Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Serikali imeondoa tozo mbalimbali zilizokuwa kero kwa wananchi katika sekta ya uvuvi lakini bado kuna mkanganyiko ni tozo zipi zimefutwa na zipi zinaendelea. (a) Je, Serikali inaweza kuainisha aina ya tozo zilizoondolewa katika sekta ya uvuvi? (b) Je, ni lini Serikali itatoa mwongozo kwa watendaji wa Halmashauri juu ya mabadiliko hayo?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Mheshimiwa Mwenyekiti, tozo nyingi katika hizi zilizoondolewa si zile zinazomgusa moja kwa moja mvuvi. Wavuvi husasan katika Ziwa Victoria, wanasumbuliwa sana na leseni kwa mfano wanazopaswa kulipa wanapotoka Halmashauri moja kwenda Halmashauri nyingine, kuna ushuru wa uvuvi kwa mfano, na tozo nyingine za SUMATRA na maeneo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa sababu nyingi katika hizi ziko chini ya Sheria ya Uvuvi Na. 22 ya mwaka 2003, Serikali sasa haioni sababu ya msingi kabisa kuleta sheria hii Bungeni ili Bunge liweze kuipitia na kuifanyia marekebisho?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa taarifa nilizonazo Mheshimiwa Waziri wewe ni mtaalam mbobezi kwenye eneo hili la uvuvi na unatoka kwenye eneo la wavuvi, kwa hiyo unaujua vizuri uvuvi na kwa sababu matatizo mengi ya wavuvi, hususan eneo la Ukerewe yanazungumzika, je, uko tayari sasa Mheshimiwa Waziri baada ya Bunge hili tuweze kuandamana kwenda katika Visiwa vya Ukerewe upate fursa ya kuzungumza na wavuvi na kusikiliza kero zao? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza anasema kwamba tozo nyingi zilizofutwa sizo zile ambazo ni kero hasa inayowasumbua wavuvi na akatuomba kuleta mabadiliko ya Sheria ya Uvuvi Na. 22 ya Mwaka 2003.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie tu kwamba matakwa yake haya tunayachukua na tayari Serikali ipo katika mpango wa kuboresha moja ya Sheria ya Uvuvi ya mwaka 2003, Sheria Na. 22 na kupitia kanuni mbalimbali ambazo zitakwenda kuboresha kwa maana ya tozo hizi zilizofutwa, sawa na majibu yangu ya msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nataka nimhakikishie; hizi tozo, hasa ile ya movement permit iliyofutwa ilikuwa ni kero kubwa kwa wavuvi wetu na ndiyo maana Serikali hii ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Jospeh Magufuli ikaona iifutilie mbali. Na nataka nimhakikishie ya kwamba kilichobaki ni usimamizi wa kuhakikisha movement permit haiendelei kutozwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni la kwenda Ukerewe; ni kweli mimi ni mvuvi na uvuvi ni maisha yetu. Nataka nimhakikishie rafiki yangu ya kwamba tutafika Ukerewe kwenda kuzungumza na wavuvi na kwenda kuwatoa majaka roho yote yanayowasumbua. Ahsante sana.

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Serikali imeondoa tozo mbalimbali zilizokuwa kero kwa wananchi katika sekta ya uvuvi lakini bado kuna mkanganyiko ni tozo zipi zimefutwa na zipi zinaendelea. (a) Je, Serikali inaweza kuainisha aina ya tozo zilizoondolewa katika sekta ya uvuvi? (b) Je, ni lini Serikali itatoa mwongozo kwa watendaji wa Halmashauri juu ya mabadiliko hayo?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachukulia mfano wa mabasi, kuna utingo, kuna dereva, kuna konda, mwenye licence ya kuendesha chombo pale ni mmoja tu ambaye ni dereva, utingo hana licence wala konda. Cha ajabu katika Ziwa Tanganyika mwenye chombo anakuwa na wavuvi wake kama kumi au kumi na tano na wote wanalazimika kuwa na leseni. Je, Serikali haioni kama ni kero?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, haya ndiyo mabadiliko tunayokwenda kuyafanya katika Kanuni za Uvuvi, kuboresha ili kuweza kumuinua mvuvi wa Tanzania. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Keissy kanuni yetu ya Uvuvi tunayokwenda kuibadilisha itazingatia matakwa haya ya Waheshimiwa Wabunge.