Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMARI KHAMIS aliuliza (a) Je, Serikali imejipanga vipi kuzuia uvuvi haramu nchini? (b) Je, ni meli ngapi zilizokamatwa kwa sababu za uvuvi haramu kuanzia mwaka 2010 – 2015? (c) Je, ni watu wangapi wametiwa hatiani na hukumu zao zikoje?

Supplementary Question 1

MHE. FAKHARIA SHOMARI KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake marefu lakini yametoa elimu kwa Watanzania. Naomba kuuliza maswali mawili madogo.
Kwa kuwa katika kupambana na uvuvi haramu baharini na katika maziwa yetu, jambo linaloonekana ni kwa mvuvi anaevua uvuvi wa haramu kwa sababu anapatikana na nyavu zenye macho madogo; na yeye ndiye hutiwa hatiani. Kuna usemi unaosema mkamatwa na ngozi ndiye mwizi. Sasa swali, je, Serikali inasemaje kwa wale wenye viwanda vya kutengeneza nyavu, wanaoleta, wanaouza, ambao wao ndio source kubwa ya kutufanyia huu uvuvi haramu kutokana na vifaa wanavyovileta, kuliko huyu mvuvi ambaye ameuziwa akaenda akaifanya hii kazi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Wizara italeta lini Bungeni Sheria ambayo itaweza kuwadhibiti hawa waletaji, wenye viwanda pamoja na wauzaji ili tuweze kuwadhibiti kisheria pamoja na hawa wanaozitumia nyavu hizi? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, niruhusu nitambue kweli jitihada za Mheshimiwa Mbunge za kufuatilia masuala ya uvuvi. Si mara ya kwanza yeye kuuliza maswali katika Bunge hili, lakini amekuwa akiwasiliana na Wizara kuonesha concern yake kuhusiana na masuala mbalimbali ya uvuvi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kuhusu kwamba ni kwa nini wavuvi tu wanaokamatwa na nyavu ndio wanachukuliwa hatua za kisheria. Nimfahamishe tu Mheshimiwa Mbunge, kwamba kwa sababu kutumia nyavu ambazo haziruhusiwi kisheria ni kosa la kisheria, yoyote yule atakayehusika kwa namna moja au nyingine katika utengenezaji, uuzaji, usafirishaji, utumiaji wa nyavu hizo anakuwa amekiuka sheria vile vile, kwa hiyo hakuna ambaye ataachwa.
Mheshimwia Mwenyekiti, kwa hiyo, kama kuna kiwanda ambacho kinatengeneza nyavu ambazo haziruhusiwi, kama kuna mfanyabiashara atafanya, kama kuna dalali, mtu yoyote atakayejihusisha kwa namna moja au nyingine sheria itachukua mkondo wake. Ni kweli kabisa si wavuvi tu ndio wanakamatwa lakini tayari tumeshakamata bidhaa za kutengenezea nyavu kama hizo, lakini vile vile hata wafanyabiashara ambao wanahusika wameshachukuliwa hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na swali lake la
pili kwamba lini tutabadilisha sheria yetu ya uvuvi ya mwaka 2003 ili sasa kushughulikia kwa utaratibu zaidi makosa mbalimbali yanayopelekea watu kujihusisha na uvuvi haramu. Nimfahamishe tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari Wizara inafanya utaratibu wa kupitia sheria ile; lakini si sheria ile tu, tunaanza kufikiria sasa kama nchi kwamba suala la uvuvi haramu ni zaidi tu ya uvuvi, inahusisha vile vile mambo ya ugaidi, lakini vile vile inahusisha uhujumu uchumi. Kwa hiyo ikiwezekana sheria nyingi zitarekebishwa ili hili suala tuweze kulishughulikia kwa mapana zaidi na kwa ufanisi zaidi.

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMARI KHAMIS aliuliza (a) Je, Serikali imejipanga vipi kuzuia uvuvi haramu nchini? (b) Je, ni meli ngapi zilizokamatwa kwa sababu za uvuvi haramu kuanzia mwaka 2010 – 2015? (c) Je, ni watu wangapi wametiwa hatiani na hukumu zao zikoje?

Supplementary Question 2

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kumuuliza swali moja Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwa kuwa Taasisi ya Hifadhi ya Bahari Mafia, imeshindwa kazi yake ya msingi ya kuzuia uvuvi haramu na uhifadhi na hivi sasa inauza visiwa na maeneo Wilaya Mafia. Je, Sasa Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kuondoa uongozi wa juu pale na kubadilisha kuleta uongozi mwingine?Ahsante.

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, jana tulielezea kwamba hakuna visiwa ambavyo vimeuzwa Mafia isipokuwa sheria tu zimefuatwa kukodisha Kisiwa cha Shungimbili kwa miaka 20 kwa Mwekezaji wa Hoteli. Vile vile kama kuna ushahidi wowote ule ambao utaonesha kwamba, maafisa anaowazungumzia wameshindwa kufanya kazi yao au wamejihusisha na vitendo ambavyo ni kinyume na sheria, lakini vile vile na maadili ya kazi yao, naomba Mheshimiwa Mbunge atuletee na sisi bila kusita tutachukua hatua.