Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:- Liko tatizo la uhaba wa dawa na madaktari katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita. Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha kuwa dawa na Madaktari wa kutosha wanakuwepo?

Supplementary Question 1

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, ninamshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri ingawa hakuwa na takwimu kabisa kwenye eneo la madaktari maana yake amekili upungufu uliopo nilioutaja.
Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali yetu ya Rufaa ya Mkoa wa Geita inahudumia takribani wagonjwa 400 kila siku. Na mwaka jana wakati Waziri wa Afya amefanya ziara kwenye Hospitali hiyo aligundua kwamba mpaka wakati tunatoka kwenye bajeti tulikuawa bado tunaichukulia Hospitali ya Geita kama Hospitali ya Wilaya, haikuwa kwenye Hospitali za Mkoa na ndiyo sababu mpaka leo pale tuna specialist mmoja ambaye ni surgeon hatuna kabisa Physiotherapy Doctor, hatuna mtu wa mionzi, hatuna gynaecologist, hatuna mtu wa usingizi kwa sababu ilikuwa inachukuliwa kama Hospitali ya Geita.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa swali langu kwa kuwa tumeongeza vituo vingine vya Nyamkumbu na Kasamba tumejenga theater kwa ajili ya upasuaji na kuna wataalam wengi wamezagaa ambao wanaomba ajira. Ni lini Wizara italeta wataalamu wanaoweza kukudhi kiwango cha Hospitali ya Mkoa?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili katika Hospitali yetu ya Mkoa wa Geita ambapo nimesema hatuna wataalam tuna ujenzi wa Hospitali ya Mkoa baada ya kuchukua Hospitali ya Wilaya ambayo tulifanya kuwa Hospitali ya Mkoa, tunajenga Hospitali y Mkoa, lakini speed ni ndogo. Nini kauli ya Serikali ili kuifanya ile Hospitali ya Halmashauri irudi kwa wananchi na huduma ziweze kupungua gharama yake?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza ilikuwa ni kuhusiana na idadi ya wataalam. Ni kweli lazima nikiri katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita kuna changamoto kubwa sana ya Madaktari Bingwa na hilo sisi tumeliona kama nilivyojibu katika swali langu la msingi. Ni kwamba tunaendelea kuhakikisha kwamba tunafanya training ya kutosha Madaktari Bingwa na pale watakapopatikana basi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita tutaipa kipaumbele kuongeza idadi ya Madaktari Bingwa ili waweze kutoa huduma pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali lake lingine la pili lilikuwa lina husiana na kwa nini sasa Serikali isiongeze mkono wake katika ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa na ile iliyokuwepo pale iweze kurudi kuwa Hospitali ya Wilaya.
Naomba nimkumbushe Mheshimiwa Mbunge ni kwamba mwishoni mwa mwaka jana Serikali ilifanya maamuzi ya kuziondoa Hospitali za Rufaa za Mkoa kutoka ngazi za Serikali za Mitaa na kuzipeleka Serikali Kuu. Jukumu hilo sasa na sisi tumelipokea, tumekabidhiwa rasmi na mimi nimuhaidi tu Mheshimiwa Mbunge sasa na sisi tutajielekeza nguvu zetu kuhakikisha kwamba tunazijenga na kuziboresha Hospitali za Rufaa za Mkoa.

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:- Liko tatizo la uhaba wa dawa na madaktari katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita. Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha kuwa dawa na Madaktari wa kutosha wanakuwepo?

