Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTATINE J. KANYASU (K.n.y JOHN P. KADUTU) Aliuliza:- Kampuni binafsi ya migodi zimekuwa zikikiuka mikataba ya kazi na pia zikikandamiza na kuwanyanyasa wafanyakazi:- (a) Je, ni lini Serikali itafanya ukaguzi wa mikataba kwa kampuni zinazofamya kazi migodini? (b) Je, kwa nini Serikali isiamue kuwaondoa nchini waajiri wakorofi kwa unyanyasaji wanaoufanya?

Supplementary Question 1

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa pamekuwepo na unyanyasaji mkubwa sana wa wafanyakazi katika migodi, ikiwepo tabia ya ku-blacklist wafanyakazi na mfanyakazi anapokuwa blacklisted hawezi kuajiriwa sehemu yoyote katika mgodi, mara nyingi wanapokuwa blacklisted hawapewi nafasi ya kusikilizwa. Napenda kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri ni kwa kiwango gani vyama vya vya wafanyakazi vina uwezo wa kuwatetea wafanyakazi linapoteka tukio kama hili? (Makofi)
Swali langu la pili, migodi mingi imekuwa ikiwashirikisha wananchi wanaozunguka migodi kwa ajili ya ulinzi lakini wananchi hao wamekuwa wakipwewa mikataba ya mwaka mmoja na miezi sita, hawana bima na hawana mikataba ya aina yoyote, hili linafanyika ili kukwepa sheria ya kuwalipia NSSF na faida zao zingine. Je, ni lini migodi hii itaelekezwa kuhakikisha kwamba wananchi hawa wanapewa mikataba na wanalipwa haki zao kama wafanyakazi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANA NA AJIRA): Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la kwanza la unyanyashaji na blacklisting ambayo imekuwa ikifanyika, kama Wizara tumeshapata malalamiko hayo kutoka kwa wafanyakazi wengi walioko katika migodi, ambao wamekuwa wakilalamika kwamba waajiri wengi katika migodi hii hasa baada ya kuwa wafanyakazi hawa wametoka katika maeneo yao, wamekuwa wakiwa- blacklist ili wasipate nafasi yakuweza kuajiriwa katika migodi mingine na makampuni zingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tumeshachukua hatua na tayari katika ukaguzi wetu huu ambao tumeufanya katika migodi yote, moja kati ya taarifa ambayo tunaisubiri ambayo itafanyiwa utekelezaji ni pamoja na jambo hilo na Serikali itatoa maelekezo kwa waajiri wote kwamba wanachokifanya ni kinyume na utaratibu wa sheria za nchi na hairuhusiwi kwa mwajiri yeyote kum-blacklist mfanyakazi. Kwa hiyo, tutaendelea kuwachukulia hatua kwa wale wote watakaoendelea kufanya jambo hili, ambalo linawaondolea haki ya kimsingi kabisa wafanyakazi wa Kitanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili kuhusu mikataba, kwa mujibu wa Sheria Na. 6 ya mwaka 2004 imeanisha vema katika Kifungu Na. 14 aina ya mikataba ambayo mwajiri anapaswa kumpatia mfanyakazi. Kama Mwajiri anakiuka katika eneo hilo, anashindwa kutoa mikataba kwa mujibu wa sheria inavyosema, Mheshimiwa Mbunge nikuhakikishie kwamba kwa sababu umeleta lalamiko hili rasmi tutalifanyia kazi na tutachukua dhidi ya wale waajiri wote ambao wanashindwa kukidhi matakwa ya Kifungu Na. 14 cha Sheria za Kazi.

Name

Joyce John Mukya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONSTATINE J. KANYASU (K.n.y JOHN P. KADUTU) Aliuliza:- Kampuni binafsi ya migodi zimekuwa zikikiuka mikataba ya kazi na pia zikikandamiza na kuwanyanyasa wafanyakazi:- (a) Je, ni lini Serikali itafanya ukaguzi wa mikataba kwa kampuni zinazofamya kazi migodini? (b) Je, kwa nini Serikali isiamue kuwaondoa nchini waajiri wakorofi kwa unyanyasaji wanaoufanya?

