Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Serikali imefanya kazi kubwa kujenga mtandao wa barabara za kiwango cha lami nchini, kipindi cha nyuma barabara kuu zilikuwa zinawekwa matuta ili kudhibiti ajali, lakini hivi karibuni Serikali imefuta utaratibu wa kuweka matuta kwenye barabara hizo na hivyo kuwa chanzo kikubwa cha ajali zinazosababisha majeruhi, ulemavu na vifo. Kwa mfano, eneo la Buigiri, Wilaya Chamwino lina ajali nyingi kutokana na barabara kukosa matuta. (a) Je, Serikali haioni kuwa kuna umuhimu wa kurejesha utaratibu wa kuweka matuta kwenye barabara? (b) Kama utaratibu wa matuta hauwezekani, je, Serikali haioni kuwa kuna haja ya kuyaondoa matuta yote kwenye barabara kuu ili kuondoa malalamiko ya wananchi kwa viongozi wao kwenye maeneo ambayo hayana matuta?

Supplementary Question 1

MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Waziri, lakini pamoja na majibu hayo mazuri naomba niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Buigiri ni eneo linalojulikana kwamba kuna Shule ya Watoto Wasiona kabisa na wengine wana uono hafifu. Je, Serikali haioni kwamba kuna kila sababu ya kulishughulikia suala hili la usalama barabarani katika eneo la Buigiri kwa umuhimu na haraka ili kuondokana na tatizo la ajali pale Buigiri?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kuna kituo kwa ajili ya wasioona sehemu za Buigiri kama alivyozungumza Mheshimiwa Mbunge. Kiutaratibu tunategemea sehemu zenye mahitaji maalum kama hayo kuwe na watu ambao wanawaongoza wanaovuka barabara ili wasiweze kupata ajali. Lakini hata hivyo, nimshauri na kumueleza Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali tutaendelea kutafuta utaratibu mzuri wa kuhakikisha kwamba watu wenye mahitaji maalum kama hao wanapokuwa wanavuka na kutumia barabara zetu wanasaidiwa ili wasiweze kupata madhara.

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Serikali imefanya kazi kubwa kujenga mtandao wa barabara za kiwango cha lami nchini, kipindi cha nyuma barabara kuu zilikuwa zinawekwa matuta ili kudhibiti ajali, lakini hivi karibuni Serikali imefuta utaratibu wa kuweka matuta kwenye barabara hizo na hivyo kuwa chanzo kikubwa cha ajali zinazosababisha majeruhi, ulemavu na vifo. Kwa mfano, eneo la Buigiri, Wilaya Chamwino lina ajali nyingi kutokana na barabara kukosa matuta. (a) Je, Serikali haioni kuwa kuna umuhimu wa kurejesha utaratibu wa kuweka matuta kwenye barabara? (b) Kama utaratibu wa matuta hauwezekani, je, Serikali haioni kuwa kuna haja ya kuyaondoa matuta yote kwenye barabara kuu ili kuondoa malalamiko ya wananchi kwa viongozi wao kwenye maeneo ambayo hayana matuta?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsantekwa kupata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Naomba nimuulize Waziri, kwa vile imethibitika kwamba baadhi ya ajali zinazotokea barabarani au zinasababishwa na ubovu wa barabara, au zinasababishwa na ukosefu wa alama mahususi za barabarani jukumu ambalo amekebidhiwa wakala wa barabara yaani TANROADS. Je, Serikali ina mpango gani wa kuiwajibisha TANROADS pale ambapo sababu ya ajali inaonekana ni kutotekeleza wajibu wa wakala huyo? Ahsante.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kuna ubovu wa barabara na Serikali imekuwa ikiendelea kufanya jitihada za kurekebisha ubovu huo kuhakikisha kwamba barabara zetu kuu na barabara za mikoa zimapitika kila wakati.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe wito tu kwa Watanzania wenzetu, kumetokea tabia ya hivi karibuni wananchi kuchukua hatua wenyewe ya kuweka matuta barabarani na hicho kimekuwa ni chanzo kimojawapo cha ajali mbalimbali kwa sababu wanapoweka matuta bila kuwashauri au bila kuwaambia TANROADS ina maana yale matuta yanakuwa hayana alama na magari yanapokuja yanafika, yanavamia yale matuta na kusababisha ajali. Niwashauri Watanzania, tunawaomba wasiweke matuta barabarani bila kuviambia vyombo husika vinavyohusika na barabara ili kuweka alama kuwaonyesha madereva kwamba kuna tuta mbele wanakokwenda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge Ndugu yangu Joseph Mhagama kwamba TANROADS wanajitahidi sana kufanya kazi zao kwa uadilifu na kwa umakini wa hali ya juu kuzingatia usalama wa Watanzania. (Makofi)

