Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- Katika msimu wa kilimo wa mwaka 2015/2016 Mawakala wa Usambazaji Pembejeo kwa Vocha katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga wanaidai Serikali jumla ya Sh.824, 000,000/= Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa deni hilo?

Supplementary Question 1

MHE. MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Kwa vile madeni haya yamechukua muda mrefu; je Serikali iko tayari kufikiria kulipa pamoja na riba kwa Mawakala hao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kumekuwepo
na tatizo la pembejeo ambazo hazina ubora; je, Serikali ina mpango gani kuimarisha ukaguzi wa maduka ya pembejeo za kilimo ili kuhakikisha wananchi hawa wanapata pembejeo zenye ubora stahiki? Ahsante sana. (Makofi)

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na madeni ulipwaji wake kucheleweshwa na hivyo kustahili kulipwa riba; nimweleze tu Mheshimiwa Mbunge kwamba ucheleweshwaji wa ulipwaji umetokana vilevile na kasoro ambazo hata Mawakala wenyewe wanahusika katika kasoro hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuliambia Bunge lako Tukufu kwamba suala la pembejeo limekuwa ni moja kati ya maeneo ambayo kuna wizi mkubwa sana wa fedha za umma. Kwa hiyo, ukiona kwamba kuna ucheleweshaji kidogo ni kwa sababu tunataka tufanye malipo sahihi, hatutakubali tena fedha za umma ziibiwe na wajanja wachache kwa kisingizio kwamba huduma imetolewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wabunge, pamoja na kwamba tunathamini mchango mkubwa sana wa Mawakala wa Pembejeo katika kuendeleza Sekta yetu ya Kilimo, lakini niwaeleze tu kwamba hili ni eneo ambalo Serikali imepoteza fedha nyingi sana. Katika ukaguzi wa awali ambao tumefanya kama Wizara katika mikoa nane ambayo imepata ruzuku kubwa, walikuwa wanadai shilingi bilioni 36. Kati ya hizo ni shilingi bilioni nane tu ambazo zimeonekana zinaweza kulipwa bila utata. Kwa hiyo, unaweza kuona ni kwa kiasi gani tumekuwa tukipoteza fedha nyingi kwa kukimbilia kulipa haraka.
Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wabunge, naombeni wale mnaotoka maeneo ambayo pembejeo ya ruzuku imepelekwa, mtufahamishe upungufu unatokea kule. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Keissy kwa sababu yeye amekuja mbele na kutueleza kuhusu udanganyifu uliofanywa na Mawakala katika Jimbo lake. Vilevile juzi Mheshimiwa Flatei Massay, naye kaeleza upungufu uliotokea Wilayani kwake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaendelea kulipa madeni yale ambayo ni sahihi, lakini kwa bahati mbaya sana kuna Mawakala ambao hawana makosa lakini wanapata matatizo kwa sababu ya makosa ya Mawakala ambao sio waaminifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile lazima niseme udanganyifu huu haukufanyika na Mawakala peke yao, hata Maafisa wa Serikali wamekuwa ni sehemu ya mfumo mbovu ambao umekuwa ukiibia fedha Serikali. Kimsingi tu, katika Serikali ya Awamu ya Tano hili hatutaki litokee na ndiyo maana tumebadilisha mfumo na kwa sasa hatuna tena mfumo wa vocha.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- Katika msimu wa kilimo wa mwaka 2015/2016 Mawakala wa Usambazaji Pembejeo kwa Vocha katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga wanaidai Serikali jumla ya Sh.824, 000,000/= Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa deni hilo?

Supplementary Question 2

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Swali lililoulizwa na Mheshimiwa Martin Mtonda kuhusu madai ya Mawakala wa Pembejeo Mbinga Vijijini linafanana kabisa na tatizo lililopo Wilaya ya Masasi Mkoa wa Mtwara na hasa Jimbo la Ndanda; kwamba katika msimu wa kilimo wa mwaka 2016 wakulima wa korosho na hapa Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri kwamba hasara nyingine huwa zinasababishwa na watumishi wa Serikali wasio waaminifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jambo hili pia limetokea Mtwara kwa wakulima wa korosho baada ya wamiliki wa maghala kwa kushirikiana na Watendaji wa Chama Kikuu cha Ushirika kuwaibia wakulima pesa zao na kesi zinaendelea kwenye Mahakama. Je, Serikali haioni sasa ni wakati wa kutoa pesa zilizopo kwenye Mfuko wa Wakfu na kufidia hasara hii waliyoipata wakulima wakati wao wanaendelea na wale watu waliopo Mahakamani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. (Makofi)

