Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. ALEX R. GASHAZA Jimbo la Ngara lina mifugo mingi hususan ng’ombe na mbuzi, lakini kuna tatizo kubwa la maeneo ya kunyweshea mifugo kwa maana ya malambo/ mabwawa kwa ajili ya kunyweshea mifugo. Je, ni lini Serikali itaanza uchimbaji na ujenzi wa malambo/mabwawa kwa ajili ya kunyweshea mifugo?

Supplementary Question 1

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali na kwa jitihada ambazo wanazifanya, natambua jitihada hizo; niombe kuuliza maswali ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Ngara kuna maeneo ambapo kuna mifugo mingi zaidi kuliko maeneo haya yaliyotajwa kuwekwa miradi hii. Kwa mfano kwenye kata za Keza, Nyamagoma, Mnusagamba katika kijiji cha Mnusagamba na Ntanga. Sasa, je, Serikali iko tayari kutenga fedha kwa ajili ya kupeleka huduma hii ya malambo katika maeneo hayo kwa sababu ndiyo maeneo yenye mifugo mingi zaidi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwenye sekta hii ya mifugo, ikiwa ni pamoja na Jimbo la Ngara, hususan baada ya mifugo mingi kutoka maporini kwenye hifadhi kurudi vijijini, kuna tatizo kubwa la migogoro kwa maana ya wakulima na wafugaji, lakini Serikali iliunda Kamati kutoka kwenye Wizara sita ili kupitia mchakato kuona ni namna gani ambavyo wanaweza wakatoa suluhisho la kudumu.
Je, ni lini Kamati hii iliyoundwa ya Wizara sita itakuja na mpango au pengine ku-implement matumzi bora ya ardhi kama suluhisho la kuondoa migogoro kati ya wakulima na wafugaji? (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Alex Gashaza, Mbunge wa Ngara, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza ameuliza juu ya lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya maeneo hayo yenye mifugo mingi. Jambo hili linapaswa yeye mwenyewe Mheshimiwa Mbunge na wenzake katika Halmashauri waliibue na sisi Serikali tuko tayari kuhakikisha ya kwamba tunawaunga mkono ili kuweza kuondoa kero hiyo ya ukosefu wa maji kwa ajili ya mifugo katika Wilaya ya Ngara na maeneo yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, ameuliza juu ya Kamati iliyoundwa na Serikali kupitia Wizara sita kuondoa matatizo ya wakulima na wafugaji, ndiyo maana nilieleza katika jibu letu la msingi ya kwamba maeneo ya Ngara yanalo tatizo kubwa la kuvamiwa na mifugo kutoka nchi jirani na ndiyo maana sisi katika Serikali tumejielekeza ya kwamba hatutarudi nyuma, tutahakikisha mifugo yote iliyotoka nchi jirani kuingia Tanzania kutufanya kuwa sisi ni eneo la malisho tutaitoa kwa namna yoyote ile ama kuikamata na kuhakikisha tunaitaifisha kwa Sheria Na. 17 ya Magonjwa ya Wanyama ya mwaka 2003. Lakini vilevile kwa sheria ya mwaka 2010 inayohusu rasilimali malisho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na juu ya task force hii iliyoundwa jitihada nyingi zimeshafanyika katika maeneo haya ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba maeneo yetu ambayo tulikuwa tumeyahifadhi kama vile Mwisa II yanakwenda kugawanywa kwa ajili ya wafugaji waweze kupata maeneo ya kufanyia shughuli zao za ufugaji kwa nafasi. Naomba sasa Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wengine watupe ushirikiano kuhakikisha jambo hili linafanikiwa.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. ALEX R. GASHAZA Jimbo la Ngara lina mifugo mingi hususan ng’ombe na mbuzi, lakini kuna tatizo kubwa la maeneo ya kunyweshea mifugo kwa maana ya malambo/ mabwawa kwa ajili ya kunyweshea mifugo. Je, ni lini Serikali itaanza uchimbaji na ujenzi wa malambo/mabwawa kwa ajili ya kunyweshea mifugo?

Supplementary Question 2

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata ya Pugu, Jimbo la Ukonga kuna Mnada wa Kimataifa wa Pugu, nimuombe Mheshimiwa Waziri kama yupo tayari tumpeleke katika eneo hili akutane na wafanyabiashara wa eneo hili ili wamueleze kero kubwa ziliyopo zikiwemo za ukosefu wa malisho na bwawa la maji na vyoo na mnada huu unaitwa wa kimataifa ambao kimsingi ndio unalisha Mkoa wa Dar es Salaam.
Mheshimiwa Waziri, upo tayari kwenda Pugu ukutane na watu hawa wakueleze kero zao kiundani zaidi? Ahsante.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, niko tayari kwenda Pugu kukutana na wafugaji hawa na wauzaji.

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. ALEX R. GASHAZA Jimbo la Ngara lina mifugo mingi hususan ng’ombe na mbuzi, lakini kuna tatizo kubwa la maeneo ya kunyweshea mifugo kwa maana ya malambo/ mabwawa kwa ajili ya kunyweshea mifugo. Je, ni lini Serikali itaanza uchimbaji na ujenzi wa malambo/mabwawa kwa ajili ya kunyweshea mifugo?

Supplementary Question 3

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipatia nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wizara imeanza kutekeleza ujenzi wa Bwawa la Mwanjolo, lakini mapungufu yaliyopo katika mkataba huo ni mabirika ya kunyweshea mifugo; je, Serikali haioni haja ya kuongeza mabirika ya kutosha ukizingatia Ukanda huo una ng’ombe wengi?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza sisi tunatambua ya kwamba mifugo ni maisha yetu na ufugaji ndiyo maisha yetu. Nataka nimhakikishie kwamba wao kupitia Halmashauri waibue miradi hii na sisi katika Serikali tutahakikisha kwamba tunawaunga mkono ili kusudi jambo hili linalohusu malisho na maji kwa ajili ya mifugo tatizo hili liweze kuisha.