Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. DAVID E. SILINDE (K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE) aliuliza:- Barabara ya Masasi – Nachingwea imekuwa na matatizo kwa muda mrefu ya kupitika kwa shida:- Je, barabara hiyo itajengwa lini kwa kiwango cha lami ili kufanya wananchi wa Jimbo la Ndanda waondoe imani kuwa wametengwa?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kuuliza maswali madogo ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutoka Masasi mpaka Nachingwea ni kama kilometa 42 na kutoka Masasi mpaka Ndanda ni kama kilometa 40; na kwenye bajeti iliyokuwa imeitengwa ambayo imeombwa mwaka 2017/2018 kama shilingi bilioni tatu, ni fedha ndogo ambayo haiwezi kukidhi kumaliza barabara hiyo. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kukamilisha barabara hiyo kwa kiwango cha lami kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge alikuwa ameomba, kwa sababu fedha iliyotengwa ni ndogo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali dogo la pili la nyongeza ni kwamba, matatizo ya Jimbo la Ndanda yanafanana kabisa na Jimbo la Momba kule; sasa naomba niulize kwamba barabara ya kutoka Kakozi kwenda Kapele mpaka Namchinka kilometa 50.1 imepandishwa hadhi na Wizara yako, lakini mpaka sasa haijawahi kuhudumiwa na hiyo barabara ni mbovu. Ni kwa nini barabara hizi mnazipandisha hadhi na hamzihudumii kwa wakati? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu udogo wa fedha, kitu ninachojaribu kumweleza ni kwamba katika ule mpangilio wa kutekeleza ahadi sasa tumefikia kuanza utekelezaji wa ahadi ya barabara hii na tumeanzia na hizi fedha ndogo kutokana na bajeti tuliyopata mwaka unaokuja wa 2017/2018. Nimhakikishie, katika miaka yote inayofuata, barabara hii itakuwa inaendelea kupewa fedha za kutosha ili hatimaye katika kipindi chetu tulichoahidi, barabara hii itakuwa imekamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu barabara ya Kakozi – Kapele na kuendelea ambayo imechukuliwa na TANROAD, nimhakikishie tu kwamba tutahakikisha TANROAD inapanga fedha za kutosha kwa ajili ya utekelezaji wa barabara hii kama ilivyokusudiwa kwa kupandishwa hadhi.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. DAVID E. SILINDE (K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE) aliuliza:- Barabara ya Masasi – Nachingwea imekuwa na matatizo kwa muda mrefu ya kupitika kwa shida:- Je, barabara hiyo itajengwa lini kwa kiwango cha lami ili kufanya wananchi wa Jimbo la Ndanda waondoe imani kuwa wametengwa?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba barabara ya Sikonge – Mibono – Kipili ilipandishwa hadhi tangu mwaka 2009 na hadi leo imetobolewa kwa kiwango cha kilometa 42 tu kati ya 282 ambayo ni kama kilometa tano kwa mwaka; ina maana kwamba hadi itakapokamilika barabara hiyo tunahitaji miaka 44. Je, Serikali iko tayari kuwaambia wananchi wa Sikonge kwamba itajenga barabara hiyo kwa kipindi cha miaka 44 ijayo? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utaratibu wa fedha za Mfuko wa Barabara zinazogawiwa mikoani kwa ajili ya matengenezo, haturuhusiwi kutumia fedha nyingi sana kwa ajili ya kutoboa barabara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ombi lake tunalichukua na tutatafuta namna ya kuhakikisha barabara hii kipande hiki kipya cha kukitoboa tunakitoboa kwa haraka zaidi na naomba wananchi wote wa Sikonge wachukue hiyo ndiyo kama commitment ya Serikali.

Name

Risala Said Kabongo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAVID E. SILINDE (K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE) aliuliza:- Barabara ya Masasi – Nachingwea imekuwa na matatizo kwa muda mrefu ya kupitika kwa shida:- Je, barabara hiyo itajengwa lini kwa kiwango cha lami ili kufanya wananchi wa Jimbo la Ndanda waondoe imani kuwa wametengwa?

Supplementary Question 3

MHE. RISALA S. KABONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Barabara ya kutoka Mlowo - Mbozi kwenda Kamsamba - Momba haipitiki wakati wa mvua, je, ni lini Serikali itatengeneza barabara hii kwa kiwango cha lami ili kuweza kusaidia uchumi wa wananchi wa Mkoa wa Songwe na Mkoa wa Katavi?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, yale ambayo tumeshayasema kabla ni ya kweli na tutayatekeleza. Tulichokiahidi, kitu cha kwanza ni kukamilisha daraja, tukishamaliza kukamilisha daraja tutashughulikia hii barabara katika kiwango cha lami. Tupeni fursa, hizo pesa ambazo tumezitenga kwa ajili ya daraja kwanza tukamilishe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina uhakika, maadam tunatenga fedha za utengenezaji wa hii barabara kuhakikisha inapitika karibu muda wote, naomba tupeni fursa tutekeleze kwa namna tulivyopanga.