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Serikali imefanya kazi kubwa kujenga mtandao wa barabara za kiwango cha lami nchini, kipindi cha nyuma barabara kuu zilikuwa zinawekwa matuta ili kudhibiti ajali, lakini hivi karibuni Serikali imefuta utaratibu wa kuweka matuta kwenye barabara hizo na hivyo kuwa chanzo kikubwa cha ajali zinazosababisha majeruhi, ulemavu na vifo. Kwa mfano, eneo la Buigiri, Wilaya Chamwino lina ajali nyingi kutokana na barabara kukosa matuta. (a) Je, Serikali haioni kuwa kuna umuhimu wa kurejesha utaratibu wa kuweka matuta kwenye barabara? (b) Kama utaratibu wa matuta hauwezekani, je, Serikali haioni kuwa kuna haja ya kuyaondoa matuta yote kwenye barabara kuu ili kuondoa malalamiko ya wananchi kwa viongozi wao kwenye maeneo ambayo hayana matuta?

Supplementary Question 3

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa hii kuweza kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa kumekuwa na tatizo la uwekaji kiholela wa matuta kwenye baadhi ya barabara za mitaani na hivyo kusababisha usumbufu mkubwa kwa watumiaji wa vyombo vya moto na ikizingatiwa kwamba wananchi hawa hawana utalaam wowote. Je, Serikali ina mkakati gani wa kukabiliana na kadhia hii? Ahsante.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyokuwa namueleza Mheshimiwa Joseph Mhagama, ninatoa wito kwa Watanzania, barabara hizi zinajengwa kwa gharama kubwa sana ya pesa za Watanzania. Tunapoweka matuta bila vyombo vinavyohusika hasa TANROADS kufahamu tunaharibu barabara zetu ambazo tumezijenga kwa gharama kubwa sana. Kitu ambacho Serikali tunakifanya, tunapanga mkakati wa kuwasiliana na Wizara ya mambo ya ndani kitengo cha usalama barabarani kutoa elimu ya kutosha kwa wananchi namna ya matumizi bora ya barabara bila kuleta ajali kwa Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunawaomba sana Watanzania wasijichukulie maamuzi ya kuweka matuta barabarani hata kwa kugongwa kwa mbuzi tu isipokuwa wawasiliane na taasisi zinazohusika tusaidie kama kuna umuhimu wa kuweka matuta tutaweka, lakini kwa utaratibu ambao unaeleweka.

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Serikali imefanya kazi kubwa kujenga mtandao wa barabara za kiwango cha lami nchini, kipindi cha nyuma barabara kuu zilikuwa zinawekwa matuta ili kudhibiti ajali, lakini hivi karibuni Serikali imefuta utaratibu wa kuweka matuta kwenye barabara hizo na hivyo kuwa chanzo kikubwa cha ajali zinazosababisha majeruhi, ulemavu na vifo. Kwa mfano, eneo la Buigiri, Wilaya Chamwino lina ajali nyingi kutokana na barabara kukosa matuta. (a) Je, Serikali haioni kuwa kuna umuhimu wa kurejesha utaratibu wa kuweka matuta kwenye barabara? (b) Kama utaratibu wa matuta hauwezekani, je, Serikali haioni kuwa kuna haja ya kuyaondoa matuta yote kwenye barabara kuu ili kuondoa malalamiko ya wananchi kwa viongozi wao kwenye maeneo ambayo hayana matuta?

Supplementary Question 4

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, changamoto zilizopo katika Jimbo la Chilonwa linafanana kabisa na changamoto zilizopo katika Wilaya ya Mpanda, Mkoa wa Katavi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi kuna ujenzi ambao unaendelea kutoka katika Mkoa wa Tabora barabara ya Inyonga - Ipole kuelekea Mpanda. Barabara hii inajengwa lakini wakandarasi hawaweki alama za ujenzi kwamba kuna madaraja yanajengwa, kuna mashimo yamechimbwa na jambo hili limekuwa linasababisha ajali nyingi kwa wakazi wa Mpanda, kwa wakazi wa Mkoa wa Katavi.
Nini tamko la Serikali kuhakikisha inatoa maekelezo kwa hawa wakandarasi ili kupunguza ajali za barabarani katika Mkoa wa Katavi?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO:
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Mbunge swali lake la ujenzi wa barabara ya kutoka Katavi mpaka Tabora. Ni kweli Serikali tumeanza ujenzi wa barabara hiyo na hatua tunayokwenda nayo sasa ni hatua ya mobilization yaani makandarasi kwa sasa wanakusanya vifaa vya ujenzi katika maeneo hayo, bado kabisa kazi ya ujenzi haijaanza. Mara itakapoanza kazi ya ujenzi tutaweka alama kuhakikisha kwamba watumiaji wote wanaotumia barabara hiyo wako salama.