Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami baraba Mnanila – Manyovu – Kasulu ili kuwasaidia wananchi wa maeneo hayo?

Supplementary Question 1

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza niipongeze Wizara kwa majibu mazuri, baada ya hapo nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii ya Manyovu - Kasulu imekuwa ni kero kubwa sana hasa wakati huu wa mvua na sasa hivi nauli ya kutoka Manyovu - Kasulu imefikia mpaka shilingi 10,000; na tunayo barabara nyingi ya lami ya kutoka Kigoma mpaka Manyovu yenye urefu wa kilometa 60 ambayo nauli yake ni shilingi 3,000. Kwa hiyo, umuhimu wa kujenga barabara hii na kuianza mapema inajionyesha kwa vigezo hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kujua, Wizara imekiri kwamba inafanya upembuzi yakifu, wananchi wa Buhigwe wanataka kujua upembuzi yakinifu unaisha lini na ujenzi unaanza lini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Rais alipokuwa akijinadi tuliita vijiji vya Mlela, Buhigwe, Kavomo, Nyankoloko, Bwelanka na akaahidi kwamba atajenga barabara ya kilometa tano katika Wilaya ya Buhigwe, je, ni lini ahadi hiyo itatimizwa?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kumpongeza sana Mheshimiwa Ntabaliba kwa kazi kubwa anayoifanya ya kufuatilia miradi mbalimbali ya Miundombinu katika Wilaya yake na Jimbo lake, nikupongeze sana. Mimi ninakuhakikishia kama ambavyo tumekuwa tukiwahikishia katika ofisi zetu mimi na Waziri wangu, kwamba tutashirikiana na wewe kuhakikisha mambo yote ambayo tuliyaahidi katika Wilaya yako yanatekelezwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika jibu la msingi, ujenzi utaanza baada ya kukamilika upembuzi na usanifu wa kina, kwa maana unaofanywa na kufuatiliwa na wenzetu wa AfDB. Nikuombe tu kwa kuwa anayefanya si Serikali, kazi hii inafanya na AfDB chini ya Afrika Mashariki suala la lini ni gumu kukueleza isije ikaonekana tunasema uongo hapa Bungeni. Nikuhakikishie suala hili litakamilika katika kipindi kifupi kijacho na baada ya hapo shughuli za ujenzi zitaanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali lake la pili, nimuhakikishie, kama ambavyo tulimuhakikishia ofisini, kwamba kilometa zake tano ambazo Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano aliahidi zitatekelezwa mara baada ya masuala haya ya miradi ambayo ni kiporo yatakapokamilika; na uzuri wake sehemu kubwa za viporo zinakamilika mwaka huu ujao wa fedha baada ya hapo tutakamilisha ahadi zingine zote ambazo Mheshimiwa Rais aliziahidi hasa za kilometa tano, kilometa sita katika sehemu mbalimbali za Miji ya Tanzania hii.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami baraba Mnanila – Manyovu – Kasulu ili kuwasaidia wananchi wa maeneo hayo?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Wananchi wa Jimbo la Geita Vijijini hususan Jimbo la Geita Vijijini ndilo Jimbo pekee linaloongoza kwa kupata chakula kingi kila mwaka kwenye Kanda ya Ziwa; wamekuwa na kilio cha barabara yao kutoka Senga - Sungusila - Lubanga mpaka Iseni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge watatu walionitangulia wote wamekuwa wakiomba Serikali barabara hii ichukuliwe angalau tu kwa kiwango changalawe sio lami na Serikali imekuwa ikitoa ahadi kila siku tunafanya tunafanya, na mipango yote sisi kwenye RCC tumeshabariki. Sasa nataka kujua Waziri ni lini barabara hii unaichukua na kuiweka kwenye angalau kiwango cha molami tu?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru sana Mheshimiwa Musukuma kwanza kwa kutukumbusha kuhusu barabara hii. Aliiongelea muda mrefu, kuanzia miaka ya nyuma na sasa tunamuhakikishi kwamba hii barabara itachukuliwa na TANROADS, kwa maana ya kukasimiwa. Barabara hii haijakidhi vigezo vya kupandishwa hadhi, lakini Waziri ameshakubali na ameshaikasimu barabara hii ili iweze kutekelezwa na TANROADS Mkoa wa Geita.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami baraba Mnanila – Manyovu – Kasulu ili kuwasaidia wananchi wa maeneo hayo?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa sera ya masuala ya ujenzi ni kuunganisha barabara ya mkoa mmoja na mwingine kwa kiwango cha lami, na kumekuwa na ahadi ya muda mrefu ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Njiapanda - Karatu - Mang’ola mpaka Lalago, ambayo inaunganisha Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Simiyu, je, ni lini barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Paresso asubiri, ni keshokutwa tu bajeti yetu inakuja, na ramani yote ya shughuli za ujenzi wa barabara zote itakuwa imeanikwa wazi. Nisinge penda kwenda kwa undani kwa sababu ni sehemu ambayo Waziri wangu ataishughulikia keshokutwa.