Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Primary Question

MHE. ALLY SALEH ALLY aliuliza:- Tanzania ni Mwanachama wa Jumuiya ya Uchumi ya Kusini mwa Afrika (SADC) yenye soko la watu milioni 200 na rasilimali lukuki katika mtawanyika wa nchi 15 wanachama, zikiwemo fursa kubwa za madini, petroli, gesi, ufundi, elimu na utalii. (a) Je, Tanzania imefaidikaje na soko hili kwa kipindi cha miaka ya uanachama wake? (b) Je, ni maeneo gani ya ushirikiano yameonekana zaidi kuwa na maslahi na Tanzania? (c) Tanzania inapakana na majirani ikiwemo Zambia, Msumbiji, Congo DRC na Malawi. Je, tuna miradi au ushirikiano wa kiuchumi na nchi hizo kupitia SADC?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Bunge hili limenipa heshima ya kuwa mwakilishi katika Bunge hili la SADC, lakini mpaka hivi sasa sifikiri kama SADC inaeleweka sana kwenye umma wa Watanzania. Ili kuongeza uhalali wake.
Je, Waziri haoni sasa kuna haja ya kuijulisha SADC kwa umma zaidi kuliko ilivyo hivi sasa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lingine ni kwamba kwa kuwa fursa zilizopo ni nyingi mno na jana tulijadili sana suala la economic diplomacy ambayo siku zote ni two way na inataka uwe very aggressive katika kuikabili; fursa zilizopo ni nyingi sana.
Je, Serikali haioni kwamba sasa wakati umefika mkakati wa Watanzania kunasa fursa zilizoko SADC uwe wazi ili Watanzania wengi waweze kuzinasa fursa hizo?

Name

Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na Mheshimiwa Ally Saleh kwamba wakati umefika wa kunadi fursa zilizoko katika Jumuiya hii ya SADC. Na sisi kama Wizara, kama mnavyojua kwamba tumeweka mkakati wa kutangaza na kutoa vipindi tofauti tofauti katika redio, tv, brochures, lakini pia tutaweka mkakati wa makusudi kwenda sehemu mbali zaidi kwa kuwaita wafanyabiashara na watu wa kawaida ili waweze kujua fursa zilizoko katika SADC.

Name

Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALLY SALEH ALLY aliuliza:- Tanzania ni Mwanachama wa Jumuiya ya Uchumi ya Kusini mwa Afrika (SADC) yenye soko la watu milioni 200 na rasilimali lukuki katika mtawanyika wa nchi 15 wanachama, zikiwemo fursa kubwa za madini, petroli, gesi, ufundi, elimu na utalii. (a) Je, Tanzania imefaidikaje na soko hili kwa kipindi cha miaka ya uanachama wake? (b) Je, ni maeneo gani ya ushirikiano yameonekana zaidi kuwa na maslahi na Tanzania? (c) Tanzania inapakana na majirani ikiwemo Zambia, Msumbiji, Congo DRC na Malawi. Je, tuna miradi au ushirikiano wa kiuchumi na nchi hizo kupitia SADC?

Supplementary Question 2

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi hii. Fursa ambazo Tanzania imezipata kupitia SADC ni sawa na ambavyo tunapata fursa kupitia Jumuiya ya Afrika Mashariki. Sambamba na mikoa mingine ambayo inazunguka nchi za Afrika Mashariki, Mkoa wa Kigoma na hususan Wilaya ya Kakonko, hatuna fursa ambazo tunazipata kwa kupakana na Burundi, matokeo yake Warundi wanateswa na kusumbuliwa katika Wilaya ya Kakonko na mwambao wote unaoambaa Wilaya zote za Kigoma. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba kupata maelezo ya Serikali, Burundi siyo sehemu ya Afrika Mashariki? Kama ni hivyo, kwa nini waendelee kuteswa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki?

Name

Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mara ya mwisho, wiki iliyopita pia alisema kwamba kuna raia wa Burundi kama 300 wamepigwa sana, lakini mimi nimefuatilia suala hilo sijaliona. Kama kuna sababu zozote zinazoonesha kwamba labda Burundi wanawafanyia ndivyo sivyo Watanzania, ningepata tu ushahidi na tutafuatilia, kwa sababu, katika vikao vyetu vya Mabaraza ya Mawaziri yanapotokea mambo ambayo hayaendani na utaratibu wa kisheria, huwa tunakaa na kuyatatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba sana Mheshimiwa Mbunge aniletee taarifa hiyo, ili sisi kama Wizara tufuatilie. (Makofi)

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. ALLY SALEH ALLY aliuliza:- Tanzania ni Mwanachama wa Jumuiya ya Uchumi ya Kusini mwa Afrika (SADC) yenye soko la watu milioni 200 na rasilimali lukuki katika mtawanyika wa nchi 15 wanachama, zikiwemo fursa kubwa za madini, petroli, gesi, ufundi, elimu na utalii. (a) Je, Tanzania imefaidikaje na soko hili kwa kipindi cha miaka ya uanachama wake? (b) Je, ni maeneo gani ya ushirikiano yameonekana zaidi kuwa na maslahi na Tanzania? (c) Tanzania inapakana na majirani ikiwemo Zambia, Msumbiji, Congo DRC na Malawi. Je, tuna miradi au ushirikiano wa kiuchumi na nchi hizo kupitia SADC?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa muda sasa nchi za SADC ili kukuza fursa za uwekezaji na soko la pamoja zimeendesha mradi wa ku-harmonise au kuwianisha sera na sheria za nchi hizi ili kuweza kuvuna rasilimali hizi, lakini pia soko liwe la pamoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, Serikali ya Tanzania imeshirikije kwenye mradi huu mpaka sasa? Tumefikia wapi? Maana bila ku-harmonise sheria zetu, soko hili haliwezi kuwa la pamoja na wala hatuwezi kuvuna rasilimali hizi vizuri zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa maana ya Wizara ya Mambo ya Nje, huwa tuna-co-ordinate na kuhamasisha Wizara za Kisekta ili zihakikishe kwamba sera au sheria ambazo zinatofautiana na sheria au sera zilizowekwa na jumuiya, ziwe zimekuwa harmonized na zoezi hili ni endelevu kwa sababu inategemea na matukio.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa data zilizokamilika nitampa Mheshimiwa Mbunge ili aweze kuelewa tulipofikia.