Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Gibson Blasius Meiseyeki

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. GIBSON B. MEISEYEKI aliuliza:- Uhaba wa maji ni moja kati ya matatizo sugu katika Jimbo la Arumeru Magharibi ingawa maji yote yanayotumika katika Jiji la Arusha yanatokea kwenye Jimbo la Arumeru Magharibi:- Je, ni nini mkakati wa haraka wa Serikali wa kutatua tatizo hilo la maji katika kata takribani 20 kati ya kata 27 za jimbo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. GIBSON B. MEISEYEKI: Mheshimiwa Spika, nimpe pole Waziri kwa kupata shida kidogo na majina.
Mheshimiwa Spika, kumekuwa na mkwamo mkubwa wa miradi ambayo Mheshimiwa Waziri ameitaja mingine hapa kutokana na urasimu wa malipo ya certificate kwa wakandarasi ambao wapo site. Miradi mingine imekwama kwa zaidi ya mwaka mmoja, mingine karibu miwili. Ni lini urasimu huu utakwisha ili miradi hii iweze kukamilika na kuwaondolea wananchi taabu hii ya maji ambayo imekuwa ni ya muda mrefu?
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, Kata zangu mbili za Odonyosambo na Odonyoas, wananchi kule wanataabika kwa kutumia maji yenye madini mengi, kwa maana hiyo wanapinda miguu na kuharibika kinywa nikiwa na maana meno yanaharibika kutokana na maji hayo na kwa sababu kuna chanzo ambacho Wilaya ya Longido wameki-abandon, wamepata chanzo kingine, ni lini Wizara sasa itaanza kuratibu kuwapelekea watu hawa ambao wanataabika kwa maji haya machafu ili kuwanusuru maisha yao na wananchi wengine waliopo pembezoni mwao waweze kufaidika na maji? Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru kwa maswali yake mazuri, lakini kikubwa ambacho nataka nilieleze Bunge lako Tukufu; sisi kama Serikali tumekuwa na utaratibu mpya wa kuhakikisha kwamba hatupeleki fedha tu, kwamba tunajiridhisha namna mkandarasi alivyofanya kazi kwa yeye ku-raise certificate, lakini kunakuwa na muda maalum, halmashauri inajiridhisha, mkoa unajiridhisha na sisi kama Wizara tunajiridhisha kazi bora iliyofanywa na mkandarasi.
Mheshimiwa Spika, lakini katika kipindi hiki cha uvumilivu au cha kusubiri, yawezekana akaona kama kuna suala la urasimu, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kama kuna certificate ambayo imekuwa-raised na inahitaji kulipwa, baada ya Bunge naomba tukutane katika ofisi yangu ili tuhakikishe kwamba tunawasimamia ili wananchi wa Arumeru Magharibi waweze kupata maji ya uhakika na salama kama lengo la Serikali ilivyokuwa imepanga…
Mheshimiwa Spika, katika swali la pili amezungumzia suala zima la wanachi kupinda mifupa kutokana na fluoride. Sisi kama Serikali lengo letu ni kuhakikisha wananchi wanapata maji, si maji tu, ni maji safi na salama. Kwa hiyo, sisi kama Serikali tumetengeneza maabara pale Arusha kuangalia teknolojia ambayo tunaweza tukapunguza fluoride, lakini pia kama Wizara tumejipanga kuangalia namna gani tunapata vyanzo vyenye mserereko ili visiwe na fluoride ili kuhakikisha kwamba wananchi wetu wanakuwa salama na wanakuwa na afya bora. Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwanza hatudaiwi senti tano kutoka kwenye halmashauri yake, fedha zote tumeshalipa.
Mheshimiwa Spika, pili, tunaendelea kuhakikisha kwamba tuna-tap maji kutoka Mlima Meru na kuwapelekea wananchi wake na kwamba hadi sasa hakuna mwananchi hata mmoja anayeteseka kwa kukosa maji yaliyo safi na salama. (Makofi)

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GIBSON B. MEISEYEKI aliuliza:- Uhaba wa maji ni moja kati ya matatizo sugu katika Jimbo la Arumeru Magharibi ingawa maji yote yanayotumika katika Jiji la Arusha yanatokea kwenye Jimbo la Arumeru Magharibi:- Je, ni nini mkakati wa haraka wa Serikali wa kutatua tatizo hilo la maji katika kata takribani 20 kati ya kata 27 za jimbo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa miradi mikubwa ya maji inachukua muda mrefu sana, ni kwa nini sasa Serikali haichimbi visima vifupi na virefu kwa kila mita 400 ili kupunguza adha ya maji kwa akinamama?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, jambo lolote kubwa na jambo zuri lenye kuleta utekelezaji mkubwa na manufaa kwa wananchi lazima lichukue muda, lakini jambo litakalokuwa bora na lenye tija kwa wananchi. Kikubwa kuhusu suala zima la kuchimba visima vifupi; sisi kama Wizara tunafanya hivyo na tutaendelea kufanya hivyo ili kuhakikisha kwamba wananchi wetu wanapata maji salama na yenye uhakika. Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nitoe taarifa kwamba Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango ametoa fedha maalum, Sh.3,900,000,000/= kwa ajili ya uchimbaji wa visima na fedha hizo tumekabidhi Mamlaka yetu ya Uchimbaji wa Visima na Ujenzi wa Mabwawa (DDCA). Kwa hiyo, tunaendelea kuchimba visima Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. GIBSON B. MEISEYEKI aliuliza:- Uhaba wa maji ni moja kati ya matatizo sugu katika Jimbo la Arumeru Magharibi ingawa maji yote yanayotumika katika Jiji la Arusha yanatokea kwenye Jimbo la Arumeru Magharibi:- Je, ni nini mkakati wa haraka wa Serikali wa kutatua tatizo hilo la maji katika kata takribani 20 kati ya kata 27 za jimbo hilo?

Supplementary Question 3

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa mwaka jana tumepitisha kwenye bajeti miradi 17 mikubwa nchini Tanzania, ikiwemo 16 Tanzania Bara na mmoja Zanzibar, ikiwemo na Makambako, kutokea fedha za kutoka India. Je, Waziri anawaambia nini wananchi wa Makambako juu ya ule mradi mkubwa ambao utajengwa katika Mji wa Makambako, lini utaanza ili wananchi hawa waweze kuondokana na adha na tabu ya maji wanayoipata katika Mji wa Makambako?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, ni kweli tumepata mkopo wa dola milioni 500 kutoka Serikali ya India na sasa hivi Wizara ya Fedha inakamilisha taratibu, wakishamaliza tunasaini financial agreement na mimi niko tayari, nimeshaandaa. Baada ya hilo tukio tu nitapeleka Wahandisi wakasanifu haraka. Wakishamaliza usanifu, tukiingia mikataba, tutajua mkataba utaanza lini na utakamilika lini, kwa hiyo niwahakikishie wananchi wake wa Makambako kwamba huo mradi unakuja.