa. Hata hivyo, nawaagiza TANROADS Mkoa wa Simiyu waangalie uwezekano katika mkataba huo kama inaweza ikafanyika variation au kama kifungu hicho kipo wahakikishe majengo yanayojengwa na mkandarasi huyo yaweze kuangalia matumizi ya baadaye ambayo Mheshimiwa Mbunge ameomba. Kama itashindikana, Serikali itatafuta njia nyingine kupitia Wizara husika ya Afya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa swali la pili, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Mfuko huo anaoungelea ndiyo tunaoutumia kujenga na kukarabati barabara zote nchi nzima. Naomba akubali mfumo tulio nao ndiyo huo, hatuna mfuko maalum kwa ajili ya barabara hii peke yake.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:- Mkoa wa Shinyanga na Simiyu inaunganishwa kwa barabara ya vumbi, tofauti na mikoa mingine ambayo imeunganishwa kwa barabara za lami. (a) Je, Serikali itaunganisha lini mikoa hiyo kwa barabara ya kiwango cha lami kwa kumalizia kilometa 102 zilizobaki katika barabara ya Lamadi - Mwigumbi kupitia Bariadi? (b) Je, Serikali itaona umuhimu wa kuunganisha makao makuu ya Wilaya za Mkoa wa Simiyu kuunganishwa kwa barabara za kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kuniona niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa katika Mpango wa Maendeleo wa mwaka mmoja ulio mbele yetu, miundombinu si kipaumbele.
Kwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Magufuli wakati akiomba kura aliahidi ujenzi wa barabara za lami nchini kote ikiwemo Jimbo langu la Babati Mjini ambako aliahidi ujenzi wa kilometa 20 za lami. Naomba nifahamu, ni lini ahadi hii itatekelezwa kwa wananchi wa Babati?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahadi zote ambazo zimetolewa kwanza na Chama Tawala kupitia Ilani yake ya mwaka 2015 - 2020 Serikali hii ina wajibu wa kuzitekeleza. na tutaitekeleza
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hiyo anayoiongelea namuomba awasiliane na TANROADS mkoa ili kuangalia vipaumbele vya sasa vilivyopo katika mkoa ule. Kama barabara hiyo ni moja kati ya vipaumbele vya mkoa, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaitekeleza katika kipindi hiki kama ambavyo iliahidiwa katika kipindi cha kampeni

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:- Mkoa wa Shinyanga na Simiyu inaunganishwa kwa barabara ya vumbi, tofauti na mikoa mingine ambayo imeunganishwa kwa barabara za lami. (a) Je, Serikali itaunganisha lini mikoa hiyo kwa barabara ya kiwango cha lami kwa kumalizia kilometa 102 zilizobaki katika barabara ya Lamadi - Mwigumbi kupitia Bariadi? (b) Je, Serikali itaona umuhimu wa kuunganisha makao makuu ya Wilaya za Mkoa wa Simiyu kuunganishwa kwa barabara za kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Na mimi kama swali la msingi lilivyoongea kuhusu Mkoa wa Simiyu kuunganishwa na mikoa mingine, ni wazi kwamba Mkoa wa Simiyu bado haujaunganishwa na Mkoa wa Singida ambao unapitia katika Daraja la Sibiti – Mkalama - Nduguti - Iguguno. Nataka nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, je, anafahamu kwamba Daraja la Mto Sibiti ndilo kiunganishi kikubwa katika Mkoa wa Simiyu na Singida na mpaka sasa mkandarasi hayupo site? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu kwamba Daraja la Sibiti ni muhimu katika mawasiliano kati ya Mkoa wa Simiyu na Singida na ndiyo maana kazi kubwa inafanywa sasa kutokana na matatizo yaliyotokea ili kuhakikisha mawasiliano yanakuwepo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mkandarasi, kwa kuwa fedha za kulipa madeni ya wakandarasi tumeanza kupata ambapo huyu naye ni mmoja kati ya wakandarasi wanaotakiwa kulipwa ili waendelee na kazi. Mara fedha zitakapopatikana, mkandarasi atarudi site ili aweze kukamilisha kazi ambayo alisaini kuifanya.