Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Ritta Enespher Kabati
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. RITTA E. KABATI (K.n.y. MHE. MAHMOUD H. MGIMWA) aliuliza:- Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa Waziri wa Miundombinu aliahidi kupandisha hadhi barabara ya kutoka Mtiri – Ifwagi – Mdaburo, Ihanu, Isipi –Mpangatazara – Mpalla Mlimba ambayo inaunganisha Wilaya ya Mufindi na Wilaya ya Kilombero pia Mkoa wa Iringa na Morogoro. Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi barabara hiyo muhimu kwa uchumi wa Wilaya ya Mufindi na Taifa kwa ujumla ambayo Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imeshindwa kuihudumia wakati wote?
Supplementary Question 1
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali tu madogo ya nyongeza. Kwa kuwa tumekuwa tukikaa katika vikao vya Bodi za Barabara mara nyingi sana hasa katika Mkoa wetu wa Iringa, barabara nyingi sana za Halmashauri zetu tunakuwa tukipeleka lakini hazipandishwi daraja. Je, ni vigezo gani sasa vinatumika maana utakuta sehemu nyingine barabara zinapandishwa lakini sehemu nyingine barabara nyingi hazipandishwi madaraja?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza pesa kwenye Halmashauri kwa sababu Halmashauri nyingi barabara zake ni mbovu sana ili Halmashauri hizi ziweze kutengeneza barabara zake kwa kiwango?
Name
Eng. Edwin Amandus Ngonyani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, vigezo vya kupandisha hadhi barabara vimeainishwa katika Sheria ya Barabara pamoja na Kanuni zake kama ambavyo nilisema katika jibu langu la swali la msingi. Vigezo hivyo havijabadilika na kama tutataka kubadilisha tutakuja Bungeni kuvibadilisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuongeza fedha; fedha nazo tumekubaliana kwamba Mfuko wa Barabara unagawa asilimia thelathini zinaenda kwenye Halmashauri na asilimia 70 zinaenda kuhudumia barabara za trunk road za mikoa. Sasa kama tunadhani kwamba formular hii kwa sasa labda haitufai bado ni suala la kuamua sisi Waheshimiwa Wabunge ndani ya Bunge hili Tukufu ili tuweze kubadilisha zile sheria ambazo tulikubaliana wenyewe.
Name
Elias John Kwandikwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Primary Question
MHE. RITTA E. KABATI (K.n.y. MHE. MAHMOUD H. MGIMWA) aliuliza:- Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa Waziri wa Miundombinu aliahidi kupandisha hadhi barabara ya kutoka Mtiri – Ifwagi – Mdaburo, Ihanu, Isipi –Mpangatazara – Mpalla Mlimba ambayo inaunganisha Wilaya ya Mufindi na Wilaya ya Kilombero pia Mkoa wa Iringa na Morogoro. Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi barabara hiyo muhimu kwa uchumi wa Wilaya ya Mufindi na Taifa kwa ujumla ambayo Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imeshindwa kuihudumia wakati wote?
Supplementary Question 2
MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona ili nami niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa hitaji la Mufindi Kaskazini linafanana na Ushetu na kwa kuwa Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliahidi kupandisha hadhi barabara hii inayounganisha mikoa mitatu; Mkoa wa Geita, Shinyanga na Tabora kwa kupitia maeneo ya Mbogwe, Mwabomba, Nyankende, Ubagwe, Uloa hadi Kaliua. Je, Serikali itaipandisha hadhi lini barabara hii? (Makofi)
Name
Eng. Edwin Amandus Ngonyani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hizo ni barabara tatu tofauti lakini zinazoungana na kwa hiyo nadhani tufuate tu utaratibu. Kwa hapa itabidi mikoa yote mitatu kwa vipande vyake ifuate taratibu za kuomba kupandisha hadhi hizo barabara. Kama tayari zimefuata taratibu hizo basi nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba maombi yake yatashughulikiwa kama ambavyo tumeongelea kwa barabara ambayo inaanzia Mtili – Ifwagi – Mdaburo na kuendelea. Utaratibu huo tutaufuata na maombi hayo tutayapitia kwa pamoja na zile zitakazotangazwa tutakuja kuwajulisha rasmi baada ya kutokea kwenye Gazeti la Serikali.
