Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Je, Serikali ilimaanisha nini kusema kuwa matibabu ni bure kwa kinamama wajawazito?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, sasa naomba nimuulize maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Naibu Waziri atakubaliana na mimi ni kwa muda mrefu sasa Sera ya Matibabu Bure kwa mama wajawazito ya mwaka 2007 imeendelea kuwabagua akina mama wanaopata miscarriage kwa kuwatoza gharama za kusafishwa.
Je, Serikali haioni kwamba hii ni ajali kama ajali nyingine, hivyo basi akinamama hawa ambao walikuwa wana kiu ya kupata watoto wanastahili kufarijiwa kwa kusafishwa bila malipo? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, ni ipi sasa kauli ya Serikali juu ya mabadiliko ya kisera ili ianze kuwa- include akina mama wanaopata miscarriage na wale ambao mimba inatunga nje ya kizazi kuanza kupata matibabu bure na sio kuwaweka kwenye group (orodha) ya magonjwa ya akina mama ambayo kimsingi yanalipiwa kwa asilimia 100? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza lilikuwa limejielekeza kwa nini akina mama ambao mimba zao zinaharibika ama kwa lugha ya kitaalam miscarriage, kwa nini nao wasipate matibabu bure?
Mheshimiwa Naibu Spika, katika jibu langu la msingi nilisema kwamba huduma za akinamama wajawazito kuanzia mwanzo wa mimba mpaka mwisho ni bure, hii inakwenda sambamba na tiba ambayo inaambatana na mimba kuharibika. Ninaomba tu niseme kwamba huduma hii ni bure kwa mujibu wa sera yetu lakini kama suala hili halitekelezeki kama inavyotakiwa katika sera niseme tu kwamba tutalichukua na kutoa maelekezo katika mamlaka husika ili sasa hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sambamba na hilo, sasa hivi Serikali tunafanya mapitio ya Sera ya Afya, tutaweka utaratibu mzuri wa kuweza kulisimamia jambo hili.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Je, Serikali ilimaanisha nini kusema kuwa matibabu ni bure kwa kinamama wajawazito?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, akina mama wengi wajawazito wanapata madhara na kufariki hasa wanapokuwa na referral kutoka zahanati kwenda vituo vya afya na hospitali.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha huduma ya ambulance ili hawa akina mama wanapopata matatizo vijijini waweza kufikishwa haraka kwenye vituo vya afya na zahanati?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tunatambua kwamba kumekuwa na changamoto ya kuwasafirisha akina mama wajawazito kwenda katika sehemu za kupata huduma, na kwa kiasi kikubwa kwa kweli kumekuwa na muitikio mkubwa sana wa akinamama kujifungulia katika vituo vya afya, hivi tunavyoongea sasa hivi ni zaidi ya asilimia 60 ya akina mama wajawazito wanajifungulia katika vituo vya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sambamba na hilo, Serikali imeendelea kuboresha vituo vya afya na fedha kama alivyosema Naibu Waziri TAMISEMI, zaidi ya vituo 205 vimefanyiwa maboresho kwa kujenga theater, wodi ya akina mama kujifungulia ili hizi huduma za kujifungulia ziweze kuwa karibu zaidi. Lakini sambamba na hilo, Serikali imeendelea kutoa magari (ambulance) katika vituo vya afya na hospitali za wilaya, na kadri muda unavyokwenda tutakuwa tunaziongeza ili tuweze kufikia vituo vyote.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Je, Serikali ilimaanisha nini kusema kuwa matibabu ni bure kwa kinamama wajawazito?

Supplementary Question 3

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, tatizo la akina mama kujifungua mara nyingi wakati mwingine linaletwa pia na matatizo ya baadhi ya ma-nurse ambao huwa wanawanyanyapaa akina mama wenzao wanapotaka kujifungua.
Sasa sijui Serikali ina mpango gani au huwa inachukua hatua gani kuwadhibiti hawa akinamama ambao wana tabia za kuwanyanyasa akina mama wenzao wanapotaka kujifungua? (Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa na tatizo la baadhi ya watoa huduma kutoa lugha zisizokuwa sahihi kwa wagonjwa ambao wanafika katika hospitali, na hili ni jambo ambalo ni kinyume kabisa na maadili na taaluma za afya ikiwa ni pamoja na ma-nurse.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeendelea kuimarisha mabaraza yetu na hivi karibuni, wiki iliyopita tu, Mheshimiwa Waziri alitoa kauli ya kuhakikisha kwamba watoa huduma wote, ikiwa ni pamoja na madaktari na ma-nurse, wanakuwa wanatoa huduma nzuri ambayo inazingatia maadili na miiko ya kazi ambayo wanayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naendelea kulisisitiza hilo, na tumeendelea kuimarisha mabaraza yetu na tumeanza kuchukua hatua kwa wale ambao wanakiuka taratibu hizo.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA aliuliza:- Je, Serikali ilimaanisha nini kusema kuwa matibabu ni bure kwa kinamama wajawazito?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na mkanganyiko katika utaratibu wa upatikanaji wa vitambulisho kwa wazee ili waweze kupata huduma za afya ambapo baadhi ya maeneo wazee hawa wamekuwa wanatakiwa kuchangia baadhi ya gharama.
Sasa Serikali inaweza kutoa kauli ni upi wajibu wa halmashauri na upi wajibu wa wazee hawa ili waweze kupata vitambulisho ili wapate huduma za afya bure? (Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni agizo la Serikali kwamba Halmashauri zitoe vitambulisho vya wazee ili waweze kutambulika kirahisi wanapokwenda kutafuta matibabu ya afya. Na hii inaendana na Sera ya Afya ya mwaka 2007 ambayo inasema kwamba wazee watapata matibabu bure.
Mheshimiwa Naibu Spika, vitambulisho hivi vinapaswa vitolewe bure kwa sababu halmshauri zinagharamia. Inawezekana kwamba zile gharama ndogondogo kama upigaji wa picha ambazo wanatakiwa wazee nao wazigharamie ambayo sio gharama kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunapenda kusema tu kwamba gharama ya kitambulisho ni bure na Halmashauri zinatakiwa zigharamie hilo.