Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA (K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI) aliuliza:- Barabara ya Makambako - Songea yenye urefu wa kilometa 295 imeharibika sana na inahitaji kufanyiwa matengenezo. Je, ni lini Serikali itakarabati barabara hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa vile barabara hii ya Makambako - Songea uharibifu wake umechangiwa kwa kiwango kikubwa na usafirishaji wa magari na mizigo mizito kutoka na kuelekea Songea. Ni lini sasa Serikali itajenga reli kutoka Makambako kuelekea Songea kupitia Madaba? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile mizigo mingi pia inatoka Mbeya kuelekea Songea mpaka Mbinga, ni lini sasa Serikali itakamilisha meli ya kutoka Kyela kwenda Mbamba Bay ili mizigo mingi inayopita barabara ya Mbeya kuelekea Songea ipite kwa kutumia meli na kuokoa barabara zetu?(Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Serikali haijafikiria kujenga reli kutoka Makambako kwenda Songea, badala yake inafikiria na kwa sasa inatekeleza upembezi yakinifu na usanifu wa kina wa reli kutoka Mtwara - Songea hadi Mbamba Bay. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili kuhusu meli, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mhagama, hivi karibuni tu TPA wamekamilisha ujenzi wa meli mbili aina ya tishali zinazojiendesha ambazo zitafanya safari za kubeba mizigo kati ya Itungi pamoja na Mbinga. Kwa hiyo, meli hizo zitasaidia sana kupunguza mizigo inayopita katika barabara ya Makambako hadi Songea. Meli hizo zitazinduliwa hivi karibuni zinaitwa Self Propelled Barges, ni meli aina ya tishali.

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA (K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI) aliuliza:- Barabara ya Makambako - Songea yenye urefu wa kilometa 295 imeharibika sana na inahitaji kufanyiwa matengenezo. Je, ni lini Serikali itakarabati barabara hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Barabara ya Makambako - Songea imefanana sana na barabara ya Manyovu - Kasulu - Kibondo hadi Kabingo na bahati nzuri barabara hiyo Naibu Waziri ameitembelea. Ni kwa nini sasa barabara hiyo wasiingie kwenye ule mtindo wa kusanifu na kujenga (design and build) wakati usanifu unachukua muda mrefu kufika mpaka Kabingo? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa barabara anayoongelea ni karibu unakamilika, kwa hiyo, nadhani kubadilisha mfumo kwa sasa haina sababu sana. Mfumo wa jenga sanifu tunapenda kuutumia lakini tunajua gharama yake ni kubwa kidogo ukilinganisha na tukifanya usanifu wenyewe na baadaye tunatoa tender.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mimi nimuombe tu, tuhakikishe tunakamilisha kazi hii inayokamilika sasa hivi na baada ya hapo tuanze kutenga fedha za kujenga barabara hiyo. Kwa sababu lengo lako ni kuhakikisha barabara hii inajengwa kwa kiwango cha lami na inajengwa haraka iwezekanavyo.

Name

Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA (K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI) aliuliza:- Barabara ya Makambako - Songea yenye urefu wa kilometa 295 imeharibika sana na inahitaji kufanyiwa matengenezo. Je, ni lini Serikali itakarabati barabara hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la barabara la Makambako - Songea yanafanana na matatizo ya barabara inayotoka Mwatasi -Kimara – Idete - Idegenda ambako uzalishaji wa mbao pamoja na matunda aina ya pears ni wa kiwango kikubwa sana lakini hali ya barabara hii siyo nzuri. Ni lini Serikali sasa itafanya mpango mkakati kuhakikisha hizi barabara zinatengenezwa kwa kiwango cha lami ili kupelekea usafirishaji wa mbao uwe salama na safi? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Songea - Makambako ni trunk road wakati barabara anayoongelea ni ya district. Ni kweli zinafanana kwa sababu zote ni barabara lakini zina hadhi mbili tofauti na district road zinashughulikiwa na Halmashauri chini ya TAMISEMI.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana na hoja yake lakini naomba Watanzania wote tuungane kama watu wamoja, tuweke vipaumbele vya hizi barabara na vile ambavyo tunakubaliana tuanze navyo, tuanze navyo, kwa sababu hatimaye fedha zinahitajika na hatuwezi kujenga barabara zote kwa wakati mmoja, ni lazima tuanze hizi, baadaye tunafuata hizi, hatua kwa hatua. Kwa hiyo, nimuombe avute subira itafika wakati baada ya kukamilisha zile ambazo tumekubaliana ni vipaumbele chini ya Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya 2015 - 2020 tutakuja huku ambako Mheshimiwa Mgonokulima anakuongelea.

