Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Wananchi wa Mbulu Vijijini hawana mawasiliano ya simu wala minara katika Kata za Tumati, Yaeda, Ampa, Gidhim na Gorati:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka minara katika Kata hizo ili kupata mawasiliano?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nataka nimpe taarifa kwamba katika Kata ya Hayderer kuna mnara wa Airtel umeanzishwa, una miaka miwili, haujamalizika kabisa, uko kwenye foundation. Sasa kwa kuwa Kata za Yaeda Ampa na Tumati zinakaribiana. Je, Wizara iko tayari sasa kujenga mnara katikati ya kata hizi ili angalau katika mnara huu uliotangazwa tender, kata hizi mbili zikapata mawasiliano?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kwa kuwa maeneo mengi mitandao haifiki, maeneo ya Endagichan, Endamasak, Enargatag, Runguamono, Munguhai, Gembak na Gidamba. Serikali sasa ituambie, ina mpango gani tena wa kuingiza vijiji hivi na kata hizi ili angalau basi Jimbo langu lipate mawasiliano? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tutafuatilia mnara wa Airtel ambao amesema umekaa kwa muda mrefu katika kiwango cha msingi. Tutafuatilia tuone tatizo ni nini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kuhusu ombi la kujenga katikati ya zile kata mbili; tumelipokea na tutalifuatilia na vilevile vijiji vyote ambavyo amevitaja tumepokea ombi hili, tutaangalia namna ya kuyashughulikia ili hatimaye vijiji hivyo vyote vipate mawasiliano. (Makofi)

Name

Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Wananchi wa Mbulu Vijijini hawana mawasiliano ya simu wala minara katika Kata za Tumati, Yaeda, Ampa, Gidhim na Gorati:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka minara katika Kata hizo ili kupata mawasiliano?

Supplementary Question 2

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kuniruhusu niulize swali la nyongeza. Matatizo ya mawasiliano ya Mbulu Vijijini yanafanana sana na matatizo ambayo yapo kule katika Tarafa ya Amani Jimbo la Muheza hususan kwenye Kata za Misarai, Kwezitu, Mbomole na kwingineko. Sasa Serikali ina mpango gani kupeleka minara kwenye sehemu hizo na Tarafa hiyo ambayo kwa kweli mawasiliano ni tabu sana?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali ni kupeleka mawasiliano ya uhakika katika Tarafa ya Amani tukiunganisha kata zote ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja. Namwomba Mheshimiwa Balozi Adadi Rajab tuwasiliane ofisini ili tupitie kwa pamoja, tuone kata gani imesahaulika katika zile ambazo Serikali tayari imeziingiza katika mipango yake ya kutekeleza mawasiliano kwa wote.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Wananchi wa Mbulu Vijijini hawana mawasiliano ya simu wala minara katika Kata za Tumati, Yaeda, Ampa, Gidhim na Gorati:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka minara katika Kata hizo ili kupata mawasiliano?

Supplementary Question 3

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa tatizo la mawasiliano ya simu katika Jimbo la Mtama ni baya kuliko ilivyo katika Jimbo la Mbulu Vijijini, kwa sababu katika Tarafa tano; Tarafa tatu mawasiliano ya simu ni tabu sana, wakati mwingine inabidi upande juu ya mnazi au juu ya kichuguu ili uweze kuwasiliana. Tulianza kupata matumaini baada ya Kampuni ya Viettel kuanza kusambaza minara, tukadhani hali itarekebishika, lakini inaonekana kama kazi ile kama imesimama hivi.
Sasa ni lini kazi ile itakamilika ili wananchi wangu waweze kufaidi matunda ya kazi nzuri ya mawasiliano ya simu katika Jimbo la Mtama?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, haikubaliki kati ya tarafa tano, tarafa mbili tu ndiyo zipate mawasiliano ya uhakika, hiyo haikubaliki. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tutalifuatilia hili, nini hasa kimesababisha ujenzi wa minara katika maeneo hayo kusimama na baada ya hapo tutaangalia namna ya kushughulikia.

Name

Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:- Wananchi wa Mbulu Vijijini hawana mawasiliano ya simu wala minara katika Kata za Tumati, Yaeda, Ampa, Gidhim na Gorati:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka minara katika Kata hizo ili kupata mawasiliano?

Supplementary Question 4

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Tatizo lililopo Mbulu Vijijini linafanana kabisa na tatizo lililopo Wilaya ya Kakonko. Wilaya ya Kakonko Kata za Nyamtukuza, Nyabibuye, Warama, Muhange, Kasuga na mwambao wote wa Burundi, simu zinaingiliana na mitambo ya Burundi na hivyo wananchi wa Wilaya ya Kakonko maeneo hayo yanayopakana na Burundi wanapata hasara kubwa sana kwa kuongeza vocha ambazo zinaliwa na mitandao ya Burundi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba commitment ya Serikali hapa; Serikali inafanya jitihada gani kuhakikisha kwamba wananchi hawa hawapati hasara katika matumizi yao ya simu? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo aliyoyataja, kama alivyosema, yako mpakani na tuna mipango maalum ya kushughulikia maeneo ya mipakani. Nitakwenda kuangalia ni kwa nini hasa eneo lake bado halijaboreshwa kwa namna ambavyo ameeleza?