Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza:- Mwaka 2014 Rais wa Awamu ya Nne alipokuja Makambako aliahidi kutoa Sh.600,000,000/= ili zisaidie kuboresha au kuchimba bwawa la maji Makambako litakalotoa huduma ya maji kwa wananchi wa mji huo:- Je, ni lini fedha hizo zitatolewa ili zifanye kazi iliyokusudiwa?

Supplementary Question 1

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nina maswali madogo mawili ya nyongeza. Naishukuru Serikali kwa namna ambavyo imeonesha nia nzuri ya kutatua tatizo kubwa la maji lililoko katika Mji wa Makambako. Swali la kwanza, kwa sababu Serikali imetenga fedha hizo dola ambazo amezitaja hapo, dola milioni 38, nataka kujua ni lini sasa mradi huu utaanza ili wananchi wa Makambako waepukane na tatizo kubwa wanalopata Makambako na hata wawekezaji wa viwanda inashindikana kwa sababu maji hatuna?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa sababu mradi huu mdogo ambao kama alivyosema tenda imetangazwa ambao ni kwa ajili ya bwawa dogo la Makambako, nilipofuatilia Mkoani wanasema tayari iko Wizarani lakini Wizara bado haijarudisha kule ili mkandarasi aanze kazi. Je, ni lini sasa mkandarasi huyu ataanza kazi kwa mradi huu kwa mwaka huu wa fedha 2016/2017?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza anauliza ni lini huu mradi mkubwa wa dola milioni 38 unatarajiwa kuanza. Kwa faida ya Wabunge wengine ambao watafaidika na mradi huu wa dola milioni 500 za mkopo nafuu kutoka Serikali ya India, niseme kwa sasa hatua inayoendelea tayari Hazina imekamilisha taratibu za kusaini makubaliano ya fedha kwa maana ya financial agreement. Pia Wizara inaendelea sasa kufanya manunuzi ya ma-consultant watakaokamilisha usanifu na makabrasha ya zabuni kwa ajili ya mradi huu. Mheshimiwa Deo Sanga baada ya kukamilisha taratibu hizi basi tutaendelea na kutangaza tenda na kuhakikisha kwamba mradi huu unaanza kwenye mwaka wa fedha wa 2017/2018. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusu tenda inayoendelea ambayo inafanywa na Halmashauri ya Mheshimiwa Deo Sanga, niseme kwamba kwa vile ametoa taarifa kwamba tayari wameshaleta hizo nyaraka Wizara ya Maji, naomba nifuatilie kama kweli zimeshaletwa na tusimamie ili waweze kurudisha haraka ili shughuli iendelee. Mheshimiwa Sanga naomba tuwasiliane kwa hili.

Name

Saumu Heri Sakala

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza:- Mwaka 2014 Rais wa Awamu ya Nne alipokuja Makambako aliahidi kutoa Sh.600,000,000/= ili zisaidie kuboresha au kuchimba bwawa la maji Makambako litakalotoa huduma ya maji kwa wananchi wa mji huo:- Je, ni lini fedha hizo zitatolewa ili zifanye kazi iliyokusudiwa?

Supplementary Question 2

MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu haya ambayo amejibu Naibu Waziri tatizo la maji ambalo lipo Makambako ni sawa kabisa na tatizo la maji ambalo kwa sasa limejitokeza katika Jiji la Tanga na linaendelea kujitokeza ambapo licha tu ya maji kukatika mara kwa mara bila ratiba na bila taarifa lakini pia maji yale takribani mwezi mmoja sasa yamekuwa yakitoka machafu yenye tope.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo hili nilimfikishia Mheshimiwa Waziri wa Maji, nilimwandikia barua lakini pia nilikwenda kumwona mimi mwenyewe lakini bado linaendelea na majibu ya uhakika bado hatujapata. Maji yamekuwa yakiendelea kutoka machafu, yakiwa na tope na bado pia yanaendelea kukatika mara kwa mara. Serikali itoe tamko sasa ni lini watu wa Tanga watapata maji safi kama walivyozoea na maji ambayo hayakatikikatiki?Ahhsante. (Makofi)

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mbunge alikuja kwangu akilalamikia hali ya maji kuwa na tope katika Jiji la Tanga. Jiji la Tanga ni mojawapo la mamlaka katika nchi ambayo imekuwa siku zote inatoa maji safi na salama.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilichojitokeza ni kwamba kumetokea hitilafu katika mtambo wa uchujaji maji na hii imetokana na uchafuzi mkubwa wa maji kule kwenye vyanzo kwa sababu wamevamia wachimbaji wa madini kwa hiyo maji yanakuja na tope na rangi. Kwa hiyo, imebidi sasa tutengeneze design nyingine ya kuchuja maji yale na tatizo lile tumeshalimaliza sasa hivi Tanga wanapata maji safi kama walivyokuwa wanapata zamani.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza:- Mwaka 2014 Rais wa Awamu ya Nne alipokuja Makambako aliahidi kutoa Sh.600,000,000/= ili zisaidie kuboresha au kuchimba bwawa la maji Makambako litakalotoa huduma ya maji kwa wananchi wa mji huo:- Je, ni lini fedha hizo zitatolewa ili zifanye kazi iliyokusudiwa?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa hii. Kama ilivyo kwa Bwawa la Makambako, Wizara ya Maji iliahidi Wilaya ya Hanang’ kuchimba Bwala la Gidahababieg kwa miaka saba. Naomba niulize ni lini bwawa hilo litachimbwa ili wale watu waliopata matatizo kwa miaka mingi waweze kupata maji?Ahsante.

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji, Kilimo na Mifugo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli bwawa hili amekuwa analipigania kwa muda mrefu lakini katika bajeti ya mwaka huu tutaanza kwanza kufanya usanifu ili tuweze kujenga bwawa hilo. Baada ya kujua gharama ya ujenzi ni kiasi gani na michoro itakuwa namna gani, basi tutajenga bwawa hilo kwa mwaka huu wa fedha unaokuja 2017/2018.