Name
Eng. James Fransis Mbatia
Sex
Male
Party
NCCR-Mageuzi
Constituent
Vunjo
Primary Question
MHE. RITTA E. KABATI (K.n.y. MHE. MAHMOUD H. MGIMWA) aliuliza:- Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa Waziri wa Miundombinu aliahidi kupandisha hadhi barabara ya kutoka Mtiri – Ifwagi – Mdaburo, Ihanu, Isipi –Mpangatazara – Mpalla Mlimba ambayo inaunganisha Wilaya ya Mufindi na Wilaya ya Kilombero pia Mkoa wa Iringa na Morogoro. Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi barabara hiyo muhimu kwa uchumi wa Wilaya ya Mufindi na Taifa kwa ujumla ambayo Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imeshindwa kuihudumia wakati wote?
Supplementary Question 3
MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa swali la msingi linaulizia ahadi ya Serikali na Mheshimiwa Dkt. Magufuli alivyokuwa Waziri wa Ujenzi aliahidi kukamilisha barabara ya Kawawa – Nduoni –Bakula – Marangu Mtoni ambayo ni barabara muhimu sana kwa ajili ya utalii, inajulikana kama utalii road. Alipokuwa anafanya kampeni wakati wa uchaguzi aliahidi pia kwamba itakamilika na imeshajengwa nusu tu kwa lami. Sasa ni lini Serikali itakamilisha barabara hii kwa maendeleo ya utalii na Serikali iweze kupata mapato. (Makofi)
Name
Eng. Edwin Amandus Ngonyani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Waziri kivuli wa Wizara hii nadhani anafahamu na tumejadili, ingawa katika kipindi kifupi kidogo hakuwepo lakini nadhani anafahamu kwamba tumekuwa tukijadili utekelezaji wa ujenzi wa barabara mbalimbali na tumesema kwamba kwanza tuzikazanie zile ambazo zina madeni ili tuondokane na madeni na baada ya hapo tutaendelea na hizi zingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hizi zingine kipaumbele cha uhamasishaji wa utalii nacho tulikiweka. Kwa hiyo, nimshukuru alitusaidia kuweka hiki kipaumbele na hivyo mara tutakapomaliza barabara hizi ambazo zina mikataba ya muda mrefu zitafuata hizi barabara zinazohamasisha utalii na vile vile zinazohamasisha viwanda.
Name
Venance Methusalah Mwamoto
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kilolo
Primary Question
MHE. RITTA E. KABATI (K.n.y. MHE. MAHMOUD H. MGIMWA) aliuliza:- Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa Waziri wa Miundombinu aliahidi kupandisha hadhi barabara ya kutoka Mtiri – Ifwagi – Mdaburo, Ihanu, Isipi –Mpangatazara – Mpalla Mlimba ambayo inaunganisha Wilaya ya Mufindi na Wilaya ya Kilombero pia Mkoa wa Iringa na Morogoro. Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi barabara hiyo muhimu kwa uchumi wa Wilaya ya Mufindi na Taifa kwa ujumla ambayo Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imeshindwa kuihudumia wakati wote?
Supplementary Question 4
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nami niulize swali dogo tu la nyongeza. Kwa kuwa tatizo ambalo lipo kule Mufindi linafanana kabisa na kule Kilolo; barabara nyingi za Kilolo zimekuwa zikiahidiwa na hasa na Mheshimiwa Waziri. Sasa je, ni hatua gani ambazo inapaswa tuchukue endapo Mheshimiwa Waziri ameahidi kwa upande wa Serikali lakini utekelezaji haujafanyika?
Name
Eng. Edwin Amandus Ngonyani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi ni dhamira, kwa hiyo tunapotoa ahadi tunaonesha dhamira ya kutaka kutekeleza hicho kitu. Hatua inayofuata baada ya kuwa na hiyo dhamira ni kutafuta fedha na mara fedha zitakapopatikana hii ahadi yetu tutaitekeleza.