Supplementary Question 2

MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kumekuwa na tabia mbaya na chafu ya udhalilishaji wa hawa waajiri wa madini ya kuwapekua wafanyakazi sehemu za siri. Hii imefanyika katika Kampuni ya Tanzanite one kule wanapovuna madini ya Tanzanite, wanawapekua sehemu za siri hasa sehemu za kujisaidia haja kubwa. Je, hakuna njia mbadala ya kufanya zoezi hilo zaidi ya kuwadhalilisha hawa wafanyakazi.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI,VIJANA NA AJIRA): Mheshimiwa Naibu Spika, anachokisema Mheshimiwa Mbunge, mimi mwenyewe nilikwenda pale Tanzanite one katika mgodi huo, nilikutana na changamoto hiyo kubwa ambayo wafanyakazi waliieleza mbele yangu.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati wa ziara ile nilitoa maelekezo na taratibu zote za namna ya ukaguzi unavyopaswa kufanyika ili usidhalilishe utu wa wafanyakazi ambao wanafanya kazi katika migodi hiyo. Maelekezo yalitolewa ya kwamba zipo taratibu za kufuata katika ukaguzi lakini siyo za kumdhalilisha mtu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimuondoe hofu tu Mheshimiwa Mbunge kwamba maelekezo tayari yapo, kama vitendo hivi vinaendelea basi niwaombe wafanyakazi wale waripoti tuchukue hatua stahiki zaidi.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONSTATINE J. KANYASU (K.n.y JOHN P. KADUTU) Aliuliza:- Kampuni binafsi ya migodi zimekuwa zikikiuka mikataba ya kazi na pia zikikandamiza na kuwanyanyasa wafanyakazi:- (a) Je, ni lini Serikali itafanya ukaguzi wa mikataba kwa kampuni zinazofamya kazi migodini? (b) Je, kwa nini Serikali isiamue kuwaondoa nchini waajiri wakorofi kwa unyanyasaji wanaoufanya?

Supplementary Question 3

MHE. RITA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo tu la nyongeza. Kwa kuwa huu udhalilishaji ambao umekuwa ukifanyika na hao wawekezaji siyo katika migodi tu, upo hata katika viwanda vyetu. Nimeshuhudia mara nyingi sana Mheshimiwa Naibu Waziri akienda kusuluhisha migogoro hasa ikihusiana na unyanyasaji wa wafanyakazi. Je, ni adhabu gani kubwa kabisa ambao wamekuwa wakipatiwa hawa waajiri au wawekezaji ambao wamekuwa wakiwanyanyasa hawa wafanyakazi. Kwa sababu nimeona jambo hili limekuwa likijirudia mara kwa mara.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI,VIJANA NA AJIRA): Mheshimiwa Naibu Spika, kila mwekezaji anayekuja kuwekeza hapa nchini hasa wale ambao wanapitia TIC na wale ambao wamejisajili katika Vyama vya Waajiri. Wamekuwa wakipewa sheria za nchi hii na utaratibu ambao unapaswa kufuatwa na jambo lolote linalojitokeza kinyume chake hapo sisi kama Serikali tumeendelea kuchukua hatua stahiki.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuna changamoto kubwa sana kwa wawekezaji raia wa China ambao wengi wamekuwa wakiingia nchini na taratibu za kisheria zimekuwa hazifuatwi, lakini wale ambao wamesajiliwa wako chini ya ATE. ATE wamefanya kazi kubwa ya tafsiri sheria za kazi za nchi yetu kwenda katika lugha ya Kichina. Maana mwanzoni wao walikuwa wanatumia excuse ya kutofahamu sheria, ingawa katika principle zile za sheria katika ile maxim inayosema ignorantia juris non excusat, ambayo inasema muhimu kabisa kwamba hakuna excuse kwa mtu ambaye hafahamu sheria. Kwa hiyo walichokifanya hawa waajiri wametafsiri sheria zile, lakini bado kuna watu ambao wanakiuka taratibu hizi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe tamko tu mbele ya Bunge hili kwamba wale waajiri wote hasa wawekezaji ambao wanafahamu sheria za nchi zetu, wanapaswa kufuata utaratibu ambao wanaendelea na unyanyasaji, tutaendelea kuwachukulia hatua stahiki ili kuhakikisha kwamba, tunaondoa dhana hii ya udhalilishaji na unyanyasaji wa wafanyakazi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia adhabu kubwa ambayo tumekuwa tukiichukua ni kwamba, tumekuwa tukiwandoa nchini mara moja wale wote ambao tunawabaini ni wageni wanawadhalilisha Watanzania katika nchi yetu ili tutengeneze kitu kinaitwa deterrence, mtu mwingine yeyote asiweze kurudia kosa hilo.