Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Barabara ya kutoka Mgakorongo, Kigarama mpaka Murongo iliwekwa kwenye ilani kuwa itajengwa kwa kiwango cha lami na wananchi waliokuwa ndani ya mradi waliowekewa alama ya ‘X’ wanashindwa kuendeleza maeneo yao wakisubiri fidia zaidi ya miaka mitano sasa:- (a) Je, ni lini wananchi hawa watapewa fidia ili waendelee na mambo ya kimaendeleo? (b) Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kweli nasikitika sana kuona majibu ambayo ametoa Mheshimiwa Waziri. Hii ni mara yangu ya pili namwuliza hili swali. Mara ya kwanza alinijibu hapahapa Bungeni, akasema kabla ya mwezi wa Sita barabara hii itakuwa imeanza ujenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri, anapotujibu siyo kuwajibu Wabunge kuwafurahisha, haya ni majibu ambayo tunakuja kuuliza kwa ajili ya wananchi wetu. Naomba Mheshimiwa Waziri atupe majibu ambayo ni ya uhakika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza; ni lini barabara hii ujenzi utaanza? Kwa sababu hii barabara ni ya muda mrefu tangu kipindi cha Mheshimiwa Rais Mkapa amestaafu; amekuja Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, sasa anakuja Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwenye bajeti ya mwaka 2017/2018, je, imetengwa pesa kwa ajili ya ujenzi huu kuanza na wananchi wapewe fidia?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimhakikishie, tunapojibu hapa kwanza tunaonesha dhamira lakini pili, tunaonesha mipango ambayo ipo mbioni. Hatuwezi kuanza ujenzi wa barabara hii kabla ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kukamilika. Hakuna aina hiyo ya ujenzi ya barabara kuu na muhimu kama hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Mbunge atupe fursa tukamilishe upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kwa mwaka huu tunakamilisha kazi hizo mbili. Kwa hiyo, hatujatenga fedha za kuweza kujenga, tumetenga fedha kwa ajili ya kukamilisha kazi hizo mbili. Nimhakikishie kwamba mara baada ya kazi hizo mbili kukamilika, ujenzi utaanza, Serikali hii ya Awamu ya Tano inachosema inakusudia kukitekeleza na huwa inakitekeleza.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Barabara ya kutoka Mgakorongo, Kigarama mpaka Murongo iliwekwa kwenye ilani kuwa itajengwa kwa kiwango cha lami na wananchi waliokuwa ndani ya mradi waliowekewa alama ya ‘X’ wanashindwa kuendeleza maeneo yao wakisubiri fidia zaidi ya miaka mitano sasa:- (a) Je, ni lini wananchi hawa watapewa fidia ili waendelee na mambo ya kimaendeleo? (b) Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Dar es Salaam – Isaka – Rusumo, inayojulikana kama central corridor ni barabara inayohudumia nchi takriban nne ambazo zipo kwenye Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, lakini kipo kipande cha kilometa 150 kutoka Lusahunga kutoka Rusumo; Nyakasanza kwenda Kobelo mpaka Bujumbura. Kipande hiki kimekuwa ni kero kwa muda mrefu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana ambao ndiyo
huu tunamalizia 2016/2017 barabara hii ilitengewa shilingi bilioni tano, lakini mpaka sasa hivi ukarabati unaofanyika ni mdogo na kwa bajeti hii ya 2017/2018 tumetengewa shilingi bilioni 1.19 tu kiasi kwamba haiwezi kufanya ukarabati unaoridhisha. Je, ni lini Serikali sasa itaweza kutenga fedha za kutosha ili kukarabati kipande hiki ambacho ni kero kwa Watanzania wanaotumia barabara hii na wageni wanaotoka kwenye nchi za Burudi na Rwanda, Kongo na Uganda ili barabara hii iweze kukidhi viwango na kukidhi mahitaji?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Gashaza kwa sababu anapita hii barabara, anafahamu kazi kubwa inayofanywa kuirekebisha hiyo barabara kuanzia Isaka na kuendelea. Tunakwenda kwa hatua; mimi mwenyewe nimeona ukarabati ulioanzia Rusahunga kuelekea Rusumo. Nimeiona, nimepita hiyo barabara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Mbunge, aridhike na hiki kinachofanyika na kwa vyovyote vile, baada ya kukamilisha hii, tutakwenda kukamilisha kipande kilichobakia. Suala siyo rahisi kupata fedha zote za kutosha kuikamilisha barabara yote kwa wakati mmoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaendelea kuikarabati barabara hii mpaka ikamilike. Tutafika Rusumo, tutafika hii njia inayokwenda Burundi.

Name

Savelina Slivanus Mwijage

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:- Barabara ya kutoka Mgakorongo, Kigarama mpaka Murongo iliwekwa kwenye ilani kuwa itajengwa kwa kiwango cha lami na wananchi waliokuwa ndani ya mradi waliowekewa alama ya ‘X’ wanashindwa kuendeleza maeneo yao wakisubiri fidia zaidi ya miaka mitano sasa:- (a) Je, ni lini wananchi hawa watapewa fidia ili waendelee na mambo ya kimaendeleo? (b) Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza?

Supplementary Question 3

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa ahadi za barabara ya Karagwe kwenda mpaka Benako kutoka Nyakaanga zimekuwa kero kwa muda mrefu; nimeingia Bungeni mwaka 2005 barabara ya kwenda mpaka Mlongwe nimeiongea barabara ya kutoka Nyakaanga kwenda Benako nimeiongea:-
Ni lini Serikali itachagua moja; kutengeneza upande
na mmoja kuumaliza na kuingia wa pili? Mnatafuta ma-engineer na Wakandarasi ambao hawana viwango. Barabara unatengeneza siku mbili, tatu, barabara inaharibika. Lini mtatafuta ma-engineer wa uhakika wa kutengeneza barabara zikawa za viwango?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemsikia Mheshimiwa Mbunge kwa makini anachokiongelea. Huwa naamini kwamba tunachagua Wakandarasi makini, ila kwa kauli yake inaonekana tunatakiwa tuongeze nguvu zaidi na macho yaangalie zaidi ili kuhakikisha kweli tunapata Wakandarasi wanaoweza kusaidia kufanya kazi bila kurudia rudia mara nyingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa ushauri wake.