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA (K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI) aliuliza:- Barabara ya Makambako - Songea yenye urefu wa kilometa 295 imeharibika sana na inahitaji kufanyiwa matengenezo. Je, ni lini Serikali itakarabati barabara hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la Makambako - Songea halina tofauti na tatizo la barabara ya Kimanzichana – Mkamba, Mkamba – Mkuruwili, Mkuruwili – Msanga hiyo ni kwa Wilaya ya Mkuranga na tatizo la Mpuyani - Mwanarumango, Mwanarumango – Msanga -Vikumbulu na hiyo inatokana na tatizo kubwa la mvua iliyonyesha na kupelekea barabara kukatika hadi kufanya wafanyabiashara ya kusafirisha abiria na magari ya mizigo yanayobeba malighafi kupeleka viwandani kushindwa kufanya safari zake.
Je, Serikali kwa kuwa haina pesa na lengo lake ni kuweka lami kwa barabara hizo, ni lini Serikali itakuwa tayari kuweka changarawe na kukarabati yale maeneo korofi ili kuweza kusaidia jamii ya maeneo hayo waweze kupita kwa usalama? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli lazima nitambue juhudi za Mheshimiwa Zaynabu Vulu katika kufuatilia barabara hizi na hasa hiyo barabara aliyoitaja ambayo inaharibiwa na magari makubwa yanayobeba malighafi zinazokwenda viwandani. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Vulu, kama ambavyo tumekuwa tukimhakikishia mimi na Waziri wangu wakati anafuatilia masuala hayo Ofisini kwetu mbele ya wataalam vilevile, aendelee kufanya kwa namna anavyofanya ili hatimaye yeye na sisi tufike hapo tunapotaka kufika. Tunajua katika barabara hii moja aliyoitaja ni ile barabara niliyosema ni kipaumbele namba mbili cha kuhamasisha viwanda au cha kuwezesha viwanda. Nikumhakikishie tuna nia thabiti na wakati wowote tutakapopata fedha tutahakikisha barabara hizi zinajengwa kwa kiwango cha lami. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kama alivyosema kwa sasa tumeshatoa maelekezo kwa Mameneja wote wa Mikoa wa TANROADS, barabara zote zilizokatika zirudishiwe kwa kutumia fedha za emergence. Washirikiane TANROADS pamoja na Mfuko wa Barabara kuhakikisha wanarudisha mawasiliono katika maeneo yote ambayo mawasiliano yamekatika. Maelezo hayo tumeyatoa na nina hakika Meneja wetu wa Mkoa wa Pwani atahakikisha maeneo hayo anayoyataja Mheshimiwa Mbunge ambayo barabara zimekatika mawasiliano yanarudi. (Makofi)

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA (K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI) aliuliza:- Barabara ya Makambako - Songea yenye urefu wa kilometa 295 imeharibika sana na inahitaji kufanyiwa matengenezo. Je, ni lini Serikali itakarabati barabara hiyo?

Supplementary Question 5

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo lililopo kwenye barabara ya Makambako – Songea linafanana kabisa na tatizo lililopo Mombo – Soni - Lushoto kilometa 36 na juzi baada ya zile mvua kubwa imesababisha uharibifu mkubwa wa barabara ile. Je, ni lini sasa Serikali itaifanyia ukarabati mkubwa barabara hii ya Mombo – Soni - Lushoto kilometa 36?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rashid Shangazi kwa sababu yeye alikuwa wa kwanza kunijulisha matatizo yaliyotokea katika barabara hii anayoongelea kabla hata ya wataalam wangu hawajaniambia. Nadhani sasa anafahamu kwamba barabara hiyo imeanza kupitika kwa sababu kazi imefanyika ya kurudisha mawasiliano na kutengeneza pale ambapo mawe yaliteremka na kuziba barabara. Tunashukuru barabara hiyo sasa inaanza kupitika baada ya matengenezo kukamilika na tutaendelea kuifanyia marekebisho pale ambapo tutaona panahitajika. Nakushukuru sana Mheshimiwa Shangazi. (Makofi)