Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:- Watanzania wenye ulemavu wanakabiliwa na kero mbalimbali za kimaisha ikiwemo ukosefu wa ajira kama ilivyo kwa Watanzania wengine, aidha, zipo changamoto za jumla kama vile kijana mwenye ulemavu wa ngozi asiye na ajira ana changamoto ya mahitaji ya kujikimu na pia ana changamoto za kipekee za mahitaji ya kiafya na kiusalama. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu umuhimu wa kuwatazama vijana wenye ulemavu mbalimbali kwa namna ya pekee na kama zipo sera na mikakati ya kiujumla kwa vijana wote nchini?

Supplementary Question 1

HE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na naishukuru Serikali kwa majibu yake, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, moja natambua jitihada za Serikali za kuweka mfumo kwa ajili ya kuwafikia walemavu, lakini suala la mfumo ni moja na suala la kufikisha huduma wanazohitaji kwa maana ya kuwafanyia upendeleo chanya (positive discrimination) ni lingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni kwa namna gani Serikali sasa imeweza kuwafikishia rasilimali fedha na rasilimali mafunzo watu wenye ulemavu kwenye vikundi vyao, tofauti na kuwajumuisha kwenye vikundi vingine ambapo mahitaji yao mahususi hayawezi kutimizwa?
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwa namna gani na kwa kiwango gani Serikali inadhani inaweza kuwapatia nafuu kwenye yale mambo ya msingi kwa mfano Bima ya Afya. Tuchukulie mfano mlemavu wa ngozi akipata ruzuku kwenye bima ya afya una uhakika wa kuhakikisha anakingwa kwa bima, kitu ambacho anakihitaji kama Watanzania wengine lakini yeye anakihitaji zaidi? Nakushukuru sana.

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijajibu nimpongeze sana kwa jinsi ambavyo anafuatilia na kushughulikia masuala ya watu wenye ulemavu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza linauliza ni jinsi gani Serikali imeweza kuwapatia vikundi vya watu wenye ulemavu fedha. Niki-refer kwamba swali lake lilikuwa linauliza kwa habari ya vijana; kuna mfuko wa maendeleo ya vijana ambao mfuko huu unawawezesha vijana.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nielezee kidogo kwamba kinachotakiwa kufanyika ni kwamba vijana wanatakiwa wajiunge kwenye vikundi, wakishajiunga kwenye vikundi mbalimbali, kwenye maeneo yalipo wanatakiwa pia kuwe na SACCOS. Kwa hiyo, kama Serikali tunapeleka hela kwenye zile SACCOS halafu baada ya kupeleka hela kwenye zile SACCOS vile vikundi vinapewa kupitia zile SACCOS.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kufanya hivyo kikubwa ambacho kinapatikana kwenye hivi vikundi ni kwamba wakati ule wa kurejesha wanatakiwa warejeshe riba ya asilimia 10. Katika hiyo riba ya asilimia 10, asilimia tano inabaki kwenye kikundi husika, asilimia mbili inabaki kwenye Halmashauri na asilimia tatu inaenda Serikalini. Kwa hiyo, hiyo ni njia mojawapo ambayo kama Serikali tunavipatia hivi vikundi fedha lakini pia kuna hii mifuko ya uwezeshaji kiuchumi wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kikubwa ambacho ninapenda niongelee hapa, nitoe wito kwa Halmashauri mbalimbali wawahamasishe watu wenye ulemavu kujiunga kwenye vikundi, kwa sababu hizi hazitolewi kwa matu mmoja mmoja. Wawahamasishe watu wenye ulemavu kujiunga kwenye vikundi, yakiwepo makundi ya vijana lakini pia na makundi mengine ambayo sio ya vijana ili waweze kunufaika na hizi fedha ambazo zinatolewa na Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia ameongelea kwa upande wa afya, kwa upande wa afya ametolea mfano wa watu wenye ualbino. Kwa upande wa watu wenye ualbino tayari Serikali imekwisha kuziagiza Halmashauri kwamba zinapoagiza dawa kutoka MSD zihakikishe zinajumuisha mafuta ya watu wenye ualbino katika madawa ambayo wanaagiza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jingine la pili ameongelea kwamba kwanini Serikali haitoi bima ya afya kwa watu wenye ulemavu. Niseme wazi kwamba Serikali, hicho ni kitu ambacho kama Serikali tunakichukua, hatuna specific kwamba hii ni bima ya afya kwa ajili ya watu wenye ulemavu. Lakini watu wenye ulemavu wasiokuwa na uwezo wanatibiwa baada ya kutambulika kwamba hawa watu hawana uwezo wa kugharamia mahitaji yao. (Makofi)

Name

Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Primary Question

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:- Watanzania wenye ulemavu wanakabiliwa na kero mbalimbali za kimaisha ikiwemo ukosefu wa ajira kama ilivyo kwa Watanzania wengine, aidha, zipo changamoto za jumla kama vile kijana mwenye ulemavu wa ngozi asiye na ajira ana changamoto ya mahitaji ya kujikimu na pia ana changamoto za kipekee za mahitaji ya kiafya na kiusalama. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu umuhimu wa kuwatazama vijana wenye ulemavu mbalimbali kwa namna ya pekee na kama zipo sera na mikakati ya kiujumla kwa vijana wote nchini?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Jana tu nilimpongeza Waziri Mkuu kwenye twitter kwa tamko lake ambalo limesema kila Wizara na Idara itoe taarifa kila mwaka imetenga kiasi gani kwenye kuimarisha huduma kwa watu wanaoishi na ulemavu. Nafikiri hili ni tamko zuri sana na linafaa kupongezwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali imejipangaje, utaratibu huu tutaanza kuuona katika mwaka huu wa fedha? (Makofi)

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu huu kama Serikali tumeu-plan kwamba uanze kuonekana katika bajeti ya mwaka huu wa fedha. (Makofi)

Name

Omary Ahmad Badwel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:- Watanzania wenye ulemavu wanakabiliwa na kero mbalimbali za kimaisha ikiwemo ukosefu wa ajira kama ilivyo kwa Watanzania wengine, aidha, zipo changamoto za jumla kama vile kijana mwenye ulemavu wa ngozi asiye na ajira ana changamoto ya mahitaji ya kujikimu na pia ana changamoto za kipekee za mahitaji ya kiafya na kiusalama. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu umuhimu wa kuwatazama vijana wenye ulemavu mbalimbali kwa namna ya pekee na kama zipo sera na mikakati ya kiujumla kwa vijana wote nchini?

Supplementary Question 3

MHE. OMARY A. BADWEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa hawa walemavu ili waweze kupata hizi ajira na huduma zingine mbalimbali ni lazima wapiti shule, vyuo na taasisi zingine ili waweze kukubalika katika hili eneo la ajira. Sasa kwa kuwa wanapitia katika shule mbalimbali ambazo zina matatizo mengi na inawafanya wasiweze kupata elimu vizuri kwa mfano Shule ya Viziwi Kigwe ambayo hakuna maji kwa muda mrefu na shule ile ni ya kitaifa na inachukua wanafunzi wengi.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapelekea maji wanafunzi wa shule ya wasiosikia Kigwe? (Makofi)

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, kama Serikali niseme kwamba hilo tumelichukua na kwa sababu ni suala mtambuka, tutafanya mawasiliano ndani ya Serikali kwa maana Wizara ya Maji ili tuweze kuona jinsi gani tunaweza tukapeleka maji katika Shule ya Kigwe, ahsante. (Makofi)