Supplementary Question 2

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, asante sana nilikuwa naomba kuuliza swali la nyongeza kwamba sasa hivi Tanzania kuna dawa hizi ambazo zinaitwa tressa medicines ambazo zinatolewa kwenye Hospitali za Rufaa ama Hospitali za Mikoa tu na kwamba kule vijijini kwenye Zahanati na Vituo vya Afya hizi dawa hazitolewi za magonjwa kama BP, magonjwa HIV, Kifua Kikuu sasa swali langu; nilikuwa naomba kujua kwa sababu wananchi wanapata tabu sana kusafiri umbali mrefu kwenda kutafuta dawa hizi kwenye Hospitali za Mikoa na Hospitali za Rufaa.
Je, Serikali ipo tayari hivi sasa kufundisha wale Medical Assistant’s kule vijijini ili dawa hizi ziweze kutolewa kule vijijini? Ahsante sana.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kutoa ufafanuzi, tumapoongelea suala la tressa medicines tuna maanisha kwamba ni dawa zile muhimu na ambazo sisi zina tusaidia katika sekta ya afya kubaini na kuangalia kwamba zile dawa muhimu zipo. Tressa medicines sio dawa ambazo unasemasijui kwa lugha ya kitaalam mnasemaje kwamba ni dawa ambazo ni muhimu ambazo zilikuwa zinatakiwa kutotolewa katika sehemu fulani tressa medicine ni general term ambayo sisi tunaitumia kuhakikisha kwamba tunazibaini na kuzipatia zile dawa muhimu kule ambapo tunazo.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa labda niendelee kwa kusema kwamba sasa hivi ndani ya Serikali na mwanzoni mwa mwezi huu tumetoa mwongozo wa utoaji wa dawa katika ngazi mbalimbali. Mwongozo huu kwa jina la kitaalam tunaitwa standard treatment guedline hapo siku za nyuma kila ngazi ilikuwa inajitolea dawa holela na kadri walivyokuwa wanaiona. Na hii changamoto tulikuwa tunaipata sana katika Hospitali kubwa makampuni ya dawa yana kuja yanamwambia mtoa huduma andika dawa hii wakiwa wanampa na yeye motisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati sisi Serikali tunaagiza dawa nyingi kwa pamoja unakuta sasa mgonjwa anaandikiwa dawa anaambiwa dawa hazipo. Serikali imeongeza sana bajeti ya dawa kutoka bilioni 30 mwaka 2015/2016 kufikia bilioni takribani 270 katika mwaka wa 2017/ 2018 ni zaidi ya mara tisa ndani ya miaka miwili. Kwa hiyo, hali ya upatikanaji wadawa sasa hivi nchini ni nzuri sana pamoja na hizi tressa medicines.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lako lingine la nyongeza ilikuwa sasa kutokana na mwongozo huu, umeweka utaratibu dawa gani kwa ugonjwa gani zitakuwa zinapatikana na kwamba hivyo vituo vya afya vitatakiwa kuzingitia dawa gani na kutoa matibabu kwa kulingana na ule mwongozo wa utoaji dawa ambao kama na sisi Serikali tumetoa. Tunatambua kwamba baadhi ya maeneo ambayo tunachangamoto ya watumishi tunaendelea kutoa mafunzo ili na wale watumishi waweze kutoa tiba kwa wale wagonjwa wanaofika pale ambapo hamna madaktari kwa kuzingatia miongozo ambayo na sisi tutakuwa tumewapa.

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:- Liko tatizo la uhaba wa dawa na madaktari katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita. Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha kuwa dawa na Madaktari wa kutosha wanakuwepo?

Supplementary Question 3

MHE. TASKA R MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa matatizo ya Mkoa wa Geita yanafanana na matizo ya Mkoa wa Katavi. Mkoa wetu wa Katavi hauna Hospitali ya Mkoa na hauna pia Hospitali ya Rufaa.
Je, ni lini sasa Serikali itamaliza ujenzi wa Hospitali ya Mkoa wa Katavi na kuleta Madaktari Bingwa wa magonjwa mbalimbali kama upasuaji wa macho, meno kwa sababu siku nyingine watu wanavimba ufizi wanashindwa kupasua? Ahsante.

Name

Dr. Elly Marko Macha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri Mkoa wa Katavi nimeutembelea ikiwa ni sehemu ya Mikoa 12 ambayo nimetembelea ndani ya miezi minne tangu nimeteuliwa kuwa Naibu Waziri. Nimeiona changamoto hiyo katika Mkoa wa Katavi, lakini kama nilivyojibu katika swala langu la msingi ni kwamba sasa hivi Serikali imechukua majukumu ya kuendesha Hospitali za Rufaa za Mikoa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ninachokuomba Mheshimiwa Taska Mbogo na Wabunge wengine wa Mkoa wa Katavi ni kuendelea kuihimiza Serikali yetu ya Mkoa kuhakikisha kwamba wanatenga eneo na kuanza maandalizi ya awali na sisi kama Serikali tutaendelea kujipanga kuhakikisha kwamba tunajenga Hospitali ya Rufaa ya Katavi.