Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUNDE T. ABDALLAH (K.n.y. MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU) aliuliza:- Wilaya ya Igunga ni miongoni mwa Wilaya zinazolima pamba kwa wingi nchini:- Je, ni lini Serikali itajenga au kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya kuchambua pamba, kutengeneza nyuzi na nguo na hata mafuta ili kutekeleza azma ya Serikali ya kujenga nchi ya viwanda?

Supplementary Question 1

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii niweze kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Waziri, lakini nina maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Mheshimiwa Waziri pale manonga tuna Kiwanda cha kuchambua pamba cha siku nyingi ambacho kina utata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuja tukaongea na Mheshimiwa Waziri, akatuahidi kumwita Rajan na Igembensabo ili kuja kutatua tatizo hili na hatimaye kiwanda hicho kiweze kufanya kazi ili wananchi wa Igunda waweze kupata ajira na sehemu rahisi ya kuuza pamba zao. Je, Mheshimiwa Waziri amefikia wapi kuwaita watu hao ambao alituahidi kuwaita hapa Dodoma ili kuja kupatanao mwongozo ili tuweze kujua tunaanzaje kuhusu kiwanda kile cha Manonga Ginnery? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Mkoa
wa Tabora umekuwa na adha kubwa ya ukosefu wa viwanda; na kwa kuwa Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara alituahidi kwamba amepata mwekezaji Mchina wa kiwanda cha kujenga Tumbaku Tabora; na lilitokea tatizo pale Airport hatimaye yule mwekezaji hakuweza kuja Tabora kuongea na sisi ili kuweza kujenga Kiwanda hicho cha Tumbaku. Je, Mheshimiwa Waziri, mpaka sasa status ya mwekezaji huyo ambaye alikuwa anakuja Tabora akapata matatizo Airport imefikia wapi? (Makofi)

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea kujadiliana na Rajan juu ya Manonga Ginnery. Tatizo ninalolipata kuhusu Rajan, aliyerithi kiwanda yuko nje ya nchi. Kwa hiyo, nawasiliana naye kupitia mtu wa kati, lakini naomba mwendelee kunikumbusha, mwendelee kunishinikiza kusudi tuweze kufikia suluhu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, inaonekana hawa Rajan hawana interest tena na kiwanda na hawako tayari kununua na mwendelee kuwapa shime watu wa Igembensabo waendelee na nia hiyo, tutafikia muafaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la tumbaku; sina mpango tena na yule Mchina ila natafuta wawekezaji wengine wa kuweza kuwekeza kwenye zao la Tumbaku kwa kujenga Kiwanda. (Makofi)

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. MUNDE T. ABDALLAH (K.n.y. MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU) aliuliza:- Wilaya ya Igunga ni miongoni mwa Wilaya zinazolima pamba kwa wingi nchini:- Je, ni lini Serikali itajenga au kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya kuchambua pamba, kutengeneza nyuzi na nguo na hata mafuta ili kutekeleza azma ya Serikali ya kujenga nchi ya viwanda?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, suala la zao la pamba na usindikaji wake au kuongeza thamani ni suala la msingi sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Busega kuna vinu ambavyo ni vya viwanda vya Pamba kama cha Ngasamo na Sir Ginnery. Maeneo yote haya yamekuwa na viwanda ambavyo vimesimama, havifanyi kazi na hivyo kupelekea wananchi wengi na wakulima wa pamba kushindwa kuuza pamba yao kwa bei yenye kuongeza thamani. Je, Mheshimiwa Waziri ana mkakati gani? Pamoja na suala la Manonga na kwingineko ambako kuna viwanda ambavyo havifanyi kazi vizuri, kama Serikali kuna namna gani ya kuweza kuboresha viwanda hivi?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, chanda chema huvikwa pete. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wanaotoka kwenye eneo la pamba, nenda kwenye mkakati wa pamba mpaka mavazi, ukurasa wa 91 majibu yote yako pale. Tutaweza kufaidika na pamba kama zamani, soko litakapokuwa linaweza kuvuta (the demand pull) na mojawapo ya mambo ya kufanya ni kuongeza ufanisi katika zao la pamba. Mwaka 2016 kwa kutumia ways and measures baada ya ku-control watu wasichafue pamba, nyie ni mashuhuda bei imepanda kidogo, tutaendelea na nikuahidi Mheshimiwa Mbunge tukitoka hapa nitakupa huo ukurasa namba 91 nilikuja nao nilijua itajitokea uone mambo mazuri. The productivity, pamba ina tatizo kwa sababu hakuna tija katika uzalishaji.

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUNDE T. ABDALLAH (K.n.y. MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU) aliuliza:- Wilaya ya Igunga ni miongoni mwa Wilaya zinazolima pamba kwa wingi nchini:- Je, ni lini Serikali itajenga au kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya kuchambua pamba, kutengeneza nyuzi na nguo na hata mafuta ili kutekeleza azma ya Serikali ya kujenga nchi ya viwanda?

Supplementary Question 3

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Mkoa wa Morogoro ni miongoni mwa mikoa ambayo ilikuwa na viwanda vingi sana. Baada ya ubinafsishaji, viwanda vingi vimekufa na vingine vimegeuka kuwa ma-godown. Je, Serikali ina mpango gani wa uhakikisha inafufua viwanda hivi viweze kutoa ajira kwa wakati wa Mkoa wa Morogoro? (Makofi)

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Devotha nawe umewahisha shughuli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, isionekane mimi ni bingwa wa kukwepa maswali, Mheshimiwa Devotha hakuna kiwanda kitabaki godown Morogoro. Tajiri namba moja alisimama Morogoro na microphone, akasema kama ningekuwa na Waziri wa Viwanda, Viwanda vya Morogoro vingefanya kazi, alikuwa ananisema mimi. Viwanda vyote unavyovisema, vinafanya kazi sasa. Kiwanda cha Canvas kitaanza ku-role Kiwanda cha MOPROCO kitaanza kutengeneza mafuta nami mambo yataendelea kuninyookea. (Kicheko/Makofi)

Name

Saada Salum Mkuya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Welezo

Primary Question

MHE. MUNDE T. ABDALLAH (K.n.y. MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU) aliuliza:- Wilaya ya Igunga ni miongoni mwa Wilaya zinazolima pamba kwa wingi nchini:- Je, ni lini Serikali itajenga au kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya kuchambua pamba, kutengeneza nyuzi na nguo na hata mafuta ili kutekeleza azma ya Serikali ya kujenga nchi ya viwanda?

Supplementary Question 4

MHE. SAADA SALUM MKUYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa maelezo yake, lakini Mheshimiwa Waziri najua kwamba karafuu ya Zanzibar ndiyo Karafuu ambayo ni quality duniani kote. Je, Wizara ya Biashara na Viwanda ya Tanzania ina mkakati gani kushirikiana na Wizara ya Biashara na Viwanda ya Zanzibar kuhakikisha kwamba tunajenga kiwanda ambacho kita-absolve karafuu ya Zanzibar kwa ajili ya kutengeneza products, kusafirisha nje lakini vile vile kupatia vijana ajira kama ambavyo tunaelezwa na ndiyo mategemeo yetu?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu Zanzibar ilikuwa ni kwamba Makatibu Wakuu wa Wizara ya Viwanda Zanzibar na wale wa Tanzania kwa upande wa Bara wakutane.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa napenda nitoe maelekezo kwamba wanapokutana sasa, kwa sababu najua wananisikiliza; na suala la Karafuu na Kiwanda na lenyewe waliunganishe walete majibu hapa tuweze kupata suluhu ya kutengeneza Kiwanda Zanzibar. (Makofi)