Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) aliuliza:- Ili kurahisisha mfumo wa kimaendeleo na kukuza uchumi katika Bonde la Ziwa Rukwa, Serikali iliahidi kujenga daraja linalopita katika Mto Momba kati ya Kata ya Kamsamba (Jimbo la Momba) na Kata ya Kipeta (Jimbo la Kwela) mwaka 2009. Je, ni lini ahadi hiyo ya Serikali itakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini zipo taarifa ambazo si rasmi sana kwamba zabuni ile ya kumpata mkandarasi wa kujenga daraja la Mto Momba zilisitishwa hivi karibuni na kuleta wasiwasi mkubwa sana kwa wananchi wa mikoa ya Songwe, Katavi na Rukwa kwamba daraja lao inawezekana lisijengwe. Leo Waziri anawathibitishia nini wananchi wa mikoa hiyo kwamba daraja hilo litaanza kujengwa lini?(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Wilaya ya Momba ina kanda mbili, kuna ukanda wa juu na kuna ukanda wa chini na katika Ukanda wa Chini kuna Kata za Msangano, Chitete, Chilulumo, Mkulwe, Kamsamba pamoja na Ivuna. Ukanda wa Juu kuna Kata za Kapele, Miunga Nzoka, Ikana pamoja na Ndalambo na Halmashauri ya Mji wa Tunduma. Barabara za kuingia katika Makao Makuu ya Wilaya mpya hazipitiki kabisa. Ni lini Serikali itahakikisha kwamba inatenga fedha za kujenga barabara ya kutoka Ikana mpaka Chitete na Tunduma kuelekea Chitete?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mwaka huu wa fedha wa 2016/2017 tumetenga shilingi milioni 2,935 na taratibu za kumpata mkandarasi zinazofanywa na TANROADS ziko katika hatua za mwisho. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba taratibu hizo mara zitakapokamilika, mkandarasi akipatikana atalipwa fedha hizo kama advance payment. Mwaka unaofuata ambao ujenzi utaendelea zimetengwa tena shilingi bilioni tatu kwa ajili ya kuendeleza ujenzi huo, naomba nimhakikishie hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu maeneo ya barabara aliyoyataja, hayo majina kwangu ni mageni kidogo lakini kama ana maana ya ile barabara inayounganisha hii mikoa mitatu ambapo sehemu kubwa inapita eneo la Mkoa wako wa Songwe, nadhani anafahamu na mara nyingi tumekuwa tukijibu hapa kwamba mara tutakapomaliza kujenga hili daraja la Momba tutaingia sasa kwenye suala la ujenzi wa barabara. Kama ana maana ya barabara nyingine, naomba nimkaribishe ofisini tukutane na wataalam tupate ratiba ya nini hasa kitafanyika katika mwaka huu wa fedha na mwaka ujao wa fedha na hatimaye tupate majibu ya suala lake na tuweze kuwaridhisha wananchi anaowawakilisha.

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) aliuliza:- Ili kurahisisha mfumo wa kimaendeleo na kukuza uchumi katika Bonde la Ziwa Rukwa, Serikali iliahidi kujenga daraja linalopita katika Mto Momba kati ya Kata ya Kamsamba (Jimbo la Momba) na Kata ya Kipeta (Jimbo la Kwela) mwaka 2009. Je, ni lini ahadi hiyo ya Serikali itakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo hili la kutokuwa na mawasiliano katika jimbo hilo la Momba linafanana kabisa na barabara ya ulinzi ambayo inaanzia Mtwara Mjini na kuzunguka Mikoa yote ya Kusini kwamba mvua zilizonyeesha hivi sasa barabara hii haipitiki na hasa katika maeneo ya kijiji cha Kivava na Mahurunga mvua imeweza kukata madaraja na barabara hii hivi sasa haipitiki. Je, Serikali hivi sasa ipo tayari kuharakisha ujenzi wa barabara hii ya ulinzi? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba sasa hivi mkandarasi yuko site kwa ajili ya ujenzi wa kipande cha kutoka Mtwara hadi Mnivata na baada ya hapo tunaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuendelea kujenga barabara hiyo mpaka Newala na baadaye tunaendelea na ile barabara inayoambaa kwenye Mto Ruvuma ambayo tunasema ni barabara ya ulinzi, nadhani hilo analifahamu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu madaraja yaliyobomoko, bahati nzuri Meneja wa TANROADS Mkoa wa Mtwara ni kati ya Mamaneja ambao ni wepesi sana na alishatujulisha hayo na tumempa maelekezo ya kufanya huku akiwasiliana na Road Board kwa ajili ya kutumia fedha za emergency kurekebisha zile barabara zilizokatika.

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA (K.n.y. MHE. DAVID E. SILINDE) aliuliza:- Ili kurahisisha mfumo wa kimaendeleo na kukuza uchumi katika Bonde la Ziwa Rukwa, Serikali iliahidi kujenga daraja linalopita katika Mto Momba kati ya Kata ya Kamsamba (Jimbo la Momba) na Kata ya Kipeta (Jimbo la Kwela) mwaka 2009. Je, ni lini ahadi hiyo ya Serikali itakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri ameeleza katika swali la msingi umuhimu wa ujenzi wa daraja la Mto Momba kwamba ni kiungo muhimu katika kuunganisha mikoa mitatu. Kwa kuwa Sera ya Serikali katika ujenzi wa barabara za lami inazingatia barabara zinazounganisha mikoa. Je, ni lini Serikali itajenga barabara hii muhimu kwa kiwango cha lami inayounganisha mikoa mitatu ya Katavi, Rukwa na Songwe?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Ignas Malocha kwa kazi kubwa anayoifanya ya kufuatilia ujenzi wa barabara hii.(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Malocha amekuja ofisini kwetu mara nyingi na tumeongea sana kuhusu barabara hii na tumemwambia mara tutakapokamilisha ujenzi wa daraja la Momba hatua itakayofuata ni kuhakikisha tunaanza na kazi ya feasibility study and detail design kwa ajili ya kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Tumeongea hayo ofisini na mimi nimwombe yale ambayo tulikubaliana ofisi tutayatekeleza kwa manufaa ya wananchi wa mikoa hii mitatu.