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na uwezekano wa Serikali kulipa fedha ambazo kwa sasa zipo kwenye Mfuko wa Wakfu kwa ajili ya kufidia zile fidia, ingekuwa ni jambo jema, lakini kwa sababu suala lenyewe bado liko Mahakamani, ni vizuri tukasubiri tupate majibu, kwa sababu inawezekana kule Mahakamani, wale ambao tunafikiri wamesababisha hasara ikaja ikatokea uamuzi tofauti. Kimsingi tunataka kila mtu abebe mzigo wake ili kama wale watakuwa wamehusika kulingana na hukumu ya Mahakama, wenyewe watabeba jukumu la kurudisha fedha za wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachofanya sisi kama Serikali ni kuhakikisha kwamba matatizo kama haya hayatokei tena. Ndiyo maana tunavyozungumza, tayari Bodi za Vyama vya Ushirika zaidi ya 200 Mtwara na Lindi zimevunjwa, ni kwa sababu tunajaribu kuwalinda wakulima wasiendelee kuibiwa na watu wachache ambao sio waaminifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile hizo kesi ziko Mahakamani na Afisa yeyote wa Ushirika au wa Serikali ambaye atabainika kuhusika katika upotevu wa fedha za wakulima, naye vilevile atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuboresha ubora, ni swali ambalo liliulizwa awali ambalo linahusiana na hili. Sasa hivi Serikali ina mpango wa kuagiza mbolea kwa mkupuo (bulk procurement) na hii itasaidia sana sisi tuweze kuchagua mbolea ambayo tunahakikisha kwamba inakuwa na ubora. Kampuni yetu inayohusika na ubora wa mbolea itahakikisha kwamba mbolea yote inayoingia ni bora lakini vilevile hata kwa mbegu…

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- Katika msimu wa kilimo wa mwaka 2015/2016 Mawakala wa Usambazaji Pembejeo kwa Vocha katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga wanaidai Serikali jumla ya Sh.824, 000,000/= Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa deni hilo?

Supplementary Question 3

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Mwaka 2016 Mheshimiwa Waziri Mkuu alifanya ziara Mkoani Rukwa na alipata nafasi ya kuonana na Wakala wa Mkoa wa Rukwa. Kama tunavyojua, Mkoa wa Rukwa ni mchangiaji mkubwa sana wa uzalishaji wa chakula hapa nchini. Mpaka sasa hakuna kilichopatikana katika madai haya na Wizara imekuwa ikitoa majibu ya namna hii hii kila siku; haioni kama inadidimiza kilimo katika nchi hii? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mawakala wamekata tamaa na ndiyo walikuwa wanatusaidia mkoani kwetu na sasa chakula kitapungua Mkoa wa Rukwa kwa sababu ahadi ya Waziri Mkuu ambaye aliongea na Mawakala, haijatimizwa kwa sababu ya majibu ya kila siku kama haya.

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba majibu yamekuwa ni kama haya kwa sababu huo ndiyo ukweli, kwamba ni vigumu sana sisi kukimbilia kulipa madeni ambayo tunafahamu kuna wizi ndani yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sasa hivi tunachofanya ni kuhakikisha kwamba tunaondokana na mfumo ambao unarahisisha wizi na ndiyo maana mfumo wa kununua mbolea kwa mkupuo hatutakuwa tena na tatizo la kuanza kuwa na madeni kwa sababu mbolea itakuwa inanunuliwa dukani kama Coca Cola. Kwa hiyo, tunachosema, watuvumilie tu, hatuwezi tukalipa fedha ambazo ni wazi ni za wizi. Tuna ushahidi.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- Katika msimu wa kilimo wa mwaka 2015/2016 Mawakala wa Usambazaji Pembejeo kwa Vocha katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga wanaidai Serikali jumla ya Sh.824, 000,000/= Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa deni hilo?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha kwamba inaondoa migogoro hii ya upatikanaji wa pembejeo za kilimo na kwetu sisi wakulima wa korosho, hapa juzi Serikali imetutangazia kutupatia sulphur kwa maana ya pembejeo ya kilimo bure. Je, Serikali imejipangaje katika usambazaji wa sulphur hii ya bure ili iweze kutufikia kwa wakati na ya kutosha?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakuja kueleza wakati wa hotuba ya bajeti yetu Ijumaa kuhusiana na hatua mbalimbali ambazo tumechukua kuboresha mifumo ya usambazaji wa pembejeo katika mazao mbalimbali ikiwepo zao la korosho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, niseme tu kwamba sulphur itagawiwa kwa utaratibu ambao umewekwa na Bodi ya Korosho. Kimsingi, hatuamini kwamba itawezekana tena sulphur ichelewe, kwa sababu kwa sasa maana yake inakuwa inatolewa bure na yule ambaye anagawa inakuwa ni Bodi. Kwa hiyo, tusubirie tutasikia kuhusu huo utaratibu.