Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuanzisha na kumiliki Bureau de Change zake yenyewe badala ya kuacha huduma hiyo kuendelea kutolewa na watu au taasisi binafsi?

Supplementary Question 1

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba Serikali imebaki katika kuweka mazingira mazuri, lakini naona kwamba mazingira mazuri hayo si kweli sana kwa sababu hayaonekani maana wananchi wanalalamika sana. Kwa sababu ukienda Bureau de Change hii ina rate hii, ukienda Bureau de Change nyingine ina rate tofauti na zimetapakaa sehemu zote kama sisimizi. Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha rates hizo zinalingana? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri kuwa Serikali imejitoa katika biashara hii ya kumiliki Bureau de Change lakini huo ulikuwa ni uamuzi wa zamani na tujue kwamba sasa hivi dunia imebadilika, ni dunia ya sasa. Je, atakubaliana nami kwamba sasa umefika wakati wa Serikali kumiliki huduma hii ili kuwaondolea wananchi wake matatizo ambayo wanakabaliana nayo? Ahsante.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kumshukuru kwa kuuliza maswali mazuri ya nyongeza ambayo yanakidhi haja na yanaakisi kinachoendelea katika maduka yetu ya kubadilisha fedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, jibu la swali lake la kwanza kwamba rates ni tofauti sana kutoka duka moja kwenda duka lingine, nakubaliana naye na hii yote ni kuonesha kwamba tuko ndani ya soko huria na kila mtu anatakiwa ku-charge anavyoona inafaa. Pia kiuchumi, sisi wachumi tunafahamu kwamba bei ya bidhaa yoyote ile hutegemea na demand na supply. Kwa hiyo, kama demand ya bidhaa hiyo ni kubwa bei zitakuwa tofauti kutoka kwa muuzaji mmoja kwenda kwa muuzaji mwingine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, Serikali iweze kurudi kwenye kuendesha biashara kama hizi na kwamba huo ulikuwa ni uamuzi wa zamani, naamini uamuzi ule ulikuwa ni sahihi na bora. Kama nilivyosema katika jibu langu la msingi kwamba tangu mwaka 1991 Serikali ilishajitoa kuendesha mabenki haya. Tunaendelea kusisitiza, sisi kama Serikali tutaendelea kutunga sera na sheria mbalimbali za kusimamia maduka haya ili yaweze kutoa huduma zilizo bora kwa wananchi wetu.