Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Musa Rashid Ntimizi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. MUSA R. NTIMIZI aliuliza:- Serikali imeanza mchakato wa kutoa maji ya Ziwa Victoria kupeleka katika Mkoa wa Tabora:- • Je, mradi huo utapita katika Wilaya ya Uyui? • Je, ni vijiji gani katika Jimbo la Igalula vitanufaika na mradi huo hasa ukizingatiwa shida kubwa ya maji waliyonayo wananchi hao?

Supplementary Question 1

MHE. MUSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Wakati tunasubiri utaratibu wa kupata maji hayo ya uhakika ya hiyo progamu ya pili ya maji hayo kutoka Ziwa Victoria, je kwa sasa Serikali ina utaratibu gani wa haraka wa kusaidia kutatua maji katika Jimbo la Igalula?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari baada ya Bunge hili kwisha, kuambatana na mimi kwenda katika Jimbo la Igalula kuona shida kubwa ya maji ya wananchi wa Jimbo la Igalula? Ahsante. (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza napenda nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Musa Ntimizi kaka yangu, Mbunge kwa namna ya kipekee anavyowapigania wananchi wake wa Igalula.
Mheshimiwa Spika, mkakati wetu, pamoja na ujenzi wa bomba la kutoka Ziwa Victoria mpaka Uyui na maeneo mengine, lakini moja ya mkakati wetu kama Wizara, Serikali na Mheshimiwa Rais nia yake ya kuwatua akinamama ndoo kichwani, tumetenga bajeti katika kila Halmashauri na Halmashauri ya Igalula imetengewa fedha katika bajeti hii ya 2017/2018. Kwa hiyo, mkakati wetu ni kusimamia kwamba wanatengenezewa visima vya haraka ili wananchi wetu wa Igalula waweze kupata maji.
Mheshimiwa Spika, kukamilika kwa mradi huu wa Ziwa Victoria kutatupa fursa sisi kama Wizara kuangalia namna gani wananchi wa Igalula wanaweza kunufaika kupitia hili bomba kuu. Hii ni kwa sababu Waswahili wanasema unapokuwa karibu na waridi lazima unukie, nataka niwahakikishie wananchi wa Igalula watanufaika na maji kutokana na ukaribu wa bomba hili. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la mimi kwenda katika Jimbo la Igalula, nipo tayari baada ya Bunge Mheshimiwa Mbunge kushirikiana naye kuhakikisha kwamba nakwenda kuzungumza na wananchi wa Igalula. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MUSA R. NTIMIZI aliuliza:- Serikali imeanza mchakato wa kutoa maji ya Ziwa Victoria kupeleka katika Mkoa wa Tabora:- • Je, mradi huo utapita katika Wilaya ya Uyui? • Je, ni vijiji gani katika Jimbo la Igalula vitanufaika na mradi huo hasa ukizingatiwa shida kubwa ya maji waliyonayo wananchi hao?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Mkoa wa Katavi ni mkoa ambao bado hauna chanzo kizuri cha maji; Mkoa wa Katavi umepakana na Ziwa Tanganyika. Je, Serikali ina mpango gani kuweza kuyatoa maji Ziwa Tanganyika na kuyaleta Makao Makuu ya Mkoa?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kuhusiana na kutumia maji ya Ziwa ya Tanganyika kupeleka Mkoa wa Katavi, tayari andiko limeshaandikwa na limeletwa. Wizara tunafanyia kazi na mwaka ujao wa fedha tutaweka mshauri ili aanze kufanya kazi na baadaye tuongeze fedha kwa ajili ya kuchukua maji kutoka Kalema kuyaleta Mji wa Mpanda kupitia Jimbo lake. (Makofi)