Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

John Peter Kadutu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. JOHN P. KADUTU aliuliza:- Miaka mingi iliyopita Serikali iliwahi kuzichukua hospitali, shule na huduma nyingine nyingi kutoka katika mashirika ya dini na baadae Serikali ilirudisha huduma hizo kwa wamiliki wake, Kanisa la Moravian Tabora lilikuwa na eneo la VETA, Serikali wakati wa kurudisha haikurudisha eneo hilo kwa Kanisa hilo. (a) Je, ni lini Serikali itarudisha eneo hilo kwa wamiliki wake? (b) Je, Serikali ipo tayari kulipa fidia kwa kuwa na eneo ambalo siyo lake?

Supplementary Question 1

MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kunipa fursa ya kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.
Kwanza, ni vigezo gani viliifanya Serikali kurudisha mali za madhehebu mengine kama hospitali ya KCMC, Bugando na mashule na kwa nini isirudishwe mali za Kanisa hili la Moravian?
Swali la pili, kwa kuwa mgogoro huu na utata huu umechukua zaidi ya miaka 44, je, sasa Serikali ipo tayari kukaa katika meza ya majadiliano na Kanisa kumaliza utata huu uliodumu kwa miaka hiyo 44? Ahsante.

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba baada ya zoezi lilioendelea baada ya miaka ya 1960 ya shule nyingi zilizokuwa chini ya mashirika ya dini kupelekwa Serikalini kwa makubaliano maalum, lakini baadaye kuna baadhi ya huduma kama za hospitali ambazo zilirudishwa.
Naomba tu nimfahamishe Mheshimiwa Mbunge kwamba urudishwaji wa hospitali zile na baadhi ya huduma imefanywa kwa makubaliano maalum na madhehebu ya dini, vivyo hivyo hata shule ambazo zimeendelea kubakia Serikalini ambazo zamani zilikuwa ni shule za taasisi za kidini, kubakia Serikaini vilevile ni suala la makubaliano. Kwa hiyo, Serikali itaendelea kusaidia na madhehebu ya dini na mashirika mbalimbali na sekta binafsi katika kuendeleza elimu ikiwa ni pamoja na kuendelea kuzihudumia shule hizo kwa sababu inafanyika kwa maslahi mapana ya Taifa. Ifahamike kwamba miaka ya 63 zoezi hilo lilivyochukuliwa kulikuwa na makubaliano kama njia mojawapo ya kuhakikisha kwamba kunakuwa na usawa wa utoaji huduma na hususani elimu Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili kwamba ni lini majadiliano yatafanyika na Kanisa la Moravian kuhusu eneo la Chuo cha VETA tunachokizungumzia, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa sasa hakuna mgogoro wowote uliopo katika umilikaji wa eneo hilo kwa sababu tokea lilipotolewa mwaka 1973 ilifanyika kwa makubaliano na makubaliano hayo bado yanafanya kazi, changamoto kidogo ambayo imetokea ni kuhusu chuo kuendelea kutumika kwa malengo yale ambayo ilianzishwa nayo na malengo yenyewe ilikuwa ni kuwasaidia wanafunzi ambao wamekosa fursa ya kwenda katika elimu ya sekondari sasa hili linaweza likajadiliwa lakini mgogoro haupo kwenye umiliki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu kwamba, Wizara yangu na Serikali iko tayari kuendelea kushirikiana na Kanisa la Moravian, ni washirika wetu tokea siku nyingi sana tokea miaka ya 1970, tunawashukuru sana, tutaendelea kujadiliana nao namna bora ya kutumia chuo hiki kwa maendeleo ya Taifa.

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOHN P. KADUTU aliuliza:- Miaka mingi iliyopita Serikali iliwahi kuzichukua hospitali, shule na huduma nyingine nyingi kutoka katika mashirika ya dini na baadae Serikali ilirudisha huduma hizo kwa wamiliki wake, Kanisa la Moravian Tabora lilikuwa na eneo la VETA, Serikali wakati wa kurudisha haikurudisha eneo hilo kwa Kanisa hilo. (a) Je, ni lini Serikali itarudisha eneo hilo kwa wamiliki wake? (b) Je, Serikali ipo tayari kulipa fidia kwa kuwa na eneo ambalo siyo lake?

Supplementary Question 2

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Waziri katika Jimbo la Kahama, Kata ya Mwendakulima kuna mgogoro wa muda mrefu sana kati ya Kanisa la Katoliki na Kijiji cha Mwendakulima na sasa ni mtaa juu ya ardhi ambayo Kanisa hili limemiliki.
Mheshimiwa Waziri, je, uko tayari kwenda na mimi katika Jimbo hili na Kata hii kuweza kutatua mgogoro huu maana umekuwa ni wa muda mrefu na unaleta hali ya kutoelewana kati ya Kanisa na wananchi wa Mwendakulima? Ahsante.

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimahakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba niko tayari kwenda naye katika eneo hilo na ikiwezekana kuwashirikisha wenzetu wa Wizara ya Ardhi tuone mgogoro huo namna ya kusuluhisha, lakini kwa kuanzia hata leo niko tayari tukutane mimi na yeye tujadiliane kuhusu hili.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. JOHN P. KADUTU aliuliza:- Miaka mingi iliyopita Serikali iliwahi kuzichukua hospitali, shule na huduma nyingine nyingi kutoka katika mashirika ya dini na baadae Serikali ilirudisha huduma hizo kwa wamiliki wake, Kanisa la Moravian Tabora lilikuwa na eneo la VETA, Serikali wakati wa kurudisha haikurudisha eneo hilo kwa Kanisa hilo. (a) Je, ni lini Serikali itarudisha eneo hilo kwa wamiliki wake? (b) Je, Serikali ipo tayari kulipa fidia kwa kuwa na eneo ambalo siyo lake?

Supplementary Question 3

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Mbulu Mjini limekuwa na migogoro ya ardhi hususani shule zetu za msingi na sekondari na kwa sasa karibu shule mbili ziko mahakamani kwa ajili ya kutetea ardhi zake.
Je, Serikali haiwezi kuchukua utaratibu sasa wa kuhakikisha kuwa maeneo yote ya shule za msingi na sekondari nchini zinapata kupimwa ili ziweze kuepukana na adha hii ya migogoro ya ardhi kwa taasisi hizi za Serikali?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama anavyosema, Serikali inahitaji kupima hayo maeneo naomba tu nimfahamishe Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari kuna mkakati na maelekezo madhubuti ili taasisi zote za umma hususani shule kuhakikisa kwamba maeneo yao yote yanapimwa na kupatiwa hati ili kuondoa migogoro ambayo inaweza ikatokea pamoja na uvamizi.